Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب احتمال الأذى
076-Mlango Wa Kuvumilia Maudhi
Alhidaaya.com [1]
قَالَ الله تَعَالَى:
وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣٤﴾
Na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. [Aal-'Imraan: 134]
وَلَمَن صَبَرَ وَغَفَرَ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ﴿٤٣﴾
Na atakayevuta subira na akasamehe, hakika hilo bila shaka ni katika mambo ya kuazimiwa. [Ash-Shuwraa: 43]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رَجُلاً ، قَالَ : يَا رسول الله ، إنّ لي قَرَابةً أصِلُهم وَيَقْطَعُونِي ، وَأُحْسِنُ إلَيْهِمْ وَيُسِيئُونَ إلَيَّ ، وَأحْلُمُ عَنهم وَيَجْهَلُونَ عَلَيَّ ! فَقَالَ : (( لَئِنْ كُنْتَ كَمَا قُلْتَ ، فَكأنَّمَا تُسِفُّهُمُ الْمَلَّ ، وَلاَ يَزَالُ مَعَكَ مِنَ اللهِ تَعَالَى ظَهيرٌ عَلَيْهِمْ مَا دُمْتَ عَلَى ذَلِكَ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mtu mmoja alisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi nina jamaa wa karibu nawaunga, wao wananikata. Nawafanyia wema wao wananitendea uovu, nawafanyia upole wao wananifanyia ujinga." Akasema: "Ukiwa kama uanvyosema basi ni kama unawalisha jivu la moto. Msaada wa Allaah hautaacha kuwa pamoja nawe maadamu utadumu juu ya hilo." [Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10795&title=076-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuvumilia%20Maudhi