Swahiyh Fiqh As-Sunnah
كِتَابُ الزَّوَاجِ
Kitabu Cha Ndoa
الحُقُوْقُ بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ
Haki Za Kutendeana Kati Ya Mke Na Mume
Alhidaaya.com [1]
08: Haki Zinazompasa Mke Kumtendea Mumewe: 8-Amlinde Kwa Kujichunga Yeye Mwenyewe, Watoto Wa Mumewe Na Mali Yake:
Allaah Ta’alaa Amesema:
"فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّـهُ"
Basi wanawake wema ni wale watiifu wenye kujihifadhi katika hali ya kutokuweko waume zao kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajihifadhi. [An-Nisaa: 34]
At-Twabariy akiifasiri aayah hii amesema: “Yaani, wanajihifadhi wenyewe wakati waume zao wanapokuwa hawapo, kwa kuzilinda tupu zao na mali za waume zao”.
Nyuma tumeitaja Hadiyth hii isemayo kuhusu mwanamke bora zaidi isemayo:
“Ni yule anayemsikiliza mumewe anapomwamrisha, anamfurahisha anapomtazama, na anamlinda kwa kujichunga yeye mwenyewe na mali ya mumewe”. [Hadiyth Swahiyh. An-Nasaaiy (6/68)]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F12021&title=09-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Kitabu%20Cha%20Ndoa%3A%20Haki%20Za%20Kutendeana%20Kati%20Ya%20Mke%20Na%20Mume%3A%20Haki%20Zinazompasa%20Mke%20Kumtendea%20Mumewe%3A%20%208-Amlinde%20Kwa%20Kujichunga%20Yeye%20Mwenyewe%2C%20Watoto%20Wa%20Mumewe%20Na%20Mali%20Yake