Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Tangulizi Za Suwrah Za Qur-aan > 055-Ar-Rahmaan: Utangulizi Wa Suwrah

055-Ar-Rahmaan: Utangulizi Wa Suwrah

 

055-Ar-Rahmaan: Utangulizi Wa Suwrah

 

Alhidaaya.com [1]

 

 

Imeteremka: Makkah

 

Idadi Za Aayah: 78

 

Jina La Suwrah: Ar-Rahmaan

 

Suwrah imeitwa Ar-Rahmaan (Jina la Allaah), na yanayodalilisha, ni kutajwa mwanzo kabisa Suwrah, Aayah namba (1).

 

Miongoni Mwa Makusudio Ya Suwrah:

 

1-Kuwakumbusha majini na waanadam Neema za Allaah (سبحانه وتعالى) zilizojificha na zilizodhahiri, na athari za Rehma Zake (Allaah) duniani na Aakhirah. [Al-Mukhtaswar Fiy Tafsiyr Al-Qur-aan Al-Kariym]

 

2-Kukumbusha Uadhimu wa Allaah (عزّ وجلّ) na kubainisha wazi Neema Zake kwa Viumbe Vyake duniani na Aakhirah na kuwapinga wenye kukosa shukurani nazo. 

 

Miongoni Mwa Maudhui Ya Suwrah:

 

1-Suwrah imefunguliwa kwa kumtukuza Allaah (سبحانه وتعالى) na ihsaan Yake kwa viumbe kwa kuwaelimisha Qur-aan, Uwezo Wake wa kuwaumba na kuwafunza ufasaha.

 

2-Imebainisha Uwezo wa Allaah (سبحانه وتعالى) na baadhi ya Neema Zake kwa Viumbe Vyake.

 

3-Suwrah imekariri baada ya kila Aayah au Aayah chache Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى) inayowahusu majini na wanaadam:

فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﴿١٣﴾

“Basi ni zipi katika Neema za Rabb wenu mnazikadhibisha.”

 

Hivyo basi imekariri mara 31 katika Suwrah hii tukufu.

 

4-Imekumbusha kutoweka kwa kila kilichopo juu ya mgongo wa ardhi, na kwamba Atakayebakia ni Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee. Na kwamba Anayepaswa kuombwa ni Yeye Pekee.

 

5-Imebainishwa udhalili na udhaifu wa majini na wanaadam kwamba hawataweza kupenya katika zoni za mbingu na ardhi. Na pindi wakijaribu kutaka kupenya, wataangamizwa kwa mwako wa moto!

 

6-Imetaja baadhi ya matukio na vitisho vya Siku ya Qiyaamah na  mwisho mbaya wa makafiri, kuingizwa katika moto wa Jahannam.

 

7-Imetajwa aina mbili za mabustani ya Jannah na kila moja zimebainishwa raha na neema zake mbalimbali: (i) bustani mbili ambazo matawi yake yametanda (ii) bustani mbili nyenginezo ambazo rangi yake ni kijani iliyokoza.

 

8-Suwrah imekhitimishwa kwa kumtukuza Allaah (سبحانه وتعالى) Mwenye Ujalali na Ukarimu na Jina Lake Ambalo Limebarikika.

 

 

 

Share [2]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/11562

Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11562&title=055-Ar-Rahmaan%3A%20Utangulizi%20Wa%20Suwrah