كِتَابُ اَلْجِنَايَاتِ
Kitabu Cha Jinai (Na Kisasi)
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْجِنَايَاتِ
Kitabu Cha Jinai
بَابُ اَلْجِنَايَاتِ
00-Mlango Wa Makosa Ya Jinai[1]
992.
عَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَحِلُّ دَمُ اِمْرِئٍ مُسْلِمٍ، يَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اَللَّهُ، وَأَنِّي رَسُولُ اَللَّهِ، إِلَّا بِإِحْدَى ثَلَاثٍ: اَلثَّيِّبُ اَلزَّانِي، وَالنَّفْسُ بِالنَّفْسِ، وَالتَّارِكُ لِدِينِهِ، اَلْمُفَارِقُ لِلْجَمَاعَةِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halaal damu ya mtu Muislam anayeshuhudia kuwa hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah na kuwa mimi ni Rasuli wa Allaah ila kwa mojawapo ya mambo matatu:[2] Mzinifu aliyeoa, nafsi kwa nafsi na aliyeacha Dini yake (aliyeritadi) aliyefarikiana na jamaa (umoja wa Waislam).” [Bukhaariy, Muslim]
993.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، عَنْ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَحِلُّ قَتْلُ مُسْلِمٍ إِلَّا فِي إِحْدَى ثَلَاثِ خِصَالٍ: زَانٍ مُحْصَنٌ فَيُرْجَمُ، وَرَجُلٌ يَقْتُلُ مُسْلِمًا مُتَعَمِّدًا فَيُقْتَلُ، وَرَجُلٌ يَخْرُجُ مِنْ اَلْإِسْلَامِ فَيُحَارِبُ اَللَّهَ وَرَسُولَهُ، فَيُقْتَلُ، أَوْ يُصْلَبُ، أَوْ يُنْفَى مِنْ اَلْأَرْضِ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halaal kumuua Muislam ila kwa mojawapo ya mambo matatu: mzinifu aliyehifadhika atapigwa mawe, mtu anayemuua Muislam kwa makusudi naye atauawa, na mtu anayetoka katika Uislam, akawa anampiga vita Allaah na Rasuli wake atauawa, au atasulubiwa na atatolewa katika nchi.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na akaisahihisha Al-Haakim]
994.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَوَّلُ مَا يُقْضَى بَيْنَ اَلنَّاسِ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ فِي اَلدِّمَاءِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Abdillaah bin Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Jambo la kwanza watakalohukumiwa watu siku ya Qiyaamah ni katika damu.”[3] [Bukhaariy, Muslim]
995.
وَعَنْ سَمُرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ قَتَلَ عَبْدَهُ قَتَلْنَاهُ، وَمَنْ جَدَعَ عَبْدَهُ جَدَعْنَاهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَهُوَ مِنْ رِوَايَةِ اَلْحَسَنِ اَلْبَصْرِيِّ عَنْ سَمُرَةَ، وَقَدْ اُخْتُلِفَ فِي سَمَاعِهِ مِنْهُ
وَفِي رِوَايَةٍ لِأَبِي دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيِّ: {وَمَنْ خَصَى عَبْدُهُ خَصَيْنَاهُ} وَصَحَّحَ اَلْحَاكِمُ هَذِهِ اَلزِّيَادَةَ
Kutoka kwa Samurah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kumuua mtumwa wake, nasi tutamuua, na mwenye kumkata pua mtumwa wake na si tutamkata.”[4] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah), na At-Tirmidhiy amesema ni Hasan nayo ni katika Riwaayah ya Al-Hasan Al-Baswriy kutoka kwa Samurah, wametofautiana katika kusikia kwake kwa Samurah au sivyo]
Katika Riwaayah ya Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy kuna ziada hii: “…na mwenye kumhasi mtumwa wake na sisi tutamhasi.” Al-Haakim ameipa daraja ya sahihi ziada hii.
996.
وَعَنْ عُمَرَ بْنِ اَلْخَطَّابِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ:{لَا يُقَادُ اَلْوَالِدُ بِالْوَلَدِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ اَلْجَارُودِ وَالْبَيْهَقِيُّ، وَقَالَ اَلتِّرْمِذِيُّ: إِنَّهُ مُضْطَرِبٌ
Kutoka kwa ‘Umar bin Al Khatwaab (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Baba halipizwi kisasi kwa mwanawe.”[5] [Imetolewa na Ahmad, At-Tirmidhiy na Ibn Maajah, na akaisahihisha Ibn Al-Jaaruwd na Al-Bayhaqiyy. Na akasema At-Tirmidhiy ni ‘Mudhwtwarib’][6]
997.
وَعَنْ أَبِي جُحَيْفَةَ قَالَ: {قُلْتُ لَعَلِيٍّ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا: هَلْ عِنْدَكُمْ شَيْءٌ مِنْ اَلْوَحْيِ غَيْرَ اَلْقُرْآنِ ؟ قَالَ: لَا وَاَلَّذِي فَلَقَ اَلْحَبَّةَ وَبَرَأَ اَلنِّسْمَةَ، إِلَّا فَهْمٌ يُعْطِيهِ اَللَّهُ رَجُلًا فِي اَلْقُرْآنِ، وَمَا فِي هَذِهِ اَلصَّحِيفَةِ. قُلْتُ: وَمَا فِي هَذِهِ اَلصَّحِيفَةِ ؟ قَالَ: "اَلْعَقْلُ، وَفِكَاكُ اَلْأَسِيرِ، وَلَا يُقْتَلُ مُسْـلِمٌ بِكَافِرٍ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
وَأَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ: مِنْ وَجْهٍ آخَرَ عَنْ عَلِيٍّ وَقَالَ فِيهِ: {اَلْمُؤْمِنُونَ تَتَكَافَأُ دِمَاؤُهُمْ، وَيَسْعَى بِذِمَّتِهِمْ أَدْنَاهُمْ، وَهُمْ يَدٌ عَلَى مَنْ سِوَاهُمْ، وَلَا يُقْتَلُ مُؤْمِنٌ بِكَافِرٍ، وَلَا ذُو عَهْدٍ فِي عَهْدِهِ} وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa Abuu Juhayfah amesema: Nilisema kumuambia ‘Aliy: Nyinyi mna chochote katika Wahyi isiyokuwa Qur-aan?[7] Akasema: Hapana naapa kwa Aliyepasua mbegu na Akaumba nafsi, isipokuwa fahamu Allaah Humpa mtu katika Qur-aan (kuielewa), na yaliyomo katika sahifa (karatasi) hii. Nikasema katika sahifa hii kuna nini? Akasema: ‘Al ‘aqlu (kanuni za malipo ya damu), diya, kumfungua mateka na Muislam hauwawi kwa kumuua kafiri.[8] [Imetolewa na Al Bukhaariy]
Na wameipokea Ahmad, Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy kwa njia nyingine kutoka kwa ‘Aliy amesema: “Waumini damu zao zinalingana, na anaenda kwa dhima yao aliye karibu nao, nao wako juu ya wengine wala Muumini hauwawi kwa (kumuua) kafiri, wala mwenye mkataba katika mkataba wake.” [Ameisahihisha Al-Haakim]
998.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ جَارِيَةً وُجَدَ رَأْسُهَا قَدْ رُضَّ بَيْنَ حَجَرَيْنِ، فَسَأَلُوهَا: مَنْ صَنَعَ بِكِ هَذَا ؟ فُلَانٌ. فُلَانٌ. حَتَّى ذَكَرُوا يَهُودِيًّا. فَأَوْمَأَتْ بِرَأْسِهَا، فَأُخِذَ اَلْيَهُودِيُّ، فَأَقَرَّ، فَأَمَرَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنْ يُرَضَّ رَأْسُهُ بَيْنَ حَجَرَيْنِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Mjakazi mmoja alipatikana hali ya kuwa kichwa chake kimepondwa katikati ya mawe mawili. Akaulizwa ni nani aliyekufanyia hivi? Ni fulani? Ni fulani? Hadi wakamtaja Myahudi, akaashiria kwa kichwa. “Ndiye” yule Myahudi akashikwa na akaungama. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaamuru kichwa chake kipondwe baina ya mawe mawili.[9] [Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
999.
وَعَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ غُلَامًا لِأُنَاسٍ فُقَرَاءَ قَطَعَ أُذُنَ غُلَامٍ لِأُنَاسٍ أَغْنِيَاءَ، فَأَتَوا اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَلَمْ يَجْعَلْ لَهُمْ شَيْئًا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالثَّلَاثَةُ، بِإِسْنَادٍ صَحِيحٍ
Kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Kijana wa watu mafukara[10] alikata sikio la watu matajiri, wakamuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) basi hawakuwapa chochote. [Imetolewa na Ahmad na Ath-Thalaathah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd) kwa isnaad Swahiyh]
1000.
وَعَنْ عَمْرِوِ بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ، رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَجُلًا طَعَنَ رَجُلًا بِقَرْنٍ فِي رُكْبَتِهِ، فَجَاءَ إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: أَقِدْنِي. فَقَالَ: "حَتَّى تَبْرَأَ". ثُمَّ جَاءَ إِلَيْهِ. فَقَالَ: أَقِدْنِي، فَأَقَادَهُ، ثُمَّ جَاءَ إِلَيْهِ. فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! عَرِجْتُ، فَقَالَ: "قَدْ نَهَيْتُكَ فَعَصَيْتَنِي، فَأَبْعَدَكَ اَللَّهُ، وَبَطَلَ عَرَجُكَ". ثُمَّ نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "أَنْ يُقْتَصَّ مِنْ جُرْحٍ حَتَّى يَبْرَأَ صَاحِبُهُ"} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَأُعِلَّ بِالْإِرْسَالِ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Mtu mmoja alimchoma mtu kwa pembe katika goti lake, (yule aliyedungwa) akamuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Nilipizie kisasi.?” Akamuambia: “Subiri mpaka upone.” Yule mtu akasisitiza: “Nilipizie kisasi.?” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamlipizia kisasi, kisha akamjia tena akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Nimekuwa kiwete.” Akamuambia: “Nilikukataza ukaniasi, Allaah Akakuweke mbali (na Rahma Zake), na ulemavu wako umebatilika.”[11] Kisha Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikataza mtu kulipiziwa kisasi cha jeraha mpaka aliyejeruhiwa apone. [Imetolewa na Ahmad na Ad-Daaraqutwniy na imetiwa ila kuwa ni Mursal]
1001.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {اِقْتَتَلَتِ اِمْرَأَتَانِ مِنْ هُذَيْلٍ، فَرَمَتْ إِحْدَاهُمَا اَلْأُخْرَى بِحَجَرٍ، فَقَتَلَتْهَا وَمَا فِي بَطْنِهَا، فَاخْتَصَمُوا إِلَى رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَضَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنَّ دِيَةَ جَنِينِهَا: غُرَّةٌ، عَبْدٌ أَوْ وَلِيدَةٌ، وَقَضَى بِدِيَةِ اَلْمَرْأَةِ عَلَى عَاقِلَتِهَا. وَوَرَّثَهَا وَلَدَهَا وَمَنْ مَعَهُمْ. فَقَالَ حَمَلُ بْنُ اَلنَّابِغَةِ اَلْهُذَلِيُّ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! كَيْفَ يَغْرَمُ مَنْ لَا شَرِبَ، وَلَا أَكَلَ، وَلَا نَطَقَ، وَلَا اِسْتَهَلَّ، فَمِثْلُ ذَلِكَ يُطَلُّ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "إِنَّمَا هَذَا مِنْ إِخْوَانِ اَلْكُهَّانِ"، مِنْ أَجْلِ سَجْعِهِ اَلَّذِي سَجَعَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَأَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ: مِنْ حَدِيثِ اِبْنِ عَبَّاسٍ، أَنَّ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ سَأَلَ مَنْ شَهِدَ قَضَاءَ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي اَلْجَنِينِ ؟ قَالَ: فَقَامَ حَمَلُ بْنُ اَلنَّابِغَةِ، فَقَالَ: كُنْتُ بَيْنَ اِمْرَأَتَيْنِ، فَضَرَبَتْ إِحْدَاهُمَا اَلْأُخْرَى... فَذَكَرَهُ مُخْتَصَرًا. وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Wanawake wawili wa Hudhayl walipigana, mmoja akamrushia jiwe mwenzie akamuuwa pamoja na kilicho tumboni mwake. Wakashtakiana kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akahukumu: Diya ya mtoto wake (aliyekuwa tumboni)[12] ni mtumwa au mjakazi. Na akahukumu Diya ya mwanamke iwe juu ya jamaa zake (kwa baba). Akamrithisha mwanaye (yule mwanamke) na jamaa zao. Hamal bin An-Naabighat Al Hudhaliy[13] akasema Ee Rasuli wa Allaah! Vipi nimlipe ambaye hajanywa wala hajala, wala hakutamka wala hakulia? Na mfano wao hawalipwi. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema kuhusu mtu huyu: “Huyu ni ndugu wa makuhani.”[14] Kwa sababu ya mizani ya maneno yake anayotoa. [Bukhaariy, Muslim]
Na imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy kutoka katika Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas kuwa: ’Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) aliuliza: Ni nani aliyeshuhudia hukumu ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) katika mtoto aliye tumboni? Hamal bin-An Naabighat akasimama akasema: Nilikuwa ni baina ya wanawake na mmoja kati yao akampiga mwenzie. Akaitaja Hadiyth hii kwa mukhtasari. Na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim
1002.
وَعَنْ أَنَسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلرُّبَيِّعَ بِنْتَ اَلنَّضْرِ عَمَّتَهُ كَسَرَتْ ثَنِيَّةَ جَارِيَةٍ، فَطَلَبُوا إِلَيْهَا اَلْعَفْوَ، فَأَبَوْا، فَعَرَضُوا اَلْأَرْشَ، فَأَبَوْا، فَأَتَوْا رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَأَبَوْا إِلَّا اَلْقِصَاصَ، فَأَمَرَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بِالْقِصَاصِ، فَقَالَ أَنَسُ بْنُ اَلنَّضْرِ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! أَتُكْسَرُ ثَنِيَّةُ اَلرُّبَيِّعِ ؟ لَا، وَاَلَّذِي بَعَثَكَ بِالْحَقِّ، لَا تُكْسَرُ ثَنِيَّتُهَا، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "يَا أَنَسُ! كِتَابُ اَللَّهِ: اَلْقِصَاصُ". فَرَضِيَ اَلْقَوْمُ، فَعَفَوْا، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ : "إِنَّ مِنْ عِبَادِ اَللَّهِ مَنْ لَوْ أَقْسَمَ عَلَى اَللَّهِ لَأَبَرَّهُ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Ar-Rubayyi’ bint An-Nadhwr[15] shangazi yake alivunja meno ya msichana mmoja, wakamuombea msamaha, wakakataa, wakawapa fidia ya jeraha, wakakataa, wakaenda kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) wakakataa ila kisasi. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaamuru walipiziwe kisasi. Anas bin An-Nadhwr[16] akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Meno ya mbele ya Ar-Rubayyi’ yavunjwe, haiwezekani! Naapa kwa Alyekutuma kwa haki meno yake hayatavunjwa. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ee Anas Kitabu cha Allaah ni kulipa kisasi.” Watu wakaridhia wakamsamehe. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Hakika miongoni mwa waja wa Allaah kuna ambao lau atamuapia Allaah (kwa jambo) Anamfanyia.”[17] [Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
1003.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ قُتِلَ فِي عِمِّيَّا أَوْ رِمِّيَّا بِحَجَرٍ، أَوْ سَوْطٍ، أَوْ عَصًا، فَعَلَيْهِ عَقْلُ اَلْخَطَإِ، وَمِنْ قُتِلَ عَمْدًا فَهُوَ قَوَدٌ، وَمَنْ حَالَ دُونَهُ فَعَلَيْهِ لَعْنَةُ اَللَّهِ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ، بِإِسْنَادٍ قَوِيٍّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuuwawa kwa (‘Immiyyan)[18] au kwa kurushiwa jiwe, mjeledi au fimbo, basi diya yake ni diya ya kuuwawa kimakosa. Na mwenye kuuwawa kwa makusudi atalipiziwa kisasi. Atakayeweka pingamizi baina ya hayo yaliyotajwa na baina ya msimamizi wa aliyeuwawa basi laana ya Allaah Iwe juu yake.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Ibn Maajah kwa isnaad ya nguvu]
1004.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِذَا أَمْسَكَ اَلرَّجُلُ اَلرَّجُلَ، وَقَتَلَهُ اَلْآخَرُ، يُقْتَلُ اَلَّذِي قَتَلَ، وَيُحْبَسُ اَلَّذِي أَمْسَكَ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ مَوْصُولًا وَمُرْسَلًا، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ اَلْقَطَّانِ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ، إِلَّا أَنَّ اَلْبَيْهَقِيَّ رَجَّحَ اَلْمُرْسَلَ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtu atakapomzuia mtu, na mtu mwingine akamuuwa, aliyeuwa atauwawa na yule aliyemzuia[19] atafungwa.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniy ikiwa ni Mursal na akaisahihisha Ibn Al-Qatwaan, wapokezi wake ni madhubuti lakini Al-Bayhaqiyy ametilia nguvu kuwa ni Mursal]
1005.
وَعَنْ عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ بْنِ الْبَيْلَمَانِيِّ، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَتَلَ مُسْلِمًا بِمَعَاهِدٍ. وَقَالَ: "أَنَا أَوْلَى مَنْ وَفَى بِذِمَّتِهِ} أَخْرَجَهُ عَبْدُ اَلرَّزَّاقِ هَكَذَا مُرْسَلًا. وَوَصَلَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، بِذِكْرِ اِبْنِ عُمَرَ فِيهِ، وَإِسْنَادُ اَلْمَوْصُولِ وَاهٍ
Kutoka kwa ‘Abdi Rahmaan bin Al-Baylamaaniy[20] amesema kuwa: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuuwa Muislam kwa kumlipizia kafiri mwenye mkataba[21] na akasema: “Mimi ni aula wa kutekeleza dhima yake.” [Imetolewa na ‘Abdu Razzaaq ameipokea ikiwa ni Mursal. Ad-Daaraqutwniy amesema ni Mawsuwl kwa kutajwa Ibn ‘Umar ndani yake. Isnaad yake Mawsuwl ni dhaifu sana]
1006.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {قُتِلَ غُلَامٌ غِيلَةً، فَقَالَ عُمَرُ: لَوْ اِشْتَرَكَ فِيهِ أَهْلُ صَنْعَاءَ لَقَتَلْتُهُمْ بِهِ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: Kijana mmoja aliuwawa kwa kuviziwa,[22] ‘Umar akasema lau watu wa Swan’aa wangalishirikiana katika mauaji yake ningaliwauwa kwa sababu yake. [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1007.
وَعَنْ أَبِي شُرَيْحٍ اَلْخُزَاعِيِّ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {فَمَنْ قُتِلَ لَهُ قَتِيلٌ بَعْدَ مَقَالَتِي هَذِهِ، فَأَهْلُهُ بَيْنَ خِيَرَتَيْنِ: إِمَّا أَنْ يَأْخُذُوا اَلْعَقْلِ. أَوْ يَقْتُلُوا} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ وَأَصْلُهُ فِي "اَلصَّحِيحَيْنِ" مِنْ حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَةَ بِمَعْنَاهُ
Kutoka kwa Abuu Shurayh Al-Khuzaa’iy[23] amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuuawa mtu wake baada ya maneno yangu haya basi watu wake wako baina ya khiyari mbili: ima wachukue diya au nao waue.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy. Asili ya hadiyth hii iko katika sahihi mbili kutoka katika hadiyth ya Abuu Hurayrah kwa maana kama hiyo]
[1] Jinayaat ni wingi wa Jinaya yenye maana ya “Kumdhuru mtu kwa kumpa adhabu ya kiwiliwili.” Vyovyote iwavyo kama ni kwa bahati mbaya au kwa makusudi.
[2] Hairuhusiwi kumuua aliyetoa Shahaadah. Mzinifu aliyeoa, muuwaji, na aliyeritadi wanauliwa. Katika Hadiyth moja tunajifunza kuwa ni ruhusa kuuwa kwa kujilinda ikitokezea mtu kuja kwa niyyah ya kuuwa. Hili ni jambo la nne katika yanayoruhusiwa kwa aliyetoa Shahaadah. Neno nafsi kwa nafsi iliyotajwa kwa Hadiyth hii ni kuuwa kwa kulipiza kisasi.
[3] Hii inaonyesha kuwa kuuwa ni moja katika madhambi makubwa sana. Ni kanuni ya msingi kuwa jambo kubwa zaidi huwa linatangulizwa zaidi, na madamu ya kuwa mauwaji ni dhambi kubwa zaidi basi na hukumu yake ndiyo itakayokuwa ya mwanzo siku ya Qiyaamah. Vivyo hivyo kwa kuwa majukumu ya watu kuswali hutangulizwa kuliko kingine chochote nacho ndicho kitakachoulizwa mwanzo hali kadhalika.
[4] ‘Ulamaa wamekubaliana kuwa mtumwa atakatwa kichwa chake kwa mauaji ya muungwana. Hata hivyo kuna rai tofauti ya ‘Ulamaa ikiwa naye muungwana atakatwa kichwa kwa kumuuwa mtumwa.
[5] ‘Ulamaa wengi wa mwanzo wamefuata rai ya kuwa ikiwa baba kamuuwa mwanawe, hawezi kuuliwa kwa kulipizwa kisasi cha mwanawe. Hata hivyo hawezi kukwepa adhabu inayomsubiri siku ya Qiyammaah. Sababu kubwa ya ubaguzi huu ni kuwa baba ndiye msingi na chanzo cha kuwepo kwa mtoto na sio kinyume chake na hivyo hawezi kuwa na haki ya kusitisha maisha ya baba yake.
[6] Al-Khatwaab amesema: “Makusudio ni kuwa zawadi haistahiki ila katika mashindno ya farasi, ngamia na mfano wa wanyama hao na kurusha mishale kwa sababu mambo haya ni maandalizi ya kupambana na adui na kutoa zawadi katika mashindano haya ni kuhimiza watu katika Jihaad.”
[7] Abuu Juhayfah aliuliza swali hili kwa sababu moja katika madhehebu ya Kishia linaamini kuwa pamoja na kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa ni Rasuli wa Allaah aliyekuwa akishushiwa Wahyi na familia yake vile vile walikuwa na sehemu ya wahyi uliokuwa ukiteremka kwao. Abuu Juhayfah alikua anataka muono huu ufutwe kutoka kwao.
[8] Hadiyth hii inajulisha kuwa Muislam hauliwi kwa kulipiza kisasi kwa kumuuwa kafiri. Ikiwa imethibitika kuwa kafiri yule anahusika na nchi iliyo na vita na dola ya Kiislam basi hatouwawa kwa kuuwa kwake. Hii ni kwa mujibu wa kongamano la ‘Ulamaa. Ama ikithibitika kuwa aliyeuwawa ni dhimmi (kafiri anayeishi katika dola ya Kiislam na anayelipa kodi na ambaye yupo chini ya dola ya Kiislam), Maimaam watatu wana rai kuwa Muislam hatouwawa kwa mauaji haya ambapo Imaam wa nne Abuu Hanifa ana rai kuwa ni lazima auwawe.
[9] Hadiyth hii inathibitisha kuwa mtu huuliwa kwa kumuuwa mwanamke. Vivyo hivyo hakuna ubaguzi kwa misingi ya utajiri na umaskini wa mtu baina ya kijana na mtu mzima.
[10] Mtumwa alikata sikio la mtumwa. Sasa watu wakawa wana chaguo: Ni kisasi au kulipa diya. Bwana wa yule mtumwa hakutaka kisasi bali diya. Bwana wa yule mtumwa aliyetenda kosa hakuwa na uwezo wa kulipa na mtumwa mwenyewe hakuwa na uwezo wowote. Aliyeshtakia akawa hajapata chochote. Hii inamaanisha kuwa mwenye kuomba (maskini) hana jukumu la kulipa diya kwa yeyote na familia yake haishurutishwi kwa hilo vile vile. Kulipa fidia inakuwa ni wajibu kwa familia inayotarajia kurithi kutoka kwa mtu huyo. Madamu mtu mwenyewe hana cha kurithiwa, suala la kulipa fidia linakuwa halipo.
[11] Hadiyth hii inatujuvya kuwa mtu asipokee fidia yoyote na asubiri hadi atakapopona kabisa. Hikmah ya jambo hili ni kuthibitika kwa jeraha lenyewe kwa kupona au kutokupona. Suala la fidia litategemea hali atakayokuwa nayo aliyejuruhiwa.
[12] Ikiwa mtoto aliye tumboni alikufa kabla ya kuzaliwa fidiya yake itakuwa ni bei ya kijakazi au mtumwa. Ikiwa mtoto alikufa baada ya kuzaliwa, fidia itakayolipwa itakuwa ni sawa na ngamia mia moja. Mauaji ya kukusudia au mauaji ya bahati mbaya hayahitaji kisasi, bali fidiya tu. Jina la kiarabu ‘Aaqila inafasiriwa kama ni ‘Asaba (jamaa wa karibu) ina maana kuwa fidiya haiwajibiki kwa muuaji peke yake bali kwa jamaa zake wa karibu.
[13] Hamal bin Maalik bin An-Naabighat Al-Hudhaliy Abuu Nadla Al-Basri alikuwa ni Swahaba.
[14] Ni wingi wa kuhani, mpiga ramli.
[15] Ar-Rubayyi’ ni mtoto wa Nadhr bin Damdam bin Zaid bin Haram, alikuwa ni shangazi wa Anas bin Maalik, Swahaba mkubwa aliyekuwa mtumishi wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na alikuwa ni mama wa Haarith bin Suraaqa aliyekufa katika vita vya Badr.
[16] Alikuwa ni kaka yake Ar-Rubayyi’ na alikuwa ni ami yake Anas bin Maalik. Hakushiriki katika vita vya Badr na alikua akijutia hilo kila mara. Hivyo basi, katika siku ya vita vya Uhud, baadhi ya Waislam walipokimbia, alikuenda mstari wa mbele wa maadui mushirikina na kujutia hali ya Waislam na kusema kwa sauti: ”Nasikia harufu ya Jannah katika mlima wa Uhud” alipigana hadi akauwawa.
[17] Maneno haya aliyoyatoa Anas hayakuwa kupinga Shariy’ah ya Allaah. Alifanya kila jitihada lakini alikuwa na Iymaan kubwa na huruma ya Allaah. Kama ingalikuwa vinginevyo basi Rasuli wa Allaah asingemsifu bali angesema kinyume chake. Hadiyth hii inaeleza kuwa kisasi kinachukuliwa hata kwa kutolewa jino la mtu.
[18] ‘Immiyyan ni mtu kuuawa kwa kuchinjwa bila kujulikana muuaji wake au sababu zilizopelekea hilo kutofahamika. Vivyo hivyo, ikiwa mtu atauwawa katika vurugu, kisasi hakitahusika, kwa kuwa hukumu ihusikayo hapa ni Diya (fidiya ya fedha kwa mauaji). Ikiwa mtu amekufa kwa kupigwa na rungu, kupigwa mijeledi, au jiwe, aina hiyo ya mauaji inazingatiwa kuwa ni mauaji ya kukusudia ambayo inahitaji fidiya.
[19] Hadiyth hii inathibitisha kuwa mtu atakayemzuia mtu ili auwawe hauwawi bali atafungwa. Aina ya kifungo itatolewa na Qaadhw, inaweza kuwa ndefu au fupi kulingana na mazingira ya mauaji yenyewe.
[20] Huyu ni ‘Abdur-Rahmaan bin Abuu Zayd, muachwa huru wa ‘Umar bin Al-Khatwaab. Alikuwa ni mkazi wa Madiynah ambaye aliishi Haran. Alikuwa Taabi’i wa kizazi cha sita. Abuu Haatim anamuelezea: “Alikuwa ni dhaifu (katika mapokezi ya hadiyth)” Ibn Hibbaan anamtaja kuwa alikuwa madhubuti. Al Haafidh Abdul-‘Azim anasema kuhusiana naye: “Hakuwa katika watu wenye mamlaka kuhusu Hadiyth.”
[21] Neno la kiarabu lililotumika ni Mu’aahid ambalo lina maana ya kafiri ambaye hana makazi ya kudumu katika dola ya Kiislam na amekwenda katika dola hiyo kwa sababu maalumu baada ya kupata ruhusa kutoka katika dola hiyo. Mauaji ya mtu kama huyo kwa makubaliano ya kongomano la ‘Ulamaa ni haraam. Hata hivyo muuaji Muislam hatolipiziwa kisasi kulingana na ‘Ulamaa wote isipokuwa Abuu Haniyfah.
[22] Tukio lilikua ni watu watatu waliomuuwa kijana mmoja kwa pamoja na kwa kumvizia. ‘Umar alitoa hukmu ya kuuwawa kwa wote. Kuna rai tofauti kama inafaa kwa watu wengi waliomuua mtu mmoja kwa kuuwawa wote. Kauli yenye nguvu ni ile hukumu ya ‘Umar.
[23] Huyu ni ‘Amr bin Khuwaylid bin ‘Amr Al-Kabi Al-‘Adawi Al-Khuzaa’iy alisilimu baada ya Fat-h ya Makkah na alifariki Madiynah katika mwaka wa 68 Hijriyyah.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْجِنَايَاتِ
Kitabu Cha Jinai
بَابُ اَلدِّيَاتِ
01-Mlango Wa Diya[1]
1008.
عَنْ أَبِي بَكْرٍ بْنِ مُحَمَّدٍ بْنِ عَمْرِوِ بْنِ حَزْمٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كَتَبَ إِلَى أَهْلِ اَلْيَمَنِ... فَذَكَرَ اَلْحَدِيثَ، وَفِيهِ: {أَنَّ مَنْ اِعْتَبَطَ مُؤْمِنًا قَتْلاً عَنْ بَيِّنَةٍ، فَإِنَّهُ قَوَدٌ، إِلَّا أَنْ يَرْضَى أَوْلِيَاءُ اَلْمَقْتُولِ، وَإِنَّ فِي اَلنَّفْسِ اَلدِّيَةَ مِائَةً مِنْ اَلْإِبِلِ، وَفِي اَلْأَنْفِ إِذَا أُوعِبَ جَدْعُهُ اَلدِّيَةُ، وَفِي اَللِّسَانِ اَلدِّيَةُ، وَفِي اَلشَّفَتَيْنِ اَلدِّيَةُ، وَفِي اَلذِّكْرِ اَلدِّيَةُ، وَفِي اَلْبَيْضَتَيْنِ اَلدِّيَةُ، وَفِي اَلصُّلْبِ اَلدِّيَةُ، وَفِي اَلْعَيْنَيْنِ اَلدِّيَةُ، وَفِي اَلرِّجْلِ اَلْوَاحِدَةِ نِصْفُ اَلدِّيَةِ، وَفِي الْمَأْمُومَةِ ثُلُثُ اَلدِّيَةِ، وَفِي اَلْجَائِفَةِ ثُلُثُ اَلدِّيَةِ، وَفِي اَلْمُنَقِّلَةِ خَمْسَ عَشْرَةَ مِنْ اَلْإِبِلِ، وَفِي كُلِّ إِصْبَعٍ مِنْ أَصَابِعِ اَلْيَدِ وَالرِّجْلِ عَشْرٌ مِنْ اَلْإِبِلِ، وَفِي اَلسِّنِّ خَمْسٌ مِنْ اَلْإِبِلِ وَفِي اَلْمُوضِحَةِ خَمْسٌ مِنْ اَلْإِبِلِ، وَإِنَّ اَلرَّجُلَ يُقْتَلُ بِالْمَرْأَةِ، وَعَلَى أَهْلِ اَلذَّهَبِ أَلْفُ دِينَارٍ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ فِي "اَلْمَرَاسِيلِ" وَالنَّسَائِيُّ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَأَحْمَدُ، وَاخْتَلَفُوا فِي صِحَّتِهِ
Kutoka kwa Abuu Bakr bin Muhammad bin ‘Amr bin Hazm[2] kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliwaandikia watu wa Yemen akaitaja Hadiyth ndani yake inasema: “Kwa hakika mwenye kumuua Muumin bila ushahidi wa kupasa kuuwawa, basi atalipiziwa kisasi, isipokuwa watakaporidhia wasimamizi wa aliyeuwawa.”[3] Katika kuuwa nafsi kuna diya kamili, nayo ni ngamia mia. Katika pua inapokatwa yote kuna diya kamili. Katika macho mawili kuna diya kamili, katika ulimi kuna diya kamili, katika midomo kuna diya kamili. Katika dhakar (uume) kuna diya kamili, katika dhakari ya mwanamume kuna diya kamili, katika uti wa mgongo kuna diya kamili, katika mguu mmoja kuna nusu ya diya. Katika mpasuko uliokaribia ubongo ni thuluthi ya diya. Katika jeraha lililovunja mifupa ni ngamia kumi na tano. Katika kila kidole miongoni mwa vidole vya mikononi na miguuni ni ngamia kumi. Katika jino ni ngamia watano. Katika jeraha linaloonyesha mfupa ni ngamia watano. Na kwa hakika mwanamume anauawa kwa kuuwa mwanamke. Na wenye dhahabu watatoa dinari elfu moja.”[4] [Imetolewa na Abuu Daawuwd katika kitabu cha Al-Maraasiyl, na An-Nasaaiy, Ibn Khuzaymah, Ibn Al-Jaaruwd, Ibn Hibbaan na Ahmad wamekhitilafiana katika kuswihi kwake]
1009.
وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {دِيَةُ اَلْخَطَأَ أَخْمَاسًا: عِشْرُونَ حِقَّةً، وَعِشْرُونَ جَذَعَةً، وَعِشْرُونَ بَنَاتِ مَخَاضٍ، وَعِشْرُونَ بَنَاتِ لَبُونٍ، وَعِشْرُونَ بَنِي لَبُونٍ} أَخْرَجَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ.
وَأَخْرَجَهُ اَلْأَرْبَعَةُ، بِلَفْظٍ: {وَعِشْرُونَ بِنِي مَخَاضٍ} ، بَدَلَ: {بُنِيَ لَبُونٍ} وَإِسْنَادُ اَلْأَوَّلِ أَقْوَى.
وَأَخْرَجَهُ اِبْنُ أَبِي شَيْبَةَ مِنْ وَجْهٍ آخَرَ مَوْقُوفًا، وَهُوَ أَصَحُّ مِنْ اَلْمَرْفُوعِ
وَأَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ: مِنْ طَرِيقِ عَمْرِوِ بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ رَفَعَهُ: {اَلدِّيَةُ ثَلَاثُونَ حِقَّةً، وَثَلَاثُونَ جَذَعَةً، وَأَرْبَعُونَ خَلِفَةً. فِي بُطُونِهَا أَوْلَادُهَا}
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Diya ya bahati mbaya ni aina tano: hiqqah[5] ishirini, jadha’ah[6] ishirini, banaati makhaadhw[7] ishirini, banaati labuwni[8] ishirini na baniy labuwni[9] ishirini.” [Imetolewa na Ad Daaraqutwniyy]
Na imepokewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) kwa tamshi: “…na baniy makhaadhw ishirini.” Badala ya: “...bin labuwni.” Isnaad ya Hadiyth ya kwanza ina nguvu.
Na Ibn Abiy Shaybah ameipokea kwa njia nyingine mawquwf ndiyo sahihi zaidi kuliko Marfuw’.
Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy wameipokea kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb naye kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake ikiwa ni Marfuw’: “Ad Diyyah ni hiqqah thalathini na jadha’ah thalathini na ngamia arubaini wenye mimba.”
1010.
وَعَنْ اِبْنِ عَمْرٍو رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِنَّ أَعْتَى اَلنَّاسِ عَلَى اَللَّهِ ثَلَاثَةٌ: مَنْ قَتَلَ فِي حَرَمَ اَللَّهِ، أَوْ قَتَلَ غَيْرَ قَاتِلِهِ، أَوْ قَتَلَ لِذَحْلِ اَلْجَاهِلِيَّةِ} أَخْرَجَهُ اِبْنُ حِبَّانَ فِي حَدِيثٍ صَحَّحَهُ
Kutoka kwa Ibn ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika watu wenye majivuno zaidi kwa Allaah ni watatu: mwenye kuuwa katika Haram ya Allaah (Makkah), au akamuuwa asiyeuwa au akauwa kwa kisasi cha kijahiliya.” [Imetolewa na Ibn Hibbaan katika hadiyth aliyoisahihisha]
1011.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {أَلَا إِنَّ دِيَةَ اَلْخَطَأِ شِبْهِ اَلْعَمْدِ مَا كَانَ بِالسَّوْطِ وَالْعَصَا مَائَةٌ مِنَ اَلْإِبِلِ، مِنْهَا أَرْبَعُونَ فِي بُطُونِهَا أَوْلَادُهَا} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr bin Al-‘Aasw (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Jueni diya ya kuuwa (bahati mbaya)[10] na kuuwa kunakofanana na makusudi inayokuwa kwa mjeledi au fimbo (diya yake ni) ngamia mia, katika hao arubaini wenye mimba.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Ibn Maajah, na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
1012.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {هَذِهِ وَهَذِهِ سَوَاءٌ يَعْنِي: اَلْخُنْصَرَ وَالْإِبْهَامَ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
وَلِأَبِي دَاوُدَ وَاَلتِّرْمِذِيَّ:{دِيَةُ اَلْأَصَابِعِ سَوَاءٌ، وَالْأَسْنَانُ سَوَاءٌ: اَلثَّنِيَّةُ وَالضِّرْسُ سَوَاءٌ}
وَلِابْنِ حِبَّانَ:{دِيَةُ أَصَابِعِ اَلْيَدَيْنِ وَالرِّجْلَيْنِ سَوَاءٌ، عَشَرَةٌ مِنْ اَلْإِبِلِ لِكُلِّ إصْبَعٍ}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hiki kwa hiki ni sawa yaani kidole kidogo na kidole gumba.”[11] [Imetolewa na Al Bukhaariy]
Na kutoka kwa Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy: “Diya ya vidole ni sawa, na diya ya meno ni sawa, na diya ya meno ya mbele na magego ni sawa.”
Na Ibn Hibbaan ameipokea: “Diya ya vidole vya mikono na miguu ni sawa na ngamia kumi katika kila kidole.”
1013.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ رَفَعَهُ قَالَ: {مَنْ تَطَبَّبَ وَلَمْ يَكُنْ بِالطِّبِّ مَعْرُوفًا فَأَصَابَ نَفْسًا فَمَا دُونَهَا، فَهُوَ ضَامِنٌ} أَخْرَجَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَهُوَ عِنْدَ أَبِي دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيِّ وَغَيْرِهِمَا، إِلَّا أَنَّ مَنْ أَرْسَلَهُ أَقْوَى مِمَّنْ وَصَلَهُ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kutibu na si mjuzi wa tiba, akauwa nafsi na kusababisha madhara mengine basi atalipa.”[12] [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy na akaisahihisha Al-Haakim. Nayo iko kwa Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na wengine. Isipokuwa alieifanya kuwa ni Mursal ana nguvu zaidi kuliko aliyeifanya Mawsuwl]
1014.
وَعَنْهُ، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {فِي الْمَوَاضِحِ خَمْسٌ، خَمْسٌ مِنْ اَلْإِبِلِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ. وَالْأَرْبَعَةُ. وَزَادَ أَحْمَدُ:{وَالْأَصَابِعُ سَوَاءٌ، كُلُّهُنَّ عَشْرٌ، عَشْرٌ مِنَ اَلْإِبِلِ} وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ.
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Katika majeraha yanayoonesha mfupa ni ngamia watano.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah)]
Na akaongezea Ahmad: “Na vidole vyote ni sawa ngamia kumi kumi.” Na akaisahihisha Ibn Khuzaymah na Ibn Al-Jaaruwd.
1015.
وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {عَقْلُ أَهْلِ اَلذِّمَّةِ نِصْفُ عَقْلِ اَلْمُسْلِمِينَ} رَوَاهُ أَحْمَدُ وَالْأَرْبَعَةُ
وَلَفْظُ أَبِي دَاوُدَ: {دِيَةُ اَلْمُعَاهِدِ نِصْفُ دِيَةِ اَلْحُرِّ}
وَلِلنِّسَائِيِّ: {عَقْلُ اَلْمَرْأَةِ مِثْلُ عَقْلِ اَلرَّجُلِ، حَتَّى يَبْلُغَ اَلثُّلُثَ مِنْ دِيَتِهَا} وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Diya ya ahlu adh-dhimmah[13] ni nusu ya diya ya Waislam.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah)]
Na katika tamshi la Abuu Daawuwd: “Diya ya aliyewekeana mkataba (Mu’aahid) ni nusu ya diya ya aliye huru.”
Na katika An-Nasaaiy: “Diya ya mwanamke ni sawa na diya ya mwanamume hadi ifikie thuluthi katika diya yake.” Na akaisahihisha Ibn Khuzaymah
1016.
وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {عَقْلُ شِبْهِ اَلْعَمْدِ مُغَلَّظٌ مِثْلُ عَقْلِ اَلْعَمْدِ، وَلَا يَقْتَلُ صَاحِبُهُ، وَذَلِكَ أَنْ يَنْزُوَ اَلشَّيْطَانُ، فَتَكُونُ دِمَاءٌ بَيْنَ اَلنَّاسِ فِي غَيْرِ ضَغِينَةٍ، وَلَا حَمْلِ سِلَاحٍ} أَخْرَجَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ وَضَعَّفَهُ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Diya ya kuuwa kunakofanana na makusudi ni diya nzito, mfano wa diya ya kuuwa kwa makusudi aliyeuwa hauwawi,[14] ni shari ya shaytwaan, damu ikamwagika baina ya watu bila ya kuwepo chuki wala kubeba silaha.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniy na ameidhoofisha]
1017.
عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {قَتَلَ رَجُلٌ رَجُلًا عَلَى عَهْدِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَجَعَلَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ دِيَتَهُ اِثْنَيْ عَشَرَ أَلْفًا} رَوَاهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَرَجَّحَ النَّسَائِيُّ وَأَبُو حَاتِمٍ إِرْسَالَهُ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: Mtu mmoja aliuwa mtu katika zama za Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akahukumu diya yake dirhamu elfu kumi na mbili. [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah)
1018.
وَعَنْ أَبِي رِمْثَةَ قَالَ: {أَتَيْتُ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَمَعِي اِبْنِي فَقَالَ: "مَنْ هَذَا ؟" قُلْتُ: اِبْنِي. أَشْهَدُ بِهِ. قَالَ: "أَمَّا إِنَّهُ لَا يَجْنِي عَلَيْكَ، وَلَا تَجْنِي عَلَيْهِ} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ
Kutoka kwa Abuu Rimthah[15] amesema: Nilimuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) pamoja na mtoto wangu, akasema: “Huyu ni nani?” Nikasema ni mtoto wangu nami namshuhudia kuwa huyu ni mwanangu. Akasema: “Hutoulizwa kwa kosa lake, naye hatoulizwa kwa kosa lako.”[16] [Imetolewa na An-Nasaaiy na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Ibn Khuzaymah na Ibn Al-Jaaruwd]
[1] Diya ni malipo ya damu iliyomwagwa. Malipo haya yanalipwa kwa warithi wake.
[2] Huyu ni Abuu Bakr bin Muhammad bin ‘Amr bin Hazm Al-Ansari An-Najari Al-Madaniy Al-Qadhwi. Alikuwa madhubuti, mwenye taqwa na alikuwa mmoja katika waliochangia kwa vitabu sita vya Hadiyth. Alikuwa ni taabi’i wa kizazi cha tano. Mke wake anamuelezea kuwa hakuweza kulala kitandani mwake kwa muda wa miaka arubaini, akimaanisha kuwa alikua akiamka visimamo vya usiku. Ibn Ma’in amemtaja kuwa ni madhubuti, na Ibn Sa’ad amesema kuwa alifariki mwaka 120 Hijriyyah.
[3] Katika hii inamaanisha kuwa katika mauaji ya kukusudia, mrithi wa aliyeuwawa bila kujali kama ni wa damu au wa kupanga, wana hiari aina nne: (a) kisasi kwa kuuwawa kwa mkosaji, (b) fidiya, (c) kumsamehe muuwaji, (d) kuwa na utaratibu mwingine wa kulipa zaidi au pungufu ya fidiya.
[4] Hadiyth hii inaelezea misingi ya Shariy’ah na wanaostahiki, kwa mfano mrithi wa aliyeuwawa, aliyeuwawa bila ya kuwepo kwa makosa kwa upande wake, ana uchaguzi ima achukue fidiya au alipe kisasa. Kiwango cha fidiya ni ngamia mia moja au thamani yake. Kuna ibara inayotaja kila jina la kiungo. Al-Ma-muwmah ni pigo linaloathiri akili ya mtu. Al-Jaaifah ni jeraha linalotokana na koo hadi tumboni na kumalizia kienani na kutokozea tumboni. Al-Muwdhwihah ni jeraha linalopasua nyama ya mtu katika mwili na kufanya mfupa uonekane.
[5] Hiqqah ni ngamia jike akiwa katika mwaka wake wa nne
[6] Jadha’ah ni ngamia jike akiwa katika mwaka wake wa tano.
[7] Banaati makhaadhw ni ngamia jike wanaoingia mwaka wao wa pili.
[8] Banaati labuwni ni ngamia jike wanaoingia katika mwaka wao wa tatu.
[9] Baniy labuwni ni ngamia dume anaoingia katika mwaka wake wa tatu.
[10] Hadiyth iliyopokelewa na Ibn Mas-‘uwd kuhusu diya inayolipwa kwa tukio la mauaji kimakosa imetajwa hapo kabla. Baadhi ya watu wakitumia Hadiyth hii wanachukulia fidiya hii kuwa ni sahihi na inaweza kutumika katika hali zote. Mantiki yake ni kuwa kila kesi ya mauaji hushughulikiwa peke yake kulingana na mazingira na hali ya aliyeuliwa. Kwa mfano ikiwa mtu kauwawa katika tukio lisilo la umwagaji damu katika hali iliyokuwa ya amani, basi adhabu yake itakuwa ni kali zaidi. Mauaji ya makusudi ni yale mtu ambayo anadhimiria na kutumia silaha yenye kuuwa na kusababisha mauti kwa mtu. Mauaji ya bahati mbaya ni yale ya mtu kutumia kitu chenye kuuwa lakini hakuwa amekusudia kumuuwa. Kwa mfano mshale, ambao umerushwa kumpiga kiwindwa, ambao ulimkosa na kumpata mwana Aadam. Mauaji ya kukusudia ni yale ya kumkusudia mtu fulani lakin silaha au ala iliyotumika kufanya jambo lile si aghlabu kusababisha kifo kama vile; mjeledi, kirungu na tofali, na kadhalika.
[11] Vidole vyote vina thamani moja katika suala la malipo ya fidiya.
[12] Maadamu si mtaalamu wa tiba, haruhusiwi kufanya kazi yenyewe kwa hatari anayoweza kusababisha. Ikiwa mgonjwa alikuwa anatibiwa na daktari kama huyu akapata matatizo kutokana na operesheni au dawa alizoandikiwa zikamuuwa ni juu ya daktari yule kulipa fidiya.
[13] Hadiyth hii inabainisha mambo mawili. Kwanza, diya kwa Ahl Adh-dhimmah ni nusu anayolipwa Muislam. Dhimmi ni neno linalotumiwa kwa maana ya kafiri anayeishi katika dola ya Kiislam. Pili, fidiya kwa mwanamke aliyejeruhiwa ni sawa na ya mwanamme, hadi itakapofikia kiwango cha theluthi ya fidiya. Chochote kinachozidi theluthi kitaingia katika nusu kama ni fidiya atakayolipwa mtu.
[14] Thamani ya fidiya kwa adhabu hii inategemea hukumu. Katika hali ya matukio ya mauaji yaliyoenea sehemu fulani au ya kwamba mauaji ametokea kuwa ni mtu mwenye tabia mbaya sana ya kikatili, ni juu ya Qadhwi kukadiria fidiya kama ya mauaji ya makusudi. Lakini kama tukio linaonesha kinyume na hivyo, Qadhwi ana uwezo wa kukadiria fidiya ndogo zaidi kama ilivyo katika mauaji yaliyofanyika kwa bahati mbaya na kwa makosa.
[15] Abuu Rimthah: Inasemekana kuwa jina lake ni Habib bin Haiyaan au Rifa’a bin Yathrib au ‘Amaarah bin Yathrib, Balwiy au Taym wa Banu Taym Ar-Rabaab. Inasemekana vile vile kuwa alikuwa Tamimi kizazi cha Amru Al-Qais bin Zayd Manaat bin Tamiym. Alikuwa ni Swahaba aliyekuwa akiishi mji wa Kufa Iraq.
[16] Lengo la kutajwa Hadiyth hii ni kuelezea kuwa mtoto habebi majukumu ya makosa aliyofanya baba yake na vivyo hivyo baba habebi dhambi ya mwanaye. Mtu haadhibiwi kwa makosa ya mwenzake.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْجِنَايَاتِ
Kitabu Cha Jinai
بَابُ دَعْوَى اَلدَّمِ وَالْقَسَامَةِ
02-Mlango Wa Kudai Damu Na Kiapo
1019.
عَنْ سَهْلِ بْنِ أَبِي حَثْمَةَ، عَنْ رِجَالٍ مِنْ كُبَرَاءِ قَوْمِهِ، أَنَّ عَبْدَ اَللَّهِ بْنَ سَهْلٍ ومُحَيِّصَةَ بْنَ مَسْعُودٍ خَرَجَا إِلَى خَيْبَرَ مِنْ جَهْدٍ أَصَابَهُمْ، فَأُتِيَ مَحَيِّصَةُ فَأُخْبِرَ أَنَّ عَبْدَ اَللَّهِ بْنِ سَهْلِ قَدْ قُتِلَ، وَطُرِحَ فِي عَيْنٍ، فَأَتَى يَهُودَ، فَقَالَ: أَنْتُمْ وَاَللَّهِ قَتَلْتُمُوهُ. قَالُوا: وَاَللَّهِ مَا قَتَلْنَاهُ، فَأَقْبَلَ هُوَ وَأَخُوهُ حُوَيِّصَةُ وَعَبْدُ اَلرَّحْمَنِ بْنُ سَهْلٍ، فَذَهَبَ مُحَيِّصَةُ لَيَتَكَلَّمَ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {"كَبِّرْ كَبِّرْ" يُرِيدُ: اَلسِّنَّ، فَتَكَلَّمَ حُوَيِّصَةُ، ثُمَّ تَكَلَّمَ مُحَيِّصَةُ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "إِمَّا أَنْ يَدُوا صَاحِبَكُمْ، وَإِمَّا أَنْ يَأْذَنُوا بِحَرْبٍ". فَكَتَبَ إِلَيْهِمْ فِي ذَلِكَ ]كِتَابًا[. فَكَتَبُوا: إِنَّا وَاَللَّهِ مَا قَتَلْنَاهُ، فَقَالَ لِحُوَيِّصَةَ، وَمُحَيِّصَةُ، وَعَبْدِ اَلرَّحْمَنِ بْنَ سَهْلٍ: "أَتَحْلِفُونَ، وَتَسْتَحِقُّونَ دَمَ صَاحِبَكُمْ؟" قَالُوا: لَا. قَالَ: "فَتَحْلِفُ لَكُمْ يَهُودُ؟" قَالُوا: لَيْسُوا مُسْلِمِينَ فَوَدَاهُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ مِنْ عِنْدِهِ، فَبَعَثَ إِلَيْهِمْ مَائَةَ نَاقَةٍ. قَالَ سَهْلٌ: فَلَقَدْ رَكَضَتْنِي مِنْهَا نَاقَةٌ حَمْرَاءُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ.
Kutoka kwa Sahli bin Abuu Hathmah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kutoka kwa wakubwa wa kabila lake kuwa: ’Abdullaah bin Sahl[1] na Muhayyiswah[2] bin Mas-‘uwd walienda Khaybar kwa sababu ya ukame uliowapata. Muhayyiswah akamuendea ‘Abdullaah bin Sahl akaambiwa kuwa ameuliwa na ametupwa katika kisima. Akawaendea Mayahudi na akawaambia: “Wa-Allaahi nyinyi mumemuuwa.” Mayahudi wakasema: “Wa-Allaahi hatukumuuwa.” Yeye na ndugu yake Huwayyiswah[3] na ‘Abdur-Rahmaan bin Sahl[4] walifika na Muhayyiswah alikuwa anataka kuzungumza na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamkatisha kwa kusema: “Mtangulize mkubwa, mtangulize mkubwa.” Huwayyiswah akazungumza kisha Muhayyisah naye akazungumza. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akawaambia: “Ima waondoe diya ya mwenzenu au watangaziwe vita.” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akawaandikia barua, nao wakajibu: “Wa-Allaahi sisi hatukumuuwa.” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia Huwayyiswah, Muhayyiswah na ‘Abdur-Rahmaan bin Sahl: “Mtaapa ili mstahiki damu ya mwenzenu?” Wakasema: “Hapana.” Akawaambia: “Basi Mayahudi wataapa.” (kuwa hawakuhusika) wakasema: “Wao sio Waislamu.” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) binafsi yake akamlipia diya,[5] akawapelekea ngamia mia. Sahli amesema: “Katika ngamia hao kuna ngamia mwekundu aliyenikanyaga.” [Bukhaariy, Muslim]
1020.
وَعَنْ رَجُلٍ مِنْ اَلْأَنْصَارِ، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَقَرَّ اَلْقَسَامَةَ عَلَى مَا كَانَتْ عَلَيْهِ فِي اَلْجَاهِلِيَّةِ، وَقَضَى بِهَا رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بَيْنَ نَاسٍ مِنَ اَلْأَنْصَارِ فِي قَتِيلٍ اِدَّعَوْهُ عَلَى اَلْيَهُودِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa mtu mmoja katika Answaar amesema kuwa: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekiri Qasaamah iliyokuwa katika zama za ujahiliya[6] na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amehukumu kwa hiyo Qasaamah (kiapo katika kesi za mauaji) baina ya watu mongoni mwa Answaar kuhusu mtu wao aliyeuwawa waliodai kuwa waliomuuwa ni mayahudi. [Imetolewa na Muslim]
[1] ’Abdullaah bin Sahl bin Zaid bin Ka’ab bin ‘Aamir Al-Answaar Al-Haarith aliuwawa Khaybar na mwili wake ulipatikana katika chemchem huku shingo yake ikionekana imevunjwa.
[2] Abu Sa’iyd Muhayyiswah bin Mas-‘uwd bin Ka’ab Al-Haarith Al-Answaar Al-Madaniy, ni jamaa wa Swahaba aliyeuwawa; ‘Abdullaah ambaye alisilimu kabla ya Hijra na alishiriki katika vita vya Uhud, Al-Khandaq na vita vingine muhimu vilivyobakia. Rasuli wa Allaah alimtuma Fadak kuenda kuwalingania watu katika Uislamu.
[3] Huyu alikuwa ni kaka wa Muhayyiswah alisilimu kwa msaada wa ndugu yake. Inasemekana alishiriki katika vita vya Khandaq, Uhud na vita vingine muhimu pamoja na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ).
[4] Huyu ni kaka yake ‘Abdullaah bin Sahl mama yake akiitwa Laylah, binti wa Nafi bin ‘Aamir. Inasemekana kuwa alipigana katika vita vya Badr, Uhud na vita vingine vyote muhimu. Aliumwa na nyoka na ‘Amaara bin Hazm alimtibu kwa Ruqyah kwa maelekezo kutoka kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Hata hivyo, Ibn Hajar aliingiwa na wasiwasi wa kuipokea na kuweka katika kitabu chake Al-Iswaabah.
[5] Qasaamah ina maana ya masharti ambapo muuaji hajafahamika, mtuhumiwa au watu husika au watu wa kabila fulani wanatakiwa watoe kiapo. Tukio kama hili linapotokea, watu hamsini wanatakiwa wajitokeze ili waape ya kwamba wao au watu wa kijiji hawajafanya mauaji hayo. Aina hii ya viapo vinatumika mahakamani tu. Viapo hivi havitumiki katika aina zingine za adhabu (huduwd). Qasaamah inatekelezwa na watu wawili (mlalamikaji au mlalamikiwa). Ikiwa mlalamikaji (warithi wa marehemu) watatoa ushahidi, au watatumia kiapo kama ushahidi haupo kuwa hawa ndio wauaji wenyewe, bila shaka itakuwa wazi kwa wanaojitetea kuwa ni wajibu kwao kulipa fidiya kwa walalamikaji. Walalamikaji wakishindwa kufanya hivyo, walalamikiwa wanatakiwa kuleta watu wapatao hamsini kisha waape kuwa hawajaua. Kiapo kilichotajwa kitatolewa na wale watu waliochaguliwa na muombaji mwenyewe. Hii ndio hukumu pekee inayohalalisha kiapo kwa upande wa muombaji vile vile.
[6] Katika hali hii, Shariy’ah inakubali kiapo kitakachoapwa na kafiri. Qasaamah haifanyi kazi kwa tuhuma zitakazoletwa na muombaji ila itakapokuwa imeambatanishwa na ushahidi mzito unaohusiana na mauaji.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْجِنَايَاتِ
Kitabu Cha Jinai
بَابُ قِتَالِ أَهْلِ اَلْبَغْيِ
03-Mlango Wa Kuwapiga Vita Waasi (Wa Kiongozi)
1021.
عَنْ اِبْنِ عُمَرَ رِضَيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ حَمَلَ عَلَيْنَا اَلسِّلَاحَ، فَلَيْسَ مِنَّا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kutubebea silaha si katika sisi.”[1] [Bukaariy, Muslim]
1022.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ خَرَجَ عَنْ اَلطَّاعَةِ، وَفَارَقَ اَلْجَمَاعَةَ، وَمَاتَ، فَمِيتَتُهُ مِيتَةٌ جَاهِلِيَّةٌ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kutoka katika utiifu (wa kiongozi) na akajitenga na jamaa na akafariki, basi kifo chake ni kifo cha kijahiliya.”[2] [Imetolewa na Muslim]
1023.
وَعَنْ أَمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {تَقْتُلُ عَمَّارًا اَلْفِئَةُ اَلْبَاغِيَةُ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “’Ammaar atauwawa na kikundi kilichoasi (kiovu).”[3] [Imetolewa na Muslim]
1024.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {هَلْ تَدْرِي يَا اِبْنَ أُمِّ عَبْدٍ، كَيْفَ حُكْمُ اَللَّهِ فِيمَنْ بَغَى مِنْ هَذِهِ اَلْأُمَّةِ ؟ "، قَالَ: اَللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ. قَالَ: "لَا يُجْهَزُ عَلَى جَرِيحِهَا، وَلَا يُقْتَلُ أَسِيرُهَا، وَلَا يُطْلَبُ هَارِبُهَا، وَلَا يُقْسَمُ فَيْؤُهَا} رَوَاهُ اَلْبَزَّارُ و اَلْحَاكِمُ وَصَحَّحَهُ فَوَهِمَ، فَإِنَّ فِي إِسْنَادِهِ كَوْثَرَ بْنَ حَكِيمٍ، وَهُوَ مَتْرُوكٌ وَصَحَّ عَنْ عَلِيٍّ مِنْ طُرُقٍ نَحْوُهُ مَوْقُوفًا. أَخْرَجَهُ اِبْنُ أَبِي شَيْبَةَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ee mwana wa Ummi ‘Abd (‘Abdullaah bin Mas-‘uwd), unajua nini hukumu ya Allaah kwa aliyeasi katika ummah huu? Akasema Allaah na Rasuli wa Allaah Wanajua. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Aliyejeruhiwa hamalizwi, mateka wake hauliwi, aliyekimbia hafuatwi na mali yake haigawanywi.”[4] [Imetolewa na Al-Bazzaar na Al-Haakim na akaisahihisha akaghafilika kwa sababu katika isnaad yake yumo Kawthar[5] bin Hakiym ambaye Hadiyth zake zinaachwa. Lakini imeswihi kutoka kwa ‘Aliy kwa njia nyingine mfano wa Hadiyth kama hii ikiwa ni Mawquwf iliyopokewa na Ibn Abiy Shaybah na Al-Haakim]
1025.
وَعَنْ عَرْفَجَةَ بْنِ شُرَيْحٍ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {مَنْ أَتَاكُمْ وَأَمَرَكُمْ جَمِيعٌ، يُرِيدُ أَنْ يُفَرِّقَ جَمَاعَتَكُمْ، فَاقْتُلُوهُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa ‘Arfajah bin Shurayh[6] amesema kuwa alimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Atakayewajia nyinyi na jambo lenu ni moja, na anataka kuwatenganisha katika umoja wenu, basi mpigeni vita.” [Imetolewa na Muslim]
[1] Kupigana dhidi ya Shariy’ah ni dhambi kubwa. Vivyo hivyo, kumtishia Muislam kumuuwa au kumtolea silaha ni dhambi kubwa. Ikiwa mtu amehalalisha damu ya Muislam au kumuuwa kwa kuona kuwa ni halaal kufanya hivyo, bila shaka mtu huyu atakuwa ameritadi. Mtu huyu anazingatiwa kuwa amekufuru kwa makubaliano ya Jamhuri ya ‘Uamaa. Hata hivyo ni halaal kuwapiga Waislam walioasi dhidi ya mamlaka ya Shariy’ah kama ilivyokuja katika Qur-aan:
فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّـهِ ۚ
“…basi piganeni na ambalo linakandamiza mpaka lielemee kwenye amri ya Allaah…” [Al-Hujuraat: 9]. Kadhalika tunajifunza hayo katika Hadiyth mbalimbali.
[2] Utiifu kwa Amiri (mtawala) ni wajibu madamu hajakwenda kinyume na Shariy’ah za Kiislam. Vivyo hivyo, hairuhusiwi kutoka katika jamaa, maadamu hafanyi yanayoweza kumtoa katika Uislam. Kwa kumkaidi Amiri anayetawala kwa misingi ya Shariy’ah ya Kiislam ni uasi. Yeyote anayevunja mamlaka ya Amiri au kujitoa katika kundi pamoja na kuwa hatoonekana kuwa ni kafiri lakini ataonekana kuwa amekwenda kombo. Tofauti yao ni kuwa si katika wao mwenye Imaam au mamlaka ya kishariy’ah.
[3] Aliuwawa katika vita vya Swiffiyn na wale waliokuwa wakipigana dhidi ya ‘Aliy.
[4] Hakuna kutokubaliana kuhusu uhalali wa kuwapiga vita watu waliodhulumu. Hata hivyo, kuna tofauti ya maoni kwa ‘Ulamaa katika kumata mali zao, kuwaacha waliojeruhiwa na kuwashawishi wanaotaka kutoroka.
[5] Alikuwa ni mkazi wa mji wa Kufa uliopo ‘Iraq na baadae akahamia Halab. Ibn Ma’iyn anamzungumzia, “Si chochote katika Hadiyth.” Ahmad bin Hanbal naye anamsema: “Hadiyth zake ni za uongo.”
[6] ‘Arfajah bin Shurayh Ashja’i alikuwa ni Swahaba aliyekuwa akiishi Kufa (mji uliopo Iraq).
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْجِنَايَاتِ
Kitabu Cha Jinai
بَابُ قِتَالِ اَلْجَانِي وَقَتْلُ اَلْمُرْتَدِّ
04-Mlango Wa Kupigana Na Anayefanya Jinai Na Kumuuwa Aliyeritadi
1026.
عَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرٍو رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مِنْ قُتِلَ دُونَ مَالِهِ فَهُوَ شَهِيدٌ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayeuliwa kwa kutetea mali yake, huyo ni Shahiyd.”[1] [Imetolewa na Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na At-Tirmidhiy na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
1027.
وَعَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {قَاتَلَ يُعْلَى بْنُ أُمِّيَّةَ رَجُلًا، فَعَضَّ أَحَدُهُمَا صَاحِبَهُ، فَنَزَعَ ثَنِيَّتَهُ، فَاخْتَصَمَا إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: "أَيَعَضُّ أَحَدُكُمْ أَخَاهُ كَمَا يَعَضُّ اَلْفَحْلُ ؟ لَا دِيَةَ لَهُ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Yu’laa bin Ummiyyah alipigana na mtu, mmoja wao akang’ata mkono wa mwingine, akauvuta mkono wake kutoka mdomoni mwake, meno yake ya mbele yakadondoka. Wakashtakiana kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Mmoja wenu anang’ata kama fahali ang’atavyo, mtu huyo hana diya.”[2] [Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
1028.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ أَبُو اَلْقَاسِمِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَوْ أَنَّ اِمْرَأً اِطَّلَعَ عَلَيْكَ بِغَيْرِ إِذْنٍ، فَحَذَفْتَهُ بِحَصَاةٍ، فَفَقَأْتَ عَيْنَهُ، لَمْ يَكُنْ عَلَيْكَ جُنَاحٌ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ .
وَفِي لَفْظٍ لِأَحْمَدَ، وَالنَّسَائِيِّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ: {فَلَا دِيَةَ لَهُ وَلَا قِصَاصَ}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Lau mtu atakuchungulia bila ruhusa na ukamrushia kijiwe ukaliharibu jicho lake, basi huna dhambi.”[3] [Bukhaariy, Muslim]
Na katika tamshi la Ahmad na An-Nasaaiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan imesema: “Hana diya wala kulipiza kisasi.”
1029.
وَعَنْ اَلْبَرَاءِ بْنِ عَازِبٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {قَضَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنَّ حِفْظَ اَلْحَوَائِطِ بِالنَّهَارِ عَلَى أَهْلِهَا، وَأَنْ حِفْظَ اَلْمَاشِيَةِ بِاللَّيْلِ عَلَى أَهْلِهَا، وَأَنَّ عَلَى أَهْلِ اَلْمَاشِيَةِ مَا أَصَابَتْ مَاشِيَتُهُمْ بِاللَّيْلِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ إِلَّا اَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ وَفِي إِسْنَادِهِ اِخْتِلَافٌ
Kutoka kwa Al-Baraa bin ‘Aazib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alihukumu kuwa kuhifadhi mashamba wakati wa mchana ni jukumu la wenyewe, na kuhifadhi wanyama wakati wa usiku ni jukumu la wenyewe, na kwamba wenye wanyama watalipa kilichoharibiwa na wanyama wao iwapo wameharibu wakati wa usiku.[4] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa At-Tirmidhiy, na akaisahihisha Ibn Hibbaan na katika isnaad yake kuna tofauti]
1030.
وَعَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ فِي رَجُلٍ أَسْلَمَ ثُمَّ تَهَوَّدَ: {لَا أَجْلِسُ حَتَّى يُقْتَلَ، قَضَاءُ اَللَّهِ وَرَسُولِهِ، فَأُمِرَ بِهِ، فَقُتِلَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ لِأَبِي دَاوُدَ: {وَكَانَ قَدْ اُسْتُتِيبَ قَبْلَ ذَلِكَ}
Kutoka kwa Mu’aadh bin Jabl (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuhusu mtu aliyesilimu kisha akawa myahudi: “Sitakaa hadi auwawe,[5] hiyo ndiyo hukumu ya Allaah na Rasuli wa Allaah.” Baada ya hapo ikaamriwa auwawe. [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika riwaayah ya Abuu Daawuwd inasema: “Kabla ya kuuwawa alipewa nafasi ya kutubia.”
1031.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ بَدَّلَ دِينَهُ فَاقْتُلُوهُ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuritadi (kuacha Uislam- anaingia katika Uislam kwa hadaa kwa lengo la kurudi katika dini yake na kuanza kuukejeli na kuutukana Uislam) muuweni.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1032.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ، {أَنَّ أَعْمَى كَانَتْ لَهُ أُمُّ وَلَدَ تَشْتُمُ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَتَقَعُ فِيهِ، فَيَنْهَاهَا، فَلَا تَنْتَهِي، فَلَمَّا كَانَ ذَاتَ لَيْلَةٍ أَخْذَ اَلْمِعْوَلَ، فَجَعَلَهُ فِي بَطْنِهَا، وَاتَّكَأَ عَلَيْهَا فَقَتَلَهَا فَبَلَغَ ذَلِكَ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ:"أَلَّا اِشْهَدُوا أَنَّ دَمَهَا هَدَرٌ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَرُوَاتُهُ ثِقَاتٌ.
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Kulikuwa kuna kipofu aliyekuwa na mjakazi, mjakazi huyu alikuwa akimtukana Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na akimdhalilisha. Alikuwa akimkataza bila kukatazika. Usiku mmoja alichukua mtaimbo akauweka juu ya tumbo lake (mjakazi) akaliegemea juu yake akamuuwa. Hili likamfikia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Fahamuni! Shuhudieni kwa hakika damu yake (mjakazi huyo) ni halaal.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd wapokezi wake ni madhubuti]
[1] Katika Hadiyth nyingine yenye mnasaba kama huu inasema: “Atakayeuwawa kwa ajili ya mali yake, nafsi, familia na dini yake huyo ni shahidi, na hivyo anastahiki Jannah.” Ikiwa jambazi atamshambulia mtu na kutaka kuchukua mali yake, mke au watoto wake, na mtu yule akajilinda na kumuuwa yule adui katika hali ile hatokuwa ni mwenye dhambi. Hukumu hii ni makubaliano ya Jamhuri ya ‘Ulamaa.
[2] Ikiwa mtu atajilinda na jambo fulani kisha mwenzake akapata madhara kwa ajili hiyo huwa hakuna fidiya.
[3] Hii inahusu sehemu ambazo huwezi kuingia bila ya ruhusa kama vile nyumba ya mtu au sehemu ya mtu maalum.
[4] Hadiyth hii inamaanisha kuwa ikiwa kundi la wanyama litaharibu mazao au shamba la mtu wakati wa mchana, basi mwenye wanyama hatolipa chochote. Hii ni kwa sababu kwa ada ya wanyama ni kupata malisho yao wakati wa mchana. Katika hali hii mwenye shamba ndiye anayetakiwa kuwa makini na shamba lake zaidi. Vivyo hivyo ni muhimu mtu kulinda wanyama wake usiku kwani kwa wakati huo wanyama wakisababisha madhara ni wajibu wake kulipa.
[5] Hadiyth hii na inayofuatia imepokewa na Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) ambazo zinaeleza kwa uwazi kabisa kuwa adhabu ya aliyeritadi ni kuuliwa. Ikiwa mtu kalazimishwa kuwa hivyo au kusema maneno ya kuonyesha kuwa ameritadi, mtu huyo atasamehewa na Shariy’ah. Baadhi ya ‘Ulamaa wanaona kuwa mwanamke aliyeritadi haadhibiwi. Muono huu sio sahihi kwani naye anaadhibiwa kwa makubaliano ya ‘Ulamaa.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/277
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10036&title=09-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Jinai%20%28Na%20Kisasi%29%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D9%92%D8%AC%D9%90%D9%86%D9%8E%D8%A7%D9%8A%D9%8E%D8%A7%D8%AA%D9%90
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10037&title=00-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Jinai%3A%20Mlango%20Wa%20Makosa%20Ya%20Jinai
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10038&title=01-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20%20Jinai%3A%20Mlango%20Wa%20Diya
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10039&title=02-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20%20Jinai%3A%20Mlango%20Wa%20Kudai%20Damu%20Na%20Kiapo
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10040&title=03-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Jinai%3A%20Mlango%20Wa%20Kuwapiga%20Vita%20Waasi%20%28Wa%20Kiongozi%29
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10041&title=04-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Jinai%3A%20Mlango%20Wa%20Kupigana%20Na%20Anayefanya%20Jinai%20Na%20Kumuuwa%20Aliyeritadi