Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika (آداب الزفاف في السنة المطهرة) > 18-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Yanayoruhusiwa Anapokuwa Katika Hedhi

18-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Yanayoruhusiwa Anapokuwa Katika Hedhi

Mume anaruhusiwa kustarehe na mkewe kwa njia yoyote isipokuwa sehemu zake za siri anapokuwa katika Hedhi. Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu jambo hili:

Kwanza:

((...اصْنَعُوا كُلَّ شَيْءٍ إِلاَّ النِّكَاحَ))

"…fanyeni kila kitu isipokuwa jimai pekee"[1]

 
 

Pili:

عن عَائِشَةَ رضي الله عنها ، قَالَتْ:  كانَ رَسُولُ اللَّهِ، يَأْمُرُ إِحْدَانَا إِذا كَانَتْ حَائِضاً أَنْ تَتَّزِرََ ثُمَّ يُضَاجِعُهَا زَوْجُهَا وَقالَتْ مَرَّةً: يُبَاشِرُهَا.

Kutoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema: "Tulipokuwa katika siku zetu (hedhi) Mtume alikuwa akituamrisha tuvae nguo kiunoni ili mume aweze kulala naye". Na akasema (mama wa waumini ‘Aaishah) pia …"Mumewe aweze kumkumbatia na kumpapasa".[2]

 

Tatu:

عن بَعْضِ أزْوَاجِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قالَتْ: إنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إذَا أرَادَ مِنَ الْحَائِضِ شَيْئاً ألْقَى عَلَى فَرْجِهَا ثَوْباً [ ثم صنع ما أراد]  

Kutoka kwa mmoja wa wake zake Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambaye amesema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipokuwa anataka kitu (kufurahi naye) kutoka kwa wake zake siku za hedhi, alikuwa anaweka nguo katika sehemu zake za siri kisha hufanya anavyotaka".[3]

 

 


[1] [1] Muslim, Abu 'Awwaanah na Abu Daawuud

[2] [2] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[3] [3] Abu Daawuud: Swahiyh

Share [4]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/1591

Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/modules/fckeditor/fckeditor/editor/fckeditor.html?InstanceName=edit-body&Toolbar=Default#_ftnref1
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/modules/fckeditor/fckeditor/editor/fckeditor.html?InstanceName=edit-body&Toolbar=Default#_ftnref2
[3] http://www.alhidaaya.com/sw/modules/fckeditor/fckeditor/editor/fckeditor.html?InstanceName=edit-body&Toolbar=Default#_ftnref3
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F1591&title=18-Adabu%20Za%20Ndoa%20Katika%20Sunnah%20Iliyotakasika%3A%20Yanayoruhusiwa%20Anapokuwa%20Katika%20Hedhi%20