أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [1]
Aal-‘Imraan 113-Hawako sawa sawa; miongoni mwa Ahlil-Kitaabi wako
لَيْسُوا سَوَاءً ۗ مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَائِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللَّـهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَهُمْ يَسْجُدُونَ ﴿١١٣﴾
113. Hawako sawa sawa; miongoni mwa Ahlil-Kitaabi wako watu wenye kusimama (kwa utiifu) wanasoma Aayaat za Allaah nyakati za usiku na wao wanasujudu (katika Swalaah).
Sababun-Nuzuwl:
Aayah hii imeteremka kama alivyohadithia Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) kwamba: (Siku moja) Rasuli (صلى الله عليه وآله وسلم) aliichelewesha Swalaah ya ‘Ishaa, kisha akatoka kuja kuiswali Masjid na akawakuta Swahaba (رضي الله عنهم) bado wanamsubiri. Akasema: “Uhakika wa mambo ulivyo ni kuwa hakuna yoyote katika Watu wa Dini hizi anayemdhukuru Allaah katika wakati huu isipokuwa nyinyi tu.” Hapo ikateremka Aayah:
لَيْسُوا سَوَاءً ۗ مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ
Hawako sawa sawa. Miongoni mwa Watu wa Kitabu…
mpaka mwisho wa Aayah 115. [Hadiyth ya Ibn Mas’uwd ameipokea Al-Imaam Ahmad]
Links
[1] http://alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8221&title=113-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20Aal-%27Imraan%20Aayah%20113%3A%20%D9%84%D9%8E%D9%8A%D9%92%D8%B3%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D8%B3%D9%8E%D9%88%D9%8E%D8%A7%D8%A1%D9%8B%20%DB%97%20%D9%85%D9%90%D9%91%D9%86%D9%92%20%D8%A3%D9%8E%D9%87%D9%92%D9%84%D9%90%20%D8%A7%D9%84%D9%92%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%90%20%D8%A3%D9%8F%D9%85%D9%91%D9%8E%D8%A9%D9%8C%20%D9%82%D9%8E%D8%A7%D8%A6%D9%90%D9%85%D9%8E%D8%A9%D9%8C%20%D9%8A%D9%8E%D8%AA%D9%92%D9%84%D9%8F%D9%88%D9%86%D9%8E%20%D8%A2%D9%8A%D9%8E%D8%A7%D8%AA%D9%90%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%91%D9%8E%D9%80%D9%87%D9%90%20