Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الأمر بتعهد القرآن والتحذير عن تعريضه للنسيان
02-Mlango Wa Kuchunga Qur-aan na Kutahadharishwa Kupelekea Kwenye Kuisahau
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
عن أَبي موسى رضي اللهُ عنه، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( تعاهدوا هَذَا القُرْآنَ ، فَوَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لَهُوَ أشَدُّ تَفَلُّتاً مِنَ الإبلِ فِي عُقُلِهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ichungeni hii Qur-aan naapa kwa ambaye nafsi ya Muhammad iko mikononi mwake hakika hii Qur-aan inaponyoka haraka mno kuliko ngamia kutoka kwenye kamba yake aliyefungiwa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّمَا مَثَلُ صَاحبِ الْقُرْآنِ كَمَثَلِ الإِبِلِ المُعَقَّلَةِ ، إنْ عَاهَدَ عَلَيْهَا أمْسَكَهَا ، وَإنْ أطْلَقَهَا ذَهَبَتْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika mfano wa mwenye kuhifadhi Qur-aan ni sawa na mwenye ngamia waliofungwa kama ataendelea kuwafunga atakuwa nao na kama atawaachilia wataondoka na kukimbia." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11096&title=02-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuchunga%20Qur-aan%20na%20Kutahadharishwa%20Kupelekea%20Kwenye%20Kuisahau