Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة النفخ في الشراب
14-Mlango Wa Karaha ya Kupulizia Ndani ya Kinywaji
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
عن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم نَهَى عَن النَّفْخ في الشَّرَاب ، فَقَالَ رَجُلٌ : القَذَاةُ أراها في الإناءِ ؟ فَقَالَ : (( أهرقها )) . قَالَ : إنِّي لا أرْوَى مِنْ نَفَسٍ وَاحدٍ ؟ قَالَ : (( فَأَبِنِ القَدَحَ إِذَاً عَنْ فِيكَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kupulizia ndani ya kinywaji. Akasema mtu mmoja: "Je, nitafanyaje kuhusu vitu vinavyoelea katika kinywaji?" Akasema: "Vitoe." Akasema: "Kiu yangu haimaliziki kwa mkupuo mmoja." Akasema: "Unaweza kupumua, lakini kiweke chombo nje ya mdomo wako." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 2
وعن ابن عباس رضي الله عنهما : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم نهى أن يُتَنَفَّسَ في الإناءِ أَوْ يُنْفَخَ فِيهِ . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kupumulia ndani ya chombo na kupulizia ndani yake." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10989&title=14-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Karaha%20ya%20Kupulizia%20Ndani%20ya%20Kinywaji