Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تجويز صلاة الضحى من ارتفاع
الشمس إِلَى زوالها والأفضل أن تُصلَّى عِنْدَ
اشتداد الحر وارتفاع الضحى
28-Mlango Wa Kufaa Swalaah ya Dhuwhaa Kuanzia Linaponyanyuka Jua Mpaka Kupinduka (Zawaal), na Bora ni Kuiswali Wakati Jua Linapokuwa Kali
Alhidaaya.com [1]
عن زيد بن أَرْقَم رضي اللهُ عنه : أنَّهُ رَأَى قَوْماً يُصَلُّونَ مِنَ الضُّحَى ، فَقَالَ : أمَا لَقَدْ عَلِمُوا أنَّ الصَّلاَةَ في غَيْرِ هذِهِ السَّاعَةِ أفْضَلُ ، إنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( صَلاَةُ الأَوَّابِينَ حِيْنَ تَرْمَضُ الفِصَالُ )) رواه مسلم .
Zayd bin Arqam (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Aliona watu wanaswali Dhuwhaa, akasema: Ama kwa hakika hawajajua kwamba Swalaah katika wakati mwingine usiokuwa huu ni bora zaidi kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalaah ya Awwaabiyn (wanaorudi kutoka kwa kughafika wakaja kuhudhuria na kutoka katika dhambi kuelekea kwa tauba na msamaha) ni wakati wa jua kali ambapo watoto wa ngamia hukusanywa." [Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11208&title=28-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kufaa%20Swalaah%20ya%20Dhuwhaa%20Kuanzia%20Linaponyanyuka%20Jua%20Mpaka%20Kupinduka%20%28Zawaal%29%2C%20na%20Bora%20ni%20Kuiswali%20Wakati%20Jua%20Linapokuwa%20Kali