Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Fataawaa: Hukmu Mbali Mbali Za Swawm > 08-Imaam Ibn Qudaamah Al-Maqdisiy: Mwanamke Anayelazimishwa Kujimai Wakati Wa Ramadhwaan

08-Imaam Ibn Qudaamah Al-Maqdisiy: Mwanamke Anayelazimishwa Kujimai Wakati Wa Ramadhwaan

Mwanamke Anayelazimishwa Kujimai Wakati Wa Ramadhwaan

 

Imaam Ibn Qudaamah Al-Maqdisiy

 

www.alhidaaya.com [1]

 

 

SWALI:

 

Ikiwa mwanamke atalazimishwa jimai, halazimiki kulipa kafara, bali analazimika kulipa  tu siku hiyo?

 

JIBU:

 

 Muhannaa kasema:  "Nilimuuliza Ahmad kama mwanamke aliyebakwa analazimika kulipa siku hiyo.  Akasema: "Ndiyo." Pia nikamuuliza kama analazimika kulipa kafara, akasema: "Hapana!"

 

Maoni haya anakubaliana nayo pia al-Hasan, Ath-Thawriy, Al-Awza'iy na Hanafiyyah. 

 

Kulingana na swali hili, inamuhusu pia mwanamke ambaye kaingiliwa wakati amelala.

 

Maalik kasema kuhusiana na mwanamke aliyelala: "Ni juu yake kulipa siku hiyo, ila hatolipa kafara. Ama kuhusiana na mwanamke ambaye amelazimishwa kujimai, analazimika kulipa siku hiyo na kutoa kafara.”

 

Ash-Shaafi'iy, Abuu Ath-Thawriy na Ibnul-Mundhir wanasema ikiwa ataingiliwa jimai  kwa matisho, basi wana maoni sawa na sisi.

 

[Al-Mughniy (4/376) Daar 'Alaam-il-kutub, 1419/1999]

 

 

 

Share [2]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/8382

Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8382&title=08-Imaam%20Ibn%20Qudaamah%20Al-Maqdisiy%3A%20Mwanamke%20Anayelazimishwa%20Kujimai%20Wakati%20Wa%20Ramadhwaan