Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Kitaab At-Tawhiyd (Word Doc) Chapisho La 2 Kimehaririwa 1438H (2017M) > 53-Kitaab At-Tawhiyd: Kusema: Allaahumma Nighufurie Ukitaka

53-Kitaab At-Tawhiyd: Kusema: Allaahumma Nighufurie Ukitaka

Mlango Wa 53

بَابٌ قَوْلُ اَللَّهُمَّ اِغْفِرْ لِي إِنْ شِئْتَ

Kusema: Allaahumma Nighufurie Ukitaka


 

 

 

فِي اَلصَّحِيحِ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ : أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ): ((لا! يَقُلْ أَحَدُكُمْ: اَللَّهُمَّ اِغْفِرْ لِي إِنْ شِئْتَ، اَللَّهُمَّ اِرْحَمْنِي إِنْ شِئْتَ، لِيَعْزِمِ الْمَسْأَلَةَ، فَإِنَّ اَللَّهَ لاَ مُكْرِهَ لَهُ))

Katika Swahiyh (Al-Bukhaariy) kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Asiseme mmoja wenu: Ee Allaah nighufurie Ukitaka. Ee Allaah Nirehemu Ukitaka, bali aazimie [kumuomba] kwani hakuna wa kumlazimisha Allaah kufanya jambo dhidi ya Idhini Yake)) [Al-Bukhaariy]

 

ولِمُسْلِمٍ : ((وَلْيُعَظِّمْ اَلرَّغْبَةَ فَإِنَّ اَللَّهَ لاَ يَتَعَاظَمُهُ شَيْءٌ أَعْطَاه))

Na katika Muslim: ((Bali akuze shauku yake kwani Allaah Halioni kubwa mno jambo Alilolitoa)) [Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Kukatazwa kufanya istithnaa (kuweka masharti) katika du’aa.

 

2-Maelezo na sababu ya ubaya wa kusema ‘Ukitaka'.

 

3-Kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwamba aombe kwa azma na raghba, 

 

4-Omba chochote upendacho kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

5-Sababu yake (kwani hakuna limshindalo).

 

 

 

Share [1]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/7909

Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7909&title=53-Kitaab%20At-Tawhiyd%3A%20Kusema%3A%20Allaahumma%20Nighufurie%20Ukitaka