كِتَابُ الْبُيُوعِ
Kitabu Cha Miamala Ya Biashara
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ شُرُوطِهِ وَمَا نُهِيَ عَنْهُ مِنْهُ
01-Mlango Masharti Yake Na Yaliokatazwa
648.
عَنْ رِفَاعَةَ بْنِ رَافِعٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ سُئِلَ: أَيُّ اَلْكَسْبِ أَطْيَبُ ؟ قَالَ: {عَمَلُ اَلرَّجُلِ بِيَدِهِ، وَكُلُّ بَيْعٍ مَبْرُورٍ} رَوَاهُ اَلْبَزَّارُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa Rifaa’ah bin Raafi’ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliulizwa: Kazi gani bora zaidi?[1] Akasema: “Ni kazi ya mtu kwa mkono wake, na kila biashara halali.” [Imetolewa na Al-Bazzaar na akaisahihisha Al-Haakim]
649.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّهُ سَمِعَ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ عَامَ اَلْفَتْحِ، وَهُوَ بِمَكَّةَ: {إِنَّ اَللَّهَ وَرَسُولَهُ حَرَّمَ بَيْعَ اَلْخَمْرِ، وَالْمَيْتَةِ، وَالْخِنْزِيرِ، وَالْأَصْنَامِ. فَقِيلَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ ! أَرَأَيْتَ شُحُومَ اَلْمَيْتَةِ، فَإِنَّهُ تُطْلَى بِهَا اَلسُّفُنُ، وَتُدْهَنُ بِهَا اَلْجُلُودُ، وَيَسْتَصْبِحُ بِهَا اَلنَّاسُ ؟ فَقَالَ: " لَا هُوَ حَرَامٌ "، ثُمَّ قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عِنْدَ ذَلِكَ: " قَاتَلَ اَللَّهُ اَلْيَهُودَ، إِنَّ اَللَّهَ لَمَّا حَرَّمَ عَلَيْهِمْ شُحُومَهَا جَمَلُوهُ، ثُمَّ بَاعُوهُ، فَأَكَلُوا ثَمَنَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa alimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema mwaka wa Fat-hi (Ukombozi wa Makkah) akiwa Makkah: “Hakika Allaah Ameharamisha kuuza (au kununua) pombe, mfu, nguruwe na masanamu.” Akaulizwa Ee Rasuli wa Allaah! Waonaje shahamu ya mfu, kwani majahazi hupakiwa nayo ngozi, hupakwa kwayo na watu wanajiangazia kwayo (wanatia kwenye taa zao). Akasema: “Laa hiyo ni haramu.” Kisha Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Allaah Awalaani mayahudi. Kwa hakika Allaah Alipowaharamishia shahamu ya mfu, wao waliiyeyusha wakawa wanaiuza; wakala thamani yake.”[2] [Al-Bukhaariy, Muslim]
650.
وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {إِذَا اِخْتَلَفَ اَلْمُتَبَايِعَانِ لَيْسَ بَيْنَهُمَا بَيِّنَةٌ، فَالْقَوْلُ مَا يَقُولُ رَبُّ اَلسِّلْعَةِ أَوْ يَتَتَارَكَانِ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Wawili wenye kuuziana watakapokhitilafiana na hakuna baina yao ubainifu, basi kauli itakayosikilizwa ni ya mwenye bidhaa, au wote wawili waache (biashara hiyo).” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha Al-Haakim]
651.
وَعَنْ أَبِي مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ ثَمَنِ اَلْكَلْبِ، وَمَهْرِ الْبَغِيِّ، وَحُلْوَانِ اَلْكَاهِنِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza thamani ya mbwa,[3] mahari ya kahaba[4] na bahashishi ya kahini[5] (mpiga ramli).” [Al-Bukhaariy, Muslim]
652.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّهُ كَانَ يَسِيرُ عَلَى جَمَلٍ لَهُ أَعْيَا. فَأَرَادَ أَنْ يُسَيِّبَهُ. قَالَ: فَلَحِقَنِي اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَدَعَا لِي، وَضَرَبَهُ، فَسَارَ سَيْراً لَمْ يَسِرْ مِثْلَهُ، قَالَ: " بِعْنِيهِ بِوُقِيَّةٍ " قُلْتُ: لَا. ثُمَّ قَالَ: " بِعْنِيهِ " فَبِعْتُهُ بِوُقِيَّةٍ، وَاشْتَرَطْتُ حُمْلَانَهُ إِلَى أَهْلِي، فَلَمَّا بَلَغْتُ أَتَيْتُهُ بِالْجَمَلِ، فَنَقَدَنِي ثَمَنَهُ، ثُمَّ رَجَعْتُ فَأَرْسَلَ فِي أَثَرِي. فَقَالَ: " أَتُرَانِي مَاكَسْتُكَ لِآخُذَ جَمَلَكَ ؟ خُذْ جَمَلَكَ وَدَرَاهِمَكَ. فَهُوَ لَكْ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ ، وَهَذَا اَلسِّيَاقُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Alikuwa juu ya ngamia wake aliyechoka, akataka amuache aende anapotaka. Akasema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaniombea na akampiga (yule ngamia), akaenda mwendo ambao hajawahi kuenda mfano wake. Kisha akasema: Niuzie kwa wakia moja.[6] Nikamuambia: Hapana. Halafu akaniambia: Niuzie. Nikamuuzia kwa wakia moja. Nikashurutisha kunibeba kwake hadi kwa watu wangu (Madiynah). Nilipofika nilimpelekea ngamia. Akalipa thamani yake. Kisha nikarejea. Akatuma mtu nyuma yangu akasema: Wadhani kuwa nimekutaradhilia unipunguzie thamani ili nichukue ngamia wako?[7] Chukua ngamia wako na dirham zako ni milki yako.” [Al-Bukhaariy, Muslim na haya ni maneno ya Muslim]
653.
وَعَنْهُ قَالَ: {أَعْتَقَ رَجُلٌ مِنَّا عَبْداً لَهُ عَنْ دُبُرٍ لَمْ يَكُنْ لَهُ مَالٌ غَيْرُهُ. فَدَعَا بِهِ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَبَاعَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema tena: “Mtu miongoni mwenu alitangaza kumuacha huru mtumwa wake baada ya kifo chake, alikuwa hana mali isipokuwa mtumwa huyo. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuita na akamuuza[8] (na thamani yake akampa mwenyewe).” [Al-Bukhaariy, Muslim]
654.
وَعَنْ مَيْمُونَةَ زَوْجِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، وَرَضِيَ عَنْهَا {أَنَّ فَأْرَةً وَقَعَتْ فِي سَمْنٍ، فَمَاتَتْ فِيهِ، فَسُئِلَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْهَا. فَقَالَ: " أَلْقُوهَا وَمَا حَوْلَهَا، وَكُلُوهُ "} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
وَزَادَ أَحْمَدُ. وَالنَّسَائِيُّ: {فِي سَمْنٍ جَامِدٍ}
Kutoka kwa Maymuwnah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) mke wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Panya aliingia katika samli akafa humo. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaulizwa kuhusu panya yule, akasema: Mtupeni na kilicho kando yake na mle (samli hiyo).” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
Ahmad na An-Nasaaiy wameongeza: “katika samli iliyoganda”
655.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِذَا وَقَعَتْ اَلْفَأْرَةُ فِي اَلسَّمْنِ، فَإِنْ كَانَ جَامِداً فَأَلْقُوهَا وَمَا حَوْلَهَا، وَإِنْ كَانَ مَايِعًا فَلَا تَقْرَبُوهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَقَدْ حَكَمَ عَلَيْهِ اَلْبُخَارِيُّ وَأَبُو حَاتِمٍ بِالْوَهْمِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Panya atakapoingia katika samli, ikiwa imeganda basi mtupeni na kilichomo kando yake, na ikiwa ni maji maji msiikaribie.” [Imetolewa na Ahmad, na Abuu Daawuwd, Al-Bukhaariy na Abuu Haatim wamesema ina shaka]
656.
وَعَنْ أَبِي اَلزُّبَيْرِ قَالَ: سَأَلْتُ جَابِرًا عَنْ ثَمَنِ اَلسِّنَّوْرِ وَالْكَلْبِ ؟ فَقَالَ: {زَجَرَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ ذَلِكَ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ .
وَالنَّسَائِيُّ وَزَادَ: {إِلَّا كَلْبَ صَيْدٍ}
Kutoka kwa Abuu Az-Zubayr[9] amesema kuwa Nilimuuliza Jaabir kuhusu thamani ya paka na mbwa,[10] akasema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikataza jambo hilo.” [Imetolewa na Muslim]
Na An-Nasaaiy akazidisha: “Isipokuwa mbwa wa kuwinda.”
657.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {جَاءَتْنِي بَرِيرَةُ، فَقَالَتْ: كَاتَبْتُ أَهْلِي عَلَى تِسْعٍ أُوَاقٍ، فِي كُلِّ عَامٍ أُوقِيَّةٌ، فَأَعِينِينِي. فَقُلْتُ: إِنْ أَحَبَّ أَهْلُكِ أَنْ أَعُدَّهَا لَهُمْ وَيَكُونَ وَلَاؤُكِ لِي فَعَلْتُ، فَذَهَبَتْ بَرِيرَةُ إِلَى أَهْلِهَا. فَقَالَتْ لَهُمْ، فَأَبَوْا عَلَيْهَا، فَجَاءَتْ مِنْ عِنْدِهِمْ، وَرَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ جَالِسٌ. فَقَالَتْ: إِنِّي قَدْ عَرَضْتُ ذَلِكَ عَلَيْهِمْ فَأَبَوْا إِلَّا أَنْ يَكُونَ اَلْوَلَاءُ لَهُمْ، فَسَمِعَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَأَخْبَرَتْ عَائِشَةُ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ . فَقَالَ: خُذِيهَا وَاشْتَرِطِي لَهُمُ اَلْوَلَاءَ، فَإِنَّمَا اَلْوَلَاءُ لِمَنْ أَعْتَقَ فَفَعَلَتْ عَائِشَةُ، ثُمَّ قَامَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي اَلنَّاسِ خَطِيباً، فَحَمِدَ اَللَّهَ وَأَثْنَى عَلَيْهِ. ثُمَّ قَالَ: " أَمَّا بَعْدُ، مَا بَالُ رِجَالٍ يَشْتَرِطُونَ شُرُوطاً لَيْسَتْ فِي كِتَابِ اَللَّهِ مَا كَانَ مِنْ شَرْطٍ لَيْسَ فِي كِتَابِ اَللَّهِ فَهُوَ بَاطِلٌ، وَإِنْ كَانَ مِائَةَ شَرْطٍ، قَضَاءُ اَللَّهِ أَحَقُّ، وَشَرْطُ اَللَّهِ أَوْثَقُ، وَإِنَّمَا اَلْوَلَاءُ لِمَنْ أَعْتَقَ "} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ .
وَعِنْدَ مُسْلِمٍ فَقَالَ:{اِشْتَرِيهَا وَأَعْتِقِيهَا وَاشْتَرِطِي لَهُمُ اَلْوَلَاءَ}
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Bariyrah[11] (mjakazi) alinijia akasema: Nimeandikiana[12] (kuniacha huru) na mabwana zangu kwa wakia tisa; kila mwaka wakia moja; basi nisaidie. Nikamuambia: Mabwana zako wakipenda niwahesabie (hizo) na walaa[13] wako uwe kwangu nitafanya. Bariyrah akawaendea mabwana wake akawaeleza, wakamkatalia. Akaja kutoka kwako na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ameketi. Akasema: nimewaambia jambo hilo wakakataa[14] isipokuwa walaa uwe kwao. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasikia. ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) akasema nikamueleza Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Akamuambia ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا): Mchukue na uwashurutishe walaa, kwani walaa ni wa mwenye kuacha huru.[15] ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) akafanya hivyo kisha Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasimama katika watu Akamhimidi Allaah na Akamsifu kisha akasema: Ammaa ba’d: wana nini watu wanashurutisha masharti yasiyokuwemo katika Kitabu cha Allaah! Sharti isiyokuwemo katika Kitabu cha Allaah ni batili, hata kama ni masharti mia. Hukumu ya Allaah ina nguvu na mno, na walaa ni wa mwenye kuacha huru.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
Na katika Riwaayah ya Muslim amesema: “Mnunue umuache huru na uwashururutishie walaa.”
658.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى عُمَرُ عَنْ بَيْعِ أُمَّهَاتِ اَلْأَوْلَادِ فَقَالَ: لَا تُبَاعُ، وَلَا تُوهَبُ، وَلَا تُورَثُ، لِيَسْتَمْتِعْ بِهَا مَا بَدَا لَهُ، فَإِذَا مَاتَ فَهِيَ حُرَّةٌ} رَوَاهُ مَالِكٌ، وَالْبَيْهَقِيُّ، وَقَالَ: رَفَعَهُ بَعْضُ اَلرُّوَاةِ، فَوَهِمَ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “’Umar amekataza kuuza mama wa watoto,[16] akasema: hawauzwi wala hawatolewi hiba, wala hawarithiwi, atastarehe naye anavyotaka, atakapokufa (bwana) mwanamke huyo ni huru.” [Imetolewa na Maalik na Al-Bayhaqiyy]
659.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {كُنَّا نَبِيعُ سَرَارِيَنَا، أُمَّهَاتِ اَلْأَوْلَادِ، وَالنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ حَيٌّ، لَا نَرَى بِذَلِكَ بَأْسًا} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Tulikuwa tukiuza vijakazi wetu mama wa watoto, na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) yuko hai, haoni ubaya kwa hilo.” [Imetolewa na An-Nasaaiy, Ibn Maajah na Ad-Daaraqutwniy, na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
660.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ قَالَ: {نَهَى اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ بَيْعِ فَضْلِ اَلْمَاءِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
وَزَادَ فِي رِوَايَةٍ: {وَعَنْ بَيْعِ ضِرَابِ اَلْجَمَلِ}
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza ziada ya maji.”[17] [Imetolewa na Muslim]
Na katika Riwaayah nyingine akaongeza: “Na kuuza mapigo ya ngamia.”[18]
661.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ عَسْبِ اَلْفَحْلِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza mapigo ya ngamia.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
662.
وَعَنْهُ، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ بَيْعِ حَبَلِ اَلْحَبَلَةِ، وَكَانَ بَيْعاً يَتَبَايَعُهُ أَهْلُ الْجَاهِلِيَّةِ: كَانَ اَلرَّجُلُ يَبْتَاعُ اَلْجَزُورَ إِلَى أَنْ تُنْتَجَ اَلنَّاقَةُ، ثُمَّ تُنْتَجُ اَلَّتِي فِي بَطْنِهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema tena kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza mimba ya wenye mimba (Habalil-habalah),[19] na (hiyo) ilikuwa ni biashara wanayouziana watu wa jahiliya. Mtu alikuwa ananunua ngamia mpaka azaliwe ngamia koo kisha kizaliwe kilichomo tumboni mwake.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
663.
وَعَنْهُ، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ بَيْعِ اَلْوَلَاءِ، وَعَنْ هِبَتِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema tena kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza walaa[20] na kuutoa hiba.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
664.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ بَيْعِ اَلْحَصَاةِ، وَعَنْ بَيْعِ اَلْغَرَرِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza biashara ya kurusha kijiwe na biashara ya udanganyifu.”[21] [Imetolewa na Muslim]
665.
وَعَنْهُ: أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنِ اِشْتَرَى طَعَاماً فَلَا يَبِعْهُ حَتَّى يَكْتَالَهُ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema tena kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kununua chakula, asikiuze mpaka akipime.” [Imetolewa na Muslim]
666.
وَعَنْهُ قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ بَيْعَتَيْنِ فِي بَيْعَةٍ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ
وَلِأَبِي دَاوُدَ: {مَنْ بَاعَ بَيْعَتَيْنِ فِي بَيْعَةٍ فَلَهُ أَوَكَسُهُمَا، أَوْ اَلرِّبَا}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema tena: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza mauzo mawili katika uzo moja.”[22] [Imetolewa na Ahmad na An-Nasaaiy na akaisahihisha At-Tirmidhiy na Ibn Hibbaan]
Na katika Riwaayah ya Abuu Daawuwd inasema: “Yeyote mwenye kuuza mauzo mawili katika uzo moja, basi ima atapata kilicho kichache kati ya viwili au riba.”[23]
667.
وَعَنْ عَمْرِوِ بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَحِلُّ سَلَفٌ وَبَيْعٌ وَلَا شَرْطَانِ فِي بَيْعٍ، وَلَا رِبْحُ مَا لَمْ يُضْمَنْ، وَلَا بَيْعُ مَا لَيْسَ عِنْدَكَ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ، وَالْحَاكِمُ
وَأَخْرَجَهُ فِي " عُلُومِ اَلْحَدِيثِ " مِنْ رِوَايَةِ أَبِي حَنِيفَةَ، عَنْ عَمْرٍو اَلْمَذْكُورِ بِلَفْظِ: " نَهَى عَنْ بَيْعٍ وَشَرْطٍ " وَمِنْ هَذَا اَلْوَجْهِ أَخْرَجَهُ اَلطَّبَرَانِيُّ فِي " اَلْأَوْسَطِ " وَهُوَ غَرِيبٌ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb amepokea kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halali kujumuisha mkopo na mauzo,[24] wala masharti mawili katika uzo moja,[25] wala faida katika mali asiyodhamini, wala kuuza kitu usichokimiliki.”[26] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha At-Tirmidhiy, Ibn Khuzaymah na Al-Haakim]
Al-Haakim ameitaja katika ‘’Uluwmul-Hadiyth’ kutoka kwa Abuu Haniyfah naye kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kwa tamko: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza biashara (iliyochanganywa) iliyokokotezwa kwa sharti.” Atw-Twabaraaniyy ameitaja katika mnyororo wa wapokezi hawa katika Al-Awsatw, na ni Hadiyth ghariyb (iliyotajwa na mpokezi mmoja tu).
668.
وَعَنْهُ قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ بَيْعِ اَلْعُرْبَانِ} رَوَاهُ مَالِكٌ، قَالَ: بَلَغَنِي عَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، بِهِ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kutoka kwa baba yake na babu yake amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza biashara ya ‘Urbaan.”[27] [Imetolewa na Maalik ambaye amesema: Imenifikia (akitaja mnyororo wa wapokezi wake) kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb]
669.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {اِبْتَعْتُ زَيْتاً فِي اَلسُّوقِ، فَلَمَّا اِسْتَوْجَبْتُهُ لَقِيَنِي رَجُلٌ فَأَعْطَانِي بِهِ رِبْحاً حَسَناً، فَأَرَدْتُ أَنْ أَضْرِبَ عَلَى يَدِ اَلرَّجُلِ، فَأَخَذَ رَجُلٌ مِنْ خَلْفِي بِذِرَاعِي، فَالْتَفَتُّ، فَإِذَا هُوَ زَيْدُ بْنُ ثَابِتٍ، فَقَالَ: لَا تَبِعْهُ حَيْثُ اِبْتَعْتَهُ حَتَّى تَحُوزَهُ إِلَى رَحْلِكَ; فَإِنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى أَنْ تُبَاعَ اَلسِّلَعُ حَيْثُ تُبْتَاعُ، حَتَّى يَحُوزَهَا اَلتُّجَّارُ إِلَى رِحَالِهِمْ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Nilinunua mafuta sokoni, nilipokabidhiwa alikuja mtu (hapo hapo) akanipa faida nzuri, nami nikataka kumuuzia, mara mtu mmoja akanishika kwa nyuma yangu, nilipogeuka alikuwa Zayd bin Thaabit, akasema: Usiuze mahala uliponunua hadi uchukue mahali pako, kwani hakika Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amakataza bidhaa kuuzwa mahali inaponunuliwa mpaka wafanya biashara wazipeleke maeneo yao (wazikabidhi).”[28] [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd, matni ya Hadiyth ni yake. Na wakaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
670.
وَعَنْهُ قَالَ: {قُلْتُ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنِّي أَبِيعُ بِالْبَقِيعِ، فَأَبِيعُ بِالدَّنَانِيرِ وَآخُذُ اَلدَّرَاهِمَ، وَأَبِيعُ بِالدَّرَاهِمِ وَآخُذُ اَلدَّنَانِيرَ، آخُذُ هَذَا مِنْ هَذِهِ وَأُعْطِي هَذَهِ مِنْ هَذِا ؟ فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: لَا بَأْسَ أَنْ تَأْخُذَهَا بِسِعْرِ يَوْمِهَا مَا لَمْ تَتَفَرَّقَا وَبَيْنَكُمَا شَيْءٌ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Nilisema: Ee Rasuli wa Allaah! Mimi ninauza ngamia Baqiy’ nikiuza kwa dinari na nikichukua dirham, na nikiuza kwa dirham na nikichukua dinari, nachukua dirhamu badala ya dinari. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Si vibaya kuchukua kwa bei ya siku ile[29] madamu hamujaachana na baina yenu kitu kipo.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha Al-Haakim]
671.
وَعَنْهُ قَالَ: {نَهَى صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنِ النَّجْشِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kupandishana bei katika biashara.”[30] [Al-Bukhaariy, Muslim]
672.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ اَلْمُحَاقَلَةِ، وَالْمُزَابَنَةِ، وَالْمُخَابَرَةِ، وَعَنْ اَلثُّنْيَا، إِلَّا أَنْ تُعْلَمَ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ إِلَّا اِبْنَ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza Muhaaqalah,[31] Muzaabanah,[32] Mukhaabarah[33] na Ath-Thun-yaa ila itakapojulikana.”[34] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ahmad) isipokuwa Ibn Maajah, na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
673.
وَعَنْ أَنَسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنِ اَلْمُحَاقَلَةِ، وَالْمُخَاضَرَةِ، وَالْمُلَامَسَةِ، وَالْمُنَابَذَةِ، وَالْمُزَابَنَةِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza Muhaaqalah, Mukhaadhwarah,[35] Mulaamasah,[36] Munaabadhah[37] na Muzaabanah.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
674.
وَعَنْ طَاوُسٍ، عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا تَلَقَّوْا اَلرُّكْبَانَ، وَلَا يَبِيعُ حَاضِرٌ لِبَادٍ ". قُلْتُ لِابْنِ عَبَّاسٍ: مَا قَوْلُهُ: " وَلَا يَبِيعُ حَاضِرٌ لِبَادٍ ؟ " قَالَ: لَا يَكُونُ لَهُ سِمْسَارًا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Twaawus[38] kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msiwapokee wasafiri, wala mkazi wa mjini asiuze kwa niaba ya mtu wa mashambani.[39] Nikamuambia ‘Abdullaah bin ‘Abbaas: Nini makusudio ya kauli yake “Wala mkazi wa mjini asiuze kwa niaba ya mtu wa mashambani?” Akasema: Asiwe dalali wake.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
675.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا تَلَقَّوا اَلْجَلَبَ، فَمَنْ تُلُقِّيَ فَاشْتُرِيَ مِنْهُ، فَإِذَا أَتَى سَيِّدُهُ اَلسُّوقَ فَهُوَ بِالْخِيَارِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msiwapokee wasafiri, atakayepokezwa bidhaa ikanunuliwa kwake, basi atakapokuja mwenyewe sokoni ana khiyari (ya kutoivunja biashara).” [Imetolewa na Muslim]
676.
وَعَنْهُ قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنْ يَبِيعَ حَاضِرٌ لِبَادٍ، وَلَا تَنَاجَشُوا، وَلَا يَبِيعُ اَلرَّجُلُ عَلَى بَيْعِ أَخِيهِ، وَلَا يَخْطُبُ عَلَى خِطْبَةِ أَخِيهِ، وَلَا تُسْأَلُ اَلْمَرْأَةُ طَلَاقَ أُخْتِهَا لِتَكْفَأَ مَا فِي إِنَائِهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ: {لَا يَسُمِ اَلْمُسْلِمُ عَلَى سَوْمِ اَلْمُسْلِمِ}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza mkazi wa mjini kumuuzia kwa niaba mtu wa kijijini, wala msipandishiane bei,[40] wala mtu asiuze juu ya biashara ya nduguye, wala asipose juu ya posa ya nduguye (Muislam), wala mwanamke asiombe dada yake kupewa talaka ili afaidike kwa kuachwa kwake.”[41] [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Muslim: “Wala Muislam asinunue juu ya biashara ya Muislam (mwenzake).”[42]
677.
وَعَنْ أَبِي أَيُّوبَ اَلْأَنْصَارِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {مَنْ فَرَّقَ بَيْنَ وَالِدَةٍ وَوَلَدِهَا، فَرَّقَ اَللَّهُ بَيْنَهُ وَبَيْنَ أَحِبَّتِهِ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَالْحَاكِمُ، وَلَكِنْ فِي إِسْنَادِهِ مَقَالٌ وَلَهُ شَاهِدٌ
Kutoka kwa Abuu Ayyuwb Al-Answaariy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Mwenye kufarikisha baina ya mama na mtoto wake, Allaah Atafarikisha baina yake na vipenzi vyake Siku ya Qiyaamah.” [Imetolewa na Ahmad na akaisahihisha At-Tirmidhiy na Al-Haakim
678.
وَعَنْ عَلِيِّ بْنِ أَبِي طَالِبٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {أَمَرَنِي رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنْ أَبِيعَ غُلَامَيْنِ أَخَوَيْنِ، فَبِعْتُهُمَا، فَفَرَّقْتُ بَيْنَهُمَا، فَذَكَرْتُ ذَلِكَ لِلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: أَدْرِكْهُمَا، فَارْتَجِعْهُمَا، وَلَا تَبِعْهُمَا إِلَّا جَمِيعًا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ، وَقَدْ صَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ، وَالطَّبَرَانِيُّ، وَابْنُ اَلْقَطَّانِ
Kutoka kwa ‘Aliy bin Abiy Twaalib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliniamrisha kuwauza vijana wawili ndugu nikawauza kwa kuwatenga. Kisha nikamuelezea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) jambo hilo. Akaniambia: watafute uwarudishe,[43] wala usiwauze isipokuwa pamoja.” [Imetolewa na Ahmad. Wapokezi wake ni madhubuti. Na wakaisahihisha Ibn Khuzaymah, Ibn Al-Jaaruwd, Ibn Hibbaan, Al-Haakim, Atw-Twabaraani na Ibn Al-Qatwaan]
679.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {غَلَا اَلسِّعْرُ بِالْمَدِينَةِ عَلَى عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ اَلنَّاسُ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ ! غَلَا اَلسِّعْرُ، فَسَعِّرْ لَنَا، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ إِنَّ اَللَّهَ هُوَ اَلْمُسَعِّرُ، اَلْقَابِضُ، اَلْبَاسِطُ، الرَّازِقُ، وَإِنِّي لَأَرْجُو أَنْ أَلْقَى اَللَّهَ تَعَالَى، وَلَيْسَ أَحَدٌ مِنْكُمْ يَطْلُبُنِي بِمَظْلِمَةٍ فِي دَمٍ وَلَا مَالٍ "} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ إِلَّا النَّسَائِيَّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Bei zilipanda Madiynah katika zama za Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) watu wakamuambia: Ee Rasuli wa Allaah! Bei zimepanda, tupange bei. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Kwa hakika Allaah Ndiye Mwenye kuwafikia (Mpanga bei), Mwenye kudhikisha, Mwenye Kukunjua, Mwenye Kuruzuku,[44] mimi nataraji kukutana na Allaah na hali hakuna miongoni mwenu mwenye kunidai kwa kudhulumiwa damu wala mali.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) isipokuwa An-Nasaaiy, na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
680.
وَعَنْ مَعْمَرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَحْتَكِرُ إِلَّا خَاطِئٌ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Ma’mar bin ‘Abdillaah[45] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amepokea kutoka kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuwa amesema: “Halimbikizi ila mkosaji.”[46] [Imetolewa na Muslim]
681.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا تَصُرُّوا اَلْإِبِلَ وَالْغَنَمَ، فَمَنِ اِبْتَاعَهَا بَعْدُ فَإِنَّهُ بِخَيْرِ اَلنَّظَرَيْنِ بَعْدَ أَنْ يَحْلُبَهَا، إِنْ شَاءَ أَمْسَكَهَا، وَإِنْ شَاءَ رَدَّهَا وَصَاعًا مِنْ تَمْرٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ: {فَهُوَ بِالْخِيَارِ ثَلَاثَةَ أَيَّامٍ}
وَفِي رِوَايَةٍ: لَهُ، عَلَّقَهَا اَلْبُخَارِيُّ: {رَدَّ مَعَهَا صَاعاً مِنْ طَعَامٍ، لَا سَمْرَاءَ}
قَالَ اَلْبُخَارِيُّ: وَالتَّمْرُ أَكْثَرُ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msivimbishe chuchu za ngamia na mbuzi (kuonesha yamejaa), na mwenye kumnunua baada ya hapo basi ana khiyari kuchagua moja kati ya mambo mawili, baada ya kumkama; akitaka atabaki nae na akitaka atamrudisha pamoja na pishi ya tende.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Muslim: “...naye yuko katika khiari kwa muda wa siku tatu.[47] (Ambapo ataamua kuyaweka au hapana).”[48]
Na katika Riwaayah yake nyingine ambayo Bukhaariy ameifanya ni Mu’allaq imesema: “…na atarudisha pamoja na pishi ya chakula isiyokuwa kawahia.”
Bukhaariy amesema katika Riwaayah: “Iliyotaja tende ndio iliyopokewa na wapokezi wengi.”
682.
وَعَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ:{مَنِ اِشْتَرَى شَاةً مَحَفَّلَةً، فَرَدَّهَا، فَلْيَرُدَّ مَعَهَا صَاعًا} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ .
وَزَادَ اَلْإِسْمَاعِيلِيُّ:{مِنْ تَمْرٍ}
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Mwenye kununua mnyama aliyevimbishwa chuchu na akamrudisha, basi atakapomrudisha amrudishe pamoja na pishi.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
Na Al-Ismaa’iliyy ameongezea: “…ya tende.”
683.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ مَرَّ عَلَى صُبْرَةِ طَعَامٍ، فَأَدْخَلَ يَدَهُ فِيهَا، فَنَالَتْ أَصَابِعُهُ بَلَلًا ، فَقَالَ: " مَا هَذَا يَا صَاحِبَ اَلطَّعَامِ ؟ " قَالَ: أَصَابَتْهُ اَلسَّمَاءُ يَا رَسُولَ اَللَّهِ. فَقَالَ: أَفَلَا جَعَلْتَهُ فَوْقَ اَلطَّعَامِ; كَيْ يَرَاهُ اَلنَّاسُ ؟ مَنْ غَشَّ فَلَيْسَ مِنِّي} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipita katika lundo la chakula (nafaka), akaingiza mkono wake ndani, vidole vyake vikagusa unyevu. Akasema: Ee mwenye chakula, ni nini hii? Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Kimepatwa na manyunyu, akamuambia: Si ungekiweka juu ya chakula ili watu wakione! Mwenye kughushi si katika mimi.”[49] [Imetolewa na Muslim]
684.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ بُرَيْدَةَ، عَنْ أَبِيهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ حَبَسَ اَلْعِنَبَ أَيَّامَ اَلْقِطَافِ، حَتَّى يَبِيعَهُ مِمَّنْ يَتَّخِذُهُ خَمْراً، فَقَدَ تَقَحَّمَ اَلنَّارَ عَلَى بَصِيرَةٍ} رَوَاهُ اَلطَّبَرَانِيُّ فِي " اَلْأَوْسَطِ " بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Buraydah amepokea kutoka kwa baba yake kuwa amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuhifadhi zabibu msimu wa kuchuma (zabibu) ili amuuzie mtengeneza pombe, kwa hakika atakuwa amejiingiza motoni kwa ujuzi.”[50] [Imetolewa na Atw-Twabaraaniyy katika kitabu chake cha ‘Al-Awsatw’ kwa Isnaad Hasan]
685.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلْخَرَاجُ بِالضَّمَانِ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَضَعَّفَهُ اَلْبُخَارِيُّ، وَأَبُو دَاوُدَ وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ، وَابْنُ اَلْقَطَّانِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kodi ni kwa dhamana.”[51] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na wameidhoofisha Al-Bukhaariy na Abuu Daawuwd, na wakaisahihisha At-Tirmidhiy, Ibn Khuzaymah, Ibn Al-Jaaruwd, Ibn Hibbaan, Al-Haakim na Ibn Al-Qatwaan]
686.
وَعَنْ عُرْوَةَ الْبَارِقِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَعْطَاهُ دِينَارًا يَشْتَرِي بِهِ أُضْحِيَّةً، أَوْ شَاةً، فَاشْتَرَى شَاتَيْنِ، فَبَاعَ إِحْدَاهُمَا بِدِينَارٍ، فَأَتَاهُ بِشَاةٍ وَدِينَارٍ، فَدَعَا لَهُ بِالْبَرَكَةِ فِي بَيْعِهِ، فَكَانَ لَوْ اِشْتَرَى تُرَابًا لَرَبِحَ فِيهِ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ إِلَّا النَّسَائِيَّ
وَقَدْ أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ ضِمْنَ حَدِيثٍ، وَلَمْ يَسُقْ لَفْظَهُ
وَأَوْرَدَ اَلتِّرْمِذِيُّ لَهُ شَاهِداً: مِنْ حَدِيثِ حَكِيمِ بْنِ حِزَامٍ
Kutoka kwa ‘Urwah Al-Baariqiyy[52] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimpa dinari (moja) ili anunulie Udhwhiyyah[53] au mbuzi. Akanunua mbuzi wawili kwa dinari hiyo, mbuzi mmoja akamuuza kwa dinari moja, akaenda kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akiwa na mbuzi na dinari. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akambariki katika biashara yake (‘Urwah)[54] akawa lau angenunua mchanga basi angepata faida.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) isipokuwa An-Nasaaiy]
Bukhaariy ameileza katika jumla ya Hadiyth nyingine wala hakuitaja tamshi lake.
At-Tirmidhiy ametaja ushahidi wake kutoka katika Hadiyth ya Hakiym bin Hizaam.
687.
وَعَنِ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ شِرَاءِ مَا فِي بُطُونِ اَلْأَنْعَامِ حَتَّى تَضَعَ، وَعَنْ بَيْعِ مَا فِي ضُرُوعِهَا، وَعَنْ شِرَاءِ اَلْعَبْدِ وَهُوَ آبِقٌ، وَعَنْ شِرَاءِ اَلْمَغَانِمِ حَتَّى تُقْسَمَ، وَعَنْ شِرَاءِ اَلصَّدَقَاتِ حَتَّى تُقْبَضَ، وَعَنْ ضَرْبَةِ اَلْغَائِصِ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ، وَالْبَزَّارُ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kununua vilivyomo matumboni mwa wanyama mpaka wazae, na amekataza kuuza vilivyomo katika chuchu za wanyama,[55] na kununua mtumwa aliyetoroka, na kununua ghanima mpaka zigawanywe, na kununua Swadaqah mpaka zikadhibiwe, na amekataza kubahatisha mpiga mbizi.”[56] [Imetolewa na Ibn Maajah, Al-Bazzaar na Ad-Daaraqutwniyy kwa Isnaad dhaifu]
688.
وَعَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا تَشْتَرُوا اَلسَّمَكَ فِي اَلْمَاءِ; فَإِنَّهُ غَرَرٌ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَشَارَ إِلَى أَنَّ اَلصَّوَابَ وَقْفُهُ
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msinunue samaki akiwemo majini, kwani ni udanganyifu.” [Imetolewa na Ahmad na ameashiria kuwa Hadiyth hii ni Mawquwf (yaani ni maneno ya Swahaba, yaani Ibn Mas-‘uwd)]
689.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنْ تُبَاعَ ثَمَرَةٌ حَتَّى تُطْعَمَ، وَلَا يُبَاعَ صُوفٌ عَلَى ظَهْرٍ، وَلَا لَبَنٌ فِي ضَرْعٍ} رَوَاهُ اَلطَّبَرَانِيُّ فِي " اَلْأَوْسَطِ " وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ
وَأَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ فِي " اَلْمَرَاسِيلِ " لِعِكْرِمَةَ، وَهُوَ اَلرَّاجِحُ.
وَأَخْرَجَهُ أَيْضاً مَوْقُوفاً عَلَى اِبْنِ عَبَّاسٍ بِإِسْنَادٍ قَوِيٍّ، وَرَجَّحَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza matunda mpaka yaive, wala manyoya kuuzwa juu ya mgongo, wala maziwa katika chuchu.”[57] [Imetolewa na Atw-Twabaraaniyy katika kitabu chake Al-Awsatw na Ad-Daaraqutwniy]
Na Abuu Daawuwd katika Al-Maraasiyl kutoka kwa Ikrimah nayo ni yenye nguvu.
Vile vile amepokea ikiwa Mawquwf Ibn ‘Abbaas ikiwa na sanadi yenye nguvu na akaipa nguvu Al-Bayhaqiyy.
690.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ بَيْعِ اَلْمَضَامِينِ، وَالْمَلَاقِيحِ} رَوَاهُ اَلْبَزَّارُ، وَفِي إِسْنَادِهِ ضَعْفٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza mimba katika matumbo ya ngamia,[58] na manii katika migongo ya ngamia.”[59] [Imetolewa na Al-Bazzaar na katika Isnaad yake kuna udhaifu]
691.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ أَقَالَ مُسْلِماً بَيْعَتَهُ، أَقَالَهُ اَللَّهُ عَثْرَتَهُ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kukubali kurudishiwa kile alichomuuzia Muislamu,[60] Allaah atamsamehe dhambi zake.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Ibn Maajah, na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
[1] Ni kazi gani au chumo gani lililo bora zaidi? Wanazuoni wametofautiana katika hili. Imaam An-Nawawiy amesema: Sawa ni kuwa chumo bora na inayokuwa kwa kazi ya mkono, japokuwa kilimo ni chumo bora kwa kukusanya kazi ya mkono na kutawakali na ndani yake kuna manufaa ya jumla ya wana Aadam, wanyama na ndege. Haafidh bin Hajar amesema: Zaidi ya hivyo ni yanayo chumwa kutokana na mali za makafiri kwenye jihadi, na hilo chumo la Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na hilo ni chumo tukufu zaidi la machumo yote, kwa kuwa ndani yake kuna kuinua neno la Allaah.” Imesemwa Hii inaingia katika chumo la mkono.
[2] Ina maana ya kufanya biashara katika pombe, wanyama wafu, najisi ya maiti na nguruwe, sanamu ni haramu. Hadiyth hii imeweka wazi kuwa faida inayotokana na kitu kilicho haramu ni haramu vile vile, kubadilika kwa namna yake hakuihalalishi kama vile Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alivyohukumu kuhusu faida inayotokana na mafuta.
[3] Kulingana na maoni ya Wanazuoni takriban wote ni kuwa biashara ya mbwa ni haramu.
[4] Mapato yanayotokana na kahaba ni haramu kulingana na maoni ya Wanazuoni wote.
[5] Hul-waan al-kaahin: Wanazuoni wamekubaliana uharamu wa kumpa kahini, na kahini ni ambaye anadai elimu ya ghaibu na kuwaeleza watu yatakayotokea ni haramu. Hali kadhaalika kuimba na kucheza kwa malipo ya kikahini ni haramu.
[6] Wakia mmoja ni sawa na Dirhaam arubaini.
[7] Yaani labda unadhani kuwa nimenunua ngamia wako kwa thamani ndogo.
[8] Hii ina maana ya kumuuza mtumwa Mudabbar ni jambo lililoruhusiwa. Mtumwa Mudabbar, mwanamme au mwanamke ni yule anayeambiwa na anayemmiliki: “Utakuwa huru baada ya kufa kwangu.”
[9] Jina lake ni Muhammad bin Muslim Tadrus Al-Asadi Al-Makki, muach ahuru wa Hakiym bin Hizaam. Alikuwa ni Taabi’ thiqah aliyekubaliwa na Wanazuoni wa Hadiyth.
[10] Kuuza na kununua paka ni jambo lisiloruhusiwa kishariy’ah. Hivyo hivyo hakuna tofauti kati ya mbwa wa kawaida kuhusu biashara yake kuwa haramu. Hata hivyo mtazamo unakuwa tofauti kuhusu mbwa wa kuwinda, ambapo baadhi ya Wanazuoni wanajuzisha.
[11] Ni mjakazi aliyeachwa huru na ‘Aaishah. Ni Swahaba aliishi hadi katika utawala wa Yaziyd. Aliolewa na Mughiyth, mtumwa katika familia ya Abuu Ahmad bin Jahsh. Alipoachwa huru Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimpa uchaguzi na akachagua kumuacha mume wake ambae alikuwa mtumwa bado na hivyo akawa ameachika.
[12] Kitaabah au Mukaatabah una maana ya mkataba ulioandikwa wa kumuacha huru mtumwa wa kike au wa kiume kwa mkabala wa malipo. Malipo haya yanaweza kupendekezwa kufanyika katika moja ya pande mbili. Kwa mfano mwenye kumiliki mtumwa akadai malipo mkabala na kumuacha huru mtumwa wake na mtumwa akaaridhi malipo mkabala na uhuru wake.
[13] Walaa: mtumwa aliyeachwa huru. Anapokufa, atarithiwa na yule aliyemuacha huru.
[14] Baada ya kifo cha mtumwa Mukattab (mwanamme au mwanamke) mali aliyoacha huitwa Walaa. Ikitokea mtu akalipa hela ya mkataba na kumuacha huru Mukattab (mtumwa mwanamme au mwanamke) katika hali ya kifo cha mtumwa, yule atakayelipa fedha basi atarithi; lakini ikiwa hela ya mkataba ililipwa na mtumwa mwenyewe mali yake inakwenda kwa jamaa zake.
[15] Ina maana kumuacha huru Mukattab (mtumwa aliyeandika mkataba) kwa gharama fulani inaruhusiwa.
[16] Makusudio ya Ummul-Walad (Mama mtoto) ni mjakazi anaeingiliwa na bwana wake kwa ujakazi na akapata mtoto kwa bwana wake huyo. Mtoto huyo awe ni mume au mke. Ummul-walad (Mama mtoto) atakuwa huru baada ya kufariki bwana wake, wala hastahiki kuuzwa wala kutolewa zawadi wala kurithiwa.
[17] Kuzuia au kuuza maji ya ziada ambayo mtu hana matumizi yake ni jambo lisilokubaliwa kishariy’ah; vyovyote itakavyokuwa asili ya maji yale ni kisima au chemchem, katika ardhi anayoimiliki au katika ardhi ya mtu mwingine. Hata hivyo, maji yaliyohifadhiwa kwa matumizi binafsi yanaweza kuuzwa ni jambo linaloruhusiwa.
[18] Mapigo ya ngamia ni kumchukua ngamia dume na kumkodisha kwa mtu mwenye ngamia jike ili ampande.
[19] Kulikuwa na aina mbili za biashara hii. Aina ya mfano wa kwanza ni kununua kizazi cha mnyama ambaye bado hajazaliwa, nayo hufanyika kwa kulipa malipo kabla. Aina ya pili ni kumuuza mnyama kwa sharti la kuchukua mtoto atakayezaliwa. Aina zote za biashara hizi zilikatazwa kwa sababu ya mikataba yake kutokuwa wazi.
[20] Al-Walaa: mtumwa aliyeachwa huru akifa na kama hana wa kumrithi basi atarithiwa na yule aliyemuacha huru. Hadiyth imeweka wazi kuwa Al-Walaa ni kama uzawa wa mtu. Ikiwa kizazi cha mtu hakiwezi kuuzwa au mtu kupewa hiba, basi hivyo hivyo kuuza Walaa au kutoka kama zawadi ni jambo lililokatazwa.
[21] Biashara ya kurusha kijiwe ziko aina nyingi ikiwemo mmoja kumuambia mwengine: “Rusha kijiwe hiki, kitakapoangukia katika nguo yoyote itakuwa ni yako”, kwa kiasi kilichopangwa kabla. Biashara hii ni ya udanganyifu na ni biashara ya kubahatisha, kama vile kuuza njiwa akiwa hewani anaruka au kuuza samaki aliye baharini au kumuuza mtumwa aliyepotea au mnyama. Hizi ni aina za biashara zilizokuwa zama za ujahiliya.
[22] Katika sampuli hii ya biashara muuzaji anapanga bei mbili katika uzo moja. Uzo moja kwa malipo taslimu na lingine kwa mkopo. Bei ya mkopo linakuwa juu zaidi, fedha iliyozidi katika bei ya mkopo ni riba ambayo ni haramu.
[23] Baadhi ya Wanazuoni wa Hadiyth hawakubaliani na mapokezi haya ya mwisho ambayo Muhammad bin ‘Amr akiwa mmoja wa wapokezi. Hata hivyo imewekwa katika Hadiyth Hasan na wengine Swahiyh. Angalia ‘Irwaa Al-Ghaliyl, Shaykh Al-Albani 5/149-150.
[24] Biashara hii ina sampuli mbili: aina ya kwanza ni kama mtu anayeuza farasi kwa riyali mia moja kwa mkopo kwa sharti kuwa mnunuzi atalipa muda fulani. Ikiwa mnunuzi atashindwa kulipa deni lile kwa muda uliopangwa basi muuzaji atamnunua farasi yule kwa shilingi mia na hamsini na kumuacha mnunuzi akidaiwa shilingi mia na hamsini. Hii ni haramu. Sampuli ya pili ni mfano wa nyumba yenye thamani ya shilingi milioni kumi na mbili, huuzwa kwa mtu kwa milioni kumi kwa sharti kuwa mnunuzi atamuazima muuzaji shilingi milioni mbili.
[25] Kama vile kumuambia mtu: “Ntakuuzia nyumba hii kwa shilingi milioni kumi pesa taslimu au kwa shilingi milioni kumi na tatu kwa mkopo.”
[26] Kuuza kitu usichokimiliki mfano wake ni kama vile kuenda sehemu na ukanunua kitu na hapo hapo dukani ukamuuzia mtu na ukamlipa mwenye duka na faida uchukue wewe.
[27] ‘Urbaan ina maana ya kuweka kwa ajili ya kukilinda kitu au kukizuia kwa ajili ya kukinunua kitu. Kwa mfano kama mtu atatoa hela ya kununua mnyama kama hivi na mnunuzi anakaa na hela ile iliyowekwa kama dhamana, kama biashara itakamilika fedha zile zitakatwa katika mauzo. Mauzo haya si halali kulingana na Hadiyth. Hata hivyo, baadhi ya Wanazuoni wanazingatia Hadiyth hii kuwa ni dhaifu. Hivyo basi, imekuwa ni haramu kwa muono wa Imaam Maalik na Shaafiy’ na kukubaliwa na Imaam Ahmad. Fedha hizi ambazo mtu anazitoa ambazo hazitarejeshwa kwake kama biashara haijakamilika huitwa ‘dhamana isiyorejeshwa’.
[28] Ina maana kuwa mtu anaponunua bidhaa sehemu hairuhusiwi kuiuza pale pale tena, hadi itakapohamia katika miliki ya mnunuzi kabla ya kuiuza tena. Hukumu hii ni kwa bidhaa ambayo inaweza kuhamishika. Kwa biashara kama ya nyumba, inawezekana pale tu baada ya kukamilisha taratibu zote za mauzo, hapo naye anaweza kuiuza.
[29] Dirhamu ni sarafu ya fedha, dinari ni sarafu ya dhahabu. Kubadilisha dinari na dirhamu na kinyume chake ni halali madamu mabadilishano haya yatamalizika na kuhitimishwa kwa bei ya siku ile na kila mtu atapokea haki yake kwa ukamilifu. Hii inafahamika kama biashara ya kubadilisha fedha.
[30] An-Najsh ni mtu kuzidisha thamani ya bidhaa kwa kutokuwa na niyyah ya kununua, bali ili watu wainunue kwa bei ya juu.
[31] Muhaaqalah: ni kuuza nafaka katika shuke lake (kabla kuvunwa) kwa kukadiria na nafaka zilizopimwa (zilizovunwa) kama ngano.
[32] Muzaabanah: ni kuuza matunda (au mazao) yaliyo katika shamba (ambayo bado hayajachumwa) kwa matunda yaliyokwisha chumwa. Mauzo haya si halali
[33] Mukhaabarah: ni mtu kukodisha shamba ili malipo yake yawe ni baadhi ya mazao yatakayotoka kama ni nusu ya mazao au theluthi. Kimsingi mauzo haya ni halali na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliyafanya kwa Mayahudi wa Khaybar. Kinachokatazwa na Hadiyth hii ni kuainisha kipande cha mazao ya ardhi mmiliki na kipande kingine cha ardhi cha aliyekodishwa. Suala hili linaleta mgongano na wamiliki wa ardhi na wakodishaji, ikiwa mazao ya mwenye shamba yasipofanikiwa kuvunwa na ya mkodishaji kuvunwa au kinyume chake. Hata hivyo hakuna tatizo kama watakubaliana kushirikiana mazao yote yaliyovunwa kwa kiwango watakachobaliana.
[34] Thun-yaa ni kuuza mazao shambani yakiwa katika mti kwa bei kadhaa kwa sharti la kuvuna baadhi ya matunda. Hii ni haramu kwa kuwa kilichovunwa hakijulikani. Hata hivyo kama kiwango kitaainishwa basi inaruhusiwa.
[35] Mukhaadhwarah: ni kuuza nafaka au matunda kabla ya kuiva.
[36] Mulaamasah: ni mtu aiguse nguo bila ya kuitazama. Mauzo kwa bei iliyokwishapangwa anainunua akiwa amefunga macho au katika kiza kwa mguso mmoja wa mkono wake. Kwa mfano mtu anakwenda kwa muuza nguo na anapendekeza anunue jora ya kitambaa kwa kiasi cha fedha. Anakubali kununua kwa sharti la kuwa atafunga macho kisha atashika jora la kitambaa, na atanunua jora ambalo atashika mwanzo. Biashara ya sampuli hii imekatazwa.
[37] Munaabadhah: ni mtu kuirusha nguo yake katika hali ya kiza kwa mtu mwingine kabla ya kuikagua au kuitazama na huyo anayerushiwa huinunua.
[38] Jina lake kamili ni Abuu ‘Abdir-Rahmaan Twaawus bin Kisan Al-Faaris, ameachwa na wao (kina Al-Himyaar). Jina lake alikuwa ni Dhakwaan na Twaawus ilikuwa ni lakabu yake. Ni madhubuti, faqihi (Mwanachuoni wa Shariy’ah). Alikuwa ni Taabiy’ wa daraja la tatu. Amepokewa akisema: “Nimekutana na Maswahaba 50 katika uhai wangu.” Ibn ‘Abbaas amesema: “Sijawahi kumuona mfano wake.” Alifariki mwaka wa 106 Hijriyyah.
[39] Kuwapokea wasafiri nje ya mji, kwa lengo la kununua bidhaa kutoka kwao kwa bei ya chini, na kuwaficha hali halisi ya soko lilivyo ni jambo lisiloruhusiwa. Misafara iruhusiwe kufika katika vituo vyake vya biashara na kujua bei ya soko. Kabla ya hili kuuza na kununua hakutakiwi. Ikiwa mtu atapatana katika mauzo na baadae muuzaji akafahamu kuwa amedanganywa anaweza kuvunja biashara ile.
[40] Najsh imeelezwa hapo kabla. Maelezo mengine ni kuwa ikiwa mtu kanunua kutoka kwa mwenye duka, mwenye duka mwingine hatakiwi kumshawishi mtu yule anunue kutoka kwake kwa kumuuzia kwa bei ya chini zaidi.
[41] Haitakiwi kwa mwanamke kuleta na kusababisha chuki baina ya mke na mume, ili asababishe talaka baina yao ili apate kuolewa yeye na mme huyo. Hali kadhaalika ni haramu kumuoa dada au ndugu ya mtu kwa sharti la kumuacha mke wake wa kwanza.
[42] Kwa mfano mtu akikubaliana na mtu kumuuzia kitu kwa shilingi elfu moja. Hairuhusiwi kwa mtu mwingine kumshawishi muuzaji asiuze kwa shilingi elfu moja, kwa yeye kutaka kununua kwa elfu moja na mia tano kwa kitu kile kile. Hata hivyo ikiwa bidhaa imewekwa kwa ajili ya ushindani kama vile mnadani, inafaa mtu kuongeza thamani.
[43] Hadiyth hii inaashiria kufarakanisha haifai. Hadiyth hii inaweka wazi kama biashara hiyo itaendelea ni haki kuivunja.
[44] Hadiyth hii inaashiria kuwa suala la kupanga bei haliruhusiwi kwani inapelekea hasara wakati mwingine kwa wafanya biashara, kwa upande wa pili inapelekea katika janga la njaa. Mahitaji muhimu ya maisha yanakosekana na uchafu unaibuka katika jamii.
[45] Ma’mar bin ‘Abdillaah bin Naafi’ bin Nadla bin Harthaan Al-‘Adawi ni Swahaba mkubwa, ni miongoni mwa waliohajiri Uhabeshi. Hijra yake Madiynah ilichelewa.
[46] Ihtikaar – Ukiritimba ni kuzuia bidhaa kwa ajili ya mauzo ya faida kubwa zaidi baadae. Ukiritimba umekatazwa na ni haramu kwani inatengeneza uhaba wa mahitaji muhimu wa chakula wakati katika hali halisi vyakula vipo.
[47] Katika Hadiyth, siku tatu zimetajwa kwa sababu kwa uchache siku tatu zinahitajika kutathmini kiasi halisi cha maziwa katika kiwele. Wakati mwingine nyasi kavu na kubadilika kwa sehemu husababisha maziwa kuongezeka. Ikiwa maziwa yataachawa katika kiwele kwa matumizi binafsi na si kwa kuuza inaruhusiwa. Kwa hali yoyote ile, kuyaacha maziwa katika kiwele cha mnyama humuumiza mnyama.
[48] Ina maana kama mnunuzi ataona ubaya wa muamala huu, anaweza kurudi baada ya siku tatu. Kama mauzo ni maziwa ya ng’ombe, yatarudishwa kwa pishi (sawa na 2.6 kg) kwa nafaka yoyote, sio lazima iwe tende.
[49] Hii ina maana kwamba udanganyifu ni jambo lililokatazwa. Maana ya Hadiyth hii ni Udanganyifu si laiki ya watu wangu. “Ni tabia ya kikafiri.” Haina maana kuwa yeye ni kafiri.
[50] Ni haramu kuuza zabibu kwa mtengeneza mvinyo. Kusaidia kitendo chochote cha ubaya na kwa malengo mabaya ni haramu. Qur-aan Suwrah Al-Maaidah (5: 2) inatuamrisha kufanya na kushirikiana kwa matendo mema na kutukataza kabisa kushirikiana na madhambi na matendo mabaya.
[51] Ina maana hadi wakati wa kurudisha bidhaa (kama haitakiwi) faida na hasara inakuwa kwa mnunuzi. Jaalia mauzo ni ya mnyama, na mnyama akafa katika muda walioahidiana arudishe basi hasara inakuwa kwa mnunuzi, hali kadhalika kama atamuuza kwa bei ya juu zaidi wakati ule faida ataichukua yule mnunuzi.
[52] Huyu ni Ibn Ja’ad au Ibn Abiy Ja’ad na inasemekana kuwa baba yake akiitwa ‘Iyyaad Al-Baariqiyy, ni sehemu ya ukoo wa Baniy ‘Azd ambaye ni Baariqiyy bin ‘Adi bin Haaritha. Alikuwa akiitwa Baariqiyy kwa sababu aliishi katika mlima ulioitwa Baariqiyy. ‘Urwah alikuwa ni Swahaba aliyemtumikia ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kama Qadhi wa mji wa Kufa, aliishi huko na Hadiyth zake nyingi zilipokewa na watu wa huko.
[53] Udhwhiyyah ni mnyama anayechinjwa katika siku ya ‘Iyd ya Hajj.
[54] Hadiyth hii inaweka wazi mambo manne: (i) Wakili anapewa nguvu na mamlaka ya kutumia utajiri wa mdhamini wake. (ii) Huwezi kuuza bidhaa ila kwa ridhaa ya mwenyewe. (iii) Kuwa ni ruhusa kumuuza mnyama wa Udhwhiyyah na kumnunua mwingine kwa badala, biashara hii haitakiwi iwe kwa ajili ya faida. Kama kutakuwepo na faida yoyote kutokana na biashara hii basi itolewe kama Swadaqah. (iv) Ya kwamba wema wowote ni lazima ushukuriwe na uwe na malipo yake.
[55] Chuchu la mnyama, yaani kiwele chake.
[56] Katika Hadiyth hii kumetajwa mambo sita yaliyokatazwa katika biashara na sababu zake zinatofautiana. Uharamu wa mawili yaliyotajwa hauna utata ndani yake kwani Wanazuoni wamekubaliana, nazo ni katika biashara za kubahatisha. La tatu ni haramu kwa sababu ya kutokuwa na hakika na hali ya mtumwa aliyekimbia. La nne ni haramu kwa kuwa haipo katika miliki, la sita ni haramu kwa kuwa hakuna uhakika kama mzamiaji atatoka na chochote anapozamia. Nayo ni hali ya kubahatisha. Kubahatisha kwa mpiga mbizi ni mtu kusema: “Nitapiga mbizi katika maji kwa shilingi kadhaa kitakachotoka ni chako.” Biashara hii imekatazwa kwa sababu ya udanganyifu.
[57] Kiwele: ziwa la mnyama. Katika Hadiyth hii aina tatu za biashara haramu zimetajwa. Ya kwanza ni matunda ambayo bado hayajawiva, matunda yaliyopo mtini kwani kuna uwezekano wa kuharibika hadi yawive. Nukta ya pili ni kuwa mti ni mali ya muuzaji na matunda yake ni mali ya mnunuzi. Ushirikiano wao wa muda mrefu hauwezi kudumu sana. Aina zingine za biashara zilizoharamishwa hapa ni Sufi ya kondoo mgongoni mwake kabla hajanyolewa na maziwa ya mnyama yakiwa katika kiwele chake. Hizi ni haramu kwa sababu kiwango cha sufi na maziwa hayajulikani, ni aina ya bahati nasibu ambayo ni biashara ya kubahatisha.
[58] Madhwaamiyn neno la kiarabu lenye maana ya kizazi kwa maana ya mimba ambayo haijazaliwa katika tumbo la mamake.
[59] Al-Malaaqiyh ni manii katika mgongo wa baba.
[60] Ikiwa wameshakubaliana kuwa mali inaweza kurudishwa, mnunuzi ana haki kamili ya kurejesha. Hata hivyo kama hawajakubaliana hapo kabla na mnunuzi anataka kurejesha, na akamrudishia muuzaji, basi yule muuzaji atakapokubali, kwa khiyari yake, kurudisha bidhaa ile, Allaah atamsamehe madhambi yake.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْخِيَارِ
02-Mlango Wa Khiyari
692.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِذَا تَبَايَعَ اَلرَّجُلَانِ، فَكُلُّ وَاحِدٍ مِنْهُمَا بِالْخِيَارِ مَا لَمْ يَتَفَرَّقَا وَكَانَا جَمِيعاً، أَوْ يُخَيِّرُ أَحَدُهُمَا اَلْآخَرَ، فَإِنْ خَيَّرَ أَحَدُهُمَا اَلْآخَرَ فَتَبَايَعَا عَلَى ذَلِكَ فَقَدَ وَجَبَ اَلْبَيْعُ، وَإِنْ تَفَرَّقَا بَعْدَ أَنْ تَبَايَعَا، وَلَمْ يَتْرُكْ وَاحِدٌ مِنْهُمَا اَلْبَيْعَ فَقَدْ وَجَبَ اَلْبَيْعُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Wakiuziana watu wawili basi kila mmoja miongoni mwao yuko katika khiyari[1] maadamu hawajaachana na wapo pamoja, au mmojawapo amkhiarishe mwingine na wakauziana juu ya maafikiano hayo; basi kuuziana kumeshapasa. Na wakiachana baada ya kuuziana, na mmoja kati yao hakuacha kuuza au kununua, basi kuuziana kumeshapasa.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
693.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {اَلْبَائِعُ وَالْمُبْتَاعُ بِالْخِيَارِ حَتَّى يَتَفَرَّقَا، إِلَّا أَنْ تَكُونَ صَفْقَةَ خِيَارٍ، وَلَا يَحِلُّ لَهُ أَنْ يُفَارِقَهُ خَشْيَةَ أَنْ يَسْتَقِيلَهُ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ إِلَّا اِبْنَ مَاجَهْ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ وَفِي رِوَايَةٍ:{حَتَّى يَتَفَرَّقَا مِنْ مَكَانِهِمَا}
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb amepokea kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake kuwa amesema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muuzaji na mnunuzi wako katika khiyari hadi watakapoachana, isipokuwa iwe na maafikiano ya khiyari, wala si halali kwake kufarikiana naye kwa kuchelea asije akabatilisha mauziano.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ahmad) isipokuwa Ibn Maajah, na imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy, Ibn Khuzaymah na Ibn Al-Jaaruwd]
Katika Riwaayaha nyingine imesema: “…mpaka wafarikiane mahala pao.”
694.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: ذَكَرَ رَجُلٌ لِلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنَّهُ يُخْدَعُ فِي اَلْبُيُوعِ فَقَالَ: {إِذَا بَايَعْتَ فَقُلْ: لَا خَلَابَةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa mtu mmoja[2] amemuambia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuwa yeye hudanganywa katika biashara. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Unapofanya biashara, muambie unayefanya naye hakuna kuhadaana.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] Ikhtiyaar au Khiyaar ni mtu kuwa na haki ya kuvunja mkataba. Kuna aina nyingi za khiyaar:
i. Khiyaar Majlis: muda wa kuwa muuzaji na mnunuzi wako pamoja, kila mmoja ana haki ya kukataa au kukubali muamala.
ii. Khiyaar Shartw: Muuzaji na mnunuzi wanaweka sharti kuwa hadi muda fulani, basi kila mmoja wao ana haki ya kukubali au kukataa mauzo.
iii. Khiyaar ‘Ayb: Mnunuzi anasema ikiwa bidhaa ni mbovu atairudisha.
Iv. Khiyaar Ru’yah: Mnunuzi anakamilisha muamala kwa sharti kuwa itakamilika baada ya kuona bidhaa.
v. Khiyaar Ta’ayiyn: Ina maana kuwa mnunuzi anaruhusiwa kuchagua anachokitaka.
[2] Bwana huyu akiitwa Habbaan bin Munqadh. Alipata ajali kichwani na kumbukumbu yake ikawa ndogo, baadhi ya watu walikuwa wakimdanganya katika biashara, kwa hivyo Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamfundisha maneno haya.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلرِّبَا
03-Mlango Wa Ribaa
695.
عَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {لَعَنَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ آكِلَ اَلرِّبَا، وَمُوكِلَهُ، وَكَاتِبَهُ، وَشَاهِدَيْهِ، وَقَالَ: " هُمْ سَوَاءٌ "} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
وَلِلْبُخَارِيِّ نَحْوُهُ مِنْ حَدِيثِ أَبِي جُحَيْفَةَ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amemlaani mlaji ribaa, mwakilishi wake, mwandishi wake, na mashahidi wake wawili na akasema: “Wote wako sawa.”[1] [Imetolewa na Muslim]
Na katika Al-Bukhaariy amepokea kama hiyo katika Hadiyth ya Abuu Juhayfah
696.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {اَلرِّبَا ثَلَاثَةٌ وَسَبْعُونَ بَابًا أَيْسَرُهَا مِثْلُ أَنْ يَنْكِحَ اَلرَّجُلُ أُمَّهُ، وَإِنَّ أَرْبَى اَلرِّبَا عِرْضُ اَلرَّجُلِ اَلْمُسْلِمِ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ مُخْتَصَراً، وَالْحَاكِمُ بِتَمَامِهِ وَصَحَّحَهُ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ribaa ina milango sabini na tatu mwepesi wake ni mfano wa mtu kumuowa mama yake. Kwa hakika ribaa kubwa zaidi ni mtu kuchafua heshima ya Muislam.” [Imetolewa na Ibn Maajah kwa mukhtasari, na Al-Haakim ameipokea kwa ukamilifu na akaisahihisha]
697.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا تَبِيعُوا اَلذَّهَبَ بِالذَّهَبِ إِلَّا مِثْلًا بِمِثْلٍ، وَلَا تُشِفُّوا بَعْضَهَا عَلَى بَعْضٍ، وَلَا تَبِيعُوا اَلْوَرِقَ بِالْوَرِقِ إِلَّا مِثْلًا بِمِثْلٍ، وَلَا تُشِفُّوا بَعْضَهَا عَلَى بَعْضٍ، وَلَا تَبِيعُوا مِنْهَا غَائِباً بِنَاجِزٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msiuze dhahabu kwa dhahabu isipokuwa sawa kwa sawa, wala msizidishe baadhi yake juu ya baadhi nyingine. Wala msiuze fedha kwa fedha isipokuwa sawa kwa sawa, wala msizidishe baadhi yake juu ya baadhi nyingine, wala msiuze kusichokuwepo kwa kilichopo.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
698.
وَعَنْ عُبَادَةَ بْنِ اَلصَّامِتِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلذَّهَبُ بِالذَّهَبِ، وَالْفِضَّةُ بِالْفِضَّةِ، وَالْبُرُّ بِالْبُرِّ، وَالشَّعِيرُ بِالشَّعِيرِ، وَالتَّمْرُ بِالتَّمْرِ، وَالْمِلْحُ بِالْمِلْحِ، مِثْلًا بِمِثْلٍ، سَوَاءً بِسَوَاءٍ، يَدًا بِيَدٍ، فَإِذَا اِخْتَلَفَتْ هَذِهِ اَلْأَصْنَافُ فَبِيعُوا كَيْفَ شِئْتُمْ إِذَا كَانَ يَدًا بِيَدٍ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit[2] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Dhahabu kwa dhahabu, fedha kwa fedha, ngano kwa ngano, shayiri[3] kwa shayiri, tende kwa tende, chumvi kwa chumvi, mfano kwa mfano, sawa kwa sawa, mkono kwa mkono,[4] zitatofautiana aina hizi basi uza unavyotaka muda wa kuwa mauzo yatafanyika mkono kwa mkono.” [Imetolewa na Muslim]
699.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلذَّهَبُ بِالذَّهَبِ وَزْناً بِوَزْنٍ مِثْلًا بِمِثْلٍ، وَالْفِضَّةُ بِالْفِضَّةِ وَزْناً بِوَزْنٍ مِثْلًا بِمِثْلٍ، فَمَنْ زَادَ أَوْ اِسْتَزَادَ فَهُوَ رِبًا} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Dhahabu kwa dhahabu, wizani kwa wizani, mfano kwa mfano, fedha kwa fedha, wizani kwa wizani, mfano kwa mfano, atakayezidisha au akataka kuzidishiwa basi hiyo itakuwa ribaa.” [Imetolewa na Muslim]
700.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ، وَأَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اِسْتَعْمَلَ رَجُلًا عَلَى خَيْبَرٍ، فَجَاءَهُ بِتَمْرٍ جَنِيبٍ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَكُلُّ تَمْرِ خَيْبَرَ هَكَذَا ؟ " فَقَالَ: لَا، وَاَللَّهِ يَا رَسُولَ اَللَّهِ، إِنَّا لَنَأْخُذُ اَلصَّاعَ مِنْ هَذَا بِالصَّاعَيْنِ وَالثَّلَاثَةِ فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " لَا تَفْعَلْ، بِعِ اَلْجَمْعَ بِالدَّرَاهِمِ، ثُمَّ اِبْتَعْ بِالدَّرَاهِمِ جَنِيبًا} وَقَالَ فِي اَلْمِيزَانِ مِثْلَ ذَلِكَ. مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ: "وَكَذَلِكَ اَلْمِيزَانُ "
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd na Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) wamesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimtawalisha mtu Khaybar,[5] akamjia na tende nzuri. Akasema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Tende zote za Khaybar ziko hivi?” Akasema: “Hapana. Wa-Allaahi Ee Rasuli wa Allaah! Hakika sisi huchukuwa pishi moja ya tende hizi kwa pishi mbili, au tatu (duni ya hizi).” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Usifanye hivyo, uza tende duni kwa dirhamu kadhaa kisha ununue tende nzuri kwa dirhamu kadhaa.” Na katika mizani alisema kama hivyo.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Muslim imesema: “…vile vile ilivyopimwa.”
701.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ بَيْعِ اَلصُّبْرَةِ مِنَ اَلتَّمْرِ لا يُعْلَمُ مَكِيلُهَا بِالْكَيْلِ اَلْمُسَمَّى مِنَ اَلتَّمْرِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza lundo la tende lisilojulikana kipimo chake kwa kipimo cha tende kilichotajwa.”[6] [Imetolewa na Muslim]
702.
وَعَنْ مَعْمَرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: إِنِّي كُنْتُ أَسْمَعُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {اَلطَّعَامُ بِالطَّعَامِ مِثْلاً بِمِثْلٍ " وَكَانَ طَعَامُنَا يَوْمَئِذٍ اَلشَّعِيرَ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Ma’mar bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Mimi nilikuwa nikimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Chakula kwa chakula, sawa kwa sawa, wakati huo chakula chetu kilikuwa ni shayiri.”[7] [Imetolewa na Muslim]
703.
وَعَنْ فَضَالَةَ بْنِ عُبَيْدٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {اِشْتَرَيْتُ يَوْمَ خَيْبَرَ قِلَادَةً بِاِثْنَيْ عَشَرَ دِينَاراً، فِيهَا ذَهَبٌ وَخَرَزٌ، فَفَصَلْتُهَا فَوَجَدْتُ فِيهَا أَكْثَرَ مِنْ اِثْنَيْ عَشَرَ دِينَاراً، فَذَكَرْتُ ذَلِكَ لِلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: "لَا تُبَاعُ حَتَّى تُفْصَلَ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Fadhwaalah bin ‘Ubayd[8] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilinunua mkufu Siku ya Khaybar kwa dinari kumi na mbili, ndani yake kuna dhahabu na kito, nikavitenganisha, nikapata zaidi ya dinari kumi na mbili, nikamuelezea jambo hilo Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaniambia: “Haiuzwi mpaka ipambanuliwe.”[9] [Imetolewa na Muslim]
704.
وَعَنْ سَمُرَةَ بْنِ جُنْدُبٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ بَيْعِ اَلْحَيَوَانِ بِالْحَيَوَانِ نَسِيئَةً} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ
Kutoka kwa Samurah bin Jun-dub (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): amekataza kuuza mnyama kwa mnyama kwa kuchelewesha.”[10] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha At-Tirmidhiy na Ibn Al-Jaaruwd]
705.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {إِذَا تَبَايَعْتُمْ بِالْعِينَةِ، وَأَخَذْتُمْ أَذْنَابَ اَلْبَقَرِ، وَرَضِيتُمْ بِالزَّرْعِ، وَتَرَكْتُمْ اَلْجِهَادَ، سَلَّطَ اَللَّهُ عَلَيْكُمْ ذُلًّا لَا يَنْزِعُهُ حَتَّى تَرْجِعُوا إِلَى دِينِكُمْ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ مِنْ رِوَايَةِ نَافِعٍ عَنْهُ، وَفِي إِسْنَادِهِ مَقَالٌ
وَلِأَحْمَدَ: نَحْوُهُ مِنْ رِوَايَةِ عَطَاءٍ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ وَصَحَّحَهُ اِبْنُ اَلْقَطَّانِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Mtakapouziana kwa Al-‘Iynah,[11] mkashika mikia ya ng’ombe,[12] mkaridhia kulima na mkaacha Jihaad, Allaah Atawasalitisha udhalili ambao hatauondoa mpaka mrudi katika Dini yenu.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd kutoka katika Riwaayah ya Naafi’[13] na katika Isnaad yake kuna maelezo]
Na Ahmad amepokea kama hivyo kutoka Riwaayah ya ‘Atwaa,[14] wapokezi wake ni madhubuti, na akaisahihisha Ibn Al-Qatwaan
706.
وَعَنْ أَبِي أُمَامَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ شَفَعَ لِأَخِيهِ شَفَاعَةً، فَأَهْدَى لَهُ هَدِيَّةً، فَقَبِلَهَا، فَقَدْ أَتَى بَابًا عَظِيماً مِنْ أَبْوَابِ اَلرِّبَا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَفِي إِسْنَادِهِ مَقَالٌ
Kutoka kwa Abuu Umaamah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kumuombea nduguye uombezi akampa zawadi akaikubali, kwa hakika atakuwa ameingia mlango mkubwa miongoni mwa milango ya ribaa.”[15] [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd, na katika Isnaad yake kuna maelezo]
707.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرِوٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {لَعَنَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اَلرَّاشِي وَالْمُرْتَشِيَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amemlaani mtoa rushwa na mpokea rushwa.”[16] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy akaisahihisha]
708.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرٍو رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّ رَسُولَ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَمَرَهُ أَنْ يُجَهِّزَ جَيْشًا فَنَفِدَتْ اَلْإِبِلُ، فَأَمَرَهُ أَنْ يَأْخُذَ عَلَى قَلَائِصِ اَلصَّدَقَةِ. قَالَ: فَكُنْتُ آخُذُ اَلْبَعِيرَ بِالْبَعِيرَيْنِ إِلَى إِبِلِ اَلصَّدَقَةِ} رَوَاهُ اَلْحَاكِمُ وَالْبَيْهَقِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuamrisha kuandaa jeshi, ngamia wakamalizika, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuamrisha kuchukua katika ngamia wa Zakaah. Akasema: “Nikawa nawabadilisha ngamia wawili wadogo wa Zakaah kwa ngamia mmoja mkubwa.” [Imetolewa na Al-Haakim na Al-Bayhaqiyy na wapokezi wake ni madhubuti][17]
709.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنِ الْمُزَابَنَةِ، أَنْ يَبِيعَ ثَمَرَ حَائِطِهِ إِنْ كَانَ نَخْلاً بِتَمْرٍ كَيْلاً، وَإِنْ كَانَ كَرْماً أَنْ يَبِيعَهُ بِزَبِيبٍ كَيْلاً، وَإِنْ كَانَ زَرْعاً أَنْ يَبِيعَهُ بِكَيْلِ طَعَامٍ، نَهَى عَنْ ذَلِكَ كُلِّهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza Al-Muzaabanah kwa kuuza matunda ya shambani mwake ikiwa ni mtende kwa tende kwa kupimwa na ikiwa ni zabibu kuziuza kwa zabibu kwa kupimwa na ikiwa ni mavuno kuyauza kwa kipimo cha chakula. Ameyakataza yote hayo.”[18] [Al-Bukhaariy, Muslim]
710.
وَعَنْ سَعْدِ بْنِ أَبِي وَقَّاصٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ سُئِلَ عَنِ اِشْتِرَاءِ اَلرُّطَبِ بِالتَّمْرِ. فَقَالَ: أَيَنْقُصُ اَلرُّطَبُ إِذَا يَبِسَ ؟ " قَالُوا: نَعَمَ. فَنَهَى عَنْ ذَلِكَ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ اَلْمَدِينِيِّ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Sa’d bin Abiy Waqqaasw[19] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akiulizwa kuhusu kununua tende mbivu kwa tende kavu, akasema: ‘Je mbivu hupungua zinapokauka?” Wakasema: “Ndio.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akakataza kufanya hivyo.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha Ibn Al-Madiyniyy, At-Tirmidhiyy, Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
711.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ بَيْعِ اَلْكَالِئِ بِالْكَالِئِ، يَعْنِي: اَلدَّيْنِ بِالدَّيْنِ} رَوَاهُ إِسْحَاقُ، وَالْبَزَّارُ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza Al-Kaali (kuuza deni) kwa Al-Kaali (kwa deni).”[20] [Imetolewa na Ishaaq na Al-Bazzaar kwa Isnaad dhaifu]
[1] Ribaa ni haraam kwa dalili zilizo wazi kabisa katika Qur-aan. Yeyote atakayetoa mkopo kwa sharti la ribaa, na atakayepokea, mwandishi wake na shahidi wake, wote wamelaaniwa.
[2] ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit bin Qays Al-Answaar, Al-Khazraj, Abul-Waliyd.
[3] Shayiri: nafaka inayofanana na ngano inayotumika kwa chakula. Ingawaje maeneo ya huku hutumika zaidi kutengeneza bia.
[4] Vitu vilivyotajwa na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) vilikuwa ni dhahabu, fedha, ngano, shayiri, tende na chumvi hakuna nyongeza au punguzo za vitu hivi vilivyotajwa katika kubadilishana navyo. Kwa mfano, mtu anataka aina nzuri ya ngano na mwingine ana aina ya chini, hairuhusiwi kubadilisha kilo 20 za ngano bora kwa kilo 30 za ngano za hali ya chini. Ikiwa mtu anataka kubadilisha aina ya ngano aliyonayo kwa nyingine, ni bora auze aliyonayo kisha kwa thamani ile anunue aina anyingine kwa fedha zile. Mabadilishano ya bidhaa hizi kwa nyongeza au nuksani hairuhusiwi kabisa. Baadhi ya Wanazuoni wamejuzisha zidisho na punguzo kwa baadhi za bidhaa zisizokuwa hizi sita, hata hivyo Maimaam wane hawakubali mabadilishano haya madamu ni aina moja ya bidhaa kwa bidhaa mfano wake.
[5] Anayezungumziwa hapa ni Sawaad bin Ghaziyya Al-Answaar.
[6] Ina maana ya kwamba bidhaa yoyote inayouzwa kwa kipimo maalumu inabidi iuzwe au kibadilishwe kwa kipimo hicho maalumu na siyo kwa kudhania kipimo au kubahatisha.
[7] Katika Hadiyth nyingine inatajwa kuwa chakula cha wakati ule kilikua ni ngano. Ma’mar anataka kuelezea kuwa ngano na shayiri ni sawa sawa na ichukuliwe kuwa ni aiana moja ya chakula na katika kubadilishana kisipungue au kisizidi. Hata hivyo Maswahaba wengine hawakukubaliana hivi. Kama ilivyoripotiwa na ‘Ubaadah bin Swaamit (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) ambayo imeweka wazi kuwa ngano na shayiri ni vyakula vya aina mbili tofauti.
[8] Huyu ni Fadhwaalah bin ‘Ubayd Al-Answaar Al-Aws, Abuu Muhammad
[9] Hadiyth hii inatoa ushahidi kuwa dhahabu ikichanganywa na kitu kingine isiuzwe isipokuwa iwe imetenganishwa na dhahabu safi nyinginezo, kwani ni vigumu kukadiria uzito wa dhahabu iliyochanganywa na kitu kingine.
[10] Inaruhusiwa kumuuza mmoja kwa thamani ya wanyama wawili lakini kumuuza myama kwa mkopo au kwa kuchelewesha kulipa hakuruhusiwi.
[11] Al-‘Iynah: mfano wa Al-‘Iynah ni mtu kutaka akopeshwe kiasi cha fedha. Hampi huo mkopo bali humpa kilichokuwa na thamani zaidi ya huo mkopo. Kisha ananunua tena kutoka kwake kwa thamani ya chini ambayo ni sawa na mkopo aliouomba. Kwa hali hii anamfanya mdaiwa kudaiwa zaidi, yaani fedha aliyompa mkopo na ziada yake. Hii ni ribaa; kufanya hivi ni haramu kwa sababu inaingia katika ribaa ya kuchelewesha. Na inadhihirisha kuwa mambo mawili hayo ni sababu ya kumdhalilisha Muislamu; moja ni kuiacha jihaad na ya pili ni kughushi na udanganyifu.
[12] “…mkashika mikia ya ng’ombe” yaani mkawa mmeshughulika na mifugo tu.
[13] Huyu ni Abuu ‘Abdillaah Naafi’ bin Sirjis Al-Madani, muachwa huru wa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) aliyetekwa katika vita. Ni mtu madhubuti na Mwanazuoni mkubwa katika Taabi’iyna. Amepokea Hadiyth nyingi zilizohadithiwa na Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا). Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) anasema: “Allaah Ametubariki kwa Naafi’.” Imepokewa kuwa Maalik naye amesema: “Nilikuwa sijisumbui kuchukua Hadiyth kwa yeyote maadamu nikiipata kwa Naafi’ kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ).” Al-Bukhaariy vile vile amesema: “Silsila ya upokezi iliyo sahihi zaidi ni ile kutoka kwa Maalik kutoka kwa Naafi’ kutoka kwa Ibn ‘Umar (kutoka kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)).” Watu wengi wamepokea Hadiyth kutoka kwa Naafi’ alifariki mwaka 117 Hijriyyah.
[14] Uwezekano mkubwa ‘Atwaa huyu akawa ni ‘Atwaa Al-Khurasani ambaye akiitwa Abuu ‘Uthmaan ‘Atwaa bin Abiy Muslim Maysarah, muachwa huru wa Al-Muhalab bin Abiy Sufra. Aliishi Shaam na alikuwa ni mtu mwenye hadhi kubwa. Alikuwa ni mtu madhubuti na alikuwa ni mwenye kudumu katika Swalaah za usiku. Kwa bahati mbaya kumbukumbu yake haikuwa nzuri kwa hiyo alikuwa na makossa katika mapokezi yake. Alifariki mwaka 135 Hijriyyah akiwa na miaka 85.
[15] Ikiwa zawadi hiyo atapewa kabla ya kumuombea pamoja na kumuombea katika yasiyofaa, uharamu wake umekubaliwa na Wanazuoni wote, na inahesabiwa ni rushwa na sio zawadi. Kuunga mkono yasiyofaa na kuchukua zawadi kwa ajili yake ni katika kundi hili hili. Ikiwa mtu amesaidia katika kufanywa kwa mambo mema kisha akapokea zawadi kwa ajili hiyo inaruhusiwa ikiwa halikuwa katika ahadi au kushurutishwa.
[16] Anayepokea rushwa amelaaniwa. Anayelazimishwa kutoa rushwa apate haki yake Allaah atamsamehe. Lakini rushwa ikitolewa kuchepua haki ya mwingine inaelekea mtu kupata laana ya Rabb wake
[17] Hadiyth hii ni dalili kuwa hakuna ribaa katika wanyama.
[18] Hii ni kwa sababu inahusika na kuuza kitu kisichojulikana thamani yake kwa kinachojulikana thamani yake. Kwa sababu biashara hii ni haraam.
[19] Aliitwa Sa’d bin Maalik bin Ahiyb (au Wuhayb) bin ‘Abd Manaaf bin Zuhrah bin Kilaab bin Murrah bin Ka’b bin Luay, na alikuwa ni wa kabila la Baniy Zuhrah. Ni wa familia ya Aaminah bint Wahb, mamake Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kwa hiyo alikuwa na udugu na ‘ammi zake Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Ukoo wake unakutana na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kwa Kilaab bin Murrah. Jina lake ndilo hilo hilo hata kabla ya kusilimu. Lakabu yake ilikuwa Abuu Ishaaq. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimbashiria Sa’d Jannah zaidi ya mara moja. Sa’d alikuwa mmoja wa watu kumi walioahidiwa Jannah na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), kumi wamo Jannah: Abuu Bakr yumo Jannah, ‘Umar yumo Jannah, ‘Uthmaan yumo Jannah, ‘Aliy, Az-Zubayr, Twalhah, ‘Abdur-Rahmaan bin ‘Awf, Abuu ‘Ubaydah bin Al-Jarraah na Sa’d bin Abiy Waqqaasw.
[20] Ipo katika aina mbili: kwa mfano: 1. ‘Aliy ananunua farasi kutoka kwa Bakr kwa Dirhamu mia moja, na anatoa ahadi kulipa baada ya mwaka mmoja, baada ya mwaka mmoja, anashindwa kulipa deni. Anakuenda kwa Bakr na kumuomba kuuziwa farasi tena kwa thamani ya juu. Hii ina maana kuwa ‘Aliy analipa ribaa kwa kuongezewa muda wa ziada wa kulipa. 2. Aina ya pili inaelezwa kwa mfano ufuatao: Jaalia kuwa ‘Umar anamdai Dirhamu kumi Zayd, naye Zayd anamdai kitambaa Bakr. Bakr anamuambia Zayd: “Nitakuuzia kipande cha kitambaa ninachomdai ‘Umar kwa Dirhamu kumi unayodaiwa na ‘Umar.” Hivyo basi, ‘Umar anampa kitambaa Zayd badala ya Bakr, naye anampa dirhamu kumi Bakr badala ya Zayd. Aina hii ya mauzo inakatazwa.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلرُّخْصَةِ فِي اَلْعَرَايَا وَبَيْعِ اَلْأُصُولِ وَالثِّمَارِ
04-Mlango Wa Ruhusa Katika ‘Araayaa Na Kuuza Mashina Na Matunda
712.
عَنْ زَيْدِ بْنِ ثَابِتٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {رَخَّصَ فِي اَلْعَرَايَا: أَنْ تُبَاعَ بِخَرْصِهَا كَيْلاً} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ:{رَخَّصَ فِي اَلْعَرِيَّةِ يَأْخُذُهَا أَهْلُ اَلْبَيْتِ بِخَرْصِهَا تَمْرًا، يَأْكُلُونَهَا رُطَبًا}
Kutoka kwa Zayd bin Thaabit (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Ameruhusu katika ‘Aryaaaa[1] ziuzwe kwa kuzikadiria kwa kipimo.” [Al-Bukaariy, Muslim]
Na katika Muslim imesema: “Ameruhusu katika ‘Ariyyah watu wa nyumbani wanazichukua kwa kuzikadiria na tende, na wale zilizoiva zikichumwa kutoka mtini.”
713.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ رَخَّصَ فِي بَيْعِ اَلْعَرَايَا بِخَرْصِهَا، فِيمَا دُونَ خَمْسَةِ أَوْسُقٍ، أَوْ فِي خَمْسَةِ أَوْسُقٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliruhusu katika biashara ya ‘Araayaa kwa kuzikadiria na tende chini ya wasaqi[2] tano au wasaqi tano.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
714.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ بَيْعِ اَلثِّمَارِ حَتَّى يَبْدُوَ صَلَاحُهَا، نَهَى اَلْبَائِعَ وَالْمُبْتَاعَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ:{وَكَانَ إِذَا سُئِلَ عَنْ صَلَاحِهَا ؟ قَالَ: "حَتَّى تَذْهَبَ عَاهَتُهُ "}
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza matunda hadi yamedhihiri kufaa kwake, amemkataza muuzaji na mnunuzi.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah nyingine imesema: “Na alikuwa anapoulizwa kuhusu kufaa kwake husema: mpaka iondoke aibu yake.”[3]
715.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ بَيْعِ اَلثِّمَارِ حَتَّى تُزْهَى. قِيلَ: وَمَا زَهْوُهَا ؟ قَالَ: " تَحْمَارُّ وَتَصْفَارُّ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza matunda mpaka yapevuke. Wakasema: Kupevuka kwake ni vipi? Akasema: Mpaka yawe mekundu au manjano.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la[4] Al-Bukhaariy]
716.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ { أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ بَيْعِ اَلْعِنَبِ حَتَّى يَسْوَدَّ، وَعَنْ بَيْعِ اَلْحَبِّ حَتَّى يَشْتَدَّ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، إِلَّا النَّسَائِيَّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuuza zabibu mpaka iwe nyeusi na amekataza kuuza nafaka mpaka iwe ngumu.”[5] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) isipokuwa An-Nasaaiy, na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
717.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَوْ بِعْتَ مِنْ أَخِيكَ ثَمَراً فَأَصَابَتْهُ جَائِحَةٌ، فَلَا يَحِلُّ لَكَ أَنْ تَأْخُذَ مِنْهُ شَيْئًا. بِمَ تَأْخُذُ مَالَ أَخِيكَ بِغَيْرِ حَقٍّ ؟} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
وَفِي رِوَايَةٍ لَهُ:{أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَمَرَ بِوَضْعِ اَلْجَوَائِحِ}
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Lau utamuuzia nduguyo matunda na yakapatwa na maafa basi si halali kwako kuchukua kitu kutoka kwake.[6] Kwa nini uchukue mali ya nduguyo bila haki?” [Imetolewa na Muslim]
Na katika Riwaayah yake nyingine amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ameamrisha kutupiliwa mbali malipo ya matunda yaliyopata maafa.”[7]
718.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنِ اِبْتَاعَ نَخْلًا بَعْدَ أَنْ تُؤَبَّرَ، فَثَمَرَتُهَا لِلْبَائِعِ اَلَّذِي بَاعَهَا، إِلَّا أَنْ يَشْتَرِطَ اَلْمُبْتَاعُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Atakayenunua mtende baada ya uchavushi,[8] basi matunda yake ni ya aliyeuza isipokuwa mnunuzi atakaposhurutisha.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] ‘Araayaa (wingi wa ‘Ariyyah) ni mtu kumzawadia maskini tende zake zinazokadiriwa wasaqi tano (kapu tano sawa na kilo 715 takriban) kisha yule mwenye shamba akaona uzito yule maskini kuingia katika shamba lake kwenda kuchuma basi akazinunua kwa kuzikadiria na tende kavu.
[2] Kipimo cha Wasaqi tano: hukisiwa kuwa ni kilo 650 takriban.
[3] Neno la kiarabu ‘Aahat lina maana ya magonjwa ya ghafla, aina hii ya biashara inakatazwa kwa sababu matunda ambao hayajawiva hayafai na matumizi yake si sawa, huenda ugonjwa ukayaangukia na kuyaharibu kwa kuyateketeza. Kwa uwezekano huu wa kuharibika ndio maana ukakatazwa kwa lugha nyingine yasiwe na baka: maradhi ya mimea.
[4] Hadiyth yamalizika hivi: Akasema: “(Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) Waonaje Allaah Akizuia (kuosha), matunda ni kwa kitu gani mmoja wenu atahalalisha mali ya nduguye?”
[5] Ina maana hadi ikomae, ndipo inaporuhusiwa kuuzwa. Hadiyth yaonyesha kuwa kuwiva kwa zabibu ni kuwa nyeusi na kuwiva kwa nafaka ni kuwa ngumu. Kila chakula kina namna yake ya kuwiva.
[6] Kama matunda yapo mtini na yakapatwa na maafa, mwenye mti atahusika na hasara ile. Ikiwa maafa ni baada ya kuchumwa kwa matunda basi hasara itabebwa na mnunuzi.
[7] Neno la kiarabu وَضْعِ اَلْجَوَائِحِ ina maana hata baada ya kuyachuma yakaonekana ambayo yameharibika muuzaji anatakiwa ampunguzie mteja wake.
[8] Uchavushi ni kupandisha ni kupasua tawi la mtende jike na kupandikiza la mtende dume.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
أَبْوَابُ اَلسَّلَمِ وَالْقَرْضِ، وَالرَّهْنِ
05-Mlango wa As-Salam (Malipo Ya Kabla),[1] Kukopesha[2] Na Kuweka Rahani
719.
عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَدِمَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اَلْمَدِينَةَ، وَهُمْ يُسْلِفُونَ فِي اَلثِّمَارِ اَلسَّنَةَ وَالسَّنَتَيْنِ، فَقَالَ: {مَنْ أَسْلَفَ فِي تَمْرٍ فَلْيُسْلِفْ فِي كَيْلٍ مَعْلُومٍ، وَوَزْنٍ مَعْلُومٍ، إِلَى أَجَلٍ مَعْلُومٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ.
وَلِلْبُخَارِيِّ: "مَنْ أَسْلَفَ فِي شَيْءٍ"
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliingia Madiynah na wao (wenyeji) wanafanya salaf katika matunda; kwa mwaka mmoja na miaka miwili. Akasema: “Atakayefanya salaf katika matunda basi afanye katika kipimo maalumu, na wizani maalumu na kwa muda maalumu.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Al-Bukhaariy imesema: “Atakayefanya salaf katika kitu chochote…”
720.
وَعَنْ عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ بْنِ أَبْزَى، وَعَبْدِ اَللَّهِ بْنِ أَبِي أَوْفَى رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَا: {كُنَّا نُصِيبُ اَلْمَغَانِمَ مَعَ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَكَانَ يَأْتِينَا أَنْبَاطٌ مِنْ أَنْبَاطِ اَلشَّامِ، فَنُسْلِفُهُمْ فِي اَلْحِنْطَةِ وَالشَّعِيرِ وَالزَّبِيبِ وَفِي رِوَايَةٍ: وَالزَّيْتِ إِلَى أَجَلٍ مُسَمًّى. قِيلَ: أَكَانَ لَهُمْ زَرْعٌ ؟ قَالَا: مَا كُنَّا نَسْأَلُهُمْ عَنْ ذَلِكَ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Abdul-Rahmaan bin Abzaa[3] na ‘Abdullaah bin Abiy Awfaa (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) wamesema: “Tulikuwa tukipata ghanima pamoja na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na tulikuwa tukijiliwa na Anbaatw[4] wa Sham (Syria, Palestina, Lebanon na Jordan) tulikuwa tukiwalipa kabla kwa ngano, shayiri[5] na zabibu.
Katika Riwaayah nyingine inasema: …na zeti (ya Zaituni) kwa muda maalumu. Wakasema: Walikuwa na mazao? Akasema: Hatukuwa tukiwauliza swala hilo.”[6] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
721.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ أَخَذَ أَمْوَالَ اَلنَّاسِ يُرِيدُ أَدَاءَهَا، أَدَّى اَللَّهُ عَنْهُ، وَمَنْ أَخَذَهَا يُرِيدُ إِتْلَافَهَا، أَتْلَفَهُ اَللَّهُ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuchukua mali ya watu anakusudia kuilipa, Allaah atamuwezesha kulipa. Na mwenye kuichukua kwa niyyah ya kuiharibu Allaah Atamuangamiza.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
722.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {قُلْتُ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ ! إِنَّ فُلَاناً قَدِمَ لَهُ بَزٌّ مِنَ اَلشَّامِ، فَلَوْ بَعَثْتَ إِلَيْهِ، فَأَخَذْتَ مِنْهُ ثَوْبَيْنِ بِنَسِيئَةٍ إِلَى مَيْسَرَةٍ؟ فَأَرْسَلَ إِلَيْهِ، فَامْتَنَعَ} أَخْرَجَهُ اَلْحَاكِمُ، وَالْبَيْهَقِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Nilisema: Ee Rasuli wa Allaah! Fulani amekuja na nguo kutoka Sham, waonaje lau ungelimtuma mtu ukachukua kwake nguo mbili kwa mkopo[7] hadi utakapopata? Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamtuma mtu, yule (muuzaji) akakataa.” [Imetolewa na Al-Haakim na Al-Bayhaqiyy. Wapokezi wake ni madhubuti]
723.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلظَّهْرُ يُرْكَبُ بِنَفَقَتِهِ إِذَا كَانَ مَرْهُونًا، وَلَبَنُ اَلدَّرِّ يُشْرَبُ بِنَفَقَتِهِ إِذَا كَانَ مَرْهُونًا، وَعَلَى اَلَّذِي يَرْكَبُ وَيَشْرَبُ اَلنَّفَقَةُ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mnyama anapandwa kwa matumizi yake[8] kama mnyama amewekwa rahani[9] na maziwa yatanywewa kwa matumizi yake ikiwa amewekwa rahani, na anayepanda na kukamua ni juu yake matumizi.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
724.
وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: {لَا يَغْلَقُ اَلرَّهْنُ مِنْ صَاحِبِهِ اَلَّذِي رَهَنَهُ، لَهُ غُنْمُهُ، وَعَلَيْهِ غُرْمُهُ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَالْحَاكِمُ، وَرِجَالهُ ثِقَاتٌ. إِلَّا أَنَّ اَلْمَحْفُوظَ عِنْدَ أَبِي دَاوُدَ وَغَيْرِهِ إِرْسَالُهُ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Rahani haitoki kwenye umiliki wa mwenyewe aliyeweka rahani, nyongeza yake ni yake, matumizi yake ni juu yake.”[10] [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy na Al-Haakim. Wapokezi wake ni waaminifu (madhubuti)
725.
وَعَنْ أَبِي رَافِعٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اسْتَسْلَفَ مِنْ رَجُلٍ بَكْرًا فَقَدِمَتْ عَلَيْهِ إِبِلٌ مِنَ اَلصَّدَقَةِ، فَأَمَرَ أَبَا رَافِعٍ أَنْ يَقْضِيَ اَلرَّجُلَ بَكْرَهُ، فَقَالَ: لَا أَجِدُ إِلَّا خَيَارًا قَالَ: " أَعْطِهِ إِيَّاهُ، فَإِنَّ خِيَارَ اَلنَّاسِ أَحْسَنُهُمْ قَضَاءً} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Raafi’ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikopesha ndama wa ngamia kwa mtu. (Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaletewa ngamia wa Swadaqah. Akamuamuru Abuu Raafi’ kumlipa yule ngamia wake. (Abuu Raafi’) akasema: Sina isipokuwa ngamia bora mwenye miaka saba. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Mpe huyo kwani ni mbora wao wa kulipa.”[11] [Imetolewa na Muslim]
726.
وَعَنْ عَلِيٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ {كُلُّ قَرْضٍ جَرَّ مَنْفَعَةً، فَهُوَ رِبًا} رَوَاهُ اَلْحَارِثُ بْنُ أَبِي أُسَامَةَ، وَإِسْنَادُهُ سَاقِطٌ.
وَلَهُ شَاهِدٌ ضَعِيفٌ عَنْ فَضَالَةَ بْنِ عُبَيْدٍ عِنْدَ اَلْبَيْهَقِيِّ
وَآخَرُ مَوْقُوفٌ عَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ سَلَامٍ عِنْدَ اَلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kila mkopo unaoleta manufaa hiyo ni ribaa.” [Imetolewa na Al-Haarith bin Abuu Usaamah na katika Isnaad yake kuna mtu ameachwa.
Al-Bayhaqiyy amepokea kama ni ushahidi mwingine ingawaje ni Hadiyth dhaifu kutoka kwa Fadhwaalah bin ‘Ubayd.
Al-Bukhaariy ameipokea ikiwa ni Mawquwf kutoka kwa ‘Abdullaah bin Salaam.
[1] Salam ina maana ya kununua kitakachozalishwa kwa malipo ya kabla. Kwa mfano mtu anampa mtu mwingine fedha na kumuambia kuwa atampa kitu chenyewe muda fulani kwa bei kadhaa. Hili linaruhusiwa maadamu kuwa bei na thamani yake imekubaliwa hapo kabla. Kwa lugha nyingine inaitwa Salaf.
[2] Kukopesha kwa kiarabu imeitwa Qardhw, ambapo maana yake ni kukata kitu. Mtu anayemkopesha mwenziwe pesa huwa anakata katika zile pesa zake na kumpatia yule anayemkopesha. Katika shariy’ah kukopesha (Qardhw) ni kumpa mtu pesa ambazo zitamsaidia, na mtu huyo anatakiwa kulipa kiwango kile kile alichopewa hapo awali bila ya nyongeza yoyote.
[3] ‘Abdul-Rahmaan bin Abzaa Al-Khuzaa’iy, ni muachwa huru wa Banuw Khuzaa’ alikuwa ni Swahaba mdogo kwa umri ambaye aliwahi kuswali nyuma ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Aliishi Al-Kufah (‘Iraaq), na ‘Aliy bin Abiy Twaalib alimfanya kuwa gavana wa Khurasaan. Alifariki Kufa.
[4] Anbaatw ni warabu waliohamia katika miji wa Waajemi na Warumi wakachanganyikana nao.
[5] Shayiri: nafaka inayofanana na ngano inayotumika kuwa chakula.
[6] Hadiyth hii inajuzisha Bayi’ As-Salam hata kama mazao hayakuwepo wakati wa mauzo. Cha msingi ni kuwa mazao yawe tayari kwa wakati ule.
[7] Ina maana kuwa kununua kitu kwa mkopo inaruhusiwa. Muuza nguo alikuwa ni Yahudi na alikuwa na uadui na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), na ndio maana alikataa.
[8] Ina maana ikiwa mtu ameweka rahani farasi au ng’ombe wake kwa mkopo aliochukua. Kuna tafsiri ya aina mbili: Ima mkopeshaji atamlisha farasi au ng’ombe na akafaidika nao au mkopaji atamlisha farasi au ng’ombe akafaidika nao. Yeyote atakayewalisha ndio anayestahiki maslahi yao. Hadiyth hii inathibitisha muono wa pili.
[9] Kulingana na Shariy’ah, rahani ni kutoa aina ya miliki au kitu cha anayekopa kama dhamana ya mkopo anaouchukua.
[10] Hii ina maana aliyepewa dhamana si mmiliki wa rahani iliyo kwake. Anaidhibiti tu. Ikiwa rahani imeharibika au kufa, aliyepewa dhamana hana majukumu ya kulipa. Vivyo hivyo kama kutakuwa na ziada ya rahani iliyoongezeka hatokuwa mmiliki wake. Hasara na faida, vyovyote ilivyo inakwenda kwa mmiliki na sio kwa aliyewekewa rahani. Hali hii imebatilisha hali ya kijahiliya ya hapo kabla. Waarabu hapo zamani walikuwa wakiwekeana rahani, yule muweka rahani anaposhindwa kulipa kile kitu chake kinachukuliwa na yule ambaye rahani iko kwake. Iwapo kilichowekwa rahani ni kitu kama matunda au mtoto, basi yule aliyeweka rahani ndiye anayelazimika kusimamia matumizi ya alichoweka rahani ili kiendelee kuishi.
[11] Ikiwa mdaiwa ametoa faida aliyoipata pamoja na ile fedha aliyokopa si vibaya ni halali kwa mkopeshaji kuchukua. Ama ikiwa mkopeshaji ameweka sharti mkopo urejeshwe na ziada inachukuliwa kama ribaa nayo ni haraam. Kurudisha kilichokua kizuri inaruhusiwa na ni halali kwa mkopeshaji lakini ikilazimishwa kurejesha ziada pamoja na mali aliyokopa ni ribaa na ni haraam. Hadiyth hii yaonesha tabia njema na huwa haihesabiwi kuwa ni mkopo wenye nyongeza, kwa sababu wakati wa kutolewa haukuwa umewekewa sharti. Ni mwenyewe aliyekopa kwa furaha yake anamtunukia zawadi mkopeshaji.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلتَّفْلِيسِ وَالْحَجْرِ
06-Mlango Wa Kufilisiwa Na Kuzuwia (Kutumia Mali)
727.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {مَنْ أَدْرَكَ مَالَهُ بِعَيْنِهِ عِنْدَ رَجُلٍ قَدْ أَفْلَسَ، فَهُوَ أَحَقُّ بِهِ مِنْ غَيْرِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَرَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَمَالِكٌ: مِنْ رِوَايَةِ أَبِي بَكْرِ بْنِ عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ مُرْسَلًا بِلَفْظِ: {أَيُّمَا رَجُلٌ بَاعَ مَتَاعًا فَأَفْلَسَ اَلَّذِي اِبْتَاعَهُ، وَلَمْ يَقْبِضِ اَلَّذِي بَاعَهُ مِنْ ثَمَنِهِ شَيْئًا ، فَوَجَدَ مَتَاعَهُ بِعَيْنِهِ، فَهُوَ أَحَقُّ بِهِ، وَإِنْ مَاتَ اَلْمُشْتَرِي فَصَاحِبُ اَلْمَتَاعِ أُسْوَةُ اَلْغُرَمَاءِ} وَوَصَلَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ، وَضَعَّفَهُ تَبَعًا لِأَبِي دَاوُدَ
وَرَوَى أَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَهْ: مِنْ رِوَايَةِ عُمَرَ بْنِ خَلْدَةَ قَالَ: أَتَيْنَا أَبَا هُرَيْرَةَ فِي صَاحِبٍ لَنَا قَدْ أَفْلَسَ، فَقَالَ: لَأَقْضِيَنَّ فِيكُمْ بِقَضَاءِ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ أَفْلَسَ أَوْ مَاتَ فَوَجَدَ رَجُلٌ مَتَاعَهُ بِعَيْنِهِ فَهُوَ أَحَقُّ بِهِ} وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَضَعَّفَ أَبُو دَاوُدَ هَذِهِ اَلزِّيَادَةَ فِي ذِكْرِ اَلْمَوْتِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Tulimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Atakayekuta mali yake ile ile kwa mtu aliefilisika, basi yeye ana haki zaidi[1] kuliko mwingine.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Abuu Daawuwd na Maalik wameipokea kwa Riwaayah ya Abuu Bakr bin ‘Abdir-Rahmaan[2][3] ikiwa ni Mursal kwa tamshi: “Yeyote mwenye kuuza bidhaa mwenye kuinunua akafilisika wala hakumlipa chochote katika thamani yake akaikuta bidhaa yake ile ile kama ilivyo, basi yeye ana haki zaidi kuichukua. Mnunuzi akifa, mwenye bidhaa akakuta mali yake kwake ana haki zaidi ya kuichukua.”[4] [Al-Bayhaqiyy ameidhoofisha akifuata Abuu Daawuwd]
Abuu Daawuwd na Ibn Maajah wameipokea kutoka katika Riwaayah ya ‘Umar bin Khaldah[5] amesema: Tulimuendea Abuu Hurayrah tukiwa na sahibu yetu aliyefilisika, akasema kwa hakika nitawahukumu kwa hukumu ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kufilisika au akafa, mtu akakuta mali yake ile ile basi yeye ana haki zaidi kwa mali hiyo.”[6] Ameisahihisha Al-Haakim. Abuu Daawuwd ameidhoofisha vile akaidhoofisha ziada hii inayoeleza kifo.
728.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ اَلشَّرِيدِ، عَنْ أَبِيهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَيُّ اَلْوَاجِدِ يُحِلُّ عِرْضَهُ وَعُقُوبَتَهُ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَعَلَّقَهُ اَلْبُخَارِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa ‘Amr bin Ash-Shariyd[7] kutoka kwa baba yake[8] amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Tajiri kuzuia haki inayofaa kutolewa inamhalalishia kuharibiwa jina na kuadhibiwa[9].”[10] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaai na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
729.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {أُصِيبَ رَجُلٌ فِي عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي ثِمَارٍ اِبْتَاعَهَا، فَكَثُرَ دَيْنُهُ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " تَصَدَّقُوا عَلَيْهِ" فَتَصَدَّقَ اَلنَّاسُ عَلَيْهِ، وَلَمْ يَبْلُغْ ذَلِكَ وَفَاءَ دَيْنِهِ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ لِغُرَمَائِهِ: " خُذُوا مَا وَجَدْتُمْ، وَلَيْسَ لَكُمْ إِلَّا ذَلِكَ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Mtu mmoja katika zama za Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipata hasara katika matunda aliyonunua, deni lake likazidi, akafilisika. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Mpeni Swadaqah, haikufikia kiasi cha kulipa deni analodaiwa. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akawaambia wanaomdai: “Chukueni mlichopata, hamna isipokuwa hicho tu.”[11] [Imetolewa na Muslim]
730.
وَعَنِ اِبْنِ كَعْبِ بْنِ مَالِكٍ، عَنْ أَبِيهِ، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ حَجَرَ عَلَى مُعَاذٍ مَالَهُ، وَبَاعَهُ فِي دَيْنٍ كَانَ عَلَيْهِ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَأَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ مُرْسَلًا، وَرُجِّحَ
Kutoka kwa Ibn Ka’b bin Maalik[12] amehadithia kutoka kwa baba yake[13] kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alizuia mali ya Mu’aadh akaiuza kulipa deni analodaiwa.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy, na akaisahihisha Al-Haakim. Abuu Daawuwd ameipokea ikiwa ni Mursal na kuipa nguvu]
731.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {عُرِضْتُ عَلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَوْمَ أُحُدٍ، وَأَنَا اِبْنُ أَرْبَعَ عَشْرَةَ سَنَةً، فَلَمْ يُجِزْنِي، وَعُرِضْتُ عَلَيْهِ يَوْمَ اَلْخَنْدَقِ، وَأَنَا اِبْنُ خَمْسَ عَشْرَةَ سَنَةً، فَأَجَازَنِي} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ لِلْبَيْهَقِيِّ: "فَلَمْ يُجِزْنِي، وَلَمْ يَرَنِي بَلَغْتُ". وَصَحَّحَهَا اِبْنُ خُزَيْمَةَ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Nilipitishwa kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) siku ya vita vya Uhud[14] nami ni mvulana wa umri wa miaka kumi na nne hakuniidhinisha. Nikapitishwa kwake siku ya vita vya Khandaq nami ni mvulana wa miaka kumi na tano akaniidhinisha.”[15] [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah nyingine ya Al-Bayhaqiyy: “…hakuniidhinisha wala hakuniona kuwa nimebaleghe.” Ameisahihisha Ibn Khuzaymah
732.
وَعَنْ عَطِيَّةَ اَلْقُرَظِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {عُرِضْنَا عَلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَوْمَ قُرَيْظَةَ، فَكَانَ مَنْ أَنْبَتَ قُتِلَ، وَمَنْ لَمْ يُنْبِتْ خُلِّيَ سَبِيلُهُ، فَكُنْتُ فِيمَنْ لَمْ يُنْبِتْ فَخُلِّيَ سَبِيلِي} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Atwiyyah Al-Quradhwiyy[16] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Tulipitishwa kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) siku ya vita vya Quraydhwa, anauwawa aliyeota nywele (za kinena) na ambaye hajaota nywele anaachwa, mimi nilikuwa miongoni mwa ambao hawakuota nywele akaniacha.”[17] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
733.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَجُوزُ لِاِمْرَأَةٍ عَطِيَّةٌ إِلَّا بِإِذْنِ زَوْجِهَا}
وَفِي لَفْظٍ:{لَا يَجُوزُ لِلْمَرْأَةِ أَمْرٌ فِي مَالِهَا، إِذَا مَلَكَ زَوْجُهَا عِصْمَتَهَا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَصْحَابُ اَلسُّنَنِ إِلَّا اَلتِّرْمِذِيَّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb amepokea kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Haifai mwanamke kutoa kitu isipokuwa kwa idhini ya mumewe.”
Katika tamshi lingine: “Haifai mwanamke kufanya lolote katika mali yake[18] endapo mumewe amemiliki hifadhi yake.”[19] [Imetolewa na Ahmad na Maimaam wa Sunan[20] isipokuwa At-Tirmidhiy, na akaisahihisha Al-Haakim]
734.
وَعَنْ قَبِيصَةَ بْنِ مُخَارِقٍ اَلْهِلَالِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِنَّ اَلْمَسْأَلَةَ لَا تَحِلُّ إِلَّا لِأَحَدِ ثَلَاثَةٍ: رَجُلٍ تَحَمَّلَ حَمَالَةً فَحَلَّتْ لَهُ اَلْمَسْأَلَةُ حَتَّى يُصِيبَهَا ثُمَّ يُمْسِكَ، وَرَجُلٍ أَصَابَتْهُ جَائِحَةٌ اِجْتَاحَتْ مَالَهُ، فَحَلَّتْ لَهُ اَلْمَسْأَلَةُ حَتَّى يُصِيبَ قِوَامًا مِنْ عَيْشٍ، وَرَجُلٍ أَصَابَتْهُ فَاقَةٌ حَتَّى يَقُولَ ثَلَاثَةٌ مِنْ ذَوِي الْحِجَى مِنْ قَوْمِهِ: لَقَدْ أَصَابَتْ فُلَانًا فَاقَةٌ، فَحَلَّتْ لَهُ اَلْمَسْأَلَةُ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Qabiyswah bin Mukhaariq Al-Hilaaliyy[21] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika kuomba si halali kwa yeyote ila kwa moja ya mambo matatu: mtu aliyechukua dhamana, hapo ni halali kwake kuomba mpaka apate kisha atajizuia, mtu iliyoangamia mali yake, ni halali kwake kuomba mpaka apate msimamo wa maisha, na mtu aliyepata na uhitaji kwa umaskini hadi watu watatu wenye busara katika jamaa zake waseme: Hakika fulani amepata umaskini. Ni halali kwake kuomba.”[22] [Imetolewa na Muslim]
[1] Hii ina maana kuwa muuzaji anaweza kuvunja mkataba na mnunuzi na kuchukuwa mali yake ikiwa mnunuzi amefilisika.
[2] Huyu ni Abuu Bakr bin ‘Abdir-Rahmaan bin Al-Haarith bin Al-Mughiyrah Al-Makhzuwm Al-Madaniy, alikuwa ni kadhi wa Madiynah. Inasemekana kuwa jina lake lilikuwa Muhammad Al-Mughiyrah au Abuu Bakr, kun-ya yake ilikuwa ni Abuu Abdir-Rahmaan. Inasemwa hali kadhalika kuwa jina lake na kun-ya yake ilikuwa sawa. Alikuwa mtu madhubuti, Mwanazuoni na mwenye taqwa. Alikuwa ni Taabi’i wa kizazi cha tatu alifariki katika ukhalifa wa Al-Waliyd bin ‘Abdil Maalik.
[3] Abuu Bakr bin ‘Abdir-Rahmaan bin Al-Haarith Al-Makhzuwm Al-Madani. Ni madhubuti, faqihi, mfanya ‘ibaadah. Alifariki mwaka wa 94 Hijriyyah.
[4] Yaani atachukua kama wale wengine wanavyochukua kulingana na mafungu yao.
[5] Huyu ni Abuu Hafsi Al-Answaar Al-Madaniy Al-Qaadhwi. Alikuwa ni mtu mwenye heshima kubwa, mkali, mwenye taqwa na mtu mwenye kutegemewa. Amepokea kutoka kwa Abuu Hurayrah na Rabiy’a Ar-Raay amepokea kutoka kwake. Inasemekana kuwa Khaldah alikuwa ni babu yake na jina la babake lilikuwa ni ‘Abdur-Rahmaan.
[6] Ikiwa mnunuzi atafilisika baada ya kulipa kiwango cha fedha, muuzaji hana haki ya mali yote. Atachukua hisa ya mali yake tu. Mdaiwa akifa watapewa mali zao bila kujali ni mali ya nani iliyouzwa na ya nani haikuuzwa.
[7] Huyu ni Abul-Waliyd ‘Amr bin Ash-Shariyd bin Suwayd At-Thaqaaf At-Twaaif. Ni madhubuti. Abuu Ash-Shariyd ni Swahaba aliyehudhuria Bay’at Ar-Ridhwaan. Alikuwa ni Taabi’i wa kizazi cha tatu.
[8] Huyu ni Shariyd Suwayd Ath-Thaqaaf. Jina lake ni Maalik, lakini Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akampa jina Shariyd (aliyetoroka) baada ya kuwa mmoja wa watu wa ukoo wake, alikimbia hadi Makkah na akasilimu. Inasemekana asili yake ni kutoka Hadhramout, ila alijulikana ni wa ukoo wa Banuu Thaqif yaani watu wa Twaaif.
[9] Ikiwa mdaiwa ana uwezo wa kulipa deni kisha asilipe kwa makusudi, kwa hali hiyo mkopeshaji ana haki ya kumfedhehesha kwa kumkashifu mbele ya kadamnasi na kisha kumfungulia mashtaka.
[10] Kumkashifu ni kusema: “Fulani amezuwia haki yangu.” Na kumuadhibu ni kumfunga.
[11] Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) anakusudia kuwa hizi ni zote zilizokuwepo. Hivyo, aliwataka wadai kugawa alichomiliki sawa kwa sawa.
[12] Abuu Al-Khatwaab ‘Abdir-Rahmaan bin Ka’b bin Maalik Al-Answaar Al-Madaniy, alikuwa madhubuti na ni miongoni mwa taabi’iyna wakubwa. Inasemekana alizaliwa wakati wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na alikuwa wakati wa Khalifa Sulaymaan bin ‘Abdil-Maalik.
[13] Ka’b bin Maalik bin Abuu Ka’b Al-Answaar As-Sulami Al-Madaniy mshairi, alikuwa ni mmoja wa washairi wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Alihudhuria Bay’atul ‘Aqaba ya pili na vita vyote isipokuwa Badr na Tabuwk. Alikuwa mmoja miongoni mwa watatu ambao toba yao ilitajwa katika Suwrat At-Tawbah kwa kubaki Madiynah wakati wa vita vya Tabuwk. Inasemekana kuwa alikufa baada ya kupofuka mwaka 50 au 51 Hijriyyah akiwa na umri wa miaka 77.
[14] Siku ya Uhud alikuenda kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuomba ruhusa kupigana katika vita vya Uhud dhidi ya makafiri wa Makkah.
[15] Sababu ya Hadiyth hii kuwekwa hapa ni kuonesha kuwa umri wa kukalifishwa mambo ni umri wa miaka 15 na maamrisho yote ya kishariy’ah yanakuwa wajibu wakati huo. Hivyo basi ambaye hajafikia umri huu muamala wake haukubaliki kama vile kuuza, kununua n.k. isipokuwa kwa ridhaa ya wazazi wake au aliyeteuliwa kuwa msimamizi wake atazuiwa yote hayo mpaka atakapo baleghe. Vivyo hivyo jambo linguine linalotibitisha kukua kwake na kuwajibika ni kuota kwa nywele za kinenani.
[16] ‘Atwiyyah Al-Quradhwiyy ni Swahaba mdogo aliyeripoti Hadiyth moja tu. Huyu ni kutoka katika kabila la Baniy Quraydhwa. Yasemekana kuwa aliishi Al-Kufah (‘Iraaq). Ibnu ‘Abdil-Barr amesema sikuweza kujua jina la baba yake. Mujaahid na wengineo wamepokea kutoka kwake.
[17] Hadiyth hii ni dalili kuwa anayemea nywele za sehemu ya siri huwa amebaleghe, yaani huchukuliwa kuwa ni mtu mzima anapitishwa hukmu zote.
[18] Mwanamke ana haki zote na mali zake bila ya ruhusa ya mumewe. Mali yake ni nini? Mahari yake, alichorithi, faida za biashara zake anazofanya mwenyewe, hizi ni mali za mke na mume hana mamlaka ya aina yoyote ile kwa mali hii. Mwanamke anaweza kumpa mumewe chochote anachotaka kumpa, na ni halali kwa mumewe. Kisa cha ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) na mkewe kimetajwa huko nyuma, jambo hili lisingetokea kama mke hana haki katika mali yake.
[19] Al-Khattabi amesema: “Hadiyth hii inahimiza uhusiano bora baina ya mtu na mkewe au kwa mke ambaye akili yake haijakaa sawa, kwani imethubutu kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliwaambia wanawake: Toeni Swadaqah na wanawake wakatoa vipuli, mikufu n.k.”
[20] Yaani walioandika vitabu vya Sunan nao ni : At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, An-Nasaai na Ibn Maajah. Vitabu vyao ni Sunan At-Tirmidhiy, Sunan Abiy Daawuwd, Sunan An-Nasaai na Sunan Ibn Maajah.
[21] Qabiyswah bin Mukhaariq bin ‘Abdillaah bin Shaddaads Al-‘Amiri. Ni Swahaba. Alimtembelea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasilimu. Katika vitabu vya Hadiyth, ana Hadiyth sita. Aliishi Al-Basra (‘Iraaq).
[22] Hadiyth ikamalizikia hivi: “Kuomba kusiko tokana na sababu hizo ni haraam ee Qabiyswa, anayekula anakula haraam.”
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلصُّلْحِ
07-Mlango wa Suluhu[1]
735.
عَنْ عَمْرِو بْنِ عَوْفٍ اَلْمُزَنِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {اَلصُّلْحُ جَائِزٌ بَيْنَ اَلْمُسْلِمِينَ، إِلَّا صُلْحاً حَرَّمَ حَلَالاً وَ أَحَلَّ حَرَاماً، وَالْمُسْلِمُونَ عَلَى شُرُوطِهِمْ، إِلَّا شَرْطاً حَرَّمَ حَلَالاً وَ أَحَلَّ حَرَاماً} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ
وَأَنْكَرُوا عَلَيْهِ. لِأَنَّ رَاوِيَهُ كَثِيرَ بْنَ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرِوِ بْنِ عَوْفٍ ضَعِيفٌ. وَكَأَنَّهُ اِعْتَبَرَهُ بِكَثْرَةِ طُرُقِهِ
وَقَدْ صَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ مِنْ حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَةَ
Kutoka kwa ‘Amr bin ‘Awf Al-Muzaniyy[2] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Suluhu[3] inafaa baina ya Waislamu isipokuwa suluhu inayoharamisha halaal[4] au inayohalalisha haraam.[5] Waislamu wako juu ya masharti yao isipokuwa sharti inayoharamisha halaal au inayohalalisha haraam.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akaisahihisha]
Ulamaa wameikataa Hadiyth hii kwa sababu mpokezi wake ni Kathiyr bin ‘Abdillaah bin ‘Amr bin ‘Awf ni dhaifu.[6]
Ibn Hibbaan ameisahihisha kutoka katika Hadiyth iliyopokewa na Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ).
736.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَمْنَعُ جَارٌ جَارَهُ أَنْ يَغْرِزَ خَشَبَةً فِي جِدَارِهِ. ثُمَّ يَقُولُ أَبُو هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ مَا لِي أَرَاكُمْ عَنْهَا مُعْرِضِينَ؟ وَاَللَّهِ لَأَرْمِيَنَّ بِهَا بَيْنَ أَكْتَافِكُمْ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Jirani asimkataze jirani yake kusimamisha mbao katika ukuta wake.”[7] Kisha Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alikuwa akisema: “Mbona nawaona mumeiacha Sunnah hii? Wa-Allaahi mtaibeba baina ya mabega yenu (hata mkichukia)” [Al-Bukhaariy, Muslim]
737.
وَعَنْ أَبِي حُمَيْدٍ اَلسَّاعِدِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَحِلُّ لِامْرِئٍ أَنْ يَأْخُذَ عَصَا أَخِيهِ بِغَيْرِ طِيبِ نَفْسٍ مِنْهُ} رَوَاهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ فِي "صَحِيحَيْهِمَا"
Kutoka kwa Abuu Humayd As-Saa’idiyy[8] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halaal kwa mtu kuchukua fimbo ya nduguye bila ya nafsi yake kuridhia.”[9] [Imetolewa na Ibn Hibbaan na Al-Haakim katika Swahiyh zao]
[1] Suluhu ni kuweka muafaka baina ya watesi wawili, kama vile mtu kudai haki ya mwengine kwa kuamini kuwa yeye ndiye mwenye haki kuliko mwingine.
[2] Huyu ni ‘Abdullaah ‘Amr bin ‘Awf bin Zayd bin Milha Al-Muzaniyy (kutoka katika kabila la Muzaynah), ni babu wa Kathiyr bin ‘Abdillaah. Alisilimu mapema, alihuduria Badr na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimpa mamlaka ya kusimamia Msikiti wa Madiynah. Alikuwa ni mwenye taqwa na mwenye kububujikwa na machozi katika ‘Ibaadah. Ni Swahaba, alifariki katika utawala wa Mu’aawiyah.
[3] Katika lugha ya kiarabu Sulhu ina maana ya amani. Kuna aina nyingi za suluhu kama vile suluhu baina ya Waislamu na wasiokuwa Waislamu, suluhu baina ya mke na mume, suluhu baina ya serikali na waasi, magomvi ya kibiashara na suluhu za mambo ya fedha. Katika Hadiyth hii inakusudiwa aina hii ya mwisho ya suluhu. Migogoro ya kifedha ina mikataba ambayo ni halaal na kuna isiyokuwa halaal na masharti ya mikataba yenyewe.
[4] Msingi wa mwanzo muhimu wa mkataba ni kuwa isiwe kinyume na shariy’ah na isibadilishe haraam kuwa halaal na halaal kuwa haraam. Kama vile kusuluhisha juu ya kuchukua mali isiyo halali kwake.
[5] Kama vile kumtaka mume asilale kwa mke wa pili.
[6] Ash-Shaafi na Abuu Daawuwd wamemtaja kuwa ni “Msingi wa uongo”. Ahmad amesema: “Hadiyth zake ni Munkar.” An-Nasaaiy naye amemzungumzia kwa kusema: “Haaminiki” na Ibn Hibbaan amesema: “Ana kitabu cha Hadiyth alichokitunga akisingizia kuwa amepokea kutoka kwa baba yake nae kutoka kwa babu yake.”
[7] Shariy’ah imejali maingiliano ya kijamii na kuiwekea miongozo kama hili la jirani kuweka mbao kuegemea ukuta wa jirani yake.
[8] Huyu ni Abuu Humayd As-Saa’idiyy. Jina lake ni Al-Mundhir bin Sa’d. alihudhuria vita vya Uhud na vilivyofuatia baada yake, aliishi hadi mwaka wa 60 Hijriyyah.
[9] Hadiyth hii ni dalili kuwa ni haraam kuchukua mali ya Muislamu hata ikiwa ni kidogo kiasi gani ila kwa radhi yake.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ الْحَوَالَةِ وَالضَّمَانِ
08-Mlango Wa Hawala[1] Na Dhamana[2]
738.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَطْلُ اَلْغَنِيِّ ظُلْمٌ، وَإِذَا أُتْبِعُ أَحَدُكُمْ عَلَى مَلِيٍّ فَلْيَتْبَعْ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةِ أَحْمَدَ: {فَلْيَحْتَلْ}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kuchelewesha tajiri (kulipa deni) ni dhulma. Na mmoja wenu atakapofuatishwa kwa mwenye uwezo na afuate.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
739.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {تُوُفِّيَ رَجُلٌ مِنَّا، فَغَسَّلْنَاهُ، وَحَنَّطْنَاهُ، وَكَفَّنَّاهُ، ثُمَّ أَتَيْنَا بِهِ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقُلْنَا: تُصَلِّي عَلَيْهِ ؟ فَخَطَا خُطًى، ثُمَّ قَالَ: " أَعَلَيْهِ دَيْنٌ ؟ " قُلْنَا: دِينَارَانِ، فَانْصَرَفَ، فَتَحَمَّلَهُمَا أَبُو قَتَادَةَ، فَأَتَيْنَاهُ، فَقَالَ أَبُو قَتَادَةَ: اَلدِّينَارَانِ عَلَيَّ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "أُحِقَّ اَلْغَرِيمُ وَبَرِئَ مِنْهُمَا اَلْمَيِّتُ؟ " قَالَ: نَعَمْ، فَصَلَّى عَلَيْهِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Alikufa mtu miongoni mwetu, tukamuosha, tukamtia dawa na tukamkafini, kisha tukamuendea Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) tukamuambia: Utamswalia? Akaenda hatua chache akasema: Ana deni? Tukasema: Ana deni la dinari mbili. Akaondoka. Abuu Qataadah akabeba deni lile (akalidhamini) tukamuendea Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), Abuu Qataadah akamuambia: zile dinari mbili juu yangu. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Haki ya mdai (kulipwa) na je maiti ameepukana nayo? Akasema ndio. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamswalia.”[3] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy, na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
740.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كَانَ يُؤْتَى بِالرَّجُلِ اَلْمُتَوَفَّى عَلَيْهِ اَلدَّيْنُ، فَيَسْأَلُ: "هَلْ تَرَكَ لِدَيْنِهِ مِنْ قَضَاءٍ ؟ " فَإِنْ حُدِّثَ أَنَّهُ تَرَكَ وَفَاءً صَلَّى عَلَيْهِ، وَإِلَّا قَالَ: "صَلُّوا عَلَى صَاحِبِكُمْ " فَلَمَّا فَتَحَ اَللَّهُ عَلَيْهِ اَلْفُتُوحَ قَالَ: " أَنَا أَوْلَى بِالْمُؤْمِنِينَ مِنْ أَنْفُسِهِمْ، فَمَنْ تُوُفِّيَ، وَعَلَيْهِ دَيْنٌ فَعَلَيَّ قَضَاؤُهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ لِلْبُخَارِيِّ:{فَمَنْ مَاتَ وَلَمْ يَتْرُكْ وَفَاءً}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa analetewa mtu aliyekufa anayedaiwa Anauliza: Ameacha cha kulipa deni lake? Akiambiwa kuwa ameacha[4] humswalia, la si hivyo alikuwa akisema Mswalieni Swahibu yenu. Allaah alipomfungulia alikuwa akisema: Mimi ni aula kwa Waumini kuliko nafsi zao, atakayekufa ilhali anadaiwa basi ni juu yangu kulipa deni lake.”[5] [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Bukhaariy: “Atakayekufa na hakuacha cha kulipia deni lake…”
741.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا كَفَالَةَ فِي حَدٍّ} رَوَاهُ اَلْبَيْهَقِيُّ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna udhamini katika hadd (adhabu).”[6] [Imetolewa na Al-Bayhaqiyy kwa Isnaad dhaifu]
[1] Hawala ina maana mbili: Ya kwanza ni mtu kumhakikishia tajiri kuwa deni lake litarudi. Hii inaruhusiwa kishariy’ah. Ya pili ni kuhamisha deni kutoka katika dhima ya mmoja hadi kwa mwingine.
[2] Dhamana ni kujitwika deni la mwenye kudaiwa.
[3] Ina maana kuwa deni au haki yoyote ya mwanadamu, haitosamehewa mpaka lilipwe au lisamehewe na mhusika. Hata baada ya kifo chake deni bado linasimama pale pale. Kadhalika tunajifunza katika Hadiyth hii mtu kumdhamini deni la maiti hata kama si jamaa yake.
[4] Yaani ameacha mali ya kutosha.
[5] Ni juu yangu kulilipa haikuwa na maana mali yake binafsi Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Wakati huo hazina ya dola ilikuwa chini ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ndio maana akasema: “Ni juu yangu kumlipia.” Jukumu hili lilikuja kuhamia kwa mkuu wa nchi kama Hadiyth nyingine itakayokuja kufafanua. Hadiyth hii imefuta Hadiyth iliyotangulia. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokuwa hana uwezo alikuwa hamswalii maiti anayedaiwa kwa sababu Swalaah yake ni Shafaa (maombezi) inayokubaliwa moja kwa moja. Lakini alipopata uwezo jukumu la madeni lilikuwa juu yake. Na katika utawala wa Kiislamu kiongozi anawajibika kumlipia maiti deni lake, asipofanya hivyo dhambi ni zake.
[6] Huduwd: adhabu iliyowekwa na Shariy’ah katika Uislam. Hakuna dhamana katika huduwd. Kwa mfano, hakutakiwi kuwepo na dhamana kwa wizi, uzinzi, kumkashifu mtu na ulevi. Kuna sababu nyingi kwa nini hairuhusiwi dhamana kwa makosa haya:
i. kimsingi dhamana hutumika kutilia nguvu ushahidi, wakati katika utekelezaji wa huduwd, jambo la msingi ni kuwepo kwa ushahidi dhidi ya mtuhumiwa inadhoofishwa na mashtaka yaende kwa mtuhumiwa.
ii. Dhamana huchelewesha maamuzi, na hakuna hakika kuwa mtuhumiwa atathibitika katika utuhumiwa wake na ataadhibiwa. Ikiwa tuhuma itathibitika, hivyo basi hakuna haja ya maombi ya msamaha wa huduwd.
iii. Mdhamini anatakiwa amlete mdhaminiwa kwenye hukumu mahakamani; kutokuwepo kwa mtuhumiwa majukumu yake atabebeshwa mdhamini. Hata hivyo adhabu za huduwd zinatekelezwa kwa mhalifu na sio kwa mtu mwingine yeyote. Hadiyth hii ingawa Isnaad yake ni dhaifu lakini maana yake ni sahihi kwa ‘Ulamaa. Iwapo kutakuwepo na udhamini katika adhabu anayopewa mtu bila shaka shariy’ah za adhabu zitabatilika.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلشَّرِكَةِ وَالْوَكَالَةِ
09-Mlango Wa Ushirika[1] Na Uwakala[2]
742.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {قَالَ اَللَّهُ: أَنَا ثَالِثُ اَلشَّرِيكَيْنِ مَا لَمْ يَخُنْ أَحَدُهُمَا صَاحِبَهُ، فَإِذَا خَانَ خَرَجْتُ مِنْ بَيْنِهِمَا} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Allaah amesema: Mimi ni wa Tatu wa washirika wawili madamu mmoja wao hajakhini mwenzake, atakapomkhini Nitatoka baina yao.”[3] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Al-Haakim]
743.
وَعَنْ اَلسَّائِبِ بْنِ يَزِيدَ اَلْمَخْزُومِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّهُ كَانَ شَرِيكَ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَبْلَ اَلْبَعْثَةِ، فَجَاءَ يَوْمَ اَلْفَتْحِ، فَقَالَ: " مَرْحَباً بِأَخِي وَشَرِيكِي} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَةَ
Kutoka kwa As-Saaib bin Yaziyda Al-Makhzuwmiyy[4] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Yeye alikuwa ni mshirika wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kabla ya Unabii akamuambia: karibu ndugu yangu na mshirika wangu.”[5] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na Ibn Maajah]
744.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {اِشْتَرَكْتُ أَنَا وَعَمَّارٌ وَسَعْدٌ فِيمَا نُصِيبُ يَوْمَ بَدْرٍ..} اَلْحَدِيثَ. رَوَاهُ النَّسَائِيُّ وَغَيْرُهُ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilishirikiana mimi, ‘Ammaar na Sa’d katika tulichopata siku ya vita vya Badr.” Hadi mwisho wa Hadiyth [Imetolewa na An-Nasaaiy]
745.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {قَالَ: أَرَدْتُ اَلْخُرُوجَ إِلَى خَيْبَرَ، فَأَتَيْتُ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: "إِذَا أَتَيْتَ وَكِيلِي بِخَيْبَرَ، فَخُذْ مِنْهُ خَمْسَةَ عَشَرَ وَسْقًا} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَصَحَّحَهُ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Nilitaka kuenda Khaybar nikamuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) nikamueleza akasema: Utakapomuendea wakala wangu Khaybar chukua wasaki (kapu) kumi na tano (tende) kutoka kwake.”[6] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha]
746.
وَعَنْ عُرْوَةَ الْبَارِقِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بَعَثَ مَعَهُ بِدِينَارٍ يَشْتَرِي لَهُ أُضْحِيَّةً..} اَلْحَدِيثَ. رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ فِي أَثْنَاءِ حَدِيثٍ، وَقَدْ تَقَدَّمَ
Kutoka kwa ‘Urwah Al-Baariqiyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimpa dinari (moja) kununulia udhw-hiyyah.” Mpaka mwisho wa Hadiyth [Imetolewa na Al-Bukhaariy na imetangulia][7]
747.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {بَعَثَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عُمَرَ عَلَى اَلصَّدَقَةِ..} اَلْحَدِيثَ. مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimtuma ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kuchukua Zakaah.” Mpaka mwisho wa Hadiyth [Al-Bukhaariy, Muslim][8]
748.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَحَرَ ثَلَاثًا وَسِتِّينَ، وَأَمَرَ عَلِيًّا أَنْ يَذْبَحَ اَلْبَاقِيَ} اَلْحَدِيثَ. رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alichinja (ngamia) sitini na tatu akamuamrisha ‘Aliy[9] kuwachinja waliobakia (thelathini na saba).” Mpaka mwisho wa Hadiyth [Imetolewa na Muslim]
749.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ فِي قِصَّةِ اَلْعَسِيفِ. قَالَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {وَاغْدُ يَا أُنَيْسُ عَلَى اِمْرَأَةِ هَذَا، فَإِنْ اِعْتَرَفَتْ فَارْجُمْهَا..} اَلْحَدِيثَ. مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema katika kisa cha muajiriwa kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ee Ubays nenda kwa mke wa bwana huyu, akikiri kosa umpige mawe…”[10] mpaka mwisho wa Hadiyth [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] Ushirika ni muafaka baina ya washirika katika asili ya mali na faida. Katika Hadiyth hii kuna dalili kuswihi ushirika katika kuchuma na ushirika huu unaitwa ushirika wa kiwiliwili (Shirkat Al-Abdaan). Ushirika uko katika mafungu manne.
[2] Wakala ni kumpa mtu unaibu atakayekuwa badala yake katika majukumu yake kama vile kuuza, kununua na mfano wake.
[3] Hii ina maana kuwa ushirika wa mali na fedha ni jambo lililoruhusiwa, la kuzingatia ni uaminifu. Ushirika wenye uaminifu ndani yake huleta faida, uaminifu unapoondoka hasara huingia kwa washirika.
[4] Ibn Jawziy ametaja katika At-Taliqiyb jina lake lilikuwa As-Saaib bin ‘Aaidh Al-Makhzuwmiyy. Ibn ‘Abdil-Barr amesema alikuwa miongoni mwa Al-Muallafatul-Quluwb na aliposilimu alikuwa Muislamu mzuri. Ni Swahaba, aliishi hadi katika zama za ukhalifa wa Mu’aawiyah.
[5] Ushirika ulikuwepo hapo kabla na Uislamu ukauelekeza vizuri.
[6] Ina maana mtu anaweza kumuweka wakala wake katika mambo ya fedha. Kuna Hadiyth nyingine ambayo Jaabir anamuuliza Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amjibu nini mtu anayemtaka asimamie ukusanyi wa tende. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia aweke mkono katika mti wa mtende wa anayemuomba, wakati huo Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alishakuwa na wakala wake. Wasaki 15 ni kilo 2145.
[7] Tazama Hadiyth ya 686.
[8] Hadiyth inamalizikia hivi: Akaambiwa: “Ibn Jamiyl, Khaalid ibn Waliyd na Al ‘Abbaas ami yake Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) wamezuia (Zakaah). Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Ibn Jamiyl hawezi kukataa isipokuwa alikuwa fukara Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Akamtajirisha. Ama Khaalid, nyinyi mnamdhulumu Khaalid. Hakika aliziweka zana zake za kivita katika njia ya Allaah. Ama Al-‘Abbaas Zakaah yake ninayo mimi na mfano wake.” Kisha akasema: Ee ‘Umar kwani hujui kuwa ami ya mtu ni mfano wa baba yake?” Katika Hadiyth hii muna dalili ya kiongozi kumwakilisha mtu kuchukua Zakaah.
[9] Ina maana kumpa wakala mtu achinje Udhwhiyya (mnyama) ni jambo linalokubalika kishariy’ah
[10] Hii ni dalili nyingine ya kuruhusu uwakala hata katika huduwd. Hadiyth hii ni dalili kuwa anayeamrishwa ni wakala wa kiongozi katika kutekeleza hadd (adhabu). Unays ni wakala katika kuhakiki madai ya zinaa, tena ni wakala katika kutekeleza adhabu.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْإِقْرَارِ
10-Mlango Wa Iqrari[1] (Kukiri Kosa)
750.
عَنْ أَبِي ذَرٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ لِي رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {قُلِ اَلْحَقَّ، وَلَوْ كَانَ مُرًّا} صَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ فِي حَدِيثٍ طَوِيلٍ
Kutoka kwa Abuu Dharr[2] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ameniambia: “Sema haki japo ni chungu.” [Kaisahihisha Ibn Hibbaan kutoka Hadiyth ndefu]
[1] Iqraar ni kuthibitisha kitu fulani, kulingana na Istwilaah ya kishariy’ah ni mtu kukubali aliyoyafanya. Ni kinyume na kukana au kukataa.
[2] Jina lake ni Jundub bin Junaadah, ni Swahaba alisilimu kitambo, imepokewa kuwa yeye alisema: “Mimi ni mtu wa tano katika Uislam.” Hupigiwa mfano katika ukweli, naye ndiye wa kwanza aliyemuamkia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) maakizi ya Kiislamu. Alifariki mwaka wa 32 Hijriyyah. Katika vitabu vya Hadiyth, ana Hadiyth 281.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْعَارِيَةِ
11-Mlango Wa Kuazima[1]
751.
عَنْ سَمُرَةَ بْنِ جُنْدُبٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {عَلَى اَلْيَدِ مَا أَخَذَتْ حَتَّى تُؤَدِّيَهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa Samurah bin Jundub (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ni wajibu wa mkono kwa ulichokichukua hadi ukirudishe.”[2] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha Al-Haakim]
752.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَدِّ اَلْأَمَانَةَ إِلَى مَنْ اِئْتَمَنَكَ، وَلَا تَخُنْ مَنْ خَانَكَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَاسْتَنْكَرَهُ أَبُو حَاتِمٍ اَلرَّازِيُّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Tekeleza amana kwa aliyekuamini, wala usimkhini aliyekukhini.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, na At-Tirmidhiy na amesema ni Hassan, na akaisahihisha Al-Haakim, na ameona ni Munkar (Hadiyth iliokataliwa) Abuu Haatim Ar-Raaziyy]
753.
وَعَنْ يَعْلَى بْنِ أُمَيَّةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِذَا أَتَتْكَ رُسُلِي فَأَعْطِهِمْ ثَلَاثِينَ دِرْعاً "، قُلْتُ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ ! أَعَارِيَةٌ مَضْمُونَةٌ أَوْ عَارِيَةٌ مُؤَدَّاةٌ ؟ قَالَ: بَلْ عَارِيَةٌ مُؤَدَّاةٌ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Ya’laa bin Umayyah[3] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Utakapojiwa na wajumbe wangu, wape deraya (nguo za kivita) thelathini. Nikasema Ee Rasuli wa Allaah! Ni za kuazima zilizodhaminiwa[4] ama ni za kuazima na kurudisha kama kawaida? Akasema: Ni za kuazima na kurudishwa kama kawaida.” [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
754.
وَعَنْ صَفْوَانَ بْنِ أُمَيَّةَ، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اِسْتَعَارَ مِنْهُ دُرُوعاً يَوْمَ حُنَيْنٍ. فَقَالَ: أَغَصْبٌ يَا مُحَمَّدُ ؟ قَالَ: بَلْ عَارِيَةٌ مَضْمُونَةٌ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ .
وَأَخْرَجَ لَهُ شَاهِدًا ضَعِيفًا عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ
Kutoka kwa Swafwaan bin Umayyah[5] amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliazima kwake deraya siku ya vita vya Hunayn, akasema: Je unaninyang’anya ee Muhammad? Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Bali ni kuazima kwa dhamana.”[6] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na akaisahihisha Al-Haakim]
Na akaishuhudisha kwa Hadiyth dhaifu kutoka kwa Ibn ‘Abbaas
755.
عَنْ سَعِيدِ بْنِ زَيْدٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ اِقْتَطَعَ شِبْرًا مِنْ اَلْأَرْضِ ظُلْماً طَوَّقَهُ اَللَّهُ إِيَّاهُ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ مِنْ سَبْعِ أَرَضِينَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Sa’iyd bin Zayd[7] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kukata shubiri moja ya ardhi kwa dhulma, Allaah atamvisha shingoni mwake siku ya Qiyaamah ardhi saba.”[8] [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] Katika lugha ya kiarabu مَضْمُونَةٌ اَلْعَارِيَةِ (Al-‘aariyah Madhwmuwnah) ni mkopo uliodhaminiwa na عَارِيَةٌ مُؤَدَّاةٌ (‘Aariyah Muaddah) ni kilichoazimwa (kisicho na dhamana). Kuhusu ya mwanzo ni kuwa dhamana ni muhimu. Jaalia mtu anachukua mkopo wenye dhamana na kilichoazimwa kikaharibika ikiwa kwa aliyekiazima, kilichokubaliwa ni kuwa muazimaji atalipa thamani yake, na ndio maana ikaitwa ‘Aariyah Madhwmuwnah. Hata hivyo ikiwa mtu ataazima kwa kuaminiwa kama ilivyo ‘Aariyah Muaddah (kisichokuwa na dhamana) na kitu chenyewe kikaharibika kwa aliyekiazima (bila uzembe kutoka kwake) hatotakiwa kulipa.
[2] Umetajwa “mkono” lakini makusudio ni mtu. Yaani aliyeazima kitu anawajibika kukirudisha alichokichukua hata kama ni kwa gharama. Hadiyth hii ni dalili kuwa ni wajibu mtu kurudisha mali ya mwenyewe ima kama aliazimia au kwa njia nyingine.
[3] Huyu ni Ya’laa bin Umayyah bin Abiy ‘Ubaydah At-Tamiym. Mama yake anaitwa Mun-yah, kwa hivyo huitwa Ibn Mun-yah. Ni Swahaba mashuhuri, alifariki baada ya mwaka wa 40 Hijriyyah.
[4] Vilivyoazimwa kwa dhamana uharibifu wake utalipwa na mwenye kuazima. Kuazima ni kumruhusu mtu kutumia mali ya mwingine, au faida ya kitu kile, na baada ya kutumia kukirejesha kwa mwenyewe. Lakini katika viazimwavyo ni vitu, hakuna mtu kuazima mkewe. Pia haifai mtu kuazima kitu ili akitumie katika kufanyia kitu cha haraam.
[5] Huyu ni Swafwaan bin Umayyah bin Khalaf bin Wahb Al-Qurayshiy Al-Jumahi Al-Makkiy, ni Swahaba alikuwa miongoni mwa watukufu wa ki Quraysh. Alikimbia siku ya Fat-hi Makkah (Ukombozi wa Makkah), akapewa Amani, akarudi. Alihudhuria pamoja na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) vita vya Hunayn na vita vya Twaaif akiwa ni kafiri, kisha akasilimu, na akawa Muislam bora. Alifariki siku za mauaji ya ‘Uthmaan
[6] Ikiwa mtu ameazima kitu na kikaharibika kwa bahati mbaya, muazimaji hatogharamia kwa hilo, lakini ikithibitika kuwa uharibifu huo ni wa makusudi au ni matokeo ya uzembe wake basi atatakiwa kulipa.
[7] Jina lake ni Sa’iyd bin Zayd bin ‘Amr bin Nufayl bin ‘Abdul ‘Uzza bin Riyaah Al-Qurayshi Al-‘Adawi na ukoo wake unakutana na ule wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kwa Ka’b bin Luay. Ni mmojawapo katika waliobashiriwa Jannah, ‘Umar bin Al-Katwaab (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alikuwa ami yake upande wa kuumeni, kwa sababu ‘Amr bin Nufayl babake Sa’iyd na Al-Khatwaab bin Nufayl babake ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) walikuwa ndugu. Sa’iyd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alikuwa mume wa Faatwimah dada yake ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ), alikua chachu iliyomsaidia kumsilimisha ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) na dada yake Sa’iyd ‘Atikah alikuwa mke wa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ). Alijulikana kwa jina Sa’iyd kabla ya kuja kwa Uislam na baada ya kusilimu. Sa’iyd alikuwa katika Muhajirina wa mwanzo.
[8] Hii ina maana ya kupora ardhi ya mtu ni katika madhambi makubwa. Kupora ardhi ya mtu maana yake ni kuichukuwa na kuanza kuilima.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْغَصْبِ
12-Mlango Wa Kunyang’anya[1]
756.
وَعَنْ أَنَسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كَانَ عِنْدَ بَعْضِ نِسَائِهِ، فَأَرْسَلَتْ إِحْدَى أُمَّهَاتِ اَلْمُؤْمِنِينَ مَعَ خَادِمٍ لَهَا بِقَصْعَةٍ فِيهَا طَعَامٌ، فَكَسَرَتِ اَلْقَصْعَةَ، فَضَمَّهَا، وَجَعَلَ فِيهَا اَلطَّعَامَ. وَقَالَ: " كُلُوا " وَدَفَعَ اَلْقَصْعَةَ اَلصَّحِيحَةَ لِلرَّسُولِ، وَحَبَسَ اَلْمَكْسُورَةَ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ .
وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَسَمَّى اَلضَّارِبَةَ عَائِشَةَ، وَزَادَ: فَقَالَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {طَعَامٌ بِطَعَامٍ، وَإِنَاءٌ بِإِنَاءٍ} وَصَحَّحَهُ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa yuko kwa baadhi ya wakeze, mmoja wa Mama wa Waumini akamtuma mtumishi wake sahani yenye chakula akapiga ile sahani kwa mkono akavunja.[2] Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akavikusanya vipande vile akaweka chakula ndani yake, akasema: Kuleni.[3] Akachukua sahani nzima akampa yule mtumishi, ile iliyovunjika akaizuia.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
Na At-Tirmidhiy akamtaja aliyepiga ni ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) na akaongeza: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Chakula kwa chakula na chombo kwa chombo.”[4] Ameisahihisa.
757.
وَعَنْ رَافِعِ بْنِ خَدِيجٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ زَرَعَ فِي أَرْضِ قَوْمٍ بِغَيْرِ إِذْنِهِمْ، فَلَيْسَ لَهُ مِنْ اَلزَّرْعِ شَيْءٌ، وَلَهُ نَفَقَتُهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ إِلَّا النَّسَائِيَّ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ.
وَيُقَالُ: إِنَّ اَلْبُخَارِيَّ ضَعَّفَهُ
Kutoka kwa Raafi’ bin Khadiyj[5] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kulima katika ardhi ya watu bila ruhusa yao hana haki yoyote katika mazao, na gharama ni yake.”[6] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa An-Nasaaiy, na At-Tirmidhiy akasema ni Hassan]
Yasemekana kuwa Al-Bukhaariy ameidhoofisha
758.
وَعَنْ عُرْوَةَ بْنِ اَلزُّبَيْرِ قَالَ: قَالَ رَجُلٌ مِنْ اَلصَّحَابَةِ، مِنْ أَصْحَابِ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِنَّ رَجُلَيْنِ اِخْتَصَمَا إِلَى رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي أَرْضٍ، غَرَسَ أَحَدُهُمَا فِيهَا نَخْلًا، وَالْأَرْضُ لِلْآخَرِ، فَقَضَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بِالْأَرْضِ لِصَاحِبِهَا، وَأَمَرَ صَاحِبَ اَلنَّخْلِ أَنْ يُخْرِجَ نَخْلَهُ. وَقَالَ: " لَيْسَ لِعِرْقٍ ظَالِمٍ حَقٌّ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَإِسْنَادُهُ حَسَنٌ
وَآخِرُهُ عِنْدَ أَصْحَابِ " اَلسُّنَنِ " مِنْ رِوَايَةِ عُرْوَةَ، عَنْ سَعِيدِ بْنِ زَيْدٍ
وَاخْتُلِفَ فِي وَصْلِهِ وَإِرْسَالِهِ، وَفِي تَعْيِين صَحَابِيِّهِ
Kutoka kwa ‘Urwah bin Az-Zubayr[7] amesema: Mmoja wa Maswahaba wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alihadithia: “Watu wawili waligombana na kuenda kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) katika ardhi ambayo mmojawapo aliotesha mtende kuhusu ardhi ya mwingine. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akahukumu kuwa ardhi ni ya mwenyewe, akamuamrisha mwenye mtende kutoa mtende wake na akasema: “Mmea uliopanda kwa dhulma hauna haki.”[8] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Isnaad yake ni Hassan]
Mwisho wa Hadiyth inapatikana katika vitabu vya As-Sunan, kutoka kwa ‘Urwah naye kutoka kwa Sa’iyd bin Zayd. Hata hivyo wametofautiana ikiwa ni Mawsuwl (iliyounga) au ni Mursal (iliyoishia kwa Taabi’) kadhalika na jina Swahaba aliyesikia na kupokea kutoka kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ).
759.
وَعَنْ أَبِي بَكْرَةَ، رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: فِي خُطْبَتِهِ يَوْمَ اَلنَّحْرِ بِمِنًى {إِنَّ دِمَاءَكُمْ وَأَمْوَالَكُمْ وَأَعْرَاضَكُمْ عَلَيْكُمْ حَرَامٌ، كَحُرْمَةِ يَوْمِكُمْ هَذَا، فِي بَلَدِكُمْ هَذَا، فِي شَهْرِكُمْ هَذَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Bakr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema katika khutbah yake ya siku ya Nahr alipokuwa Minaa alisema: “Hakika damu zenu na mali yenu ni haraam juu yenu kama uharamu wa siku yenu hii, katika mwezi wenu huu katika mji wenu huu.”[9] [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] اَلْغَصْبِ (Al Ghaswb) ina maana ya kuchukua mali ya mtu kwa nguvu bila ridhaa yake.
[2] Alifanya hivyo kwa sababu ya wivu ikiwa wanawake wana wivu na waume wa kawaida.
[3] Akiwaambia wale aliokuwa nao.
[4] Kuna tofauti ya rai baina ya Wanazuoni, ikiwa kimeharibika au kuvunjika kwa aliyekiazima, itabidi alipe thamani yake au kukibadilisha na mfano wake. Hii inahusu vitu vinavyoweza kutiwa thamani tu. Ama vinginevyo lazima virudishwe vilivyo. Hadiyth hii inatilia mkazo vitu kurudishwa kama vilivyo.
[5] Raafi’ bin Khadiyj, Abuu ‘Abdillaah, Al-Khazraj Al-Answaariy. Ni mwenyeji wa Madiynah. Hakupigana katika vita vya Badr kwa sababu alikuwa na umri mdogo, lakini alihudhuria vita vya Uhud na vilivyofuatia. Alifariki mwaka wa 73 Hijriyyah.
[6] Ikitokezea mtu akalima shamba la mtu ya ruhusa ya mwenye shamba, hana haki ya mazao yake. Kikubwa anachoweza kudai ni gharama ya mbegu alizotia, na mazao yatakuwa ni ya mwenye kumiliki shamba.
[7] Huyu ni Abuu ‘Abdillaah ‘Urwah bin Az-Zubayr bin Al-‘Awwaam bin Khuwayldi Al-Asad Al-Madaniy. Ni katika Mafuqahaa (Ulamaa wa Shariy’ah) saba wa Madiynah, na ni mmojawapo wa ‘Ulamaa wa kitabi’iyna. Alikuwa ni mtu madhubuti amepokea Hadiyth kutoka kwa baba yake, mama yake, Khalati yake ambaye ni ‘Aaishah Ummul-Mu-uminiyna (Mama wa Waumini), ‘Aliy, Muhammad bin Maslamah na Abuu Hurayrah. Ibn Sa’d amesema: “Ni madhubuti na ana Hadiyth nyingi, Faqihi, Mwanachuoni, thabiti, muaminiwa.” Alikuwa akisoma robo ya Qur-aan kila usiku (yaani juzuu saba na nusu). Alizaliwa mwanzoni mwa ukhalifa wa ‘Umar katika mwaka wa 23 Hijriyyah. Alifariki mwaka 94 Hijriyyah.
[8] Neno ظَالِمٍ (Dhwaalim) ni neno lenye maana mbaya sana, hapa ina maana ni mtu muovu, asiye na uadilifu. Hadiyth hii ni dalili kuwa anayetumia ardhi ya mwenyewe, ima kwa kupanda mimea, kujenga au kwa jambo lingine, anawajibika kutoa na kubomoa alichojenga, na gharama za kubomoa ni juu yake huyu mnyang’anyi. Lakini ile mimea na majengo ni mwenyewe (mwenye ardhi).
[9] Hadiyth hii imetajwa hapa kuwa kupora mali ya Muislam ni haraam. Na jambo hili limekubaliwa na Wanazuoni wote.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلشُّفْعَةِ
13-Mlango Wa Ash-Shuf’ah (Shufaa)[1]
760.
عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {قَضَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بِالشُّفْعَةِ فِي كُلِّ مَا لَمْ يُقْسَمْ، فَإِذَا وَقَعَتِ اَلْحُدُودُ وَصُرِّفَتْ اَلطُّرُقُ فَلَا شُفْعَةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ .
وَفِي رِوَايَةِ مُسْلِمٍ: {اَلشُّفْعَةُ فِي كُلِّ شِرْكٍ: أَرْضٍ، أَوْ رَبْعٍ، أَوْ حَائِطٍ، لَا يَصْلُحُ أَنْ يَبِيعَ حَتَّى يَعْرِضَ عَلَى شَرِيكِهِ}
وَفِي رِوَايَةِ اَلطَّحَاوِيِّ: {قَضَى اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بِالشُّفْعَةِ فِي كُلِّ شَيْءٍ} وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alihukumu shufaa katika kila mali isiyogawanywa. Itakapowekwa mipaka na njia zikabainishwa hakuna shufaa.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
Na katika Riwaayah ya Muslim: “Shufaa katika kila ushirika, iwe ardhi, nyumba ya kuishi na bustani hairuhusiwi.” Katika tamshi linguine: “si halali (kuuza mshirika) mpaka amfahamishe mshirika mwenzake.”
Katika Riwaayah nyingine ya Atw-Twahaawiyy imesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amehukumu shufaa katika kila kitu.” Wapokezi wake ni madhubuti.
761.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {جَارُ اَلدَّارِ أَحَقُّ بِالدَّارِ} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَلَهُ عِلَّةٌ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema “Jirani wa nyumba ana haki zaidi ya (kununua) nyumba.” [Imetolewa na An-Nasaaiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan lakini ina ila]
762.
وَعَنْ أَبِي رَافِعٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلْجَارُ أَحَقُّ بِصَقَبِهِ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ، وَفِيهِ قِصَّةٌ
Kutoka kwa Abuu Raafi’ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Jirani wa nyumba ana haki zaidi kwa nyumba.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy. Hadiyth hii ina kisa chake][2]
763.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلْجَارُ أَحَقُّ بِشُفْعَةِ جَارِهِ، يُنْتَظَرُ بِهَا وَإِنْ كَانَ غَائِبًا إِذَا كَانَ طَرِيقُهُمَا وَاحِدًا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Jirani ana haki zaidi kwa shufaa ya jirani yake atamngojea hata kama hayuko iwapo njia yao ni moja.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) wapokezi wake ni madubuti (thiqah)]
764.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {اَلشُّفْعَةُ كَحَلِّ اَلْعِقَالِ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ وَالْبَزَّارُ، وَزَادَ: "وَلَا شُفْعَةَ لِغَائِبٍ" وَإِسْنَادُهُ ضَعِيفٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Shufaa ni kama kufungua kamba (inayomzuia ngamia).”[3] [Imetolewa na Ibn Maajah na Al-Bazzaar akaongezea: “…wala hakuna shufaa kwa asiyekuwepo.” Na Isnaad yake ni dhaifu]
[1] اَلشُّفْعَةِ (Ash-Shuf’ah) shufaa ni mshirika kuchukua hisa ya mshirika mwenzake ambayo ameiuza kwa thamani yake aliyouzia nayo mshirika.
uzindushi: Kuna tofauti baina ya Ash-Shufa’ah (shufaa) na Ash-Shafaa’ah (shafaa) na Ash-shifaa’ah. Shufaa ni hii tuliyoieleza. Shafaa ni kuombea mtu msamaha. Shifaa ni poza.
[2] Kisa chenyewe ni hiki: kuwa Abuu Raafi’ akiwa pamoja na Miswaar bin Makhrama alimkabili Sa’d ibn Abii Waqqaasw na kumuaridhia kumuuzia nyumba yake iliyokuwa jirani yake na nyumba ya Sa’d. Miswaar aliongea na Sa’d kuhusu jambo hilo. Sa’d alikubali kulipa Dinari mia nne (sarafu za dhahabu) kwa ajili ya nyumba ya Abuu Raafi’. Alikuwa tayari kulipa malipo ya mara moja au ya kidogo kidogo kama alivyotaka Abuu Raafi’. Aliposikia hivi Abuu Raafi’ akasema hakuuza nyumba hizi kwa fedha alizoahidiwa Dinari mia tano taslimu kwa sababu alimsikia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema kuwa majirani wana haki zaidi kuliko wengine. Akasema vile vile lau angelisikia kabla asingeuza nyumba zake kwa bei ile.
[3] حَلِّ اَلْعِقَالِ (Hallil-‘Iqaal) ina maana muda tu magoti ya ngamia yatakapofunguliwa, wakati huo mara moja huamka. Hivyo hivyo, muda wa kuwa nyumba ishauzwa, au mtu ana haki kufahamu kuwa mwenzake anauza kitu naye asiharakishe mpaka ukapita muda mrefu basi hapo haki yake ya shufaa imeanguka. Na hii ndio maana ya msemo wa Hallil-‘Iqaal kawaida ya kufungua kamba hakuchukui muda mrefu.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْقِرَاضِ
14-Mlango Wa Qiraadhw[1]
765.
عَنْ صُهَيْبٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {ثَلَاثٌ فِيهِنَّ اَلْبَرَكَةُ: اَلْبَيْعُ إِلَى أَجَلٍ، وَالْمُقَارَضَةُ، وَخَلْطُ اَلْبُرِّ بِالشَّعِيرِ لِلْبَيْتِ، لَا لِلْبَيْعِ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ
Kutoka kwa Swuhayb[2] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mambo matatu ndani yake kuna Baraka: kuuza kwa muda maalumu, Muqaaradhwah na kuchanganya ngano na shayiri[3] kwa matumizi ya nyumbani si kwa kuuza.” [Imetolewa na Ibn Maajah kwa Isnaad dhaifu]
766.
وَعَنْ حَكِيمِ بْنِ حِزَامٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّهُ كَانَ يَشْتَرِطُ عَلَى اَلرَّجُلِ إِذَا أَعْطَاهُ مَالًا مُقَارَضَةً: أَنْ لَا تَجْعَلَ مَالِي فِي كَبِدٍ رَطْبَةٍ، وَلَا تَحْمِلَهُ فِي بَحْرٍ، وَلَا تَنْزِلَ بِهِ فِي بَطْنِ مَسِيلٍ، فَإِنْ فَعَلْتَ شَيْئًا مِنْ ذَلِكَ فَقَدَ ضَمِنْتَ مَالِي} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
وَقَالَ مَالِكٌ فِي " اَلْمُوَطَّأِ " عَنْ اَلْعَلَاءِ بْنِ عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ بْنِ يَعْقُوبَ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ: {أَنَّهُ عَمِلَ فِي مَالٍ لِعُثْمَانَ عَلَى أَنَّ اَلرِّبْحَ بَيْنَهُمَا} وَهُوَ مَوْقُوفٌ صَحِيحٌ
Kutoka kwa Hakiym bin Hizaam (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Alikuwa anampa mtu masharti anapompa mali kwa Muqaaradhwah akimuambia: Usifanyie biashara mali yangu katika viumbe vyenye uhai, wala usiibebe baharini, wala usiteremke nayo maporomoko ya mito; utakapofanya hivyo utaidhamini mali yangu.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy na wapokezi wake ni madhubuti]
Maalik amesema katika kitabu chake “Al-Muwatwa” kutoka kwa Al-‘Alaa[4] bin ‘Abdir-Rahmaan bin Ya’quwb naye kutoka kwa baba yake[5] kutoka kwa babu yake[6]: “Kwamba yeye alifanyia biashara mali ya ‘Uthmaan kwa sharti ya kugawana faida baina yao.”[7] Hadiyth hii ni Mawquwf.
[1] Qiraadhw na Muqaaradhw yote ni majina ya kitu kimoja; ni mtu ampe mwenzie mali afanyie biashara na mwingine atatoa nguvu za kufanyia kazi, faida itakayopatikana watagawana, kama washirika. Kama kutakuwa na hasara, itaangukia katika rasilimali aliyotoa muekezaji. Kwa jina lingine huitwa Mudhwaarabah.
[2] Huyu ni Abuu Yahya Swuhayb bin Sinaan bin Maalik Ar-Rumi, Abuu Yahya. Alikuwa mwarabu wa kabila la An-Nimir bin Qaasitw bin Waail ambaye alichukuliwa mateka na Waroma na ndipo alipopata jina Ar-Rumi, akakulia kwao, na akawa miongoni mwao. Inasemekana kuwa alipobaleghe na kuwa mkubwa alikimbia na kurudi Makkah na akawa katika wafuasi wa ‘Abdullaah bin Jad’an. Inasemekana kuwa mmoja katika watu wa kabila la Baniy Kalb alimnunua na akamleta Makkah. ‘Abdullaah bin Jad’an akamnunua. Swuhayb alikuwa Swahaba mkubwa ambaye alisilimu mapema, alipata mateso kwa ajili ya dini yake. Alihamia Madiynah na kufariki Madiynah mwaka wa 38 Hijriyyah.
[3] Shayiri: nafaka inayofanana na ngano inayotumika kwa chakula.
[4] Huyu ni Abuu Sibli Al-‘Alaa bin ‘Abdir-Rahmaan bin Ya’quwb Al-Juhani, muachwa huru wa Al-Huraaqa Al-Madaniy. Alikuwa katika Taabi’iyna maarufu wa kizazi cha tano. Alikuwa ni mkweli lakini alikuja kuchanganyikiwa kuhusu Hadiyth. Ahmad na wengineo wanaithibitisha uaminifu wake. Al-Waaqidi anasema kuwa alikufa wakati wa ukhalifa wa Al-Manswuwr.
[5] ‘Abdur-Rahmaan bin Ya’quwb Al-Juhani alikuwa miongoni mwa Taabi’iyna na alikuwa katika kizazi cha tatu. Alichukua Hadiyth za Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kutoka kwa baba yake, Abuu Hurayrah na Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy.
[6] Ya’quwb Al-Juhani alikuwa ni muachwa huru wa Al-Huraaqa na alikuwa kiongozi katika kizazi cha pili katika Taabi’iyna. Aliishi wakati wa ‘Umar bin Al-Khatwaab na miongoni mwa wapokezi wachache wa Hadiyth
[7] Al-Mudhwaarabah au Al-Qiraadhw ni aina za mikataba. Ambayo fidia inasamehewa kwa watu. Kama hasara inatokana na uzembe au makossa ya mfanyakazi, atawajibika kwa hilo. Vinginevyo, hawajibiki. Hivyo hivyo, kutekeleza kinyume na maagizo au maelekezo ya muekezaji, mshirika katika biashara atawajibika na hasara iliyotokea.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْمُسَاقَاةِ وَالْإِجَارَةِ
15-Mlango Wa Kumwagilia Musaaqaah[1] Na Kukodisha[2]
767.
عَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَامَلَ أَهْلَ خَيْبَرَ بِشَطْرِ مَا يَخْرُجُ مِنْهَا مِنْ ثَمَرٍ، أَوْ زَرْعٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ.
وَفِي رِوَايَةٍ لَهُمَا: فَسَأَلُوا أَنْ يُقِرَّهُمْ بِهَا عَلَى أَنْ يَكْفُوا عَمَلَهَا وَلَهُمْ نِصْفُ اَلثَّمَرِ، فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نُقِرُّكُمْ بِهَا عَلَى ذَلِكَ مَا شِئْنَا "، فَقَرُّوا بِهَا، حَتَّى أَجْلَاهُمْ عُمَرُ
وَلِمُسْلِمٍ:{أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ دَفَعَ إِلَى يَهُودِ خَيْبَرَ نَخْلَ خَيْبَرَ وَأَرْضَهَا عَلَى أَنْ يَعْتَمِلُوهَا مِنْ أَمْوَالِهِمْ، وَلَهُ شَطْرُ ثَمَرِهَا}
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliamiliana na watu wa Khaybar (Mayahudi) kwa makubaliano kuwa atapewa nusu ya kitakachotoka humo kutokana na matunda au mazao.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Katika Riwaayah yao nyingine: “… (Mayahudi) Wakamuomba Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) awaache waishi (Khaybar) kwa sharti walime mali na yao iwe nusu ya tende. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Tumewaruhusu muishi kwa sharti hiyo mpaka tutakapotaka.” Akawaruhusu kuishi humo mpaka ‘’Umar alipowafukuza’
Katika Riwaayah ya Muslim: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliwapa Mayahudi wa Khaybar mitende ya Khaybar na ardhi ya huko kwa sharti walime kwa mali yao nao wapate nusu ya matunda yake.”[3]
768.
وَعَنْ حَنْظَلَةَ بْنِ قَيْسٍ قَالَ:{سَأَلْتُ رَافِعَ بْنَ خَدِيجٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ كِرَاءِ اَلْأَرْضِ بِالذَّهَبِ وَالْفِضَّةِ ؟ فَقَالَ: لَا بَأْسَ بِهِ، إِنَّمَا كَانَ اَلنَّاسُ يُؤَاجِرُونَ عَلَى عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَلَى الْمَاذِيَانَاتِ، وَأَقْبَالِ اَلْجَدَاوِلِ، وَأَشْيَاءَ مِنْ اَلزَّرْعِ، فَيَهْلِكُ هَذَا وَيَسْلَمُ هَذَا، وَيَسْلَمُ هَذَا وَيَهْلِكُ هَذَا، وَلَمْ يَكُنْ لِلنَّاسِ كِرَاءٌ إِلَّا هَذَا، فَلِذَلِكَ زَجَرَ عَنْهُ، فَأَمَّا شَيْءٌ مَعْلُومٌ مَضْمُونٌ فَلَا بَأْسَ بِهِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ .
وَفِيهِ بَيَانٌ لِمَا أُجْمِلَ فِي اَلْمُتَّفَقَ عَلَيْهِ مِنْ إِطْلَاقِ اَلنَّهْيِ عَنْ كِرَاءِ اَلْأَرْضِ
Kutoka kwa Handhwalah bin Qays[4] amesema: “Nilimuuliza Raafi’ bin Khadiyj (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) juu ya kuikodisha ardhi kwa dhahabu na fedha. Akasema: “Hapana ubaya. Kwani watu walikuwa wakiajiriana wakati wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) sehemu zilizopo juu ya mito mikubwa na katika vianzio vya mito midogo na kwa sehemu ya mazao. Basi sehemu moja inaangamia,[5] na sehemu nyingine ikisalimika, na sehemu hii ikisalimika nyingine inaangamia. Watu walikuwa hawana upangaji isipokuwa huu. Kwa ajili hiyo kakataza. Ama kikikodishwa kwa kitu chenye kujulikana na chenye dhamana basi hakina ubaya.” [Imetolewa na Muslim]
Haya yanathibitisha yaliyokumuishwa katika Al-Bukhaariy na Muslim katika uharamu wa kukodisha ardhi.
769.
وَعَنْ ثَابِتِ بْنِ اَلضَّحَّاكِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ اَلْمُزَارَعَةِ وَأَمَرَ بِالْمُؤَاجَرَةِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ أَيْضًا
Kutoka kwa Thaabit bin Adhw-Dwahhaak[6] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza Muzaara’ah[7] na akaamrisha kuajiriana.”[8] [Imetolewa na Muslim]
770.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّهُ قَالَ: {اِحْتَجَمَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَأَعْطَى اَلَّذِي حَجَمَهُ أَجْرَهُ} وَلَوْ كَانَ حَرَاماً لَمْ يُعْطِهِ. رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliumika na akampa muumikaji ujira wake.” Lau ingalikuwa haraam basi asingalimpa. [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
771.
وَعَنْ رَافِعِ بْنِ خَدِيجٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {كَسْبُ اَلْحَجَّامِ خَبِيثٌ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Raafi’ bin Khadiyj (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Chumo la muumikaji ni chafu.”[9] [Imetolewa na Muslim]
772.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {قَالَ اَللَّهُ (عَزَّ وَجَلَّ) ثَلَاثَةٌ أَنَا خَصْمُهُمْ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ: رَجُلٌ أَعْطَى بِي ثُمَّ غَدَرَ، وَرَجُلٌ بَاعَ حُرًّا ، فَأَكَلَ ثَمَنَهُ، وَرَجُلٌ اِسْتَأْجَرَ أَجِيرًا ، فَاسْتَوْفَى مِنْهُ، وَلَمْ يُعْطِهِ أَجْرَهُ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Allaah (عزّ وجلّ) amesema: Watu watatu Mimi ni Mtesi wao siku ya Qiyaamah: mtu ametoa kwa jina Langu kisha akahini, mtu anamuuza muungwana na akala thamani yake, na mtu amemuajiri muajiriwa naye akamkamilishia kazi yake wala hakumpa ujira wake.”[10] [Imetolewa na Muslim]
773.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِنَّ أَحَقَّ مَا أَخَذْتُمْ عَلَيْهِ حَقًّا كِتَابُ اَللَّهِ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika cha haki zaidi mliochukua malipo juu yake ni Kitabu cha Allaah.”[11] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
774.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَعْطُوا اَلْأَجِيرَ أَجْرَهُ قَبْلَ أَنْ يَجِفَّ عَرَقُهُ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ
وفي الباب: عن أبي هريرة رضي الله عنه عند أبي يعلى والبيهقي. وجابر عند الطبراني، وكلها ضعاف
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mumpeni muajiriwa malipo yake kabla jasho lake kukauka.”[12] [Imetolewa na Ibn Maajah]
Katika mlangu huu kuna Hadiyth iliyopokewa na Abuu Hurayrah iliyo kwa Abuu Ya’laa na Bayhaqiyy na iliyopokewa kutoka kwa Jaabir iliyo kwa Atw-Twabaraaniy, Riwaayah zote ni dhaifu.
775.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: {مَنِ اِسْتَأْجَرَ أَجِيراً، فَلْيُسَلِّمْ لَهُ أُجْرَتَهُ} رَوَاهُ عَبْدُ اَلرَّزَّاقِ وَفِيهِ اِنْقِطَاعٌ، وَوَصَلَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ مِنْ طَرِيقِ أَبِي حَنِيفَةَ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuajiri muajiriwa amkabidhi malipo yake.”[13] [Imetolewa na ‘Abd Ar-Razzaaq, na Isnaadi yake ni Munqatwi’ (imekatika). Na Al-Bayhaqiyy ameipokea kwa Isnaadi Mawsuwl (iliyounga) kutoka kwa Abuu Haniyfah.
[1] Kumpa mtu kazi ya kumwagilia mti na kuusimamia na kupata malipo katika hilo huitwa Musaaqaah. Kwa jina lingine huitwa Muzaara’ah. Tofauti baina ya Musaaqaah na Muzaara’ah ni kuwa Musaaqaah ni kwa miti ya matunda, wakati Muzaara’ah ni kwa ajili ya nafaka
[2] Kumfanya mtu awe ni mshirika wa faida au kodi inaitwa Ijaarah.
[3] Hadiyth hii inatoa dalili y akuwepo kwa Musaaqaah na Muzaara’ah.
[4] Hanthwalah bin Qays Az-Zurqi Al-Answaar, ni miongoni mwa watu madhubuti Madiynah, na ni katika tabi’iyna wadogo.
[5] Ina maana ya kuwa ardhi ya chini inaweza kuchukuliwa na mafuriko na ardhi ya miinuko ikasalimika na wakati wa ukame ardhi ya chini karibu na maji ikasalimika na ardhi ya kwenye miinuko ikaangamia.
[6] Thaabit bin Adhw-Dwahaak Al-Answaar, Abuu Zayd, naye ni katika walioshuhudia Bay’at Ar-Ridhwaan, alikuwa Hudaybiyah mwaka wa sita Hijriyyah. Alifariki katika balaa ya ‘Abdullaah bin Az-Zubayr yakaribia mwaka wa 70 Hijriyyah.
[7] Katika kiarabu Muzaara’ah ni kumpa mtu shamba alime malipo yake ni baadhi ya kitakachovunwa. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) hakukataza hili, bali ardhi ilipokuwa ndogo kwa Answaar na Muhajiriyna walipoongezeka kwa njia ya dharura walilima ardhi kadiri walivyoweza na akawafundisha kuwa wasigawane mazao kwa njia ya ushirika wa Muzaara’ah bali wakodishe kwani Ijaarah inawapunguzia uzito kwa wapangaji au wakodishaji.
[8] Jina lililotumika Al-Ijaarah lina maana ya kukodisha ardhi kwa muda maalum, jambo ambalo ni la halaal.
[9] Kiarabu neno khabiyth lina maana ya tabia mbaya lakini haina maana ya haraam. Wakati mwingine linatumika kama lina maana ya istiara kwa maana ya bakhili.
[10] Hadiyth hii imehimiza kulipa mishahara kwa wakati wake kwa mfanyakazi. Siku hizi watu wengi wanakuwa siyo waadilifu katika miamala yao na si waaminifu katika malipo yao.
[11] Hadiyth hii inaeleza kwa uwazi kupokea ujira au mshahara kwa kufundisha kitabu cha Allaah na Hadiyth ni halaal. Mwalimu anayefundisha watu kusoma au kuhifadhi Qur-aan anayo haki ya kuchukua malipo.
[12] Ina maana ujira na mashahara kwa mfanyakazi lazima ilipwe mapema. Ambaye hatolipa malipo ya mfanyakazi Allaah atamuadhibu siku ya hukumu.
[13] Ina maana ya kuwa ujira kwa mfanyakazi ushughulikiwe mapema ili kuondosha migogoro. Vivyo hivyo, katika mas-ala kama Mudhwaarabah, Salaam, Muzaara’ah, Muwaajarah, n.k. kanuni ile ile iliyotekelezwa na shariy’ah lazima ifanye kazi na watu wote watekeleze na kufuata.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ إِحْيَاءِ اَلْمَوَاتِ
16-Mlango Wa Kufufua Ardhi Iliyokufa[1]
776.
عَنْ عُرْوَةَ، عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ عَمَّرَ أَرْضاً لَيْسَتْ لِأَحَدٍ، فَهُوَ أَحَقُّ بِهَا} قَالَ عُرْوَةُ: وَقَضَى بِهِ عُمَرُ فِي خِلَافَتِهِ. رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Urwah naye kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuamrisha (kuendeleza) ardhi isiyo na mwenyewe, basi mtu huyo ana haki zaidi katika ardhi hiyo.” ‘Urwah amesema: ‘Umar alihukumu hukumu hii katika Ukhalifa wake. [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
777.
وَعَنْ سَعِيدِ بْنِ زَيْدٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ أَحْيَا أَرْضاً مَيْتَةً فَهِيَ لَهُ} رَوَاهُ اَلثَّلَاثَةُ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ.
وَقَالَ: رُوِيَ مُرْسَلاً. وَهُوَ كَمَا قَالَ، وَاخْتُلِفَ فِي صَحَابِيِّهِ، فَقِيلَ: جَابِرٌ، وَقِيلَ: عَائِشَةُ، وَقِيلَ: عَبْدُ اَللَّهِ بْنُ عَمْرٍو، وَالرَّاجِحُ اَلْأَوَّلُ
Kutoka kwa Sa’iyd bin Zayd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuimarisha ardhi iliyokufa, ardhi hiyo ni yake.”[2] [Imetolewa na Ath-Thalaathah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd) na At-Tirmidhiy akaipa daraja ya Hassan]
Akisema kuwa imepokewa ikiwa ni Mursal. Hata hivyo hakuna makubaliano kuhusu Maswahaba waliosikia Hadiyth hii kutoka kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Inasemekana kuwa ni Jaabir, ‘Aaishah au ‘Abdullaah bin ‘Amr na kauli yenye nguvu ni ya kwanza yaani Jaabir.
778.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ، أَنَّ اَلصَّعْبَ بْنَ جَثَّامَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَخْبَرَهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا حِمَى إِلَّا لِلَّهِ وَلِرَسُولِهِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amesema Asw-Swa’b bin Jath-thaamah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alimueleza kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna himaya[3] isipokuwa ya Allaah na Nabiy Wake.”[4] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
779.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا ضَرَرَ وَلَا ضِرَارَ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَابْنُ مَاجَهْ .
وَلَهُ مِنْ حَدِيثِ أَبِي سَعِيدٍ مِثْلُهُ، وَهُوَ فِي اَلْمُوَطَّإِ مُرْسَلٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halaal kudhuriana wala kulipiziana madhara.”[5] [Imetolewa na Ahmad na Ibn Maajah]
Kadhalika Ibn Maajah ameripoti Hadiyth mfano wa hii kutoka kwa Abuu Sa’iyd. Hadiyth hii inapatikana katika Muwatwa ikiwa ni Hadiyth Mursal
780.
وَعَنْ سَمُرَةَ بْنِ جُنْدُبٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ أَحَاطَ حَائِطًا عَلَى أَرْضٍ فَهِيَ لَهُ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ اَلْجَارُودِ
Kutoka kwa Samurah bin Jundub (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuzungusha ukuta katika ardhi yoyote (ardhi tupu), ardhi hiyo ni yake.”[6] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Ibn Al-Jaaruwd]
781.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ مُغَفَّلٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ حَفَرَ بِئْرًا فَلَهُ أَرْبَعُونَ ذِرَاعًا عَطَنًا لِمَاشِيَتِهِ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mughaffal (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuchimba kisima basi ana dhiraa arubaini kwa ajili ya wanyama wake[7] (karibu na maji).” [Imetolewa na Ibn Maajah kwa Isnaad dhaifu]
782.
وَعَنْ عَلْقَمَةَ بْنِ وَائِلٍ، عَنْ أَبِيهِ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَقْطَعَهُ أَرْضًا بِحَضْرَمَوْتَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa ‘Alqamah bin Waail[8] naye kutoka kwa baba yake amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimkatia kipande cha ardhi[9] Hadhwramawt (Yemen).” [Imetolewa na Abuu Daawud na At-Tirmidhiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
783.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَقْطَعَ اَلزُّبَيْرَ حُضْرَ فَرَسِهِ ، فَأَجْرَى اَلْفَرَسَ حَتَّى قَامَ ، ثُمَّ رَمَى سَوْطَهُ. فَقَالَ: " أَعْطُوهُ حَيْثُ بَلَغَ اَلسَّوْطُ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَفِيهِ ضَعْفٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimkatia ardhi Az-Zubayr kiasi cha kuruka farasi wake, akamkimbiza farasi mpaka akasimama kisha (Az-Zubayr) akarusha mjeledi wake, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema:[10] Mpeni (kipande cha ardhi) hadi ulipofika mjeledi.”[11] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na katika Isnaad yake kuna udhaifu]
784.
وَعَنْ رَجُلٍ مِنْ اَلصَّحَابَةِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {غَزَوْتُ مَعَ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَسَمِعْتُهُ يَقُولُ: اَلنَّاسُ شُرَكَاءُ فِي ثَلَاثٍ: فِي اَلْكَلَأِ ، وَالْمَاءِ ، وَالنَّارِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ ، وَأَبُو دَاوُدَ ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Mtu mmoja katika Maswahaba amesema: “Nilipigana Jihaad pamoja na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) nikamsikia anasema: “Watu ni washirika katika mambo matatu: Majani, maji na moto.” [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd na wapokezi wake ni madhubuti]
[1] Neno Al-Mawaat nimelitafsiri kwa ‘ardhi iliyokufa’, lakini makusudio ni ardhi ambayo haijaimarishwa, au ardhi isiyo na mmiliki wala hakuna anayenufaika nayo.
[2] Ina maana ya kuwa yeyote atakayelima katika ardhi tupu, basi ni yake, maadamu kuwa ardhi hiyo si miliki ya Muislamu au Dhimmi (asiyekuwa Muislamu anayeishi katika nchi ya Kiislamu). Baadhi ya Wanazuoni wana mtazamo kuwa kuomba ruhusa serikali husika nalo ni jambo la lazima, kwa wengine sivyo.
[3] Wakati wa Jaahiliyya ilikuwa ni ada mkuu wa ukoo au kabila kutenga ardhi yenye rutuba kulishia mifugo yao. Jambo hili limekatazwa katika Uislamu. Hata hivyo, kiongozi au mkuu wa nchi anaweza kutenga ardhi kama Swadaqah katika njia ya Allaah. Ardhi iliyotolewa Swadaqah kwa kulishia mifugo ni ya Allaah na Nabiy wake. Mkuu wa nchi hawezi kutumia ardhi hii kwa maslaha yake au mifugo yake.
[4] Hima ni ardhi ambayo si milki ya mtu. Kiongozi wa Waislamu huwa anaizuwia kwa ajili ya maslahi fulani kama vile kuwalisha wanyama wa Zakaah na kwa dharura nyinginezo.
[5] Katika lugha ya kiarabu Dhwaraar ina maaana ya kumdhuru na kumuumiza mwingine pasina haki, na Dhwiraar ni kulipa kisasi kwa aliyeanza kukudhuru. Hadiyth hii ni kanuni ya msingi. Shariy’ah haitaki kudhuru au kudhuriwa kwa yeyote. Mbali na haya kuna maelezo mengi kuhusu Hadiyth hii. Mifano ni mingi katika maisha yetu ambayo watu kwa makusudi wamedhamiria kuwaudhi wenzao mara kwa mara.
[6] Kwa ajili ya ujengaji wa nyumba, kuzungushia ukuta kwa kadiri ya uchache wa futi tatu kuenda juu inathibitisha kuwa ni aliyefanya hivyo, muda wa kuwa ardhi hiyo haina mwenyewe. Hata hivyo, kuthibitisha uhalali wa ardhi ya kilimo ni kwa kulima.
[7] Yaani atakayechimba kisima kwa maslahi ya watu, Shariy’ah inamruhusu kuwa na nafasi ya dhiraa arubaini kuzunguka kisima kwa ajili ya mifugo yake.
[8] Huyu ni ‘Alqamah bin Waail bin Hujr Al-Hudhrami Al-Kufi, alipokea Hadiyth hii kutoka kwa baba yake na kwa Al-Mughiyrah.
[9] Hii ina maana katika dola ya Kiislamu inaruhusiwa kukata kipande cha ardhi kumpa mtu fulani. Kuna aina mbili za hali hii: kutoa kama milki yake na kuruhusu kutumia ardhi kwa muda fulani.
[10] Hapa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akizungumza na wale aliokuwa nao pamoja.
[11] Dola kutoa zawadi au hiba kwa mtu aliyeutumikia Uislamu na Ummah wake, inaruhusiwa na ni halaal kishariy’ah maadamu kuwa ardhi hiyo si milki ya mtu binafsi. Ama mtu kuzawadiwa kwa kusaliti akipewa na dola isiyokuwa ya Kiislamu ni haraam.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْوَقْفِ
17-Mlango Wa Waqf[1]
785.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِذَا مَاتَ اَلْإِنْسَانُ اِنْقَطَعَ عَنْهُ عَمَلُهُ إِلَّا مِنْ ثَلَاثٍ: صَدَقَةٍ جَارِيَةٍ ، أَوْ عِلْمٍ يُنْتَفَعُ بِهِ، أَوْ وَلَدٍ صَالَحٍ يَدْعُو لَهُ} رَوَاهُ مُسْلِم
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanadamu akifa amali yake hukatika ila kwa mambo matatu: Swadaqah inayoendelea, na ilmu inayonufaisha, au mtoto mwema anayemuombea du’aa.” [Imetolewa na Muslim]
786.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {أَصَابَ عُمَرُ أَرْضًا بِخَيْبَرَ ، فَأَتَى اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَسْتَأْمِرُهُ فِيهَا ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ ! إِنِّي أَصَبْتُ أَرْضًا بِخَيْبَرَ لَمْ أُصِبْ مَالًا قَطُّ هُوَ أَنْفَسُ عِنْدِي مِنْهُ قَالَ: " إِنْ شِئْتَ حَبَسْتَ أَصْلَهَا ، وَتَصَدَّقْتَ بِهَا " . قَالَ: فَتَصَدَّقَ بِهَا عُمَرُ ، غَيْرَ أَنَّهُ لَا يُبَاعُ أَصْلُهَا، وَلَا يُورَثُ ، وَلَا يُوهَبُ ، فَتَصَدَّقَ بِهَا فِي اَلْفُقَرَاءِ ، وَفِي اَلْقُرْبَى ، وَفِي اَلرِّقَابِ ، وَفِي سَبِيلِ اَللَّهِ ، وَابْنِ اَلسَّبِيلِ ، وَالضَّيْفِ ، لَا جُنَاحَ عَلَى مَنْ وَلِيَهَا أَنْ يَأْكُلَ مِنْهَا بِالْمَعْرُوفِ ، وَيُطْعِمَ صَدِيقاً} غَيْرَ مُتَمَوِّلٍ مَالًا مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ .
وَفِي رِوَايَةٍ لِلْبُخَارِيِّ: {تَصَدَّقْ بِأَصْلِهِ ، لَا يُبَاعُ وَلَا يُوهَبُ ، وَلَكِنْ يُنْفَقُ ثَمَرُهُ}
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “’Umar alipata ardhi huko Khaybar. Akamuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akimuomba amri na ushauri katika ardhi hiyo. Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Nimepata ardhi Khaybar, sijawahi kupata mali iliyo nzuri zaidi kwangu kuliko hiyo (utaniamuru nifanyeje?). Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ukipenda, uizuie waqf asili yake na uitoe swadaqah yake.” ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) akaitoa swadaqah isipokuwa asili yake haiuzwi wala hairithiwi wala haitolewi hiba. ‘Umar akalitoa swadaqah kwa mafukara, jamaa zake wa karibu, watumwa na katika Njia ya Allaah, msafiri na mgeni. Hapana ubaya kwa anayelisimamia kula ndani yake kwa wema na amlishe rafiki ila asilimbikize mali kwa ajili yake.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
Katika Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy imesema: “Akatoa swadaqah asili yake, lakini kwa sharti isiuzwe[2] wala kutolewa kama hiba ila matunda yake hutolewa (kugawiwa watu).”
787.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {بَعَثَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عُمَرَ عَلَى اَلصَّدَقَةِ . .} اَلْحَدِيثَ ، وَفِيهِ :{وَأَمَّا خَالِدٌ فَقَدْ اِحْتَبَسَ أَدْرَاعَهُ وَأَعْتَادَهُ فِي سَبِيلِ اَللَّهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimtuma ‘Umar kuchukua Zakaah…” mpaka mwisho wa Hadiyth inasesema: “(Nabiy akasema): …ama Khaalid[3] ametoa Waqf deraya na zana zake za vita katika njia ya Allaah…”[4] [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] Waqf ni ile hali ya kuweka mali au feda na kuizuia kwa ajili ya kutumika kwa maslahi ya Ummah, na kubakia asili yake katika uangalizi na siyo kuuzwa, kurithi au kutoa zawadi. Huku ni kama vile mtu kutoa nyumba au sehemu yake kulipia mahitaji ya Msikiti.
[2] Waqf hairuhusiwi kuuzwa. Mdhamini wa Waqf anaweza kuchukua kiasi kidogo cha kuikimu familia yake.
[3] Huyu ni Abuu Sulaymaan Khaalid bin Al-Waliyd bin Al-Mughiyrah Al-Makhzuwm Al-Qurayshi. Mama yake akiitwa Asmaa alikuwa Lubaabah mdogo mtoto wa Al-Haarith na dada wa Ummul-Fadhwl. Khaalid alisilimu mwaka wa 8 Hijriyyah kabla ya ufunguzi wa Makkah. Inasemekana vile vile kuwa alisilimu mwaka wa 5 au wa 6 Hijriyyah. Alishiriki katika ufunguzi wa Makkah katika vita vya Hunayn na Tabuwk. Panga tisa zilikatika mkononi mwake alipokuwa akipigana katika vita vya Mu’ta, wakati huo ndipo Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipompa jina la ‘Upanga wa Allaah’. Abuu Bakr alimtuma kupigana katika vita vya Ar-Ridda (walioritadi), na baada ya hapo akavamia Fursi. Alitumwa Shaam na akateka ardhi nyingi huko na akaendelea kubaki huko hadi ukhalifa wa ‘Umar akiwa kamanda mkuu wa majeshi ya Kiislam Shaam, ‘Umar bin Al-Khatwaab alimuzulu Khaalid. Baada ya hapo Khaalid alikuwa ni muangalizi wa kujitolea wa mji wa Hims hadi alipofariki mwaka wa 21 Hijriyyah, alizikwa katika kijiji kimoja umbali wa maili moja nje ya mji wa Hims.
[4] ‘Umar alidhania kuwa Khaalid alibaki na deraya kwa ajili ya kufanyia biashara. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimjulisha ‘Umar kuwa Khaalid alizitoa deraya kama zile kama Waqf kwa njia ya Allaah.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْهِبَةِ
18-Mlango Wa Kutoa Hiba[1]
788.
عَنْ اَلنُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ أَبَاهُ أَتَى بِهِ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: {إِنِّي نَحَلْتُ اِبْنِي هَذَا غُلَامًا كَانَ لِي، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " أَكُلُّ وَلَدِكَ نَحَلْتَهُ مِثْلَ هَذَا" ؟. فَقَالَ: لَا . فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " فَارْجِعْهُ" }
وَفِي لَفْظٍ: {فَانْطَلَقَ أَبِي إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ لِيُشْهِدَهُ عَلَى صَدَقَتِي. فَقَالَ: " أَفَعَلْتَ هَذَا بِوَلَدِكَ كُلِّهِمْ" ؟. قَالَ: لَا. قَالَ: " اِتَّقُوا اَللَّهَ، وَاعْدِلُوا بَيْنَ أَوْلَادِكُمْ " فَرَجَعَ أَبِي، فَرَدَّ تِلْكَ اَلصَّدَقَةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ قَالَ: {فَأَشْهِدْ عَلَى هَذَا غَيْرِي" ثُمَّ قَالَ: " أَيَسُرُّكَ أَنْ يَكُونُوا لَكَ فِي اَلْبِرِّ سَوَاءً" ؟ قَالَ: بَلَى . قَالَ: " فَلَا إِذًا}
Kutoka kwa An-Nu’maan bin Bashiyr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa baba yake alienda naye kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Mimi nimempa zawadi mtoto wangu huyu mtumwa aliyekuwa wangu. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Watoto wako wote umewazawadia kama hivyo? Akasema: Hapana. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Irudishe.”
Katika tamshi nyingine inasema: “Baba yangu akaenda kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ili amshuhudishe swadaqah yangu. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Umefanya hivi kwa wanao wote? Akasema hapana. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Mcheni Allaah na mfanye uadilifu baina ya watoto wenu.[2] Baba yangu akarejea na akairudisha swadaqah hiyo.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah nyingine ya Muslim: “Mshuhudishe jambo hili asiyekuwa mimi. Kisha akasema: Unapendezewa watoto wako wote wakufanyie wema kwa usawa? Akasema: Ndiyo. Akasema: Basi usifanye hivyo.”
789.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلْعَائِدُ فِي هِبَتِهِ كَالْكَلْبِ يَقِيءُ، ثُمَّ يَعُودُ فِي قَيْئِهِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ لِلْبُخَارِيِّ:{لَيْسَ لَنَا مَثَلُ اَلسَّوْءِ، اَلَّذِي يَعُودُ فِي هِبَتِهِ كَالْكَلْبِ يَرْجِعُ فِي قَيْئِهِ}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayeirudia hiba yake[3] ni kama mbwa anayetapika na kuyarudia matapishi yake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Al-Bukhaariy inasema: “Sisi hatuna mfano mbaya, ambaye anayerudia hiba yake ni kama mbwa, anatapika kisha anarudia matapishi yake.”[4]
790.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ، وَابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمْ، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَحِلُّ لِرَجُلٍ مُسْلِمٍ أَنْ يُعْطِيَ اَلْعَطِيَّةَ، ثُمَّ يَرْجِعَ فِيهَا، إِلَّا اَلْوَالِدُ فِيمَا يُعْطِي وَلَدَهُ"} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِم
Kutoka kwa Ibn ‘Umar na Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمْ) wamesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halaal kwa Muislamu kutoa zawadi kisha akairudia isipokuwa baba katika alichompa mtoto wake.”[5] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy, Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
791.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقْبَلُ اَلْهَدِيَّةَ، وَيُثِيبُ عَلَيْهَا} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيّ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akikubali zawadi, na akiilipa.”[6] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
792.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {وَهَبَ رَجُلٌ لِرَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَاقَةً، فَأَثَابَهُ عَلَيْهَا، فَقَالَ: " رَضِيتَ" ؟ قَالَ: لَا. فَزَادَهُ، فَقَالَ: "رَضِيتَ" ؟ قَالَ: لَا. فَزَادَهُ. قَالَ: "رَضِيتَ" ؟ قَالَ: نَعَمْ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّان
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Mtu mmoja alimpa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) hiba ngamia, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamlipa akasema: Umeridhika? Yule akasema: Hapana. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamzidishia na akasema: Umeridhika? Akasema Hapana. Akamzidishia kisha akasema: Umeridhika? Akasema: Ndiyo.” [Imetolewa na Ahmad na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
793.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ { اَلْعُمْرَى لِمَنْ وُهِبَتْ لَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ: {أَمْسِكُوا عَلَيْكُمْ أَمْوَالَكُمْ وَلَا تُفْسِدُوهَا ، فَإِنَّهُ مَنْ أَعْمَرَ عُمْرَى فَهِيَ لِلَّذِي أُعْمِرَهَا حَياً وَمَيِّتًا، وَلِعَقِبِهِ}
وَفِي لَفْظٍ: {إِنَّمَا اَلْعُمْرَى اَلَّتِي أَجَازَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنْ يَقُولَ: هِيَ لَكَ وَلِعَقِبِكَ، فَأَمَّا إِذَا قَالَ: هِيَ لَكَ مَا عِشْتَ، فَإِنَّهَا تَرْجِعُ إِلَى صَاحِبِهَا}
وَلِأَبِي دَاوُدَ وَالنَّسَائِيِّ:{لَا تُرْقِبُوا ، وَلَا تُعْمِرُوا، فَمَنْ أُرْقِبَ شَيْئًا أَوْ أُعْمِرَ شَيْئًا فَهُوَ لِوَرَثَتِهِ}
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kuzawadia ‘Umraa[7] ni kwa aliyepewa nyumba hiyo.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Muslim inasema: “Zuieni mali zenu wala msiharibu,[8] hakika anayetoa ‘Umraa basi ikiwa ni ya yule aliyezawadiwa akiwa hai na akifariki ni ya kizazi chake.”
Katika tamshi linguine inasema: “Hakika ‘Umraa aliyoijuzisha Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ni kusema: Hiba hii ni yako na vizazi vyako. Ama akisema: Hiba hii ni yako muda wa maisha yako. Basi hiba hiyo humrudia mwenyewe (aliyeitoa).”
Na katika Riwaayah ya Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy imesema: “Msitoe mali yenu kwa Ruqbaa wala ‘Umraa, atakayepewa chochote kwa njia ya Ruqbaa[9] au ‘Umraa basi ni cha warithi wake.”
794.
وَعَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {حَمَلْتُ عَلَى فَرَسٍ فِي سَبِيلِ اَللَّهِ، فَأَضَاعَهُ صَاحِبُهُ، فَظَنَنْتُ أَنَّهُ بَائِعُهُ بِرُخْصٍ، فَسَأَلْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ ذَلِكَ. فَقَالَ: " لَا تَبْتَعْهُ ، وَإِنْ أَعْطَاكَهُ بِدِرْهَمٍ …} اَلْحَدِيثَ. مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilitoa hiba farasi katika njia ya Allaah, mwenyewe hakujali (niliyempa). Nikadhani kuwa mwenyewe atamuuza kwa bei rahisi (kwa kuwa amedhoofika). Nikamuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuhusu jambo hilo akasema: Usimnunue hata akikupa kwa dirhamu moja….” Mpaka mwisho wa Hadiyth[10] [Al-Bukhaariy, Muslim]
795.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {تَهَادُوْا تَحَابُّوا} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ فِي " اَلْأَدَبِ اَلْمُفْرَدِ " وَأَبُو يَعْلَى بِإِسْنَادٍ حَسَن
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Peaneni zawadi[11] mutapendana.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy katika ‘Al-Adab Al-Mufrad’ na Abuu Ya’laa ameipokea kwa Isnaad Hasan]
796.
وَعَنْ أَنَسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {تَهَادَوْا، فَإِنَّ اَلْهَدِيَّةَ تَسُلُّ اَلسَّخِيمَةَ} رَوَاهُ اَلْبَزَّارُ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Peaneni zawadi, kwa hakika zawadi huondoa chuki.” [Imetolewa na Al-Bazzaar kwa Isnaad dhaifu]
797.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {يَا نِسَاءَ اَلْمُسْلِمَاتِ! لَا تَحْقِرَنَّ جَارَةٌ لِجَارَتِهَا وَلَوْ فِرْسِنَ شَاةٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Enyi wanawake Waislamu! Jirani asidharau kamwe kumzawadia jirani yake japo kwa kwato ya mbuzi.”[12] [Al-Bukhaariy, Muslim]
798.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ وَهَبَ هِبَةً، فَهُوَ أَحَقُّ بِهَا، مَا لَمْ يُثَبْ عَلَيْهَا} رَوَاهُ اَلْحَاكِمُ وَصَحَّحَهُ، وَالْمَحْفُوظُ مِنْ رِوَايَةِ اِبْنِ عُمَرَ، عَنْ عُمَرَ قَوْلُه
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kutoa hiba yeye ana haki zaidi madamu hajalipwa.”[13] [Imetolewa na Al-Haakim na akaisahihisha. Hata hivyo kauli yenye nguvu ni kuwa ni mapokezi ya Ibn ‘Umar kutoka kwa ‘Umar]
[1] Hiba ni zawadi kwa ajili ya kupata radhi za Allaah. Waqfu ni milki ya Ummah. ‘Umraa ni mtu kumuachia nyumba yake mtu kama zawadi muda wa umri wake kisha inarudi kwa mwenyewe. Ruqbaa ni nyumba ambayo anapewa zawadi mtu kwa sharti kama mmoja wao atakufa basi nyumba ile itabaki kwa aliye hai katika wao.
[2] Kwa mujibu wa Wanazuoni ni kwamba uadilifu na usawa miongoni mwa watoto ni jambo linalopendeza. Ama kwa mujibu wa Imaam Al-Bukhaariy na Muslim jambo hili ni la wajibu.
[3] Ni makubaliano ya Wanazuoni kuwa baba anaweza kuchukua kitu kutoka kwa mwanae na akamrudishia kama hiba (zawadi); lakini jambo hilo hilo haruhusiwi kulifanya kwa ndugu na jamaa zake wengine na akifanya hivyo itakuwa amefanya jambo la haraam.
[4] Hadiyth hii ni dalili ya uharamu wa mtu kuirudia hiba yake.
[5] Hii ina maana kuwa ni baba peke yake akimpa zawadi mtoto wake, anaweza kuirudia tena na kufanya hivyo hakufanya jambo la haraam. Kwa Wanazuoni wengi mama vile vile anaweza kufanya hivyo katika hiba.
[6] Hii ina maana kupokea zawadi kisha kuitoa zawadi hiyo kwa mwingine ni Sunnah.
[7] ‘Umraa ni kutoa nyumba kumpa mtu kukaa nayo kwa maisha yake kunaitwa ‘Umraa, ipo katika hali tatu i- Ni ile hali ya kutoa moja kwa moja, ii-Kutoa kwa muda wa umri wa mtu, iii-Kutoa kwa masharti (kwamba irudi kwa mwenyewe baada ya kifo cha aliyepewa). Tulichomaanisha hapa ni ile hali ya mwanzo na ya mwisho.
[8] Wakati ule watu walifikiri kuwa ‘Umraa ni mkopo anayepewa mtu kwa muda maalumu, na baada ya muda mwenye mali huichukuwa mali yake. Hata hivyo, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliweka jambo hili wazi kwa kusema anayeazima kitu chenyewe kinakuwa ni milki yake. Mtoaji anaweza kuwa na niyyah yoyote anapotoa zawadi, hata hivyo jambo hilo huwa haliangaliwi. Kwa hivyo basi inapendekezwa kwa mtu kabla hajatoa zawadi ya ‘Umraa afikirie vizuri kabla ya kujuta kwake.
[9] Ruqbaa ina maana ya mtu kumpa mtu mwingine nyumba yake (au anachomiliki) ili aishi humo daima, atabaki na nyumba. Hata hivyo, ikiwa aliyeazimwa akifa kabla nyumba itarudi kwa mwenyewe (mmiliki wa asili). Hii inaitwa Ruqbaa kwani kila mmoja anasubiri kifo cha mwenzake.
[10] Hadithi yenyewe inasema hivi: “’Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Nilimtoa hiba farasi katika njia ya Allaah (nikampa mmoja katika wapiganaji Jihaadi). Yule aliyekuwa naye hakumsimamia vema (yule farasi akadhoofika). Nikataka kumnunua. Nikadhani kuwa mwenyewe atamuuza kwa bei rahisi (kwa kuwa amedhoofika). Nikamuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Usimnunue wala usirudie swadaqah yako hata akikupa kwa dirhamu moja. Kwani anayeirudia hiba yake ni kama anaeyarudia matapishi yake.”
[11] Hii ina maana jambo la kupeleka au kutoa zawadi linapendeza kishariy’ah. Wapokezi wote katika mlolongo wa Hadiyth hii wana ila. Hata hivyo, wengine wanaungwa na wengine na ndio maana Hadiyth ikaonekana kuwa ni nzuri (Hasan). Angalia kitabu Irwaa Al-Ghaliyl cha Sheikh Al-Albaniy (6/44) namba (16010.
[12] Mfano huu unatufundisha mambo ya msingi kuhusu utoaji wa zawadi. Suala la zawadi halijali ukubwa au thamani ya zawadi bali chochote kile. Na atakayepokea aheshimu matakwa ya mtoaji yaani apokee kwa niyyah njema na moyo msafi.
[13] Hadiyth hii imezungumzia nukta mbili muhimu: i-Zawadi itakayotolewa ifidiwe, ii-Mtoaji anaweza kubadilisha mawazo na kuirejesha hiba yake. Hata hivyo, mapokezi haya ni dhaifu.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَللُّقَطَةِ
19-Mlango Wa Al-Luqatwah (Kiokotwa)[1]
799.
عَنْ أَنَسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {مَرَّ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بِتَمْرَةٍ فِي اَلطَّرِيقِ، فَقَالَ: " لَوْلَا أَنِّي أَخَافُ أَنْ تَكُونَ مِنَ الصَّدَقَةِ لَأَكَلْتُهَا"} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipita akaona tende akasema: Lau kama mimi sichelei tende hii kuwa ni swadaqah ningeila.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
800.
وَعَنْ زَيْدِ بْنِ خَالِدٍ اَلْجُهَنِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {جَاءَ رَجُلٌ إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَسَأَلَهُ عَنِ اللُّقَطَةِ ؟ فَقَالَ: " اِعْرِفْ عِفَاصَهَا وَوِكَاءَهَا، ثُمَّ عَرِّفْهَا سَنَةً، فَإِنْ جَاءَ صَاحِبُهَا وَإِلَّا فَشَأْنُكَ بِهَا"
قَالَ: فَضَالَّةُ اَلْغَنَمِ ؟
قَالَ: "هِيَ لَكَ ، أَوْ لِأَخِيكَ ، أَوْ لِلذِّئْبِ " .
قَالَ: فَضَالَّةُ اَلْإِبِلِ؟
قَالَ: " مَا لَكَ وَلَهَا؟ مَعَهَا سِقَاؤُهَا وَحِذَاؤُهَا، تَرِدُ اَلْمَاءَ، وَتَأْكُلُ اَلشَّجَرَ، حَتَّى يَلْقَاهَا رَبُّهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa Zayd bin Khaalid Al-Juhaniyy[2] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuuliza kuhusu kilichookotwa. Akasema: Kijue chombo chake na uzi wake kisha kitangaze mwaka mzima. Atapokuja mwenyewe utampa, na asipokuja utaangalia wewe. Na akamuuliza kuhusu mbuzi aliyepotea. Akasema: (Mchukue) ni wako au ni wa nduguyo au ni wa mbwa mwitu. Akamuuliza kuhusu ngamia aliyepotea. Akasema: Unataka kuwafanyia nini? Wana matumbo yao na miguu yao. Wanaweza kuenda kwenye maji na kula majani ya miti hadi wakutane na bwana wao.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
801.
وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ آوَى ضَالَّةً فَهُوَ ضَالٌّ ، مَا لَمْ يُعَرِّفْهَا} رَوَاهُ مُسْلِم
Kutoka kwa Zayd bin Khaalid Al-Juhaniyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayezuia mnyama aliyemuokota, mtu huyo amepotea maadamu hajamtolea taarifa.”[3] [Imetolewa na Muslim]
802.
وَعَنْ عِيَاضِ بْنِ حِمَارٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَنْ وَجَدَ لُقَطَةً فَلْيُشْهِدْ ذَوَيْ عَدْلٍ، وَلْيَحْفَظْ عِفَاصَهَا وَوِكَاءَهَا، ثُمَّ لَا يَكْتُمْ، وَلَا يُغَيِّبْ، فَإِنْ جَاءَ رَبُّهَا فَهُوَ أَحَقُّ بِهَا، وَإِلَّا فَهُوَ مَالُ اَللَّهِ يُؤْتِيهِ مَنْ يَشَاءُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ إِلَّا اَلتِّرْمِذِيَّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa ‘Iyaadhw bin Himaar[4] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayepata kitu alichookota ashuhudishe waadilifu wawili[5] na ahifadhi chombo chake na uzi wake kisha asikifiche wala asikifunike, mwenyewe akija basi ana haki (na kitu chake) na asipokuja hiyo ni mali ya Allaah Humpa Amtakaye.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa At-Tirmidhiy, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah, Ibn Al-Jaaruwd na Ibn Hibbaan]
803.
وَعَنْ عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ بْنِ عُثْمَانَ التَّيْمِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ نَهَى عَنْ لُقَطَةِ اَلْحَاجِّ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa ‘Abdur-Rahmaan bin ‘Uthmaan At-Taymiyy[6] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza mtu kuokota alichopoteza Haajj (mwenye kuhiji).”[7] [Imetolewa na Muslim]
804.
وَعَنْ اَلْمِقْدَامِ بْنِ مَعْدِ يكَرِبَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَلَا لَا يَحِلُّ ذُو نَابٍ مِنَ السِّبَاعِ، وَلَا اَلْحِمَارُ اَلْأَهْلِيُّ، وَلَا اَللُّقَطَةُ مِنْ مَالِ مُعَاهَدٍ، إِلَّا أَنْ يَسْتَغْنِيَ عَنْهَا} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ
Kutoka kwa Al-Miqdaam bin Ma’d Yakrib[8] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Fahamuni! Si halaal kula wanyama mwitu, wala kula punda wa mjini, wala kuokota kutoka katika mali ya dhimmi[9] isipokuwa kiwe ni kitu kisichohitajika.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd]
[1] Al-Luqatwah ni kitu kilichoanguka au kupotea. Shariy’ah imegawanya katika mafungu matatu: i-kama ni kitu duni au chakula kinaweza kuokotwa na kuliwa. ii-Kitu cha kawaida kisicholiwa; kinaweza kuokotwa na mtu atangaze hadharani siku tatu. iii-Kitu chenye thamani ambacho shariy’ah inaamrisha; Kikiokotwa kitangazwe muda wa mwaka. Kisha ikiwa mweyewe atapatikana arudishiwe. Laa sivyo kinaweza kutumiwa. Kuna rai za kukhitilafiana kuhusu nukta hii kama kurudishiwa mwenyewe au laa ikiwa atapatikana mwenyewe baada ya kuwa kimeshatumiwa.
[2] Lakabu yake ni ni Abuu ‘Abdir-Rahmaan au Abuu Twalhah Zayd bin Khaalid Al-Juhaniyy Al-Madaniy, ni mkazi wa Madiynah. Swahaba maarufu. Alikuwa amebeba bendera ya watu wa kabila la Juhaynah katika siku ya Fat-h Makkah (Ufunguzi wa Makkah). Aliishi katika mji wa Kufa. Alifariki Madiynah mwaka wa 78 Hijriyyah akiwa na umri wa miaka 85.
[3] Ikiwa mtu ataokota kitu kilichopotea au kumuanguka mtu na akawa na niyyah ya kukitangaza, au kuwazuiwa watu anaodhania wakichukua hawatotangaza inafaa kufanya hivyo. Kuchukua au kuokota kitu kwa niyyah mbaya ya kukihodhi haitakiwi na ni jambo ambalo halipendezi kishariy’ah.
[4] ‘Iyaadhw bin Himaar At-Tamiym Al-Mujashi’ ni Swahaba aliishi Basra (‘Iraaq) hadi miaka ya 50 Hijriyyah
[5] Ikiwa kilichookotwa chenyewe ni kitu kilichopotea au kilichodondoka, wanahitajika mashahidi wawili mara moja. Vile vile, wakati wa mwenyewe kuja kukichukua mashahidi waitwe vile vile kushuhudia. Mashahidi wote hao ni muhimu sana. Hii ni kwa sababu mwenye nacho akishachukua anaweza kujitokeza mtu mwingine ambaye atatoa wasifu ule ule wa kiokotwa na kudai kuwa ni chake na hili litapelekea kwenye mzozo.
[6] ‘Abdur-Rahmaan bin ‘Uthmaan At-Taymiyy Al-Qurayshi, ni mpwa wa Twalhah bin ‘Ubaydillaah, ni Swahaba. Inasemekana kuwa pamoja ya kuwa aliishi katika zama za Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) lakini hakuwahi kukutana naye. Alisilimu wakati wa Hudaybiyah au katika Fat-h ya Makka. Aliuawa pamoja na ‘Abdullaah bin Az-Zubayr katika mwaka 73 Hijriyyah.
[7] Hii ni kwa sababu Haajj ni msafiri na ni nadra kwa Haaj kukutana na aliyeokota kiokotwa, ndiyo maana ikawekwa amri ya kutookota alichokipoteza au alichokiangusha Haajj. Na hii ni zaidi kwa mwenye niyyah ya kukimiliki.
[8] Al-Miqdaam bin Ma’d Yakrib bin ‘Amr Al-Kindiy, aliyejulikana kwa Abuu Karimah au Abuu Yahya. Alikuwa ni Swahaba maarufu. Aliishi Shaam na Hadiyth yake ilienea kwa watu wengi sana katika watu wake. Alifariki mwaka 47 Hijriyyah akiwa na umri wa miaka 91.
[9] Dhimmi ni kafiri anayeishi katika Dola ya Kiislamu na anayefuata shariy’ah za nchi na Mu’ahid mtu kafiri anayetembelea nchi za Kiislamu akiwa na ruhusa ya kusafiri visa na akifanya shughuli zake kwa amani. Dola ya Kiislamu ni jukumu lake kuangalia amani yake na mali zake n.k. Hakuna tofauti kati ya kiokotwa cha dhimmi, Mu’ahid na Muislamu kadiri ya shariy’ah ya kiokotwa inavyohusika. Hata hivyo kikiwa ni kitu duni kinaweza kuokotwa.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْفَرَائِضِ
20-Mlango Wa Faraaidhw (Mafungu Ya Wanaorithi)[1]
805.
عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَلْحِقُوا اَلْفَرَائِضَ بِأَهْلِهَا، فَمَا بَقِيَ فَهُوَ لِأَوْلَى رَجُلٍ ذَكَرٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Wapeni mafungu wenye mafungu yao[2] kitakachobaki (baada ya kuwapa wenye mafungu yao) ni cha mwanamume aliye karibu zaidi (na maiti).” [Al-Bukhaariy, Muslim]
806.
وَعَنْ أُسَامَةَ بْنِ زَيْدٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَرِثُ اَلْمُسْلِمُ اَلْكَافِرَ، وَلَا يَرِثُ اَلْكَافِرُ اَلْمُسْلِمَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Usaamah bin Zayd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muislamu hamrithi kafiri wala kafiri hamrithi Muislamu.”[3] [Al-Bukhaariy, Muslim]
807.
وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ فِي بِنْتٍ، وَبِنْتِ اِبْنٍ، وَأُخْتٍ { قَضَى اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "لِلِابْنَةِ اَلنِّصْفَ، وَلِابْنَةِ اَلِابْنِ اَلسُّدُسَ تَكْمِلَةَ اَلثُّلُثَيْنِ وَمَا بَقِيَ فَلِلْأُخْتِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesimulia katika kumrithisha binti, binti ya mtoto wa kiume na dada: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alihukumu binti apate nusu, binti ya mtoto wa kiume apate sudus kukamilisha thuluthi mbili[4] na kilichobakia ni cha dada.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
808.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرٍو رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَتَوَارَثُ أَهْلُ مِلَّتَيْنِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ إِلَّا اَلتِّرْمِذِيَّ وَأَخْرَجَهُ اَلْحَاكِمُ بِلَفْظِ أُسَامَةَ. وَرَوَى النَّسَائِيُّ حَدِيثَ أُسَامَةَ بِهَذَا اَللَّفْظِ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Wenye dini tofauti hawarithiani.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa At-Tirmidhiy, Al-Haakim ameipokea kwa maneno ya Usaamah; na An-Nasaaiy ameitaja Hadiyth ya Usaamah kwa tamshi hili]
809.
وَعَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَينٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: جَاءَ رَجُلٌ إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: {إِنَّ اِبْنَ اِبْنِي مَاتَ، فَمَا لِي مِنْ مِيرَاثِهِ؟ فَقَالَ: " لَكَ اَلسُّدُسُ " فَلَمَّا وَلَّى دَعَاهُ، فَقَالَ: "لَكَ سُدُسٌ آخَرُ" فَلَمَّا وَلَّى دَعَاهُ. فَقَالَ : "إِنَّ اَلسُّدُسَ اَلْآخَرَ طُعْمَةٌ} رَوَاهُ أَحْمَدُ وَالْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ
وَهُوَ مِنْ رِوَايَةِ اَلْحَسَنِ اَلْبَصْرِيِّ عَنْ عِمْرَانَ، وَقِيلَ : إِنَّهُ لَمْ يَسْمَعْ مِنْهُ
Kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Mtoto wa mtoto wangu amefariki, nitapata nini katika mirathi yake? Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Utapata sudusi. Alipogeuka alimuita akasema: Utapata sudusi nyingine.[5] Alipogeuka tena alimuita tena akasema: Ile sudusi nyingine ni ziada.”[6] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
Nayo ni katika Riwaayah ya Al-Hassan Al-Baswriyy[7] kutoka kwa ‘Imraan na inasemekana kuwa hajamsikia.
810.
وَعَنِ ابْنِ بُرَيْدَةَ، عَنْ أَبِيهِ، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ جَعَلَ لِلْجَدَّةِ اَلسُّدُسَ، إِذَا لَمْ يَكُنْ دُونَهَا أُمٌّ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ ، وَقَوَّاهُ اِبْنُ عَدِيٍّ
Kutoka kwa Ibn Buraydah naye kutoka kwa baba yake amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amempa bibi[8] sudusi iwapo hakuna mama pamoja naye.”[9] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah, Ibn Al-Jaaruwd na akaipa nguvu Abn ‘Adiyy
811.
وَعَنْ اَلْمِقْدَامِ بْنِ مَعْدِ يكَرِبَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلْخَالُ وَارِثُ مَنْ لَا وَارِثَ لَهُ} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ سِوَى اَلتِّرْمِذِيِّ، وَحَسَّنَهُ أَبُو زُرْعَةَ اَلرَّازِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Al-Miqdaam bin Ma’d Yakrib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mjomba ni mrithi wa asiyekuwa na mrithi.”[10] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa At-Tirmidhiy, na Abuw Zur’ah Ar-Raaziy amesema ni Hasan, na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim
812.
وَعَنْ أَبِي أُمَامَةَ بْنِ سَهْلٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {كَتَبَ مَعِي عُمَرُ إِلَى أَبِي عُبَيْدَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمْ، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: " اَللَّهُ وَرَسُولُهُ مَوْلَى مَنْ لَا مَوْلَى لَهُ، وَالْخَالُ وَارِثُ مَنْ لَا وَارِثَ لَهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ سِوَى أَبِي دَاوُدَ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Abuu Umaamah bin Sahl[11] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “’Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alimuandikia barua Abuu ‘Ubaydah[12] kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: Allaah na Rasuli wa Allaah ni Wasimamizi wa asiyekuwa na msimamizi. Mjomba ni mrithi wa asiyekuwa na mrithi.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Ibn Maajah) isipokuwa Abuu Daawuwd, na At-Tirmidhiy amesema ni Hasan, na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
813.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِذَا اِسْتَهَلَّ اَلْمَوْلُودُ وُرِّثَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema “Mtoto aliyezaliwa akilia, anarithi.”[13] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
814.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَيْسَ لِلْقَاتِلِ مِنَ الْمِيرَاثِ شَيْءٌ} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَقَوَّاهُ اِبْنُ عَبْدِ اَلْبَرِّ، وَأَعَلَّهُ النَّسَائِيُّ، وَالصَّوَابُ: وَقْفُهُ عَلَى عُمَرَ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Muuaji hana chochote katika mirathi.”[14] [Imetolewa na An-Nasaaiy, Ad-Daaraqutwniy na akaipa nguvu Ibn ‘Abdi-Barr, na akaidhoofisha An-Nasaaiy. Lakini sawa ni kuwa Hadiyth hii ni Mawquwf]
815.
وَعَنْ عُمَرَ بْنِ اَلْخَطَّابِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ:{مَا أَحْرَزَ اَلْوَالِدُ أَوْ اَلْوَلَدُ فَهُوَ لِعَصَبَتِهِ مَنْ كَانَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ اَلْمَدِينِيِّ، وَابْنُ عَبْدِ اَلْبَرِّ
Kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khatwaab (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Anachochukua baba au mtoto (katika walaa) ni cha ‘Aswabah yake[15] yeyote awaye.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Ibn Maajah, na akaisahihisha Ibn Al-Madiyniy na Ibn ‘Abdil-Barr]
816.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلْوَلَاءُ لُحْمَةٌ كَلُحْمَةِ اَلنَّسَبِ، لَا يُبَاعُ، وَلَا يُوهَبُ} رَوَاهُ اَلْحَاكِمُ: مِنْ طَرِيقِ اَلشَّافِعِيِّ، عَنْ مُحَمَّدِ بْنِ اَلْحَسَنِ، عَنْ أَبِي يُوسُفَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَأَعَلَّهُ اَلْبَيْهَقِيُّ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Walaa[16] ni udugu kama udugu wa nasaba, hauuzwi wala hautolewi hiba (zawadi).” [Imetolewa na Al-Haakim kwa njia ya Ash-Shaafi’iyy kutoka kwa Muhammad bin Al-Hasan[17] kutoka kwa Abuw Yuwsuf,[18] na akaisahihisha Ibn Hibbaan, na akaitia kasoro Al-Bayhaqiyy]
817.
وَعَنْ أَبِي قِلَابَةَ، عَنْ أَنَسٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَفْرَضُكُمْ زَيْدُ بْنُ ثَابِتٍ} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ سِوَى أَبِي دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ، وَأُعِلَّ بِالْإِرْسَالِ
Kutoka kwa Abuu Qilaabah[19] kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mjuzi wenu katika Faraaidhw (Mirathi) ni Zayd bin Thaabit.”[20] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa Abuu Daawuwd, na akaisahihisha At-Tirmidhiy, Ibn Hibbaan na Al-Haakim, na imepewa dosari kuwa ni Mursal]
[1] Faraaidhw ni wingi wa Fardhw yenye maana ya Shariy’ah inayohusu ugawaji wa mirathi.
[2] Hawa ni watu wenye mafungu kama walivyotajwa katika Qur-aan nao wanaitwa Dhul-Faraaidhw na warithi wengine wanaowezekana kurithi huitwa ‘Aswabah. Baadhi ya Dhul-Faraaidhw ni ‘Aswabah vile vile. Katika Qur-aan aina sita za mafungu zimetajwa. Hizi ni: Nusu, moja ya nne (robo), moja ya nane (thumuni), theluthi mbili, theluthi moja na sudusi.
[3] Hii ikiwa miongoni mwa waliokufa kuna jamaa wasiokuwa Waislamu hawawezi kumrithi. Yaani Muislamu hawezi kumrithi kafiri kama ilivyo kafiri hawezi kumrithi Muislamu.
[4] Nusu kwa binti na sudusi kwa mjukuu wa kike (upande wa baba) na theluthi itakuenda kwa dada. Hii ina maana ya kuwa dada akiwa pamoja na binti na mjukuu wanakuwa ni ‘Aswabah
[5] Maiti aliacha binti wawili na babu yao kama warithi. Binti wawili watapata theluthi mbili, wakati babu atapata sudusi kama Dhul-Faraaidhw na mwingine sudusi kama ‘Aswabah. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimjulisha kuhusu sudusi ya mwanzo hapo kabla, ili asifikiri fungu lake kuwa ni theluthi kisha akamuelezea mwishoni.
[6] Mas-ala haya yako hivi. Maiti aliacha mabinti wawili na babu ambaye ndiye muulizaji, wale mabinti wawili wakapata thuluthi mbili, ikabaki thuluthi moja, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akampa yule muulizaji (Babu) sudus akamuambia “utapata sudusi nyingine ikiwa ni ziada (‘Aswabah).” Kwa hivyo babu amepata sudusi ikiwa ni fungu lake na amepata kilichobakia ikiwa ni ‘Aswabah. Tazama: anayerithi kwa ta’siyb (salio) ni mrithi asiye na kiwango maalumu kilichowekwa na Qur-aan na Hadiyth. Lakini endapo atakuwa yuko peke yake, mali yote itakuwa ni yake, na iwapo atapata fungu na kikabakia kitu hicho kitakuwa ni chake.
[7] Al-Hassan bin Abdil-Hassan Al-Baswriyy alikuwa ni mtumwa wa Kianswaar. Babake akiitwa Yassaar. Al-Hassan alikuwa ni Imaam muadilifu. Alikuwa ni madhubuti, mwenye taqwa, Mwanazuoni maarufu, fasaha na mwenye umbuji. Alikua kiongozi wa kizazi cha tatu cha Taabi’iyna, alizaliwa miaka miwili kabla ya ukhalifa wa ‘Umar bin Al-Khatwaab (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kuisha. Alipata kumuona ‘Uthmaan bin ‘Affaan na ‘Aliy bin Abiy Twaalib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) lakini hakupata kupokea Hadiyth kutoka kwao. Alifariki mwezi wa Rajab mwaka 110 Hijriyyah alipokuwa ana miaka 90 takriban.
[8] Bibi kwa lugha ya kiarabu ni Jaddah Swahiyhah (mama mzaa baba) na Jaddah Fasiydad (mama mzaa mama). Ikiwa mama wa aliyekufa hayupo, fungu la mama litakuenda kwa mama mzaa baba au mama mzaa mama. Ikiwa wote wapo watagawana fungu hilo.
[9] Lau mama atakuwa pamoja naye angalimzuia nyanya kurithi kishariy’ah.
[10] Hadiyth hizi ni dalili kuwa ikiwa hakuna ‘Aswabah au Dhul-Faraaidhw (wenye undugu na maiti), kwa hali hiyo basi mjomba anakuwa mrithi. Hii ina maana kwamba mjomba ni mrithi wa mwisho. Ikiwa naye mjomba huyo hayupo mali hiyo itakuenda kwenye Baytul-Maal. Mama mdogo ana nafasi kama nafasi aliyokuwa nayo mjomba.
[11] Jina lake ni As’ad au Sa’d lakini alikuwa akijulikana zaidi kama Abuu Umaamah bin Sahl bin Hunayf bin Wahiyb Al-Answaar Al-Aws Al-Madaniy. Alikuwa ni Swahaba na alimuona Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) lakini hakupata kusikia Hadiyth yoyote kutoka kwake. Alifariki mwaka 100 Hijriyyah akiwa na umri wa miaka 92.
[12] Huyu ni Abuu ‘Ubaydah ‘Aamir bin ‘Abdillaah bin Al-Jarraah bin Hilaal Al-Qurayshi Al-Fihri. Alikuwa ni mmoja katika kumi waliobashiriwa Jannah. Alisilimu mapema na alihamia Uhabeshi katika Hijrah ya pili. Alishiriki vita vya Badr na vita vinginevyo muhimu pia. Siku ya Uhud alipoteza meno yake mawili alipojaribu kutoa pete ya kofia ya chuma ilipoingia katika kidevu cha Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Abuu ‘Ubaydah aliliongoza jeshi la Kiislam wakati wa kuiteka Shaam. Alifariki katika ugonjwa wa ndui huko Amwaas katika mwaka wa 18 Hijriyyah akiwa na miaka 58.
[13] Hii ina maana mtoto yu hai, mtoto huyu anatakiwa kufanyiwa haki zote kama vile kuswaliwa Swalaah ya maiti kama atakufa baada ya hapo na atakuwa na haki ya kurithi na kurithiwa hali kadhalika.
[14] Muuaji hana haki ya kurithi katika mali ya aliyeuliwa. Muuaji hapati fungu lolote hata kama akiwa ni ‘Aswabah au Dhul-Faraaidhw wa aliyeuwawa. Aliyeuwa kwa kukusudia na hata kwa kutokusudia wote wako sawa katika hili kulingana na Maimaam wengi isipokuwa Imaam Maalik peke yake.
[15] Walaa (Mirathi ya mtumwa aliyeachwa huru) haigawanywi kama mirathi ya Dhul-Faraaidhw. Badili yake, wale ‘Aswabah walio karibu wana haki ya mirathi hiyo (Walaa). Hii ndiyo rai sahihi zaidi ingawaje kuna Wanazuoni wenye rai tofauti.
[16] Baada ya kifo cha mtumwa aliyeachwa huru, alichokiacha huitwa Walaa na mwenye kulipa fidia ya uhuru wake huwa ndie mrithi wake baada ya kifo chake aliyekuwa mtumwa ikiwa hana ndugu wa damu wa kumrithi.
[17] Huyu ni Abuu ‘Abdullaah Muhammad bin Al-Hassan bin Farqad, Ash-Shaybaan kwa ukoo, alikuwa mmoja wa Maimaam wa dhehebu la Hanafi. Alizaliwa mwaka 132 Hijriyyah huko Waasit na kukulia katika mji wa Kufa huko ‘Iraaq. Alisafiri ili atafute elimu ya Hadiyth na alikutana na Wanazuoni maarufu. Alihudhuria darasa la Abuu Haniyfah kwa miaka, kisha akajifunza elimu ya Fiqhi kwa Abuu Yuwsuf. Aliandika vitabu vingi muhimu na hivyo kutawanya elimu ya Imaam Haniyfah kwa watu wengi. Kadhalika alipata kusoma kwa Imaam Maalik kwa muda wa miaka mitatu. Wanazuoni wa Hadiyth wanaziona Hadiyth alizopokea kama ni dhaifu kutokana na udhaifu wa kumbukumbu yake ilivyokuwa. Alifariki mwaka 189 Hijriyyah huko Ranbuwaih, kijiji kilichopo Ar-Ray.
[18] Abuw Yuwsuf alikuwa Mwanazuoni wa Fiqhi huko ‘Iraaq. Jina lake kamili ni Imaam Al-Qaadhw Abuw Yuwsuf Ya’quwb bin Ibrahiym Al-Answaar Al-Kufi, alikua ni mfuasi wa Abuu Haniyfah. Alikulia huku akitafuta elimu. Baba yake alikuwa maskini na Abuu Haniyfah alikuwa akimsaidia baba yake mara kwa mara. Yahya bin Ma’iyn anasema: “Hakuna Mwanazuoni wa Fiqhi ambaye anafahamu Hadiyth au alikuwa madhubuti (katika upokezi wa Hadiyth) kuliko Abuw Yuwsuf.” Yahya bin Yahya At-Tamimi anasema: “Nilimsikia Abuw Yuwsuf akisema wakati wa kifo chake, najikosha na rai ya Fiqhi yoyote niliyoitoa wakati wa uhai wangu isipokuwa inayothibitishwa na Qur-aan na Sunnah katika Riwaayah nyingine isipokuwa ile iliyothibitishwa na Qur-aan na makubaliano ya Waislamu.” Alifariki mwezi wa Rabiy’ Al-Aakhir mwaka 182 akiwa na umri wa miaka 69.
[19] Abuu Qilaabah jina lake sahihi ni Zayd bin ‘Amr au ‘Aamir Al-Jurmi Al-Basri. Alikuwa ni Taabi’ maarufu, ni madhubuti na mpokezi wa Hadiyth nyingi zilizokuwa Mursal. Alikuwa katika kizazi cha sita na alifariki Shaam mwaka 104 Hijriyyah au 106 au 107 kwa kukimbia asije akapewa jukumu la Ukadhi.
[20] Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwaminifu wa Ummah huu ni Abuu Bakr; mkali zaidi wa Dini ni ‘Umar bin Al-Khatwaab; mpole zaidi miongoni mwao ni ‘Uthmaan; hakimu mzuri zaidi ni ‘Aliy msomaji mzuri wa Qur-aan ni ‘Ubay bin Ka’b; mwenye kujua halaal na haraam miongoni mwao ni Mu’aadh bin Jabal; mjuzi wao wa Faraaidhw ni Zayd bin Thaabit. Jueni kwamba, katika kila Ummah kuna amini wake na amini wa Ummah huu ni Abuu ‘Ubaydah bin Jaraah.” Katika Hadiyth hii Zayd bin Thaabit anatangulizwa kuhusu mas-ala ya migogoro katika mirathi.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْوَصَايَا
21-Mlango wa Wasia[1]
818.
عَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَا حَقُّ اِمْرِئٍ مُسْلِمٍ لَهُ شَيْءٌ يُرِيدُ أَنْ يُوصِيَ فِيهِ يَبِيتُ لَيْلَتَيْنِ إِلَّا وَوَصِيَّتُهُ مَكْتُوبَةٌ عِنْدَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Haitakiwi kwa Muislamu iwapo ana jambo linalotakiwa kuusiwa, alale siku mbili ila awe ameshaandika wasia wake[2].”[3] [Al-Bukhaariy, Muslim]
819.
وَعَنْ سَعْدِ بْنِ أَبِي وَقَّاصٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قُلْتُ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ! أَنَا ذُو مَالٍ، وَلَا يَرِثُنِي إِلَّا اِبْنَةٌ لِي وَاحِدَةٌ، أَفَأَتَصَدَّقُ بِثُلُثَيْ مَالِي؟ قَالَ: " لَا " قُلْتُ: أَفَأَتَصَدَّقُ بِشَطْرِهِ ؟ قَالَ: " لَا " قُلْتُ: أَفَأَتَصَدَّقُ بِثُلُثِهِ ؟ قَالَ: " اَلثُّلُثُ، وَالثُّلُثُ كَثِيرٌ، إِنَّكَ أَنْ تَذَرَ وَرَثَتَكَ أَغْنِيَاءَ خَيْرٌ مِنْ أَنْ تَذَرَهُمْ عَالَةً يَتَكَفَّفُونَ اَلنَّاسَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Sa’d bin Abiy Waqqaasw (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alimuambia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Ee Rasuli wa Allaah! Mimi ni mwenye mali nyingi, wala hakuna atakayenirithi isipokuwa binti yangu mmoja tu. Je nitoe swadaqah thuluthi mbili za mali yangu? Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Hapana” nikasema: “Basi nitoe nusu yake?” akasema: “Hapana” Nikasema: “Je thuluthi (moja)? Akasema: “Thuluthi,[4] na hiyo thuluthi ni nyingi, kuwaacha warithi wako wakwasi, ni bora kuliko kuwaacha mafukara wakiomba watu.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
820.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا أَنَّ رَجُلاً أَتَى اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ أُمِّي اُفْتُلِتَتْ نَفْسُهَا وَلَمْ تُوصِ، وَأَظُنُّهَا لَوْ تَكَلَّمَتْ تَصَدَّقَتْ، أَفَلَهَا أَجْرٌ إِنْ تَصَدَّقْتُ عَنْهَا؟ قَالَ: " نَعَمْ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa mtu mmoja[5] alimjia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Mama yangu amekufa ghafla wala hakuusia na nadhani lau angelizungumza, angeliamuru itolewe swadaqah, je atapata ujira nikimtolea swadaqah? Akasema: “Ndio.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
821.
وَعَنْ أَبِي أُمَامَةَ اَلْبَاهِلِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {إِنَّ اَللَّهَ قَدْ أَعْطَى كُلَّ ذِي حَقٍّ حَقَّهُ، فَلَا وَصِيَّةَ لِوَارِثٍ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ إِلَّا النَّسَائِيَّ ، وَحَسَّنَهُ أَحْمَدُ وَاَلتِّرْمِذِيُّ ، وَقَوَّاهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ ، وَابْنُ اَلْجَارُودِ
وَرَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ مِنْ حَدِيثِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، وَزَادَ فِي آخِرِهِ: {إِلَّا أَنْ يَشَاءَ اَلْوَرَثَةُ} وَإِسْنَادُهُ حَسَنٌ
Kutoka kwa Abuu Umaamah Al-Baahiliyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amemsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Kwa hakika Allaah Amempa kila mwenye haki haki yake, kwa hivyo hakuna wasia kwa mwenye kurithi.”[6] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa An-Nasaaiy, Ahmad na At-Tirmidhiy wamesema ni Hasan, Ibn Khuzaymah na Ibn Al-Jaaruwd wameipa nguvu]
Pia Ad-Daaraqutwniyy ameipokea kutoka katika Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) mwisho wake akaongeza: “…isipokuwa watakapopenda wanaorithi.” [Isnaad yake ni Hassan]
822.
وَعَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِنَّ اَللَّهَ تَصَدَّقَ عَلَيْكُمْ بِثُلُثِ أَمْوَالِكُمْ عِنْدَ وَفَاتِكُمْ، زِيَادَةً فِي حَسَنَاتِكُمْ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ
وَأَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَالْبَزَّارُ مِنْ حَدِيثِ أَبِي اَلدَّرْدَاءِ
وَابْنُ مَاجَهْ: مِنْ حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَةَ وَكُلُّهَا ضَعِيفَةٌ، لَكِنْ قَدْ يَقْوَى بَعْضُهَا بِبَعْضٍ. وَاَللَّهُ أَعْلَمُ
Kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kwa hakika Allaah Amekupeni swadaqah[7] theluthi ya mali yenu mtoe wakati wa kufa kwenu ili kuzidisha mema yenu.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniy]
Ahmad na Al-Bazzaar wameipokea kutoka katika Hadiyth ya Abuu Ad-Dardaa.
Na Ibn Maajah ameipokea kutoka katika Hadiyth ya Abuu Hurayrah. Mapokezi yote ni dhaifu. Hata hivyo zimetiliana nguvu zenyewe na zikawa ni Hasan. Allaah ni Mjuzi.
[1] Kilugha Waswiyyah (wasia) ina maana ya kuagiza, kushauri, kupendekeza kitu. Kulingana na Shariy’ah ni wasia anaoacha (kwa theluthi moja) ya mali ya marehemu kutumika baada ya kifo chake.
[2] Kabla ya kuteremka kwa Aayah ya mirathi, kuweka wasia ilikuwa ni wajibu. Hata hivyo baada ya Wahyi huu amri hii ilibatilishwa. Hata hivyo inawezekana mtu akaweka wasia katika yasiyokuwa mambo ya kurithi. Leo hii, suala hili limekuwa muhimu sana, kwa mfano kwa mtu kuwepo na mtoto wake pamoja nae kuweka wasia kwa ajili ya mjukuu wa mtoto wa aliyefariki. Uandishi wa wasia sio muhimu. Hata hivyo ni muhimu kuthibitisha wasia uliotamkwa, ili kuzuia sintofahamu yoyote inayoweza kujitokeza huko mbeleni.
[3] Katika Riwaayah nyingine ya Muslim imesema: “Awe atalala masiku matatu.” Ibn ‘Umar amesema: “Tangu nimsikie Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema maneno hayo sijapitiwa na usiku ila wasia wangu uko kwangu.”
[4] Wasia unaweza kuweka kwa thamani ya juu zaidi isizidi theluthi moja tu kwa mali yote mtu anayomiliki. Ikiwa ni chini ya theluthi ni bora. Hata hivyo kwa niaba ya warithi wengine anaweza kuusia zaidi ya theluthi moja ikiwa warithi wenyewe wako hai, vinginevyo hairuhusiwi kuusia zaidi ya theluthi moja.
[5] Mtu huyu alikuwa ni Sa’d bin ‘Ubaadah. Tunajifunza katika Hadiyth hii kuwa watoto wa kike na wa kiume wanaorithi wanaweza kutoa swadaqah katika mali ya mirathi bila ya wasia wa hilo.
[6] Hii ina maana wasia hauwekwi kwa wanaorithi, lakini kwa ruhusa ya warithi wengine, inaruhusiwa, kama ilivyo kuweka wasia wa zaidi ya theluthi moja inaruhusiwa kwa mtu yeyote kwa ruhusa ya warithi wengine.
[7] Katika lugha ya kiarabu neno Ihsaan ni kupendezesha, mtu akiwa hai mwenye nguvu anatumia mali na utajiri wake autakavyo, baada ya kufa kwake hana mamlaka na mali aliyoacha. Hapa ndipo Allaah Akamtaka mtu kuweka wasia wa theluthi ya mali yake kabla ya kufa kwake ili imuongezee katika amali yake.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْبُيُوعِ
Kitabu Cha Biashara
بَابُ اَلْوَدِيعَةِ
22-Mlango Wa Al-Wadiy’ah (Kuweka Amana)
823.
عَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ ، عَنْ أَبِيهِ ، عَنْ جَدِّهِ، عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ أُودِعَ وَدِيعَةً، فَلَيْسَ عَلَيْهِ ضَمَانٌ} أَخْرَجَهُ اِبْنُ مَاجَهْ، وَإِسْنَادُهُ ضَعِيفٌ.
وَبَابُ قَسْمِ اَلصَّدَقَاتِ تَقَدَّمَ فِي آخِرِ اَلزَّكَاةِ .
وَبَابُ قَسْمِ اَلْفَيْءِ وَالْغَنِيمَةِ يَأْتِي عَقِبَ اَلْجِهَادِ إِنْ شَاءَ اَللَّهُ تَعَالَى.
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb naye kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuwekewa amana hana dhamana.”[1] [Imetolewa na Ibn Maajah na Isnaad yake ni dhaifu]
Mlango wa kugawa Zakaah umetangulia katika mwisho wa “Kitabu cha Zakaah.”.
Mlango wa kugawa Fay na Ghaniymah utakuja baada ya “Kitabu cha Jihaad” In Shaa Allaah
[1] Tofauti kati ya amaanah (amana) na ‘aariyah (mkopo) ni kuwa pale mtu anapoazima kwa ajili yake inakuwa ni ‘aariyah wakati amana ni ile mali mtu anayoiacha kwa mtu mwingine amuwekee. Mtu anaweza kutumia mali ya ‘aariyah kwa kuazima na kutumia lakini mali ya amaanah hairuhusiwi. Ikiwa ‘aariyah imeharibika na kupotea, aliyeazima itabidi alipe. Ama kuhusu mali ya amaanah ikiwa imeharibika au kuangamia kwa ajali, hatakiwi kulipa aliyewekewa dhamana, hata hivyo ikiwa mali ya amaanah imetumika au sehemu katika mali ile itabidi ailipe aliyekabidhiwa amaanah ile.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/277
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9254&title=07-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Miamala%20Ya%20Biashara%20-%20%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D9%92%D8%A8%D9%8F%D9%8A%D9%8F%D9%88%D8%B9%D9%90
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9266&title=01-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Masharti%20Yake%20Na%20Yaliokatazwa
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9267&title=02-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Khiyari
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9278&title=03-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Ribaa
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9294&title=04-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Ruhusa%20Katika%20%E2%80%98Araayaa%20Na%20Kuuza%20Mashina%20Na%20Matunda
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9382&title=05-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20%20Mlango%20wa%20As-Salam%20%28Malipo%20Ya%20Kabla%29%2C%20%20Kukopesha%20%20Na%20Kuweka%20Rahani
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9383&title=06-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Kufilisiwa%20Na%20Kuzuwia%20%28Kutumia%20Mali%29
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9390&title=07-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Suluhu
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9391&title=08-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Mlango%20Wa%20Hawala%20Na%20Dhamana
[11] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9392&title=09-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Ushirika%20Na%20Wakala
[12] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9393&title=10-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Iqrari%20%20%28Kukiri%20Kosa%29
[13] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9394&title=11-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Kuazima
[14] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9395&title=12-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Kunyang%E2%80%99anya
[15] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9396&title=13-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Ash-Shuf%E2%80%99ah%20%28Shufaa%29%20
[16] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9397&title=14-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Qiraadhw
[17] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9398&title=15-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Kumwagilia%20Musaaqaah%20%20Na%20Kukodisha
[18] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9399&title=16-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Kufufua%20Ardhi%20Iliyokufa
[19] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9400&title=17-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Waqf
[20] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9401&title=18-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Kutoa%20Hiba
[21] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9402&title=19-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Al-Luqatwah%20%28Kiokotwa%29
[22] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9403&title=20-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Faraaidhw%20%28Mafungu%20Ya%20Wanaorithi%29
[23] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9404&title=21-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20wa%20Wasia
[24] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9405&title=22-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Biashara%3A%20Mlango%20Wa%20Al-Wadiy%E2%80%99ah%20%28Kuweka%20Amana%29