Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Fataawaa: Twawaaf Na Sa'y > 10-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Amefanya Twawaaful-Widaa'i Kisha Hakuweza Kuondoka Makkah Wakati Huo

10-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Amefanya Twawaaful-Widaa'i Kisha Hakuweza Kuondoka Makkah Wakati Huo

 

Amefanya Twawaaful-Widaa'i Kisha Hakuweza Kuondoka Makkah Wakati Huo

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com [1]

 

 

SWALI:

 

Mtu amefanya Hajj, alipomaliza kafanya twawaaful-widaa'i usiku lakini akashindwa kuondoka Makkah baada ya twawaaf, hivyo akabakia Makkah hadi asubuhi kisha akasafiri. Nini hukmu ya yake?

 

JIBU:

 

Shariy’ah inavyopasa ni kuwa twawaaful-widaa'i iwe pindi mtu anapokuwa tayari kuondoka Makkah pale pale kutokana na Hadiyth kutoka kwa Ibn 'Abbaas: "Watu waliamrishwa kuwa kitendo chao cha mwisho (kabla ya kuondoka Makkah) kiwe ni twawaaf katika Ka'abah, isipokuwa kwa wanawake wenye hedhi". [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

Hivyo ikiwa alifanya twawaaf kwa niyyah ya kuondoka usiku kisha akazuilika hadi asubuhi, basi hakuna ubaya In Shaa Allaah. Akiweza kurudia twawaaful-widaa'i kabla ya kuondoka ni bora zaidi.

 

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 [Fataawa al-Hajj wal-'Umrah waz-Ziyaarah – Uk.84]

 

 

 

Share [2]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/9250

Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9250&title=10-Al-Lajnah%20Ad-Daaimah%3A%20Amefanya%20Twawaaful-Widaa%27i%20Kisha%20Hakuweza%20Kuondoka%20Makkah%20Wakati%20Huo%20