Shaykh Fawzaan: Sha'baan: Je Laylatul-Qadr Inatokea Katika Nisfwu Sha'baan?

 

Je, Laylatul-Qadr Inatokea Katika Nisfwu Sha'baan?

 

Shaykh Swaalih bin Fawzaan Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

SWALI:

 

Je, Laylatul-Qadr inakuwa tarehe 15 Sha'baan?

 

 

JIBU:

 

Hapakuthibiti fadhila yoyote katika usiku wa Niswfu Sha´baan inayotofautiana na masiku wala usiku wowote wa mwezi wa Sha´baan. Hapakuthibiti lolote katika hili.

 

Vilevile wanasema kuwa Laylatul-Qadr inakuwa katika usiku wa Niswfu Sha´baan, si kweli. Laylatul-Qadr inakuwa katika Ramadhwaan. Kwa sababu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)  Amesema:

إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ ﴿١﴾

1. Hakika Sisi Tumeiteremsha Qur-aan katika Laylatil-Qadr (usiku wa Qadar). [Al-Qadr: 01]

 

Laylatul-Qadr inakuwa katika masiku kumi ya mwisho ya Ramadhwaan. Hili ni kwa Ijmaa´. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anaitafuta katika Ramadhwaan na hakuwa anaitafuta katika mwezi wa Sha´baan.

 

Wapi wametoa haya kwamba Laylatul-Qadr inakuwa katika usiku wa Niswfu Sha´baan?

 

 

[Al-Mawqi’ Ar-Rasmiy li-Ma’aaliy Ash-Shaykh Ad-Duktuwr Swaalih bin Fawzaan Bin ‘Abdillaah Al-Fawzaan]

 

 

Share