Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > 10D-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: كتاب الزواج Kitabu Cha Ndoa: الإِشْتِرَاطُ فِيْ عَقْدِ النِّكَاحِ Kuwekeana Masharti Katika ‘Aqdi Ya Ndoa > 01-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Ndoa: Kuwekeana Masharti Katika ‘Aqdi Ya Ndoa: (a) Vigawanyo Vya Masharti

01-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Ndoa: Kuwekeana Masharti Katika ‘Aqdi Ya Ndoa: (a) Vigawanyo Vya Masharti

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الزَّوَاجِ

 

Kitabu Cha Ndoa

 

 

الإِشْتِرَاطُ فِيْ عَقْدِ النِّكَاحِ

 

Kuwekeana Masharti Katika ‘Aqdi Ya Ndoa

 

 

Alhidaaya.com [1]

 

 

 

01:  Vigawanyo Vya Masharti: (a) Sehemu Ya Kwanza:  Masharti yanayoendana na dhana ya ‘aqdi na makusudio ya kisharia.

 

Linalokusudiwa kiujumla ni mmoja kati ya wanandoa watarajiwa kumwekea mwenzake masharti yanayofungamanishwa na ‘aqdi ya ndoa au kabla ya kufungwa ‘aqdi.

 

Masharti haya yanagawanyika katika sehemu tatu:

 

Sehemu ya kwanza:  Masharti yanayoendana na dhana ya ‘aqdi na makusudio ya kisharia.

 

Ni kama mke mtarajiwa kushurutisha mumewe mtarajiwa atangamane naye kwa wema, ampe matumizi, amnunulie mavazi na ampatie nyumba ya kuishi, na kama ana wake wengine, basi awatendee wote kwa usawa.

 

Au mume mtarajiwa ashurutishe mke asitoke nyumbani ila kwa idhini yake, au asimkatalie tendo la ndoa wakati akihitajia, au asitumie mali yake ila kwa ridhaa yake na mfano wa hayo.

 

Hukmu Ya Masharti Haya: 

 

Kwa mujibu wa itifaki ya ‘Ulamaa, masharti haya yanakubalika kisharia, yako sahihi, na ni lazima yatekelezwe.

 

 

 

Share [2]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/11937

Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11937&title=01-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Kitabu%20Cha%20Ndoa%3A%20Kuwekeana%20Masharti%20Katika%20%E2%80%98Aqdi%20Ya%20Ndoa%3A%20%28a%29%20Vigawanyo%20Vya%20Masharti