Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Al-Ahaadiyth Al-Qudsiyyah > 35-Hadiyth Al-Qudsiy: Mtu Aliyewausia Wanawe Wamuunguze Baada Ya Kufariki Kwa kukhofu Adhabu Ya Allaah

35-Hadiyth Al-Qudsiy: Mtu Aliyewausia Wanawe Wamuunguze Baada Ya Kufariki Kwa kukhofu Adhabu Ya Allaah

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 35

Mtu Aliyewausia Wanawe Wamuunguze Baada Ya Kufariki Kwa kukhofu Adhabu Ya Allaah

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((كَانَ رَجُلٌ يُسْرِفُ عَلَى نَفْسِهِ فَلَمَّا حَضَرَهُ الْمَوْتُ قَالَ لِبَنِيهِ: إِذَا أَنَا مُتُّ فَأَحْرِقُونِي ثُمَّ اطْحَنُونِي،  ثُمَّ ذَرُّونِي فِي الرِّيحِ،  فَوَاللَّهِ لَئِنْ قَدَرَ عَلَيَّ رَبِّي لَيُعَذِّبَنِّي عَذَابًا مَا عَذَّبَهُ أَحَدًا.  فَلَمَّا مَاتَ فُعِلَ بِهِ ذَلِكَ،  فَأَمَرَ اللَّهُ الْأَرْضَ فَقَالَ: اجْمَعِي مَا فِيكِ مِنْهُ فَفَعَلَتْ،  فَإِذَا هُوَ قَائِمٌ،  فَقَال:َ مَا حَمَلَكَ عَلَى مَا صَنَعْتَ؟ قَالَ: يَا رَبِّ خَشْيَتُكَ.  فَغَفَرَ لَهُ)) البخاري، مسلم، النسائي و ابن ماجه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mtu alifanya maasi makubwa na wakati mauti yalipomfikia aliwausia wanawe akiwaambia: Nitapokufa, nichomeni, munisage na mulitawanye jivu langu baharini kwani, wa-Allaahi, Allaah Atakaponipata, Ataniadhibu adhabu ambayo hajapata kuadhibiwa mtu mwingine. (Wanawe) walifanya walivyousiwa. Kisha Allaah Aliiamrisha ardhi kwamba: “Toa kile ulichokichukua.” Mara hapo akasima.  (Allaah) Akamuambia: Kitu gani kilichokufanya ufanye hayo uliyofanya? (Yule mtu) akasema: Yaa Rabb wangu! Ni kukukhofu Wewe. Basi Allaah Akamghufuria))  [Al-Bukhaariy, Muslim, An-Nasaaiy na Ibn Maajah]

 

Share [1]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/2690

Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F2690&title=35-Hadiyth%20Al-Qudsiy%3A%20Mtu%20Aliyewausia%20Wanawe%20Wamuunguze%20Baada%20Ya%20Kufariki%20Kwa%20kukhofu%20Adhabu%20Ya%20Allaah