KUMSAHIHISHA IMAAM
Ametoa (صلى الله عليه وآله وسلم)mfano katika kumsahihisha Imaam anapobabaika au anapochanganyikiwa na kisomo chake. Mara moja aliswali, akasoma ndani yake kisomo, akasahau. Alipomaliza alimwambia Ubayy: ((Uliswali na sisi?)). Alijibu: "Ndio". Akasema: ((Hivyo nini kilichokuzuia [kunisahihisha]?))([1]).
KUJIKINGA NA SHAYTWAAN NA KUTEMA MATE KIDOGO WAKATI WA SWALAH ILI KUONDOSHA WASIWASI
'Uthmaan bin Abil-Aasw (رضي الله عنه) alimwambia: "Ewe Mjumbe wa Allaah! Shaytwaan ameingia baina yangu na baina ya Swalah yangu na kisomo changu, ananibabaisha katika kisomo changu!" Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Huyo ni Shaytwaan anayeitwa Khinzab, hivyo utakapomuhisi jikinge kwa Allaah naye, na tema mate kidogo([2]) upande wa kushoto kwako mara tatu)). Akasema: "Nikafanya hivyo, na Allaah Akamuondoshelea mbali nami".([3]).
[1] Abu Daawuud, Ibn Hibbaan, Atw-Twabaraaniy, Ibn 'Asaakir (2/296/2) na Adhw-Dhwiyaa katika Al-Mukhtaarah kwa isnaad Swahiyh.
[2] "At-Tafl" ni mpulizo ikiwa na mate kidogo, hivyo ni zaidi ya kupuliza. (An-Nihaayah).
[3] Muslim na Ahmad. An-Nawawiy (رحمه الله) amesema: "Hadiyth hii ina mapendekezo ya kujikinga na Shaytwaan anaposhawishi, pamoja na kutema mate upande wa kushoto mara tatu".
Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F3411&title=031-Sifa%20Ya%20Swalah%20Ya%20Mtume%20%28Swalla%20Allaahu%20%27Alayhi%20Wa%20Aalihi%20Wa%20Sallam%29%3A%20Kumsahihisha%20Imaam%20Na%20Kujikinga%20Na%20Shaytwaan