Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب صوم الإثنين والخميس
50-Mlango Wa Kupendeza Kufunga Jumatatu na Alkhamis
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
عن أَبي قتادة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم سُئِلَ عَنْ صَومِ يَوْمِ الإثْنَيْنِ ، فَقَالَ : (( ذَلِكَ يَومٌ وُلِدْتُ فِيهِ ، وَيَومٌ بُعِثْتُ ، أَوْ أُنْزِلَ عَلَيَّ فِيهِ )) رواه مسلم .
Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu funga ya Jumatatu, akasema: "Hiyo ni siku niliyozaliwa na ni siku niliyopewa Utume au niliyoteremshiwa Wahyi nadani yake." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( تُعْرَضُ الأَعْمَالُ يَومَ الإثْنَيْنِ وَالخَمِيسِ ، فَأُحِبُّ أنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأنَا صَائِمٌ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) ، ورواه مسلم بغير ذِكر الصوم .
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kwa hakika matendo ya waja huonyeshwa siku ya Jumatatu na Alkhamisi, hivyo napenda amali zangu zionyeshwe nami nikiwa nimefunga." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan], Na ameipokea Muslim bila kutaja funga.
Hadiyth – 3
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَتَحَرَّى صَومَ الإثْنَيْنِ وَالخَمِيس . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) ameema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akifunga sana siku ya Jumatatu na Alkhamisi. [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11230&title=50-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kufunga%20Jumatatu%20na%20Alkhamis