Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > 002-Al-Baqarah: Aayah Na Mafunzo > 172-Aayah Na Mafunzo: Du’aa Ya Mwenye Kula Haraam Haikubalilwi

172-Aayah Na Mafunzo: Du’aa Ya Mwenye Kula Haraam Haikubalilwi

Aayah Na Mafunzo

Al-Baqarah

Du’aa Ya Mwenye Kula Haraam Haikubalilwi

 

www.alhidaaya.com [1]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُلُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا رَزَقْنَاكُمْ وَاشْكُرُوا لِلَّـهِ إِن كُنتُمْ إِيَّاهُ تَعْبُدُونَ ﴿١٧٢﴾

172. Enyi walioamini! Kuleni vizuri Tulivyokuruzukuni na mshukuruni Allaah mkiwa mnamwabudu Yeye Pekee.

Mafunzo:

 

 

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Enyi watu! Hakika Allaah ni Mzuri na Hapokei ila kilicho kizuri. Na Allaah Amewaamrisha Waumini kama Alivyowaamrisha Rasuli Anaposema: “Enyi Rusuli! Kuleni katika vizuri na tendeni mema, hakika Mimi kwa yale myatendayo ni Mjuzi.” [Al-Muuminuwn (23: 51)] Na Anasema: “Enyi walioamini! Kuleni vizuri Tulivyokuruzukuni.” Kisha akataja kisa cha mtu aliyekuwa safarini akiwa katika hali ya uchafu na mavumbi akiinua mikono yake mbinguni akiomba: Eee Rabb! Ee Rabb! Na hali chakula chake ni haramu, kinywaji chake ni haramu na kajengeka mwili wake kwa haramu vipi atakubaliwa du'aa yake?’ [Muslim]   

 

Share [2]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/7990

Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7990&title=172-Aayah%20Na%20Mafunzo%3A%20Du%E2%80%99aa%20Ya%20Mwenye%20Kula%20Haraam%20Haikubalilwi