Swahiyh Fiqh As-Sunnah
كِتَابُ الأَطْعِمَةِ وَالأَشْرِبةِ وَمَا يَتَعَلَّقُ بِهِمَا
Kitabu Cha Vyakula Na Vinywaji Na Yanayohusiana Na Viwili Hivi
Alhidaaya.com [1]
Adabu Za Kula
027-Kumwombea Du’aa Aliyeandaa Au Kualika Chakula
12- Kumwombea Du’aa Aliyeandaa Au Kualika Chakula. Kati ya du’aa zilizothibiti kwa hilo ni:
"أَفْطَـرَ عِنْدَكُمُ الصَّـائِمُوْنَ ، وَأَكَلَ طَعَامَـكُمُ الأبْـرَارُ ، وَصَلَّـتْ عَلَـيْكُمُ الملائِكَـةُ"
“Wamefungua kwenu waliofunga, na wamekula chakula chenu watu wema, na Malaika wamewaombeeni rahmah”. [Hadiyth Swahiyh kwa wenza wake. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (3854), Ibn Maajah (1747) na wengineo].
"اللّهُـمَّ بارِكْ لَهُمْ فيما رَزَقْـتَهُم، وَاغْفِـرْ لَهُـمْ وَارْحَمْهُمْ"
“Ee Allaah! Wabarikie katika Ulivyowaruzuku, Waghufirie na Warehemu”.
[Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (3805), At-Tirmidhiy (3500) na Abu Daawuwd (3241)].
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11186&title=027-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Kitabu%20Cha%20Vyakula%20Na%20Vinywaji%3A%20Kumwombea%20Du%E2%80%99aa%20Aliyeandaa%20Au%20Kualika%20Chakula