كِتَابُ اَلْعِتْق
Kitabu Cha Ukombozi
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْعِتْقِ
00-Kitabu Cha Ukombozi
1220.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"أَيُّمَا امْرِئٍ مُسْلِمٍ أَعْتَقَ اِمْرَأً مُسْلِماً، اِسْتَنْقَذ َ اَللَّهُ بِكُلِّ عُضْوٍ مِنْهُ عُضْوًا مِنْهُ مِنَ النَّارِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِلتِّرْمِذِيِّ وَصَحَّحَهُ، عَنْ أَبِي أُمَامَةَ: {"وَأَيُّمَا امْرِئٍ مُسْلِمٍ أَعْتَقَ اِمْرَأَتَيْنِ مُسْلِمَتَيْنِ، كَانَتَا فِكَاكَهُ مِنَ النَّارِ"}
وَلِأَبِي دَاوُدَ: مِنْ حَدِيثِ كَعْبِ بْنِ مُرَّةَ: {"وَأَيُّمَا اِمْرَأَةٍ أَعْتَقَتْ اِمْرَأَةً مُسْلِمَةً، كَانَتْ فِكَاكَهَا مِنْ اَلنَّارِ}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muislaam yeyote atakayemkomboa Muislaam mwenzake, Allaah Atamuacha huru na moto,[1] kila kiungo chake kwa kila kiungo cha mtu huyo.” [Bukhaariy, Muslim]
At-Tirmidhiy amepokea na ameisahihisha kutoka kwa Abuu Umaamah: “Na mtu yeyote Muislaam atakayekomboa wanawake wawili Waislaam basi watakuwa ni kuokoka kwake dhidi ya moto.”
Abuu Daawuwd amepokea kutoka katika Hadiyth ya Ka’b bin Murrah[2]: “Na mwanamke yeyote Muislaam atakayemkomboa mwanamke Muislaam basi atakuwa ni kuokoka kwake dhidi ya moto.”
1221.
وَعَنْ أَبِي ذَرٍّ رضى الله عنه {قَالَ: سَأَلْتُ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم أَيُّ اَلْعَمَلِ أَفْضَلُ؟ قَالَ: "إِيمَانٌ بِاَللَّهِ، وَجِهَادٌ فِي سَبِيلِهِ" . قُلْتُ: فَأَيُّ اَلرِّقَابِ أَفْضَلُ؟ قَالَ: " أَعْلَاهَا ثَمَنًا، وَأَنْفَسُهَا عِنْدَ أَهْلِهَا"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Dharr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilimuuliza Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ni amali gani bora zaidi? Akasema: ‘Ni kumuamini Allaah na jihaad katika njia yake’ Nikasema: ni kuacha kupi mtumwa huru kuliko bora? Akasema: “Mwenye thamani kubwa na mzuri zaidi kwa watu wake.” [Bukhaariy, Muslim]
1222.
وَعَنِ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"مَنْ أَعْتَقَ شِرْكًا لَهُ فِي عَبْدٍ، فَكَانَ لَهُ مَالٌ يَبْلُغُ ثَمَنَ اَلْعَبْدِ، قُوِّمَ قِيمَةَ عَدْلٍ، فَأَعْطَى شُرَكَاءَهُ حِصَصَهُمْ، وَعَتَقَ عَلَيْهِ اَلْعَبْدُ، وَإِلَّا فَقَدْ عَتَقَ مِنْهُ مَا عَتَقَ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْه ِ
وَلَهُمَا: عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه {"وَإِلَّا قُوِّمَ عَلَيْهِ، وَاسْتُسْعِيَ غَيْرَ مَشْقُوقٍ عَلَيْهِ"} وَقِيلَ: إِنَّ اَلسِّعَايَةَ مُدْرَجَةٌ فِي اَلْخَبَر ِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuacha huru fungu lake katika mtumwa akawa na mali inayofikia thamani ya mtumwa (yule), atathaminishwa thamani ya uadilifu awape washirika wake mafungu yao na atamuacha huru mtumwa.[3] Vinginevyo atakuwa ameacha huru katika fungu lake.” [Bukhaariy, Muslim]
Wamepokea kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ): “La si hivyo atathaminishwa na aombwe kufanya kazi ili alipie ushuru wake bila kumtia uzito.” Imesemwa haya ya kufanya kazi ni maneno Mudrajah (yaliyoingizwa na siyo ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ
1223.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {" لَا يَجْزِي وَلَدٌ وَالِدَهُ، إِلَّا أَنْ يَجِدَهُ مَمْلُوكًا فَيُعْتِقَهُ"} رَوَاهُ مُسْلِم ٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtoto hawezi kumlipa mzazi wake isipokuwa amkute ni mtumwa amnunue na amuache huru.”[4] [Imetolewa na Muslim]
1224.
وَعَنْ سَمُرَةَ رضى الله عنه أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"مَنْ مَلَكَ ذَا رَحِمٍ مَحْرَمٍ، فَهُوَ حُرٌّ"} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَة ُ وَرَجَّحَ جَمْعٌ مِنَ الْحُفَّاظِ أَنَّهُ مَوْقُوف ٌ
Kutoka kwa Samurah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kumiliki mwenye kizazi ambaye ni maharimu,[5] basi yuko huru.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah). Kundi la wahifadhi Hadiyth wametilia nguvu kuwa ni Mawquwf]
1225.
وَعَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ رَجُلاً أَعْتَقَ سِتَّةً مَمْلُوكِينَ لَهُ، عِنْدَ مَوْتِهِ، لَمْ يَكُنْ لَهُ مَالٌ غَيْرَهُمْ، فَدَعَا بِهِمْ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَجَزَّأَهُمْ أَثْلَاثًا، ثُمَّ أَقْرَعَ بَيْنَهُمْ، فَأَعْتَقَ اِثْنَيْنِ، وَأَرَقَّ أَرْبَعَةً، وَقَالَ لَهُ قَوْلاً شَدِيدًا} رَوَاهُ مُسْلِم ٌ
Kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Mtu mmoja aliwaacha huru watumwa sita wakati wa kifo chake wala hakuwa na mali zaidi ya hiyo.[6] Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akawaita akawagawa mafungu matatu kisha akapiga kura miongoni mwao, akawaacha huru wawili na wanne akawabakisha kwenye utumwa. Na akamuambia maneno mazito yule mwenyewe.”[7] [Imetolewa na Muslim]
1226.
وَعَنْ سَفِينَةَ رضى الله عنه {قَالَ: كُنْتُ مَمْلُوكًا لِأُمِّ سَلَمَةَ فَقَالَتْ: أُعْتِقُكَ، وَأَشْتَرِطُ عَلَيْكَ أَنْ تَخْدِمَ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم مَا عِشْتَ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَالْحَاكِم ُ
Kutoka kwa Safiynah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilikuwa mtumwa wa Ummu Salamah akaniambia: ‘Nitakuacha huru na nitakupa sharti uwe ukimtumikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) katika maisha yako.”[8] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Al-Haakim]
1227.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"إِنَّمَا اَلْوَلَاءُ لِمَنْ أَعْتَقَ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ فِي حَدِيث ٍ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika Al-Walaau ni wa mwenye kuacha huru.”[9] [Bukhaariy, Muslim katika Hadiyth ndefu]
1228.
وَعَنِ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {" اَلْوَلَاءُ لُحْمَةٌ كَلُحْمَةِ اَلنَّسَبِ، لَا يُبَاعُ وَلَا يُوهَبُ"} رَوَاهُ اَلشَّافِعِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِم ُ وَأَصْلُهُ فِي "اَلصَّحِيحَيْنِ" بِغَيْرِ هَذَا اَللَّفْظ ِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Al-Walaau ni undugu kama undugu wa nasaba, hauuzwi wala hautolewi bure (hiba/zawadi).” [Imetolewa na Ash-Shaafi’iy na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim. Asili yake imo katika Swahiyh Al-Bukhaariy na Swahiyh Al-Muslim kwa tamshi lingine lisilokuwa hili]
[1] Malipo na thawabu ayapatayo mtu ni yale ya kumuacha huru mtumwa Muumini, Pamoja na kuwa kuna malipo na fadhila za kumuacha huru mtumwa kafiri. Hata hivyo kumuacha huru mtumwa Muumini kuna malipo makubwa zaidi.
[2] Ka’b bin Murrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alikuwa ni Swahaba na inasemekana kuwa alikuwa akiitwa Murrah bin Ka’b. Aliishi Basra kisha akahamia Jordan hadi yalipomkuta mauti yake mwaka 57 au 59 Hijriyyah.
[3] Hadiyth hii inatujulisha kuwa mtumwa ambae ameacha huru nusu ana hadhi ya dhamana iliyozuiwa hawezi kuuzwa au kutolewa kama zawadi.
[4] Kulingana na Hadiyth hii Wanazuoni wa Zahiriyah wana muono kuwa baba hawezi kuzingatiwa kuwa yuko huru kwa sharti la kulipiwa na mwanae, bali atakuwa huru hadi mwanae atakapotamka hivyo. Wanazuoni wengine wanaona kuwa baba keshakuwa huru madamu amenunuliwa na mwanae. Hukumu hii pia inamhusu mama. Hadiyth hii kwa upande mmoja inatuelezea nafasi za wazazi wawili na kwa upande mwingine inaelezea fadhila za kumuacha huru mtumwa.
[5] Ndugu wa karibu kama vile baba, mtoto, kaka, dada, ndugu ya baba, kaka wa mama n.k. ambao wapo karibu kiasi cha kuwa huwezi kuoa (au kuolewa) hawawezi kuwa katika hadhi ya mtumwa na bwana wake. Ikiwa aliyekuwa utumwani ni mwanamke, basi hukumu inakuwa ni wazi zaidi. Katika hali hiyo itaangaliwa kama wanaweza kuoana au sivyo. Kama ni sawa, basi hukumu ile inatumika kwao, kwani watakuwa ni Mahram.
[6] Mafundisho tunayoyapata katika Hadiyth hii ni kuwa swadaqah inayotolewa na mtu mgonjwa ni kama vile kuacha wasia. Mtu haruhusiwi kuacha wasia zaidi ya theluthi ya mali yake au kama ni zawadi au wakfu. Maneno makali aliyoyasema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kwa mtu yule yalikuwa: “Kama ningejulishwa habari za mtu yule hapo kabla basi nisingeruhusu kuzikwa katika makaburi ya Waislaam.”
[7] Kwa sababu theluthi mbili za mali ya marehemu yanatakiwa kuenda kwa warithi wake.
[8] Kuwa inawezekana kuweka sharti unapoacha huru mtumwa kama alivyofanya Ummu Salamah kuwa aendelee kumtumikia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kwa muda uliokubaliwa. Uhalaal wa hili unaonekana pale Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokuwa hakulikataza jambo hili.
[9] Al-Walaau ni mirathi ya mtumwa aliyeachwa huru inamilikiwa na aliyemuacha huru. Haitakiwi kuuzwa wala kutolewa zawadi.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْعِتْقِ
Kitabu Cha Ukombozi
بَابُ اَلْمُدَبَّرِ وَالْمُكَاتَبِ وَأُمِّ اَلْوَلَدِ
01-Mlango Wa Mudabbar,[1] Al-Mukaatab[2] Na Ummul-Walad[3]
1229.
عَنْ جَابِرٍ رضى الله عنه {أَنَّ رَجُلًا مِنْ اَلْأَنْصَارِ أَعْتَقَ غُلَامًا لَهُ عَنْ دُبُرٍ، لَمْ يَكُنْ لَهُ مَالٌ غَيْرُهُ، فَبَلَغَ ذَلِكَ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم . فَقَالَ: "مَنْ يَشْتَرِيهِ مِنِّي؟" فَاشْتَرَاهُ نُعَيْمُ بْنُ عَبْدِ اَللَّهِ بِثَمَانِمَائَةِ دِرْهَمٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْه ِ وَفِي لَفْظٍ لِلْبُخَارِيِّ: فَاحْتَاج َ وَفِي رِوَايَةٍ لِلنَّسَائِيِّ: {وَكَانَ عَلَيْهِ دَيْنٌ، فَبَاعَهُ بِثَمَانِمَائَةِ دِرْهَمٍ، فَأَعْطَاهُ وَقَالَ: " اِقْضِ دَيْنَكَ"}
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Mtu mmoja miongoni mwa Answaar aliahidi uhuru wa mtumwa wake[4] baada ya kufa hakuwa na mali isipokuwa mtumwa huyo. Habari hiyo ikamfikia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: ‘Ni nani atakayemnunua?’ Nu’aym bin ‘Abdillaah[5] akamnunua kwa dirhamu mia nane.” [Bukhaariy, Muslim, katika tamshi lingine la Al-Bukhaariy: ‘akahitajia’]
Katika Riwaayah ya An-Nisaaiy: “Alikuwa ana deni akamuuza kwa dirhamu mia nane na akampa mwenyewe akamuambia: ‘lipa deni lako’.”
1230.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ، عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم {قَالَ: " اَلْمُكَاتَبُ عَبْدٌ مَا بَقِيَ عَلَيْهِ مِنْ مُكَاتَبَتِهِ دِرْهَمٌ"} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ بِإِسْنَادٍ حَسَن ٍ وَأَصْلُهُ عِنْدَ أَحْمَدَ، وَالثَّلَاثَةِ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِم ُ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb amepokea kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Al-Mukaatab ni mtumwa madamu katika mkataba wake imebakia dirhamu moja.”[6] [Imetolewa na Abuu Daawuwd kwa Isnaad Hasan. Asili yake imo kwa Ahmad na Ath-Thalaathah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd) na akaisahihisha Al-Haakim]
1231.
وَعَنْ أَمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {إِذَا كَانَ لِإِحْدَاكُنَّ مُكَاتَبٌ، وَكَانَ عِنْدَهُ مَا يُؤَدِّي، فَلْتَحْتَجِبْ مِنْهُ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَة ُ وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيّ ُ
Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Iwapo mmoja wenu ana Mukaatab naye anacho cha kutoa basi ajisitiri kwake.”[7] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
1232.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {يُودَى اَلْمُكَاتَبُ بِقَدْرِ مَا عَتَقَ مِنْهُ دِيَةَ اَلْحُرِّ، وَبِقَدْرِ مَا رَقَّ مِنْهُ دِيَةَ اَلْعَبْدِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيّ ُ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Al-Mukaatab hufidiwa fidiya ya muungwana kiasi alicholipia katika mali ya kuandikiana na hufidiwa fidiya ya mtumwa kiasi kilichobakia katika deni.”[8] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na An-Nisaaiy]
1233.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ اَلْحَارِثِ أَخِي جُوَيْرِيَةَ أُمِّ اَلْمُؤْمِنِينَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {مَا تَرَكَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم عِنْدَ مَوْتِهِ دِرْهَمًا، وَلَا دِينَارًا، وَلَا عَبْدًا، وَلَا أَمَةً، وَلَا شَيْئًا، إِلَّا بَغْلَتَهُ اَلْبَيْضَاءَ، وَسِلَاحَهُ، وَأَرْضًا جَعَلَهَا صَدَقَةً} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيّ ُ
Kutoka kwa ‘Amr bin Al-Haarith[9] nduguye Juwayriyah Ummul-Mu-miniyna (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipofariki hakuacha dirhamu wala dinari wala mtumwa wala mjakazi wala chochote isipokuwa nyumbu wake mweupe, silaha yake na ardhi aliyoitoa swadaqah.”[10] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1234.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {أَيُّمَا أَمَةٍ وَلَدَتْ مِنْ سَيِّدِهَا، فَهِيَ حُرَّةٌ بَعْدَ مَوْتِهِ} أَخْرَجَهُ اِبْنُ مَاجَهْ، وَالْحَاكِمُ بِإِسْنَادٍ ضَعِيف ٍ
وَرَجَّحَ جَمَاعَةٌ وَقْفَهُ عَلَى عُمَرَ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mjakazi yeyote aliyezaa na bwana wake, basi yuko huru baada ya kufa kwake.” [Imetolewa na Ibn Maajah na Al-Haakim kwa Isnaad Dhaifu. Kundi la Wanazuoni wa Hadiyth wana mtazamo kuwa Hadiyth hii ni Mawquwf kwa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ)]
1235.
وَعَنْ سَهْلِ بْنِ حُنَيْفٍ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {مَنْ أَعَانَ مُجَاهِدًا فِي سَبِيلِ اَللَّهِ، أَوْ غَارِمًا فِي عُسْرَتِهِ، أَوْ مُكَاتَبًا فِي رَقَبَتِهِ، أَظَلَّهُ اَللَّهُ يَوْمَ لَا ظِلَّ إِلَّا ظِلُّهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِم ُ
Kutoka kwa Sahl bin Hunayaf (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kumsaidia mpigana jihaad katika Njia ya Allaah, au mwenye deni katika uzito wake, au Mukaatab katika utumwa wake, Allaah Atamfunika kivuli siku ambayo hakuna kivuli isipokuwa kivuli Chake.” [Imetolewa na Ahmad na akaisahihisha Al-Haakim]
[1] Ni maneno anayoambiwa mtumwa na bwana wake, “Uko huru baada ya kufa kwangu.”
[2] Mtumwa anapoingia katika mkataba na bwana wake ili anunue uhuru wake.
[3] Kijakazi anayemzalia bwana wake.
[4] Tumejifunza katika Hadiyth hii kuwa bwana anaweza kumuacha mtumwa wake Mudabbar, maadamu ya kuwa hayuko katika hali ya ugonjwa. Wanazuoni wana muono kuwa ichukuliwe kutoka katika theluthi ya mali yake kama usia. Wanazuoni wengine wanaona kuwa ruhusa kumuuza Mudabbar ila kwa mahitaji, au kulipa madeni ya bwana wake.
[5] Kun-ya yake ilikuwa ni An-Nakhkham, alikuwa Mqurayshi wa ukoo wa ‘Aad. Alisilimu mda mrefu akafanya kuwa ni siri, alipotaka kuhama watu wa kabila lake wakamtaka akae na afuate dini aitakayo, kwani alikuwa akiwasaidia wajane wao na mayatima wao, hivyo alibaki. Alihama katika mwaka wa Hudaybiyah. Aliuwawa katika Fat-hi ya Shaam wakati wa Ukhalifa wa Abuu Bakr Asw-Swidiq au wa ‘Umar Al-Faruwq.
[6] Ina maana kuwa ikiwa Al-Mukaatab hajamaliza deni lake kulipa dhamana yake, ataendelea kubaki kuwa ni mtumwa. Hili linathibitisha nukta moja kuwa mtumwa anamiliki anachopata. Haina maana kuwa mtumwa hawezi kumiliki kitu. Al-Mukaatab ni mwanamme au mwanamke mtumwa ambaye anaingia katika mkataba na bwana wake kuwa iwapo atamuacha huru atampa kadha na kadha kwa ajili ya uhuru wake. Aina hii ya mkataba unaitwa Mukaatabah na mtumwa anayeingia katika mkataba huu anaitwa Al-Mukaatab.
[7] Bi mkubwa kishariy’ah hana haja ya kuficha uso wake kwa mtumwa wake, kwani anakuwa kama mtoto wake. Lakini ikiwa Al-Mukaatab ameshakusanya kiasi cha fedha cha kujikomboa, itabidi aanze kuvaa hijab kamili kwake. Hadiyth hii inabainisha kuwa maadamu Al-Mukaatab hajakamilisha malipo kamili katika mkataba wake bado anahesabiwa kuwa ni mtumwa.
[8] Al-Khatwaab amesema: “Makubaliano ya Wanazuoni wa Fiqh ni kuwa Al-Mukaatab ni mtumwa kulingana na adhabu pamoja na fidiya, muda wa kuwa bado hajakamilisha dirhamu moja. Hata hivyo, Ibraahiym An-Nakhai na rai kutoka kwa ‘Aliy wanakubaliana na maana ya wazi yaliyopokewa kutoka kwenye Hadiyth hii.”
[9] Huyu ni Al-Haarith bin Abuu Dhirar bin Habib Al-Khuza’i Al-Mustwaliqi. Alikuwa ni Swahaba na ana Hadiyth moja tu kulingana na Wanazuoni wa Hadiyth.
[10] Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipofariki, Maria Qibtwiyyah mama wa mtoto wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) Ibraahiym alikuwa bado yu hai. Alikuwa ni mtumwa wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Kwa kuwa alikuwa mama wa mtoto wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), alikuwa huru baada ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kufariki. Lengo la kutaja Hadiyth hii ni kuwa Ummul-Walad (mtumwa wa kike aliyemzalia bwana wake), anakuwa huru baada ya kufariki bwana mwenyewe.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/277
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10262&title=15-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Ukombozi%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D9%92%D8%B9%D9%90%D8%AA%D9%92%D9%82%D9%90
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10263&title=00-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Ukombozi
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10264&title=01-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Ukombozi%3A%20Mlango%20Wa%20Mudabbar%2C%20%20Al-Mukaatab%20%20Na%20Ummul-Walad