Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب آداب السلام
03-Mlango Wa Adabu za Salam
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يُسَلِّمُ الرَّاكِبُ عَلَى المَاشِي ، وَالمَاشِي عَلَى القَاعِدِ ، وَالقَليلُ عَلَى الكَثِيرِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
وفي رواية للبخاري : (( والصغيرُ عَلَى الكَبيرِ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Aliyepanda atamsalimia anayetembea kwa miguu, na anayetembea kwa miguu atamsalimia aliyekaa na wachache watawasalimia walio wengi." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: "Na mtoto atamsalimia mkubwa."
Hadiyth – 2
وعن أَبي أُمَامَة صُدَيِّ بن عجلان الباهِلي رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ أَوْلى النَّاسِ بِاللهِ مَنْ بَدَأهُمْ بِالسَّلامِ )) رواه أَبُو داود بإسنادٍ جيدٍ .
ورواه الترمذي عن أَبي أُمَامَةَ رضي الله عنه ، قِيلَ : يَا رسول الله ، الرَّجُلانِ يَلْتَقِيَانِ أَيُّهُمَا يَبْدَأُ بِالسَّلاَمِ ؟ ، قَالَ : (( أَوْلاَهُمَا بِاللهِ تَعَالَى )) قَالَ الترمذي : (( هَذَا حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Umamah Swudayy bin 'Ajlaan Al-Baahiliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika aliye karibu zaidi na Allaah ni yule anayeanza kutoka salamu." [Abu Daawuwd kwa Isnaad nzuri].
Na ameipokea At-Tirmidhiy kutoka kwa Abu Umamah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Aliulizwa: "Ee Rasuli wa Allaah! Watu wawili wanaokutana, ni yupi anayefaa kutoa salamu?" Akasema: "Yule aliye karibu na Allaah Ta'aalaa." [At-Tirmidhiy na akasema ni Hadiyth Hasan].
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11024&title=03-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Adabu%20za%20Salam