كِتَاب اَلْأَطْعِمَةِ
Kitabu Cha Vyakula
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَاب اَلْأَطْعِمَةِ
00-Kitabu Cha Vyakula
1134.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {" كُلِّ ذِي نَابٍ مِنْ اَلسِّبَاعِ، فَأَكَلَهُ حَرَامٌ"} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
وَأَخْرَجَهُ: مِنْ حَدِيثِ اِبْنِ عَبَّاسٍ بِلَفْظٍ: نَهَى. وَزَادَ: {" وَكُلُّ ذِي مِخْلَبٍ مِنْ اَلطَّيْرِ"}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kila mnyama mwenye kuwinda kwa meno, kumla kwake ni haraam.”[1] [Imetolewa na Muslim]
Pia amepokea kutoka katika hadiyth ya ‘Abdullaah ibn ‘Abbaas kwa tamshi hili: “Amekataza.” Na akaongeza: “Na kila ndege anayewinda kwa kucha.”
1135.
وَعَنْ جَابِرٍ رضى الله عنه قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَوْمَ خَيْبَرَ عَنْ لُحُومِ اَلْحُمُرِ اَلْأَهْلِيَّةِ، وَأْذَنْ فِي لُحُومِ اَلْخَيْلِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ. وَفِي لَفْظِ اَلْبُخَارِيِّ: {وَرَخَّصَ}
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza nyama za punda kihongwe (wa mjini)[2] siku ya Vita vya Khaybar, akaruhusu nyama za farasi.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika tamshi la Bukhaariy: “Na ameruhusu.”
1136.
وَعَنْ اِبْنِ أَبِي أَوْفَى قَالَ: {غَزَوْنَا مَعَ رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم سَبْعَ غَزَوَاتٍ، نَأْكُلُ اَلْجَرَادَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn Abiy Awfaa amesema: “Tumepigana pamoja na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) vita saba, tunakula nzige.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
1137.
وَعَنْ أَنَسٍ فِي قِصَّةِ اَلْأَرْنَبِ {قَالَ: فَذَبَحَهَا، فَبَعَثَ بِوَرِكِهَا إِلَى رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَبِلَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Anas katika kisa cha sungura: “…akamchinja, akampelekea Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) paja lake naye akalikubali.”[3] [Al-Bukhaariy, Muslim]
1138.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم عَنْ قَتْلِ أَرْبَعِ مِنْ اَلدَّوَابِّ: اَلنَّمْلَةُ، وَالنَّحْلَةُ، وَالْهُدْهُدُ، وَالصُّرَدُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuwa wanyama wanne sisimizi, nyuki, hudihudi na kipwe (ndege).” [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
1139.
وَعَنْ اِبْنِ أَبِي عَمَّارٍ قَالَ: {قُلْتُ لِجَابِرٍ: اَلضَّبُعُ صَيْدُ هِيَ ؟ قَالَ: نِعْمَ. قُلْتُ: قَالَهُ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: نِعْمَ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةَ وَصَحَّحَهُ اَلْبُخَارِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Ibn Abiy ‘Ammaar[4] amesema: “Nilimuuliza Jaabir fisi analiwa? Akasema Ndiyo.[5] Nikasema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema hivyo? Akasema ndiyo.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha Al-Bukhaariy na Ibn Hibbaan]
1140.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رضى الله عنه ، أَنَّهُ سُئِلَ عَنْ اَلْقُنْفُذِ، فَقَالَ: ﴿ قُلْ لَا أَجدُ فِي مَا أُوحِيَ إِلَيَّ مُحَرَّمًا عَلَى طَاعِمٍ ﴾ فَقَالَ شَيْخٌ عِنْدَهُ: سَمِعْتَ أَبَا هُرَيْرَةَ يَقُولُ: {ذَكَرَ عِنْدَ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: خِبْثَةَ مِنْ اَلْخَبَائِثِ"} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَإِسْنَادُهُ ضَعِيفٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Aliulizwa kuhusu nungu akasema kwa kusoma Aayah hii: (Sema: Sipati katika yale niliyofunuliwa Wahyi kwangu kilichoharamishwa kwa mlaji…) Qur-aan 6: 145. Mzee mmoja aliye kwake akasema: ‘Nilimsikia Abuu Hurayrah anasema alitajwa mbele ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ni mchafu miongoni mwa vichafu’.” [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd na isnaad yake ni dwaifu]
1141.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم عَنْ اَلْجَلَّالَةِ وَأَلْبَانِهَا} أَخْرَجَهُ اَلْأَرْبَعَةِ إِلَّا النَّسَائِيُّ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kula mnyama anayekula uchafu na kunywa maziwa yake.”[6] [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa An-Nasaaiy, na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
1142.
وَعَنْ أَبِي قَتَادَةٌ رضى الله عنه {فِي قِصَّةِ اَلْحِمَارِ اَلْوَحْشِيِّ فَأَكَلَ مِنْهُ اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abiy Qataadah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema katika kisa cha punda milia: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamla.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
1143.
وَعَنْ أَسْمَاءِ بِنْتِ أَبِي بَكْرٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {نَحَرْنَا عَلَى عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَرَساً، فَأَكَلْنَاهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Asmaa bint Abiy Bakr (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Katika zama za Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) tulichinja farasi na tukamla.”[7] [Al-Bukhaariy, Muslim]
1144.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {أَكُلَّ اَلضَّبِّ عَلَى مَائِدَةِ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Kenge aliliwa katika meza ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ).”[8] [Al-Bukhaariy, Muslim]
1145.
وَعَنْ عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ بْنِ عُثْمَانَ اَلْقُرَشِيُّ رضى الله عنه {أَنَّ طَبِيباً سَأَلَ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم عَنْ اَلضِّفْدَعِ يَجْعَلُهَا فِي دَوَاءٍ، فَنَهَى عَنْ قَتْلِهَا} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Abdir-Rahmaan bin ‘Uthmaan Al-Qurashiyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Kuwa tabibu mmoja alimuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuhusu chura kumfanya dawa. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akakataza kuuwa chura.”[9] [Imetolewa na Ahmad na akaisahihisha Al-Haakim]
[1] Hadiyth hii inatoa maelezo kwamba kila mnyama mwenye kula mnyama na mwenye chonge ni haraam kuliwa. Vivyo kwa ndege anayenyofoa kiwindwa chake na kutumia ukucha ndege wa aina hiyo ni haraam kuliwa.
[2] Punda wa porinini (Pundamilia) ni halaal kuliwa.
[3] Sungura ni halaal kwa mujibu wa ‘Ulamaa wengi.
[4] Huyu ni ‘Abdur-Rahmaan bin ‘Abdillaah bin Abuu ‘Ammaar Al-Qurayshiy Al-Makkiy. Alikuwa ni Mwenye Taqwa na An-Nasaaiy anamthibitisha kuwa ni madhubuti.
[5] Hadiyth inaonesha kuwa kumla fisi kumeruhusiwa. Kulingana na baadhi ya Maimaam (kama vile Shaafi’y) ni halaal. Wengine kama Hanafiy wanaona kuwa ni haraam. Sababu ya kuwa kwake ni haraam ni kuwa anapenda kula nyama ya mwana Aadam na kuichimbia chini.
[6] Katika lugha ya Kiarabu Jallaala ina maana ya wanyama wenye kula kwenye vinyaa, uchafu, awe mnyama huyo ni ngamia jike, ng’ombe au mbuzi. Hata ikiwa ni halaal kutumia nyama au maziwa yake, hili ni jambo lenye tofauti ya rai kati ya Wanazuoni tokea awali. Baadhi ya Wanazuoni wanaona kwamba ni halaali na wengine wakiona kuwa ni haraam. Mnyama ataonekana kuwa ni Jallaala ikiwa kiasi kikubwa cha chakula chake ni uchafu wa mwana Aadam. Ama ikiwa kiwango kikubwa cha chakula chake ni kinachoruhusiwa basi hatoingia katika kundi hili la Jallaala.
[7] Kuna Hadiyth iliyotangulia kabla ya hii ikisisitiza kuwa kula farasi ni halaal. Na hadiyth hii inathibitisha jambo hilo hilo.
[8] Tunajifunza katika baadhi ya Hadiyth kuwa Dhabbu (mburukenge) analiwa, pamoja na kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) mwenyewe hakumla, lakini Maswahaba wake walimla mbele yake katika meza yake. Alialikwa kumla lakini hakushiriki. Hakuwakataza watu kumla. Wanazuoni wanataja katika maandiko yao kuwa ni chukizo la Tanzihi (vile vilivyokuwa chini ya daraja la makatazo).
[9] Tunajifunza katika Hadiyth hii kuwa ni haraam kuuwa chura na kadhalika kumla.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَاب اَلْأَطْعِمَةِ
Kitabu Cha Vyakula
بَاب اَلصَّيْدِ وَالذَّبَائِحِ
01-Mlango Wa Kuwinda Na Kuchinja
1146.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"مَنِ اتَّخَذَ كَلْباً، إِلَّا كَلْبَ مَاشِيَةٍ، أَوْ صَيْدٍ، أَوْ زَرْعٍ، اِنْتَقَصَ مِنْ أَجْرِهِ كُلَّ يَوْمٍ قِيرَاطٌ" } مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kufuga mbwa isipokuwa mbwa wa kuwinda au wa mifugo au wa kulima[1] hakika kila siku anapunguziwa Qiyraatw kutoka katika ujira wake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
1147.
وَعَنْ عَدِيِّ بنِ حَاتِمٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ لِي رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"إِذَا أَرْسَلَتَ كَلْبَكَ فَاذْكُرِ اسْمَ اَللَّهِ، فَإِنْ أَمْسَكَ عَلَيْكَ فَأَدْرَكْتَهُ حَيًّا فَاذْبَحْهُ، وَإِنْ أَدْرَكْتَهُ قَدْ قُتِلَ وَلَمْ يُؤْكَلْ مِنْهُ فَكُلْهُ، وَإِنْ وَجَدْتَ مَعَ كَلْبِكَ كَلْبًا غَيْرَهُ وَقَدْ قُتِلَ فَلَا تَأْكُلْ: فَإِنَّكَ لَا تَدْرِي أَيَّهُمَا قَتَلَهُ، وَإِنْ رَمَيْتَ سَهْمَكَ فَاذْكُرِ اسْمَ اَللَّهِ، فَإِنْ غَابَ عَنْكَ يَوْماً، فَلَمْ تَجِدْ فِيهِ إِلَّا أَثَرَ سَهْمِكَ، فَكُلْ إِنْ شِئْتَ، وَإِنْ وَجَدْتَهُ غَرِيقاً فِي اَلْمَاءِ، فَلَا تَأْكُلْ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَهَذَا لَفْظُ مُسْلِمٍ
Kutoka kwa ‘Adiyy bin Haatim[2] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alisema: “Unapomtuma mbwa wako, taja jina la Allaah[3] juu yake, akikukamatia (mnyama) nawe ukamkuta hai, basi mchinje na ukikuta ameuwa naye hakula chochote humo, basi kula, na ukikuta pamoja na mbwa wako kuna mbwa mwingine naye ameuwa basi usile, kwani hujui ni yupi aliyemuuwa. Na utakaporusha mshale wako taja Jina la Allaah. Itakapokupotea siku moja na (ukalipata halafu) usikute ila athari ya mshale wako, kula ukipenda. Na atakapompata ameghariki kwenye maji, usile.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
1148.
وَعَنْ عَدِيٍّ قَالَ: {سَأَلْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم عَنْ صَيْدِ اَلْمِعْرَاضِ فَقَالَ: "إِذَا أَصَبْتَ بِحَدِّهِ فَكُلْ، وَإِذَا أَصَبْتَ بِعَرْضِهِ، فَقُتِلَ، فَإِنَّهُ وَقِيذٌ، فَلَا تَأْكُلْ"} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Adiyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuhusu kuwinda kwa Mi’raadhw (mshale). Akasema: ‘Utakapolenga katika ukali wake,[4] kula na utakapolenga kwa ubavu wake na ikauwa, basi mnyama huyo ni mawquwdha[5] usile.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1149.
وَعَنْ أَبِي ثَعْلَبَةَ رضى الله عنه عَنِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {" إِذَا رَمَيْتَ بِسَهْمِكَ، فَغَابَ عَنْكَ، فَأَدْرَكْتَهُ فَكُلْهُ، مَا لَمْ يُنْتِنْ"} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abiy Tha’labah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Utakaporusha mshale wako ukakupotea[6] ukaukuta (umeua windo), basi lile maadam halikuvunda harufu mbaya.” [Imetolewa na Muslim]
1150.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، {أَنَّ قَوْمًا قَالُوا لِلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم إِنَّ قَوْماً يَأْتُونَنَا بِاللَّحْمِ، لَا نَدْرِي أَذُكِرَ اِسْمُ اَللَّهِ عَلَيْهِ أَمْ لَا ؟ فَقَالَ: " سَمُّوا اَللَّهَ عَلَيْهِ أَنْتُمْ، وَكُلُوهُ"} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Watu walimuambia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) watu wanatujia na nyama hatujui kama wametaja Jina la Allaah juu yake ama hawakutaja? Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: ‘Nyinyi tajeni Jina la Allaah juu yake na muile.”[7] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1151.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بنِ مُغَفَّلٍ الْمُزَنِيِّ رضى الله عنه {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم نَهَى عَنِ اَلْخَذْفِ، وَقَالَ: "إِنَّهَا لَا تَصِيدُ صَيْدًا، وَلَا تَنْكَأُ عَدُوًّا، وَلَكِنَّهَا تَكْسِرُ اَلسِّنَّ، وَتَفْقَأُ اَلْعَيْنَ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ. وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa ‘Abdillaah bin Mughaffal Al-Muzaniyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza mtu kurusha kijiwe na akasema: ‘Kwani kurusha kijiwe[8] hakuwindi windo wala hakuui adui, lakini huvunja jino na kupofua.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
1152.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"لَا تَتَّخِذُوا شَيْئاً فِيهِ اَلرُّوحُ غَرَضًا"} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msichukue kitu chenye roho kulengea shabaha.” [Imetolewa na Muslim]
1153.
وَعَنْ كَعْبِ بْنِ مَالِكٍ رضى الله عنه {أَنّ امْرَأَةً ذَبَحَتْ شَاةً بِحَجَرٍ، فَسُئِلَ اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم عَنْ ذَلِكَ، فَأَمَرَ بِأَكْلِهَا} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ka’b bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Mwanamke mmoja alichinja mbuzi kwa jiwe. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaulizwa kuhusu hilo akaamuru kuliwa kwake.”[9] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1154.
وَعَنْ رَافِعِ بْنِ خَدِيجٍ رضى الله عنه عَنِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"مَا أُنْهِرَ اَلدَّمُ، وَذُكِرَ اِسْمُ اَللَّهِ عَلَيْهِ، فَكُلْ لَيْسَ اَلسِّنَّ وَالظُّفْرَ، أَمَّا اَلسِّنُّ، فَعَظْمٌ، وَأَمَّا اَلظُّفُرُ: فَمُدَى اَلْحَبَشِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Raafi’ bin Khadiyj (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kinachomwaga damu na Jina la Allaah likatajwa juu yake, kula. Isipokuwa jino na kucha.[10] Ama jino ni mfupa. Na ama kucha ni kisu cha Wahabeshi.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
1155.
وَعَنْ جَابِرِ بنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَنْ يُقْتَلَ شَيْءٌ مِنَ اَلدَّوَابِّ صَبْرًا} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza mnyama kuuwawa kwa kutesa.”[11] [Imetolewa na Muslim]
1156.
وَعَنْ شَدَّادِ بْنِ أَوْسٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {" إِنَّ اَللَّهَ كَتَبَ اَلْإِحْسَانَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ، فَإِذَا قَتَلْتُمْ فَأَحْسِنُوا اَلْقِتْلَةَ، وَإِذَا ذَبَحْتُمْ فَأَحْسِنُوا اَلذِّبْحَةَ، وَلْيُحِدَّ أَحَدُكُمْ شَفْرَتَهُ، وَلْيُرِحْ ذَبِيحَتَهُ"} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Shaddaad bin Aws (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika Allaah Ameandika hisani juu yake kila jambo. Mnapouwa, uweni kwa namna nzuri, na mnapochinja chinjeni kwa uzuri. Mmoja wenu akinoe kisu chake na amuondolee mashaka mnyama anayemchinja.”[12] [Imetolewa na Muslim]
1157.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"ذَكَاةُ اَلْجَنِينِ ذَكَاةُ أُمِّهِ"} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Abiy Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kumchinja mtoto tumboni ni kwa kumchinja mama yake.”[13] [Imetolewa na Ahmad na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
1158.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {" اَلْمُسْلِمُ يَكْفِيهِ اِسْمُهُ، فَإِنْ نَسِيَ أَنْ يُسَمِّيَ حِينَ يَذْبَحُ، فَلْيُسَمِّ، ثُمَّ لِيَأْكُلْ"} أَخْرَجَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَفِي إِسْنَادِهِ مُحَمَّدُ بنُ يَزِيدَ بنِ سِنَانٍ، وَهُوَ صَدُوقٌ ضَعِيفُ اَلْحِفْظِ
وَأَخْرَجَهُ عَبْدُ اَلرَّزَّاقِ بِإِسْنَادٍ صَحِيحٍ إِلَى اِبْنِ عَبَّاسٍ، مَوْقُوفًا عَلَيْهِ
وَلَهُ شَاهِدٌ عِنْدَ أَبِي دَاوُدَ فِي "مَرَاسِيلِهِ" بِلَفْظِ: {"ذَبِيحَةُ اَلْمُسْلِمِ حَلَالٌ، ذَكَرَ اِسْمَ اَللَّهِ عَلَيْهَا أَوْ لَمْ يَذْكُرْ"} وَرِجَالُهُ مُوَثَّقُونَ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muislam linamtosha jina lake, akisahau BismiLLaah wakati wa kuchinja, basi aseme BismiLLaah kisha ale.”[14] [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy]
Katika Hadiyth hii kuna mpokezi hifadhi yake ni dhaifu ambaye ni Muhammad bin Yaziyd bin Sinaan[15] ni mkweli mwenye udhaifu wa kuhifadhi.
Abdur-Razzaaq ameipokea kwa isnaad sahihi ikinasibishwa kwa ‘Abdullaah bin ‘Abbaas ikiwa ni Marfuw’.
Ina ushahidi kwa Abuu Daawuwd katika Maraasil kwa tamshi: “Chinjo la Muislam ni halaal, ataje Jina la Allaah wakati wa kuchinja ama asitaje.” Wapokezi wake ni madhubuti.
[1] Kwa sababu zisizokuwa za kuwinda na kuchunga vitu, ni haraam kumfuga mbwa kama mnyama wa nyumbani. Qiraatw ni kitu chenye thamani kubwa.
[2] ‘Adiyy bin Haatim bin At-Ta’i na baba yake walikuwa mashuhuri kwa ukarimu wao. Alimtembelea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) mwaka wa 7 HIjriyyah. Yeye pamoja na watu wake walithibitisha Uislam wao zaidi wakati wa Ar-Ridda. Zakkaah ya kwanza kumfikia Abuu Bakr ilikuwa kutoka kwa ‘Adiyy na watu wake. Alihudhuria ufunguzi wa Madain na alikuwa pamoja na ‘Aliy wakati wa vita vya Al-Jamaal, alifariki mwaka 120 Hijriyyah akiwa na miaka 68.
[3] Kuwinda kwa sababu ya kutafuta chakula au kuuza ni ruhusa. Ama ikiwa hilo linafanyika kwa sababu ya kutembea, kufurahi na kupoteza muda haitakiwi. Ni ruhusa kutumia mbwa au wanyama wengine kwa ajili ya kuwindia. Hata hivyo, kuna mambo mawili yanayotawala jambo hili: Kwanza unapomtuma mbwa wako unataja Jina la Allaah na pili, mbwa aliyetumwa anatakiwa yule aliyefundishwa kuwinda. Ikiwa mbwa yule kamla yule aliyemkamata anakuwa si halaal kwako kwani atakuwa amejiwindia na hakukuwindia.
[4] Moja katika hukumu ya uhalaal wa kuliwa kwa kiwindo ni kuwa ikiwa mnyama amekufa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali, basi ni halaal kuliwa ama ikiwa amekufa kwa kupigwa na kitu kikafa (kisichokuwa na ncha) usile kwani kitakuwa kimekufa kwa kupigwa.
[5] Yaani mnyama anayekufa kwa kupigwa na kitu kama vile fimbo au jiwe bila ya kuchinjwa.
[6] Ikiwa mnyama amepigwa mshale, kisha akakimbia usimuone na baadae ukakuta amekufa katika maji, hairuhusiwi kuliwa. Hata hivyo, ikiwa mnyama huyo huyo amepatikana akiwa hai, anatakiwa achinjwe. Ikiwa amekufa amelala chini na hana majeraha mengine zaidi ya mshale wako, ni halaal kumla. Ama akikutwa na jeraha lingine lisilokuwa la mshale wako basi ni haraam kumla.
[7] Hadiyth hii inatoa kanuni ya msingi kuwa mwana Aadam hakuna hakika kuwa nyama fulani si halaal, huna haja ya kusema kuwa si halaal maadamu huna hakika, na haswa zaidi ikiwa inatoka kwa Muislam.
[8] Hadiyth inaonesha kuwa vijiwe vinavyokusudiwa hapa ni vile vidogo visivyokuwa na manufaa.
[9] Mafundisho tuyapatayo katika Hadiyth hii yanaonesha kuwa ni halaal kwa mwanamke kuchinja kwa masharti kuwa: (a) Awe ni Muislam (b) Kabla ya akuchinja ataje Jina la Allaah kwa kusema BismiLLaah Allaahu Akbar.
[10] Kitu chochote chenye ncha kali (mbali na ukucha, mfupa au meno) ambayo itafanya damu ya mnyama kutiririka katika mwili wake, ni halaal kutumika kuchinjia.
[11] Katika lugha ya Kiarabu Swabr ina maana mbili: (a) kumuuwa mnyama kwa kumzuilia na maji au kufa kwa njaa, (b) Kumtumia mnyama kama kitu cha kulengea shabaha au kumtumia katika mazoezi ya kulenga shabaha. Yote haya ni haraam.
[12] Hata kama ni mtu anatakiwa kuuwawa basi anatakiwa auwawe kwa haraka bila kupata masumbuko yoyote ili afe kwa haraka.
[13] Hadiyth hii inaonesha kuwa kichanga kinafuata hukumu ya mama yake. Ikiwa mama ni halaal basi na kilicho ndani yake kinafuata hukumu hiyo. Ikiwa kichanga katika tumbo la mama ni hai basi atachinjwa kwa mujibu wa Wanazuoni.
[14] Ikiwa Muislam hakutaja Allaahu Akbar kwa makusudi wakati wa kuchinja basi nyama ile inakuwa ni haraam. Kama atakuwa amesahau basi ni halaal. Na hii ndio rai ya Wanazuoni.
[15] Huyu ni Abuu ‘Abdillaah alikuwa katika kabila la At-Tamiym. Abuu Haatim anamuelezea: ‘Hakuwa makini katika Hadiyth lakini pamoja na hayo alikuwa Mwenye Taqwa.’ Abuu Daawuwd anamuelezea: ‘Si wa kutegemewa’ na An-Nasaaiy anasema: ‘Hakuwa madhubuti.’ Ama Ibn Hibbaan amemtaja kuwa alikuwa Ath-Thiqah (kuwa alikuwa madhubuti). Alikufa mwaka 220 Hijriyyah.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَاب اَلْأَطْعِمَةِ
Kitabu Cha Vyakula
بَاب اَلْأَضَاحِيِّ
02-Mlango Wa Kuchinja Udhw-hiyyah[1]
1159.
عَنْ أَنَسِ بنِ مَالِكٍ رضى الله عنه {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يُضَحِّي بِكَبْشَيْنِ أَمْلَحَيْنِ، أَقْرَنَيْنِ، وَيُسَمِّي، وَيُكَبِّرُ، وَيَضَعُ رِجْلَهُ عَلَى صِفَاحِهِمَا. وَفِي لَفْظٍ: ذَبَحَهُمَا بِيَدِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ . وَفِي لَفْظِ: {سَمِينَيْنِ} وَلِأَبِي عَوَانَةَ فِي "صَحِيحِهِ" : {ثَمِينَيْنِ} . بِالْمُثَلَّثَةِ بَدَلَ اَلسِّين
وَفِي لَفْظٍ لِمُسْلِمٍ، وَيَقُولُ: {بِسْمِ اَللَّهِ. وَاَللَّهُ أَكْبَرُ}
وَلَهُ: مِنْ حَدِيثِ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، {أَمَرَ بِكَبْشٍ أَقْرَنَ، يَطَأُ فِي سَوَادٍ، وَيَبْرُكُ فِي سَوَادٍ، وَيَنْظُرُ فِي سَوَادٍ، لِيُضَحِّيَ بِهِ، فَقَالَ: "اِشْحَذِي اَلْمُدْيَةَ" ، ثُمَّ أَخَذَهَا، فَأَضْجَعَهُ، ثُمَّ ذَبَحَهُ، وَقَالَ: "بِسْمِ اَللَّهِ، اَللَّهُمَّ تَقَبَّلْ مِنْ مُحَمَّدٍ وَآلِ مُحَمَّدٍ، وَمِنْ أُمّةِ مُحَمَّدٍ"}
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akichinja kondoo wawili madume wa kijivu walio na pembe. Akipiga BismiLLaah na akipiga Takbiyr, na akiweka mguu wake juu ya pambizo za shingo zao. Katika tamshi lingine: “Aliwachinja kwa mkono wake.” Katika tamshi lingine: “…walionona.” Abuu ‘Awaanah amepokea katika Swahiyh yake: “…wenye thamani kubwa.”
Vile vile katika tamshi lingine la Muslim: “Na alikuwa akisema: BismiLLaah Wa-Allaahu Akbar.”
Pia Muslim amepokea kutoka kwa Hadiyth ya ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا): “Ameamrisha kondoo mwenye pembe, mwenye miguu myeusi, mwenye tumbo leusi, na kando ya macho yake ni weusi pia. Akaletewa ili amchinje, akamuambia ‘Aaishah: ‘Ee ‘Aaishah niletee kisu’ kisha akaniambia: ‘Kinoe kwa jiwe’, nikafanya hivyo. Akachukua kisu kile na akamchukua kondoo akamlaza, akamchinja akasema:
بِسْمِ اَللَّهِ، اَللَّهُمَّ تَقَبَّلْ مِنْ مُحَمَّدٍ وَآلِ مُحَمَّدٍ، وَمِنْ أُمّةِ مُحَمَّدٍ
“BismiLLaah, Allaahumma taqabbal min Muhammad wa aali Muhammad, wa min ummati Muhammad.” Kisha akamchinja
1160.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"مَنْ كَانَ لَهُ سَعَةٌ وَلَمْ يُضَحِّ، فَلَا يَقْرَبَنَّ مُصَلَّانَا"} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَابْنُ مَاجَه، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، لَكِنْ رَجَّحَ اَلْأَئِمَّةُ غَيْرُهُ وَقْفَهُ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye uwezo na hakuchinja basi asikaribie katu Muswallaa[2] wetu.” [Imetolewa na Ahmad na Ibn Maajah na akaisahihisha Al-Haakim. Maimaam wengine wametilia nguvu kuwa ni Mawquwf]
1161.
وَعَنْ جُنْدُبِ بْنِ سُفْيَانَ رضى الله عنه قَالَ: {شَهِدْتُ اَلْأَضْحَى مَعَ رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا قَضَى صَلَاتَهُ بِالنَّاسِ، نَظَرَ إِلَى غَنَمٍ قَدْ ذُبِحَتْ، فَقَالَ: "مَنْ ذَبَحَ قَبْلَ اَلصَّلَاةِ فَلْيَذْبَحْ شَاةً مَكَانَهَا، وَمَنْ لَمْ يَكُنْ ذَبَحَ فَلْيَذْبَحْ عَلَى اسْمِ اَللَّهِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Jundub bin Sufyaan (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilishuhudia Udhw-hiyyah pamoja na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipomaliza kuswalisha watu alitazama mbuzi aliyekuwa amechinjwa, akasema: “Aliyechinja kabla kuswali achinje mnyama mwingine mahala pake na ambaye hajachinja basi achinje kwa Jina la Allaah.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
1162.
وَعَنِ اَلْبَرَاءِ بنِ عَازِبٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَامَ فِينَا رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: {"أَرْبَعٌ لَا تَجُوزُ فِي اَلضَّحَايَا: اَلْعَوْرَاءُ اَلْبَيِّنُ عَوَرُهَا، وَالْمَرِيضَةُ اَلْبَيِّنُ مَرَضُهَا، وَالْعَرْجَاءُ اَلْبَيِّنُ ظَلْعُهَا وَالْكَسِيرَةُ اَلَّتِي لَا تُنْقِي"} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ . وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Al-Baraa bin ‘Aazib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alisimama akatuhutubia: “Wanyama aina nne[3] hawafai katika Udhw-hiyyah: mwenye chongo, inayoonekana wazi chongo yake, mgonjwa anayeonekana dhahiri ugonjwa wake, kiwete anayeonekana waz ulemavu wake na mkongwe ambaye hana uboho.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha At-Tirmidhiy na Ibn Hibbaan]
1163.
وَعَنْ جَابِرٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"لَا تَذْبَحُوا إِلَّا مُسِنَّةً، إِلَّا أَنْ يَعْسُرَ عَلَيْكُمْ فَتَذْبَحُوا جَذَعَةً مِنَ اَلضَّأْنِ"} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msichinje (Udhw-hiyyah) isipokuwa musinnah,[4] isipokuwa ikiwa uzito kwenu, hapo mtachinja koo la kondoo (mwenye umri wa miezi sita hadi kumi).” [Imetolewa na Muslim]
1164.
وَعَنْ عَلِيٍّ رضى الله عنه قَالَ: {أَمَرَنَا رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَنْ نَسْتَشْرِفَ اَلْعَيْنَ وَالْأُذُنَ، وَلَا نُضَحِّيَ بِعَوْرَاءَ، وَلَا مُقَابَلَةٍ، وَلَا مُدَابَرَةٍ، وَلَا خَرْمَاءَ، وَلَا ثَرْمَاءَ"} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ. وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alituamuru kuchunguza macho na masikio, wala tusidhahi mnyama chongo, wala aliyekatwa ncha ya sikio, wala aliyekatwa masikio kwa upana wala asiye na meno ya mbele.”[5] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy, Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
1165.
وَعَنْ عَلِيِّ بْنِ أَبِي طَالِبٍ رضى الله عنه قَالَ: {أَمَرَنِي اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم أَنَّ أَقْوَمَ عَلَى بُدْنِهِ، وَأَنْ أُقَسِّمَ لُحُومَهَا وَجُلُودَهَا وَجِلَالَهَا عَلَى اَلْمَسَاكِينِ، وَلَا أُعْطِيَ فِي جِزَارَتِهَا مِنْهَا شَيْئاً} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aliy bin Abiy Twaalib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliniamuru nimsimamie ngamia wake (wa Udhw-hiyyah) na nigawe nyama yao, ngozi yake na masaruji yake kwa masikini.[6] Na nisimpe chochote mchinjaji kutokana na ngamia hao.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
1166.
وَعَنْ جَابِرِ بنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَحَرْنَا مَعَ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم عَامَ اَلْحُدَيْبِيَةِ: اَلْبَدَنَةَ عَنْ سَبْعَةٍ، وَالْبَقَرَةَ عَنْ سَبْعَةٍ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Tulichinja pamoja na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) mwaka wa Vita Vya Hudaybiyah watu saba kwa kuchinja ngamia mmoja na watu saba wakishirikiana kwa kuchinja ng’ombe mmoja.”[7] [Imetolewa na Muslim]
[1] Kuchinja ni aina mbili: Ya kwanza ni Hady na ya pili ni Udhw-hiyyah. Hady ni ile inayotolewa na Hujaji Minaa. Ama Udhw-hiyyah ni ile inayotolewa na Waislamu maeneo mengine ulimwenguni wakati wa ‘Iydul Adhw-haa au wakati wa Tashriyq. Kulingana na Wanazuoni wengi, kutoa Udhw-hiyyah ni Sunnah, kwa Wanazuoni wengine ni waajib. ‘Ibaadah hii inaitwa udhw-hiyyah kwa sababu inafanyika wakati wa dhwuha.
[2] Baadhi ya Wanazuoni wanahitimisha katika Hadiyth hii kuwa swala la kuchinja udhw-hiyyah ni la waajib. Hata hivyo Wanazuoni wengi wanaona kuwa ni Sunnah Muakkada. (Sunnah iliyosisitizwa).
[3] Mgonjwa, kiguru, chongo na dhaifu hawaruhusiwi kuchinjwa kwa ajili ya Udhw-hiyyah. Wanazuoni wanaona kuwa hukumu hii inahusu pia magonjwa mengine mwilini.
[4] Katika lugha ya Kiarabu Musinnah ni mnyama ambaye meno yake ya mwanzo yameshaondoka na kuanguka na kubadilishwa kwa meno mengine ya kawaida. Kila mnyama ana muda wake wa kutoka kwa meno. Mbuzi, kondoo na kondoo dume aliyehasiwa wanapokuwa mwaka wa kwanza na kuingia mwaka wa pili wanakuwa musinnah. Ng’ombe na jamusi wanakuwa katika hali hii wanapoingia mwaka wa tatu wa umri wao. Ngamia anakuwa anakuwa katika hali hiyo anapoingia mwaka wa sita wa umri wake.
[5] Mnyama ambaye amekatwa sikio au hata kukaruzwa, au aliyekatwa pembe haruhusiwi kuchinjwa. Hukumu inayohusu sikio na pembe ni ikiwa nusu ya viungo hivi kama vimekatwa basi hairuhusiwi kuchinjwa. Lakini ikiwa zaidi ya nusu ya viungo hivi vikiwa katika hali nzuri basi wanyama hawa wanafaa kuchinjwa. Ikiwa mnyama atakuwa amezaliwa bila ya pembe haizingatiwi kama ni ila, hata hivyo ikiwa pembe yenyewe imekatika baada ya kuzaliwa itakuwa ni ila.
[6] Ngozi, sufi na nyama ya mnyama inabidi itolewe kama Swadaqah. Mtu anayetoa Udhw-hiyyah anaruhusiwa kula nyama ile na anaweza kutumia ngozi yake. Kumpa mchinjaji nyama kama ujira wake ni jambo lenye kukatazwa. Watu wengine hawawalipi wachinjaji ujira wao, ambalo ni jambo lisilopendeza. Katika hali ambayo mchinjaji hachukui ujira wake kwa mapenzi yake basi inaruhusiwa.
[7] Udhw-hiyyah wa kondoo mmoja inatosheleza hata kwa watu ishirini wa nyumba moja. Ama udhw-hiyyah wa ng’ombe, jamusi na ngamia mmoja wanashirikiana watu saba kwa maana hiyo nyumba saba zitafaidika na udhw-hiyyah hiyo. Ikiwa udhw-hiyyah hiyo ni ya Sunnah au ni ya waajib, yote ni sawa hakuna tofauti. Siyo lazima ikawa kwa watu saba hata mtu mmoja anaweza kufanya hivyo.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَاب اَلْأَطْعِمَةِ
Kitabu Cha Vyakula
بَابُ اَلْعَقِيقَةِ
03-Mlango Wa ‘Aqiyqah[1]
1167.
عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم عَقَّ عَنْ اَلْحَسَنِ وَالْحُسَيْنِ كَبْشًا كَبْشًا} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ، وَعَبْدُ اَلْحَقِّ
لَكِنْ رَجَّحَ أَبُو حَاتِمٍ إِرْسَالَهُ
وَأَخْرَجَ اِبْنُ حِبَّانَ: مِنْ حَدِيثِ أَنَسٍ نَحْوَهُ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Alimfayia ‘Aqiyqah Hasan na Husayn[2] kondoo mmoja mmoja.”[3] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Ibn Khuzaymah, Ibn Al-Jaaruwd na ‘Abdul Haqq. Lakini Abuu Haatim ameitilia nguvu kuwa ni Mursal]
Na amepokea Ibn Hibbaan kutoka kwa Anas mfano wake.
1168.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَمْرَهُمْ، أَنْ يُعَقَّ عَنْ اَلْغُلَامِ شَاتَانِ مُكَافِئَتَانِ، وَعَنْ اَلْجَارِيَةِ شَاةٌ} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ
وَأَخْرَجَ اَلْخَمْسَةُ عَنْ أُمِّ كُرْزٍ الْكَعْبِيَّةِ نَحْوَهُ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliwaamrisha mvulana afanyiwe ‘aqiyqah kwa mbuzi wawili wanaolingana, na mtoto wa kike afanyiwe ‘Aqiyqah mbuzi mmoja.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akaisahihisha]
Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) wameipokea kutoka kwa Ummu Kurzi Al-Ka’biyyah[4] Hadiyth kama hii.
1169.
وَعَنْ سَمُرَةَ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"كُلُّ غُلَامٍ مُرْتَهَنٌ بِعَقِيقَتِهِ، تُذْبَحُ عَنْهُ يَوْمَ سَابِعِهِ، وَيُحْلَقُ، وَيُسَمَّى"} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ
Kutoka kwa Samurah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kila kijana amewekwa rahani[5] kwa ‘Aqiyqah yake, huchinjiwa siku yake ya saba,[6] hunyolewa na hupewa jina.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
[1] ‘Aqiyqah ni istwilaah inayotumika kwa wanyama, ni kichinjo kwa ajili ya mtoto mchanga anayezaliwa.
[2] Husayn alikuwa ni mdogo kuliko Hasan na takriban alikuwa mdogo kwa mwaka mmoja. Alikuwa ni mjukuu wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na maarufu kwa taqwa yake. Aliuwawa Karbala ‘Iraq tarehe kumi ya Muharram, 61 Hijriyyah.
[3] ‘Aqiyqah ni Sunnah. Hadiyth inayofuata inaelezea kuwa kuchinja kondoo wawili anachinjiwa ikiwa mtoto mwenyewe ni wa kiume, wakati Hadiythi hii inaeleza kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ameeleza kuwa kondoo mmoja ni kwa ajili ya mtoto mmoja. Hii inawezekana kuwa hapakuwepo na kondoo wengine wa kuchinja kwa wakati ule. Vinginevyo, ni kuwa kuchinja kondoo wawili kwa mtoto mmoja wa kiume ndiyo Sunnah.
[4] Ummu Kurzi Al-Ka’biyyah alikuwa ni Swahaabiyya katika kabila la Khuza’a na amepokea baadhi za Hadiyth.
[5] Hii ina maana ya kitu kilichowekwa kama dhamana, hakitumiwi. Kwa maelezo hayo ni kuwa huyo mtoto hawezi kumuombea baba yake siku ya Qiyaamah.
[6] Ni sawa sawa kama amechinjwa ng’ombe katika ‘Aqiyqah. Siku mtoto anapozaliwa ndipo atakaposomewa adhaana kwa sikio lake la kuume na Iqaamah katika sikio lake la kushoto, kulingana na baadhi ya ‘Ulamaa. Hata hivyo, Hadiyth iliyoripotiwa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy kuwa maelezo haya si sahihi. ‘Aqiyqah itekelezwe siku ya saba baada ya kuzaliwa kwa mtoto. Katika siku hiyo hiyo mtoto anapewa jina na ananyolewa nywele zake. Baada ya hapo, nywele zilizotolewa zinapimwa na thamani yake ya fedha inatolewa kama swadaqah. Vivyo hivyo, mtoto ataombewa du’aa na kufanyiwa tahniyk (kulainishiwa tende na kupewa mdomoni).
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/277
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10213&title=12-%20Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Vyakula%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D9%92%D8%A3%D9%8E%D8%B7%D9%92%D8%B9%D9%90%D9%85%D9%8E%D8%A9%D9%90
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10233&title=00-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Vyakula
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10234&title=01-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Vyakula%3A%20Mlango%20Wa%20Kuwinda%20Na%20Kuchinja
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10235&title=02-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Vyakula%3A%20Mlango%20Wa%20Kuchinja%20Udhw-hiyyah
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10240&title=03-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Vyakula%3A%20Mlango%20Wa%27%27Aqiyqah