Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب ركعتين بعد الوضوء
30-Mlango Wa Kupendeza Kuswali Rak'ah Mbili Baada Wudhuu
Alhidaaya.com [1]
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ لِبِلاَلٍ : (( يَا بِلاَلُ ، حَدِّثْنِي بِأَرْجَى عَمَلٍ عَمِلْتَهُ فِي الإسْلاَمِ ، فَإنِّي سَمِعْتُ دَفَّ نَعْلَيْكَ بَيْنَ يَدَيَّ في الجَنَّةِ )) قَالَ : مَا عَمِلْتُ عَمَلاً أرْجَى عِنْدي مِنْ أَنِّي لَمْ أتَطَهَّرْ طُهُوراً فِي سَاعَةٍ مِنْ لَيْلٍ أَوْ نَهَارٍ إِلاَّ صَلَّيْتُ بِذَلِكَ الطُّهُورِ مَا كُتِبَ لِي أنْ أُصَلِّي . متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimuuliza Bilaal (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Ee Bilaal! Niambie amali uliyoifanya katika Uislamu, kwani mimi nimesikia sauti ya viatu vyako ukiwa mbele yangu Peponi." Akasema: "Sijafanya amali yoyote ambayo kwayo natarajia hayo isipokuwa ninapojitwahirisha katika wakati wowote wa usiku au mchana ila huswali kwa tohara hiyo zile Alizoniandikia Allaah kuziswali." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11210&title=30-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kuswali%20Rak%27ah%20Mbili%20Baada%20Wudhuu