Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Fataawaa: Yanayobatilisha Na Yasiyobatilisha Swawm

Fataawaa: Yanayobatilisha Na Yasiyobatilisha Swawm

Fataawa Za Ramadhwaan-'Iyd [1]

 

 

 

www.alhidaaya.com [2]

 

 

 

Share [3]

01-Imaam Ibn Baaz: Dawa Ya Mswaki Inabatilisha Swawm?

Dawa Ya Mswaki Inabatilisha Swawm?

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com [4]

 

SWALI:

 

Je, dawa ya mswaki inabatilisha Swawm?

 

JIBU:

 

Dawa ya mswaki haibatilishi Swawm ikiwa atasafisha meno yake kisha ateme bila ya kuimeza. Ikiwa atameza kwa kukusudia, Swawm yake imebatilika.

 

[Mawqi’ Ar-Rasmiy – Imaam Ibn Baaz] [5]

 

 

Share [6]

03-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Alisukutua Maji Baridi Akiwa Katika Swawm Kutokana Na Mdomo Kuwa Mkavu Mno

Alisukutua Maji Baridi Akiwa Katika Swawm Kutokana Na Mdomo Kuwa Mkavu Mno

 

 Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com [4]

 

 

SWALI:

 

Nilikuwa mja mzito na hali ya hewa ilikuwa ni joto mno mdomo wangu ukawa umekauka, basi nikafanya madhwmadhwah (kusukutua) kwa maji ya baridi ili kuurutubisha mdomo wangu, lakini nilijitahadharisha kutokumeza maji. Je, nimefanya dhambi na je, nilipe kafara kwa hilo?

 

 

JIBU:

 

Kutokana na ulivyosema, hakuna dhambi juu yako na huwajibiki kulipa siku hiyo uliyofanya madhwmadhwah kwa maji kwa sababu haibatilishi swawm ya mtu.

 

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 

[Fataawa Al-Lajnah Ad-Daaimah Lil Buhuwth Al-‘Ilmiyyah Wal Iftaa (20344)]

 

 

Share [7]

04-Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Kujipaka Au Kunusa Mafuta Mazuri Akiwa Katika Swawm

Kujipaka Au Kunusa Mafuta Mazuri Akiwa Katika Swawm

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com [4]

 

 

SWALI:

 

Nini hukumu ya mtu aliyefunga na kutumia mafuta mazuri  siku za Ramadhaan?

 

JIBU:

 

Hakuna ubaya kutumia na kunusa mafuta mazuri  siku za Ramadhwaan isipokuwa kufukiza bukhuwr (udi) usikaribie hadi ukavuta pumzi za moshi na ukaingia tumboni.

 

[Imaam Muhammad bin Swaalih Ibn ‘Uthyamiyn - Fiqhul ‘Ibaadaat Uk. No. 217 Maktabatul-Iymaan]

 

Share [8]

05-Imaam Ibn Qudaamah Al-Maddisiyy: Aliyesilimu Katika Ramadhwaan Anawajibika Swiyaam?

Aliyesilimu Katika Ramadhwaan Anawajibika Swiyaam?

 

Imaam Ibn Qudaamah Al-Maddisiyy

 

www.alhidaaya.com [4]

 

 

Al-Khiraqiy kasema:

"Ikiwa Kafiri atasilimu wakati wa Ramadhwaan, anatakiwa kufunga mwezi (masiku) yaliyobakia.

Ama kuhusu siku za mwezi huo zilizompita kabla hajakuwa Muislamu, sio waajib kwake kulipa siku hizo. Kauli hii ni ya Ash-Sha'biy, Qataadah, Maalik, Al-Awza'iy, Ash-Shaafi'iy, Abu Thawr na Hanafiyyah.

'Atwaa kasema analazimika kulipa siku hizo.

 

Kutoka kwa al-Hassan [Al-Baswriy] kumepokelewa kauli zote mbili.

Ama kuhusu sisi – Hanaabilah – hatuoni kama ni waajib kwake kulipa siku hizo ambazo zilipita hali ya kuwa alikuwa kafiri. Hali kadhalika si waajib kwake kulipa Ramadhwaan iliyopita.

 

 [Al-Mughniy  (4/414-415)]

 

 

Share [9]

06-Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Akijitoa Manii Swawm Inabatilika Na Je, Anawajibika Kafara?

Akijitoa Manii Swawm Inabatilika Na Je, Anawajibika Kafara?

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com [4]

 

 

SWALI:

 

Je, kutoa manii kunabatilisha Swawm? Na je, anapaswa kulipa kafara?

 

 

JIBU:

 

Mtu akitoa manii Swawm yake inabatilika, inabatilika na mtu analazimika kulipa siku hiyo na kufanya tawbah [kwa kuwa ni haramu].

 

Kulipa kafara ni pindi mtu anapofanya jimai wakati wa Swawm.

 

 

[Imaam Muhammad Swaalih Ibn 'Uthaymiyn - Fataawa Arkaanil-Islaam, uk. 478]

 

 

Share [10]

07-Imaam Ibn ‘Uthyamiyn: Akimeza Maji Bila Kukusudia Kutokana Na Kusukutua Swawm Yake Inabatilika?

Akimeza Maji Bila Kukusudia Kutokana Na Kusukutua Swawm Yake Inabatilika?

 

Imaam Ibn ‘Uthyamiyn (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com [4]

 

SWALI:

 

Je, Swawm ya mfungaji inabatilika ikiwa atasukutua kinywa au pua na kwa bahati mbaya akameza maji?

 

JIBU:

 

Aliyekuwa katika swawm akaukutua kinywa au pua na maji yakamuingia, Swawm yake haibatiliki, kwa kuwa hakukusudia hilo. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema:

 

وَلَـٰكِن مَّا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ ۚ

lakini isipokuwa katika yale yaliyoyakusudia nyoyo zenu  [Al-Ahzaab 33;5]

 

[Imaam Muhammad  Swaalih Ibn 'Uthaymiyn -  Fiqhul-'Ibaadat, uk. 253]

 

Share [11]

08-Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Kipulizio Cha Kusaidia Upungufu Wa Pumzi Hakibatilishi Swawm

Kipulizio Cha Kusaidia Upungufu Wa Pumzi Hakibatilishi Swawm

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn  (Rahimahu-Allaah)

www.alhidaaya.com [4]

 

 

 

SWALI:

 

Nini hukmu ya kutumia kipulizio kwa ajili ya kusaidia matatizo ya upungufu wa pumzi?

 

JIBU:

 

Kipulizio ni mvuke na haufikii tumboni. Kwa hiyo tunasema kwamba hakuna ubaya kutumia mtu anapokuwa katika swawm na haitabatilisha swawm yako kwa sababu kama tulivyosema hakuna kitu kitakachoingia tumboni. Kwa vile ni kitu kinachovutwa na kutoka mvuke kisha unapotea, basi hakuna kinachofika tumboni kwa hiyo inarushusiwa kutumia wakati una swawm na swawm haibatiliki kwayo.

 

[Imaam Ibn ‘Uthaymiyn Fataawaa Arkanul-Islaam Darus-salaam Mjalada 2 Uk. 658]

 

 

Share [12]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/8444

Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/261
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8444&title=Fataawaa%3A%20%20Yanayobatilisha%20Na%20Yasiyobatilisha%20Swawm
[4] http://www.alhidaaya.com
[5] https://binbaz.org.sa/noor/9809
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8445&title=01-Imaam%20Ibn%20Baaz%3A%20Dawa%20Ya%20Mswaki%20Inabatilisha%20Swawm%3F
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8447&title=03-Al-Lajnah%20Ad-Daaimah%3A%20Alisukutua%20Maji%20Baridi%20Akiwa%20Katika%20Swawm%20Kutokana%20Na%20Mdomo%20Kuwa%20Mkavu%20Mno%20
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8448&title=04-Imaam%20Ibn%20%E2%80%98Uthaymiyn%3A%20Kujipaka%20Au%20Kunusa%20Mafuta%20Mazuri%20Akiwa%20Katika%20Swawm
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8449&title=05-Imaam%20Ibn%20Qudaamah%20Al-Maddisiyy%3A%20Aliyesilimu%20Katika%20Ramadhwaan%20Anawajibika%20Swiyaam%3F
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8450&title=06-Imaam%20Ibn%20%E2%80%98Uthaymiyn%3A%20Akijitoa%20Manii%20Swawm%20Inabatilika%20Na%20Je%2C%20Anawajibika%20Kafara%3F
[11] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8451&title=07-Imaam%20Ibn%20%E2%80%98Uthyamiyn%3A%20Akimeza%20Maji%20Bila%20Kukusudia%20Kutokana%20Na%20Kusukutua%20Swawm%20Yake%20Inabatilika%3F
[12] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8534&title=08-Imaam%20Ibn%20%E2%80%98Uthaymiyn%3A%20Kipulizio%20Cha%20Kusaidia%20Upungufu%20Wa%20Pumzi%20Hakibatilishi%20Swawm