Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الصدقة عن الميت والدعاء لَهُ
19-Mlango Wa Kumtolea Swadaqah Maiti na Kumuombea Dua
Alhidaaya.com [1]
قَالَ الله تَعَالَى:
وَالَّذِينَ جَاءُوا مِن بَعْدِهِمْ يَقُولُونَ رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ ﴿١٠﴾
Na wale waliokuja baada yao wanasema: Rabb wetu! Tughufurie na ndugu zetu ambao wametutangulia kwa iymaan. [Al-Hashr: 10]
Hadiyth – 1
وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ رجلاً قَالَ للنبيِّ صلى الله عليه وسلم : إنَّ أُمِّي افْتُلِتَتْ نَفْسُهَا وَأُرَاهَا لَوْ تَكَلَّمَتْ تَصَدَّقَتْ ، فَهَلْ لَهَا أجْرٌ إنْ تَصَدَّقْتُ عَنْهَا ؟ قَالَ : (( نَعَمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) alisema mtu fulani alimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Mama yangu amekufa nadhani lau angesema angetoa sadaka. Je, anapata thawabu nikimtolea sadaka?" Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Ndiyo." [Al-Bukhaariy na muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا مَاتَ الإنْسَانُ انْقَطَعَ عَمَلُهُ إِلاَّ مِنْ ثَلاثٍ : صَدَقةٍ جَاريَةٍ ، أَوْ عِلْمٍ يُنْتَفَعُ بِهِ ، أَوْ وَلَدٍ صَالِحٍ يَدْعُو لَهُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kwake Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapokufa mwanadamu hukatika amali yake isipokuwa mambo matatu: Sadaka endelevu, au elimu yenye manufaa au mtoto mwema anamuombea dua." [Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11068&title=19-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kumtolea%20Swadaqah%20Maiti%20na%20Kumuombea%20Dua