Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Kutoa Zakaah (Zakaatul-Maal) > 011-Kutoa Zakaah: Mtoto Na Mpungufu Wa Akili

011-Kutoa Zakaah: Mtoto Na Mpungufu Wa Akili

 

Kutoa Zakaah: Mtoto Na Mpungufu Wa Akili

 

Alhidaaya.com [1]

 

 

Inamuwajibikia aliyekabidhiwa mali ya yatima au ya mtu mwenye upungufu wa akili kuitolea Zakaah mali hiyo ikifikia kiwango chake.

 

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amru (Radhwiya Allaahu ‘anhu), anasema kuwa; Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

"Mwenye kumlea yatima mwenye mali, basi aifanyie biashara mali hiyo na asiiache mpaka ikamalizika kwa kuliwa na Swadaqah (Zakaah)".

 

Anasema Shaykh Sayyid Saabiq katika Fiqhis Sunnah kuwa; Isnadi yake ina udhaifu ndani yake. Akaendelea kusema:

 

“Anasema Al-Haafidh kuwa Hadiyth hii ina ushahidi kuwa ni 'Mursal' iliyorushwa moja kwa moja mpaka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) bila ya kutaja isnadi. Ama Imaam Ash-Shaafi’iy ameikubali (hadithi hii) kwa sababu zipo Hadiyth nyingi zinazoelezea juu ya kuwajibika kwa Zakaah katika mali yoyote ile.  Anasema Imaam At-Tirmidhiy kuwa wanavyuoni wamekhitalifiana juu ya kuwajibika kuitolea Zakaah mali ya yatima,” amemaliza kusema Shaykh Sayyid Saabiq.

 

Share [2]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/4619

Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F4619&title=011-Kutoa%20Zakaah%3A%20Mtoto%20Na%20Mpungufu%20Wa%20Akili