Je, Laylatul-Qadr Inatokea Katika Nisfwu Sha'baan?
Shaykh Swaalih bin Fawzaan Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)
Alhidaaya.com [2]
SWALI:
Je, Laylatul-Qadr inakuwa tarehe 15 Sha'baan?
JIBU:
Hapakuthibiti fadhila yoyote katika usiku wa Niswfu Sha´baan inayotofautiana na masiku wala usiku wowote wa mwezi wa Sha´baan. Hapakuthibiti lolote katika hili.
Vilevile wanasema kuwa Laylatul-Qadr inakuwa katika usiku wa Niswfu Sha´baan, si kweli. Laylatul-Qadr inakuwa katika Ramadhwaan. Kwa sababu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amesema:
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ ﴿١﴾
1. Hakika Sisi Tumeiteremsha Qur-aan katika Laylatil-Qadr (usiku wa Qadar). [Al-Qadr: 01]
Laylatul-Qadr inakuwa katika masiku kumi ya mwisho ya Ramadhwaan. Hili ni kwa Ijmaa´. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anaitafuta katika Ramadhwaan na hakuwa anaitafuta katika mwezi wa Sha´baan.
Wapi wametoa haya kwamba Laylatul-Qadr inakuwa katika usiku wa Niswfu Sha´baan?
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/208
[2] http://www.alhidaaya.com/
[3] http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/liqo-24-07-1435-01.mp3
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9069&title=Shaykh%20Fawzaan%3A%20Sha%27baan%3A%20Je%20Laylatul-Qadr%20Inatokea%20Katika%20Nisfwu%20Sha%27baan%3F