Skip navigation.
Home kabah

Nasiha Ya Ijumaa

Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Mwezi Mtukufu Wa Rajab

 

AlhamduliLLaah. Inapasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Kutupa umri hadi kutufikisha katika mwezi huu mtukufu wa Rajab ambao ni fursa kwetu kutenda mema yatakayotuchumia thawabu nyingi kuliko miezi mingine. Mema ambayo hatuna budi kuyatenda kwa ajili ya kujenga Aakhirah yetu kabla ya siku hii kufika. Siku ambayo hakuna mmoja wetu yeyote atakayeweza kuikwepa. Basi hebu kila mmoja wetu ajiulize: "Nimetanguliza nini kwa ajili ya siku hiyo?" Siku ambayo safari yake ni ndefu mno. Mahmaa tutakavyobeba zawadi huko hazitoshi wala hatuna hakika nazo kama zitapendekezeka au zitakuwa na thamani huko tuendako ambako kuna makazi ya milele tusiyokuwa na hakika nayo; ima moto au Pepo.   

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

(( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ وَاتَّقُوا اللَّهَ إِنَّ اللَّهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ))

 

((Enyi mlioamini! Mcheni Allaah,, na kila nafsi iangalie inayoyatanguliza kwa ajili ya Kesho. Na mcheni Allaah, Hakika Allaah, Anazo khabari ya mnayoyatenda)) [Al-Hashr: 18]

 

Mpya - Maswali

 TAFADHALI SOMA MAELEZO MUHIMU KABLA YA KUTUMA MASWALI

1- Tunasikitika kuona kwamba Maswali mengi yanayotumwa na baadhi ya ndugu zetu yameshaulizwa kabla na kujibiwa. Wenye kutuma Maswali mnaombwa kwanza kutafuta Maswali na Majibu yenu katika milango (categories) inayohusika kwani mengi mno yameshaulizwa na kujibiwa. Mnaweza pia kutafuta Maswali kwa kuweka maneno machache ya maudhui unayotaka kuuliza katika 'Search'.  Kufanya hivyo, mtaweza kupata majibu kwa haraka zaidi na pia mtahifadhi muda wenu na wetu.
 
2- Ikiwa unataka kutuma maswali zaidi ya moja tafadhali tuma KILA SWALI katika barua ya pekee na uweke maudhui (Subject) iliyo wazi ili iwe wepesi kufuatilia na kuweza kukujibuni haraka.
 
Tunatumai kupata ushirikiano wenu mwema ili mtufanyie wepesi hizi kazi  ambazo ni nyingi sana  khaswa  za Maswali  na watendaji ni wachache sana.
 
Jazaakum Allaahu Khayra.