Kutazama Mswahafu Bila Ya Kutamka Kitu
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu-Allaah)
Alhidaaya.com [2]
Hakuna ubaya kutazama Qur-aan bila ya kuisoma kwa ajili ya kuzingatia na kutia akilini na kuifahamu maana, lakini haitohesabiwa kuwa ni kuisoma wala hatopata mtu fadhila za kusoma isipokuwa ikiwa ataitamka Qur-aan hata ikiwa hatomsikia aliye karibu naye kutokana na kauli ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((Someni Qur-aan kwani itakuja Siku ya Qiyaamah ikiwa ni kiombezi kwa Swahibu wake)) [Muslim]
Na alokusudia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa ni ‘Swahibu wake’ ni wale ambao wanaifanyia kazi kama vile ilivyotajwa katika Hadiyth nyingine. Na akasema:
((Atakayesoma herufi moja katika Qur-aan atapata kwayo hasanah (jema) moja, na hasanah moja ni sawa na kumi mfano wake)) [At-Tirmidhiy na Ad-Daarimiy].
Wala hatohesabiwa kuwa ni kuisoma isipokuwa aitamke kama walivyonukuu Ahlul-‘Ilm (‘Ulamaa).
[Fataawaa Manshuwrah fiy Mawqi’ Rasmiy li ibn Baaz]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/205
[2] http://www.alhidaaya.com
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8529&title=Imaam%20Ibn%20Baaz%3A%20Kutazama%20Mswahafu%20Bila%20Ya%20Kutamka%20Kitu