كِتَابُ اَلطَّهَارَة
Kitabu Cha Twahara
Abu Maalik Kamaal Bin As-Sayyid Saalim
Imetarjumiwa na 'Abdullaah Mu'aawiyah (Abu Baasim)
Imepitiwa Na 'Abu 'Abdillaah
Alhidaaya.com
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Utangulizi Wa Alhidaaya:
Alhidaaya.com [3]
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
Tumekichagua kitabu hiki miongoni mwa vitabu vya Fiqhi kufasiriwa na kuwekwa kwenye tovuti hii, kwa sababu tumekiona ndicho kitabu sahihi zaidi cha Fiqhi kuliko vingine kutokana na Hadiyth zake kufanyiwa tahakiki na kuthibitishwa usahihi wake. Hiki ni tofauti na kitabu maarufu kijulikanacho kama Fiqhus-Sunnah cha mwanachuoni wa Ki-Misr, Sayyid Saabiq pamoja na kufanana kiasi majina yake. Mwandishi wa kitabu hiki, mwanachuoni wa Ki-Misr aitwaye Abu Maalik Kamaal Bin As-Sayid Saalim, kakiita “Swahiyh” kwa sababu ya kuhakikisha kuwa Hadiyth zote alizotolea ushahidi humo ndani, zimethibitishwa usahihi wake na wanachuoni wakubwa wa Hadiyth.
Vilevile kitabu hiki kimepitiwa na kutolewa maoni na maelezo ya kisasa kabisa na ‘Ulamaa wakubwa; Imaam Muhammad Naaswiru-Ddiyn Al-Albaaniy ambaye ni bingwa wa elimu ya Hadiyth, na pia aliyekuwa Mufti wa Saudia Imaam 'Abdil-'Aziyz bin Baaz, na Mwanachuoni Faqiyh Imaam Muhammad bin Swaalih bin 'Uthaymiyn (Allaah Awarehemu wote na Awalaze kwenye pepo ya juu kabisa).
Hizo ndizo sababu kuu za kukichagua kitabu hiki kuwa ni rejea za mafunzo ya elimu ya shariy'ah za Dini kwa wana-Alhidaaya wote na Waislam kwa ujumla.
Na bila shaka hiki ndicho kitabu cha kwanza katika vitabu vikubwa (Mijalada) cha Fiqhi kwa lugha ya kiswahili. Tunaamini Waislam wengi watanufaika kwa kazi hii na yaliyomo ndani yake.
Allaah Amlipe malipo mema Shaykh Abuu Maalik Kamaal mwandishi wa kitabu, ‘Ulamaa; Imaam Al-Albaaniy, Imaam Ibn Baaz, Imaam Ibn 'Uthaymiyn na kadhalika ndugu yetu mfasiri wa kitabu hiki, Al-Akh 'Abdallaah Mu'aawiyah ambaye bado anaendelea na kazi hiyo. Tusiwasahau hao wote kwa du'aa in shaa Allaah pamoja na wahusika wa Alhidaaya ambao wameisimamia kazi hii na nyenginezo.
Kimehaririwa tarehe 22 Rabiy'u Al-Aakhir 1440 H (29 Decemba 2018M)
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara:
001-Taarifu Ya Twahara Na Umuhimu Wake
Alhidaaya.com [3]
Maana Ya Twahara Katika Lugha Ya Kawaida:
Ni usafi na kuondosha uchafu au takataka za kihisia (kugusika) kama najsi ya mkojo au kinginecho, na za kidhahania kama kasoro (mapungufu) na maasi.
Kutwaharisha ni kusafisha, nako ni kupaweka mahala maalumu katika hali ya usafi. [Al-Libaab Sharhul Kitaab (1/10) na Ad-Durru Al-Mukhtaar (1/79)].
Ama kisharia (kitaaluma):
Ni kuondosha kinachozuia kuswali kama hadathi au najsi kwa kutumia maji (au kinginecho), au kuondosha hukmu yake kwa mchanga. [Al-Mughniy cha Ibn Qudaamah (1/12)].
Hukmu ya twahara:
Kutwaharisha najsi na kuiondosha ni jambo la wajibu ikiwa mtu atakumbuka na ataweza. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aala) Anasema:
((وَثِيَابَكَ فَطَهِّر))
((Na nguo zako zitwaharishe)) [Al-Muddath-thir (74:4)]
Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aala):
((أَن طَهِّرَا بَيْتِيَ لِلطَّائِفِينَ وَالْعَاكِفِينَ وَالرُّكَّعِ السُّجُودِ))
((Ya kwamba itakaseni Nyumba Yangu kwa ajili ya wanaoizunguka kwa kutufu na wanaojitenga humo kwa ‘ibaadah, na wanaoinama na kusujudu)). [Al Baqarah (2:125)]
Ama kujitwaharisha na hadathi, hilo ni lazima ili ruhusa ya kuswali ipatikane kwa neno lake Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
(( لَا تُقْبَلُ صَلَاةُ بغير طهور))
((Swalaah haikubaliwi bila ya wudhuu). [Swahiyh Muslim 224]
Umuhimu Wake:
1- Twahara ni sharti ya kusihi kwa sala ya mja. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((لَا تُقْبَلُ صَلَاةُ مَنْ أَحْدَثَ حَتَّى يَتَوَضَّأَ ))
((Haikubaliwi Swalaah ya mtu mwenye hadathi mpaka atawadhe)). [Imepasishwa na Al Bukhaariy (135), Muslim (225].
Kuswali na twahara ni kumtukuza Allaah. Na hadathi na janaba – ingawa si najsi zenye kuonekana – lakini hata hivyo ni najsi za kidhahania zenye kukifanya kilichoingiwa navyo kuonekana kichafu. Hivyo basi, kuwepo kwake huteteresha utukuzo kwa Allaah, na huenda kinyume na msingi wa usafi.
2- Allaah (Subhaanahu wa Ta'aala) Amewasifu wenye kujitwaharisha. Anasema:
((إِنَّ اللّهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ))
((Hakika Allaah Anawapenda wenye kutubia mara kwa mara na Anawapenda wenye kujitwaharisha)). [Al Baqarah 2:222]
Akawasifu watu wa Masjid Qubaa kwa Neno Lake:
((فِيهِ رِجَالٌ يُحِبُّونَ أَن يَتَطَهَّرُواْ وَاللّهُ يُحِبُّ الْمُطَّهِّرِينَ))
((Ndani yake kuna watu wanaopenda kujitwaharisha, na Allaah Anawapenda wenye kujitwaharisha)). [At Tawbah 9:108]
3- Kutojali au kutotilia maanani kujitakasa na najsi, ni moja kati ya sababu za kuadhibiwa watu makaburini. Imepokelewa na Ibn 'Abbaas akisema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita kwenye makaburi mawili akasema:
(( إِنَّهُمَا لَيُعَذَّبَانِ وَمَا يُعَذَّبَانِ فِي كَبِيرٍ، أَمَّا هذا فَكَانَ لَا يَسْتَنزه مِنْ بَوْلِهِ، ))
((Kwa hakika wawili (hawa) wanaadhibiwa, na hawaadhibiwi kwa jambo kubwa. (la kuwashinda kutekeleza au kujiepusha nalo). Ama huyu, alikuwa hajitakasi na mkojo wake)). [Abu Daawuud (20), An Nasaaiy (31-69), na Ibn Maajah (347) kwa Sanad Swahiyh].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara:
002-Aina Za Twahara
Alhidaaya.com [3]
Maulamaa wanaigawanya twahara ya kisharia katika vigawanyo viwili:
1- Twahara halisi, nayo ni kuondosha uchafu (najsi) unaokuwepo katika mwili, nguo na mahala.
2-Twahara ya kihukmu, nayo ni kujitwaharisha kutokana na hadathi. Twahara hii inahusiana na mwili tu, na iko aina tatu:
-Twahara kubwa, nayo ni kuoga.
-Twahara ndogo, nayo ni kutawadha.
-Na badala ya viwili hivyo vinaposhindikana, nayo ni kutayamamu.
Kwanza: Twahara Halisi
Makusudio Ya Najsi:
Najsi ni kinyume cha twahara. Ni jina la kitu chenye kuonekana kichafu kisharia. Ni lazima Muislamu ajiepushe nacho na akioshe kile kilichompata katika kitu hicho.
Aina Za Najsi:
Vitu ambavyo dalili za kisharia zimethibitisha kuwa ni najsi ni:
1, 2- Kinyesi na mkojo wa mwanadamu
Viwili hivi ni najsi kwa Ijma’a ya Maulamaa.
Dalili ya kinyesi kuwa ni najsi ni neno lake Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
(( إذَا وَطِئَ أَحَدكُمْ بِنَعْلِهِ الْأَذَى فَإِنَّ التُّرَابَ لَهُ طَهُورٌ ))
((Akikanyaga mmoja wenu kinyesi kwa kiatu chake, basi udongo ndio kitwaharisho chake)). [Abuu Daawuud (385) kwa Sanad Swahiyh].
Pia zinadulisha unajsi wake Hadiyth zote zenye kuamuru kustanji ambazo zitakuja karibuni.
Ama mkojo, ni kwa Hadiyth ya Anas kwamba bedui mmoja alikojoa ndani ya masjid na baadhi ya watu wakamnyanyukia kutaka kumpiga. Hapo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akawaambia:
((دعوه لا تزرموه))
((Mwacheni msimkatishe)).
Akasema: “Alipomaliza, aliagiza ndoo ya maji akaimimina juu yake”. [Imepasishwa na Al-Bukhaariy (6025) na Muslim (284)].
3, 4- Madhii na wadii
Madhii ni maji mepesi mno yenye kunatanata yanayotoka wakati wa matamanio ya kimwili kama kuchezeana, au mtu anapokumbuka tendo la kujimai au kuwa na hamu nalo. Maji haya hayachupi au kufuatiwa na mchoko, na mtu anaweza asiyahisi yanapomtoka. Humtoka mwanamume na mwanamke, lakini wanawake ni zaidi. [Angalia Fat-hul Baariy (1/379), na Sharhu Muslim cha An-Nawawiy (1/599)].
Nayo ni najsi kwa Ijma’a ya Maulamaa. [Angalia Al-Majmuu cha An-Nawawiy (2/6) na Al-Mughniy cha Ibn Qudaamah (1/168)].
Na kwa ajili hiyo, Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamuru kuuosha utupu maji hayo yanapotoka.
Katika Swahiyh Mbili panaelezwa kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia aliyemuuliza kuhusu madhii:
((يغسل ذكره ويتوضأ))
((Aoshe dhakari yake na atawadhe)). [Imepasishwa na Al-Bukhaariy (269) na Muslim (303)]
Ama wadii, haya ni maji mazito meupe yanayotoka baada ya kukojoa. Ni najsi kwa Ijma’a ya Maulamaa.
Imepokelewa na Ibn 'Abbaas akisema: "Manii, wadii na madhii. Ama manii, ni yale ambayo yakitoka, ni kuoga. Ama wadii na madhii (yakitoka), basi osha dhakari yako – au nyuchi zako – na tawadha wudhuu wako wa Swalaah". [Sunan Al-Bayhaqiy (1/115). Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh katika Swahiyh Sunan Abuu Daawuud (190)].
5- Damu ya hedhi
Ni kwa Hadiyth ya Asmaa binti Abuu Bakr (Radwiya Allaahu 'anhuma), amesema: "Alikuja mwanamke mmoja kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Afanyaje mmoja wetu nguo yake ikiingia damu ya hedhi?” Akasema Rasuli:
((تحته ثم تقرصه بالماء ثم تنضحه، ثم تصلي فيه))
((Ataipikicha, kisha ataikwangua kwa ncha ya kidole na maji, halafu ataisuuza, na kisha ataswalia)). [Imepasishwa na Al-Bukhaariy (227) na Muslim (291].
6- Kinyesi cha mnyama asiyeliwa
Imepokelewa toka kwa ‘Abdullah ibn Mas'uud, amesema: Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitaka kwenda haja kubwa akaniambia:
((ائتني بثلاثة أحجار))
((Niletee vijiwe vikubwa vitatu)).
Nilimpatia viwili na kinyesi cha (punda). Akachukua vijiwe viwili akakitupa kinyesi na kuniambia:
((هي رِجْسٌ ))
((Hicho ni najsi)). [Swahiyh Al-Bukhaariy (156), At-Tirmidhiy (17), An-Nasaaiy (42), na Ibn Khuzaymah ambaye ameongeza (punda wake].
Kitendo hiki kinaonyesha kwamba kinyesi cha mnyama asiyeliwa ni najsi.
7- Mate ya mbwa
Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
(( طُهُورُ إِنَاءِ أحَدِكُمْ إِذَا وَلَغَ فِيهِ الكَلْبُ أنْ يَغْسِلَهُ سَبْعَ مَرَّاتٍ أُولاَهُنَّ بِالتُّرَابِ.))
((Utwaharisho wa chombo cha mmoja wenu mbwa akikitia ulimi ni kukiosha mara saba, ya kwanza kati yake kwa udongo)). [Swahiyh Muslim (279)].
Hadiyth hii inaonyesha kwamba mate ya mbwa ni najsi.
8- Nyama ya nguruwe
Ni najsi kwa Ijma’a ya Maulamaa kwa kuelezewa wazi katika neno Lake Subhaanah:
((قُلْ لَا أَجِدُ فِي مَا أُوحِيَ إِلَيَّ مُحَرَّمًا عَلَىٰ طَاعِمٍ يَطْعَمُهُ إِلَّا أَنْ يَكُونَ مَيْتَةً أَوْ دَمًا مَسْفُوحًا أَوْ لَحْمَ خِنْزِيرٍ فَإِنَّهُ رِجْسٌ ))
(( Sema: Sioni katika yale niliyofunuliwa mimi kitu kilichoharamishwa kwa mlaji kukila isipokuwa kiwe ni nyamafu, au damu inayomwagika, au nyama ya nguruwe, kwani hayo ni uchafu )). [Al An-Aam (6:145].
9- Nyamafu
Naye ni mnyama aliyejifia mwenyewe bila kuchinjwa chinjo la kisharia. Ni najsi kwa Ijma’a ya Wanazuoni kwa neno lake Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam:
(( إِذَا دُبِغَ الإِهَابُ؛ فَقَدْ طَهُرَ))
((Ngozi ya nyamafu ikisafishwa na kukaushwa kwa madawa, basi imetwaharika)). [Swahiyh Muslim (366)].
Haviingii katika hukmu hii:
(a) Maiti ya samaki na nzige.
Viwili hivi ni twahara kwa neno lake Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((أُحِلَّتْ لَنَا مَيْتَتَانِ وَدَمَانِ: أما الميتتان فالحوت وَالْجَرَادُ ، وأما َالدمان فالْكَبِدُ ، وَالطِّحَالُ ))
((Tumehalalishiwa mfu mbili na damu mbili. Ama mfu mbili, ni samaki na nzige. Ama damu mbili, ni ini na wengu)). [Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Maajah (3218, 3314) na Ahmad (2/97) kwa Sanad Swahiyh].
(b) Mfu wa mnyama asiye na damu ya kuchuruzika
Ni kama nzi, nyuki, sisimizi, chawa na kadhalika kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
(( إذا وقع الذباب في إناء أحدكم فليغمسه كله أو ليطرحه، فإن في أحد جناحيه داء وفي الآخر شفاء))
((Akiangukia nzi katika chombo cha mmoja wenu, basi amzamishe wote au amtupe, kwani katika bawa lake moja kuna ugonjwa na katika jingine kuna ponya)).[Swahiyh Al-Bukhaariy (3320)].
(c) Mifupa ya mfu, pembe zake, kucha zake, manyoya yake na magoya yake.
Hivi vyote asili yake ni twahara. Al-Bukhaariy katika Swahiyh yake (1/342) ameeleza: “Amesema Az-Zuhriy - kuhusu mifupa ya mzoga wa mnyama kama vile tembo na wengineo - : Niliwakuta watu katika Maulamaa waliotangulia wakichana nywele na kujitia mafuta kwa vitu hivyo, nao hawaoni ubaya wowote kwa hilo”.
Hammaad amesema: “Hakuna ubaya kwa ugoya wa mfu”.
10- Kilichokatwa toka kwa mnyama aliye hai
Kilichokatwa toka kwa mnyama hai kina hukmu ya nyamafu kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((ما قطع من البهيمة وهي حية فهو ميتة))
((Kilichokatwa kwa mnyama akiwa hai, basi ni nyamafu)).[Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy (1480), Abu Daawuud (2858) na Ibn Maajah (3216)].
11- Makombo ya maji ya wanyama mwitu na wanyama wasioliwa.
Unajsi wake unagusiwa na kauli ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipoulizwa kuhusu maji ya jangwani (nyikani), na yale yanayonywewa mara kwa mara na wanyama mwitu na wanyama wasioshambulia akasema:
((إِذَا كَانَ الْمَاءُ قُلَّتَيْنِ؛ لَمْ يَحْمِلِ الْخَبَثَ))
((Maji yakiwa kullatayni, hayabebi uchafu (najsi)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Daawuud (63), An Nasaaiy (1/46), na At-Timidhiy (67). Ipo katika Swahiyh Al-Jaami’i (758)].
Ama mabaki ya paka na mfano wake, hayo ni twahara kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
(( إِنَّهَا لَيْسَتْ بِنَجَسٍ ، إِنَّهَا مِنَ الطَّوَّافِينَ عَلَيْكُمْ وَالطَّوَّافَاتِ ))
((Yeye si najsi, bali ni katika waume na wake wanaowazungukieni)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad (5/303) na Aswhaab As-Sunan. Angalia Al-Irwaa (173)].
12- Nyama ya mnyama asiyeliwa
Hii ni kwa Hadiyth ya Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Tuliipata nyama ya punda – yaani siku ya Khaybar – na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akanadi:
((إن الله ورسوله ينهاكم عن لحوم الحمر فإنها رجس، أو نجس))
((Hakika Allaah na Rasuli Wake Anakukatazeni nyama ya punda. Ni uchafu, au najsi)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (1940) na Ahmad (3/121). Ipo kwenye Al-Bukhaariy bila ya neno: (فإنها رجس)]
Na kwa Hadiyth ya Salamah bin Al Akwa'a, amesema:
“Ilipoingia jioni ya siku Khaybar imekombolewa, waliwasha mioto mingi. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akawaambia:
((ما هذه النار على أي شيئ توقدون))
((Moto huu ni wa nini? Mnauwashia kwa jambo gani?))
Wakasema: "Kwa ajili ya nyama". Akauliza:
((Ya mnyama gani?)).
Wakasema: “Nyama ya punda wa mjini”. Akasema:
((Imwageni na vivunjeni)).
Akasema mtu mmoja: “Ee Rasuli wa Allaah! Je, tuimwage na tuvioshe”? Akasema:
((Au hilo)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (1802)].
Katika Hadiyth hizi mbili, kuna dalili kwamba nyama ya punda wa mjini (kienyeji) ni najsi kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika Hadiyth ya kwanza:
((Ni uchafu, au najsi)), na katika Hadiyth ya pili kwa kukivunja chombo kwanza, kisha kuruhusu kutumika kwa kukiosha mara ya pili.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara:
003-Je Manii Ni Twahara Au Najsi?
Alhidaaya.com [3]
Wanazuoni wamehitilafiana juu ya suala hili kwa kauli mbili:
Kauli ya kwanza:
Inasema kwamba manii ni najsi. Kauli hii ameisema Abu Haniyfah na Maalik, nayo ni riwaya iliyopokelewa toka kwa Ahmad. Wamelitolea dalili hilo kwa Hadiyth ya 'Aaishah alipoulizwa kuhusu manii yaliyoingia kwenye nguo akasema: "Nilikuwa nikiyaosha kwenye nguo ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), kisha anatoka moja kwa moja kwenda kuswali huku athari ya doa la maji ikiwa katika nguo yake". [Imepasishwa na Al-Bukhaariy (230) na Muslim (289)].
Na kuosha hakuwi ila kwa kitu najsi.
Kauli ya pili:
Wenye kauli hii wamesema kuwa manii ni twahara. Kati ya waliolisema hilo ni Ash-Shaafi'i na Daawuud. Hii ni riwaya Swahiyh zaidi kati ya riwaya mbili zilizopokelewa toka kwa Ahmad. Wamelitolea dalili hilo kwa Hadiyth ya 'Aaishah kuhusu manii, aliposema: "Nilikuwa nikiyakwangua kuyatoa kweye nguo ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)”. [Hadiyth Swahiyh: Muslim (288)].
Na kwa Hadiyth yake nyingine kwamba mgeni alishukia kwa 'Aaishah na akawa anaiosha nguo yake. 'Aaishah akamwambia: "Ilikuwa inakutosha tu ikiwa utayaona, uoshe mahala pake, na ikiwa hukuyaona, unyunyizie maji kuzungukia hapo. Na bila shaka umeniona nikiyakwangua kwa umakini kwenye nguo ya Nabiy wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na yeye akaiswalia". [Hadiyth Swahiyh: Muslim (288)].
Na kutosheka kuyakwangua, kunaonyesha kuwa manii ni twahara.
Wenye kusema kuwa manii ni najsi, wamejibu kuwa kukwangua hakuonyeshi kuwa manii ni twahara, bali kunaonyesha namna ya kuyatwaharisha kama vinavyotwaharishwa viatu kwa kuvipangusa katika mchanga.
Hili linajibiwa kwa kusema kuwa 'Aaishah alipoyakwangua manii mara moja na kuyaosha mara nyingine, hilo halihukumii kuwa ni najsi, kwani nguo inaoshwa kwa kuingia makamasi, mate au uchafu. Na hivi ndivyo walivyosema baadhi ya Maswahaba kama vile Sa'ad bin Abiy Waqqaasw, Ibn 'Abbaas na wengineo. Wamesema:
"Manii ni kama makamasi na mate, jisafishe uyaondoshe japokuwa kwa kijiti." [Majmuu Al-Fataawaa (21/605)].
Na kwa hili, inadhihiri kuwa kitendo cha 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa), kinaingia katika mlango wa kujichagulia namna ya kusafisha. [Sharhu Muslim].
Hukmu ya kuwa manii ni twahara inapata nguvu tunapojua kwamba Maswahaba walikuwa wakiota wakati wa enzi ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na manii hayo yalikuwa yakiingia katika miili na nguo za baadhi yao. Na lau kama yangelikuwa ni najsi, basi ingelikuwa ni lazima kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) awaamrishe wayasafishe kama alivyowaamrisha wastanji. Na kwa kuwa hakuna yeyote aliyelinukuu hili, inajulikana kwa yakini kuwa kuyaondosha hakukuwa ni jambo la lazima. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi. [Majmuu Al-Fataawaa (21/604)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
004-Je, Pombe Ni Najsi?
Alhidaaya.com [3]
Wanazuoni wamehitilafiana juu ya hukmu ya pombe katika kauli mbili:
Kauli ya kwanza:
Pombe ni najsi.
Huu ni mwelekeo wa Jamhuri ya Maulamaa wakiwemo Maimamu wanne. Shaykh wa Uislamu yupo katika kundi hili. Na hoja yao ni Neno Lake Subhaanah:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالأَنصَابُ وَالأَزْلاَمُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ))
((Enyi walioamini! Bila shaka ulevi, kamari, kuabudu masanamu na kupiga ramli, ni uchafu katika kazi ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo ili mpate kufanikiwa)). [Al Maaidah 5:90].
Wanasema kwamba uchafu "rijsu" ni najsi, na kwa hivyo, wamehukumu kuwa pombe yenyewe ni najsi ya kihisia.
Kauli ya pili:
Pombe ni twahara.
Rai hii wameisema akina Rab-y'a, Al-Layth, Al-Muzany na watangu wema wengineo. Na imetiliwa nguvu na Ash-Shawkaany, As Swan-’aaniy, Ahmad Shaakir na Al-Albaaniy (Allaah Awarehemu). Kauli hii ndio yenye nguvu kwa dalili zifuatazo:
1- Ni kwamba katika Aayah hakuna dalili juu ya unajsi wa pombe. Na hii ni kwa njia zifuatazo:
(a) Ni kwamba neno uchafu "rijsu", ni katika visawe, kwani linabeba maana tofauti. [Angalia kitabu cha An-Nihaaya cha Ibn Al-Athyr pamoja na Lisaan Al-‘Arab, Mukhtaar As-Swihaah na Tafsiyr mbalimbali]. Kati ya maana hizo ni kitu kichafu, kitu kilichoharamishwa, kitu kibaya, adhabu, laana, ukafiri, shari, dhambi, najsi na kadhalika.
(b) Ni kwamba "sisi hatujakuta" au kugundua kauli ya mwanasalafi yeyote aliyefasiri "Ar-Rijsu" katika Aayah hii kwa maana ya najsi, bali Ibn 'Abbaas amesema kuwa "Ar-Rijsu" ni hasira, wakati Ibn Zayd amesema kwamba "Ar-Rijsu” ni shari.
(c) Kwamba neno "rijsu", mbali na Aayah hii, limekuja katika Kitabu cha Allaah katika pahala patatu, na hakuna pahala popote kati yake ambapo "rijsu" ina maana ya najsi. Katika Neno Lake Subhaanah:
((كَذَلِكَ يَجْعَلُ اللّهُ الرِّجْسَ عَلَى الَّذِينَ لاَ يُؤْمِنُون))
Hivyo ndivyo Allaah Anavojaalia unajisi (na adhabu) juu ya wale wasioamini. [Al-An’aam: 125]
…neno "Ar-Rijsu" hapa, maana yake ni adhabu.
Na katika neno Lake Subhaanah kuhusu wanafiki:
إِنَّهُمْ رِجْسٌ ۖ وَمَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ
hakika wao ni najsi, na makazi yao ni Jahannam. Ni jazaa kwa yale waliyokuwa wakiyachuma. [At-Tawbah: 95]
..makusudio ni kuwa vitendo vyao ni vichafu, yaani vibaya.
Na katika Neno Lake Subhaanah:
((فَاجْتَنِبُوا الرِّجْسَ مِنَ الْأَوْثَانِ))
Basi jiepusheni na uchafu wa (kuabudu) masanamu [Al-Hajj: 30]
..masanamu yameitwa uchafu kwa vile yenyewe ndio sababu ya makamio na adhabu, na wala makusudio sio najsi ya kukamatika, kwani mawe yenyewe na masanamu si najsi.
(d) Na ilipotuka katika Aayah kuwa pombe ipo sanjari na masanamu na upigaji ramli, hilo limekuwa ni kielelezo chenye kuengua maana ya uchafu kupelekea katika unajsi usio wa kisharia. Na ndivyo hivyo hivyo katika Kauli Yake Subhaanah:
((إِنَّمَا الْمُشْرِكُونَ نَجَسٌ ))
((Hakika washirikina ni najsi)). [At Tawbah (9:28)]
..zilipokuja dalili sahihi zinazothibitisha kuwa miili ya washirikina si najsi.
(e) Kwamba kuharamishwa pombe, hakuwajibishi kuwa ni najsi, kwani tunaona ni haramu kuvaa hariri na dhahabu ingawa vyenyewe ni twahara ikiwa ni udharura wa kisharia na kwa makubaliano ya wote.
(f) Kwamba neno "Ar-Rijsu" katika Aayah limeainishwa (muqayyad) kuwekwa ndani ya (kazi ya shaytwaan). Kwa hiyo ni uchafu wa kivitendo, kwa maana ya kuwa ni kitu kibaya au kilichoharamishwa au dhambi, na wala si uchafu wa kiini cha kitu wa kuvifanya vitu hivi kuwa ni najsi.
2- Na kati ya vinavyotolewa ushahidi juu ya utwahara wa pombe ni aliyoyasema Anas katika kisa cha kuharamishwa pombe. Anasema: "…Na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwamrisha mwenye kunadi atangaze: Jueni kwamba pombe imeharamishwa,…". Akasema: "Nikatoka nikaimwaga, ikatiririka katika barabara za Madiynah” [Swahiyh Al-Bukhaariy (2332), na Muslim (1980)].
3- Na katika kisa cha mtu aliyekuwa na mapipa mawili ya pombe
((…Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Hakika Allaah Aliyeharamisha kuinywa, Ameharamisha kuiuza)). Mtu yule akayafungulia mapipa mawili mpaka vikamalizika vilivyomo ndani yake…).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa ‘ikhraaj” na Muslim, na Maalik (1543)].
Na lau kama tembo ingelikuwa najsi, basi Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) angeliamrisha kumwagia maji juu ya ardhi ili kuitwaharisha kama alivyoamrisha kumwagia maji juu ya mkojo wa bedui, na angeliwaamuru kujikinga nayo.
4- Kwamba asili yake ni twahara, na hanukui kuhusu utwahara huo ila mnukuzi sahihi. Na kwa kuwa hakuna dalili yoyote inayothibitisha unajsi wake, pombe inabakia katika asili yake.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
005-Je Damu Ni Najsi?
Alhidaaya.com [3]
Damu ina vigawanyo:
1- Damu ya hedhi:
Damu hii ni najsi kwa makubaliano ya Maulamaa. Dalili ya unajsi wake imekwisha elezewa nyuma.
2- Damu ya mwanadamu
[Tafsiyr Al-Qurtubiy (2/221), Al-Majmuu (2/511), Al-Muhalla (1/102),Al-Kaafiy (1/110), As-Sayl Al-Jarraar na Bidaayat Al-Mujtahid (1/31), Ash Sharh Al-Mumtani-’i (1/376), As Silsilat As-Swahiyhah , na Tamaam Al-Minna (uk.50)].
Ni damu iliyosababisha mahitalifiano juu ya hukmu yake. Lililo mashuhuri kwa wafuasi wa madhehebu ya kifiqhi ni kwamba damu ni najsi, lakini hawana dalili. Isipokuwa damu imeharamishwa kwa matni ya Qur-aan katika neno Lake Aliyetukuka:
((قُل لاَّ أَجِدُ فِي مَا أُوْحِيَ إِلَيَّ مُحَرَّمًا عَلَى طَاعِمٍ يَطْعَمُهُ إِلاَّ أَن يَكُونَ مَيْتَةً أَوْ دَمًا مَّسْفُوحًا أَوْ لَحْمَ خِنزِيرٍ فَإِنَّهُ رِجْسٌ ))
(( Sema: Sioni katika yale niliyofunuliwa mimi kitu kilichoharamishwa kwa mlaji kukila isipokuwa kiwe ni nyamafu, au damu inayomwagika, au nyama ya nguruwe, kwani hiyo ni uchafu)).[Al An-‘aam (6:145)].
Kwa hiyo, kutokana na kuharamishwa kwake, wao wameichukulia kwamba ni najsi - kama walivyofanya katika pombe - na yaliyomo ndani yake hayafichikani. Lakini amenukuu zaidi ya Mwanachuoni mmoja katika Maulamaa kuwa wanakubaliana wote kwamba damu ni najsi. Maelezo zaidi yatakuja katika hilo.
Ni wakati ambapo kundi la waliokuja baadaye akiwemo Ash-Shawkaany, Siddiyq Khaan, Al-Albaaniy, Ibn ‛Uthaymiyn (Allaah Awarehemu) wameelekea kusema kuwa damu ni twahara kwa kutothibiti Ijma’a kwa upande wao. Wao wametoa dalili vilevile kwa haya yafuatayo:
1- Asili ya vitu ni twahara mpaka iwepo dalili kuthibitisha unajsi wake. Na sisi hatujui kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliamuru kuosha damu nyingine zaidi ya hedhi ingawa mtu hupatwa mara nyingi na majeraha na mfano wake. Na lau kama damu ni najsi, basi Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) angelibainisha, kwa sababu hali ya mambo inahitajia hilo.
2- Ni kwamba Waislamu waliendelea kuswali na majeraha yao, na waliweza kuchuruzikwa na damu nyingi ambayo si ya kusameheka. Na wala haikupokelewa toka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba aliamuru kuiosha, au kupokelewa kuwa wao walikuwa wakijilinda kwa hadhari isiwapate.
Amesema Al-Hasan: "Waislamu bado wanaswali wakiwa na majeraha yao". [Isnadi yake ni Swahiyh. Ameisimulia Al-Bukhaariy ikiwa ni “Mu’allaq” (1/336). Ibn Abiy Shaybah ameiunga kwa Sanad Swahiyh kama ilivyo katika Al-Fat-h (1/337)].
Na katika kisa cha Swahaba Muanswaar aliyekuwa akiswali usiku, ni kuwa mpagani alimpiga mshale, naye akauchomoa. Akampiga mwingine hadi ikafika mitatu. Kisha alirukuu, akasujudu na akaendelea na Swalaah yake na huku akivuja damu. [Hadiyth Swahiyh. Al-Bukhaariy ameifanya ni “Mu’allaq” (1/336), na Ahmad na wengineo wameseama ni “Mawsuwl”iunga, nayo ni Hadiyth Swahiyh].
Al-Albaaniy (Allaah Amrehemu) amesema: [Tamaam Al-Minnah (51,52)].
"Nayo iko katika hukmu ya Hadiyth Marfu’u, kwa vile kwa kawaida haiyumkiniki Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) asilijue hilo. Na lau kama damu nyingi ingelikuwa inabatilisha Swalaah, basi Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) angebainisha hilo, kwani haifai kuchelewesha taarifa wakati ule inapohitajika kama inavyojulikana katika taaluma ya "usuul". Na kama tutachukulia kwamba hilo lilifichikana kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), basi halifichikani kwa Allaah Ambaye hakifichikani Kwake chochote kikiwa ardhini au mbinguni. Na lau kama (damu) ingelikuwa inabatilisha au ni najsi, basi Rasuli angeliteremshiwa wahyi kama inavyojulikana kwa kila mtu".
Na katika kisa cha kuuawa ‘Umar bin Al-Khatw-twaab (Allaah Amridhie): "Umar aliswali, na huku jeraha lake linachuruzika damu". [Hadiyth Swahiyh. Maalik ameifanyia “ikhraaj”, na Al-Bayhaqiy kutoka kwake (1/357) na wengineo kwa Sanad Swahiyh].
3- Ni kwa Hadiyth ya 'Aaishah katika kisa cha kufa kwa Sa'ad bin Mu’aadh. Alisema: " Sa'ad bin Mu’aadh alipojeruhiwa siku ya Khandaq baada ya kupigwa mshale kwenye mshipa wa damu mkononi na mtu mmoja, Rasuli alimjengea hema Msikitini ili apate kumtizama kwa ukaribu. Na mara ghafla usiku, jeraha lake lilipasuka na damu ikachuruzika kwa wingi. Wakasema: Enyi wenyeji wa nyumba! Nini hiki kinatujia toka kwenu? Wakatazama. Wakashtuka kuona jeraha la Sa'ad limepasuka na damu inafoka, naye akafariki hapo hapo. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (3100) kwa ufupi, na Atw-Twabaraaniy katika kitabu cha Al-Kabiyr (6/7)].
Ninasema (Abuu Maalik): "Na wala haikupokelewa kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliamuru maji yamwagiwe juu yake na hasa pakizingatiwa kwamba yuko Msikitini kama alivyoamuru kumwagia maji juu ya mkojo wa bedui.
4- Kwamba Ibn Rushdi wakati alipotaja hitilafu za Maulamaa kwa upande wa damu ya samaki, alieleza kwamba sababu ya kuhitalifiana kwao ni kuhitilafiana kwa upande wa maiti yake. Mwenye kuzingatia kwamba maiti yake inaingia ndani ya ujumuishi wa kuharamishwa, basi na damu yake ataizingatia hivyo hivyo. Na asiyezingatia hivyo, basi ataitoa damu yake kwa kipimo cha maiti yake.
Na tunasema: "Wao wanasema kuwa maiti ya mwanadamu ni twahara, na kwa hivyo damu yake iwe hivyo hivyo kwa mujibu wa kaida yao".
Na kwa ajili hiyo, Ibnu Rushdi alisema baada yake: "Na matni ya Hadiyth ishaonyesha kwamba damu ya hedhi ni najsi. Ama damu nyingine, basi hiyo iko katika uasili uliokubaliwa na wenye kuzozana ya kwamba ni twahara. Na haitoki kwenye utwahara, ila kwa matni ya kusimamishia hoja".
Na ikiwa mtu atauliza: "Kwa nini damu ya hedhi isifanywe kipimo, na damu hii ni najsi?”
Tunasema: "Hiki ni kipimo kisichoendana, kwani damu ya hedhi ni damu ya maumbile ya asili kwa wanawake. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((ان هذا شيئ كتبه الله على بنات آدم))
((Hakika hiki ni kitu ambacho Allaah Amekiandika kwa mabinti wa Aadam (wanawake)).[Hadiyth Swahiyh. Al-Bukhaariy (294) na Muslim (1211)].
Na akasema kuhusu istihaadhwah:
((انه دم عرق))
((Hakika hiyo ni damu ya mshipa (asili)). [Hadiyth Swahiyh, Al-Bukhaariy (327) na Muslim (333)].
Kisha damu ya hedhi ni damu nzito ya mvundo na harufu kali. Inafanana na mkojo na kinyesi, si damu yenye kutoka katika zisizo njia mbili.
3- Damu ya mnyama mwenye kuliwa
Mjadala kuhusu damu hii ni kama mjadala kuhusu damu ya mwanadamu kwa upande wa kutokuwepo dalili juu ya unajsi wake. Kwa hivyo inaambatana na utwahara wa asili.
Kusema kuwa ni twahara kunaungwa mkono vilevile na:
Yaliyoelezewa na Ibn Masu’ud, amesema: "Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali mbele ya Al-Ka’abah, na Abuu Jahli na marafiki zake wamekaa. Wakaambizana: “Ni nani kati yenu anaweza kwenda kwa ngamia wa akina fulani, kisha akusanye vinyesi, damu, na matumbo yao, halafu aje amsubiri mpaka atakaposujudu, amwagie mabegani mwake”? Mwovu wao akachomoka haraka, na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliposujudu, alim-mwagia kati ya mabega yake, na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alitulia tuli katika sijdah, na wao wanacheka.[Hadiyth Swahiyh, Al-Bukhaariy (240) na Muslim (1794)].
Na lau kama damu ya ngamia ingelikuwa ni najsi, basi Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) angeliitenga kando nguo yake, au angeikatisha Swalaah yake.
Aidha, imethibiti kwa njia sahihi kwamba Ibnu Mas-’oud aliswali na tumboni mwake kuna kinyesi na damu ya ngamia aliowachinja, lakini hakutawadha. [Isnadi yake ni Swahiyh. Muswannaf ‘Abdul Razzaaq (1/25), na Ibn Abiy Shaybah (1/392)].
Athar hii inaweza kuleta mvutano katika kutolea ushahidi juu ya utwahara wa damu ya mnyama, kwa vile Ibnu Mas-’oud hakuwa akiona kwamba utwahara wa mwili na nguo ni sharti ya kusihi Swalaah, bali anaona kuwa ni jambo linalopendeza (mustahab).
Ninasema (Abuu Maalik): “Lau kama imethibiti kwa Ijma’a kwamba damu ni najsi, basi hatutaziangalia dalili za waliofuatia baadaye. Na kama haikuthibiti, basi asili ni utwahara, na sisi hatuhitajii dalili hizo. Na lililodhihiri kwangu - baada ya kuchagua kauli (isemayo kuwa) damu ni twahara kwa kipindi cha miaka kumi - ni kwamba Ijma’a katika suala imethibiti. Ijma’a hii imenukuliwa na Maulamaa wengi na hakikuthibiti chenye kuitengua. Na nukuu ya juu zaidi kati ya hizo ni yale yaliyonukuliwa toka kwa Imaam Ahmad, kisha yale aliyoyanukuu Ibn Hazm, kinyume na yule aliyedhani kwamba madhehebu yake yanasema kwamba damu ni twahara!! Na kati ya niliyoyafahamu katika hilo ni:
Ibnu Al-Qayyim katika Ighaathat Al Lahafaan (1/420) amesema:
“Ahmad aliulizwa: Je, damu na usaha kwako ni sawa"? Akasema: "Hapana, watu hawakuhitilafiana kuhusu damu".
Na alisema mara moja: "Usaha kwangu ni afadhali kuliko damu".
Na imenukuliwa toka kwa Ibnu Hazm katika Maraatib Al Ijma’a: "Maulamaa wamekubaliana kwamba damu ni najsi ".
Vile vile Al-Haafidh katika Al Fat-h (1/420) amekunukuu kukubaliana huko.
Na Ibnu ‘Abdul-Barri katika At-Tamhiyd (22/230) anasema:
"Na hukmu ya kila damu ni kama damu ya hedhi, isipokuwa damu kidogo husamehewa kwa vile Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ameweka sharti ya unajsi wa damu kuwa iwe ni yenye kuchuruzika, na hapo inakuwa ni uchafu, na uchafu ni najsi. Na hii ni Ijma’a ya Waislamu kwamba damu yenye kuchuruzika ni uchafu na najsi..".
Na Ibnu Al-Araby katika Ahkaam Al-Qur-aan (1/79) anasema:
"Maulamaa wamekubaliana kwamba damu ni haramu na ni najsi kwa kinacholiwa na haitumiwi kwa manufaa yoyote. Na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ameiainisha hapa kwa kuifanya ni damu ya aina yoyote ile (mutwlaq), na katika Suwrat Al-An 'Aam Ameiainisha kwa kuiwekea mpaka (muqayyad) ile tu ya kuchuruzika. Na Maulamaa kwa Ijma’a hapa, wameichukulia damu yoyote wakaiacha iliyoainishwa".
Na An-Nawawy katika Al-Majmu’u (2/576) amesema:
"Na dalili juu ya unajsi wa damu zinatiliana nguvu zenyewe kwa zenyewe, na mimi sijui kama kuna hitilafu yoyote toka kwa Muislamu yeyote ila tu yale aliyoyaelezea mtunzi wa Al-Haawiy toka kwa baadhi ya Maulamaa wa tawhiyd. Amesema kuwa ni twahara, lakini maneno ya Maulamaa wa tawhidi hayachukuliwi katika Ijma’a au mahitalifiano…".
Ninasema (Abuu Maalik): “Ninalolipa nguvu na uzito ni kuwa damu ni najsi kwa kuthibiti Ijma’a mpaka inukuliwe toka kwa Imaam mwingine atakayempiku Imaam Ahmad – (Allaah Amrehemu) – kwa kusema kuwa damu ni twahara. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
006- Je, Matapishi Ya Mwanadamu Ni Najsi?
Alhidaaya.com [3]
Tumetangulia kusema mara nyingi kwamba asili ya vitu vyote ni twahara, na kwamba havihamishwi toka kwenye asili yake ila kwa kinukuo sahihi cha kutolea hoja kisichopingana na kile chenye kutiliwa nguvu au kuwa sawa nacho. Na ikiwa tutalipata hilo, basi ni vizuri. Na kama hatukulipata, basi itatulazimu tusimame msimamo wa kumpinga anayedai kuwa ni najsi. Kwani kudai huku kunamaanisha kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amewajibisha kwa Waja Wake kuviosha vitu hivyo vinavyodaiwa kuwa ni najsi, na kwamba kuwepo kwake kunazuia kuswali navyo. Basi ni ipi dalili ya hilo?!
Matapishi na mfano wake, hakuna kilichothibiti kwa njia sahihi chenye kuyahamisha toka kwenye utwahara wake wa asili.
Kuna kauli ya ‘Ammaar iliyopokelewa kuhusu matapishi akisema: "Wewe utaosha nguo yako iliyoingiwa na mkojo, kinyesi, matapishi, damu na manii".
Lakini kauli hii ni dhaifu haitolewi hoja. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi.
Na imethibiti toka kwa Abu Ad-Dardaai akisema kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitapika, akafungua na akatawadha. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (2381), At-Tirmidhiy (87), Ahmad (6/443) na wengineo].
Katika Hadiyth hii, hakuna kiashirio chochote chenye kuonyesha kuwa matapishi ni najsi, na wala hakuna dalili juu ya ulazima wa kutawadha akitapika mtu, na wala haionyeshi kuwa wudhuu unatenguka kwayo, bali lengo lake ni kusunisha mtu atawadhe anapotapika. Kwani kwa kitendo tu cha Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), hakuonyeshi kuwa ni wajibu.
Pamoja na hayo, si kila chenye kutengua wudhuu kinahesabiwa kuwa ni najsi. Ibnu Hazmi amelikhitari hili, na pia Shaykh wa Uislamu katika Al-Fataawaa.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
007- Nini Hukmu Ya Majimaji Yanayotoka Kwenye
Utupu Wa Mwanamke Au Unyevunyevu Wa Utupu Wake?
Alhidaaya.com [3]
Maulamaa wana mielekeo miwili kuhusu unyevunyevu wa utupu wa mwanamke: [Al-Mughny (2/88), na Al-Majmu'u (1/570)].
Mwelekeo wa kwanza:
Ni najsi, kwa kuwa yako ndani ya utupu, si maji ya uzazi na yanafanana na madhii. Wametolea dalili kwa Hadiyth ya Zayd bin Khaalid kwamba alimuuliza 'Uthmaan bin ‘Affaan (Allaah Amridhie) akisema: "Nieleze, (nini hukmu) mtu anapomwingilia mkewe na wala hakumwaga manii? Akasema 'Uthmaan: "Atatawadha kama anavyotawadha kwa ajili ya Swalaah, na ataiosha dhakari yake". 'Uthmaan akasema: "Nimeyasikia toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)". [Isnadi Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (292), na Muslim (347), lakini imekuwa Mansuwkh]
.
Na Hadiyth ya Ubayy bin Ka-'ab kwamba alisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Inakuwa vipi mtu akimwingilia mkewe bila kumwaga? Akasema:
(يغسل ما مس المرأة منه ثم يتوضأ ويصلي)
((Ataiosha sehemu aliyomgusa nayo mwanamke, kisha atatawadha, na ataswali)). [Isnadi Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (293), na Muslim (346), lakini imekuwa Mansuwkh].
Wamesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuamrisha kuiosha sehemu iliyogusana na utupu wa mwanamke, ni dalili juu ya unajsi wa unyevu wa utupu wa mwanamke”.
“Mimi ninapinga (Abuu Maalik) kwa kusema kuwa Hadiyth hizo mbili zimenasikhiwa na Hadiyth nyingine zenye kuamrisha kuoga kama itakavyokuja katika sehemu yake inshaAllaah”. [Angalia kwenye Kitabu cha Fat-hul Baary (1/473)].
Na pia kuna uwezekano wa kuwa amri ya kuosha ni kutokana na madhii yanayomtoka mwanamume au mwanamke.
Vile vile, wametolea ushahidi juu ya unajsi wa (majimaji hayo) kwa kuwa yanatoka katika moja ya njia mbili. Na kaida inasema:
"Chenye kutoka katika njia mbili, basi ni najsi isipokuwa manii".
Mwelekeo wa pili:
Ni kwamba majimaji ya utupu ni twahara. [Angalia kwenye Jaami'i Ahkaamu An-Nasaaiy (1/68) cha Shaykh wetu Mustwafa bin Al-'Adawy Allaah Amhifadhi].
Mwelekeo huu unatolewa dalili kwa haya yafuatayo:
1- Kwamba 'Aaishah - Allaah Amridhie,- alikuwa akiyakwangua manii kutoka katika nguo ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) yakiwa yametokana na kukutana kimwili, kwani Rasuli kamwe hakuota kuwa anaingilia. [Hivi ndivyo alivyosema katika Al-Mughny (2/88). Na Shaykh wetu amesema: "Hili linahitajia matni toka katika Qur-aan au Hadiyth, na wala hatukuikuta matni katika mfano wa hili"].
Anapoingilia, hukutana na umajimaji wa utupu. Na kwa vile sisi, lau kama tungelihukumia unajsi wa utupu wa mwanamke, basi tungelihukmu unajsi wa manii yake, kwani manii hayo yanatokea kwenye utupu wake, na kwa hivyo yananajsika kwa unyevunyevu wake.
2- Kwamba majimaji haya ni jambo ambalo liko wazi, nayo huwatoka sana wanawake. Na hakuna shaka kwamba jambo hili lilikuwepo kwa wanawake katika enzi za Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kama ilivyo kwa wanawake wa zama zetu hizi. Na wala haikupokelewa kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaamrisha kuosha, au kutawadha kutokana na hali hiyo.
3- Kwamba sehemu ya kutokea majimaji haya, si sehemu ya kutokea mkojo ambao ni najsi.
4- Kwamba kauli ya Maulamaa isemayo: "Kila chenye kutoka kwenye njia mbili ni najsi isipokuwa manii", si kauli iliyopokelewa toka kwa Rasuli Al Ma’aswuwm (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na wala kauli hii haijafanyiwa Ijma’a ya Ummah. Bali imepokelewa kwamba baadhi ya vinavyotoka kwenye njia mbili havitengui wudhuu, mfano wa damu ya istihaadhwah ambayo tutakuja kuielezea mbeleni.
Ninasema (Abuu Maalik): “Ninaloliona mimi lenye nguvu, ni kwa ufafanuzi huu:
"Ikiwa majimaji haya yanamtoka mwanamke wakati wa kuchezeana na mumewe, au wakati anapokuwa na hamu ya kujamiiana na mfano wa hili hasa, basi hayo ni madhii. Na mimi nimejua kwamba madhii ni najsi ambayo ni lazima ioshwe, na pia inatengua wudhuu.
Ama ikiwa majimaji haya yanatoka kwenye utupu wa mwanamke takriban nyakati zote, na yanazidi wakati wa ujauzito, au wakati anapofanya kazi kwa bidii, au anapotembea mwendo mrefu, basi majimaji hayo ni twahara kiasili kwa kutokuwepo dalili juu ya unajsi wake. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
008-Najsi Zinazosamehewa
Alhidaaya.com [3]
Kuna kauli mbalimbali za Maulamaa kuhusu aina na kiasi cha najsi ambayo inaweza kuingia katika nguo, au mahala, au mwilini na inakuwa ni yenye kusamehewa. Isipokuwa kidhibiti cha najsi zinazosamehewa ni udharura, kuenea kwa wingi, kuwa ni vigumu kujikinga nayo, na kuwepo tabu na uzito mkubwa katika kuiondosha. [Al-Fiqh Al-Islaamiy wa Adillatuhu (169 – 177)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
009-Namna Ya Kuzitwaharisha Aina Za Najsi Zilizobainishwa na Hadiyth
Alhidaaya.com [3]
1- Kuitwaharisha nguo yenye damu ya hedhi
Inakuwa ni kwa kuikwangua na kuigandua, kisha kuisugua kwa ncha za vidole ili iachiane na itoke, kisha utaiosha kwa maji. Ni kutokana na Hadiyth ya Asmaa binti Abu Bakr, amesema: "Mwanamke mmoja alikuja kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Mmoja wetu nguo yake ikiingiwa na damu ya hedhi, afanyaje"? Akasema Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
تحته, ثم تقرصه بالماء ثم تنضحه, ثم تصلي فيه
((Ataipikicha, kisha ataikwangua kwa ncha za vidole na maji, kisha atainyunyizia maji, na halafu ataswalia)).
[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy na Muslim (291)].
Na kwa Hadiyth ya 'Aaishah, amesema: " Mmoja wetu alikuwa akipatwa na hedhi, huikwangua damu kwenye nguo yake wakati anapotwaharika, kisha huiosha, na hunyunyizia maji sehemu iliyobaki, halafu huswali nayo". [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (308), na Ibn Maajah (630)].
Na kama mwanamke atapenda kutumia kijiti au kinginecho ili kuondosha damu, au kuosha nguo kwa maji na sabuni na mfano wake katika madawa ya kusafishia, basi itakuwa ni bora zaidi.
Hii ni kwa Hadiyth ya Ummu Qays binti Muhswan, amesema: "Nilimuuliza Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu damu ya hedhi iliyoingia kwenye nguo, naye akasema:
((حكيه بضلع، واغسليه بماء وسدر))
((Ikwangue kwa ujiti, na uioshe kwa maji na mkunazi)). [Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (363), An-Nasaaiy (1/195) na Ibn Maajah (628)].
2- Kuitwaharisha nguo yenye mkojo wa mtoto mchanga
Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((يغسل من بول الجارية, ويرش من بول الغلام))
((Huoshwa ikiingia mkojo wa mtoto wa kike, na hurashiwa maji ikiingia mkojo wa mtoto wa kiume)). [Hadiyth Swahiyh “Lighayrih”. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (376), An Nasaaiy (1/158), na Ibn Maajah (526). Kuna Hadiyth kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine].
3- Kuitwaharisha nguo yenye madhii
Na kwa vile madhii yanakithiri sana kutoka na kuwa uzito kwa wengi, Allaah Mwekaji wa sharia, Ametuhafifishia namna ya kuyatwaharisha. Inatosha kuinyunyizia nguo maji sehemu iliyoingia madhii kutokana na Hadiyth ya Sahl bin Hunayf kwamba yeye alikuwa akipata tabu na uzito kutokana na madhii. Akamuuliza Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): "Ni vipi kwa yale yanayoingia katika nguo yangu? Akasema:
((يكفيك أن تأخذ كفا من ماء فتنضح به ثوبك حيث ترى أنه قد أصاب منه))
((Inakutosha kuchukua teko la maji, ukanyunyizia kwalo nguo yako pale unapoona yameingia)). [Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (210), At-Tirmidhiy, na Ibn Maajah (506)].
4- Kuitwaharisha ncha ya nguo ya mwanamke (inayoburuzika)
Inaponajsika sehemu ya nguo ya mwanamke inayoburuzika, basi hutwaharika kwa kugusana na ardhi iliyo twahara. Mwanamke mmoja alimuuliza mke wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Ummu Salamah akimwambia: "Mimi ni mwanamke ninayerefusha ncha za nguo yangu na ninatembea sehemu chafu". Ummu Salamah akamwambia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((يطهره ما بعده))
((Huitwaharisha (ardhi) iliyo baada yake)). ] Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (383), At-Tirmidhiy (143) na Ibn Maajah (531).]
5- Kuitwaharisha soli ya viatu
Imepokelewa na Abuu Sa’iyd Allaah Amridhie kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((اذا جاء أحدكم المسجد فليقلب نعليه ولينظرفيهما، فان رأى خبثا فليمسحه بالأرض، ثم ليصل بهما))
((Anapokuja mmoja wenu Msikitini, basi avipindue viatu vyake na aangalie vina nini. Ikiwa ataona najsi, basi aipanguse kwa ardhi, kisha aswali navyo)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (646)].
6- Kukitwaharisha chombo mbwa akikitia ulimi
Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((طهور اناء أحدكم اذا ولغ فيه الكلب أن يغسله سبع مرات أولاهن بالتراب))
((Kukitwaharisha chombo cha mmoja wenu mbwa akitia ulimi wake ndani, ni akioshe mara saba, ya kwanza yake kwa udongo)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (279) na Abuu Daawuud (71)].
7- Kuitwaharisha ngozi ya nyamafu
Ni kwa kusafishwa na kukaushwa kwa madawa. Ni kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((اذا دبغ الاهاب فقد طهر))
((Ngozi ya nyamafu ikisafishwa na kukaushwa kwa madawa, basi imetwaharika)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim na wengineo].
8- Kuitwaharisha ardhi iliyoingia mkojo na mfano wake
Ni kwa kumiminia maji juu yake kama alivyomrisha ((Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kumwagia maji juu ya mkojo wa bedui Msikitini. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (219) na Muslim (283)].
Bila shaka aliamuru hilo kwa ajili ya kuharakia usafi. Na kama si hivyo, lau kama angeliacha mpaka ukakauka na athari ya najsi ikaondoka, basi (ardhi) ingekuwa imetwaharika.
9- Kukitwaharisha kisima au samli inapoingia ndani yake najsi
Ni kwa kuichota na kuiondosha najsi pamoja na sehemu za pambizoni mwake, na iliyosalia inabakia twahara. Ni kwa Hadiyth ya Ibnu ‘Abbaas kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu panya aliyeangukia katika samli akasema:
((ألقوها، وما حولها فاطرحوه، وكلوا سمنكم))
((Mtupeni, na sehemu za pambizoni mwake ziondosheni, na samli yenu itumieni)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (Wanyawa wa kuchinjwa mlango wa 34)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
010-Je, Ni Lazima (Kutumia) Maji Katika Kuondoshea Najsi? Au Inajuzu Kuondoshea Kwa Vimiminika Vinginevyo Au Mada Nyinginezo?
Alhidaaya.com [3]
Maulamaa wamehitalifiana katika suala kwa kauli mbili mashuhuri:
Kauli ya kwanza:
Ni sharti kutumia maji kuondoshea najsi. Haiswihi kwa kinginecho ila kwa dalili.
Na hili ndilo mashuhuri katika madhehebu ya Maalik na Ahmad. Na pia ni madhehebu ya Ash-Shaafi'iy katika "Al-Jadyd" (rai mpya). Ash-Shawkaany na waliomfuata, ameliunga mkono hili. [Bidaayat Al-Mujtahid (1/99), Al-Ummu (1/49) na As Sayl Al-Jarraar (1/49)].
Na hoja yao ni:
1- Neno Lake Ta'aala
((وَيُنَزِّلُ عَلَيْكُم مِّن السَّمَاء مَاء لِّيُطَهِّرَكُم بِهِ))
((Na Anawateremshieni maji toka mbinguni ili Awatwaharisheni kwayo)).[Al Anfaal (8:11)]
Pamoja na dalili nyinginezo zinazotaarifu kwamba maji ni twahara.
2- Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliamuru maji yamwagwe juu ya mkojo wa bedui. [Imepasishwa na Al-Bukhaariy na Muslim].
Wamesema kwamba amri ni ya wajibu, na kwa hivyo haitoshelezi kuondosha najsi ila kwa maji!!
3- Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), kama ilivyo katika Hadiyth ya Abuu Tha'alabah, aliamuru kukiosha chombo cha Ahlul-Kitaab kwa maji. [Imepasishwa na Al-Bukhaariy na Muslim. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (5170) na Muslim (1930)].
4-Amesema Ash-Shawkaany: "Maji ndio asili katika kutwaharisha najsi kwa kusifiwa na Allaah Mpangaji sharia kuwa ni twahara yenyewe na yenye uwezo wa kutwaharisha kingine. Hivyo, haiwezekani yakaachwa kikatumika kingine ila kama litathibiti hilo toka kwa Allaah Mpangaji sharia. Na kama si hivyo, basi haiwezekani, kwani itakuwa ni kuufumbia macho ujulikano huo wa kuwa ni twahara yenye uwezo wa kutwaharisha kingine na kutumia kitu kingine kisichojulikana kuwa ni twahara chenye uwezo wa kutwaharisha kingine. Na hiyo ni kutoka nje ya vile mikondo ya kisharia inavyokwenda".
Kauli ya pili:
Inatosheleza kujitwaharisha kwa kila chenye kuweza kuondosha najsi, na si lazima maji.
Na haya ndio madhehebu ya Abuu Haniyfah, na riwaya nyingine toka kwa Maalik na Ahmad, na kauli ya zamani ya Ash-Shaafi'iy, na Ibnu Hazm. Nalo ndilo chaguo la Shaykh wa Uislamu Ibnu Taymiyah, na pia Mwanachuoni Mkubwa Ibnu 'Uthaymiyn. [Al-Badaai-’i (1/83), Fat-hul Qadiyr (1/200), Majmuu Al-Fataawaa (21/475), Al-Muhallaa (1/92-94) na Ash Sharh Al- Mumti’i (1/361-363)].
Ni kauli yenye nguvu kwa yafuatayo:
1- Kwamba maji kuwa ni twahara yenyewe na yenye uwezo wa kutwaharisha kingine, hakuzuii kingine kuwa ni chenye kutwaharisha vilevile. Kwani kaida inasema: "Kukosekana sababu maalumu, hakuhukumii kuondoka kisababisho maalumu, sawasawa ikawa dalili au isiwe dalili". Kwa vile chenye kuathiri kinaweza kuwa ni kitu kingine. Na hii ndio hali halisi kwa upande wa najsi. [Ash Sharhu Al-Mumti’i (1/362)].
Ninasema (Abuu Maalik): "Bali baadhi ya vimiminika kama vile siki na madawa ya kusafishia ya viwandani, huondosha najsi kama maji au zaidi kuliko maji".
2- Kwamba Allaah Mpangaji sharia Ameamuru kuondosha najsi kwa maji katika mambo maalumu, lakini Hakuamuru amri jumuishi kwamba kila najsi iondoshwe kwa maji.
3- Kwamba sharia imeruhusu kuondosha baadhi ya najsi bila kutumia maji kama kustanji kwa jiwe, au kuvisugua viatu kwa mchanga, au kutwaharika nguo inayoburuzika kwa ardhi, na mengineyo yaliyotangulia.
4- Kwamba kuondosha najsi hakuingii kwenye amri, bali kunaingia katika mlango wa kujiepusha na kilichokatazwa. Na ikitokea (ikaondoshwa) kwa sababu yoyote ile, basi hukmu itathibiti. Na kwa ajili hiyo, niya haishurutishwi katika kuondosha najsi. Lakini kama itaondoka kwa kitendo cha mtu aliyenuia, basi atalipwa thawabu kwa hilo. Na kama si hivyo, ikiondoshwa bila kitendo chake wala niya yake, basi athari itaondoka, na hatokuwa na thawabu wala madhambi.
Na hili linatiliwa nguvu na kwamba tembo inapobadilika na kuwa siki, basi inakuwa imetwaharika – kwa wale wanaosema kuwa pombe ni najsi – kwa makubaliano ya Waislamu.
Ninasema (Abuu Maalik): "Lenye nguvu ni kuwa najsi inapoondoka kwa kitu chochote, hukmu yake inaondoka na inakuwa ni twahara".
Hapa Kuna Faida Kadhaa
1- Mtu mwenye najsi katika nguo yake au mwili wake, kisha akatumia mada yoyote twahara ya kusafishia – yasiyo maji – ili kuondosha najsi hiyo, basi hilo humtosheleza na wala si lazima aoshe kwa maji.
2- Haijuzu kutumia vyakula au vinywaji katika kuondoshea najsi bila dharura, kwani huo ni uharibifu wa mali. [Majmuu Al-Fataawaa (21/475)].
3-Utwaharishaji bila maji kwa (kutumia) vimiminika vingine au mada nyinginezo, utafanyika tu katika (kiini cha) najsi yenyewe katika nguo au mwili au mahala. Ama utwaharishaji wa kihukmu (twahara ya hadathi) kama vile wudhuu, kuoga na mfano wake, haukamiliki ila kwa maji.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
011-Kustanji (Kuchamba)
Alhidaaya.com [3]
Maana Ya Kustanji Na Hukmu Yake
Kustanji ni (neno la Kiarabu katika wazn wa) "Istif'-aal" kutokana na neno: (نجوت الشجرة) yaani: "Nimeukata mti". Ni kana kwamba amejiondoshea adha.
Na katika istilahi, ni kusafisha athari ya kilichotoka kwenye njia mbili (ya mbele na nyuma) kwa jiwe au karatasi na mfano wake.
Pia huitwa "Al-Istijmaar" kwa vile mtu hutumia vijiwe vidogo katika kustanji, na na huitwa pia Al-Istitwaabah", kwa vile mtu huutakasa mwili wake kwa kuuondoshea uchafu. [Al-Mughniy (1/205)].
Hukmu Yake:
Kustanji ni lazima kwa kila kilichozoeleka kutoka katika njia mbili kama mkojo, madhii na kinyesi (kwa mujibu wa Jamhuri ya Maulamaa kinyume na Abuu Haniyfah). [Mahanafi wamesema: Kustanji ni Sunnah iliyokokotezwa madhali najsi haijavuka sehemu yake ya kutokea. Wanatolea dalili Hadiyth isemayo: ((Mwenye kustanji kwa vijiwe, basi afanye kwa idadi ya witri. Mwenye kufanya, basi kafanya vizuri, na ambaye hakufanya, basi hapana ubaya kwake)). Na hii ni Hadiyth Dhwa’iyf. Angalia Kitabu cha Dhwa’iyf Al Jaami’i (5468)].
Ni kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((إذا ذهب احدكم إلى الغائط فليستطب بثلاثة احجار فإنها تجزيء عنه))
((Anapokwenda mmoja wenu haja kubwa, basi astanji kwa vijiwe vitatu, kwani vinamtosheleza)). [Hadiyth Hasan. Kuna Hadiyth kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (40), An-Nasaaiy (1/18), Ahmad (6/108 – 133) kwa Sanad Dhwa’iyf. Kuna Hadiyth nyingine kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine yenye kuitilia nguvu. Angalia Al-Irwaa (44)].
Na hii ni amri, nayo ni amri ya wajibu. Kisha neno lake:
((فإنها تجزيء))
((kwani humtosheleza))…
…na neno kutosheleza hutumika katika wajibu. Na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((لا يستنجى أحدكم بدون ثلاثة أحجار))
((Asistanji mmoja wenu kwa chini ya vijiwe vitatu)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (262), An-Nasaaiy (1/16), At-Tirmidhiy (16) na Abuu Daawuud].
Na katazo la kupunguza chini ya vijiwe vitatu, kunahukumia uharamu. Na itakapokuwa ni haramu kuacha baadhi ya najsi, basi kuiacha yote ni vibaya zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
012-Kitu Gani Hutumika Kustanjia?
Alhidaaya.com [3]
Inatosheleza kustanji kwa moja ya vitu viwili:
1- Mawe na mfano wake kati ya kila kitu kigumu chenye kuondosha najsi na kisicho na thamani kubwa.
Ni kama karatasi, vitambaa, mbao na vyote vyenye kutakasa najsi.
Imepokelewa toka kwa Mama wa Waumini 'Aaishah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((إذا ذهب احدكم إلى الغائط فليستطب بثلاثة احجار فإنها تجزيء عنه))
((Anapokwenda mmoja wenu haja, basi astanji kwa vijiwe vitatu, kwani hivyo humtosheleza)). [Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (40), An Nasaaiy (1/18), Ahmad (6/108 – 133) kwa Sanad Dhwa’iyf. Kuna Hadyth nyingine kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine yenye kuitilia nguvu. Angalia Al- Irwaa (44)].
Haijuzu kustanji kwa chini ya vijiwe vitatu, kwa kauli hizi zenye nguvu:
(a) Ni kwa Hadiyth ya Salmaan, amesema:
"Hakika alitukataza sisi (yaani Rasuli (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuelekea Qibla wakati wa kukidhi haja kubwa au ndogo, au kustanji kwa mkono wa kulia, au kustanji kwa chini ya vijiwe vitatu, au kustanji kwa kinyesi au mfupa".[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (262), An-Nasaaiy (1/16), At-Tirmidhiy (16) na Abuu Daawuud].
(b) Imepokelewa toka kwa Jaabir, amesema:
Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((إذا استجمر أحدكم فليستجمر ثلاثا))
((Anapostanji mmoja wenu kwa vijiwe, basi astanji mara tatu)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad, Ibn Abu Shaybah, na Ibn Khuzaymah. Al Huwayniy Allaah Amhifadhi anasema kwamba Sanad yake ni Swahiyh katika kitabu cha Badhl Al Ihsaan].
(c) Imepokelewa toka kwa Khilaal bin As-Saaib toka kwa baba yake ikiwa ni Marfu’u:
((إذا دخل أحدكم الخلاء فليتمسح بثلاثة أحجار))
((Anapoingia mmoja wenu msalani, basi ajipanguse kwa vijiwe vitatu)). [Hadiyth Hasan kutokana na yaliyotangulia. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Twabaraaniy katika Al-Kabiyr (7/6623). Angalia Al-Badhl (1/352)].
Ninasema (Abuu Maalik): "Ikiwa patasafika kwa vijiwe vitatu, basi ni vyema. Na kama si hivyo, itabidi kuongeza zaidi ya vitatu mpaka pasafike".
Haifai kustanji kwa mifupa au kinyesi cha mnyama kutokana na Hadiyth ya Ibnu Mas'uud kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
(( لا تَسْتَنْجُوا بِالرَّوْثِ وَلا بِالْعِظَامِ فَإِنَّهُ زَادُ إِخْوَانِكُمْ مِنَ الْجِنِّ ))
((Msistanji kwa kinyesi cha mnyama wala mifupa, kwani hivyo ni masurufu ya ndugu zenu katika majini)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (682), At-Tirmidhiy (18) na Ahmad (1/436)]
Na imepokelewa toka kwa Ibnu Masu'ud, amesema:
"Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikwenda haja, akaniamuru nimletee vijiwe vitatu. Nilipata viwili na nikatafuta cha tatu lakini sikukipata. Nikachukua kinyesi cha mnyama nikamletea. Alivichukua vijiwe viwili na akakitupa kinyesi. Akasema:
((هذا ركس))
((Hii ni najsi)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (156) na wengineo. Imeshatajwa nyuma].
2- Maji
Imepokelewa toka kwa Anas, amesema:
"Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiingia msalani, na mimi na kijana pembeni mwangu tunabeba ndoo ya maji na kiegemeo, na yeye (Rasuli) akistanji kwa maji".[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (151), Muslim (270, 271) na wengineo].
Na kustanji kwa maji ni bora zaidi kuliko kustanji kwa mawe, kwani Allaah Mtukufu Amewasifu watu wa Qubaa kwa kustanji kwa kutumia maji.
Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Allaah Amridhie) ikiwa marfu'u:
"Aayah hii iliteremka kwa watu wa Qubaa:
(( فِيهِ رِجَالٌ يُحِبُّونَ أَن يَتَطَهَّرُواْ))
(( Humo wamo watu wanaopenda kujitakasa)).[At Tawbah ( 9:108)].
Akasema: "Walikuwa wakistanji kwa maji, na Aayah hii ikateremka kuwazungumzia wao". [Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (44), At-Tirmidhiy (3100) na Ibn Maajah kwa Sanad Dhwa’iyf. Kuna Hadyth nyingine kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine yenye kuitilia nguvu. Angalia Al-Irwaa (45)].
At-Tirmidhiy anasema (1/31): “Hili ndilo ambalo Wanachuoni wanalolifanya. Wamekhitari kustanji kwa maji ingawa kustanji kwa mawe kunawatosheleza. Wamependelea kustanji kwa maji na wamelionelea hilo ni bora zaidi. Na hayo hayo ameyasema Sufyaan Ath-Thawriy, Ibn Al-Mubaarak, Ash-Shaafi'iy, Ahmad na Is-haaq na wengineo”.
Mtu Hastanji Kwa Kutokwa na Upepo, Na Si Lazima Kustanji Kabla ya Kutawadha
Si lazima kustanji kwa mtu aliyetokwa na upepo au aliyeamka toka usingizini. Ibnu Qudaamah anasema:
" Hatujui katika hili mahitilafiano yoyote".
Abuu ‘Abdullah anasema:
"Hakuna katika Kitabu cha Allaah wala katika Hadiyth za Rasuli Wake kwamba mtu astanji kwa kutokwa na upepo, bali linalompasa ni kutawadha".
Na imepokelewa toka kwa Zayd bin Aslam katika Neno Lake Allaah Mtukufu:
((إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلاةِ فاغْسِلُواْ وُجُوهَكُمْ))
((Mnaposimama kwa ajili ya Swalaah, basi osheni nyuso zenu)). [Al Maaidah (5:6)].
..akisema: "Mnapotoka usingizini, na Hakuamuru jingine zaidi. Hivyo basi, inaonyesha si lazima, kwa kuwa la wajibu hubainishwa na shariyah. Na hapa Aayah haikutaja kustanji, wala kustanji huko hakuko katika maana iliyoelezewa, kwani kustanji kumewekwa kwa ajili ya kuondosha najsi, na hapa hakuna najsi.." [Al-Mughniy cha Ibn Qudaamah (1/206)].
Kustanji si lazima kuungamane na wudhuu, hilo halikusuniwa na wala halikupendezeshwa kama wanavyodhani watu wengi, bali hiyo ni ‘ibaadah peke yake kando. Makusudio yake ni kupatakasa mahali kutokana na najsi. Na wala hakuna yeyote aliyenukuu kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akistanji kila anapotawadha au aliamuru hilo.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
013-Baadhi Ya Adabu Za Kustanji
Alhidaaya.com [3]
Kati ya adabu ambazo inatakikana mtu ajipambe nazo wakati wa kustanji ni:
1- Asistanji kwa mkono wa kulia
Ni kutokana na Hadiyth ya Abuu Qataadah, amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
(( لا يمسكن احدكم ذكره بيمينه وهو يبول، ولا يتمسح من الخلاء بيمينه، ولا يتنفس في الاناء))
((Asikamate kabisa mmoja wenu dhakari yake kwa mkono wake wa kulia wakati anakojoa, wala asijisafishe haja kwa mkono wake wa kuume, wala asipumulie ndani ya chombo)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy ( 153) Muslim (267) na wengineo].
Na imepokelewa toka kwa Salmaan, amesema: “Mtu mmoja aliniambia: “Hakika mwenzenu huyu anawafundisheni hata kwenda haja kubwa”. Akasema (Salmaan): “Ndiyo. Ametukataza kuelekea Qiblah wakati wa kukidhi haja kubwa au ndogo, ametukataza kustanji kwa mikono yetu ya kulia, au kustanji kwa chini ya vijiwe vitatu”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (262), Abuu Daawuud (7), At-Tirmidhiy (16) na An-Nasaaiy (1/16).
2- Asiuguse utupu kwa mkono wake wa kulia
Ni kwa Hadiyth ya Abuu Qataadah iliyotangulia.
3- Ausugue mkono wake kwenye udongo, au auoshe kwa sabuni na mfano wake baada ya kustanji
Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah, amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa akiingia msalani, nilikuwa nikimpelekea maji katika kijidoo kidogo, halafu hustanji na kisha huupangusa mkono wake juu ya ardhi”. [Hadiyth Hasan Lighayrihi. Imefanyiwa “ikhraaj” na …(45), Ibn Maajah (678) na An-Nasaaiy (1/45). Angalia Kitabu cha Al-Mishkaat (360)].
Hili linatiliwa nguvu na Hadiyth ya Maymuunah isemayo: “Kisha Rasuli alijimwagia maji juu ya utupu wake, akauosha kwa mkono wake wa kushoto, kisha akaupiga mkono wake juu ya ardhi, halafu akauosha”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (266) na Muslim (317)].
4- Aunyunyizie utupu wake maji pamoja na nguo yake baada ya kukojoa ili kuondosha shaka na wasiwasi
Imepokelewa na Ibn ‘Abbaas kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitawadha mara moja, halafu akaunyunyizia maji utupu wake. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ad-daaramiy (711) na Al-Bayhaqiy (1/161). Al-Albaaniy amesema katika kitabu cha Tamaam Al-Minnah (uk. 66) kwamba Sanad yake ni Swahiyh juu ya sharti ya Masheikh wawili].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
014-Ni Vipi Mgonjwa Wa Kichocho Au Mfano Wake Anastanji?
Alhidaaya.com [3]
Mwenye kichocho, atastanji na kutawadha kwa kila Swalaah. Na vinavyomtoka vinakuwa havina madhara yoyote kwake madhali wakati wa Swalaah nyingine haujaingia. Na hii ndiyo kauli sahihi zaidi kati ya kauli mbili za Maulamaa. Kauli hii imesemwa na Abuu Haniyfah, Ash-Shaafi’iy, Ahmad, Is-haaq, Abuu Thawr na wengineo.
Mwenye ugonjwa huu, atakuwa na hukmu ya damu ya istihaadhwah. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amelizungumzia hilo aliposema:
((انما ذلك عرق، وليست بالحيضة، فاذا أقبلت الحيضة فدعي الصلاة، فاذا ذهب قدرها، فاغسلي عنك الدم وصلي))
((Hakika hiyo ni damu ya mshipa na si ya hedhi. Na hedhi ikija, basi acha Swalaah. Muda wake ukimalizika, oga ujitwaharishe damu, kisha swali)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (228), Muslim (333) na wengineo. An-Nasaaiy (1/185) ameisimulia kwa tamko la: “Basi oga ujitwaharishe na damu, utawadhe na uswali” kwa nyongeza ya “utawadhe”, nayo ni “Shaadha”. An-Nasaaiy na Al-Bayhaqiy ( 1/327) wameikosoa. Naye Muslim ameashiria kwamba ina walakini, na Al-Bukhaariy hakuifanyia “ikhraaj”. Angalia “Jaami’u Ahkaamin Nisaa” kilichotungwa na Sheikh wetu Mustwafa Al- ‘Adawy – Allaah Amnyanyulie hadhi yake – (1/223-226)].
Na kwa upande wa Al-Bukhaariy, amesema: Na akasema Ubayy: “Kisha tawadha kwa kila Swalaah mpaka uje wakati huo”. [Tamko hili linawezekanika kuwa ni Marfu’u toka kwa kauli ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), au kutoka kwa kauli ya ‘Urwa bin Az Zubayr msimulizi wa Hadiyth toka kwa ‘Aaishah. Aliwajibu kwa kauli hiyo akina mama waliomuuliza kuhusiana na hilo kama ilivyo kwa Ad-Daaramy (1/199). Al Haafidh katika “Al-Fat-h” (1/332), amepondokea kwenye uwezekaniko wa kwanza, na Al-Bayhaqiy kwenye “As-Sunan” (1/344), amepondokea kwenye uwezekaniko wa pili. Naye Sheikh letu – Allaah Amhifadhi – ameitilia nguvu katika “Jaami’u Ahkaamin Nisaa” (1/227)].
Ninasema (Abuu Maalik): "Hukmu hii bila shaka ni kwa mwenye udhuru kwa ajili ya kumwondoshea uzito. Na hakuna shaka kuwa sharia imekuja kwa ajili ya kuuondoshea umma uzito. Allaah Mtukufu Anasema:
(( يُرِيدُ اللَّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ ))
(( Allaah Anawatakieni wepesi na wala Hawatakieni uzito)).[Al-Baqarah: (2:185)]
Maalik na wengineo wanaona kwamba haimpasi mgonjwa huyo kustanji wala kutawadha ila tu kama atapata hadathi nyingine".
Ninasema (Abuu Maalik): "Ama kutokupasa kutawadha kwa kila Swalaah endapo kama hajapata hadathi, huenda hilo lina mwono kwa wale waliotia udhwa’iyf katika kuongezwa neno “na utawadhe kwa kila Swalaah” katika Hadiyth iliyotangulia. Na lenye nguvu hapa ni kutawadha kwa kila Swalaah kama itakavyokuja katika mlango wa hedhi. Ama kutopasa kustanji, basi hilo halina cha kuzungumziwa, kwani anaweza kutokwa na kinacholazimisha kustanji na akawa na wasaa wa kufanya hivyo kabla ya Swalaah bila ya uzito wowote. Anachosamehewa ni kile tu kinachomtoka wakati wa Swalaah kwa ajili ya kuepuka uzito. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi".
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
015-Adabu Za Kukidhi Haja
Alhidaaya.com [3]
Mwenye kutaka kukidhi haja ndogo au kubwa, inatakikana ajihimu kwa adabu zifuatazo:
1. Ajisitiri na ajiweke mbali na watu na hasa hasa uwandani.
Imepokelewa na Jaabir (Radhi za Allaah ziwe juu yake), amesema: “Tulitoka na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika safari. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa hafiki uwandani, isipokuwa hupotea asionekane”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (2) na Ibn Maajah (335), na tamshi ni lake].
2- Asiwe na kitu chenye utajo wa Allaah Mtukufu [Angalia Al-Majmuu (2/87), Al-Mughniy (1/227) na Al-Awswat (1/342)].
Ni kama pete iliyotiwa nakshi ya Jina la Allaah na vinginevyo. Hii ni kwa vile kulitukuza Jina la Allaah Mtukufu ni jambo ambalo kidini linajulikana na wote. Allaah Mtukufu Anasema:
ذَلِكَ وَمَنْ يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِنْ تَقْوَى الْقُلُوبِ
(( Ndivyo hivyo! Na anayetukuza alama za ‘Ibaadah za Allaah, basi hayo ni katika taqwa ya nyoyo)). [Al-Hajji (22:32)).
Hii ni kwa yaliyopokelewa toka kwa Anas kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiivua pete yake anapoingia msalani. [Hadiyth Dwa’iyf. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na Ibn Maajah. Al-Albaaniy kasema ni Dhwa’iyf.
Na Hadiyth hii ni Munkar, wahafidhi wameitia dosari.
Na linalojulikana ni kwamba pete ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ilikuwa imetiwa nakshi iliyoandikwa “Muhammad Rasuwlul Laah”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (5872), Muslim (2092) na wengineo.]
Ninasema (Abuu Maalik): “Ikiwa pete hii au mfano wake imesitiriwa kwa kitu kama kuwekwa mfukoni au sehemu nyingine kama hiyo, basi itajuzu kuingia nayo. Ahmad bin Hanbal anasema: “Akitaka ataifumbata katika kiganja chake”.
Ikiwa atahofia kupotea kama ataiacha nje, basi itajuzu kuingia nayo kwa vile imelazimu. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.
3- Apige BismiLlaah na ajilinde kwa Allaah wakati wa kuingia msalani
Atafanya hivi kama ataingia sehemu iliyojengwa (choo). Lakini kama itakuwa ni uwandani, basi atafanya hivyo wakati anapoinyanyua nguo yake. Hii ni kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((ستر مابين الجن وعورات بني آدم اذا دخل أحدهم الخلاء أن يقول: بسم الله))
((Kinga iliyoko kati ya jini na tupu za wanaadamu anapoingia mmoja wao msalani, ni kusema “BismiLlaah”)).[Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy na Ibn Maajah. Angalia “Swahiyh Al- Jaami’i” (3611)].
Na imepokelewa na Anas (Radhi za Allaah ziwe juu yake) akisema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anasema wakati anapoingia msalani:
اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِك من الْخُبُثِ وَالْخَبَائِثِ
((Ee Allaah! Hakika mimi ninajilinda Kwako na majini wa kiume na majini wa kike)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (142) na Muslim (372)].
4- Atangulize mguu wa kushoto wakati wa kuingia, na mguu wa kulia wakati wa kutoka
Abuu Maalik: “Sikupata katika hili kauli thibitishi toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Lakini Ash-Shawkaaniy amesema katika “As-Saylu Al-Jarraar” (1/64): Ama kutanguliza mguu wa kushoto wakati wa kuingia na mguu wa kulia wakati wa kutoka, basi hili lina hikmah yake. Ni kuwa vitu vitukufu huanziwa kwa kulia na visivyo vitukufu huanziwa kwa kushoto. Na bila shaka yenye kuonyesha hilo yamekuja katika ujumuishi.”
5- Asielekee Qiblah au kukipa mgongo wakati anapokaa kukidhi haja
Ni kwa Hadiyth ya Abu Ayyuub Al-Answaariy (Radhi za Allaah ziwe juu yake) aliyepokea toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), amesema:
(( إذا أتيتم الغائط فلا تستقبلوا القبلة ولا تستدبروها، ولكن شرقوا أو غربوا))
((Mnapokwenda haja kubwa, msikielekee Qiblah wala msikipe mgongo, bali elekeeni mashariki au magharibi)).
Abuu Ayyuub anasema: “Tukafika Shaam, tukakuta vyoo vimejengwa kuelekea Ka’abah, tukawa tunakiepa na kumwomba Allaah Mtukufu maghfirah”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (394), Muslim (264) na wengineo.
Lakini hata hivyo, imepokelewa kwa njia sahihi toka kwa Ibn ‘Umar kwamba amesema: “Siku moja nilipanda juu ya paa la nyumba yetu, nikamwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya matofali mawili akikidhi haja na ilhali ameelekea Baytul Maqdis”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (145), Muslim (266) na wengineo.]
Na ikiwa ameelekea Baytul Maqdis na yeye yuko Madiynah, basi atakuwa ameipa mgongo Ka’abah!!
Ninasema (Abuu Maalik): “Na ili kuzifahamu Hadiyth hizi mbili, kuna kauli nne mashuhuri za Maulamaa: [Amezitaja An Nawawiy kwenye Al-Majmuu’i (2/82), na Al-Haafidh kwenye Al-Fat-h (1/296), na ameongeza kauli tatu nyingine].
1- Ni kuwa katazo la kuelekea Qiblah na kukipa mgongo ni kwa hali zote sawasawa ikiwa ndani ya jengo au uwandani.
Haya ni madhehebu ya Abuu Haniyfah, Ahmad na Ibnu Hazm. Shaykh wa Uislamu pia ana msimamo huu. Ibnu Hazm amelinukulu hili toka kwa Abuu Hurayrah, Abuu Ayyuub, Ibn Mas’uud na Suraaqah bin Maalik. Pia amepokea toka kwa Atwa’a An-Nakh’i, Ath-Thawriy, Al-Awzaa’iy na Abuu Thawr. [Al-Muhallaa (1/194), Al-Fat-h (1/296), Al-Awswat (1/334), As Sayl Al-Jarraar (1/69) na Al-Ikhtiyaaraat Al- Fiqhiyyah (8)]. Wametoa hoja yao kwa kuitumia Hadiyth ya Abuu Ayyuub iliyotangulia.
Wameijibu Hadiyth ya Ibn Umar kwa mambo haya:
(a) Lililokatazwa linatangulizwa kabla ya lililoruhusiwa.
(b) Hakuna ndani ya Hadiyth hiyo kwamba hilo lilikuwa baada ya kukatazwa kuelekea Ka’abah au kuipa mgongo.
(c) Kitendo chake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakipingani na kauli inayouhusu umma isipokuwa kwa lile lenye dalili yenye kuashiria kwamba alitaka kumuiga katika hilo. Na kama si hivyo, basi kitendo chake kilikuwa kinamuhusu yeye mwenyewe.
Ninasema: “Huenda kauli yao hii ya mwisho inapata nguvu ya kuwa Ibn ‘Umar kumwona Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kumeafikiana naye bila ya kukusudia. Kana kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakutaka kwa hilo kubainisha hukmu mpya ya kisharia”.
2- Ni kuwa katazo hilo linahusiana na sehemu wazi tu lakini si ndani ya jengo.
Hili limesemwa na Maalik na Ash-Shaafi’iy. Kwa kauli yao hii, wao wamepitia mkondo wa kukusanya baina ya dalili mbili. Wamesema: “Kaida isemayo “Kauli hutangulizwa kabla ya kitendo”, bila shaka hutumiwa katika hali ya kuthibiti umahususi, na umahususi huo hauna dalili yoyote”.
3- Ni kuwa inajuzu kukipa mgongo Qiblah lakini haifai kukielekea.
Hili limehadithiwa toka kwa Abuu Haniyfah na Ahmad, wakiuchukulia udhahiri wa Hadiyth ya Ibn ‘Umar na Hadiyth ya Abuu Ayyuub.
4- Ni kuwa inajuzu kuelekea Qiblah na kukipa mgongo katika hali zote.
Hii ni kauli ya ‘Aaishah, ‘Urwah, Raby’a na Daawuud. Hoja yao wanasema kuwa Hadiyth zimegongana, na kwa hivyo suala linarejea katika asili yake ya uhalali.
Ninasema (Abuu Maalik): ”Huenda kauli ya kwanza ya kuharamisha kabisa hali zote mbili, ndiyo dalili yenye nguvu zaidi na yenye kinga zaidi kuitumia. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
5- Ajiepushe kabisa na maneno ila kwa dharura.
Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Umar (Radhi za Allaah ziwe juu yake) akisema kwamba mtu mmoja alimpitia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa anakidhi haja ndogo, akamsalimia na Rasuli hakujibu. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (370), Abuu Daawuud (16), At Tirmidhiy, An Nasaaiy (1/15) na Ibn Maajah (353).
Kujibu maamkizi ni wajibu. Na Rasuli alipoacha kujibu, inaonyesha kuwa ni haramu kuzungumza na hasahasa kama ni kumtaja Allaah Mtukufu. Lakini ikiwa atazungumza kwa ajili ya haja isiyoepukika kama kumwongoza mtu, au kuomba maji au mfano wa hayo, basi itaruhusika kutokana na dharura. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
6- Ajiepushe kukidhi haja njiani wanamopita watu, sehemu wanapopumzikia kupata kivuli na mfano wa sehemu hizo.
Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((اتقوا اللاعنين، قالوا: وما اللاعنان يا رسول الله؟ قال: الذي يتخلى في طريق الناس أو في ظلهم))
((Waogopeni wawili waliolaaniwa)). Wakasema: Ni nani hao wawili waliolaaniwa ee Rasuli wa Allaah? Akasema: ((Ni yule anayejisaidia njiani wanamopita watu au katika kivuli chao)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (68) na Abuu Daawuud(25)].
7- Ajiepushe kukojoa mahala pa kuogea.
Na hasahasa kama maji yanajikusanya mahala hapo kama kwenye hodhi (bath tub) na kadhalika. Kwani Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza mtu kukojoa mahala anapoogea. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na An Nasaaiy (1/130) na Abuu Daawuud (28)].
8- Ajiepushe kukojoa katika maji yaliyotuama tuli.
Ni kwa Hadiyth ya Jaabir aliyesema kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza watu kukojoa katika maji yaliyotuama. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (281) na An Nasaaiy (1/34).
09- Atafute sehemu laini wakati wa kukojoa na ajiepushe sehemu ngumu ili kujikinga najsi isimrudie.
10- Ashikamane na adabu za kustanji tulizotangulia kuzitaja.
11- Aseme wakati anapotoka: “Ghufraanak”.
Imepokelewa toka kwa ‘Aaishah akisema kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa anatoka msalani, alikuwa akisema: “Ghufraanak”.[Hadiyth Hasan Lighayrihi. Imefanyiwa “ikhraaj” na At Tirmidhiy (7), Abuu Daawuud (30) na Ahmad (6/155)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
016- Je, Inafaa Mtu Kukojoa Kwa Kusimama?
Alhidaaya.com [3]
Katika mlango huu, kuna Hadiyth tano toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Tatu kati ya hizo ni Hadiyth Swahiyh. Katika Hadiyth ya kwanza, ‘Aaishah anakanusha Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kukojoa kwa kusimama. Na katika Hadiyth ya pili, inaelezwa kuwa alikojoa kwa kusimama, na ya tatu inaelezwa kuwa alikojoa kwa kukaa (kuchuchumaa).
Ama Hadiyth mbili Dhwa’iyf, moja inakataza kukojoa kwa kusimama na nyingine inakuelezea kukojoa kwa kusimama kama ni utovu wa hishma. Hadiyth zenyewe ndizo hizi:
1- Hadiyth ya ‘Aaishah, amesema: “Atakayewaambieni kuwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikojoa kwa kusimama, basi msimsadiki. Hakuwa akikojoa ila kwa kuchuchumaa”.[Hadiyth Swahiyh Lighayrih. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy (12), An-Nasaaiy (1/26), Ibn Maajah (307) na Ahmad (6/36)].
2- Hadiyth ya Hudhayfah, anasema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikwenda mwishoni mwa jalala la watu, akakojoa kwa kusimama. Mimi nilijivuta kando, lakini aliniambia nikurubie. Nilikurubia mpaka nikasimama nyuma yake, akatawadha na kupukusa juu ya khofu zake mbili”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (226), Muslim (273), na wengineo].
3- Ni Hadiyth ya ‘Abdur-Rahmaan bin Hasanah, amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitutokea akiwa ameshika mkononi mwake kitu kama ngao. Alikiweka kitu hicho, kisha akakaa nyuma yake na kukojoa akikielekea”.[Hadiyth Swahiyh Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (22), An-Nasaaiy (1/27), Ibn Maajah (346) na Ahmad (4/196)].
4- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Umar, amesema: “Alisema ’Umar: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliniona nikikojoa kwa kusimama akaniambia:
((يا عمر، لا تبل قائما))
((Ee ‘Umar! Usikojoe kwa kusimama)).
Akasema: “Sikukojoa tena kwa kusimama”. [Hadiyth Dhwaiyf. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Maajah (308), Al-Bayhaqiy (1/202) na Al-Haakim (1/185). At- Tirmidhiy amesema ni “Hadiyth Mu’allaq” na Dhwaiyf (1/67 – Ahwadhiy)].
5- Imepokelewa toka kwa Buraydah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
(( ثلاث من الجفاء: أن يبول الرجل قائما، أو يمسح جبهته قبل أن يفرغ من صلاته، أو ينفخ في سجوده))
((Mambo matatu ni utovu wa adabu: Mtu kukojoa kwa kusimama, au kuupangusa uso wake kabla hajamaliza kuswali, au kupuliza wakati yuko katika sijdah)). [Hadiyth Munkari. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy katika kitabu cha “At-Taariykh” (496) na “Al-Bazzaaz” (1/547). Al-Bukhaariy na At-Tirmidhiy, wamesema ni Hadiyth Munkar, lakini imethibiti kutokana na kauli ya Ibn Mas-’oud].
Ninasema (Abuu Maalik): “Kutokana na Hadiyth hizi, Maulamaa wametofautiana juu ya hukmu ya kukojoa kwa kusimama katika kauli tatu”: [Al-Majmuu (2/98) na Al-Awswat (1/333)].
1- Ni karaha bila ya udhuru
Haya yamesemwa na ‘Aaishah, Ibn Masu’d na ‘Umar katika moja ya riwaya mbili. Pia Abuu Muusa, Ash-Sha’abiy, Ibn ‘Uyaynah, Hanafiy na Shaafi’iy.
2- Kunajuzu kwa hali yoyote
Haya yamesemwa na ‘Umar (katika riwaya ya mwisho), ‘Aliy, Zayd bin Thaabit, Ibn ‘Umar, Sahl bin Sa’ad, Anas, Abuu Hurayrah na Hudhayfah. Hii ndiyo kauli ya wafuasi wa madhehebu ya Hanbali.
3- Kama mtu yuko sehemu laini ambapo mkojo hauwezi kumrukia itajuzu, lakini kama si hivyo, basi ajizuie.
Haya ni madhehebu ya Maalik. Kauli hii imeungwa mkono na Ibn Al Mundhir.
Ninasema (Abuu Maalik): “Lenye nguvu ni kwamba hakuna ukaraha wowote wa kukojoa kwa kusimama madhali mtu ana uhakika kwamba mkojo hauwezi kumrukia. Hii ni kwa sababu zifuatazo:
1- Ni kwamba hakuna Hadiyth yoyote Swahiyh iliyopokelewa toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) iliyokataza hilo.
2- Ni kuwa yaliyopokelewa kuhusu Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kukojoa kwa kukaa (kuchuchumaa), hayapingani na kujuzu kukojoa kwa kusimama, bali hilo linaashiria kujuzu kwa yote mawili.
3- Ni kwa kuthibitika kuwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikojoa kwa kusimama.
4- Ni kuwa ‘Aaishah kukanusha Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kukojoa kwa kusimama, kumejengewa juu ya kile anachokijua yeye kwa mujibu wa yale ambayo Rasuli anayafanya akiwa nyumbani. Kwa hiyo kukojoa kwake nje ya nyumba yake kwa kusimama, hakukanushiki. Na hakuna shaka kwamba kutojua jambo, hakumaanishi kwamba jambo hilo halipo. Na aliyejua kama vile Hudhayfah na wengineo, ni hoja kwa yule ambaye hakujua, na kwamba jambo yakinishi hutangulizwa kabla ya kanushi. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
017- Sunnah Za Hulka Asilia
Alhidaaya.com [3]
Nini Maana Ya Sunnah Za Hulka Asili? Ni Zipi Sunnah Hizo?
Sunnah za hulka asili ni mambo ambayo mtu akiyafanya, huipata hulka asili ambayo Allaah Amewaumbia kwayo waja, Atawakusanya wakiwa nayo (Siku ya Qiyaamah), na Amewapendelea waifanye ili wawe juu ya ukamilifu wa sifa na utukufu wa sura.
Mambo haya ni mwenendo wa kale ambao Manabii waliuchagua na sharia zote zikakubaliana juu yake. Inakuwa ni kama jambo la kimaumbile waliloumbiwa kwalo watu. [Nayl Al-Awtwaar (1/109) na Umdat Al-Qaariy cha Al’ Ayniy (22/45)].
Maslaha ya kidini na kidunia hufungamana na mambo ya hulka asili ambayo hudirikiwa kwa ufuatiliaji. Kati ya mambo hayo ni kuliweka umbo katika picha nzuri na kuutakasa mwili ndani na nje, na kwa mapana na marefu. [Faydh Al-Qadiyr cha Al-Minnaawiy (1/38)].
Baadhi ya mambo haya yamepokelewa katika haya yafuatayo:
1- Hadiyth ya Abuu Hurayrah, amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((الفطرة خمس: الختان، والاستحداد، وقص الشارب، وتقليم الأظافر، ونتف الآباط))
((Hulka asili ni matano: Kutahiri, kunyoa kinena, kukata sharubu, kukata kucha na kunyofoa vikwapa)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (5891) na Muslim (257)].
2- Hadiyth ya ‘Aaishah, amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((عشر من الفطرة: قص الشارب، واعفاء اللحية، والسواك، واشتنشاق الماء، وقص الأظفار، وغسل البراجم، ونتف الابط، وحلق العانة، وانتقاص الماء))
((Mambo kumi ni katika hulka asili: Kunyoa sharubu, kuziachilia ndevu, kupiga mswaki, kupaliza maji puani, kukata kucha, kuosha vifupachanda, kunyofoa nywele za kwapa, kunyoa kinena na kustanji)).
Mus’ab mmoja wa wapokezi wa Hadiyth anasema: “Nimelisahau la kumi kama halitakuwa ni kusukutua”.[Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (261), Abuu Daawuud (52), At-Tirmidhiy (2906), An-Nasaaiy (8/126) na Ibn Maajah (293).
Kutokana na Hadiyth hizi mbili, tunafahamu kuwa mambo ya hulka asili hayaishilii kwenye haya kumi tu, bali yako mengineyo. Kwa ufupi mambo haya ni:
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
018-Kutahiri
Alhidaaya.com [3]
Maana Na Hukmu Yake
Kutahiri (katika Lugha ya Kiarabu) ni kisoukomo (Maswdar) cha kitenzi ,(ختن)yaani amekata. Na kutahiriwa ni ima kukata ngozi inayofunika kichwa cha uume, au kukata ngozi iliyopo upande wa juu wa utupu wa mwanamke (ukeketaji). [Angalia Tuhfat Al-Mawduwd cha Ibn Al-Qayyim (uk 106, 132) na Al-Majmuu (1/301)].
Ama kwa upande wa hukmu yake, Maulamaa wana rai tatu:
1- Ni wajibu kwa mwanamume na mwanamke.
2- Ni jambo mustahabu kwao.
3- Ni wajibu kwa mwanamume, lakini kwa mwanamke ni mustahabu.
Ibn Qudaamah katika kitabu cha Al Mughny (1/85) anasema: “Ama kutahiriwa, hilo ni wajibu kwa wanaume na ni ukirimio kwa upande wa haki ya wanawake na wala si lazima kwao. Hii ndio kauli ya Maulamaa wengi….”
Naye An-Nawawy katika kitabu cha Al Majmu’i (1/301) anasema: “Na madhehebu sahihi kwa matni ya Ash-Shaafi’iy na yaliyokubaliwa kwa sauti moja na Jamhuri ya Maulamaa ni kuwa kutahiriwa ni wajibu kwa wanaume na wanawake…”
Ninasema (Abuu Maalik): “Ama kutahiriwa mwanamume, inavyoonekana ni kuwa jambo hilo ni la lazima kutokana na dalili zifuatazo:
1- Hilo ni mila ya Ibraahiym (‘Alayhis Salaam). Kwani imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((أختتن إبراهيم خليل الرحمن بعد ما أتت عليه ثمانون سنة))
((Kipenzi cha Ar-Rahmaan Ibraahiym alitahiriwa baada ya kufikisha miaka 80)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (6298) na Muslim (370)].
Na Allaah Mtukufu Anamwambia Rasuli Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((ثُمَّ أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ أَنِ اتَّبِعْ مِلَّةَ إِبْرَاهِيمَ حَنِيفاً وَمَا كَانَ مِنَ المُشْرِكِينَ))
((Kisha Tukakufunulia ya kwamba ufuate mila ya Ibraahiym mwongofu, wala hakuwa miongoni mwa washirikina)).[ An-Nahl (16:123].
2- Ni kwa yale yaliyopokelewa kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia mtu mmoja aliyesilimu:
((ألق عنك شعر الكفر واختتن ))
((Jitakase na taka za ukafiri na utahiriwe)). [Al-Albaaniy ameifanya Hadiyth Hasan kwa
Hadiyth nyingine kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (356) na Al-Bayhaqiy (1/172). Katika Sanad yake kuna wapokezi wawili wasiojulikana pamoja na mkatiko. Lakini Al-Albaaniy amesema kuwa ni Hadiyth Hasan kwa Hadiyth nyingine kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine aliyoinasibishia katika Swahiyh ya Abuu Daawuud (383). Na katika “Al-Irwa’i” (79), “mimi sikuviona”. An-Nawawiy na Ash-Shawkaaniy wamesema kuwa ni Dhwa’iyf].
3- Kwamba kutahiriwa ni katika ‘ibaadah ya Waislamu, na ni sifa yao maalumu inayowatofautisha na Mayahudi na Wakristo. Na kwa ajili hiyo, imekuwa ni wajibu kama zilivyo ‘ibaadah nyinginezo.
4- Ni kwamba kutahiri ni kukata sehemu ya mwili, na hili ni haramu, na la haramu halihalalishwi ila kwa la wajibu.
Haya ndio madhehebu ya Maalik, Ash-Shaafi’iy na Ahmad. Lakini Maalik amelichukulia msimamo mkali na kusema: “Mtu ambaye hakutahiriwa, basi hafai kuwa Imaam na ushahidi wake haukubaliwi”. Na Maulamaa wengi wamenukulu toka kwa Maalik akisema kuwa hilo ni Sunnah. Lakini kuacha Sunnah kwa mujibu wa Maalik, ni dhambi. [Tuhfat Al-Mawduwd (uk 113)].
Ama kwa mwanamke, bila shaka sharia ya kutahiriwa amewekewa. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
(( إذا التقى الختانان وجب الغسل))
((Zinapokutana tupu mbili zilizotahiriwa, ni lazima kukoga)).[Hadiyth Swahiyh. Ibn Maajah ameitoa kwa tamko hili (611). Na katika Swahiyh Mbili, imekuja kwa tamko la: ((Na utupu kuugusa utupu, hakika imepasa kuoga))].
Na "Al-Khitaanaani" ni mahala pa kukatwa katika dhakari ya kijana na utupu wa msichana. Na hii yaonyesha kuwa wasichana walikuwa wakikeketwa.
Kuna Hadiyth zilizopokelewa juu ya wajibu wa kumkeketa mwanamke. Hadiyth zote hizo zimekosolewa. Kati ya Hadiyth hizo ni ile ya Ummu ‘Atwiyyah aliyesema kwamba kuna mwanamke fulani aliyekuwa akikeketa mjini Madiynah. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia:
((لا تنهكي، فإن ذلك أحظى للمرأة وأحب إلى البعل))
((Usikate sana, kwani hilo linampa hadhi zaidi mwanamke na linapendwa zaidi na mume)).[Hadiyth Dwa’iyf. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (5271), na amesema ni dhwa’iyf].
Na katika riwaya:
(( إذا خفضت فأشمي ولا تنهكي، فإنه أنضر للوجه، وأحظى عند الزوج))
((Unapokata, basi bakisha kidogo wala usikate chote, kwani hilo linapendeza zaidi usoni na linashabikiwa zaidi na mume)). [Hadiyth Munkar: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Khatiyb katika kitabu cha At-Taariykh (5/327). Tazama pia Jaami’ul Ahkaam An-Nisaa’i (1/19)].
Hadiyth hizi Sanad zake ni Dhwa’iyf ingawa Mwanachuoni Al-‘Allaamah Al-Albaaniy amesema kuwa ni Swahiyh katika As-Silsilat As-Swahiyhah (722).
Na kama mambo ni hivi, basi mwenye kusema anaweza kusema: “Kutahiri ni wajibu kwa wanawake kama ilivyo kwa wanaume ingawa Hadiyth hizi ni Dhwa’iyf. Kwani asili ni kuwa wote wawili wako sawa katika hukmu isipokuwa kama kuna dalili ya kuwapambanua, na dalili hiyo haipo”.
Na mwingine anaweza kusema: “Bali hilo ni jambo mustahabu, na ni takrima kwa mwanamke, lakini si wajibu. Na picha ya kupambanua hapa kati ya mwanamume na mwanamke ni kuwa kutahiriwa kwa upande wa mwanamume, kuna maslaha kwake yanayofungamana na utwahara ambao ni moja kati ya sharti za Swalaah. Kwani endapo kama govi hilo litabakia, basi mkojo hubaki na hujikusanya ndani”. [Muono huu ameuelezea Mwanachuoni Al-‘Allaamah Ibn ‘Uthaymiyn (Allaah Amrehemu) kama ilivyo katika Al-Mumti’i (1/134)].
Ama kwa upande wa mwanamke, faida kubwa kwake ni kuwa kukeketa humpunguzia matamanio yake. Na hii ni kutafuta ukamilifu na wala si katika mlango wa kuondosha adha.
Ninasema (Abuu Maalik): “Kukeketa wanawake kunazungukia kati ya mustahabu na wajibu. Na imepokelewa toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
(( الختان سنة للرجال مكرمة للنساء))
((Kutahiriwa ni Sunnah kwa wanaume na ukirimio kwa wanawake)).[Hadiyth Dhwa’iyf].
Lakini Hadiyth hii ni dhwa’iyf. Na lau kama ingelikuwa ni Swahiyh, basi ingemaliza mzozo. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi."
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
019-Kupiga Mswaki
Alhidaaya.com [3]
Maana Yake Na Usharia Wake
Ni neno linalotokana na kitenzi (ساك) anaposugua. Ama maana ya kiistilahi ni kutumia kijiti au mfano wake kwenye meno ili kuondosha unjano na mabaki mengineyo. [Nayl Al-Awtwaar (1/102)].
Inapendeza zaidi kutumia mswaki nyakati zote kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
(( السواك مطهرة للفم، مرضات للرب))
((Mswaki ni utwaharisho kwa mdomo, na maridhio ya Mola)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na An-Nasaaiy (1/50), Ahmad (6/47, 62) na wengineo.]
Kupiga mswaki kunakuwa ni mustahabu zaidi katika nyakati zifuatazo:
1- Wakati wa kutawadha
Ni kutokana na Hadiyth ya Abu Hurayrah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((لَوْلَا أَنْ أَشُقَّ عَلَى أُمَّتِي لَأَمَرْتُهُمْ بِالسِّوَاكِ مع الوُضُوءٍ))
((Lau kama si kuuonea uzito umma wangu, basi ningeliwaamuru kupiga mswaki sambamba na wudhuu)).[Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad, nayo iko katika Swahiyh Al-Jaami’i (5316)].
2- Wakati wa kuswali
Ni kutokana na Hadiyth ya Abu Hurayrah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((لَوْلَا أَنْ أَشُقَّ عَلَى أُمَّتِي لَأَمَرْتُهُمْ بِالسِّوَاكِ عند كل صلاة))
((Lau kama si kuuonea uzito umma wangu, basi ningeliwaamuru kupiga mswaki kila wakati wa Swalaah)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (6813), na Muslim (252)].
3- Wakati wa kusoma Qur-aan
Ni kutokana na Hadiyth ya ‘Aliyy anayesema: “Tumeamrishwa kupiga mswaki. Amesema (yaani Rasuli): ((Mja anaposimama katika Swalaah, humjia Malaika akasimama nyuma yake huku akiisikiliza Qur-aan na kumsogelea. Huendelea kusikiliza na kumjongelea hadi anakiweka kinywa chake kwenye kinywa chake. Na hapo mja hasomi Aayah yoyote, isipokuwa huingia ndani ya kinywa cha Malaika huyo)). [Al-Al Baaniy kasema ni Swahiyh. Al-Bayhaqy ameifanyia “ikhraaj” (1/246). Angalia kitabu cha Asw Swahiyhah (1213).
4- Wakati mtu anapoingia nyumbani kwake
Ni kutokana na Hadiyth ya Al Miqdaam bin Shurayh toka kwa baba yake. Anasema:
“Nilimuuliza Aa’ishah: Ni jambo gani la kwanza alilokuwa akilifanya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anapoingia nyumbani? Akasema: Ni kupiga mswaki”.
5- Wakati wa kuamka kwa ajili ya Swalaah ya Usiku
Ni kutokana na Hadiyth ya Hudhayf anayesema:
((Rasuli Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam alikuwa akiyasafisha meno yake kwa mswaki wakati anaposimama kuswali tahajjudi)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (246) na Muslim (255)].
Ni vizuri zaidi kutumia mswaki wa miti (Al Araak) wakati wa kupiga mswaki. Na kama haukupatikana, basi utatosheleza mswaki wa aina nyingine wenye uwezo wa kusafisha kinywa na kung’arisha meno. Ni kama miswaki ya brashi pamoja na dawa maalum za meno. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
020-Je, Kuna Wakati Maalum Wa Kukata Kucha, Kukata Sharubu,
Kunyofoa Nywele Za Kikwapa Na Kunyofoa Kinena?
Alhidaaya.com [3]
Mambo haya hayana wakati maalumu wa kuyafanya, bali kinachoyadhibiti ni haja. Wakati wowote mtu anapohisi kwamba anahitajia kulifanya moja wapo, basi huo ndio wakati wake. La muhimu ni kuwa mtu asijiachie zikapita zaidi ya siku arobaini bila ya kufanya chochote. Na hii ni kutokana na Hadiyth ya Anas aliyesema:
((Tumewekewa muda wa kuwa tusiachie zikapita siku zaidi ya arobaini bila kukata sharubu, kukata kucha, kunyofoa nywele za kikwapa na kunyoa kinena)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (275) na wengineo].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
021-Kufuga Ndevu
Alhidaaya.com [3]
Hukmu ya kufuga ndevu
Kufuga ndevu ni lazima kwa wanaume, na hii ni kwa Hadiyth zifuatazo:
1- Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameamuru kuzifuga. Agizo hili ni la wajibu, kwani hakuna kiashirio chochote chenye kulipindisha na kulifanya liwe ni la Sunnah. Kati ya maagizo hayo ni neno lake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((خالفوا المشركين: وفروا اللحى وأحفوا الشوارب))
((Khalifianeni na washirikina. Fugeni ndevu na punguzeni masharubu)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (5892) na Muslim (259)].
Na neno lake:
((جزوا الشوارب، وأرخوا اللحى، خالفوا المجوس))
((Kateni masharubu, ziachilieni ndevu, khalifianeni na wamajusi)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (260)].
1- Anayezinyoa, anajifananisha na makafiri kama ilivyotangulia katika Hadiyth hizo mbili.
2- Anayezinyoa, anabadili Umbile la Allaah na anamtii shaytwaan aliyesema:
(( وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّهِ ))
((Na kwa hakika, nitawaamrisha, na wao bila kusita, watalibadilisha Umbile la Allaah)). [An-Nisaa (4:119].
3- Anayezinyoa, anajifananisha na wanawake. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amewalaani wanaume wanaojifananisha na wanawake. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (5885) na At-Tirmidhy (2935)].
Na kwa ajili hiyo, Sheikh wa Uislamu anasema: “Ni haramu mtu kunyoa ndevu zake”. [Al-Ikhtiyaarat Al-Fiqhiyyah cha ‘Alaaud Diyn Al Baaly (uk 10). Angalia pia Al-Furu’u cha Ibn Muflih (1/291)].
Ibn Hazm na wengineo, ameinukuu Ijma’a ya Maulamaa kwamba ni haramu kunyoa ndevu. [Maratibul Ijma’a na Raddul Mukhtaar (2/116)].
Je, Inajuzu Kunyoa Ndevu Zilizozidi Mkamato Wa Mkono?
Baadhi ya Maulamaa wanaona kwamba inajuzu kuzikata ndevu zilizozidi mkamato wa mkono kwa kigezo cha Hadiyth ya Ibn ‘Umar ya kwamba alipokuwa anahiji au kufanya ‘Umrah, alikuwa akikamata ndevu zake, na zile zinazozidi, huzikata.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (5892) na Muslim (259)].
Wanasema: “Yeye ndiye mpokezi wa Hadiyth inayoamuru kufuga ndevu, na kwa hivyo, anayajua zaidi madhumuni yake”.
Hujja ya Maulamaa hawa haina mashiko katika athari hii kutokana na haya yafuatayo: [Ameyaelezea haya Sheikh Al-Habiyb Wahiyd ‘Abdus Salaam Baaly – Allaah Ainyanyue hadhi yake – katika kitabu cha Al-Ikliyl].
1- Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu Anhu) alikuwa akilifanya hilo wakati anapojifungua na ihram ya Hijjah au ya ‘Umrah. Lakini wao wanalijuzisha hilo katika hali zote.
2- Kitendo hiki cha Ibn ‘Umar, kinatokana na yeye kuliawilisha Neno Lake Allaah Mtukufu:
((مُحَلِّقِينَ رُءُوسَكُمْ وَمُقَصِّرِينَ))
((Mkinyoa vichwa vyenu na mkipunguza)).[Al-Fat-h (48:27].
..kuwa ni katika amali ya Hijjah. Kunyoa ni kwa kichwa, na kupunguza ni kwa ndevu. [Angalia Sharhul Kirmaany Al-Bukhaary (21/111)].
3- Swahaba akisema au akifanya kinyume na aliyoyasimulia, basi kinachoangaliwa ni kile alichokisimulia, si ufahamu wake wala kitendo chake. Kinachoangaliwa ni kile alichokisema Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) moja kwa moja.
Kutokana na vigezo hivi, la sahihi ni kuwa kufuga ndevu ni wajibu na kuzikata haijuzu kwa msingi wa kuyafuata maagizo jumuishi yaliyokuja kwenye Hadiyth nyingi Swahiyh kama wanavyoona Jamhuri ya Maulamaa. Allaah Ndiye Mjuzi zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
022-Twahara Za Kihukmu
Alhidaaya.com [3]
Aina Za Maji
Maji juu ya kutofautiana sampuli zake, hayatoki nje ya aina mbili:
1- Maji Mutwlaq (Maji Twahara)
Ni yale yenye kubakia kwenye asili ya maumbile yake. Na haya ni maji yoyote yaliyochimbuka toka ardhini au yaliyoteremka toka mbinguni. Allaah Mtukufu Anasema:
((وَيُنَزِّلُ عَلَيْكُمْ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً لِيُطَهِّرَكُمْ به))
((Akakuteremshieni maji kutoka mbinguni ili Akusafisheni kwayo)). [Al-Anfaal (8:11)].
Katika aina hii, yanaingia maji ya mito, theluji, mvua barafu, na visima, hata kama yatabadilika kwa kukaa sana au kwa kuchanganyika na kitu twahara ambacho ni vigumu kuepukana nacho. Vile vile maji ya bahari, kwani Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipoulizwa kuhusu maji ya bahari alisema:
((هو الطهور ماؤه الحل ميتته))
((Maji yake ni twahara na mfu yake ni halali)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (83), At-Tirmidhy (69), An-Nasaaiy (1/176) na Ibn Maajah (386)].
Maji haya yote yanafaa kutawadhia na kuogea bila hitilafu yoyote kati ya Maulamaa, na hata kama yatachanganyika kidogo na kitu twahara yataendelea kubeba jina la maji. Katika Hadiyth ya Ummu Haani ni kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alioga yeye na Maymunah katika kijibeseni kimoja chenye athari ya kinyunya. [Imefanyiwa “ikhraaj” na An Nasaaiy (240) na Ibn Maajah (378)].
Na (ushahidi mwengine ni) kwa amri ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam kwa wanawake waliomwosha binti yake Zaynab alipowaambia:
((اغسلنها ثلاثا بماء وسدر واجعلن في الآخرة كافورا))
((Mwosheni mara tatu; kwa maji na mkunazi, na osho la mwisho fanyeni kwa kafuri)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1253) na Muslim (939)].
Ama kama yatachanganyika na kitu twahara kikaondosha jina la maji na kuwa jina jingine kama chai kwa mfano, basi haijuzu kujitwaharisha nayo. Aidha, haijuzu kujitwaharisha hadathi kwa kutumia vimiminika vilivyokamuliwa toka vitu twahara kama maji ya waridi na mfano wake, kwani hayo si maji halisi.
Ibnu Al-Mundhir anasema: “Maulamaa wote tuliohifadhi kauli zao, wamekubaliana kwa kauli moja kuwa wudhuu haufai kwa maji ya waridi, maji ya miti na maji ya m-’asfara. Na haifai kujitwaharisha ila kwa maji “mutwlaq” yenye jina la maji..” [Al-Mughny (1/11) na Al-Muhallaa (1/199)].
2- Maji yaliyonajisika
Ni maji yaliyochanganyika na najsi ikaathiri moja kati ya sifa zake kwa kubadilisha harufu yake, au rangi yake au ladha yake, kwa namna ambayo mtu akiyatumia, ataona kwa yakini kwamba anatumia najsi (badala ya maji).
Haijuzu kutawadhia kwa maji haya kwa vile yenyewe ni najsi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
023-Kutawadha Kwa Maji Yanayochuruzika Toka Viungo Vya Wudhuu
Alhidaaya.com [3]
Maji yanayochuruzika toka kwenye viungo vya mwenye kutawadha na mfano wake, huitwa “maji yaliyotumika”. Na bila shaka Maulamaa wamehitalafiana kuhusu maji hayo kama yanapoteza sifa ya kuwa ni yenye kutwaharisha au la.
Rai yenye nguvu ni kuwa maji hayo yanabakia ni yenye kutwaharisha madhali hayajapoteza jina la maji “mutwlaq” na wala hayajachanganyika na najsi ikaathiri moja kati ya sifa zake.
Haya ndio madhehebu ya ‘Aliy bin Abi Twaalib, Ibn ‘Umar, Abuu Umaamah na watangu wema wengi. Ni mashuhuri pia katika madhehebu ya Maalik. Aidha, ni moja kati ya riwaya mbili zilizopokelewa toka kwa Ash-Shaafi’iy na Ahmad. Pia ni madhehebu ya Ibn Hazm na Ibn Al-Mundhir. Mwelekeo huu pia umekhitariwa na Shaykh wa Uislamu (Ibnu Taymiyah). [Al-Mughny (1/31), Al-Majmuu (1/205), Al-Muhallaa (1/183), Majmuu Al-Fataawaa (20/519) na Al-Awswat (1/285)].
Kauli hii inatiliwa nguvu na dalili zifuatazo:
1- Kwamba asili ni kuwa maji ni twahara wala hayanajsiwi na chochote. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((الماء طهور لا ينجسه شيئ))
((Maji ni twahara, hayanajsiwi na chochote)).[Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (266), At-Tirmidhy (66) na An-Nasaaiy (1/173)].
Isipokuwa kama sifa yake moja itabadilika au yakapoteza jina la maji “mutwlaq” kwa kuchanganyika na kitu twahara.
2- Imethibiti kwamba Maswahaba walikuwa wakitumia mabaki ya maji aliyotawadhia Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). (Hii ni kwa dalili zifuatazo):
(a) Imepokelewa toka kwa Abuu Juhayfah akisema:
“Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitutokea mchana wa jua kali, akaja na maji ya kutawadhia kisha akatawadha. Hapo watu wakaanza kuchukua mabaki ya maji aliyotawadhia na kujipangusa nayo”.[Hadiyh Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (187)].
Al-Haafidh katika “Al-Fat-h” (1/353) anasema: “Inawezekana kuwa walichukua yale yaliyochuruzika toka kwenye viungo vya wudhuu vya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Na hii ni dalili wazi kuwa maji yaliyotumika ni twahara.
(b) Na katika Hadiyth ya Al-Masuur bin Makhramah: “…na anapotawadha Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), walikuwa wakikaribia kupigana kugombea maji aliyotawadhia”.[Hadiyh Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (189)].
(c) Imepokelewa na Abuu Musa Al-Ash’ary kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliagizia bilauri ya maji. Akaoshea mikono yake na uso wake humo na akatema. Kisha akamwambia yeye (Abuu Muusa) na Bilaal:
(( إشربا منه، وأفرغا على وحوهكما ونحوركما))
((Kunyweni humo, na yamiminieni kwenye nyuso zenu na shingo zenu)).[Hadiyh Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (188)].
3- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Umar akisema: “Katika enzi ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), wanaume na wanawake walikuwa wakitawadha wote pamoja”. [Hadiyh Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (193), Abuu Daawuud (79), An-Nasaaiy (1/57), na Ibn Maajah (381). Riwaya baada yake ni ya Abuu Daawuud kwa Sanad Swahiyh].
Na katika riwaya: “Katika enzi ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), tulikuwa sisi na wanawake tukitawadha katika chombo kimoja tukiingiza mikono yetu ndani”.
4- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiogea kwa mabaki (ya maji) ya Maymunah. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (323). Iko kwenye Swahiyh Mbili kwa tamko lisemalo: “Walikuwa wakiogea chombo kimoja”].
5- Imepokelewa toka kwa Al-Rubayi’i bin Mu’awwadh kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipangusa kichwa chake kwa mabaki ya maji yaliyokuwa mkononi mwake. [Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (130) na Ad Daaraqutwny (1/87)].
6- Ibn Al-Mundhir katika Al-Awswaat (1/288) amesema: “Na katika Ijma’a ya Maulamaa ni kwamba matone tone yaliyobakia katika viungo vya mwenye kutawadha au mwenye kuoga, na yale maji yaliyotona kwenye nguo zao, hayo yote ni twahara. Na hii ni dalili kuwa maji yaliyotumika ni twahara. Na kama ni twahara, basi hakuna maana kuzuia kutawadhia maji hayo bila ya hoja wanayoirejelea wale wenye rai tofauti na kauli”.
Inafaa kueleza hapa kwamba kundi la baadhi ya Maulamaa wamesema: “Haijuzu kutawadhia maji yaliyotumika”. Yamesemwa haya na Maalik, Al-Awzaa’iy, Ash-Shaafi’iy – katika riwaya moja kati ya mbili – na Abuu Haniyfah na wenzake. [Al-Istidhkaar (1/253), At-Tamhyid (4/43), Al-Mughny (1/19), na Al-Awswat (1/285)].
Maulamaa hawa hawana dalili yakinifu za kuridhisha. Mwenye kutaka, azirejee katika rejea tajwa.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
024- Inajuzu Kwa Mwanaume Kuogea Kwa Mabaki Ya Maji (Aliyojitwaharishia Mwanamke)
Alhidaaya.com [3]
'Ulamaa wana mielekeo miwili katika hukmu ya mtu kujitwaharisha kwa maji yaliyobakia baada ya mwanamke kutawadhia au kuogea.
Mwelekeo Wa Kwanza:
Haijuzu kwa mwanaume kujitwaharisha kwa mabaki ya mwanamke. Na haya ni madhehebu ya Ibn ‘Umar, ‘Abdullaah bin Sarjas, Mama wa Waumini Juwayriyah bint Al-Haarith, Al-Hasan, Ahmad bin Hanbal, Is-haaq, Ash-Sha’abiy na Daawuud Adh-Dhaahiriy. [Al-Awswat (1/292) na Al-Mughny (1/282)].
Hoja yao ni:
1- Yaliyopokewa toka kwa Al-Hakam bin ‘Amr kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza mtu kutawadhia mabaki ya maji aliyojitwaharishia mwanamke. [Maulamaa wameitia ila. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (82), At-Tirmidhiy (64), An-Nasaaiy (1/179), Ibn Maajah (373) na Ahmad (5/66). Al-Bukhaariy, Ad-Daarqutwniy na An-Nawawy wameitia dosari pia. Ama Ibn Hajar na Al-Albaaniy, wao wamesema ni Swahiyh katika “Al-Irwaai (1/43)].
2- Imepokelewa toka kwa Humayd Al-Humayriy akisema: “Nilikutana na mtu aliyesuhubiana na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa miaka minne kama alivyosuhubiana Abu Hurayrah. Alisema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza mwanamke kuogea mabaki ya mwanaume, au mwanaume kuogea mabaki ya mwanamke. (wachote wote kwa pamoja)”.[Isnadi yake ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (81), An-Nasaaiy (1/130) na Al-Bayhaqiy (1/190)].
3- Ni yale yaliyopokelewa toka kwa ‘Aliy bin Abiy Twaalib aliyesema: “Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na ahli wake, walikuwa wakiogea chombo kimoja, na haogei mmoja wao kwa mabaki ya mwenzake”.[Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Maajah (1/133)].
Mwelekeo Wa Pili:
Inajuzu mtu kujitwaharisha kwa mabaki ya mwanamke. Yamesemwa haya na “Umar, Abu Hurayrah, ‘Abdullah ibn ‘Abbaas, Ibn ‘Umar, Sa’ad bin Abiy Waqqaas, mjumuiko wa watangu wema, Abu ‘Ubayd na Ibn Al-Mundhir. Haya pia ndio madhehebu ya Hanafi, Maalik, Ash-Shaafi’iy na riwaya ya Ahmad. [Muswannaf ya ‘Abdur-Razzaak (1/110), Ibn Abi Shaybah (1/38), Al-Awswat (1/297), At-Twahuwr cha Abu ‘Ubayd (236), Al-Mabsutw (1/61), Al-Ummu (1/8) na Al-Mughny (1/283)].
Wametoa hoja kwa haya yafuatayo:
1- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiogea kwa mabaki ya Maymuunah. [Hadiyth Swahiyh. Imeshafanyiwa “ikhraaj” hapo nyuma].
2- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Abbaas akisema: “Ahli mmoja wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliogea kwenye beseni. Na Rasuli alipokuja alimwambia: Ee Rasuli wa Allaah! Mimi nilikuwa na janaba. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia:
(( إن الماء لا ينجس))
((Hakika maji hayapati janaba)). [Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (68), At-Tirmidhiy (65), An-Nasaaiy (1/173) na Ibn Maajah (370). Baadhi ya Maulamaa wameitia ila kwa riwaya ya Simaak toka kwa ‘Ikrimah. Riwaya hii imekorogeka. Lakini Al-Haafidh katika kitabu cha Al-Fat-h amewajibu kwamba Shu-’ubah amepokea toka kwake, na yeye hapokei toka kwa Mashaykh zake isipokuwa Hadiyth Swahiyh.. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi].
3- Imepokelewa toka kwa Mama wa Waumini ‘Aaishah aliyesema: “Nilikuwa mimi na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) tukioga katika chombo kimoja nailhali wote tuna janaba)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (299) na Muslim (321)].
Na katika riwaya nyingine: ((…wote tunachota humo)).
Lenye Nguvu:
Lenye kuridhisha na kuondosha shaka katika dalili za mwelekeo wa kwanza ni Hadiyth ya mtu aliyesuhubiana na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa miaka minne (ingawa Al-Bayhaqiy ameitia ila) pamoja na dalili zote za mwelekeo wa pili. Na dalili hizo zinaweza kuoanishwa kwa moja ya mawili: [Fat-hul Baary (1/300- Al Ma-’arifah), Subulus Salaam (1/28), na Naylul Awtwaar (1/26)].
1- Hadiyth zinazokataza zichukuliwe juu ya maji yanayochuruzika toka kwenye viungo, na Hadiyth za kujuzisha zichukuliwe juu ya maji yenye kubaki ndani ya chombo. Hivi ndivyo Al-Khatwaabiy alivyooanisha.
2- Katazo lichukuliwe juu ya ukaraha pamoja na kujuzu yote mawili.
Ninasema: “Na huenda hili la pili ndilo bora zaidi. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi".
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
025-Wudhuu Taarifu Yake Na Dalili Ya Usharia Wake
Alhidaaya.com [3]
Ama kiistilahi (kitaaluma), ni kutumia maji kwenye viungo maalumu; uso, mikono miwili, kichwa na miguu miwili, ili kuondosha kwayo kinachozuia kuswali na mfano wake.
Uthibiti wake umeashiriwa na Qur-aan, Hadiyth na Ijma’a. Ama katika Qur-aan, Allaah Mtukufu Anasema:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى الْكَعْبَيْنِ ۚ))
((Enyi walioamini! Mnaposimama kwa ajili ya Swalaah, basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni)). [Al-Maaidah (5:6)].
Ama katika Hadiyth, tunakuta kama vile:
1- Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) aliyesema: “Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((لا تقبل صلاة أحدكم إذا أحدث حتى يتوضأ))
((Haikubaliwi Swalaah ya yeyote kati yenu anapokuwa na hadathi mpaka atawadhe)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (135), Muslim (225) na wengineo].
2- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Umar akisema: “Hakika nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((لا يقبل الله صلاة بغير طهور، ولا صدقة من غلول))
((Allaah Haikubali Swalaah bila twahara, wala swadaqah ya mali haramu)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (224).
3- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Abbaas akisema: “Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((إنما أمرت بالوضوء إذا قمت إلى الصلاة))
((Hakika mimi nimeamrishwa kutawadha ninaposimama kuswali)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhy (1848), Abuu Daawuud (3760) na An-Nasaaiy ((1/73). Angalia kitabu cha Swahyhul Jaami’i (5761)].
4- Imepokelewa toka kwa Abuu Sa’iyd kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((مفتاح الصلاة الطهور، وتحريمها التكبير، وتحليلها التسليم))
((Ufunguo wa Swalaah ni kujitwaharisha, uingio wake ni Takbiyr, na utokaji wake ni kusema “Assalaamu ‘alaykum wa RahmatuLlaah”)). [Hadiyth Hasan Lighayrih. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhy (3), Abuu Daawuud ((60) na Ibn Maajah (275). Al- Albaany katika Swahiyhul Jaami’i ameizingatia kama ni Swahiyh].
Ama Ijma’a, ni kuwa Maulamaa wa Ummah wamekubaliana kwamba Swalaah haikamiliki ila kwa twahara kama itakuwa ni wepesi kufanya hivyo. [Al-Awsatw cha Ibn Al-Mundhir (1/107)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
026-Fadhla Za Wudhuu
Alhidaaya.com [3]
1- Ni kama nusu ya iymaan:
Ni kama katika Hadiyth ya Abuu Maalik Al-Ash‘ariy (Radhi za Allaah ziwe juu yake) aliyesema: “Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((الطهور شطر الايمان))
((Twahara ni nusu ya iymaan)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (223) na wengineo.]
2- Hufuta madhambi madogo madogo:
(a) Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((إذا توضأ العبد المسلم – أو المؤمن – فغسل وجهه خرج من وجهه كل خطيئة نظر إليها مع قطر الماء – أو مع آخر قطر الماء-، فإذا غسل يديه خرجت من يديه كل خطيئة كان بطشتها يداه مع الماء – أو مع آخر قطر الماء – فإذا غسل رجليه خرجت كل خطيئة مشتها رجلاه مع الماء – أو مع آخر قطر الماء – حتى يخرج نقيا من الذنوب))
((Anapotawadha mja Muislamu – au Muumini – akauosha uso wake, hutoka katika uso huo pamoja na matone ya maji kila kosa la kuangalia – au pamoja na tone la mwisho la maji - , na anapoosha mikono yake miwili, hutoka katika mikono hiyo pamoja na maji, kila kosa ambalo mikono yake imetumilia nguvu – au pamoja na tone la mwisho la maji - , na anapoosha miguu yake miwili, hutoka pamoja na maji kila kosa ambalo miguu yake ililiendea – au pamoja na tone la mwisho la maji, mpaka hutoka akiwa ametakasika kabisa na madhambi)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (244) na wengineo].
(b) Imepokelewa toka kwa ‘Uthmaan (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((من توضأ هكذا غفر له ما تقدم من ذنبه، وكانت صلاته ومشيه إلى المسجد نافلة))
((Mwenye kutawadha hivi, husamehewa dhambi zake zilizopita, na Swalaah yake na kwenda kwake Msikitini huwa ni thawabu ziada. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (229) na wengineo].
Fadhila na thawabu hizi hupatikana kwa uhakika zaidi kwa mwenye kuswali moja kwa moja Swalaah ya faradhi au ya Sunnah baada ya kutawadha.
(c) Katika Hadiyth ya ‘Uthmaan akizungumzia namna wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ulivyo, anasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((من توضأ مثل وضوئي هذا ثم قام فصلى ركعتين لا يحدث فيهما نفسه، غفر له ما تقدم من ذنبه))
((Mwenye kutawadha kama ninavyotawadha mimi hivi, kisha akasimama akaswali rakaa mbili, haizungumzishi nafsi yake ndani yake, ila hufutiwa dhambi zake zilizotangulia)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (6433), Muslim (226) na wengineo].
3- Hunyanyua daraja za mja:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((ألا أدلكم على ما يمحو الله به الخطايا ويرفع به الدرجات؟)) قالوا: بلى يا رسول الله! قال: ((إسباغ الوضوء على المكاره، وكثرة الخطا إلى المساجد، وانتظار الصلاة بعد الصلاة، فذلكم الرباط، فذلكم الرباط، فذلكم الرباط))
((Je, niwaambieni lile ambalo kwalo Allaah Huyafuta makosa na Hunyanyua kwalo daraja? Wakasema: “Tuambie, ee Rasuli wa Allaah! Akasema: Kutawadha kikamilifu pamoja na kuwepo uzito na ugumu, kukithirisha hatua kwenda Msikitini, na kusubiri Swalaah baada ya Swalaah, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo, basi hayo ni mambo ya mtu kujifunga nayo)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (251) na wengineo].
4- Ni njia ya kuelekea peponi:
(a) Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah iwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Bilaal:
(( يا بلال! حدثني بأرجى عمل عملته فى الاسلام، إني سمعت دف نعليك بين يدي في الجنة)). قال : ((ماعملت عملا أرجى عندي من أني لم أتطهر طهورا في ساعة من ليل أو نهار إلا صليت بذلك الطهور ما كتب لي أن أصلى))
((Ee Bilaal! Nielezee amali yenye matarajio zaidi uliyoifanya katika Uislamu, kwani mimi nimesikia mtaharuki wa viatu vyako mbele yangu huko peponi)).
Bilaal akasema: “Sikufanya amali yoyote yenye matarajio makubwa kwangu zaidi ya kuwa sikupata kujitwaharisha wakati wowote wa usiku au mchana, ila huswali kwa twahara hiyo kile nilichoandikiwa kukiswali”. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1149), Muslim (2458) na wengineo].
(b) Imepokelewa toka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (Radhi za Allaah ziwe juu yake) akisema: “Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((من توضأ فأحسن الوضوء ثم صلى ركعتين، يقبل عليهما بقلبه ووجهه، وجبت له الجنة))
((Mwenye kutawadha, akaukamilisha vyema wudhuu wake kama inavyotakikana, kisha akaswali rakaa mbili, akafanya khushui kwa moyo wake na uso wake (viungo vyake), basi ni lazima aingie peponi)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (234) An-Nasaaiy (1/80) na wengineo].
(5) Utakuwa ni alama itakayoupambanua Ummah huu wakati wa kupita kwenye hawdh:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikwenda makaburini akasema:
((السلام عليكم دار قوم مؤمنين وإنا- إن شاء الله- بكم عن قريب لاحقون، وددت لو أنا قد رأينا إخواننا)) قالوا: أو لسنا إخوانك يا رسول الله؟ قال: ((أنتم أصحابي، وإخواننا الذين لم يأتوا بعد)) فقالوا: كيف تعرف من لم يأت من أمتك يا رسو ل الله؟ قال: (( أرأيت لو أن رجلا له خيل غر محجلة بين ظهري خيل دهم بهم ألا يعرف خيله؟)) قالوا: بلى يا رسول الله، قال: ((فإنهم يأتون غرا محجلين من الوضوء، وأنا فرطهم على الحوض، ألا ليذادن رجال عن حوضى كما يذاد البعير الضال أناديهم ألا هلم فيقال: إنهم قد بدلوا بعدك، فأقول: سحقا سحقا))
((Amani iwe juu yenu nyumba ya jamaa ya Waumini. Na sisi bila shaka Apendapo Allaah tutakuwa nanyi hivi karibuni. Ningependa lau sisi tungeliwaona ndugu zetu)). Wakasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Je, sisi sio ndugu zako”? Akasema:
((Nyinyi ni Maswahaba zangu. Ama ndugu zangu, hao ni wale ambao hawajakuja bado)). Wakasema: “Ni vipi utamtambua yule ambaye bado hajakuja katika umati wako ee Rasuli wa Allaah?”. Akasema: ((Niambieni, lau kama mtu ana farasi wenye alama usoni na miguuni wakawa baina ya farasi weusi wasio na mabaka, je hawezi kuwatambua farasi wake?)). Wakasema: “Ndio, atawatambua ee Rasuli wa Allaah”. Akasema: ((Basi wao watakuja nailhali wana nuru nyusoni, miguuni na mikononi kutokana na wudhuu. Na mimi ndiye nitakayewatangulia kwenye hawdh. Basi jueni kwa yakini kwamba watu watazuiliwa na kufukuzwa wasije kwenye hawdh langu kama wanavyozuiliwa ngamia wasio na mchunga. Nitawaita: Haya njooni! Patasemwa: “Hakika hao walibadili baada yako”. Nitawaambia: Poteleeni mbali kabisa)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (234), An-Nasaaiy (1/80) na wengineo].
(6) Ni nuru kwa mja siku ya Qiyaamah:
Imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) akisema: “Nimemsikia Kipenzi changu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((تبلغ الحلية من المؤمنين حيث يبلغ الوضوء))
((Nuru ya Waumini itafikilia pale wudhuu unapofikilia)).
(7) Unafungua kifundo cha shaytwaan:
Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((يعقد الشيطان على قافية رأس أحدكم إذا هو نام ثلاث عقد يضرب كل عقدة: عليك ليل طويل فارقد، فإن استيقظ فذكر الله انحلت عقدة، فإن توضأ انحلت عقدة، فإن صلى انحلت عقدة، فأصبح نشيطا طيب النفس، وإلا أصبح خبيث النفس كسلان))
((Anapolala mmoja wenu, shaytwaan hufunga kisogoni mwake vifundo vitatu. Hupiga kila kifundo (kumwambia): Umebakiwa na usiku mrefu, basi lala. Anapoamka akamtaja Allaah, kifundo kimoja hufunguka. Anapotawadha, hufunguka kingine, na anaposwali cha tatu hufunguka. Hapo huwa mchangamfu na mwenye nafsi nzuri, na kama si hivyo, huwa na nafsi mbaya na mvivu)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1142) na Muslim (776)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
027-Sifa Ya Wudhuu Uliokamilika (Kiujumla)
Alhidaaya.com [3]
Imepokelewa toka kwa Humraan mwachwa huru wa ‘Uthmaan kwamba alimwona ‘Uthmaan bin ‘Affaan akiagiza chombo, kisha akamimina juu ya viganja vyake mara tatu na kuviosha. Kisha akauingiza mkono wake wa kuume kwenye chombo, akasukutua na kupaliza maji puani. Kisha akaosha uso wake mara tatu, na mikono yake hadi kwenye viwiko mara tatu. Halafu akapukusa kichwa chake, kisha akaosha miguu yake mara tatu hadi kwenye vifundo, kisha akasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
(( من توضأ نحو وضوئي هذا، ثم صلى ركعتين لا يحدث فيهما نفسه، غفر له ما تقدم من ذنبه))
((Mwenye kutawadha mfano wa wudhuu wangu huu, kisha akaswali rakaa mbili, haizungumzishi nafsi yake ndani yake, hughufiriwa madhambi yake yaliyopita)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (158) na Muslim (226)].
Na kutokana na Hadiyth hii na nyinginezo zitakazokuja kuzungumziwa kwa ufafanuzi, tunaweza kuiweka sifa ya wudhuu katika haya yafuatayo:
1-Atanuwia wudhuu kwa ajili ya kuondosha hadathi.
2-Atalidhukuru Jina la Allaah Mtukufu.
3-Ataviosha viganja vyake mara tatu.
4-Atateka maji kwa mkono wake wa kuume, kisha atayaweka mdomoni na puani kwa teko moja, atasukutua na kupaliza.
5-Atapenga kwa kutumia mkono wake wa kushoto. Atafanya hivi mara tatu.
6-Ataosha uso wake wote mara tatu pamoja na kupachanyisha ndevu.
7-Ataiosha mikono yake miwili – wa kulia kisha wa kushoto – mpaka juu ya viwiko viwili pamoja na kupachanyisha vidole vya mikono miwili.
8-Atapukusa kichwa chake chote kwenda nyuma na mbele mara moja.
9-Atapukusa masikio yake mawili nje na ndani.
10-Ataosha miguu yake miwili pamoja na vifundo vyake viwili - wa kulia kisha wa kushoto - pamoja na kupachanyisha vidole vya miguu miwili.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
028-Niya Ni Sharti Ya Kuswihi Wudhuu
Alhidaaya.com [3]
[Sharti ni jambo ambalo kutokuwepo kwake hulazimisha kutokuwepo, na kuwepo kwake hakulazimishi kuwepo au kukosekana kwa dhati yake. Sharti ni lazima iwepo kabla ya kitendo nje ya uhalisia wake].
Ili wudhuu uwe sahihi, ni lazima pawepo niya. Niya ni kuazimia kwa moyo juu ya kufanya tendo la kutawadha kwa ajili ya kufuata Maagizo ya Allaah Mtukufu na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kama ilivyo kwenye ‘ibaadah nyinginezo za kisharia. Allaah Mtukufu Anasema:
(( وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ))
(( Na hawakuamrishwa isipokuwa kumwabudu Allaah huku wakimtakasia Dini na kuwa mbali na shirki)). [Al Bayyinah (98:5)]
Na Rasuli ((Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
(( إنما الأعمال بالنيات، وإنما لكل امرء ما نوى...))
((Hakika matendo ni kwa niya, na kila mtu ni kwa lile alilolinuwiya..)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1) na Muslim (1907)].
Huu ndio msimamo walioukhitari Maalik, Ash Shaafi’iy, Ahmad, Abuu Thawr na Daawuud. [“Bidaayatul Mujtahid” (1/6), “Al-Majmuu” (1/374), na “At-Tamhiyd” (22/100,101)].
Lakini Abuu Haniyfah msimamo wake ni kuwa niya si sharti kwa ajili ya wudhuu, kwa kuwa wudhuu ni ‘ibaadah ya kidhahania na wala haikusudiwi kwa dhati yake. [Badaai’u Asw Swanaai-’i” (1/19 – 20)].
Mfano wake ni kama kutwaharisha uchafu. Kauli ya Jamhuri ya Maulamaa ndio sahihi kwa kuwa matni inatutaarifu kuwa thawabu zinapatikana katika kila wudhuu, na kwamba thawabu hazipatikani kwa kisichonuwiliwa kwa Ijma’a, na kuwa wudhuu ni ‘ibaadah ambayo haijulikani ila kwa sharia. Na kwa ajili hiyo, niya imekuwa ni sharti. [Al-Furu’u” cha Muflih (1/111)].
Mahala Pa Niya Ni Moyoni
Shaykh wa Uislamu (Allaah Amrehemu) anasema: [Majmuuat Ar-Rasaail Al-Kubraa (1/234)].
“Mahala pa niya ni moyoni na si katika ulimi kwa makubaliano ya Maimamu wa Kiislamu katika ‘ibaadah zote; twahara, Swalaah, Zakaat, Swaum, Hajji, kuacha huru mtumwa, Jihaad na kadhalika”.
Hakuna usharia ya kuitamka kwa sauti au kuikariri. Aliyezoea kufanya hivyo na hususan kama anawaudhi watu, inatakikana atiwe adabu au afanyiwe izari lakini baada ya kueleweshwa. Mwenye kuitamka niya, ni mkosa, na lau kama ataitakidi kwamba kuitamka ndio dini na ‘ibaadah kwa Allaah, basi huyo amezua. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba Zake hawakuwa wakiitamka niya kabisa, na hilo halikurekodiwa kutoka kwao. Na lau kama lingekuwa ni jambo la kisharia, basi Allaah Angelibainisha kupitia kwa Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Mbali ya hivyo, hakuna haja ya kuitamka niya, kwa kuwa Allaah Anaijua. [Angalia Zaadul Ma’aad (1/196), Ighaathat Al-Lahafaan (1/134), Badaai’ul Fawaaid (3/186), Al-Furu’u (1/111) na Sharhul Mumti-’i (1/159)].
Faida
1- Shaykh wa Uislamu anasema:
“Lau kama atatamka kwa ulimi wake kinyume na alichonuwia moyoni, kinachozingatiwa ni kile alichokinuwia na si alichokitamka. Na lau kama atatamka kwa ulimi bila kunuwia moyoni, basi hilo halitosihi kwa makubaliano ya Maimamu wa Kiislamu, kwa kuwa niya ndio makusudio na azima yenyewe”.
2- Hadathi zinazowajibisha kutawadha zikikusanyika pamoja kama mtu kwenda haja ndogo, kisha kubwa, halafu akalala, ikiwa atanuwia kuondosha moja tu kati ya hizo, basi zote zitaondoka – kwa kauli sahihi – kwa kuwa hadathi wasifu wake ni mmoja ingawa sababu zake ni tofauti. [Angalia Al-Majmu’u (1/385) na Ash Sharhul Mumti’i (1/165)].
3- Ni vyema kwa mwenye kutawadha anuwie kuondosha hadathi tu ili kuepukana na mahitilafiano ya Maulamaa katika kujuzisha baadhi ya picha za niya pasina nyinginezo. Picha hizi ni kunuwia kuondosha hadathi, au kunuwia twahara kwa lililo wajibu kwake, au kunuwia twahara kwa lililo sunna kwake, au kunuwia kujadidisha wudhuu kulikosuniwa. [Angalia namna Maulamaa walivyokhitilafiana katika masuala haya katika kitabu cha Al-Majmu’u (1/385)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
029-Nguzo Za Wudhuu
Nguzo za wudhuu ni mambo ambayo uhakika wake unajengekea kwayo kwa namna ambayo ikikosekana nguzo yoyote kati yake, basi wudhuu unabatilika na unakuwa hauzingatiwi kisharia. Nguzo hizo ni:
1- Kuosha uso wote:
Uso ni sehemu ya makabiliano. Na mpaka wake ni kutokea kwenye mapindio ya kipaji cha uso (au tokea kwenye maoteo ya kawaida ya nywele) mpaka kwenye mashukio ya ndevu na kidevu kwa urefu, na tokea kwenye sikio hadi sikio jingine kwa upana.
Kuosha uso ni nguzo kati ya nguzo za wudhuu. Wudhuu hautoswihi bila ya nguzo hii kwa neno Lake Subhaana:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ ))
(( Enyi walioamini! Mnaposimama kuswali, basi osheni nyuso zenu)). [Al Maaidah 5:6]
Kila aliyehadithia sifa ya wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), amethibitisha kuoshwa uso. Na Maulamaa wote wamekubaliana juu ya hili.
Ni Lazima Kusukutua Na Kupaliza:
Kusukutua ni kusafisha mdomo na kuyazungusha maji ndani yake. Na kupaliza, ni kuyafikisha maji mpaka ndani ya pua na kuyavuta kwa pumzi hadi mwisho wake. Ama kupenga, ni kuyatoa maji puani (kwa mpumuo) baada ya kuyapaliza.
Kusukutua na kupaliza maji, ni mambo ya lazima wakati wa kutawadha kwa mujibu wa kauli sahihi zaidi za Maulamaa. Na hii ni kwa dalili zifuatazo:
1- Ni kwamba Allaah Mtukufu Ameamuru kuosha uso kama ilivyotangulia. Na pua na mdomo ni sehemu ya uso, na wala hakuna chenye kuwajibisha kuhusisha nje yake bila ndani yake, kwani vyote hivyo viwili vinaitwa “uso” katika Lugha ya Kiarabu. Na kama utasema: “Tundu ya pua ina jina lake na pua ina jina lake, na hivyo haviitwi uso katika Lugha ya Kiarabu”, tunajibu tukisema: “Vilevile vitefute viwili, kipaji, mgongo wa pua, nyusi mbili na sehemu nyingine za uso, zina majina yake, na hivyo haviitwi uso! Huku ni kujikwaa kubaya, kwa kuwa kutamaanisha kwamba si lazima kuosha uso”. [Angalia Naylul Awtwaar (1/174) chapa ya Al-Jiyl na Ahkaamul Qur-aan cha Ibnul ‘Araby (2/563)].
2- Ni kwamba Allaah Mtukufu Ameamuru kuosha uso kiujumla, na Rasuli alilifasiri hilo kwa kulifanya kivitendo na kulifundisha. Akasukutua na akapaliza maji katika kila wudhuu aliotawadha. Na hakuna yeyote aliyenukulu kuwa aliacha kufanya hayo pamoja na kufupishia kwake juu ya kichache chenye kutosheleza. Na ikiwa kitendo chake kimefanyika kwa ajili ya kufuata amri, basi hukmu yake inakuwa ni hukmu ya jambo hilo katika kuhukumia ulazima. [Sharhul ‘Umdah cha Ibn Taymiyah (1/178) na At-Tamhiyd cha Ibn ‘Abdul Barri (4/36)].
3- Amri ya kupaliza na kupenga imethibiti kutokana na neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((من توضأ فليستنثر))
((Mwenye kutawadha, basi apenge)).
Na katika riwaya nyingine:
((إذا توضا أحدكم فليجعل في أنفه ماء ثم ليستنثر))
((Anapotawadha mmoja wenu, basi aingize maji puani mwake kisha apenge)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (161), Muslim (237) na wengineo].
Na kauli yake:
(( إذا توضأ أحدكم فليستنشق..))
((Anapowatadha mmoja wenu, basi apalize maji puani)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (237)].
Na kauli yake:
(( وبالغ في الاستنشاق إلا أن تكون صائما..))
((na ubalighishe katika kupaliza isipokuwa kama umefunga)).[Hadiyth Swahiyh. Itakariri mara nyingi].
Shaykh wa Uislamu anasema: “…Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutoa amri maalumu ya kupaliza, hakumaanishi kwamba ni muhimu zaidi kuliko kusafisha mdomo. Itawezekana vipi nailhali mdomo ndio sehemu tukufu zaidi ya kufanyia dhikri na kusoma, na mara nyingi hubadilika na kuwa na harufu mbaya?! Lakini kinachofananishwa hapa - na Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi – ni kuwa, mdomo ulipowekewa usharia wa kupigwa mswaki na jambo hilo likasisitizwa, na pia kuuosha kabla na baada ya kula, itakuwa imejulikana kuwa Allaah Mtukufu Ametoa kipaumbele zaidi cha kuusafisha kinyume na pua ambayo imetajwa kwa ajili ya kubainisha hukmu yake ili isipuuzwe…”. [Sharhul ‘Umdah (1/179 – 180)].
4- Ni kwamba amri ya kusukutua imekuja vile vile katika Hadiyth nyinginezo zenye uhakika zaidi. Ni kama Hadiyth ya Laqyt bin Swabrah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
(( إذا توضأت فمضمض))
((Ukitawadha, basi sukutua)).
Ninasema: “Na lau kama mtu atasema kwamba dalili za kuwajibisha kusukutua na kupaliza zimegeuzwa na kuelekezwa katika Sunnah kutokana na Hadiyth ya Rifa’a bin Raafi’i katika kisa cha mwenye kuswali vibaya ambaye Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia:
(( إنها لا تتم صلاة أحدكم حتى يسبغ الوضوء كما أمره الله تعالى، فيغسل وجهه ويديه إلى المرفقين ويمسح رأسه ورجليه إلى الكعبين...))
((Hakika haikamiliki Swalaah ya mmoja wenu mpaka akamilishe wudhuu wake kama Alivyoamrisha Allaah. Aoshe uso wake na mikono yake miwili hadi kwenye vifundo, na apake kichwa chake, na (aoshe) miguu yake miwili hadi kwenye vifundo…)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (859), At Tirmidhy (302), An Nasaaiy (2/20, 193) Ibn Maajah (460) na wengineo].
Hapa hakutaja kusukutua au kupaliza katika hayo ambayo Allaah Amemwamuru, na kwa hivyo amekwenda sawa na Aayah Tukufu. Hoja hii pia ni madhubuti na makinifu. Allaah Ndiye Mjuzi zaidi".
Faida
Fahamu kwamba Wanazuoni wamehitalifiana juu ya hukmu ya kusukutua na kupaliza katika wudhuu na kuoga katika kauli nne. [Ikhtilaaful ‘Ulamaa cha Al-Muruuziy (uk. 23-24), At-Tamhiyd (4/34), Al-Awsatw (1/379), At-Tahqiyq cha Ibn Al-Jawziy (1/143) na Al-Muhalla (2/50)].
Kauli ya kwanza:
Ni wajibu kusukutua na kupaliza wakati wa kuoga tu, lakini kwa wudhuu haipasi. Yamesemwa haya na Ath-Thawriy, Abu Haniyfah na wenzake na wengineo.
Kauli ya pili:
Ni Sunnah wakati wa kuoga na kutawadha. Haya yamesemwa na Maalik, Ash-Shaafi’iy, Al-Layth, Al-Awzaa’iy na jama‘ah.
Kauli ya tatu:
Yote mawili ni wajibu wakati wa kuoga na kutawadha. Haya yamesemwa na ‘Atwaa, Ibn Jurayj, Ibn Mubarak, Is-Haaq na riwaya iliyonukuliwa toka kwa Ahmad. Suala hili ni mashuhuri katika madhehebu ya Hanbali.
Kauli ya nne:
Kupaliza ni wajibu wakati wa kuoga na kutawadha, lakini kusukutua ni Sunnah. Yamesemwa haya na Ahmad katika riwaya, Abu ‘Ubayd, Abu Thawr na jopo la Maulamaa wa Hadiyth. Ibn Al-Mundhir ameichagua kauli hii.
Kuosha Ndevu Na Nywele Nyingine Za Uso
[Sharhu Fat-hil Qadiyr (1/12), Al-Mughniy (1/87) na Al-Majmuu’i (1/380)].
Ikiwa nywele zilizoota usoni (ndevu, masharubu, kilambamchuzi, kope na nyusi) ni nyingi kiasi ambacho ngozi inakuwa haionekani, basi itatosheleza kuosha juu yake tu. [Kilambamchuzi ni nywele zinazoota kati ya mdomo wa chini na kidevu].
Na kama ngozi inaonekana, basi itabidi ipate maji. Na ikiwa baadhi ni ndogo na nyingine ni nyingi, basi ni lazima ngozi ya nywele ndogo ipate maji na yenye nywele nyingi ioshwe juu tu.
Ama ndevu refu za singa, si lazima kuziosha zile zilizoshuka, bali inatosheleza kuosha zile tu zilizo katika mpaka wa uso, kwa vile kinachokusudiwa katika uso ni ngozi basi. Hii ni kwa mujibu wa kauli ya Abuu Haniyfah na riwaya toka kwa Ahmad.
Ama kwa mujibu wa Ash-Shaafi’iy na madhehebu ya Ahmad, ni lazima kuosha nywele singa vyovyote zitakavyokuwa zimeshuka, kwani nywele hizo zimeota katika mahali pa faradhi, na kwa ajili hiyo zinaingia katika wigo wa vyenye kuonekana. Na rai hii ina nguvu zaidi. Na Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi.
2- Kuosha mikono miwili hadi kwenye vifundo
Allaah Mtukufu Anasema:
(( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلاةِ فاغْسِلُواْ وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ))
(( Enyi mlioamini! Mnaposimama kwa ajili ya Swalaah, basi osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka vifundoni )).[Al Maaidah (5:6)].
Maulamaa wamekubaliana kwa sauti moja kuwa ni lazima kuosha mikono miwili wakati wa kutawadha.
Fahamu kuwa herufi ya )) (( إلىkatika Neno Lake Allaah Mtukufu:
(( أَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ ))
mikono yenu mpaka vifundoni
..ina maana ya “pamoja” kama ilivyo katika Neno Lake Allaah Mtukufu:
((وَلَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَهُمْ إِلَىٰ أَمْوَالِكُمْ ))
(( Na wala msile mali zao pamoja na mali zenu)). [An Nisaa (4:2)].
Na Neno Lake:
((وَيَزِدْكُمْ قُوَّةً إِلَىٰ قُوَّتِكُمْ))
(( Na Atawaongezeeni nguvu pamoja na nguvu zenu)). [Huud (11:52].
Al Mubarrid amesema: “Ikiwa mpaka unatokana na jinsi ya chenye kuwekewa mpaka, basi nao huingia”.
Na kwa ainisho hili, ni lazima vifundo viwili vijumuishwe wakati wa kuosha mikono. Na haya ndio madhehebu ya Jamhuri ya Maulamaa kinyume na baadhi ya wafuasi wa madhehebu ya Maalik. [Al-Mabswuut (1/6), Bidaayatul Mujtahid (1/11), Al-Majmu’u (1/389), na Al-Mughny (1/90)].
Msimamo huu wa Jamhuri ya Maulamaa unatiliwa nguvu na kitendo cha Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Imenukuliwa toka kwa Abuu Hurayrah kwamba yeye alitawadha, akaosha mikono yake hata akaingia katika kipanya, na akaosha miguu yake mpaka akaingia katika miundi miwili. Kisha alisema: “Hivi ndivyo nilivyomwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akitawadha.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (246)].
Kisha kaida ‘qaaidah’ (kanuni) inasema: “Lile ambalo wajibu hautimu ila kwalo, basi linakuwa ni wajibu”. Na kuosha mkono kikamilifu hakutojulikana ila kwa kuyazungusha maji kwenye vifundo viwili. [Ikhtiyaarat Ibn Qudaamah cha Al-Ghaamidiy (1/164)].
3- Kupaka kichwa
Allaah Mtukufu Anasema:
(( وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ ))
(( Na pakeni vichwa vyenu)). [Al Maaidah (5:6)]
.
Maulamaa wamekubaliana kwa sauti moja kuwa kupaka maji kichwani ni lazima. Lakini hata hivyo wamehitalifiana juu ya kiasi kinachotosheleza upakaji huo katika kauli tatu:
Kauli ya kwanza:
Ni lazima kupaka kichwa chote maji sawasawa kwa mwanamke au kwa mwanamume.
Haya ni madhehebu ya Maalik na Dhwaahir. Pia ni madhehebu ya Ahmad na kundi la wenzake, Abu ‘Ubayd na Ibn Al-Mundhir. Na Ibn Taymiyah ameuridhia msimamo huu. [Al-Mudawwanah (1/16), Al-Mughniy (1/92), Atw-Twahuur (uk. 358), Al-Awsatw (1/399) na Majmuu’i Al-Fataawa (21/123)].
Ushahidi wao ni haya yafuatayo:
1- Ni Neno Lake Allaah Mtukufu:
((وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ))
((Na pakeni vichwa vyenu))
Hapa “ب baa” ni ya kuambatisha (si ya usehemu). Kwa hiyo makadirio ya Aayah yanakuwa ni:
((وَامْسَحُوا رُءُوسِكُمْ))
Hii ni kama kuosha uso katika tayammum, kwani vyote katika Qur-aan Tukufu vimekuja kwa tamko moja. Allaah Anasema:
((فَامْسَحُوا بِوُجُوهِكُم))
((Na mwoshe nyuso zenu)). [Al Maaidah (5:6)] yaani uso wote.
2- Ni kwamba jambo hili limefasiriwa na Sunnah iliyonukuliwa toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Ni kuwa, yeye alipotawadha, alikuwa akipaka kichwa chake chote. Na kati ya yanayothibitisha hili, ni Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Zayd aliyesema: “Alitujia sisi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) tukamtolea maji katika ndoo ya shaba. Akatawadha; akaosha uso wake mara tatu, akaosha mikono yake mara mbili hadi katika vifundo, akapaka maji kichwani kwa kupeleka mkono mbele na nyuma na akaosha miguu yake miwili”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (185) na Muslim (235)].
Na katika tamko jingine “akapaka kichwa chake chote”.
3- Ni Hadiyth ya Al-Mughiyrah bin Shu’ubah aliyesema: “Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitawadha, akapukusa juu ya khufu zake, mbele ya utosi wake na juu ya kilemba chake”. [Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (275), Abuu Daawuud (150) na At-Tirmidhy (100). Hadiyth hii imejadiliwa sana. Na Al-Albaany Allaah Amrehemu, amesema kuwa ni Swahiyh].
Na lau kama ingetosheleza kupukusa mbele ya utosi, basi asingelipukusa juu ya kilemba. Kwa hivyo, hilo limeonyesha kuwa ni lazima kueneza (kichwa kizima).
Kauli ya pili:
Inatosheleza kupaka sehemu ya kichwa.
Ni madhehebu ya Abu Haniyfah na Ash-Shaafi’iy. [Al-Mabswuut (1/8), Al-Majmu’u (1/399), na Al-Mughny (1/92)].
Lakini pamoja na hivyo, wao wamehitalifiana juu ya kiasi kinachotosheleza. Wamesema ni nywele tatu, au robo ya kichwa au nusu!! Na hoja yao ni:
1- Kwamba “ب baa” katika Neno Lake Allaah Mtukufu:
((وَامْسَحُوا برُءُوسِكُمْ))
((Na pakeni vichwa vyenu)),
ni ya sehemu na si ya kuambatisha.
2- Yale yaliyopokelewa toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ya kuwa alipaka katika utosi wake.
Kauli ya tatu:
Ni lazima kupaka kichwa chote kwa mwanamume tu, si kwa mwanamke.
Ni riwaya iliyonukuliwa toka kwa Ahmad. Amesema: “Ninataraji kupaka maji kichwani kwa mwanamke kuwe ni sahali zaidi. ‘Aaishah (Allaah Amridhie) alikuwa akipaka mbele ya utosi wake.
Ibn Qudaamah anasema: “Na Ahmad ni katika mabingwa wa Hadiyth. Na hatolei dalili kwa tukio la kitu ila kama limethibiti kwake kwa Uwezo wa Allaah”. [Al-Mughny (1/93)].
Ninasema: “Ninaloliona lenye nguvu katika hayo yaliyotangulia ni kuwa ni lazima kupaka maji kichwa chote wakati wa kutawadha kutokana na nguvu ya hoja zake. Ama wale waliosema kuwa “ب baa” katika Aayah ni ya usehemu, basi hilo Siybawayhi amelikanusha katika sehemu kumi na tano katika kitabu chake. Na Ibn Burhan amesema: “Mwenye kudai kwamba “ب baa” inaonyesha usehemu, basi atakuwa amewaletea mabingwa wa Lugha jambo wasilolijua. [Naylul Awtwaar (1/155) na Al-Mughny (1/87)].
Mbali ya hivyo, hakuna Hadiyth yoyote Swahiyh toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inayoeleza kuwa yeye alifupishia kupaka baadhi ya kichwa chake tu. Lililothibiti ni kuwa yeye alipokuwa akipaka utosi wake, alikamilishia juu ya kilemba. [Majmu’u Al-Fataawa (21/122), Ahkaam Al-Qur-aan cha Ibn Al-‘Arabiy (2/571) na Subul As-Salaam (1/107)].
Ama mwanamke, mimi siijui dalili yoyote ya kumbagua yeye na mwanamume katika hilo. Lakini inajuzu kwake kupaka maji juu ya mtandio wake. Na lau kama amepaka utosi wake pamoja na mtandio wake, basi hilo litakuwa ni bora ili kuepukana na mvutano. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi”.
Faida
Ikiwa kichwa kimepakwa hina ghafi au mfano wake, itajuzu kupaka maji juu yake. Kwani imethibiti toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba yeye alikuwa akikipaka kichwa chake hina akiwa katika ihramu yake na hakuwa akijisumbua kuitoa kwa ajili ya wudhuu (kama itakavyokuja katika mlango wa Hijjah). Hii ni kwa vile kilichowekwa kichwani kinakuwa ni sehemu ya kichwa. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
4- Kupaka masikio mawili:
Ni lazima kupaka masikio mawili pamoja na kichwa, kwani masikio ni sehemu ya kichwa. Imepokelewa toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba amesema:
(( الأذنان من الرأس ))
((Masikio mawili ni sehemu ya kichwa )). [Hadiyth Dhwa’iyf: Ina njia nyingi na zote zina kasoro. Pia pamekhitalifiwa katika kuifanya ni Hadiyth Hasan kwa vikundi vyake. Na Mwanachuoni Mweledi Al-Albaaniy Allaah Amrehemu katika Kitabu chake cha Asw-Swahiyhah amesema kuwa huenda Hadiyth hii ikapanda kufikia ngazi ya Hadiyth Mutawaatir kwa baadhi ya Maulamaa!! Shaykh wetu (Allaah Amhifadhi), ameitolea maelezo ya kichambuzi katika Al-Nadhwaraat na akatilia nguvu udhwaifu wake, nalo ni jambo sawa kabisa. Na Shaykh Mash-huur Hasan (Allaah Amhifadhi) amesema kuwa ni Dhwa’iyf baada ya utafiti wa kina alioufanya pambizoni mwa Kitabu cha Al-Khilaafiyyaat kilichotungwa na Al-Bayhaqiy (1/448)].
Hadiyth hii ni Dhwa’iyf Marfu’u kwa kauli yenye nguvu. Lakini hata hivyo imethibiti kwa watangu wema wengi akiwemo Ibn ‘Umar. [Isnadi yake ni Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ad-Daar Qutwniy (1/98), Ibn Abuu Shaybah (1/28) na wengineo].
Na kuna Hadiyth zinazolitolea hilo ushahidi. Ni kama ile inayoashiria kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipaka kichwa chake na masikio yake mara moja. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (133), At-Tirmidhiy (36), An-Nasaaiy (1/74), Ibn Maajah (439) na wengineo. Ina njia mbalimbali za kuifanya kuwa Swahiyh zilizonukuliwa toka kwa Ibn ‘Abbaas. Na asili yake iko kwa Al-Bukhaariy (157) kwa ufupi. Pia ina ushahidi toka kwa Hadiyth ya Ar-Rubayi’i binti Mu’awwidh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (126), At-Tirmidhiy (33) na Ibn Maajah (418). Vilevile imenukuliwa toka kwenye Hadiyth ya Al-Miqdaam].
Hadiyth hizi ni nyingi zilizonukuliwa toka kwa ‘Aliy, Ibn ‘Abbas, Ar-Rubayyi’i na ‘Uthmaan. As-Swan-’aaniy anasema: “Wote wamekubaliana kuwa kuyapaka masikio na kichwa ni mara moja tu”, yaani kwa maji hayo hayo kama inavyoonekana kutokana na tamko la “mara moja”. Kwa vile, lau kama masikio yangekuwa yanatekewa maji mapya, basi kusingelithibitishwa ya kuwa “yeye alipaka kichwa na masikio mara moja”. Na kama itachukulika kwamba mapendeleo ni kuwa yeye hakukariri kuyapaka bali aliyatekea maji mapya, basi huo ni uwezekano wa mbali”. [Subulus Salaam (1/49)].
Ninasema: "Na kama atateka maji mengine ya kupaka masikio, basi hapana ubaya. Kwani hilo limethibiti toka kwa Ibn ‘Umar". [Isnadi yake ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na ‘Abdur Razzaaq (29) na Al-Bayhaqiy (1/65).]
Angalizo
Hakuna usharia wowote wa kuosha shingo wakati wa kutawadha, kwa vile hakuna Hadiyth yoyote Swahiyh iliyopokelewa toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ikiligusia hilo. [Majmu'u Al-Fataawa (1/56) na Zaad Al-Ma’ad (1/49). Tizama As-Silsilat Adh-Dhwa’iyfah (69-744)].
5- Kuosha miguu miwili pamoja na vifundo
Vifundo viwili ni mifupa miwili iliyochomoza katika pambizo mbili za mguu. Kuosha miguu miwili ni lazima kwa Jamhuri ya Maulamaa wa Ahlus-Sunnah kutokana na Neno Lake Allaah Mtukufu:
((وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى الْكَعْبَيْنِ))
((Na miguu yenu hadi kwenye vifundo viwili)). [Al Maaidah (5:6)].
Ni kwa kuweka “fat-hah” juu ya “arjulakum” kuunganishia kwenye viungo vinavyooshwa.
Na kila aliyehadithia sifa ya wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amethibitisha kwamba aliosha miguu miwili hadi kwenye vifundo viwili. Na kati ya yaliyoelezewa ni yale yanayomhusu ‘Uthmaan yanayosema: “..Kisha akaosha miguu yake miwili hadi katika vifundo mara tatu….”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (158) na Muslim (226)].
Na vifundo viwili hujumuishwa katika kuoshwa, kwani ikiwa mpaka unatokana na jinsi ya chenye kuwekewa mpaka, basi nao huingia kama ilivyotangulia. Na Hadiyth ya Ibn ‘Amri (Allaah Amridhie) inaonyesha juu ya haya. Anasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikawia nyuma katika safari. Kisha alituwahi nailhali alasiri imekurubia kumalizika wakati wake. Tukaanza kutawadha huku tukipaka miguu yetu. Hapo akanadi kwa sauti kubwa:
((ويل للأعقاب من النار))
((Ole wao na moto kwa (kutoosha) visigino)).
Alisema mara mbili au tatu. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (161) na Muslim (241)].
Ama yale yaliyopokelewa ya kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipaka (miguu) katika wudhuu wake, linalochukuliwa ni kupaka juu ya khufu mbili, nalo ni jambo ambalo yeye aliliruhusu. Suala hili Maraafidha na Mashia wengi wamekwenda kinyume nalo wakisema kuwa ni lazima kupaka miguu miwili badala ya kuosha. Na lililo sahihi kutumiwa ni la kwanza. ‘Abdur-Rahmaan bin Abi Layla anasema: “Maswahaba wote wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wamekubaliana juu ya kuosha miguu miwili”. [Fat-hul Baariy (1/266) na Al-Mughniy (1/120)].
6-Kupachanyisha vidole vya miguu na mikono:
Vidole na sehemu zilizo kati yake, ni sehemu ya mahala pa faradhi. Kwa hiyo ni lazima zioshwe. Na kama haitowezekana kuoshwa ila kwa kupachanyishwa, basi ni lazima kufanya hivyo. Na kama itawezekana, basi itapendeza kama itakavyokuja.
7- Kupangilia:
Ni kuvitwaharisha viungo vya wudhuu kimoja baada ya kingine kwa mpangilio ambao Allaah Ameamrisha katika Aayah Tukufu. Ataosha uso, kisha mikono miwili, kisha atapaka kichwa, halafu ataosha miguu miwili. Mpangilio huu ni wajibu katika kauli sahihi zaidi kati ya kauli mbili za Maulamaa. Na hayo ndiyo madhehebu ya Ash-Shaafi’iy, Hanbali, Abu Thawr, Abu ‘Ubayd na Adh-Dhwaahiriyya. [Al-Majmu’u (1/433), Al-Mughny (1/100), na Al-Muhalla (2/66)]. Wajibu huu wameutolea hoja kwa haya yafuatayo:
1- Ni kwamba Allaah Mtukufu Ametaja katika Aayah ya faradhi za wudhuu kimpangilio pamoja na kutenganisha miguu miwili na mikono (ambavyo ni lazima vioshwe) kwa kichwa ambacho ni lazima kipakwe. Na Waarabu hawakitenganishi kitu na chenziye ila kwa faida fulani. Na hapa Aayah inaashiria ulazima wa kupangilia. [Kama hivyo katika Al-Mughny (1/100)].
2- Ni kwamba kila aliyehadithia kuhusu wudhuu wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), ameuelezea ukiwa umepangika. [Maswahaba 20 wamehadithia sifa ya wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakinukulu toka kwake. Wote wameuelezea kwa mpangilio isipokuwa katika Hadiyth mbili Dhwa’iyf ambazo Al-Albaaniy amesema kuwa ni Swahiyh katika kitabu cha Tamaam Al-Minnah (uk.85)].
Na kitendo chake hicho kinafasiri Kitabu cha Allaah Mtukufu.
3- Ni kwa yale yaliyohadithiwa kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitawadha kimpangilio kisha akasema:
(( هذا وضوء لا يقبل الله الصلاة إلا به))
((Huu ndio wudhuu, Allaah Haikubali Swalaah ila kwao)).
Lakini Hadiyth hii ni Dhwa’iyf. [Hadiyth Dhwa’iyf. Angalia Al-Irwaa (85)].
Lakini Maalik, Ath-Thawriy na Abuu Haniyfah na wenzake, wao wanasema kuwa kupangilia ni jambo lililosuniwa na wala si wajibu. [Al-Mudawwanah (1/14), Al-Mabsuwtw (1/55), na Sharhu Fat-hil Qadyr (1/30)].
Hoja yao ni:
1- Kwamba kiunganishi kihusishi “و waw” katika Aayah, hakihukumii mpangilio. Jibu la haya, liko katika yaliyotangulia.
2- Ni yale yaliyopokelewa toka kwa ‘Aliy na Ibn Mas-’oud kwamba wamesema: “Haijalishi ni kwa kiungo gani nilichoanzia”. [Athar ya ‘Aliy. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad katika kitabu cha Al-’Ilal (1/205), Ibn Abiy Shaybah (1/55) na Ad-Daarqutwniy (1/88), Sanad yake ni Dhwa’iyf. Pia athar ya Ibn Mas-’oud iliyofanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy katika kitabu cha Al-Taariykh (1650) na Abu ‘Ubayd katika At Twahuur (325) kwa Sanad Hasan kwa tamko la: “Akitaka ataanza kushoto kwake katika wudhuu kama alivyosema Imaam Ahmad].
Hili linajibiwa kwa kauli ya Al- Imam Ahmad kama ilivyo katika “Masuala ya mwanawe ‘Abdullaah” aliposema (27-28):
“Bila shaka ina maana ya kushoto kabla ya kulia. Na hakuna ubaya kuanza kwa kushoto kwake kabla ya kulia kwake, kwani matoleo yake toka katika Qur-aan ni mamoja. Allaah Mtukufu Anasema:
((فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ))
(( Basi osheni nyuso zenu na mikono yenu hadi kwenye vifundo, na mpake vichwa vyenu, na (mwoshe) miguu yenu)). [Al Maaidah (5:6)].
Kwa hiyo, hapana ubaya kuanza kushoto kabla ya kulia”.
Ninasema: “Na ingawa ubora ni kuanzia kulia kwa ajili ya kufuata Sunnah. Na Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi".
8- Kuandamisha:
Ni kufuatilizia uoshaji wa viungo vya wudhuu kwa namna ambayo kisikauke kiungo kabla hajaingia kiungo kingine katika muda wa wastani.
Ash-Shaafi’iy katika kauli yake ya zamani na Ahmad katika Al-Mash-hur wanasema kuwa ni lazima kuandamisha. Pia Maalik anasema hivyo hivyo isipokuwa yeye ametofautisha kati ya aliyekusudia kutoandamisha na kati ya mwenye udhuru. Na haya ndiyo aliyoyachagua Shaykh wa Uislamu. [Al-Ummu (1/30), Al-Majmu'u (1/451), Kash-Shaaf Al-Qina’i (1/93), Al-Mudawwanah (1/15), Al-Istidhkaar (1/267) na Majmu'u Al-Fataawaa (21/135)].
Ulazima wa kuandamisha unaashiriwa na Hadiyth ya ‘Umar bin Al-Khattwaab kwamba mtu mmoja alitawadha akaacha sehemu ndogo ya kucha katika miguu yake. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwangalia kisha akamwambia:
(( إرجع فأحسن وضوءك ))
(( Rejea ukatawadhe vizuri)).
Akarejea, kisha akaswali. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (232), Ibn Maajah (666) na Ahmad (1/21). Hadiyth hii imetiwa baadhi ya dosari, lakini ina vithibitisho vyake vinavyoifanya kuwa Swahiyh bila ya shaka yoyote. Angalia katika At-Talkhiysw (1/95) na Al-Irwaa (86)].
Na katika riwaya iliyopokelewa na baadhi ya Maswahaba wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwona mtu mmoja akiswali nailhali juu ya mguu wake kuna sehemu nyeupe ya ukubwa wa dirham haikupata maji. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwamrisha atawadhe upya na aswali tena. [Al-Albaaniy amesema ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (175) na Ahmad (3/424) kupitia kwa Buqayyah bin Al-Waliyd toka kwa Bahiyr aliyepokea toka kwa Khaalid. Buqayyah ameeleza kwamba amesikia toka kwa Bahiyr kwa mujibu wa yaliyoandikwa na Ahmad, na ambaye amesema kwamba Isnadi yake ni Hasan. Na kwa ajili hiyo, Al-Albaaniy katika Al-Irwaa (86), amesema ni Swahiyh. Ninasema: “Ni Hadiyth Hasan lau si kuhofiwa kumwadilisha Buqayyah. Hakueleza kwamba Bahiyr amesikia toka kwa Khaalid!”].
Abu Haniyfah na Ash-Shaafi’iy katika madhehebu mapya wanasema kuwa kuandamisha si lazima. Nayo ni riwaya iliyopokelewa toka kwa Ahmad, na pia ni madhehebu ya Ibn Hazm. [Al-Mabsuwtw (1/56), Al-Ummu (1/30), Al-Majmuu’ (1/451) na Al-Muhalla (2/70)].
Wamesema:
1- Kwa vile Allaah Mtukufu Amewajibisha kuosha viungo, hivyo basi, mwenye kuviosha, atakuwa amefanya wajibu wake, ni sawa awe ameviosha kiholela bila mpangilio au akaviosha kwa mpangilio uliopangika.
2- Ni kwa aliyoyahadithia Naafi’i kwamba Ibn ‘Umar alitawadha sokoni, akaosha uso wake na mikono yake na akapaka kichwa chake. Kisha aliitwa kwenda kuswalia maiti, akaingia Msikitini, kisha akapaka juu ya khufu zake na akaswali. [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Maalik (48) na kutoka kwake akapokea Ash-Shaafi’iy (16) na Al-Bayhaqiy katika Al-Ma’arifah (99)].
3- Hadiyth yenye amri ya kutawadha na kuswali upya, wanaizingatia kwamba ni Dhwa’iyf.
4- Wameliawilisha neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Rejea ukatawadhe vizuri)) kwamba makusudio yake ni kukamilisha kuosha sehemu ambayo haikupata maji mguuni.
Ninasema: “Hukmu ya mvutano wa yaliyotangulia ni Hadiyth ya Khaalid bin Mi’idaan yenye amri ya kutawadha tena na kuswali upya aliyoinukuu toka kwa baadhi ya Maswahaba wa Rasuli. Aliyeifanya kuwa ni Swahiyh, amesema ni lazima, na kama si hivyo, basi hoja zilizobakia zina uwezekano wa hili au lile. Ninaloliona mimi kuwa ni sawa, ni ulazima wa kuandamisha kutokana na Hadiyth hii. Pia, ni kwa vile wudhuu ni ‘ibaadah moja, isitenganishwe. Ama athar ya Ibn ‘Umar, inavyoonekana ni kuwa hiyo ni katika hali ya udhuru na kulazimika, na kwa hivyo, haipimiwi na hali ya kawaida. Na Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi. Lakini ikiwa patatokea mtengano kidogo katika kuosha viungo, basi hakuna ubaya. Na Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi.”
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
030-Sunnah Za Wudhuu
Alhidaaya.com [3]
1- Kupiga mswaki:
Jambo hili limekwishadokezwa kuwa linapendeza katika mlango wa “Sunnah za hulka asili”.
2- Kupiga Bismillaah mwanzoni:
Kiilivyo, kupiga Bismillaahi ni jambo zuri la kisharia katika mambo yote. Kuna Hadiyth dhwa’iyf zilizopokelewa kuhusu kupiga bismillaahi wakati wa kutawadha ingawa baadhi ya Maulamaa wamesema kuwa Hadiyth ni Swahiyh. Kati ya Hadiyth hizo ni ile isemayo:
((ولا وضوء لمن لم يذكر اسم الله عليه))
((Hana wudhuu asiyelitaja Jina la Allaah)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (101), At-Tirmidhiy (25), Ahmad (2/418) na wengineo. Lenye nguvu ni kuwa Hadiyth hii ni Dhwa’iyf. Shaykh Al-Albaaniy Allaah Amrehemu katika kitabu cha Al-Irwaai”(1/122), amesema kuwa ni Hadiyth Hasan. Shaykh Mtukufu Abuu Is-Haaq Al Huwayny – Allaah Amhifadhi – amechangia kidogo katika kuupitisha uswahiyh wake. Uswahiyh wake uko karibu zaidi. Allaah Ndiye Mjuzi zaidi].
Na kuna Hadiyth nyingine Dhwa’iyf sana zisizofaa kabisa kutegemewa kwa hoja. Na kwa ajili hiyo, Imaam Ahmad amesema: “Siijui Hadiyth yoyote katika mlango huu yenye Isnadi Hasan”.
Ninasema (Abuu Maalik): “Linalotilia nguvu kutokuwepo ulazima wa kupiga bismillaahi ni kuwa watu walioelezea sifa ya wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hawakutaja kuhusu bismillaahi. Na haya ni madhehebu ya Ath-Thawriy, Maalik, Ash-Shaafi’iy na Abuu Haniyfah na wenzake. Ni riwaya toka kwa Ahmad. [Vitabu vya Fat-hul Qadiyr (1/22), Mawaahib Al-Jaliyl (1/266), Majmu'u (1/385) na Al-Insaaf (1/128)].
3- Kuosha viganja viwili mwanzoni:
Ni kwa yale yaliyomo katika Hadiyth ya ‘Uthmaan katika sifa ya wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). ‘Uthmaan anasema: “Akamiminia katika viganja vyake mara tatu, akaviosha…”[Hadiyth Swahiyh Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (159) na Muslim (226)].
4- Kusukutua na kupaliza maji mara tatu kwa teko moja:
Ni kwa yale yaliyomo katika Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Zayd alipokuwa akifundisha namna Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alivyokuwa akitawadha: “Kwamba yeye (Rasuli) alisukutua na akapaliza kwa teko moja. Akafanya hivyo mara tatu”.[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (235), At-Tirmidhy (28) na Ibn Maajah (405)].
5- Kuyakomeza maji hadi mwisho wakati wa kusukutua na kupaliza kwa ambaye hakufunga:
Ni kwa Hadiyth Marfu’u ya Laqiyt bin Swabrah:
وبالغ في الاستنشاق إلا أن تكون صائما
((Na komeza maji hadi mwisho isipokuwa kama umefunga)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (142), An-Nasaaiy (1/66), Ibn Maajah (407) na Ahmad (4/33)].
6- Kutanguliza kulia kabla ya kushoto:
Katika Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas kuhusu sifa ya wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “…kisha alichukua teko la maji akaosha kwalo mkono wake wa kulia, kisha akachukua teko jingine akaosha kwalo mkono wake wa kushoto, kisha alipaka kichwa chake maji, kisha alichukua teko la maji, akanyunyizia kwalo mguu wake wa kulia mpaka akauosha, kisha alichukua teko jingine akaosha kwalo mguu wake, yaani wa kushoto….”[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (140)].
Na imepokelewa toka kwa ‘Aaishah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akipenda kuanza kwa upande wa kulia wakati wa kuvaa viatu, kutembea, kujitwaharisha na katika kila jambo lake alilolifanya. [Hadiyh Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (168) na Muslim (268)].
7- Kuviosha viungo mara tatu:
Imepokelewa Hadiyth Swahiyh toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ya kwamba alitawadha (akiviosha viungo) “mara moja moja”, [Hadiyh Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (156) toka kwa Ibn ‘Abbaas.]…na kwamba aliviosha “mara mbili mbili”. [Hadiyh Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (157) toka kwa ‘Abdullaah bin Yaziyd]. Na ukamilifu na utimilifu zaidi wa wudhuu ni kuviosha viungo mara tatu kama alivyofanya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mujibu wa ilivyoelezewa katika Hadiyth za ‘Uthmaan na ‘Abdullaah bin Zayd. Hadiyth hizi zimekwisha zungumziwa.
Zindushi mbili
(a) Kupukusa kichwa ni mara moja tu:
Asipukuse mara mbili au tatu kulikoelezewa kiujumla katika Hadiyth za sifa ya wudhuu wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Ama riwaya zinazoelezea kuwa kupukusa kichwa ni mara tatu, riwaya hizo si Swahiyh. Ama zile zinazoelezea kwamba Rasuli alipukusa mara mbili, basi hiyo ni tafsiri ya neno lake:
((فأقبل بهما وأدبر))
((Ipeleke mbele na nyuma)), kama alivyosema Ibn ‘Abdul Barri. [Al-Khilaafiyyaat cha Al-Bayhaqiy (1/336). Kimetolewa maelezo na maoni na Shaykh Mash-huur Aali Salmaan. Angalia pia At-Twahuwr cha Abu ‘Ubayd (uk 359)].
Kuipelekea mikono miwili mbele na nyuma wakati wa kupukusa kichwa, hakuzingatiwi kama ni kukariri, kwa kuwa kukariri kunakuwa ni kwa kuchukua tena maji upya. Kisha kukariri, kumestahabiwa tu kwa viungo vinavyooshwa na si kwa vile vinavyopukuswa. [Muqaddimaat Ibn Rushd Alal Mudawwanah (uk 16)].
Na kati ya dalili imara zinazoonyesha kwamba kichwa hakipukuswi zaidi ya mara moja, ni Hadiyth ya bedui aliyekwenda kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumuuliza namna ya kutawadha. Rasuli akamwonyesha kila kiungo mara tatu tatu, kisha akasema:
(( هذا الوضوء، فمن زاد على هذا فقد أساء وتعدى وظلم))
((Huu ndio wudhuu. Atakayezidisha zaidi ya hivi, basi amefanya ubaya, amepetuka mipaka, na amedhulumu)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na An Nasaaiy (1/88), Ibn Maajah (422) na Ahmad (2/180)].
Al Haafidh katika “Al Fat-h” (1/298) anasema: “Riwaya ya Sa’iyd bin Mansour, ina kiashirio kwamba alipukusa kichwa chake mara moja tu, hivyo basi, inaonyesha kwamba kupukusa kichwa zaidi ya mara moja, si jambo mustahabu. Yaliyokuja kwenye Hadiyth zinazoelezea kupukusa mara tatu – kama zitakuwa ni Swahiyh – yanaweza kuchukulika kama ni kwa lengo la kukipukusa kichwa chote kikamilifu, na si kwamba kila mpukuso na hesabu yake. Na hii ni kwa ajili tu ya kuoanisha kati ya dalili”.
Ninasema: “Haya ni madhehebu ya Abuu Haniyfah, Maalik na Ahmad (katika Swahiyh kutoka kwake) kinyume na Ash Shaafi’iy Allaah Awarehemu”. [Al-Mabsuwtw (1/5), Haashiyat Ad-Dusuwqy (1/98), Al-Mughny (1/127) na Al-Umm (1/26)].
(b) Ni karaha kuzidisha zaidi ya mara tatu kwa aliyeosha viungo kikamilifu:
Kuosha mara tatu viungo vya wudhuu, ndio wudhuu uliokamilika na uliotimia. Ni karaha kuzidisha zaidi ya mara tatu kutokana na Hadiyth:
((فمن زاد على هذا فقد أساء وتعدى وظلم))
((Atakayezidisha zaidi ya hivi, basi amefanya ubaya, amepetuka mipaka, na amedhulumu)).
Mahala pa maneno haya, ni pale ziada inapofanywa si kwa ajili ya kukamilisha upungufu. Na kama viungo vyake vitaosheka kikamilifu mara tatu au chini yake, itakuwa ni karaha kuongeza zaidi ya mara tatu. Haya hayana mabishano kabisa. [At-Tamhiyd cha Ibn ‘Abdul Barri (20/117) kwa mfano wake kwa muhtasari].
8- Kuziasulia ndevu nyingi:
Tumekwisha eleza kwamba kama ndevu ni nyingi zilizoficha ngozi, basi itatosha kuosha nje yake tu. Na hapa tunaongeza kusema kuwa imesuniwa kuziasulia kwa maji kutokana na Hadiyth ya Anas isemayo kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakati wa kutawadha, alikuwa akichukua teko la maji, kisha huliingiza chini ya kaakaa na kuasulia kwalo pia. Kisha Rasuli husema:
((هكذا أمرني ربي عز وجل))
((Hivi ndivyo Mola wangu Ázza wa Jalla Alivyoniamuru)). [Hadiyth Swahiyh Lighayrih. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (145), Al-Bayhaqy (1/54) na Al-Haakim (1/149). Angalia Al-Irwaa (92).
Na jambo hili linageuzwa kuwa Sunnah kutokana na Hadiyth iliyotangulia hapo kabla ya Rifa’a bin Raafi’i inayozungumzia kisa cha mwenye kuswali vibaya.
9- Kusugua viungo:
Ni kwa Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Zubayr aliyesema: “Nilimwona Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akitawadha, na kisha akaingia kuisugua mikono yake miwili”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Hibaan (1082) na Al-Bayhaqy (1/196)].
10- Kuasulia vidole vya mikono na miguu:
Ni kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((أسبغ الوضوء، وخلل الأصابع، وبالغ في الاستنشاق إلا ان تكون صائما))
((Tawadha wudhuu kamili, asulia vidole, na ubalighishe katika kupaliza maji, isipokuwa kama umefunga)).[Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo].
Na kama vidole na sehemu za kati yake haviosheki ila kwa kuasulia, basi wakati huo itakuwa ni lazima kufanya hivyo kama tulivyotangulia kusema.
11- Kuosha zaidi ya mpaka wa faradhi:
Imesuniwa kutawadha kikamilifu, kurefusha kuosha uso hadi katika ncha ya utosi, na kuosha juu zaidi ya vifundo viwili na visigino. Katika Hadiyth ya Abu Hurayrah, Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((إن أمتي يأتون يوم القيامة غرا محجلين من آثار الوضوء))
((Hakika umati wangu utakuja siku ya Qiyaama hali ya kuwa nyuso zao, mikono yao na miguu yao inang’ara kutokana na athari za wudhuu)).
Abu Hurayrah anasema: “Basi yeyote kati yenu atakayeweza kurefusha kuosha uso, basi na afanye”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (36) na Muslim (246)].
Na imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah kwamba alitawadha, akaosha mikono yake hadi akaingia kuosha vipanya vyake, akaosha miguu yake miwili hadi akaingia kuosha miundi yake. Kisha alisema: “Hivi ndivyo nilivyomwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akitawadha”.[ Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (246).
Na imepokelewa tena toka kwake akisema: Nimemsikia kipenzi changu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((تبلغ الحلية من المؤمن حيث يبلغ الوضوء))
((Nuru ya Muumini inafikia pale wudhuu unapofikia)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (250)].
12- Kutumia maji kwa uangalifu:
Ni kwa Hadiyth ya Anas aliyesema: “Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiogea maji ya lita 2 hadi lita 2½, na akitawadha kwa maji ya ½ lita”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (198) na Muslim (325)].
13- Du’aa baada ya kutawadha:
Imepokelewa toka kwa ‘Umar amesema: Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((ما منكم من أحد يتوضأ فيسبغ ثم يقول: أشهد أن لا إله إلا الله وحده لا شريك له، وأشهد أن محمدا عبده ورسوله إلا فتحت له أبواب الجنة الثمانية يدخل من أيها شاء))
((Hakuna yeyote kati yenu anayetawadha akautimiza vilivyo wudhuu wake, kisha akasema: “Nashuhudia ya kwamba hapana mola mwingine isipokuwa Allaah Aliye Peke Yake na Asiye na mshirika, na nashuhudia ya kwamba Muhammad ni Mja Wake na Rasuli Wake, isipokuwa hufunguliwa milango minane ya pepo aingie wowote autakao)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (234)].
Imepokelewa na Abu Sa‘iyd kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((من توضأ فقال: سبحانك اللهم وبحمدك، أشهد أن لا إله إلا أنت، أستغفرك وأتوب إليك، كتب فى رق ثم طبع بطابع فلا يكسر إلى يوم القيامة))
((Mwenye kutawadha akasema: “Umetakasika ee Mola na kwa Himdi Yako, ninashuhudia ya kwamba hapana mola mwingine ila Wewe, nakuomba maghfirah na ninatubia Kwako”, huandikwa katika karatasi nyeupe, kisha hutiwa chapa, halafu haichanwi mpaka Siku ya Qiyaamah)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa ”Ikhraaj” na An Nasaaiy katika kitabu cha Al-Kubraa (9909), na Al-Haakim (1/564). Kuna Hadiyth kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine].
14- Kuswali rakaa mbili baada ya kutawadha:
Ni kwa Hadiyth ya ‘Uthmaan aliyesema: “Nilimwona Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akitawadha kama hivi ninavyotawadha akasema”:
((من توضأ نحو وضوئي هذا، ثم صلى ركعتين لايحدث فيهما نفسه، غفر له ما تقدم من ذنبه))
((Mwenye kutawadha kama wudhuu wangu huu, kisha akasimama akaswali rakaa mbili haizungumzishi nafsi yake, basi husamehewa madhambi yake yaliyotangulia)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (6433) na Muslim (226)].
Na imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Bilaal wakati wa Swalaah ya alfajiri:
(( يا بلال! حدثني بأرجى عمل عملته فى الاسلام، إني سمعت دف نعليك بين يدي في الجنة)). قال : ماعملت عملا أرجى عندي من أني لم أتطهر طهورا في ساعة من ليل أو نهار إلا صليت بذلك الطهور ما كتب لي أن أصلى))
((Ee Bilaal! Nielezee amali yenye matarajio zaidi uliyoifanya katika Uislamu, kwani mimi nimesikia mtaharuki wa viatu vyako mbele yangu huko peponi)).
Bilal akasema: “Sikufanya amali yoyote yenye matarajio makubwa kwangu zaidi ya kuwa sikupata kujitwaharisha wakati wowote wa usiku au mchana, ila huswali kwa twahara hiyo kile nilichoandikiwa kukiswali”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (1149) na Muslim (2458)].
Inajuzu Kukausha Viungo Baada Ya Kutawadha Kwa Kutopokelewa Lolote La Kuzuia Hilo
Na asili ni kufaa hilo. Na kama itasemwa kuwa imethibiti kwamba Maymuunah (Allaah Amridhie) alimletea Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kitambaa cha kujifutia baada ya kuoga, na yeye hakujifutia nacho, na akaondoka na ilhali anakung’uta mikono yake miwili.. [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (270)]…..basi tunasema: “Tukio hili lina mwelekeo wa kuwa na mambo kadhaa. Inawezekana kuwa alikirejesha kitambaa hicho kutokana na sababu inayohusiana nacho kama kutokuwa kisafi, au kuhofia kukilowesha na maji au sababu nyingine. Kisha Bi Maymuunah kumletea Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kitambaa hicho, inaonyesha kuwa ilikuwa ni mazoea yake. [Faida zaidi zipo kwenye Ash Sharhul Mumti’i (1/181). Angalia Kitabu cha Zaadul Maad (1/197)].
Kujuzu huku kunatiliwa nguvu na yaliyopokelewa kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitawadha, akaligeuza juba la sufi alilokuwa nalo, kisha akajifuta nalo.” [Isnadi yake iko karibu na Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Maajah (468, 3564)].
At-Tirmidhiy (54) anasema: “Baadhi ya Maswahaba wasomi wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na wa baada yao, wameruhusu kujifuta kwa kitambaa baada ya kutawadha. Na mwenye kulifanya hilo kuwa makruhu, basi amefanya hivyo kwa yale yaliyosemwa kuwa “wudhuu hupimwa”.
Wudhuu Haufai Kwa Aliyepaka Kucha Rangi [Yamenukuliwa kutoka kitabu changu cha Fiqhus Sunnah Lin Nisaa (uk 39)].
Kwa vile hilo huzuia maji kupenya na kufika sehemu ya faradhi. Ama rangi nyingine ya kawaida kama vile hina na mfanowe, hiyo haiathiri. Lakini hata hivyo ni vizuri kuiondosha kabla ya kutawadha na kuswali kwa kauli ya Ibn ‘Abbaas: “Wake zetu hujipaka hina bora kabisa. Hujipaka baada ya Swalaah ya ‘Ishaa na huiondosha kabla ya Alfajiri”. [Isnadi yake ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibnu Abi Shaybah (1/120)].
Na imepokelewa kuwa Ibraahiym An-Nakh’iy aliulizwa kuhusu mwanamke anayepaka mikono yake hina bila ya kuwa na wudhuu kisha wakati wa Swalaah ukafika. Alijibu akisema: “Ataondosha vilivyomo mkononi mwake kama atataka kuswali”. [Isnadi yake ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bayhaqy (1/77, 78)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
031-Yanayotengua Wudhuu
Alhidaaya.com [3]
1- Ni kutoka mkojo, au kinyesi, au upepo katika moja ya njia mbili (utupu wa mbele au wa nyuma)
Ama mkojo na kinyesi, ni kwa Neno Lake Subhaana:
أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِّنكُم مِّنَ الْغَائِطِ
((Au mmoja wenu ametoka chooni)). [Al Maaidah (5:6)]
“Al-Ghaait” ni kinaya cha kukidhi haja ndogo au haja kubwa. Wanachuoni wote wamekubaliana kuwa wudhuu unatenguka kwa kutoka kinyesi au mkojo toka moja ya njia mbili (mbele au nyuma). [Al-Ijma’a (uk 17), na Al-Awsatw (1/147) cha Ibn Al-Mundhir].
Ama ikiwa vitatoka sehemu isiyo ya mbele au nyuma kama kutoka kwenye jeraha la kwenye kibofu au tumbo, hapa wanachuoni wamevutana. Wanachuoni wenye kukizingatia kile tu kinachotoka (kiini chenyewe) kama Abu Haniyfah, Ath-Thawriy, Ahmad na Ibn Hazm, hao wamesema: “Wudhuu unatenguka kwa kila najsi inayobubujika toka mwilini iliyotokea sehemu yoyote”. Ama wale wenye kuyazingatia matokeo mawili (nyuma na mbele) kama Ash-Shaafi’iy, hao wamesema: “Unatenguka kinapotoka kitu chochote toka sehemu hizo mbili hata kama si najsi kama kijiwe na mfanowe”. [Al-Muhalla (1/232), Bidaayat Al-Mujtahid (1/40) na Al-Awsatw (1/137)].
Ama upepo, ikiwa utatoka kwa nyuma, kwa sauti au bila sauti, basi unatengua wudhuu. Hii ni kwa Ijma’a ya Maulamaa na kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
لا يقبل الله صلاة أحدكم إذا أحدث حتى يتوضأ
((Allaah Haikubali Swalaah ya mmoja wenu akipata hadathi mpaka atawadhe)).
Mtu mmoja toka Hadhramawt akauliza: “Ni nini hadathi ee Abu Hurayrah? Akajibu: “Ni ushuzi wa kimya kimya au wa sauti ”. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (135) na Muslim (135), lakini kwake bila kauli ya Abu Hurayrah].
Na ikiwa upepo utatokea utupu wa mbele, Jamhuri ya Maulamaa wamesema unatengua. [Bidaayat Al-Mujtahid (1/40) na Al-Ummu (1/17)].
Lakini Abu Haniyfah aliyeungwa mkono na Ibn Hazm amesema upepo huo hautengui wudhuu kwa vile ushuzi wa kimya na ushuzi wa sauti ni majina mawili ambayo hayaitwi upepo ila tu kama utatokea kwa nyuma. [Al-Muhalla (1/232) na Al-Mabsuwtw (1/83)].
Ninasema: “Ikiwa mtu atauhisi upepo unaojulikana (kwa harufu yake), basi utatengua wudhuu sawasawa ukiwa umetoka kwa mbele au kwa nyuma. Na ikiwa hauna harufu, basi ni ule tu unaotoka nyuma”.
Tanbihi
Mwanamke anaweza kuhisi kitu kinachofanana na upepo kikitoka kwenye utupu wake wa mbele. Hiki si kingine bali ni mjazo na mtaharuki wa ndani kwa ndani na wala si ushuzi unaotoka. Huo hautengui wudhuu wake, kwani ni kama kuteuka na mfano wake. Lakini ikiwa mwanamke huyo ni yule ambaye njia yake ya haja ndogo na kubwa zimeingiliana, basi atatawadha kiakiba tu kwa kuwepo uwezekano wa kuwa pengine upepo huo umetokea nyuma. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi.
2- Kutoka manii, wadii na madhii:
Kutoka manii kunatengua wudhuu kwa ijmai ya Wanazuoni na kunawajibisha kuoga kama itakavyokuja. [Al-Ifswaah (1/87) na Al-Ijma’a (uk 31)].
Na kila lile lenye kupasisha kuoga, basi linabatilisha wudhuu kwa Ijma’a ya Wanazuoni.
Na madhii nayo inatengua kwa Hadiyth ya ‘Aliy bin Abiy Twaalib Allaah Amridhie aliyesema: “Nilikuwa ni mtu ninayetokwa sana madhii. Nikamwamuru mtu mmoja amuulize Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutokana na hishma ya binti yake. Akamwuliza, naye akasema:
توضأ واغسل ذكرك
((Tawadha na uoshe utupu wako)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (269) na Muslim 303)].
Madii pia ni hivyo hivyo. Ni wajibu mtu aoshe utupu wake na atawadhe.
Ibn ‘Abbaas anasema: “Manii, wadii na madhii; ama manii, ni yale ambayo inapasa kuoga kwa kutoka. Ama wadii na madhii, akasema: Osha utupu wako, au nyuchi zako, na utawadhe wudhuu wako wa Swalaah”.[Isnadi yake ni Swahiyh: Al-Bayhaqy (1/115)].
Faida
Aliyepata bahati mbaya ya kusumbuliwa na kichocho cha mkojo au cha madhii, au akawa mara kwa mara anatokwa na kimoja ya viwili hivyo vilivyotangulia kutokana na kasoro ya kimwili mpaka ikawa ni uzito kwake, basi huyo ataosha nguo yake na mwili wake, na atatawadha kwa kila Swalaah kama mwanamke mwenye damu ya istihaadhwah (maelezo yatakuja). Kisha hakitakuwa na neno kitakachomtoka akiwa ndani ya Swalaah au kati ya wudhuu wake na Swalaah yake.
3- Usingizi mzito wa kutojifahamu:
Athar zilizokuja kuhusu kutawadha baada ya mtu kulala zimetofautiana, na maana zake kama zinavyoonekana zimegongana. Kuna Hadiyth ambazo maana zake kama zinavyoonekana, huonyesha kuwa kimsingi hakuna kutawadha kwa sababu ya kulala (usingizi), wakati ambapo kuna nyingine maana yake ya nje inalazimisha kuwa kulala ni hadathi (kunatengua). Kwa hivyo basi, Maulamaa katika suala hili, wameelekea mielekeo miwili: Madhehebu ya kukusanya na Madhehebu ya kutilia nguvu.
Maulamaa wa madhehebu ya kutilia nguvu, hawa ima wameliondosha kabisa suala la kutawadha baada ya kulala wakisema kuwa (kulala) si hadathi, au ima wameliwajibisha hilo moja kwa moja wakisema kuwa kulala ni hadathi. Ama Maulamaa wa madhehebu ya kukusanya, hawa wamesema kuwa kulala si hadathi bali ni kwa kuzoeleka kuwa hupelekea katika hadathi. Maimamu hawa wamehitalifiana kuhusu namna ya ulalaji unaowajibisha kutawadha.
Na kutokana na mielekeo hii mitatu ya Maulamaa hawa, pamechipuka kauli nane. [Ziangalie katika vitabu vya Al-Muhalla (1/222-231), Al-Istidhkaar (1/191), Al-Awsatw (1/142), Fat-h Al-Baariy (1/376), Sharhu Muslim cha An-Nawawiy (370) na Nayl Al-Awtwaar (1/241)].
Nazo ni:
Kwanza: Kulala hakutengui wudhuu kabisa
Haya yameelezewa yakinukuliwa toka kwa kundi la Maswahaba akiwemo Ibn ‘Umar na Abu Musa Al-Ash‘ariy. Nayo ni kauli ya Sa‘iyd bin Jubayr, Mak-huul, ‘Ubaydah As-Salmaaniy, Al-Awzaa‘iy na wengineo. Hoja yao ni:
(a) Hadiyth ya Anas bin Maalik (Allaah Amridhie) aliyesema: “Swalaah ilikimiwa nailhali Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anazungumza chemba na mtu fulani. Basi aliendelea kuzungumza naye mpaka Maswahaba zake wakalala. Halafu alikuja, akawaswalisha”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (6192) na Muslim (376), na tamshi ni lake].
(b) Imenukuliwa toka kwa Qataadah akisema: “Nilimsikia Anas akisema: “Maswahaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) walikuwa wakilala, kisha wanaswali wala hawatawadhi”. Akasema: Nikasema: Je, umesikia toka kwa Anas? Akasema: Ndiyo, naapa kwa Allaah”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (376) na At-Tirmidhy (78)].
Na tamko jingine lasema: “Wakingojea Swalaah, wakasinzia mpaka vichwa vyao vikajigonga (vikainamia chini), kisha husimama wakaswali”.
(c) Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas aliyesema: “Nililala kwa mama yangu mdogo Maymuunah. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasimama, nami nikasimama upande wake wa kushoto. Akauvuta mkono wangu akanisimamisha upande wake wa kulia. Nikawa kila ninaposinzia, hunivuta ndwele ya sikio. Aliswali rakaa 11”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (117) na Muslim (763), na tamshi ni lake].
(d) Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas wakati alipolala kwa Maymuunah. Anasema: “…kisha Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alilala mpaka nikasikia mkoromo wake, kisha alitoka akaenda kuswali”.[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (117), Muslim (184), na Ahmad (1/341)].
Na katika tamko jingine: “Kisha alisimama, akaswali na wala hakutawadha”.
Pili: Kulala kwa hali yoyote kunatengua wudhuu
Hakuna tofauti kati ya kulala kidogo au kulala sana. Haya ni madhehebu ya Abu Hurayrah, Abu Raafi’i, ‘Urwa bin Zubayr, ‘Atwaa, Al-Hasan Al-Baswriy, Ibn Al-Musayyib, Az-Zuhriy, Al-Mazniy, Ibn Al-Mundhir na Ibn Hazm. Ni chaguo la Al-Albaaniy. Ni kwa hoja zifuatazo:
(a) Ni kwa Hadiyth ya Swafwaan bin ‘Assaal. Amesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akituamuru tunapokuwa safarini, tupukuse (tupanguse kwa maji) juu ya khofu zetu na wala hatuzivui kwa muda wa siku tatu hata kama tutakwenda haja kubwa au ndogo au kulala, ila kwa janaba”. [Hadiyth Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na An-Nasaaiy (1/32), At-Tirmidhiy (3535) na Ibn Maajah (478). Angalia pia kitabu cha Al-Irwaai (104)].
Wamesema: “Hapa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amechukulia kiujumla usingizi wote wala hakuhusisha usingizi hafifu au mzito, wala hali hii kwa ile, na akaufanya sawa na haja kubwa na ndogo”.
(b) Ni kwa yaliyohadithiwa toka kwa ‘Aliy bin Abi Twaalib (Allaah Amridhie) aliyepokea toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((العينان وكاء السه، فمن نام فليتوضأ))
((Macho mawili ni kizibo cha tundu la haja kubwa. Basi mwenye kulala, atawadhe)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Daawuud (203), Ibn Maajah (477) na wengineo. Ni dhwa’iyf kwa kauli yenye nguvu. Al-Albaaniy amesema ni Hadiyth Hasan].
"السه" ni tundu la nyuma la haja kubwa, na "الوكاء"ni uzi unaofungiwa mdomo wa kiriba. Kwa hiyo kuwa macho kwa jicho, kumefanywa ni kama kizibo cha kiriba. Na jicho linapolala, kifuniko hicho huchopoka na hadathi huwa.
(c) Ni kwa Hadiyth ya ‘Aaishah kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((إذا نعس أحدكم وهو يصلي فليرقد حتى يذهب عنه النوم، فإن أحدكم إذا صلى وهو ناعس لا يدري لعله يستغفر فيسب نفسه))
((Anaposinzia mmoja wenu wakati anaswali, basi alale mpaka usingizi umwishe, kwani mmoja wenu anaposwali hali ya kuwa anasinzia, hajui pengine yeye anaona kuwa anaomba maghfirah huku kumbe anajitukana mwenyewe)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (212) na Muslim (222)].
Katika “Swahiyh yake”, Al-Bukhaariy ameitolea dalili Hadiyth hii juu ya ulazima wa kutawadha baada ya kulala. Lakini ninaloliona mimi ni kuwa kuna kijinukta cha kukizungumzia katika utoaji dalili kwa kutumia Hadiyth hii. Ikiwa ataifanya sababu ya kuikatiza Swalaah kutokana na usingizi ni kuchelea kujiombea mwenyewe vibaya, au kusoma asichokijua, au kutouhudhurisha moyo wake kukawa hakuna khushui, basi haya hayana uhusiano na kutawadha baada ya kulala. Bali huenda wenye kusema kuwa wudhuu hautenguki kwa usingizi wameitumia dalili hii kuthibitishia hoja yao. Basi atazame.
(d) Wamesema: "Maulamaa wote wamekubaliana kwamba ni lazima kutawadha kwa mtu aliyeondokewa na akili kwa wendawazimu au kupotewa na fahamu kwa hali yoyote iwayo. Pia aliyelala".
Tatu: Usingizi mzito unatengua kwa hali yoyote, na mwepesi hautengui
Hii ni kauli ya Maalik, riwaya ya Ahmad, Az-Zuhriy Rabi‘ah na Al-Awzaa‘iy!! Wameichukulia Hadiyth ya Anas ya kulala Maswahaba kuwa ni usingizi hafifu. Na pia wametolea dalili kwa Hadiyth ya Abu Hurayrah:
من استحق النوم فقد وجب عليه الوضوء
((Mwenye kustahiki kulala, basi lazima atawadhe)). [Hadiyth Swahiyh Mawquwf. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Abi Shaybah (1/158) na ‘Abdur-Raaziq (481) ikiwa Mawquwf kwa Sanad Swahiyh. Na imepokelewa ikiwa Marfu’u. Na si Swahiyh, kama alivyosema Ad-Daara Qutwniy katika Al’Ilal (8/954). Angalia Adh-Dhwa’iyfah (954)].
Lililo sahihi ni kuwa Hadiyth hii ni Mawquwf. Na Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas:
((وجب الوضوء على كل نائم إلا من خفق رأسه خفقة أو خفقتين))
((Ni lazima kutawadha kwa kila aliyelala, isipokuwa kwa yule aliyegonga kichwa mara moja au mara mbili)). [Hadiyth Dhwa’iyf Mawquwf Marfu’u. Imefanyiwa “ikhraaj” na ‘Abdur Raaziq (479), na Al- Bayhaqiy (1/119). Angalia ‘Ilal Ad Daaru Qutwniy].
Nne: Kulala hakutengui ila kama atalala kwa ubavu au kwa kuegemea
Mwenye kulala kwa umbo lolote kati ya maumbo ya Swalaah kama kwa staili ya mwenye kurukuu, au mwenye kusujudu, au mwenye kusimama, au mwenye kukaa, basi wudhuu wake hautenguki, sawasawa akiwa katika Swalaah au nje ya Swalaah. Hii ni kauli ya Hammaad, Ath-Thawriy, Abu Haniyfah na wenzake, Daawuud na Ash-Shaafi’iy. Na hoja yao ni:
(a) Ni yale yaliyohadithiwa toka kwa ‘Amri bin Shu’ayb toka kwa baba yake aliyepokea toka kwa babu yake ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
ليس على من نام جالسا وضوء حتى يضع جنبه
((Hakuna kutawadha kwa aliyelala kwa kukaa mpaka aweke ubavu wake)).
[Hadiyth Munkar: Imefanyiwa “ikhraaj” na ibn ‘Uday katika Al-Kaamil (6/2459), Ad-Daara Qutwniy (1/160) na At-Twabaraaniy katika Al-Awsatw..
Ni Hadiyth Dhwa’iyf, haifai.
(b) Ni Hadiyth ya Anas toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliyesema:
((إذا نام العبد في سجوده باهى الله تعالى به الملائكة يقول: أنظروا إلى عبدي روحه عندي وجسده في طاعتي))
((Anapolala mja katika sijda yake, Allaah Hujifaharisha kwake kwa Malaika Akiwaambia: “Mwangalieni Mja Wangu; roho yake iko Kwangu na mwili wake uko katika kunitii Mimi)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Angalia kitabu cha As-Silsilat Adh-Dhwa’iyfah (953).
Na wamevipimia vipambo vingine vya mwenye kuswali kwa sijda.
Ninasema: “Hadiyth hii Sanad yake ni Dhwa’iyf. Al-Bayhaqiy amesema: “Kisha hakuna linaloashiria kuwa hatoki kwenye Swalaah yake. Na makusudio ya yaliyoelezwa - kama yatakuwa ni sawa - ni kumsifia mja anayedumu katika Swalaah mpaka usingizi ukamlemea”.
Tano: Hakutengui ila kwa aliyelala kwa umbo la kurukuu au kusujudu
An-Nawawiy ameinasibisha kauli hii kwa Ahmad. Na huenda mwono wake ni kuwa mwinamo wa kurukuu na kusujudu ulivyozoeleka, hupelekea kutenguka wudhuu.
Sita: Hakutengui ila kwa aliyelala kwa umbo la kusujudu
Kauli hii imepokelewa vilevile toka kwa Ahmad.
Saba: Usingizi ndani ya Swalaah hautengui kabisa, lakini nje ya Swalaah hutengua
Kauli hii imepokelewa na Abu Haniyfah kwa mujibu wa Hadiyth iliyotangulia katika kauli ya nne.
Nane: Wudhuu hautenguki kama atalala kwa kuambatisha barabara makalio yake chini, sawasawa ikiwa ni ndani ya Swalaah au nje yake, usingizi ukiwa mzito au mwepesi.
Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy, kwa vile kwa mujibu wa anavyoona yeye ni kuwa usingizi wenyewe si hadathi, bali ilivyozoeleka ni kuwa hupelekea kwenye hadathi. Anasema Ash-Shaafi’iy: “Kwa vile mwenye kulala, hujiambatisha barabara na ardhi na hakiwezi kutoka chochote isipokuwa hukishtukia”. Ash-Shawkaaniy ameichagua kauli hii.
Ninasema: “Wenye kuisema kauli hii, wameichukulia Hadiyth ya Anas ya kulala Maswahaba juu ya kuwa walikuwa wamekaa. Al-Haafidh katika kitabu chake cha “Al-Fat-h” (1/251) amelijibu hilo kwa kusema: “Lakini katika musnadi ya Al-Bazzaar kwa Sanad Swahiyh katika Hadiyth hii (panaelezwa): “Wakaweka ubavu wao, wengine wakilala, kisha hunyanyuka wakaswali”. [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bazzaaz. Na kama hiyo hiyo, imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Daawuud katika kitabu cha Masaail Ahmad (uk.318). Na Isnadi yake ni Swahiyh kwa sharti ya Mashaykh Wawili. Tazama pia katika Tamaam Al-Minnah (uk.100)].
Lenye Nguvu
Usingizi mzito wa kutojifahamu kiasi ambacho mtu hawezi kusikia sauti, au kuhisi kudondoka kitu toka mkononi mwake, au kutokwa na udenda na mfano wa hayo, bila shaka usingizi huo unatengua wudhuu, kwani ilivyozoeleka hupelekea hadathi. Ni sawasawa ikiwa mtu amesimama, au amekaa, au amelala ubavu, au amerukuu au amesujudu, hakuna tofauti kati ya milalo hiyo.
Na ikiwa wenye kauli ya kwanza wanamaanisha usingizi wa aina hii, basi sisi tuko nao. Na kama si hivyo, basi usingizi mwepesi wa kusinzia ambao mtu huhisi yanayopita, hautengui wudhuu kwa hali yoyote iwavyo. Ni kwa Hadiyth ya kulala kwa Maswahaba mpaka vichwa vyao vikajigonga (vikainama). Pia kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas aliposwali na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).
Na kwa haya, zinakusanyika dalili zote zilizokuja katika mlango huu.
Ni Zake Allaah Himdi na Ihsaan.
Faida
Ilivyokuwa usingizi umezoeleka kuwa hupelekea kwenye hadathi yenye kuwajibisha kutawadha, basi kutenguka kwake kutategemezewa kwa mwenye wudhuu kwa mujibu wa mwenyewe alivyolala na kwa jinsi dhana yake itakavyopondokea. Na ikiwa atafanya shaka kama alivyolala kunatengua au la, basi lililo na nguvu ni kuwa asihukumie kutenguka wudhuu wake, kwa vile twahara ni yenye kuthibiti kwa yakini na haiondoki kwa shaka. Na hili ndilo alilolichagua Shaykh wa Uislamu katika kitabu cha Al-Fataawaa (21/230).
4- Kuondokewa na akili kwa kulewa au kupoteza fahamu au wendawazimu:
Hili linatengua wudhuu kwa makubaliano ya Maulamaa wote. [Al-Awsatw cha Ibn Al-Mundhir (1/155)].
Na kupatwa na mfadhaiko au mshtuko kuna uzito zaidi kuliko kulala.
5- Kugusa utupu bila kizuizi sawasawa ikiwa ni kwa matamanio au bila ya matamanio
Maulamaa wana kauli nne kuhusu kugusa utupu baada ya kutawadha. Kauli mbili kwa kutilia nguvu na kauli mbili kwa kukusanya.
Kauli ya kwanza:
Kugusa utupu hakutengui kabisa wudhuu.
Ni madhehebu ya Abuu Haniyfah na riwaya moja toka kwa Maalik. Pia kauli hii imepokelewa toka kwa kikundi cha Maswahaba. [Al-Badaai-’i (1/30), Sharhu Fat-hil Qadiyr (1/37), Al-Mudawwanah (1/8-9) na Al-Istidhkaar (1/308 na baada yake)].
Hoja zao ni haya yafuatayo:
(a) Ni Hadiyth ya Twaliq bin ‘Aliy kwamba mtu mmoja alimwuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu mtu anayegusa utupu wake baada ya kutawadha. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia:
هل هو إلا بضعة منك
((Hakika hiyo ni sehemu tu ya mwili wako)). [Isnadi yake ni Tepetepe: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Daawuud (182), At-Tirmidhiy (85) na An-Nasaaiy (1/101). Maulamaa wamekhitalifiana juu ya kuwa ni Swahiyh au la. Kauli yenye nguvu ni kuwa Hadiyth hii ni Dhwa’iyf kwa ajili ya Qays bin Twaliq. Lakini Al-Albaaniy ameipasisha kuwa ni Swahiyh. Kwa hiyo kila mmoja na mwono wake. Na sisi hatuubani wasaa. Na Allaah Ndiye Mwelewa zaidi].
Na katika kauli nyingine, mwenye kuuliza alisema: “Wakati nikiwa katika Swalaah, niliingia kukuna paja langu na mkono wangu ukagusa dhakari yangu”. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia:
إنما هو منك
((Hiyo ni sehemu ya mwili wako)). [Isnadi yake ni Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Dawuud (183), Ahmad (4/23), Al-Bayhaqiy (1/135) na wengineo].
(b) Wamesema: Wote wanakubaliana kwamba dhakari ikiligusa paja, basi hakuwajibishi kutawadha, na hakuna tofauti kati ya mkono na paja. Hakuna mahitilafiano yoyote kati ya Maulamaa katika suala hili. Na wameizungumzia Hadiyth ifuatayo ya Bisarrah inayogusia amri ya kutawadha kwa kuugusa uume. [Al-Awsatw (1/203). Na tizama pia Sharhu Ma’aaniy Al-Aathaar (1/71-79)].
Kauli ya pili:
Kugusa utupu kunatengua wudhuu kwa hali yoyote.
Ni madhehebu ya Maalik – kama anavyojulikana - , Ash-Shaafi’iy, Ahmad na Ibn Hazm. Kauli hii imepokelewa toka kwa Maswahaba wengi. [Al-Istidhkaar (1/308), Al-Mudawwanah (1/8-9), Al-Ummu (1/19), Al-Majmu’u (1/24), Al-Mughniy (1/178), Al-Insaaf (1/202), Al-Muhalla (1/235)].
Hoja yao ni:
(a) Hadiyth ya Bisarrah binti Swafwaan kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema:
من مس ذكره فليتوضأ
(( Mwenye kugusa dhakari yake, basi atawadhe)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Daawuud (181), An-Nasaaiy (1/100) na Ibn Hibaan (1112)].
(b) Hadiyth ya Ummu Habiybah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
من مس فرجه فليتوضأ
((Mwenye kuugusa utupu wake, basi atawadhe)). [Ni Swahiyh kwa Hadiyth nyingine kama hii iliyopokelewa na Swahaba mwingine. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Maajah (481), Abu Ya-’alaa (7144) na Al-Bayhaqiy (1/130). Angalia Al-Irwaa (117)].
Mfano wa Hadiyth hizi mbili umepokelewa katika Hadiyth ya Abuu Hurayra iliyohadithiwa na Binti Unays, ‘Aaishah, Jaabir, Zayd bin Khaalid na ‘Abdullahi bin ‘Amri.
Wamesema: Hadiyth ya Bisarrah inatiliwa nguvu kuliko Hadiyth ya Twaliq. Hii ni kwa sababu zifuatazo:
(a) Kwamba Hadiyth ya Twaliq ina kasoro. Imekosolewa na Abu Zar-’a, na Abu Hatim. Na An-Nawawiy katika Majmu’u (2/42), amezungumza sana akieleza kuwa wahafidhi wamekubaliana kuifanya Hadiyth hii dhwa’iyf!!
(b) Ingelikuwa ni Swahiyh, basi Hadiyth ya Abuu Hurayrah yenye maana sawa na Hadiyth ya Bisarrah, ingelitangulizwa, kwa vile Twaliq alikuja Madiynah wakati wanaujenga Msikiti nailhali Abu Hurayrah alisilimu mwaka wa Khaybar baada ya hilo kwa miaka sita. Na kwa ajili hiyo, Hadiyth yake itaondosha hukmu ya Hadiyth ya Twaliq. [Na kati ya waliosema kuwa hukmu yake imeondoshwa (naskh) ni: At-Twabaraaniy katika Al-Kabiyr (8/402), Ibn Hibaan (3/405), Ibn Hazm katika Al-Muhalla (1/239), Al-Haazimiy katika Al-I’itibaar (77), Ibn Al-‘Arabiy katika Al-‘Aaridhwa (1/117) na Al-Bayhaqiy katika Al-Khilaafiyyaat (2/289)].
(c) Kwamba Hadiyth ya Twaliq inaubakisha uasili, lakini Hadiyth ya Bisarrah ni yenye kunukuu. Nayo hutangulizwa kwa vile hukmu za kisharia ni zenye kunukuu yale waliyokuwa wakiyafanya.
(d) Kwamba wapokezi wa kutenguka wudhuu kwa kugusa ni wengi na Hadiyth zake ni mashuhuri zaidi.
(e) Ni kauli ya Maswahaba wengi.
(f) Kwamba Hadiyth ya Twaliq imechukuliwa kuwa yeye alijikuna paja akaigusa dhakari yake juu ya nguo kama inavyoonyesha riwaya kuwa yeye alikuwa katika Swalaah.
Kauli ya tatu:
Wudhuu unatenguka ikiwa mtu kagusa dhakari yake kwa matamanio, na kama si kwa matamanio, basi hautenguki.
Hii ni riwaya toka kwa Maalik, na ni kauli iliyochaguliwa na Al-‘Allaamah Al-Albaaniy. [Angalia vitabu rejea vilivyotangulia vya madhehebu ya Maalik na kitabu cha Tamaam Al-Minna (uk 103). Hapo ameinasibisha kauli hii kwamba ni chaguo la Ibn Taymiyah. Amesema: “Ninavyokumbuka”. Ninasema: “Bali ni madhehebu ya nne ya Ibn Taymiyyah kama utakavyokuja kuona. Ametukuka Allaah Asiyesahau”].
Wenye kusema hivi, wameichukulia Hadiyth ya Bisarrah juu ya kama itakuwa ni kwa matamanio, na Hadiyth ya Twaliq juu ya kama si kwa matamanio. Wamesema kuwa kiashirio cha hilo ni neno lake:
((Hiyo ni sehemu ya mwili wako)).
Kwa hiyo kama ataugusa utupu wake bila ya matamanio, basi anakuwa ni kama aliyegusa kiungo chake kingine chochote.
Kauli ya nne:
Kutawadha kwa sababu ya kugusa dhakari kumesuniwa kwa hali yoyote na wala si wajibu.
Ni madhehebu ya Ahmad katika moja ya riwaya zake mbili na Shaykh wa Uislamu Ibn Taymiyah. Ni kauli ambayo Al-‘Allaamah Ibn ‘Uthaymiyn - Allaah Amrehemu – anaonekana kuwa ameipondokea zaidi, isipokuwa amelijaalia hilo kuwa ni Sunnah endapo kama ataigusa dhakari bila matamanio, na akatilia nguvu kuwa ni wajibu kama ni kwa matamanio kwa njia ya tahadhari. [Majmu’u Al-Fataawaa (21/241) na Ash-Sharhu Al-Mumti’i (1/233)]. Kwa hivyo wameichukulia Hadiyth ya Bisarrah kuwa ni Sunnah na Hadiyth ya Twaliq kuwa maswali yaliyoulizwa yalikuwa ni kwa upande wa wajibu.
Kauli mbili za mwisho zinazosimamia juu ya mkondo wa kukusanya zinatolewa dalili kwa haya yafuatayo:
(a) Ni kwamba dai la kuwepo “naskh” kwa vile Twaliq alitangulia kusilimu kabla ya Bisarrah, ni lazima liangaliwe. Kwa kuwa dai hilo si dalili ya kuwepo “naskh” kwa upande wa wahakiki waliobobea katika fani ya taaluma ya “Uswuul”, kwa sababu aliyetangulia kusilimu anaweza kuwa alihadithia akiwa amenukulu toka kwa mwingine.
(b) Katika maelezo ya Twaliq, kuna sababu ambayo haiwezi kuondoka, nayo ni kuwa dhakari ni sehemu ya mwili wake. Na kama hukmu itafungamanika na sababu isiyoweza kuondoka, basi hukmu haiondoki. Kwa hiyo “naskh” haiwezekani kuwepo.
(c) Kisha ni kuwa suala halipelekwi katika “naskh” ila baada ya kushindikana kukusanya na hasahasa tukizingatia kuwa haifai kufanya “naskh” kama ilivyotangulia.
Ninasema: "Kauli ya mwisho ndiyo yenye nguvu kwa mujibu wa hali. Lakini endapo kama Hadiyth ya Twaliq bin ‘Aliy itakuwa ni Swahiyh - na hili liko mbali bali kauli ya kuifanya Dhwa’iyf ndiyo yenye mwelekeo zaidi - , basi kauli itakayokuwa na uzito ni ile isemayo kuwa kugusa uume kunatengua wudhuu kwa hali yoyote, ni sawasawa ikiwa ni kwa matamanio au bila ya matamanio, kwa vile matamanio hayana mpaka na wala hakuna dalili ya kipimo chake. Na Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi.
Faida Kuhusu Yaliyotangulia
(a) Mwanamke akigusa utupu wake atatawadha:
Ni kwa Hadiyth ya ‘Amri bin Shu’ayb toka kwa baba yake aliyenukuu toka kwa babu yake, amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((من مس ذكره فليتوضأ، وأيما امرأة مست فرجها فلتتوضأ))
((Mwenye kuigusa dhakari yake atawadhe, na mwanamke yeyote aliyeugusa utupu wake, basi atawadhe)). [Swahiyh kwa nyingine: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad (2/223) na Al-Bayhaqiy (1/132)].
Hadiyth hii inatiliwa nguvu na kauli ya ‘Aaishah Allaah Amridhie isemayo:
“Mwanamke akiugusa utupu wake, atawadhe”. [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ash-Shaafi’iy katika “Musnadi yake” (90) na Al-Bayhaqiy (1/133). Al-Haakim amesema ni Swahiyh (1/138)].
Na asili ni kwamba wanawake ni washiriki wa wanaume katika hukmu. Na haya ndiyo madhehebu ya Ash-Shaafi’iy na Ahmad kinyume na Abu Haniyfah na Maalik!!
(b) Kugusa utupu wa mwingine:
Ikiwa mwanamume ataugusa utupu wa mkewe, au mkewe akaigusa dhakari yake, basi hakuna dalili ya kutenguka wudhuu wa yeyote kati yao isipokuwa tu kama madhii au manii yatatoka. Hapo wudhuu utatenguka kwa kutokwa na maji hayo na si kwa kuguswa. Lakini Maalik na Ash-Shaafi’iy wamesema kuwa ni lazima kutawadha kwa kujengea juu ya madhehebu yao kuwa wudhuu unatenguka kwa kumgusa mwanamke. Baadaye tutakuja kuona kwamba kauli yenye nguvu ni kinyume cha hivyo. [Mawaahib Al-Jaliyl (1/296) na Al-Ummu (1/20)].
Aidha, wudhuu hautenguki ikiwa mwanamke au mwanamume ataugusa utupu wa mtoto. Maalik amekubaliana na hili. Nayo pia ni kauli ya Az-Zuhriy na Al-Awzaa’iy. [Al-Kaafiy cha Ibn ‘Abdu Al-Barri (1/149) na Al-Awsatw (1/210)].
(c) Yote ni sawasawa kuugusa utupu kwa makosa au kwa kukusudia [Al-Muhalla (1/241) na Al-Awsatw (1/205-207)].
Ni madhehebu ya Al-Awzaa’iy, Ash-Shaafi’iy, Is-Haaq na Ahmad.
Na kundi la Maulamaa linaona kuwa lenye kutengua wudhuu ni kukusudia kuugusa. Kati yao ni Mak-huul, Jaabir bin Zayd na Sa’iyd bin Jubayr. Pia ni madhehebu ya Ibn Hazm aliyetolea dalili kwa Neno Lake Subhaanah:
((وَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ فِيمَا أَخْطَأْتُمْ بِهِ وَلَٰكِنْ مَا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ ۚ وَكَانَ اللَّهُ غَفُورًا رَحِيمًا))
((Wala si lawama juu yenu kwa mlivyokosea, lakini zipo lawama katika yale ziliyofanya nyoyo zenu kwa makusudi)). [Al Ahzaab (33:6)]
Yenye nguvu zaidi ni kauli ya kwanza. Ibn Al-Mundhir amesema: “Inampasa aliyekufanya kuugusa utupu kwa maana ya hadathi yenye kuwajibisha kutawadha, akufanye kukusudia kwake au kutokusudia kuwa ni sawa kama ilivyo kwa hadathi nyinginezo”.
Ninasema: “Kukosea na kusahau kwa yanayohusiana na masharti na nguzo, kunasamehewa lakini hakuondoshi hukmu. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi".
(d) Kugusa juu ya nguo hakutengui:
Kwa vile hili haliitwi kugusa kama inavyoonekana. Hili linatiliwa nguvu na Hadiyth ya Abu Hurayrah ambayo ni marfu’u:
إذا أفضى أحدكم بيده إلى ذكره ليس بينهما شيئ فليتوضأ
((Akipeleka mmoja wenu mkono wake katika dhakari yake bila kuwepo kizuizi kati yao, basi atawadhe)). [Hadiyth Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ad-Daara Qutwniy (1/147) na Al-Bayhaqiy (1/133). Na tizama pia katika Asw-Swahiyhah (1235)].
(e) Kugusa tundu ya nyuma hakutengui [Al-Muhallaa (1/238) na Al-Awsatw (1/212)].
Ni kwa vile tundu ya nyuma haiitwi utupu. Na si sahihi kuwekwa mizani moja na dhakari kwa kutokuwepo sababu jumuishi kati ya kugusa tundu ya nyuma na dhakari. Na kama mtu atasema kuwa sehemu zote mbili ni mapitio ya najsi, basi atajibiwa kuwa hiyo siyo sababu ya kutenguka wudhuu kutokana na kugusa. Halafu ikiwa kugusa najsi hakutengui wudhuu, basi vipi utenguke kwa kugusa mapitio yake?!! Hii ni kauli ya Maalik, Ath-Thawriy na Abuu Haniyfah na wenzake kinyume na Ash-Shaafi’iy.
6- Kati ya yanayotengua wudhuu ni kula nyama ya ngamia:
Aliyekula nyama ya ngamia sawasawa ikiwa mbichi, iliyopikwa au ya kuchoma, ni lazima atawadhe. Hii ni kwa Hadiyth ya Jaabir bin Samrah anayesema kwamba mtu mmoja alimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “Je, tutawadhe kwa kula nyama ya kondoo au mbuzi?” Akamjibu:
((إن شئت توضأ، وإن شئت فلا تتوضأ))
((Ukitaka tawadha, ukitaka usitawadhe)).
Akamuuliza: “Je, tutawadhe kwa kula nyama ya ngamia?” Akasema:
((نعم، توضأ من لحوم الابل))
((Ndiyo, tawadha ukila nyama ya ngamia)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (360) na Ibn Maajah (495)].
Na imepokelewa toka kwa Al-Barraa bin ‘Aazib kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
توضأوا من لحوم الابل، ولا توضأوا من لحوم الغنم
((Tawadheni kwa kula nyama ya ngamia, na msitawadhe kwa kula nyama ya kondoo na mbuzi)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (184), At-Tirmidhiy (81) na Ibn Maajah (494)].
Na haya ni madhehebu ya Ahmad, Is-haaq, Abu Khaythamah, Ibn Al-Mundhir na Ibn Hazm. Pia ni moja kati ya kauli mbili za Ash-Shaafi’iy na ni chaguo la Shaykh wa Uislamu. Aidha, ni kauli iliyopokelewa toka kwa Ibn ‘Umar na Jaabir bin Samrah.
Lakini Jamhuri ya Maulamaa kama Abu Haniyfah, Maalik, Ash-Shaafi’iy, Ath-Thawriy na kundi la watangu wema, hawa wanaona kwamba si lazima kutawadha kwa kula nyama ya ngamia bali ni Sunnah. [Al-Mabsuwtw (1/80), Mawaahib Al-Jaliyl (1/320), Al-Majmuu (1/57), Al-Mughniy (1/138), Al-Muhalla (1/241) na Al-Awsatw (1/138)].
Na hii ni kutokana na Hadiyth ya Jaabir aliyesema: “Amri mbili za mwisho toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni kutotawadha kwa kula kilichoivishwa kwa moto”.[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (192), Attirmidhiy (8) na An-Nasaaiy (1/108)].
Wakiizungumzia kauli hii wamesema: “Neno lake “kile kilichoivishwa kwa moto” linakusanya nyama ya ngamia vilevile, nayo imethibiti kunasikhiwa”.
Hili linajibiwa kwa mambo mawili: [Al-Muhallaa (1/244) na Al-Mumti’i (1/249)].
La kwanza:
Ni kwamba Hadiyth ya Jaabir ni jumuishi, na yale yaliyopokelewa katika kutenguka wudhuu kwa kula nyama ya ngamia ni hali maalumu. Na jambo jumuishi hutangulizwa kabla ya jambo maalumu, na hapo hutoka lile ambalo umaalumu wake umeainishwa na dalili. Na hapa naskhi haizungumziwi kwa vile inawezekana kukusanya.
La pili:
Amri iliyokuja kuamuru kutawadha kwa kula nyama ya ngamia, ni hukmu inayohusiana na iliyoivishwa kwa moto au mbichi. Kwa hiyo kuivishwa kwa moto hakuwajibishi kutawadha, na kwa hivyo hukmu yake inakuwa nje ya habari zilizokuja kuhusu kutawadha kwa kula kilichopikwa na kwa kunaskh wudhuu.
Baadhi yao wanasema kwamba makusudio ya wudhuu katika Hadiyth ni kuosha mkono!! [Majmu’u Al-Fataawaa (21/260 na baada yake)].
Hili ni batili kwani hakuna wudhuu mwingine uliokuja kupitia maneno ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) zaidi ya wudhuu wa Swalaah. Kisha, katika Hadiyth ya Jaabir bin Samrah iliyopokelewa na Muslim, amri ya kutawadha kwa sababu ya kula nyama ya ngamia, imefungamanishwa na kuswali katika sehemu ya malalio yao kwa kutofautisha kati ya hilo na kuswali katika mapumzikio ya mbuzi. Hivi ndivyo unavyojulikana wudhuu wa Swalaah bila mjadala.
Lenye Nguvu:
Ni kuwa ni lazima kutawadha kwa kula nyama ya ngamia kwa hali yoyote ile. Na kwa ajili hiyo, An-Nawawiy katika kitabu cha “Sharh Al-Muslim” (1/328) anasema: Madhehebu haya yana nguvu zaidi ingawa Jamhuri ya Maulamaa wako kinyume nayo.
Tanbihi:
Ya kwanza:
Katika “Sharh Al-Muslim” (1/328), An-Nawawiy ameinasibisha kauli ya kutolazimu kutawadha kwa kula nyama ya ngamia kwa Makhalifa Wanne Waongofu!! Madai haya hayana dalili yoyote wala haijulikani Sanad yoyote kwao inayohusiana na hilo. Ibn Taymiyah Allaah Amrehemu ametanabahisha kuhusu madai haya akisema: “Ama yule aliyenukulu toka kwa Makhalifa Waongofu au Jamhuri ya Maswahaba kwamba wao walikuwa hawatawadhi kwa kula nyama ya ngamia, basi amewatendea kosa. Hilo anakuwa ameliwazia na kulidhania tu kutokana na yale yaliyonukuliwa kuhusu wao ya kuwa walikuwa hawatawadhi kwa kula kilichoivishwa kwa moto…”. [Al-Qawaaid An-Nuwraaniya (uk.9) ikinukulu toka kwa Tamaam Al-Minnah (uk.105)].
Ya pili:
Kisa Mashuhuri Cha Uzushi [Tizama Adh-Dhwa’iyfah ya Al-Albaaniy (1132) na Qaswasun Laa Tathbut cha Mash-huur Hasan (uk.59)].
Kimetangaa baina ya watu wa kawaida kisa wanachokihadithia mara kwa mara. Kisa hiki wamekisikia toka kwa wanafunzi wanaoeleza kwamba ni lazima kutawadha kwa kula nyama ya ngamia. Kisa hiki kinaeleza kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa katika kundi la Maswahaba wake, akasikia harufu ya ushuzi kwa mmoja wao. Swahaba huyo akaona haya kunyanyuka kati ya watu, naye alikuwa amekula nyama ya ngamia. Hapo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:
((من أكل لحم جزور فليتوضأ))
((Aliyekula nyama ya ngamia basi akatawadhe)).
Hapo wote waliokuwa wamekula ngamia wakanyanyuka wakaenda kutawadha!!
Kisa hiki ni Dhwa’iyf kwa upande wa Sanad na Munkari kwa upande wa Matni.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
032-Mambo Yasiyotengua Wudhuu
Alhidaaya.com [3]
Mambo haya Maulamaa wamehitilafiana juu ya kutengua kwake wudhuu. Na kwa kuyatafiti kwa kina, itabainika kwamba hayatengui. Kati ya mambo hayo ni:
1- Mwanaume kumgusa mwanamke bila ya kizuizi
Suala hili lina kauli tatu za Maulamaa:
Kauli ya kwanza:
Mwanamume kumgusa mwanamke kunatengua wudhuu kwa hali yoyote. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy. Ibn Hazm amemuunga mkono. Ibn Mas’uud na Ibn ‘Umar wamesema hivyo hivyo. [Al-Ummu (1/15), Al-Majmu’u (2/23 na baada yake) na Al-Muhalla (1/244)].
Kauli ya pili:
Hakutengui kwa hali yoyote. Ni madhehebu ya Abu Haniyfah na Muhammad ibn Al-Hasan Ash-Shaybaaniy. Pia ni kauli ya Abbaas, Twaawus, Al-Hasan na ‘Atwaa. Kauli hii pia imeungwa mkono na Shaykh wa Uislamu Ibn Taymiyah, nayo ndio kauli yenye nguvu. [Al-Mabsuwtw (1/68), Al-Badaai-’i (1/30), Al-Awsatw (1/126) na Majmu’u’ Al-Fataawaa (21/410)].
Kauli ya tatu:
Kugusa kunatengua kama ni kwa matamanio. Haya ni madhehebu ya Maalik na Ahmad kama ilivyo mashuhuri kwake. [Al-Mudawwanah (1/13), Haashiyat Ad-Dusuwqiy (1/119), Al-Mughniy (1/192) na Kash-Shaaf Al-Qinaa’i (1/145)].
Ninasema (Abu Maalik): "Kigezo cha kimsingi walichokitolea dalili waliosema kwamba wudhuu unatenguka kwa kumgusa mwanamke, ni kauli Yake Allaah Mtukufu:
(( أوْ لامَسْتُمُ النِّسَاءَ فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً فَتَيَمَّمُوا))
((..au mmewagusa wanawake, na hamkupata maji, basi tayammum..)). [Al-Maaidah (5: 6)]
Imepokelewa kwa njia sahihi toka kwa Ibn Mas-’oud na Ibn ‘Umar wakisema: “Kugusa ni chini ya daraja ya kuingilia”. [Kauli Swahiyh: Tafsiyr At-Twabariy (1/502) kwa Sanad tofauti Swahiyh].
Lakini Mwanachuoni Mweledi wa umma Ibn ‘Abbaas amehitilafiana nao akisema: “Kugusa na “mubaasharah”, kunamaanisha kuingilia, lakini Allaah Hukifanyia kinaya Akitakacho kwa Akitakacho”. [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Twabariy (9581) na Ibn Abu Shaybah (1/166)].
Na hakuna shaka kwamba tafsiyr yake inapewa kipaumbele kuliko ya wengineo. Halafu, ndani ya Aayah yenyewe, kuna dalili juu yake. Neno Lake Allaah Mtukufu:
(( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا))
((Enyi mlioamini! Mnaposimama kwa ajili ya Swalaah, basi osheni…)).[Al-Maaidah (5: 6)]
Hii ni twahara ya hadathi ndogo kwa kutumia maji. Kisha Akasema:
(( وَإِنْ كُنْتُمْ جُنُبًا فَاطَّهَّرُوا ۚ ))
((..na mkiwa na janaba, basi ogeni..))
Hii ni twahara ya hadathi kubwa kwa kutumia maji. Kisha Akasema:
(( وَإِنْ كُنْتُمْ مَرْضَىٰ أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِنْكُمْ مِنَ الْغَائِطِ أَوْ لَامَسْتُمُ النِّسَاءَ فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً فَتَيَمَّمُوا))
(( Na mkiwa wagonjwa au mmo safarini, au mmoja wenu ametoka chooni, au mmewagusa wanawake na hamkupata maji, basi tayamamuni..))
Na Neno Lake:
(( فَتَيَمَّمُوا))
((Basi tayamamuni)).
Hii ni badali ya twahara mbili. Kwa hiyo Neno Lake:
(( أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِنْكُمْ مِنَ الْغَائِطِ ))
((..au mmoja wenu ametoka chooni… ))
…ni ubainisho wa sababu ndogo. Na Neno Lake:
(( أَوْ لَامَسْتُمُ النِّسَاءَ ))
((Au mmewagusa wanawake..))
..ni ubainisho wa sababu kubwa. [Ash-Sharh Al-Mumti’i (1/239) na mfanowe katika Al-Awsatw (1/128)].
Ijulikane kwamba taawili ya Ash-Shaafi’iy mwenyewe ya maana ya Aayah Tukufu, haikuwa kwa njia ya kukata moja kwa moja, bali inavyoonekana kutokana na maelezo yake ni kuwa yeye amelielezea hilo kwa aina fulani ya tahadhari. [Ameyaelezea haya Shaykh Al-Mash-huwr (Allaah Amhifadhi) katika uhakiki wake wa “Masuala Yenye Mivutano” (2/217)].
Ninasema: "Na kati ya yanayotilia nguvu kwamba kumgusa mwanamke hakutengui wudhuu ni haya yafuatayo:
(a) Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: “Nilimkosa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) usiku kitandani. Nikapapasa kumtafuta na mkono wangu ukagusa tumbo la nyayo zake mbili zikiwa zimesimamishwa na yeye yuko katika sijdah. Alikuwa akisema:
((اللهم إني أعوذ برضاك من سخطك))
((Ee Mola! Hakika mimi najilinda kwa radhi Zako kutokana na hasira Zako)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (222), Abuu Daawuud (865) na At-Tirmidhiy (3819)].
(b) Na imepokelewa vile vile kutoka kwa ‘Aaishah akisema: “Nilikuwa nikilala mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hali ya kuwa miguu yangu iko sehemu yake ya Qibla. Anaposujudu, alikuwa akinibonyeza na mimi huikunja miguu, na anaposimama nainyoosha”. Anaongeza akisema: “Na nyumba nyakati hizo zilikuwa hazina taa”.[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (382), Muslim (272) na wengineo].
Na katika tamko jingine: “Hata anapotaka kuswali witri, alikuwa akinigusa kwa mguu wake”.[Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na An-Nasaaiy (1/101)].
(c) Waislamu wamekuwa siku zote wakiwagusa wake zao. Na hakuna yeyote aliyenukulu toka kwake (Rasuli) kuwa alikuwa akiwaamuru Waislamu kutawadha kwa kufanya hilo. Na wala haikunukuliwa toka kwa Maswahaba wakieleza kwamba alitawadha kutokana na hilo katika maisha yake. Na wala haikunukuliwa kutoka kwake kwamba alitawadha kwa sababu ya hilo, bali lililonukuliwa kutoka kwake katika As-Sunan, ni kuwa alikuwa akiwapiga busu baadhi ya wakeze na wala hatawadhi. [Maimamu wameitia doa: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (178) na An-Nasaaiy (1/104). Na waliotangulia wameitia ila. Tazama Sunan Ad-Daar Qutwniy (1/135-142)].
Kuwa Hadiyth hii ni Swahiyh kuna hitilafu. Lakini hata hivyo, hakuna hitilafu kuhusu kwamba haikunukuliwa kuwa yeye alitawadha kwa sababu ya kumgusa (mwanamke). [Majmu’u Al-Fataawaa (21/410, 20/222) na sehemu nyinginezo].
Ama kauli ya kutenguka wudhuu kwa kugusa kwa matamanio au kutotenguka kwa kugusa bila matamanio, kauli hii haina hoja. Lakini hata hivyo inaweza kusemwa: “Ikiwa atatawadha kwa sababu amemgusa mwanamke kwa matamanio lakini bila ya kumwingilia, basi itakuwa ni vizuri kwa ajili ya kuzima matamanio kama ilivyokuwa imesuniwa kutawadha kwa sababu ya hasira ili kuzituliza. Ama kulazimu kutawadha, hilo haliko. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi".
2- Kutoka damu sehemu isiyo ya kawaida sawasawa ikiwa ni kwa jeraha au kuumikwa, au ikiwa ni nyingi au kidogo
Hili halitengui kwa mujibu wa kauli mbili sahihi za Maulamaa. Ni madhehebu ya Ash-Shaafi'iy na Maalik. Lakini Abuu Haniyfah anasema kwamba hili linatengua. Na wafuasi wa Hanbali wanasema kuwa wudhuu hutenguka kama damu ni nyingi. [Al-Ummu (1/180), Al-Majmu’u (2/55), Al-Istidhkaar (2/269), Al-Mabsuwtw (1/74) na Al-Mughniy (1/184)].
Kauli ya kwanza ndio yenye nguvu zaidi kutokana na mambo yafuatayo:
(a) Hadiyth zinazowajibisha kutawadha kutokana na kutokwa damu si Swahiyh.
(b) Ni kwamba asili (ya mambo) ni uhalali. Kwa hiyo anayetawadha wudhuu sahihi, wudhuu huu hautenguki ila kwa matni au Ijma’a.
(c) Ni Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillah katika kisa cha vita vya Dhaat Ar-Riqaa’i. Anasema: “Swahaba Muhaajir alilala, na mwenzake Mwansari alisimama kuswali. (Akiendelea kuswali) mtu mmoja alimlenga mshale. Akauchomoa akauweka mpaka ikafikia mishale mitatu. Kisha alirukuu na kusujudu na mwenzake (aliyelala) akagutuka. Na alipojua (mlenga mshale) kuwa wao wataweza kumkamata, alikimbia. Na mara Swahaba Muhaajir alipoziona damu zikimchuruzika Mwansari alisema: “ Subhaana Llaah. Kwa nini usingenigutusha mara tu alipokulenga? Akasema: “Nilikuwa nikiisoma Surah na sikupenda kuikatisha”. [Isnadi yake ni Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy kama ni Hadiyth Mu’allaq (1/280), Ahmad ameitoa kama ni Hadiyth Mawswuwl (195), Ahmad (3/343), Ibn Hibaan (1096), Al-Haakim (1/156) na Ad-Daara Qutwniy (1/223) na Sanad yake ni Dhwa’iyf kwa sababu ya ‘Uqayl bin Jaabir. Katika Swahiyh Abiy Daawuud (193), Al-Albaaniy ameiona ni Swahiyh!!].
Inavyojulikana ni kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alilijua hilo na wala hakumkatalia kuendelea na Swalaah baada ya kutokwa na damu. Na lau kama damu ingelikuwa inatengua wudhuu, basi Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) angelimbainishia hilo na wengineo wote waliokuwepo katika vita hivyo. Haijuzu kuchelewesha kulibainisha jambo wakati inapohitajika kufanya hivyo. [As-Sayl Al-Jarraar (1/99)].
(d) Imethibiti kuwa ‘Umar bin Al-Khattwaab alipochomwa kisu, aliswali na hali jeraha lake linafuka damu.
(e) Habari zimetangaa kutoka zama hadi zama kwamba askari waliokuwa wakipigana Jihadi, walikuwa wakipata maumivu ya majeraha. Hakuna anayeweza kupinga kwamba majeraha haya hayakuwa yakitoka damu na nguo zao kutapakaa damu. Pamoja na haya, walikuwa wakiswali hivyo hivyo. Na hakuna yeyote aliyenukulu toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba aliwaamuru watoke kwenye Swalaah au wasiswali. Na kwa ajili hiyo, Al-Hasan Al- Baswriy anasema: “Waislamu wangali wanaswali na majeraha yao”. [Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy kama ni Hadiyth Mu’allaq (1/280). Na Ibn Abi Shaybah ameifanya kuwa Hadiyth Mawswuul kwa Sanad Swahiyh kama ilivyo katika Al-Fat-h (1/281)].
3- Kutapika na mfano wake
Madhehebu ya Maulamaa katika suala hili, yako vilevile kama yalivyo katika suala la kutokwa damu. Na lililo sahihi ni kuwa kutapika hakutengui wudhuu kwa vile hoja zinazowajibisha kutawadha hazina usahihi wowote na kwamba asili ya mambo ni uhalali.
Ama Hadiyth ya Mi’idaan bin Twalha aliyenukuu toka kwa Abi Ddardaai kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitapika, akafungua kisha akatawadha, hakuna shaka kwamba Hadiyth hii haimaanishi kuwa ni lazima kutawadha kama mtu ametapika, kwani hicho ni kitendo tu. Na lengo la kitendo hicho ni kuonyesha kuwa ni vizuri (mustahabbu) kufanya hivyo. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy (87) na Abu Daawuud (2381). Tazama Al-Irwaa (111)].
4- Kucheka ndani ya Swalaah au nje yake
Maulamaa kwa sauti moja wamekubaliana kwamba kucheka nje ya Swalaah hakutengui twahara wala hakuwajibishi kutawadha, na kwamba kucheka ndani ya Swalaah huibatilisha. Lakini Maulamaa hao wamehitalifiana katika kutenguka wudhuu kwa kucheka ndani ya Swalaah. Abu Haniyfah na wenzake, Ath-Thawriy, Al-Hasan na An-Nakh’iy wanaona kwamba hilo linatengua wudhuu. Wao wameitolea hoja Hadiyth Munqati’i isiyozingatiwa, nayo ni Hadiyth ya Abu Al-‘Aaaliyah isemayo: “Mtu mmoja kipofu alikuja hali ya kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anaswalisha watu. Mtu yule aliporomoka katika shimo ndani ya Msikiti na baadhi ya watu wakacheka. Hapo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwamuru kila aliyecheka atawadhe na aswali upya”.[Isnadi yake ni dhwa’iyf sana: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ad-Daara Qutwniy (1/162) na Ibn ‘Uday (2/716)].
Hadiyth iliyothibiti ni ya Jaabir, nayo ni Mawquuf isemayo: “Ni kwamba (Rasuli) aliulizwa kuhusu mtu anayecheka ndani ya Swalaah”. Naye akajibu:
((يعيد الصلاة ولا يعيد الوضوء))
((Atarudia tena Swalaah yake, lakini hatotawadha upya)). [Hadiyth Swahiyh Mawquwf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy ikiwa Mu’allaq (1/280), Al-Bayhaqiy kama Hadiyth Mawswuwl (1/144) na Ad-Daara Qutwniy (1/172)].
Hadiyth hii ndio Swahiyh. Ni madhehebu ya Ash-Shaafi'iy, Maalik, Ahmad, Is-Haaq na Abu Thawr. [Al-Majmu’u (2/61), Al-Kaafiy (1/151), Al-Mughniy (1/117) na Al-Awsatw (1/227)].
5- Kuosha maiti na kuibeba
Mwenye kuosha maiti au kumbeba, basi wudhuu wake hautenguki kwa mujibu wa kauli yenye nguvu. Lakini baadhi ya Maulamaa wanaona ni vizuri kuoga kwa aliyemwosha maiti, na kutawadha kwa aliyembeba. Hii ni kwa Hadiyth ya Abu Hurayrah anayesema kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((من غسل ميتا فليغتسل، ومن حمله فليتوضأ))
((Mwenye kumwosha maiti aoge, na mwenye kumbeba atawadhe)). [Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (3162), At-Tirmidhiy (993), Ibn Maajah (1463) na Ahmad (2/433). At-Tirmidhiy, Ibn Hajar na Al-Albaaniy wameifanya Hadiyth Hasan katika Al-Irwaa (1/174). Lakini linaloonekana ni kuwa inahitaji kuchunguzwa zaidi, kwani imekosolewa!!]
Lakini ikiwa Hadiyth hii ni Swahiyh.
6- Mwenye wudhuu kufanya shaka ya kutenguka wudhuu wake
Mwenye kutawadha wudhuu sahihi, kisha akafanya shaka kama wudhuu umemtenguka au la, basi atabakia juu ya uasili wa kile alichokiyakinisha katika utwahara mpaka atakapopata uhakika kwamba wudhuu wake umetenguka. Na ikiwa atafanya shaka nailhali yuko ndani ya Swalaah, basi hatoivunja mpaka ayakinishe kutenguka wudhuu. Hii ni kwa Hadiyth ya ‘Abdullah bin Zayd aliyesema: “Rasuli alishtakiwa kuhusu mtu anayekuwa na wasiwasi katika Swalaah”. Rasuli akasema:
((لا ينصرف حتى يسمع صوتا أو يجد ريحا))
((Haivunji mpaka asikie sauti au anuse harufu)). [Hadiyth Swahiyh: Imetangulia kuelezwa hivi karibuni].
Al-Baghawiy katika Sharhus Sunnah (1/353) amesema: “Maana yake: Mpaka apate uhakika wa hadathi, kwa vile kusikia sauti au kuwepo harufu ni sharti”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
033-Wudhuu Unapasa Kwa Ajili Ya Swalaah Tu Na Si Vinginevyo
Alhidaaya.com [3]
Wudhuu unapasa kwa yule anayetaka kuswali – kama hana wudhuu – sawasawa ikiwa Swalaah ni ya Faradhi, Sunnah au Maiti. Hii ni kwa Neno Lake Subhaana:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُواا))
(( Enyi mlioamini! Mnaposimama kuswali, basi osheni…..)). [Al Maaidah (5:6)]
Na kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((لايقبل الله صلاة بغير طهور))
((Allaah Haikubali Swalaah bila ya wudhuu)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (224) na wengineo].
Haipasi kutawadha kwa jambo jinginelo lisilokuwa Swalaah, na wala haikatazwi kwa asiyekuwa na wudhuu kufanya jambo jingine lolote isipokuwa Swalaah. Lakini wudhuu umesuniwa katika mambo yafuatayo:
Kutufu Al-Ka’abah
“Hatujagundua au kuipata dalili yoyote sahihi na ya wazi yenye kuwajibisha kutawadha kwa wenye kutufu. Maelfu kwa maelfu ya Maswahaba ambao idadi yao hakuna aijuaye ila Allaah, walikuwa wakitufu katika enzi ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Na sisi hatujapata habari yoyote inayoeleza kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwamrisha yeyote kati yao kutawadha kwa ajili ya kutufu pamoja na kuwepo uwezekano wa kutenguka wudhuu kwa wengi kati yao wakati wa kutufu, na kuingia wengi wao katika ‘ibaadah hiyo bila ya wudhuu na hususan katika siku hizo ambapo msongamano ulikuwa mkubwa kama katika twawaf za “Quduwm” na “Ifaadhwah”.
Na kwa vile hakuna dalili yoyote iliyopokewa juu ya kupasa kutawadha kwa ajili ya twawaf, na wala hakuna Ijma’a ya Maulamaa juu ya kupasa hilo pamoja na kuhitajika, basi inabainika kwamba si lazima”. [Jaami'u Ahkaamin Nisaai cha Shaykh wetu Allaah Amhifadhi (2/515)].
Maulamaa wameitolea dalili Hadiyth Marfu’u ya Ibn 'Abbaas juu ya ulazima wa kutufu isemayo:
((الطواف بالبيت صلاة إلا أن الله أباح فيه الكلام))
"Kutufu Nyumba ni Swalaah, isipokuwa Allaah Ameruhusu kuzungumza ndani yake". [Hadiyth Mawquwf: Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Al-Haakim na wengineo.
Na haifai kuwa ni Hadiyth Marfu’u, bali lililo sawa ni kuwa ni Hadiyth Mawquwf kama alivyobainisha Shaykh wetu Allaah Amnyanyulie cheo chake katika kitabu cha Jaami'u Ahkaamin Nisaai (2/515-521) kinyume na Mwanachuoni Mkubwa Al-Albaaniy (Allaah Amrehemu) aliyesema kuwa ni Swahiyh katika kitabu cha Al-Irwaa'i (1/156)].
Wamesema: "Ikiwa twawaf ni Swalaah, basi inapasa kutawadha kama ilivyo katika Swalaah". Lakini kauli yao hii inakataliwa kwa mambo mawili:
Kwanza: Si sahihi kwamba Hadiyth hii ni Marfu’u. Lililo sawa ni kuwa ni Hadiyth Mawquuf kutokana na maneno ya Ibn 'Abbaas. Aidha, hili limetiliwa nguvu na At-Tirmidhiy, Al-Bayhaqiy, Ibn Taymiyah, Ibn Hajar na wengineo.
Pili: Na kama tukijaalia kuwa ni Hadiyth Swahiyh, basi haimaanishi kuwa twawaf ni kama Swalaah katika kila kitu mpaka ishurutishiwe masharti yanayohusiana na Swalaah. [Tazama katika Majmu'u Al-Fataawaa (26/198) na Jaami'u Ahkaamin Nisaai (2/522). Ndani yake kuna tofauti 11 kati ya Swalaah na twawaf].
Si hivyo tu, bali Swalaah ya kisharia ambayo sharti yake ni utwahara na mfano wake, ni ile inayofunguliwa kwa takbiyr na kumalizwa kwa tasliym.
Na kwa ajili hiyo, Shaykh wa Uislamu amesema: " Imenidhihirikia kwamba kujitwaharisha na hadathi, - bila shaka yoyote - hakushurutishwi katika twawaf na wala si wajibu. Lakini twahara ndogo (wudhuu) imesuniwa katika twawaf, kwani dalili za kisharia zinaonyesha kuwa si wajibu, na hakuna katika sharia lenye kuthibitisha wajibu wa kutawadha katika twawaf." [Majmu'u Al-Fataawaa (26/298)].
Abu Muhammad Ibn Hazm amekubaliana na hili. [Al-Muhalla (7/179)].
Kugusa Mswahafu:
Maalik, Ash-Shaafiiy, Ahmad na Jamhuri ya Maulamaa, wanaona kwamba haijuzu kwa mwenye hadathi kugusa Mswahafu. [Al-Majmu'u (1/17), Al-Istidhkaar (8/10), Al-Mughniy (1/147) na Al-Awsatw (2/102)].
Kigezo cha ushahidi wao ni mambo mawili:
1- Neno Lake Allaah Mtukufu:
((لَا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ))
(( Hapana akigusaye ila waliotakaswa)). [Al-Waaqi'ah (56: 79)].
2- Hadiyth ya Amri bin Hazm kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaandikia watu wa Yemen barua. Kati ya yaliyoandikwa ni:
((لا يمس القرآن إلا طاهر))
((Asiiguse Qur-aan isipokuwa aliye twahara)). [Hadiyth Dhwaíyf: Ina Sanad Dhwa’iyf na baadhi yake ni karatasi tu zisizo na Sanad yoyote. Maulamaa wametofautiana katika kuipandisha ifikie ngazi ya Hadiyth Hasan. Lakini Al-Albaaniy amesema kuwa ni Swahiyh katika kitabu cha Al-Irwaa (1/158). Lililo wazi zaidi ni kuwa Hadiyth hii haipandi. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi].
Ninasema: "Waliyoyatolea ushahidi yanajibiwa kwa yafuatayo:
1- Haiwezekani kuitolea dalili Aayah hiyo Tukufu isipokuwa kama kiwakilishi kilichopo katika (يمسه) kitarejeshwa kwa Qur-aan. Na kauli dhahiri iliyoshikiliwa na wafasiri wengi ni kuwa kiwakilishi hicho kinarejea kwa Kitabu kilichohifadhiwa huko mbinguni; nacho ni "Al-Lawh Al-Mahfuwdh". Na waliotwaharika ni Malaika. Na hili linaonyeshwa kutokana na muundo wa Aayah Tukufu:
إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ ﴿٧٧﴾
Hakika hii bila shaka ni Qur-aan tukufu.
فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ ﴿٧٨﴾
Katika Kitabu kilichohifadhiwa.
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ ﴿٧٩﴾
Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa. [Al-Waaqi'ah (56: 77-79)].
Na hili linatiliwa nguvu na Neno Lake Subhaanah:
فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ ﴿١٣﴾
Katika Sahifa zenye kuadhimishwa.
مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ ﴿١٤﴾
Zimetukuzwa na zimetakaswa.
بِأَيْدِي سَفَرَةٍ ﴿١٥﴾
Katika mikono ya Malaika waandishi.
كِرَامٍ بَرَرَةٍ ﴿١٦﴾
Watukufu, watiifu. ['Abasa (80 : 13-16)].
2- Ama Hadiyth, basi ni Dhwa’iyf na haifai kutolewa dalili, kwa vile imetokana na nyaraka zisizosikika mbali na kuwepo mvutano mkali kuhusu wapokezi wake.
Ama kama tukijaalia kuwa Hadiyth hii ni Swahiyh na kwamba kiwakilishi kinarejea kwa Qur-aan, basi tunasema:
"Kilichotwahara" ni katika visawe vya kilafudhi. Inaweza kuwa kwa maana ya Muumini, au kwa maana ya mtu aliyejitwaharisha na hadathi kubwa, au kwa maana ya mtu aliyejitwaharisha na hadathi ndogo, au kwa maana ya mtu ambaye hana najsi katika mwili wake. Hivyo suala inabidi lirejeshwe katika taaluma ya fani ya "Uswuul" isemayo:
"Mwenye kujuzisha kukichukulia kisawe cha kilafudhi kwa maana zake zote, basi maana hizo atazichukulia hapa. Lakini kwa vile haijuzu kutumia jina la najsi kwa Muumini asiye na wudhuu au mwenye janaba sawasawa ikiwa ni kweli anayo najsi hiyo, au kimajazi, au kilugha kwa kauli ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((المؤمن لا ينجس))
((Muumini hawi najsi)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (279) na Muslim (371)]…….mbali na kuthibiti kuwa Muumini daima ni twahara, basi haiwezekani Aayah au Hadiyth kuitumia maana hiyo. Hivyo basi, inalazimu kulichukulia tamshi kwa asiye mushriki kama Alivyosema Allaah Mtukufu:
((إنَّمَا الْمُشْرِكُونَ نَجَس))
((Hakika washirikina ni najsi)). [At-Tawbah (9 : 28)].
Na kwa Hadiyth iliyokataza kusafiri na Qur-aan kwenda nayo katika nchi ya adui.
Na mwenye kusema kuwa kisawe tamshi kimekusanya maana zote, kwa hivyo hakiwezi kutumiwa mpaka ibainishwe, atajibiwa kuwa hakuna hoja katika Aayah wala Hadiyth na hata kama jina la "aliyetwaharika" litakuwa na maana ya mtu asiye na hadathi ndogo au kubwa. [Limezungumziwa katika Nayl Al- Awtwaar (1/260)].
Kwa hivyo, imejulikana kuwa hakuna dalili yoyote inayoashiria kuwa ni lazima kutawadha kwa ajili ya kugusa Msahafu. Na haya ni madhehebu ya Abu Haniyfah, Daawuud na Ibn Hazm. Na ndivyo hivyo hivyo alivyosema Ibn 'Abbaas na kikundi cha watangu wema. Pia Ibn Al-Mundhir yupo katika mkondo huo huo. [Al-Badaai-'i (1/33), Haashiyat Ibn 'Aaabidiyn (1/173), Al-Muhalla (1/81) na Al-Awsatw (2/103)].
Faida
Hakuna ubaya kusoma Qur-aan kwa mwenye hadathi ndogo au hadathi kubwa bila kugusa Msahafu kwa mujibu wa kauli za Maulamaa zenye nguvu. Suala la kusoma Qur-aan ni jepesi zaidi hapa kuliko suala la kugusa Msahafu kwa mambo yafuatayo:
1- Hakuna Hadiyth yoyote Marfu’u ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inayokataza kusoma. Kila Hadiyth iliyopokelewa ni dhwa’iyf na haina hoja yoyote. Ni kama Hadiyth Marfu’u ya ‘Abdullah bin 'Amr:
((لا يقرأ الجنب ولا الحائض شيئا من القرآن))
((Mwenye janaba au hedhi asisome chochote katika Qur-aan)).
Na Hadiyth ya Ibn Rawaaha:
((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza yeyote kati yetu kusoma Qur-aan akiwa na janaba)).
Na Hadiyth ya ‘Abdullahi bin Maalik:
((إذا توضأت وأنا جنب أكلت وشربت، ولا أصلي ولا أقرأ حتى أغتسل))
"Ninapotawadha nami nina janaba, ninakula na kunywa, lakini siswali wala sisomi mpaka nioge".
Hadiyth zote hizi si Swahiyh. [Zitazame katika Al-Irwaa (192, 485) cha Mwanachuoni Mkubwa Al-Albaaniy na maelezo ya Shaykh Mash-huwr katika Al-Khilaafiyyaat cha Al-Bayhaqiy (2/11). Basi ni vizuri yapitiwe].
2- Imethibiti kutoka kwa 'Aaishah kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akimdhukuru Allaah Mtukufu katika nyakati zake zote. [Hadiyth Swahiyh Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (373), na imetolewa maelezo na Al-Bukhaariy kabla ya Hadiyth ya (608)].
3- Ni kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaamuru wanawake wenye hedhi kutoka siku ya ‘Iyd waketi nyuma ya watu na wafuatilize takbiri zao na du’aa zao. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (971) na Muslim (890)].
Kwa hiyo, hii inaonyesha kuwa mwenye hedhi hupiga takbiyr na humdhukuru Allaah Mtukufu.
4- Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia 'Aaishah wakati alipokuwa na hedhi:
((إفعلي ما يفعل الحاج غير أن لا تطوفي بالبيت))
((Fanya yote ayafanyayo mwenye kuhiji isipokuwa tu usizunguke Ka’abah)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (1650)].
Inajulikana kwamba mwenye kuhiji humdhukuru Allaah na husoma Qur-aan.
Na kwa vielelezo hivi, inafahamika kuwa mwenye hadathi hazuiliwi kusoma Qur-aan. Shaykh wa Uislamu anasema: "Haya ndiyo madhehebu ya Abu Haniyfah na ndio madhehebu mashuhuri ya Ash-Shaafi'iy na Ahmad". [Majmuu Al-Fataawaa (21/459) na Al-Awsatw (2/97)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
34-Mambo Ambayo Mtu Akiyafanya Imesuniwa Awe Na Wudhuu
1- Wakati wa kumdhukuru Allaah Mtukufu
Hapa unaingia uradi wowote, kusoma Qur-aan, kutufu Al Ka’abah na mengineyo.
Wudhuu umesuniwa kwa hayo kutokana na Hadiyth ya Al-Muhaajir bin Qunfudh kwamba yeye alimsalimia Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa anatawadha, naye hakumjibu mpaka alipomaliza. Kisha akamwambia:
((إنه لم يمنعني أن أرد عليك إلا أني كرهت أن أذكر الله إلا على طهارة))
((Hakika hakuna kilichonizuilia kukujibu isipokuwa tu niliona uzito kumdhukuru Allaah mpaka niwe katika twahara)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (17), An-Nasaaiy (1/16), Ibn Maajah (350), Ad-daaramiy (2/287) na Ahmad (5/80). Ni Hadiyth Swahiyh kama ilivyo katika As-Silsilat As-Swahiyhah (834)].
Lakini, Hadiyth hii haiambatani na Hadiyth ya 'Aaishah iliyosajiliwa na Muslim (4/68) isemayo:
Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akimtaja Allaah katika nyakati zake zote.
2- Wakati wa kulala
Imepokelewa toka kwa Al-Barraa bin 'Aazib Allaah Amridhie, amesema: " Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((إذا أتيت مضجعك فتوضأ وضوئك للصلاة، ثم اضطجع على شقك الأيمن، ثم قل: اللهم أسلمت نفسي إليك...))
((Unapotaka kulala, basi tawadha wudhuu wako wa Swalaah, kisha lala kwa ubavu wako wa kulia, halafu sema: Ee Allaah! Nimeisalimisha nafsi yangu Kwako)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (247), Muslim (2710) na wengineo].
3- Kwa mwenye janaba kama akitaka kula, au kunywa, au kulala, au kumwingilia tena mkewe
Imepokelewa toka kwa 'Aaishah Allaah Amridhie, amesema: "Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anapokuwa na janaba na akataka kula au kulala, alikuwa akitawadha wudhuu wa Swalaah". [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (288), Muslim (305) na tamko ni lake, Abuu Daawuud (222), At-Tirmidhiy (118), An-Nasaaiy (1/138) na wengineo].
Na imepokelewa na Abuu Sa'iyd Allaah Amridhie toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((إذا أتى أحدكم أهله ثم أراد أن يعود فليتوضأ))
((Anapomwingilia mmoja wenu mkewe kisha akataka kurejea tena, basi atawadhe)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (3/217), Abu Daawuud (217), At-Tirmidhiy (141) na An-Nasaaiy (1/42)].
4- Kabla ya kuoga
Imepokelewa na 'Aaishah Allaah Amridhie, amesema: "Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa akioga janaba, huanza kwa kuosha mikono yake, kisha humimina maji katika mkono wake wa kushoto kwa kutumia mkono wa kulia na kuosha utupu wake, kisha hutawadha wudhuu wake wa Swalaah".[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (248), Muslim (316) na wengineo].
5- Baada ya kula kilichopikwa kwa moto
Ni kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):
((توضأوا مما مست النار))
((Tawadheni kwa (kula) kilichopikwa kwa moto)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (351), Abuu Daawuud (192), At-Tirmidhiy (79), An-Nasaaiy (1/105) na Ibn Maajah (485)].
Amri hapa ni ya kupendezeshea kutokana na Hadiyth ya 'Amri bin Umayyah Adh-Dhamriy aliyesema: "Nilimwona Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akilikata bega la kondoo, akala sehemu, kisha akaitwa kwenda kuswali, akasimama, akakitupa kisu, akaswali na wala hakutawadha". [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (1/50), Muslim (4/45 An-Nawawiy) na Ibn Maajah (490)].
6- Kujadidisha wudhuu kwa kila Swalaah
Ni kwa Hadiyth ya Buraydah Allaah Amridhie, amesema: "Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akitawadha wakati wa kila Swalaah. Na ilipokuwa siku ya Al Fat-h, alitawadha, akapukusa juu ya khufu zake, akaswali Swalaah nyingi kwa wudhuu mmoja.." Hadiyth. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (277), Abuu Daawuud (171), At-Tirmidhiy (61), An-Nasaaiy (1/89) na Ibn Maajah (510)].
7- Kila pale wudhuu unapotenguka
Ni kutokana na Hadiyth ya Bilal iliyotajwa nyumba ya kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisikia mchakato wa viatu vyake mbele yake peponi. Akamwambia:
((بم سبقتني إليها))
((Ni kwa jambo gani umenitangulia kuelekea huko))?
Akasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Kamwe sikuadhini ila niliswali rakaa mbili, na wala kamwe sikupata hadathi ila nilitawadha".
Na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:
((لهذا))
((Ni kwa hili)). [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy alipotaja wudhuu wakati wa hadathi (3689), Abuu Daawuud (3055), Ahmad (21962) na tamko ni lake. Asili yake ni katika Swahiyh Mbili bila ya sehemu ya ushahidi].
8- Kwa kutapika
Ni kwa Hadiyth ya Mu'daan bin ‘Abi Twalha toka kwa Abu Ad-Dardaai kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitapika, akafungua, kisha akatawadha. Kisha alikutana na Thawbaan katika Msikiti wa Damascus akalitaja hilo kwake na Thawbaan akamwambia: "Amesema kweli, na mimi ndiye niliyemmiminia maji yake ya kutawadhia". [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy (87) na Abuu Daawuud (2381) kwa Sanad Swahiyh].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
035-Kupaka Juu Ya Vizuizi
Kwanza: Kupaka Juu Ya Khufu Mbili
Alhidaaya.com [3]
Taarifu yake: Khufu ni viatu vya ngozi vinavyofunika visigino viwili. [Nayl Al-Awtwaar (1/241)].
Na kupaka kilugha ni kisoukomo (masdwar) cha kitenzi cha “amepaka”, nako ni kuupitisha mkono juu ya kitu kwa kuukunjua. [Al-Qaamuws Al-Muhiyt na Maqaayiys Al-Lughah].
Na kupaka juu ya khufu mbili maana yake ni kuitia umajimaji khufu maalumu katika wakati na mahala maalumu badala ya kuosha miguu miwili wakati wa kutawadha. [Ad-Durru Al-Mukhtaar].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
036- Hukmu Ya Kupukusa Juu Ya Khufu Mbili
Alhidaaya.com [3]
Kupukusa juu ya khufu mbili kunajuzu, lakini kuosha miguu ni bora zaidi kwa mujibu wa Jamhuri ya Wanazuoni. Mahanbali wanaona kwamba kupukusa juu ya khufu mbili ni bora zaidi kwa ajili ya kuitumia ruksa. [Fat-h Al-Qadiyr (1/126), Ash-Sharh Asw-Swaghiyr (1/227), Al-Majmu’u (1/502) na Muntahaa Al-Iraadaat (1/23)].
La sawa ni kuwa lililo bora kwa kila mtu ni kwa mujibu wa hali yake ya uvaaji. Kwa aliyezivaa, basi apukuse juu yake na wala asizivue kwa ajili ya kumfuata Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba zake. Ama kwa asiyezivaa, basi aoshe miguu na wala asifanye uchu wa kuzivaa ili tu apukuse. [Hili ni chaguo la Shaykh wa Uislamu kama ilivyo katika Al-Ikhtiyaaraat (uk.13)].
Pia, asipapie kuzivua ndani ya muda wake ili tu apate kuosha miguu. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
036-Usharia Wa Kupaka Juu Ya Khufu Mbili
Alhidaaya.com [3]
Wanachuoni wote wamekubaliana kwamba mwenye kutawadha kikamilifu, kisha akazivaa khufu zake mbili, halafu wudhuu ukamtenguka, basi anaruhusika kupukusa juu yake. [Al-Ijma’a cha Ibn Al-Mundhir (20) na Al-Awsatw (1/434)].
Ibn Mubaarak kasema: “Hakuna khitilafu yoyote kuwa kupukusa juu ya khufu mbili, kunajuzu. Na hii ni kwa vile kila Swahaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye imeripotiwa kuwa amekirihisha kupaka juu ya khufu mbili, imethibiti kinyume chake. [Al-Awsatw (1/434), Sunan Al-Bayhaqiy (1/272) na Al-Fat-h (1/305)].
Usharia wake umethibiti kwa Sunnah Swahiyh iliyo “Mutawaatir” toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Na madhubuti zaidi linaloonyesha usharia huo ni Hadiyth ya Hammam aliyesema: “Jurayr alikojoa, kisha akatawadha, halafu akapaka juu ya khufu zake. Akaulizwa: Unafanya hivi? Akasema: Ndio. Nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekojoa, kisha akatawadha na akapukusa juu ya khufu zake mbili”.
Al-A’amash anasema: “Ibrahim amesema: Walikuwa wakiipenda Hadiyth hii, kwani Jurayr alisilimu baada ya kuteremka Suwrat Al- Maaidah”. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (387) na Muslim (1568), na tamko ni lake].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
037-Muda Wa Kupukusa
Alhidaaya.com [3]
Sharia imeweka muda wa siku tatu na masiku yake kupukusa juu ya khufu mbili kwa msafiri, na siku moja na usiku wake kwa mkazi. Haya ndiyo yaliyokubaliwa na Jamhuri ya Maulamaa wa Hanafi, Hanbali, Dhwaahir na Ash-Shaafi’iy katika madhehebu mapya na Adh-Dhwaahiriyyah. [Al-Mabsuwtw (1/98), Al-Ummu (1/34), Al-Mughniy (1/209) na Al-Muhalla (2/80)].
Dalili ya hayo ni haya yafuatayo:
1- Ni Hadiyth ya ‘Aliy (Allaah Amridhie) aliyesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameweka muda wa siku tatu na masiku yake kwa msafiri, na siku moja na usiku wake kwa mkazi”.[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (276) na An-Nasaaiy (1/84)].
2- Ni Hadiyth ya ‘Ouf bin Maalik Al-Ashja’iy aliyesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliamuru kupukusa juu ya khufu mbili katika Vita vya Tabuk siku tatu na masiku yake kwa msafiri, na siku moja na usiku wake kwa mkazi”.[Hadiyth Swahiyh.: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad (6/27) kwa Sanad Swahiyh, nayo ina ushahidi toka Hadiyth ya Abu Bakrah iliyoko kwa Ibn Maajah (556) na wengineo].
3- Hadiyth ya Swafwan bin ‘Assal, amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akituamrisha tunapokuwa safarini, tusizivue khufu zetu siku tatu na masiku yake ila kwa janaba, lakini si kwa kwenda haja kubwa, au ndogo, au kulala”. [Hadiyth Hasan: Imetajwa hivi karibuni].
Maalik amekwenda kinyume na haya (nayo ni kauli ya zamani ya Ash-Shaafi’iy). Yeye anaona kwamba hakuna muda wake maalumu, bali mtu anaweza kupukusa juu ya khufu zake madhali hakuzivua au kupatwa na janaba!! Na ndivyo hivi hivi alivyosema Al-Layth. [Al-Mudawwanah (1/41) na Bidaayat Al-Mujtahid (1/24)].
Wao wametoa hoja kwa Hadiyth ambazo ni Dhwa’iyf. Kati ya Hadiyth hizo ni:
1- Iliyopokelewa toka kwa Ubayya bin ‘Ammaarah, amesema: “Nilisema: Ee Rasuli wa Allaah! Je, nipukuse juu ya khufu mbili? Akasema: Ndiyo. Nikasema: Siku moja? Akasema: Siku moja. Nikasema: Na siku mbili je? Akasema; Na siku mbili. Nikasema: Na siku tatu je? Akasema: Na siku uzitakazo”.[Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (157), At-Tirmidhiy na Ibn Maajah (553).]
2- Yaliyopokelewa toka kwa Khuzaymah bin Thaabit, amesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametuwekea siku tatu, na lau kama tungelimtaka atuongezee, basi angetuongezea”.[Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bayhaqiy (1/280)]. Yaani kupukusa juu ya khufu mbili kwa msafiri. Na hili lau kama lingekuwa sahihi, basi haliwezi kuwa hoja, kwani ni dhana tu ya Swahaba, na sisi tusingelichukulia.
3- Yaliyopokelewa toka kwa Anas bin Maalik kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
((إذا توضأ أحدكم ولبس خفيه فليصل فيهما، وليمسح عليهما، ثم لا يخلعهما إن شاء إلا من جنابة))
((Anapotawadha mmoja wenu akazivaa khufu zake, basi aswali nazo na apukuse juu yake, kisha asizivue muda autakao, isipokuwa kwa janaba)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bayhaqiy (1/280), Atw-Twahaawiy (1/48) na Ad-Daara Qutwniy (72).
Hadiyth zote hizi ni dhwa’iyf na hazifai kwa ushahidi.
4- Ni athar iliyopokelewa toka kwa ‘Aamir akisema: “Nilitoka Sham kuelekea Madiynah. Niliondoka siku ya ijumaa na nikaingia Madiynah siku ya ijumaa. Kisha niliingia kwa ‘Umar bin Al-Khattwaab akaniuliza: Ni lini uliziivaa khufu zako? Nikajibu: Siku ya ijumaa. Akauliza: Je, ulizivua? Nikajibu: Hapana. Akasema: Umefanya sawa”.
Hii pia ni dhwa’iyf. Al-Bayhaqiy amesema: “Tumepokea toka kwa ‘Umar kuhusu wakati. Basi inawezekana kuwa ima alirejea katika kauli hiyo wakati ilipomfikia toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), au iwe kauli yake iliyowafikiana na Sunnah Swahiyh iliyo mashuhuri zaidi. Na kwa ajili hiyo, Ibn Hazm amesema katika kitabu cha Al-Muhalla (2/93): “ Haiswihi kwa Swahaba yeyote kukhalifu muda uliowekwa isipokuwa Ibn ‘Umar peke yake”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
038-Muda Wa Kupukusa Unapoanzia
Alhidaaya.com [3]
Imejulikana kwamba muda wa kupukusa kwa mkazi ni siku moja na usiku wake, na kwa msafiri ni siku tatu na masiku yake. Basi ni wakati gani muda huo unaanza kuhesabiwa? Katika hili, Wanachuoni wana kauli tofauti:
Ya kwanza
Unaanza pale anapopata hadathi ya kwanza baada ya kuzivaa. Hii ni kauli ya Sufyaan Ath-Thawriy, Ash-Shaafi’iy, Abu Haniyfa na wenzake. Na hili li wazi katika madhehebu ya Hanbali. [Al-Mabsuwtw (1/99), Al-Majmu’i(1/470), Al-Mughniy (1/291) na Al-Awsatw (1/443)].
Wamesema kuwa kipindi cha baada ya hadathi, ni wakati unaoruhusiwa kupukusa.
Ya pili
Unaanza kuanzia wakati wa kuzivaa. Ni kauli ya Al-Hasan Al-Baswriy. [Al-Ikliyl Sharh Manaar As-Sabiyl cha Shaykh Wahiyd ‘Abdu Ssalaam (1/136)].
Ya tatu
Atapukusa Swalaah tano, yaani Swalaah 15 kwa msafiri (3X5), na wala asipukuse zaidi ya hivyo. Ni madhehebu ya Ash-Sha’abiy, Is-haaq, Abu Thawr na wengineo. [Al-Mughniy (1/291), Al-Majmu’u (1/466) na Al-Awsatw (1/444)].
Ya nne
Unaanza pale inapojuzu kwake kupukusa baada ya hadathi, sawasawa ikiwa alipukusa au hajapukusa na wala hakutawadha kwa namna ambayo lau kama atapukusa baada ya kupita sehemu ya muda, itambidi apukuse ule muda uliosalia basi. Haya ni madhehebu ya Ibn Hazm. Yeye ameyajadili madhehebu mengi. [Al-Muhalla cha Ibn Hazm (2/95 na kurasa zinazofuatia)].
Ya tano
Unaanza tokea pukuso la kwanza baada ya hadathi. [Masaail Ahmad cha Abu Daawuud (10) na Al-Muhallaa (2/95)].
Ni kauli ya Ahmad bin Hanbali na Al-Awzaa’iy. Pia ni kauli iliyoungwa mkono na An-Nawawiy, Ibn Al-Mundhir na Ibn ‘Uthaymiyn. Na hii ndio kauli yenye nguvu zaidi kutokana na maana bayana ya neno lake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((يمسح المسافر)) و ((يمسح المقيم))
((Msafiri hupukusa)) na ((Mkazi hupukusa)).
Na haiwezekani kuthibitishwa kwamba mtu anapukusa, ila kwa kitendo cha kupukusa. Na haijuzu kuipiga pande maana hii bayana bila dalili au ushahidi. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Na kwa haya, ikiwa mtu ametawadha wakati wa Swalaah ya adhuhuri na akavaa khufu zake saa sita kwa mfano, kisha akabakia na utwahara wake hadi saa tisa alasiri, kisha wudhuu ukamtenguka na wala hakutawadha mpaka saa kumi (baada ya Swalaah ya alasiri) na akapukusa, basi atapukusa mpaka saa kumi alasiri ya kesho yake ikiwa ni mkazi, na mpaka siku ya nne ikiwa ni msafiri.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
039-Mkazi Akipukusa Kisha Akasafiri
Alhidaaya.com [3]
Aliyepukusa khufu zake naye ni mkazi kwa muda wa chini ya siku na usiku wake kisha akasafiri, basi Maulamaa wana kauli mbili:
Ya kwanza:
Ni haki yake kupukusa mpaka akamilishe siku tatu na masiku yake kwa kujumlisha na ule muda aliopukusa kabla ya kusafiri. Haya ni madhehebu ya Ath-Thawriy, Abu Haniyfah na wenzake, na riwaya iliyopokelewa toka kwa Ahmad. Ibn Hazm pia amesema hivyo. [Ikhtilaaf Al’ulamaa cha Al- Maruuziy (uk.31), Al-Mughniy (1/299) na Al-Muhalla (2/109)].
Ya pili:
Ni haki yake kupukusa mpaka akamilishe siku moja na usiku wake, kisha itampasa aoshe miguu yake anapotawadha. Hii ni kauli ya Ash-Shaafi’iy, Ahmad na Is-Haaq. [Al-Ummu (1/35), Ikhtilaaf Al’ulamaa (uk.31) na Al-Awsatw (1/446)].
Yenye nguvu ni kuwa ni haki yake kupukusa mpaka akamilishe siku tatu na masiku yake kwa vile mtu huyu inapomalizika siku na usiku wake na yeye ni msafiri, basi ana haki ya kuutimiza muda kutokana na uwazi wa maana ya Hadiyth:
((يمسح المسافر ثلاثة أيام ولياليهن))
((Msafiri hupukusa siku tatu na masiku yake)).
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
040-Msafiri Akipukusa Kisha Akawasili Mjini Kwake
Alhidaaya.com [3]
Ikiwa msafiri atapukusa juu ya khufu zake siku moja na usiku wake au zaidi kisha akawasili kwake, ni lazima azivue khufu zake, aoshe miguu yake anapotawadha, kisha atakuwa na hali ile ile ya mkazi.
Na ikiwa msafiri amepukusa kwa muda wa chini ya siku na usiku wake, basi inajuzu kwake anapowasili mjini akamilishe muda uliosalia wa siku moja na usiku wake, kisha ni lazima azivue.
Ibn Al-Mundhir amenukulu Ijma’a ya kila Mwanachuoni anayezungumzia kwa kuainisha kuhusu muda wa kupukusa. [Al-Awsatw (1/446)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
041-Mlango Wa Twahara: Masharti Ya Kupukusa
Alhidaaya.com [3]
Ili kupukusa juu ya khufu mbili kuweze kujuzu, ni sharti mtu azivae akiwa twahara. Imepokelewa toka kwa Al-Mughyrah bin Shu’ubah amesema: “Nilikuwa na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika safari usiku mmoja. Nilimmiminia maji toka katika chombo, naye akaosha uso wake na mikono yake, na akapaka kichwa chake. Kisha niliinama mzima mzima ili nizivue khufu zake naye akanambia:
((دعهما، فإني أدخلتهما طاهرتين))
((Ziwache, kwani mimi nimezivaa nailhali miguu ni twahara)).
Kisha akapukusa juu yake. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (206) na Muslim (232)].
Hadiyth hii imeufanya utwahara kuwa ni sharti ya kujuzu kupukusa kabla ya kuzivaa khufu mbili. Na jambo lenye kufungamanishwa na sharti, halijuzu ila kwa kuwepo sharti hilo. Na wudhuu ndio utwahara wa kisharia uliochukuliwa na Jamhuri ya Maulamaa. [Fat-h Al-Baariy (1/370)].
Faida
Mwenye kutawadha, kisha akaosha mguu wake mmoja halafu akauvisha khufu, kisha akauosha mguu wake mwingine halafu akauvika khufu, basi wudhuu wake unapotenguka, haitojuzu kwake kupukusa kwa sababu alivaa khufu moja kabla ya kukamilisha wudhuu wake. Lakini kama aliivua ya kwanza kisha akaivaa, basi itajuzu kupukusa. Haya yamesemwa na Maalik, Ash-Shaafi’iy na Ahmad. [Al-Muwattwa (1/46), Al-Ummu (1/33) na Al-Mughniy (1/282)].
Ama Abu Haniyfah na Ahmad (katika moja ya riwaya mbili), Ibn Hazm, Ibn Al-Mundhir na Shaykh wa Uislamu, wao wanaona kwamba inajuzu kwake kupukusa juu ya khufu hizo kwa mazingatio ya ukweli kuwa alizivaa katika miguu yake yote miwili hali ya kuwa ni twahara. [Al-Mabsuwtw (1/99), Al-Awsatw (1/442), Majmu’u Al-Fataawaa (21/209) na Al-Muhalla (1/100)].
Ninasema:
“Kusema kuwa inajuzu, hakuna tatizo lolote mpaka itakapoonyesha dalili kwamba utwahara haugawanyiki, na hivyo kupelekea kwenye kuzuia. Na kwa kiakiba tu na tahadhari, ni vizuri kuingiza miguu miwili katika khufu baada ya kumaliza kutawadha. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
042-Je, Khufu Iliyotoboka Hupukuswa?
Alhidaaya.com [3]
Mafuqahaa wengi wameshurutisha kwamba ili kupukusa juu ya khufu mbili kujuzu, ni lazima ziwe ni zenye kusitiri mahala palipolazimu kuoshwa katika wudhuu. Kwa ajili hiyo, wamekataza kupukusa juu ya khufu iliyotoboka, kwani huonekana kupitia khufu hiyo, mahala pa viungo vinavyolazimu kuoshwa. Na kuosha na kupukusa havikutani pamoja, na kwa hivyo hukmu ya kuosha inapewa uzito zaidi.
Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy na Ahmad. [Al-Ummu (1/28), Masaail Ahmad cha Ibn Haani (1/18) na Al-Mughniy (1/287)].
Na Maalik na Abuu Haniyfah wamesema kuwa inajuzu kupukusa juu ya khufu iliyotoboka madhali inaweza kutembelewa na jina lake bado lipo. Na hivi ndivyo alivyosema Ath-Thawriy, Is-Haaq, Abu Thawr, Ibn Hazm, Ibn Al-Mundhir na Ibn Taymiyah. [Al-Mudawwanah (1/44), Al-Mabsuwtw (1/100), Al-Awsatw (1/449), Al-Muhalla (2/100) na Majmuu Al-Fataawaa (21/173)].
Haya ndiyo sahihi, kwani ruksa ya kupukusa juu ya khufu mbili ni ruksa jumuishi; kinaingia kila kiitwacho khufu kwa mujibu wa uhalisia ulivyo, na haiwezekani kuibagua khufu fulani ikaachwa nyingine ila kwa dalili. Na lau kama kutoboka kunazuia kupukusa, basi Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) angelibainisha hilo na hasa tukizingatia kwamba Maswahaba wengi walikuwa ni masikini katika enzi yake. Khufu za wengi wao zilikuwa hazikosi matobo.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
043-Mahala Pa Kupukusa Na Sifa Yake
Alhidaaya.com [3]
Linalo ruhusika kisharia, ni kuzipukusa khufu mara moja tu nje (juu) na sio ndani (chini ya unyayo). Hii ni kwa Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib aliyesema: “ Lau kama dini ingelikuwa ni kwa rai, basi kupukusa chini ya khufu ingelikuwa ni bora kuliko juu yake. Na hakika nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akipukusa juu ya khufu zake mbili”.[Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (162), Ad-Daara Qutwniy (73) na Al-Bayhaqiy (2/111). Tazama Al-Irwaa (103)].
Na haya ni madhehebu ya Ath-Thawriy, Al-Awzaa’iy, Ahmad, Abuu Haniyfay na wenzake. Na haya ndio sahihi. [Ikhtilaaf Al-‘Ulamaa (uk.30), Masaail Ahmad cha Ibn Haaniy (1/21), Al-Awsatw (1/453) na Al-Muhalla (2/111)].
Maalik na Ash-Shaafi’iy wamesema: “Hupukusa juu yake na chini yake. Na kama atapukusa juu tu, basi itamtosheleza. [Nihaayat Al-Muhtaaj (1/191), Al-Mudawwanah (1/39) na Al-Khurshiy (1/177)].
Hili limetolewa dalili kwa Hadiyth ya Al-Mughyrah bin Shu’ubah aliyesema kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitawadha, kisha akapukusa chini na juu ya khufu zake. [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (165), At Tirmidhy (97), Ibn Maajah (550) na Ahmad (4/251). Ahmad, Al-Bukhaary, Abuu Haatim, Ad-Daara Qutwniy na Ibn Hajar wamesema ina dosari].
Hii ni kauli dhwa’iyf, lakini lililo na uthibitisho toka kwa Al-Mughyrah ni kauli yake isemayo: “Nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akipukusa juu ya khufu zake mbili”.[Hadiyth Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (161), At Tirmidhy (98) na wengineo].
Hivyo basi, haifai kupukusa isipokuwa juu ya khufu mbili tu. Na kama atapukusa chini tu akaacha juu, basi kupukusa huko hakutatosheleza. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
044-Yanayotengua Kupukusa
Alhidaaya.com [3]
Imetangulia katika Hadiyth iliyoelezewa na Swafwan bin ‘Assal akisema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi waalihi wa sallam), alikuwa akituamuru tunapokuwa safarini, tusizivue khufu zetu siku tatu na masiku yake ila kwa janaba, lakini si kwa kwenda haja kubwa, au ndogo, au kulala”.
Kwa Hadiyth hii, imejulikana kuwa haifai kupukusa juu ya khufu mbili linapotokea moja kati ya mambo yafuatayo:
1- Janaba na mengineyo yenye kuwajibisha kuoga kama vile kujitwaharisha na hedhi au nifasi.
2- Kumalizika muda wa kupukusa.
3- Kuivua khufu na kupata hadathi kabla ya kuivaa.
Endapo ataivua khufu yake - ijapokuwa kabla ya kumalizika muda – kisha akapata hadathi, basi haitojuzu kuivaa na kupukusa, kwani anakuwa hakuivaa wakati huo akiwa na twahara.
Kwa hivyo, kama litatokea lolote kati ya mambo haya matatu, haitojuzu kupukusa juu ya khufu mbili, bali linalopasa kwake anapopata hadathi, ni kutawadha na kuosha miguu yake miwili, kisha anaweza kuzivaa khufu zake na kupukusa juu yake kama ilivyotangulia.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
045-Uzindushi: Kubatilika Upukusaji Hakumaanishi Kutenguka Wudhuu
Alhidaaya.com [3]
Mtu ambaye alikuwa anapukusa juu ya khufu zake mbili kisha akazivua bila ya kupata hadathi, Maulamaa wana kauli nne juu ya hukmu yake:
Ya kwanza:
Itampasa atawadhe upya. Haya ni madhehebu ya An-Nakh’iy, Al-Awzaa’iy, Ahmad, Is-haaq na Ash-Shaafi’iy katika madhehebu yake ya zamani. [Ikhtilaaful ‘Ulamaa (uk. 31), Masaail Ahmad cha Ibn Haaniy (1/19) na Al-Majmu’u (1/557)].
Wanasema kuwa sababu ya hilo ni kuwa kupukusa panachukua mahala pa kuosha. Na kwa ajili hiyo, anapokiondosha kinachopukuswa, basi utwahara katika miguu miwili hubatilika, na matokeo yake ni kubatilika katika viungo vyote kwa sababu havigawanyiki.
Ya pili:
Itampasa aoshe miguu yake basi. Haya ni madhehebu ya Ath-Thawriy, Abuu Haniyfah na wenzake na Abu Thawr. Pia ni kauli mpya ya Ash-Shaafi’iy. [Ikhtilaaful ‘Ulamaa (uk. 31), na Al-Awsatw (1/458)].
Ya tatu:
Ni lazima aoshe miguu yake miwili baada tu ya kuzivua khufu. Ikiwa atachelewa, basi atatawadha upya. Haya ni madhehebu ya Maalik na Al-Layth. [Al-Mudawwanah (1/41)].
Ya nne:
Hawajibiki kutawadha wala kuosha miguu. Hii ni riwaya iliyopokelewa toka kwa An-Nakh’iy. Haya haya yamesemwa na Al-Hasan Al-Baswriy, ‘Atwaa na Ibn Hazm. Aidha, yamekhitariwa na An-Nawawiy, Ibn Al-Mundhir na Ibn Taymiyah. [Al-Muhalla (1/105), Al-Awsatw (1/460), Al-Majmu’u (1/558) na Al-Ikhtiyaaraat (uk.15)].
Haya ndiyo madhehebu sahihi. Hii ni kwa vile, mtu huyu akiwa na khufu zake, kwa mujibu wa Hadiyth iliyothibiti, anakuwa na utwahara kamili. Na hilo haliwezi kutanguka anapozivua khufu zake isipokuwa kama kutapatikana dalili toka katika Hadiyth au Ijma’a. Na wanaosema kuwa itamlazimu kutawadha tena au kuosha miguu miwili, hao hawana hoja. Kauli hii inatiliwa nguvu na yale yaliyothibiti toka kwa Abu Dhwabyaan kwamba yeye alimwona ‘Aliy (Allaah Amridhie) akikojoa kwa kusimama, kisha akaomba aletewe maji, akatawadha na kupukusa juu ya viatu vyake. Halafu akaingia Msikitini, akavivua viatu vyake, kisha akaswali. [Isnad yake ni Swahiyh: Imetolewa na Al-Bayhaqiy (1/288) na At-Twahaawiy (1/58). Tazama Tamaam Al-Minnah (uk115)].
Kisha imefanyiwa kipimo kwa mtu aliyepaka maji kichwani kisha akazinyoa nywele. Bila shaka wao hawasemi kuwa itapasa kupaka maji tena kichwani au kutawadha tena!! Na hii ndiyo sawa hasa katika suala hili. Anapozivua khufu zake bila ya kupata hadathi, basi anaweza kuswali Swalaah zozote azitakazo mpaka pale wudhuu wake utakapotenguka. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
046-Kupaka Juu Ya Soksi Na Viatu
Alhidaaya.com [3]
1- Kupaka Juu Ya Soksi
Soksi ni kile anachokivaa mtu miguuni sawasawa zikiwa zimetengenezwa kwa sufi au pamba au katani au mfano wa hivyo.
Maulamaa wana kauli tatu kuhusu hukmu ya kupukusa juu ya soksi:
Ya kwanza:
Haijuzu kupukusa juu yake ila tu kama zitafunikwa na viatu vya ngozi.
Haya ni madhehebu ya Abuu Haniyfah (ambaye baadaye aliachana na msimamo huu), Maalik na Ash-Shaafi'iy. [Al-Mabsuwtw (1/102), Al-Mudawwanah (1/40), Al-Ummu (1/33) na Al-Awsatw (1/465)].
Wao wanasema kuwa sababu ni kuwa soksi haiitwi khufu, na kwa hivyo haichukui hukmu yake, na wala hakuna Hadiyth yoyote inayothibitisha kupukusa juu ya soksi!!
Ya pili:
Inajuzu kupukusa juu ya soksi lakini kwa sharti ziwe nzito na zenye kusitiri mahala penye kulazimu kuoshwa.
Haya ni madhehebu ya Al-Hasan, Ibn Al-Musayyib na Ahmad. Pia Mafuqahaa wa Hanafi, Shaafi'iy na Hanbali. [Masaail Ahmad ya Ibn Haaniy (1/21), Al-Awsatw (1/464), Al-Majmu'u (1/540) na Fat-h Al-Qadiyr (1/157)].
Ya tatu:
Inajuzu kupukusa kwa hali yoyote hata kama ni nyepesi.
Ni madhehebu ya Ibn Hazm na Ibn Taymiyah kama inavyojulikana. Kauli hii pia imekhitariwa na Ibn 'Uthaymiyn na Al-'Allaamah Ash-Shanqiytwiy nayo ndiyo yenye nguvu. [Al-Muhalla (2/86), Al-Masaail Al-Maardiyniya (uk.58), Majmuu Al-Fataawaa (21/184), Al-Mumt'i (1/190) na Adhwaau Al-Bayaan (2/18,19) ambayo ina utafiti murua kabisa].
Maulamaa wenye kauli mbili za mwisho wamejuzisha kupukusa juu ya soksi kwa dalili zifuatazo:
1- Ni Hadiyth ya Al-Mughiyrah bin Shu'ubah aliyesema kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitawadha, akapukusa juu ya soksi zake na viatu vyake. [Al-Albaaniy amesema ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (159), At-Tirmidhiy (99) na Ahmad (4/252), naye ndiye mzungumzaji. Angalia katika Al-Irwaa (101)].
2- Imepokelewa toka kwa Al-Azraq bin Qays akisema: "Nilimwona Anas bin Maalik ametengukwa na wudhuu, akaosha uso wake, mikono yake miwili na akapukusa juu ya soksi zake za sufi. Nikamuuliza: Je, wapukusa juu yake? Akasema: Hakika hizi ni khufu mbili, lakini ni za sufi". [Ahmad Shaakir amesema kuwa ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ad-Duwlaabiy katika Al-Kunaa (1/181)].
Anas Allaah Amridhie akaeleza hapa kuwa khufu si lazima iwe ni ya ngozi tu, bali ni zaidi ya hivyo, naye ni Swahaba anayeijua vyema lugha.
3- Ni kwamba kuna Maswahaba 11 waliozungumzia kuhusu kujuzu kupukusa juu ya soksi mbili. Kati yao ni 'Umar na mwanawe ‘Abdullaah, 'Aliy, Ibn Mas'uud, Anas na wengineo. Na hakuna yeyote katika enzi yao aliyekwenda kinyume, na hilo likawa limekubaliwa na wote.
Kisha Jamhuri ya Maulamaa ikaja kupiga marufuku kupukusa juu ya soksi nyepesi kwa vile hazisitiri mahala panapolazimu kuoshwa. Tumekwisha eleza nyuma kuwa hili si sharti – kwa mujibu wa utafiti – kwa kuchukulia kipimo cha khufu iliyotoboka. Na kwa vile siku hizi zinazovaliwa zaidi ni soksi nyepesi, tutaona kwamba kushurutisha mfano wa masharti kama haya, kunakwenda kinyume na makusudio ya sharia iliyotufanyia ukunjufu kwa kuwabana watu na kuwatia uzito. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Faida
Inaingia katika maana ya soksi bendeji, plasta na matambara anayofungwa mtu mguuni kwa udhuru, kwani hizo ni vigumu kuzifungua. Yeye atapaka tu juu yake kama alivyolikhitari hilo Shaykh wa Uislamu.
Na hukmu za kupukusa juu ya soksi mbili ni hukmu zile zile za kupukusa juu ya khufu mbili.
Anapovaa Soksi Juu Ya Nyingine
Hili lina hali mbalimbali:
1- Akitawadha kisha akavaa soksi juu ya nyingine (mbili), basi atapukusa soksi ya juu tu endapo kama atatengukwa na wudhuu.
Na haya ni madhehebu ya Hanafiy. Na ni kauli yenye nguvu kwa Maalik na Hanbali. Aidha ni kauli ya zamani ya Ash-Shaafi'iy aliyetofautiana nao katika kauli yake mpya. [Haashiyat Ibn 'Aabidiyn (1/179), Jawaahir Al-Ikliyl (1/24) na Rawdhat At-Twaalibiyn (1/127). Mengi wameyazungumzia hapa kuhusu khufu, lakini hukmu ni moja].
2- Akitawadha akavaa soksi juu ya nyingine, kisha akapukusa juu yake, halafu akaivua ya juu baada ya kupukusa, basi inajuzu kwake kuukamilisha muda kwa kuzipukusa soksi za ndani, kwa kuwa cha msingi hapa ni kuwa yeye alizivaa miguu yake ikiwa twahara.
3- Akitawadha akavaa soksi, kisha akaivaa nyingine juu yake kabla ya kutengukwa na wudhuu, basi atapukusa juu ya soksi zozote azitakazo (za ndani au za nje. [Mahanbali wamelielezea hili katika Kash-Shaaf Al-Qina'a (1/117-118)].
4- Akitawadha akaivaa soksi moja, akapukusa juu yake kisha akaivaa nyingine hali ya kuwa ana twahara, itajuzu kwake kupukusa ya juu, kwa vile kimsingi ameiingiza miguu yake ikiwa ni twahara. Na kama alitengukwa na wudhuu kisha akaivaa nyingine, haitojuzu kwake kupukusa ya juu, bali itajuzu ya chini. [Imeelezwa katika Kash-Shaaf Al-Qina'a (1/117-118) kwamba hapukusi. Amesema: "Kwa vile khufu iliyopukuswa ni badala ya kuosha ile iliyo chini yake. Na badali haijuzu kuwa na badali nyingine, bali atapukusa ya chini kwa vile ruhusa imefungamana nayo!!].
2- Kupaka Juu Ya Viatu
Imetangulia katika Hadiyth ya Al-Mughiyrah bin Shu'ubah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitawadha, akapukusa juu ya soksi zake na viatu vyake. [Tumeitaja nyuma kidogo]
Hadiyth hii tukisema kuwa ni Swahiyh, inaweza kubeba mambo mawili:
1- Ni kuwa alivaa viatu na soksi na akapukusa juu yake, na hukmu ya viwili hivyo ni moja kama ilivyotangulia katika kuvaa soksi juu ya soksi au khufu juu ya khufu.
2- Ni kuwa Al-Mughiyrah alimwona Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akipukusa mara juu ya soksi na mara nyingine juu ya viatu. Na hii inakuwa ni dalili kuwa inajuzu kupukusa juu ya viatu ijapokuwa bila ya soksi. Na hili ingawa liko mbali kidogo, lakini linaweza kutolewa dalili juu ya kujuzu hilo kutokana na yaliyotangulia katika Hadiyth ya Abuu Dhwabyaan kwamba "Aliy bin Abi Twaalib alitawadha, akapukusa juu ya viatu vyake, kisha akaingia Msikitini, akavua viatu vyake, kisha akaswali…" Na hapa hakutaja soksi. [Tumeitaja nyuma kidogo]
Na pengine kujuzu kupukusa juu ya viatu kunatilika nguvu vile vile kwa kutoshurutishwa kuwa chenye kupukuswa kiwe ni chenye kusitiri mahala pa lazima kuoshwa. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
047-Tatu: Kupaka Juu Ya Kinachofunika Kichwa
Alhidaaya.com [3]
1- Kupaka Juu Ya Kilemba Katika Wudhuu
Inajuzu kupukusa juu ya kilemba – badala ya kupukusa kichwa – wakati wa kutawadha kwa hali yoyote. Na haya ni madhehebu ya Ahmad, Is-haaq, Abu Thawr, Al-Awzaa'iy, Ibn Hazm na Ibn Taymiyah. Nayo ni kauli ya Abu Bakr, 'Umar, Anas na Maswahaba wengineo (Radhwiya Allaahu ‘anhum). [Masaail Abuu Daawuud (8), Al-Mughniy (1/300), Al-Majuu'u (1/406), Al-Awsatw (1/468), Al-Muhalla (2/58) na Majmu'u Al-Fataawaa (21/184)].
Na bila shaka, hilo limethibiti toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
Imepokelewa toka kwa 'Amri bin Umayyah Adh-Dhumariy akisema: "Nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akipukusa juu ya khufu mbili na kilemba". [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaji” na Al-Bukhaariy (205)].
Kauli kama hiyo hiyo imepokelewa toka kwa Al-Mughiyrah bin Shu'ubah. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaji” na Al-Muslim (275)].
Pia imepokelewa toka kwa Bilaal akisema: "Nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akipukusa juu ya khufu mbili na khimaar”.[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaji” na Muslim (285)].
Khimaar hapa ni kile chenye kufunika kichwa, na makusudio ni kilemba.
Na kwa upande mwingine, Abuu Haniyfah na wenziwe, Maalik na Ash-Shaafi'iy, wameelekea kwingine wakisema kuwa mwenye kutawadha hapukusi juu ya kilemba tu, bali hupukusa juu yake pamoja na utosi, na utosi unakuwa ni fardhi na kilemba ni Sunnah (ziada) kwa kujengea juu ya kujuzisha kwao kupaka sehemu tu ya kichwa!! [Haashiyat Ibn 'Aabidiyn (1/181), Haashiyat Ad-Dusuwqiy (1/164) na Al-Majmu'u (1/407)].
Lakini pamoja na hivyo, Ash-Shaafi'iy anasema: “Ikiwa Hadiyth ya kupukusa juu ya kilemba ni Swahiyh, basi hiyo ndiyo kauli yangu”. Na bila shaka yoyote Hadiyth hiyo ni Swahiyh, kwa hiyo ndiyo kauli yake.
Wenye kupinga kupukusa juu ya kilemba wametoa hoja kwa Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillaah aliyesema: "Nilimwona Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akikivuta nyuma kilemba chake na akapukusa juu ya utosi wake". [Sikuipata na wala haipo katika kitabu chochote kati ya vitabu vya Hadiyth nilivyonavyo. Na Ibn Al-Mundhir ameitaja bila ya Isnaad (1/469)].
Sijaipata Sanad yoyote ya Hadiyth hii!!
Na kwa Hadiyth ya Al-Mughiyrah akisema kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipukusa juu ya kilemba chake, na juu ya utosi na khufu zake mbili". [Hadiyth Swahiyh: Imetajwa katika mlango wa wudhuu].
Ninasema: "Kauli yenye nguvu ni kuwa inajuzu kwa hali yoyote kupukusa juu ya kilemba kwa kuthibiti kuelezewa hilo toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na kwa kufanywa hilo na Makhalifa wawili waliokuja baada yake, na kukosa uzito hoja iliyotolewa na wenye kulipinga hilo. [Angalia hoja zao na zilivyojibiwa katika "Al-Muhalla" (2/61)]. Lakini pamoja na hivyo, ni bora kupukusa sehemu ya utosi pamoja na kilemba ili kuepuka mahitilafiano. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
2- Kupukusa Mwanamke Juu Ya Ushungi / Mtandio
Shaykh wa Uislam anasema: "Ikiwa mwanamke atahofia baridi au mfano wa baridi, basi atapukusa juu ya ushungi wake, kwani Ummu Salamah alikuwa akipukusa juu ya ushungi wake. Lakini akipukusa ushungi, anatakiwa apukuse baadhi ya nywele zake. Na ikiwa hakuhitajia hilo, basi hapa kuna mvutano baina ya Maulamaa.” [Majmu'u Al-Fataawaa (21/218)].
Ninasema: "Katika riwaya, [Al-Mudawwanah (1/42), Al-Ummu (1/26), Al-Badaai-'i (1/5) na Al-Mughniy (1/305)]…..Hanafiy, Maalik, Ash-Shaafi'iy na Hanbali, wameelekea mwelekeo wa kusema kuwa haijuzu kutokana na yale yaliyopokelewa toka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) kwamba yeye aliingiza mkono wake chini ya ushungi wake na akapukusa kichwa chake, akasema: "Hivi ndivyo alivyoniamuru Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)". [Sijapata kuiona bali ameitaja Al-Kaasaaniy katika Al-Badaai-'i (1/5), nami sijaiona katika kitabu chochote cha Hadiyth!!]
Wamesema: "Na kwa vile hicho ni kivazi cha kichwani kwa mwanamke na hakuna uzito katika kukiondosha, haijuzu kupukusa juu yake."
Al-Hasan Al-Baswriy amechukua msimamo wa kuwa inajuzu kupukusa juu ya ushungi. Hayo hayo wameyasema Mahanbal, - lakini wameshurutisha kuwa ni lazima mitandio au shungi ziwe zimezungushiwa chini ya koo!! – kwa kuchukulia kipimo cha kilemba, kwani khimaar kikawaida huvaliwa kichwani.
Ninasema: “Ingelikuwa Hadiyth ya 'Aaishah ni Swahiyh, basi ingelimaliza mjadala katika kuzuia kupukusa juu ya ushungi. Na kama si hivyo, basi kipimo kitachukuliwa juu ya kilemba. Na ili kuondosha wasiwasi, ni vyema mwanamke apukuse juu ya ushungi wake pamoja ncha ya utosi wake. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.”
3- Kupukusa Juu Ya Kofia Katika Wudhuu
Jamhuri ya Maulamaa imeshikilia mwelekeo wa kuwa haijuzu wakati wa kutawadha kupukusa juu ya kofia badala ya kichwa, kwani fardhi ni kupukusa kichwa. Lakini hilo limeachiliwa katika kilemba kutokana na uzito wa kukivua kwa Jamhuri ya Maulamaa, au kwa matni ya Ahmad.
Ibn Hazm, Ibn Taymiyah na watafiti kati ya wadau wa taaluma hii, wameshikilia mwelekeo wa kujuzu kupukusa juu ya kofia.
[Al-Muhalla (2/58) na Majmu'u Al-Fataawaa (21/ 184-187, 214)].
Hii ni kwa vile, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipopukusa juu ya kilemba, sisi tumejua kwa hilo kuwa si fardhi kugusanisha maji na kichwa, bali inajuzu kupukusa juu ya kitu chochote kilichovaliwa kichwani hata kama hakisitiri mahala pa lazima kuoshwa na wala haikuwa ni uzito kukivua. Na hili ndilo sawa, na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Faida
- Si Sharti Kuwa Na Twahara Wakati Wa Kuvaa Chenye Kufunika Kichwa Ili Ijuzu Kupukusa Juu Yake.
Hili halipimiwi na kupukusa juu ya khufu mbili, kwa vile hakuna sababu ya kuvikutanisha viwili hivyo, bali Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameelezea ulazima wa twahara wakati wa kuvaa khufu mbili na wala hakulielezea hilo kwa upande wa kilemba na ushungi. Na lau kama ingelikuwa ni lazima, basi angelibainisha. [Al-Muhalla (2/64)]
Ninasema: “Hii ni kwa vile, khufu mbili ni badala ya kilicho fardhi kukiosha. Ama kichwa, fardhi yake ni kupukusa, na kilicho juu ya kichwa, huchukua hukmu yake. Kwa hiyo vimekuwa ni vitu viwili tofauti. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
- Hakuna Wakati Wala Muda Maalumu Wa Kupukusa Juu Ya Chenye Kufunika Kichwa
Ni kwa kutofaa kipimo cha kupukusa juu ya khufu mbili. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipukusa juu ya kilemba na khimaar na wala hakulipangia hilo wakati. Na hili limepokelewa toka kwa 'Umar bin Al-Khattwaab (Allah Amridhie). [Al-Muhalla (2/65)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
048-Nne: Kupaka Juu Ya “Al Jabiyrah”
Alhidaaya.com [3]
"Al Jabiyrah" ni majiti mawili ambayo huungiwa kwayo mifupa iliyovunjika ili ishikamane. Na katika maisha yetu ya leo, plasta ya jasi (piopi) hutumiwa badala yake.
Na mtu ambaye katika kiungo chake kimoja cha wudhuu kutakuwa na "jabiyrah" (piopi) kama mikono miwili au miguu miwili, basi inajuzu kwake kupukusa kwa mujibu wa rai ya Jamhuri ya Maulamaa wakiwemo Maimamu wanne na wengineo. [Sharh Fat-h Al-Qadiyr (1/140), Al-Mudawwanah (1/23), Al-Mughniy (1/203) na Al-Majmu'u (2/327)].
Wao wametolea dalili yafuatayo:
1- Hadiyth ya Jaabir kwa yule aliyepatwa na mpasuko usoni, na kauli ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((Hakika inamtosheleza tu kufunga jeraha lake kwa kitambaa, kisha akapukusa juu yake)). Na hii ni Hadiyth Dhwa’iyf. [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (236) na wengineo. Angalia Al-Irwaa (105)].
2- Ni kauli ya Ibn 'Umar: "Mwenye jeraha lililofungwa, atatawadha na atapukusa juu ya bendeji, na ataosha pembezoni mwa bendeji".[Isnadi yake ni Swahiyh: Imekharijiwa na Ibn Abi Shaybah (1/126) na Al-Bayhaqiy (1/228)].
Na hajulikani Swahaba yeyote aliyekwenda kinyume na Ibn 'Umar.
3- Ni kuchukulia kipimo cha kupukusa juu ya khufu mbili, kwani kupukusa juu ya khufu mbili kunajuzu bila ya dharura, basi vipi kwa upande wa "jabiyrah" (piopi) ambayo ni dharura? Hivyo inachukua uzito zaidi.
Na Ibn Hazm ameshikilia msimamo wa kuwa mwenye kufungwa "jabiyrah", basi halazimiki kupukusa juu yake na kwamba hukmu ya mahali hapo inaondoka. [Al-Muhallaa (2/74)].
Ninasema: "Hii ni kwa vile Ibn Hazm amezichukulia Hadiyth za kupukusa juu ya bendeji, plasta n.k kuwa ni Dhwa’iyf na wala haoni Qiyaas kuwa ni hujjah!! Na Hadiyth hizi hazifai kama alivyosema. Ama Qiyaas, bila shaka itakuwa ni hujjah endapo kama nguzo na sharti zake zitakuwepo. Lakini inaweza kusemwa kuwa Qiyaas hapa hakifai kutokana na kutofautiana tanzu na asili. Ni Qiyaas waajib (kupukusa juu ya piopii kwa Jamhuri ya Maulamaa) juu ya mubaah (kupukusa juu ya khufu mbili). Na hapa basi, madhehebu ya Ibn Hazm yanang'aa. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Faida
1- Kupukusa juu ya "jabiyrah" (piopi) kunatosheleza, sawasawa katika wudhuu au katika kuoga, kwa vile "jabiyrah" (piopi) ni jambo lisilo na budi, na kwa hivyo hakuna tofauti ndani yake kati ya hadathi ndogo na hadathi kubwa. Ni kinyume na kupukusa juu ya khufu mbili, kwani hili limeruhusiwa (kwa atakaye).
2- Si lazima kufungwa "jabiyrah" wakati mtu ana twahara wala hakuna muda maalumu wa kupukusa juu yake.
Hii ni kwa vile, hilo linakwenda kinyume na makusudio ya sharia katika kuruhusu kupukusa kati ya kuondosha uzito na tabu. Aidha, kufungwa (piopi) ni hali ya kulazimika ambayo huja ghafla bila kutegemewa kinyume na khufu mbili. Mbali ya hivyo, hakuna matni au Ijma’a.
Hivyo basi, hakuna muda maalumu wa kupukusa juu ya "al-Jabiyrah". Lakini wakati wowote atakapoliondosha au kiungo kikapona, basi haitojuzu kupukusa.
3- Bendeji na plasta za kitiba (hospitali) zilizofungwa katika kiungo cha wudhuu, zina hukmu ya "al-Jabiyrah" (piopi) kama lilivyohakikiwa hilo na Shaykh wa Uislamu. [Majmuu Al-Fataawaa (21/185)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
049-Kuoga
Alhidaaya.com [3]
Kilugha maana yake ni kuchuruzika maji juu ya kitu. Ama kisharia, ni kumiminisha maji yaliyo twahara katika mwili wote kwa njia maalumu. [Kash-Shaaf Al-Qinai (1/158)].
Yenye Kupasisha Kuoga
1- Ni kutokwa na manii mtu akiwa macho au usingizini
Ni kwa Neno Lake (Subhaanahu wa Ta’aalaa):
((وإن كنتم جنبا فاطهروا))
((Na mkiwa na janaba, basi ogeni)). [Al-Maaidah (5:6)].
Na Neno Lake (Subhaanahu wa Ta’aalaa):
(( يا أ يها الذين لا تقربوا الصلاة وأنتم سكارى حتى تعلموا ما تقولون ولا جنبا إلا عابري سبيل حتى تغتسلوا))
((Enyi walioamini! Msikaribie Swalaah hali mmelewa, mpaka muyajue mnayoyasema, wala hali mna janaba – isipokuwa mmo safarini – mpaka mkoge)). [An-Nisaa (4:43)].
Na imepokelewa toka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba amesema:
(( إنما الماء من الماء))
((Hakika maji ni kutokana na maji)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (343) na Abuu Daawuud (214)].
Yaani kuoga (kwa maji), sababu yake ni kumwaga (maji), nayo ni manii.
Na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia 'Aliy:
((إذا فضخت الماء فاغتسل))
((Ukimwaga maji, basi oga)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (206), An Nasaaiy (193) na Ahmad (1/247). Asili yake ni kutoka Swahiyh Mbili.
Na katika tamko jingine:
((إذا حذفت))
((Utakapokatia))
Na hayawi kwa sifa hii ila yanapotoka kwa matamanio kama Alivyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):
((خلق من ماء دافق))
((Ameumbwa kutokana na maji yenye kuchupa)). [At Twaariq (86:6)].
Na imepokelewa toka kwa Ummu Salamah (Allaah Amridhie) akisema:
"Alikuja Ummu Sulaym, naye ni mke wa Abu Twalha, kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika Allaah Haonei haki hayaa. Je, inampasa mwanamke kuoga kama ameota? Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:
((نعم، إذا رأت الماء))
((Naam, kama akiyaona maji)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (282) na Muslim (313)].
Kauli hii inafahamisha kuwa si lazima manii yatoke kwa matamanio na kuchupa wakati wa kuota ndipo ipase kuoga, bali itambidi kuoga anapoyaona manii katika nguo yake. Na kama hakuyaona, basi hapaswi kuoga hata kama atakumbuka kuwa aliota. Hii ni kutokana na Hadiyth ya Mama wa Waumini 'Aaishah (Allaah Amridhie) aliyesema:
"Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu mtu anayekuta ubichi ubichi na wala hakumbuki kama aliota. Akasema:
((يغتسل))
((Ataoga))
Na kuhusu mtu anayeona kwamba aliota lakini hakukuta ubichi bichi, akasema:
((لا غسل عليه))
((Hapaswi kuoga)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhy (113) na Abuu Daawuud (233)].
Zindushi Mbili
(a) Katika yote yaliyotangulia, mwanamke ni kama mwanamume, sawa kwa sawa.
(b) Yeyote mwenye kuchuruzikwa na manii bila ya matamanio kutokana na ugonjwa, au baridi au mfano wa hayo, basi hana lazima kuoga kwa mujibu wa kauli mbili zilizo sahihi zaidi za Maulamaa. Na haya ndiyo madhehebu ya Jamhuri kinyume na Ash-Shaafi'iy na Ibn Hazm.
Na Maulamaa kwa sauti moja wamesema kuwa ni lazima kuoga mtu anapotokwa na manii kwa matamanio wakati yu macho, na anapotokwa na manii akiota usingizini. [Al-Majmuu (1/139), Bidaayat Al-Mujtahid (1/58) na As-Sayl Al-Jarraar (1/104)].
Isipokuwa yale yaliyopokelewa toka kwa Ibraahiym An-Nakh'iy kwamba yeye alikuwa haoni kuwa inampasa mwanamke kuoga anapoota na kujimwagia.
2- Kukutana tupu mbili ijapokuwa bila ya kumwaga manii
Kinapozama kichwa cha dhakari ya mwanamume katika utupu wa mwanamke, basi inawalazimu wote wawili kuoga ni sawa ikiwa wamemwaga manii au hawakumwaga. Hii ni kutokana na Hadiyth ya Abu Hurayrah aliyoipokea toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
(( إذا جلس بين شعبها الأربع، ثم جهدها فقد وجب الغسل)) (وإن لم ينزل))
((Anapokaa kati ya tanzu zake nne, kisha akamtoa jasho, basi ni lazima kuoga)) ((hata kama hakumwaga)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (291) na Muslim (348) na ziada ni yake yeye].
Na imepokelewa toka kwa Mama wa Waumini 'Aaishah (Allaah Amridhie) kwamba mtu mmoja alimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu mtu anayemwingilia mkewe kisha akaishiliwa nguvu, je, ni lazima waoge? – nailhali Mama wa Waumini 'Aaishah yuko hapo amekaa - Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia:
(( إني لأفعل ذلك أنا وهذه ثم نغتسل ))
((Hakika mimi nafanya hilo na huyu, kisha tunaoga)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (350)]
Amesema An-Nawawiy: "Na hili halina mvutano hivi leo. Lilikuwa na mvutano kwa baadhi ya Maswahaba na waliokuja baada yao. Kisha ikafungika Ijma’a’ juu ya tuliyoyataja."
Ninasema: “Ama hitilafu ya Maswahaba katika suala hili, miongoni mwake ni Hadiyth ya Zayd bin Khaalid ambapo yeye alimuuliza 'Uthmaan bin 'Affaan akimwambia: "Unasemaje endapo mtu atamwingilia mkewe na wala hakumwaga manii"? 'Uthmaan akamwambia: "Atatawadha kama anavyotawadha kwa ajili ya Swalaah na ataosha dhakari yake". Akasema 'Uthmaan: "Nimelisikia hilo toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na nikaliulizia hilo kwa ‘Aliy bin Abi Twaalib, Az-Zubayr bin Al-'Awwaam, Twalha bin 'Ubayd Allaah na Ubay bin Ka'ab, nao wakamwamuru hilo". [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (292) na Muslim (347)].
Daawuud Adh-Dhwaahiriy ameelekea msimamo wa kutolazimu kuoga kama mtu hakumwaga kwa Hadiyth:
((Hakika maji ni kutokana na maji)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (348). Imeshatajwa nyuma.]
Na Hadiyth ya Abu Sa'iyd kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia mtu fulani:
(( إذا أعجلت ـ أو قطحت – فعليك الوضوء))
((Ukiingilia bila kumwaga, basi yakupasa kutawadha)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (180) na Muslim (345)].
Ama Maswahaba hawa, bila shaka imethibiti kutoka kwao kuwa waliachana na kauli ya kutokupasa kuoga. [Angalia athar kutoka kwao katika kitabu cha Jaami'u Ahkaamin Nisaa cha Shaykh wetu (Allaah Amhifadhi) (1/89,90)].
Ama kauli ya Daawuud, bila shaka imekwenda kinyume na Jamhuri ya Maswahaba wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Mafuqahaa wa Taabi-'iyna na waliokuja baada yao. Hawa wanaona kwamba Hadiyth ya ((Maji ni kutokana na maji)) na yaliyo katika maana yake, ilikuwa ni mwanzoni mwa Uislamu kisha ikanasikhiwa.
At-Tirmidhiy amesema (1/185):
"Na hivi ndivyo alivyopokea zaidi ya mtu mmoja katika Maswahaba wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akiwemo Ubay bin Ka'ab na Raafi'i bin Khudayj. [Hadiyth ya Ubayya ni Swahiyh kwa njia zake kama alivyoibainisha Shaykh wetu Abu ‘Umayr Al-Athariy- Allaah Amstareheshe katika maisha yake- katika Shifaau Al'ayyi Bitahqiyq Musnad Ash-Shaafi'iy (100)].
Na hili ndilo linalofanywa na Maulamaa wengi zaidi kuwa mtu anapomwingilia mkewe katika tupu, inawabidi wote wawili kuoga hata kama hajamwaga manii”.
Faida [Zimetolewa toka kwenye kitabu changu cha Fiqhu As Sunnah Lin Nisaa (uk 46)].
1- Dhakari ya mwanamume ikigusa uchi wa mwanamke bila kuingizwa ndani, basi haiwapasi kuoga kwa makubaliano ya Maulamaa. [Al-Mughniy cha Ibn Qudaamah (1/204)].
Ibraahiym An-Nakh'iy aliulizwa kuhusu mtu anayemwingilia mkewe sehemu isiyokuwa tupu (farji) kisha akamwaga. Alijibu akisema:
"Atakoga yeye, lakini mkewe hakogi bali ataosha sehemu iliyochafuka". [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na ‘Abdu Rrazzaaq (971). Angalia athar mfano wake kutoka baadhi ya watangu wema katika Jaami Ahkaam An-Nisaa (1/95)].
2- Mtu akimwingilia mkewe, akaingiza sehemu ndogo tu ya kichwa cha dhakari, kisha manii yake yakaingia katika utupu wa mkewe, na mkewe hakumwaga, basi haimpasi mke kuoga.
Amesema An-Nawawiy: "Anapoingiziwa mwanamke manii katika utupu wake wa mbele au wa nyuma kisha manii hayo yakatoka, basi hapaswi kuoga. Hili ndilo sahihi lililopitishwa na Jamhuri." [Al-Majmu’u (2/151). Tazama Al-Muhalla (2/7)].
3- Mtu anapomwingilia mkewe kisha mkewe akakoga, halafu baadaye yakamtoka manii ya mumewe toka kwenye utupu wake, basi hapaswi kuoga tena. Lakini je, itamlazimu kutawadha?
Kwa mujibu wa kauli ya Jamhuri, itamlazimu kutawadha kwa vile maji hayo yametoka kupitia moja ya njia mbili ingawa ni twahara. [Al-Majmu’u (2/151)
Ibn Hazm amesema:
"Wudhuu utampasa kutokana na hadathi yake yeye na wala si kutokana na hadathi ya mwingine. Na kutoka manii ya mumewe toka kwenye utupu wake hakuzingatiwi kuwa yeye ndiye anayemwaga, wala haizingatiwi kuwa ni hadathi yake yeye. Kwa hivyo, hakogi wala hatawadhi." [Al-Majmu’u (2/151).
Ninasema: “Ama kaida ya kutawadha kwa kila chenye kutoka katika moja ya njia mbili, kaida hii haikubaliki kama ilivyotangulia, kwani mapitio ya manii kwa mwanamke, siyo mapitio ya mkojo. Hivyo basi madhehebu ya Ibn Hazm yanakuwa na nguvu zaidi. Lakini pamoja na hivyo, pachukuliwe tahadhari kuwa manii haya yanaweza kuchanganyika na madhii ya mwanamke. Hivyo la akiba zaidi atawadhe, na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
4- Mume akimwingilia mkewe mdogo ambaye bado hajaanza kuingia hedhini, au mtoto mdogo ambaye hajabaleghe akamwingilia mwanamke, basi inamlazimu mwanamke kuoga vile vile kama alivyosema Imam Ahmad:
"Hebu nielezeni! Je, 'Aaishah, Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa akimwingilia, alikuwa hakogi?! [Al-Mughniy (1/206)].
5- Mume anapomtaka mkewe kufanya mapenzi, basi haitakikani kumkatalia hilo kwa kisingizio cha kutokuwepo maji ya kukogea.
Shaykh wa Uislamu katika "Al-Fataawaa" 21/454" anasema:
"Haitakikani kwa mwanamke kumkatalia mumewe tendo la ndoa. Amwachie amwingilie. Na ikiwa ataweza kuoga, basi akoge, na kama hakuweza, atatayammamu na kuswali".
3, 4 – Hedhi na nifasi
Mambo haya mawili ni sababu mbili zenye kuwajibisha kukoga. Na kwa vile kukoga kunatokana na sababu ambapo hakufanyiki ila baada ya kukatika kwake na kumalizana nayo, inabidi kukoga baada ya kukatika hedhi na nifasi.
Imepokelewa na Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Faatwimah binti Abi Hubaysh:
((إذا أقبلت الحيضة فدعي الصلاة، وإذا أدبرت فاغتسلي وصلي))
((Hedhi ikija basi acha Swalaah, na ikiondoka basi oga na uswali)). [Hadiyth Swahiyh: Takhriyj yake itakuja katika mlango wa hedhi].
Na nifasi ni kama hedhi kwa Ijma’a. Kisha imethibiti toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akiielezea nifasi kama hedhi na hedhi kama nifasi.
Hukmu za hedhi na nifasi zitakuja kuelezewa kwa uchambuzi InshaAllaah.
5- Kafiri anaposilimu
Maulamaa wana kauli tatu kwa upande wa hukmu ya kuoga wakati kafiri anaposilimu:
Kwanza:
Ni lazima aoge kwa hali yoyote. Haya ni madhehebu ya Maalik, Ahmad, Abu Thawr na Ibn Hazm. Pia Ibn Al-Mundhir na Al-Khattwaabiy wamelikhitari. [Mawaahib Al-Jaliyl (1/311), Al-Mughniy (1/152), Al-Majmu’u, (2/175) na Al-Muhalla (2/4)].
Dalili zao ni:
1- Hadiyth ya Qays bin ‘Aaswim aliyesema kwamba aliposilimu, Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwamuru akoge kwa maji na mkunazi. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (355), At-Tirmidhiy (605) na An-Nasaaiy (1/109). Tazama “Al-Mishkaat” (543)]. Na asili ya amri hii ni ulazima.
2- Ni yale yaliyomo katika Hadiyth ya Abu Hurayrah katika kusilimu Thumaamah bin Uthaal kutokana na kauli ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((Nendeni naye hadi katika bustani ya Bani fulani, kisha mwamrisheni akoge)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad (2/304) na Ibn Khuzaymah (252). Na asili yake ni kutoka Swahiyh Mbili, lakini hakuna amri ya kuoga. Angalia vilevile Al-Irwaa (128)].
3- Kisa cha kusilimu Usayd bin Hudhayr. Kisa hiki kinaeleza kwamba Usayd aliwauliza Mus’ab bin ‘Umayr na As’ad bin Zuraarah: “Mnafanya vipi mkitaka kuingia katika Dini hii?” Wakajibu: “Unaoga unatwaharika, halafu unazitwaharisha nguo zako mbili, kisha unashuhudia shahada ya haki, halafu unaswali…” Hadiyth. [Isnadi yake ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Twabary katika kitabu cha At Taariykh (1/ 560), na Ibn Hishaam katika As Siyrah (2/285)].
Pili:
Inapendeza (imesuniwa) kafiri akoge, isipokuwa tu kama alikuwa na janaba kabla ya kusilimu, hapo italazimu akoge. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy na Abu Haniyfah. [Al-Majmu’u (1/174), Al-Ummu (1/38) na Ibn ‘Aaabidyn (1/167)].
Tatu:
Si lazima kukoga kwa hali yoyote. Ni madhehebu ya Abu Haniyfah. [Al-Mabsuwtw na Sharh Fat-h Al-Qadiyr (1/59)].
Hawa wametoa dalili zao katika haya yafuatayo:
1. Neno Lake Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
(( قل للذين كفروا إن ينتهوا يغفر لهم ما قد سلف ))
((Waambie waliokufuru, ikiwa wataacha (ukafiri), watasamehewa yaliyopita)). [Al-Anfaal (8:38)]
2. Hadiyth ya ‘Amru bin Al-‘Aasw ikiwa Marfu’u:
((Uislamu unapomosha yaliyopita)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (121) kutoka kwa Hadiyth ya ‘Amri bin Al ‘Aasiy].
Katika kutolea ushahidi wa Aayah na Hadiyth, kuna mlahadha. Ni kuwa yanayokusudiwa katika Aayah na Hadiyth ni kughufiriwa madhambi. Maulamaa wamekubaliana wote kuwa anayesilimu lau kama alikuwa na deni au kisasi, basi hayo hayafutiki kwa kusilimu kwake, na hasa kwa vile kuwa kulazimika kuoga si uchukulifu au ukalifisho kwa yaliyomlazimu katika ukafiri, bali ni ulazimisho wa sharti katika masharti ya Swalaah katika Uislamu, kwani yeye ana janaba. Na Swalaah haisihi mtu akiwa na janaba. Naye havuliki na janaba hiyo kwa kuwa ameingia katika Uislamu. [Al-Majmu’u (2/174)].
3. Wamesema:
“Watu wengi walisilimu wakiwa na wake na watoto lakini Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakuwaamrisha kuoga kwa njia ya lazima. Na lau ingelikuwa ni wajibu, basi angeliwaamrisha hilo”.
Na hapa kuna mlahadha:
Lililo dhahiri ni wajibu kuoga, kwani kuamrishwa baadhi, kuna maana kuwa wao washafikishiwa amri. Ama kudai kuwa wengineo hawakuamrishwa, hilo halifai kwa kushikilia tu, kwani ukomo wake ni wao tu kutokuwa na habari nalo, nako si kutojua kwa sababu ya kutojulikana. [Nayl Al-Awtwaar (1/281)].
Kwa hivyo, lenye nguvu zaidi ni kuwa inamlazimu kafiri – sawasawa akiwa kafiri wa asili au aliyeritadi – aoge kwa hali yoyote anaposilimu. Na linalotuhisisha kwamba kuoga wakati wa kuingia katika Uislamu lilikuwa ni jambo linalojulikana vizuri na Maswahaba, ni yale yaliyomo ndani ya kisa cha kusilimu mama wa Abu Hurayrah. Kisa kinaeleza kuwa mama huyo alioga na akavaa deraya yake.[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (2491) na Ahmad (7911)].
Pia kisa kilichotangulia cha kusilimu Usayd bin Hudhayr. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
6- Swalaah ya Ijumaa
Kukoga siku ya ijumaa ni jambo la lazima, na mwenye kuacha, basi anapata dhambi kwa mujibu wa kauli mbili sahihi zaidi za Maulamaa. Haya yamesemwa na Abuu Hurayrah, 'Ammaar bin Yaasir, Abuu Sa'iyd Al-Khudriy na Al-Hasan. Haya yamekuja pia katika riwaya iliyopokelewa toka kwa Maalik na Ahmad. Aidha, ni madhehebu ya Ibn Hazm. [Al-Muhalla (2/12) na Al-Awsatw (4/43)].
Dalili za hili ni:
1- Hadiyth ya Abuu Sa'iyd Al-Khudriy kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) amesema:
((غسل يوم الجمعة واجب على كل محتلم)(
((Kukoga siku ya ijumaa ni wajibu kwa kila aliyebaleghe)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (2491) na Ahmad (7911)].
2- Hadiyth ya Ibn 'Umar kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) amesema:
((من جاء منكم إلى الجمعة فليغتسل))
((Anayekwenda ijumaa kati yenu, basi aoge)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (2/6) na Muslim (844)].
3- Hadiyth ya Abuu Hurayrah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) amesema:
((حق على كل مسلم أن يغتسل في كل سبعة أيام يوما، يغسل رأسه وجسده))
((Haki iliyo juu ya kila Muislamu, ni kuoga siku moja katika kila siku saba. Aoshe kichwa chake na mwili wake)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (2/318) na Muslim (849)].
4- Hadiyth ya Thawbaan kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) amesema:
((حق على كل مسلم السواك، وغسل يوم الجمعة، وأن يمس من طيب أهله إن كان))
((Haki iliyo juu ya kila Muislamu ni mswaki, kuoga siku ya ijumaa na ajipake mafuta uzuri ya ahli wake kama yapo)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad (4/34). Tizama "Asw-Swahiyhah" (1796)].
5- Hadiyth ya Hafswa kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) amesema:
((على كل محتلم رواح الجمعة، وعلى من راح الجمعة أن يغتسل))
((Kila aliyebaleghe ni lazima aende ijumaa, na mwenye kwenda ijumaa ni lazima akoge)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (338), An-Nasaaiy (3/89) na Ahmad (3/65)].
6- Imepokelewa toka kwa Ibn 'Umar, amesema:
"Tuliamrishwa kukoga siku ya ijumaa, na tusitawadhe (ili kuondosha janaba) kutokana na kujamii".[Isnadi yake ni Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Bakr Al-Muruuziy katika "Ijumaa na fadhila zake”].
Wamesema:
“Na kuyafanya kuwa si wajibu wala si haki kwa mfano wa dalili hizi zilizotajwa hapo juu, hayo aliyoyaelezea Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) ya kwamba ni haki ya Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa) kwa kila Muislamu na kwamba ni wajibu kwa kila aliyeota (aliyebaleghe), basi hili ni jambo ambalo ngozi husisimka kwalo!! [Mfano wake katika Al-Muhalla].
Nayo Jamhuri ya Maulamaa wakiwemo Ibn Mas'uud na Ibn 'Abbaas ambao ni katika Maswahaba, msimamo wao ni kuwa kukoga siku ya ijumaa ni jambo mustahabbu na wala si lazima. Na kati ya dalili muhimu walizozitoa ni:
1- Hadiyth Marfu’u ya Samurah bin Jun-dub:
((من توضأ يوم الجمعة فبها ونعمت، ومن اعتسل فالغسل أفضل))
((Mwenye kutawadha siku ya ijumaa, basi hilo ni jambo zuri, na mwenye kukoga, basi kukoga ni jambo bora)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (354), An-Nasaaiy (3/94), At-Tirmidhiy (497) na wengineo. Hadiyth hii ina njia ambazo nimezitafiti kwa kina na kuzizungumzia katika Allam-'at Fiy Aadaab Wa Ahkaam Al-Jum-'ah. Al-'Allaamah Al Al-Baaniy amesema ni Hadiyth Hasan].
Haya ni maneno yaliyo wazi zaidi katika dalili yao ijapokuwa Hadiyth ni Dhwa’iyf kwa kauli yenye nguvu.
2- Hadiyth Marfu’u ya Abuu Hurayrah:
((من توضأ فأحسن الوضوء ثم أتى الجمعة فاستمع وأنصت، غفر له ما بينه وبين الخمعة وزيادة ثلاثة أيام .....))
((Mwenye kutawadha, akatawadha ipasavyo, kisha akenda ijumaa, akasikiliza na akanyamaza, hughufiriwa yaliyo baina yake na kati ya ijumaa pamoja na nyongeza ya siku tatu…..)).[Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (857), At-Tirmidhiy (498) na wengineo].
Wamesema:
“Lau kama kuoga kwa ajili ya ijumaa kungelikuwa ni lazima, basi Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) asingelitaja wudhuu peke yake”.
Al-Haafidh ameijibu kauli hii katika "Al-Fat-h" (2/422) kwa kusema:
" Kukoga hakujakanushwa, kwani Hadiyth imekuja kwa njia nyingine katika Asw-Swahiyh kwa tamko "Mwenye kukoga". Kwa hiyo inawezekana kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) ametaja wudhuu kwa yule ambaye alikwishaoga kabla ya kwenda, na akahitajia kutawadha tena".
Ninasema:
"Wao wana dalili nyinginezo nilizozitafiti kwa kina na kuzijadili moja baada ya nyingine katika Kitabu changu cha "اللمعة في آداب وأحكام الجمعة". Na hitimisho la suala ni kuwa wenye kusema kwamba kukoga ni wajibu, dalili zao zina nguvu zaidi, Sanad zake ni Swahiyh zaidi na kuzitumia ni salama zaidi”.
7- Kufa
Ni moja kati ya sababu zenye kuwajibisha kukoga, lakini si kwa maiti mwenyewe, bali ni kwa Muislamu aliyeko kwa maiti. Uchambuzi wake utakuja katika mlango wake wa "Kitaab Al-Janaaiz".
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
050-Majosho Yaliyo Mustahabbu
Alhidaaya.com [3]
1- Kwa ajili ya ‘Iyd mbili
Imepokelewa toka kwa Al-Faakih bin Sa'ad kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) alikuwa akikoga wakati wa ‘Iyd el fitr na ‘Iyd el adh-ha. Lakini Hadiyth hii ni Dhwa’iyf sana. [ Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Maajah (1316)].
Lakini inaweza kutolewa dalili juu ya kustahabiwa hilo kwa yaliyothibiti toka kwa 'Aliy bin Abi Twaalib na Ibn 'Umar kuwa imepokelewa toka kwa Zaadhaan kuwa mtu mmoja alimuuliza ‘Aliy Allaah Amridhie kuhusu kuoga. Akamjibu akimwambia:
"Oga kila siku ukipenda". Akasema: "Hapana. Kuoga kunakotakikana hasa". Akamwambia: "Siku ya Ijumaa, Siku ya Arafah, Siku ya Kuchinja na Siku ya Fitwr". [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ash-Shaafi'iy katika Musnadi yake (114) na kwa njia yake Al-Bayhaqiy 3/278)].
Na imepokelewa toka kwa Naafi'i kwamba ‘Abdullaah bin 'Umar alikuwa akikoga siku ya ‘Iyd el Fitwr kabla ya kwenda sehemu ya kuswalia. [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Maalik (426), na kutoka kwake imepokelewa na Ash-Shaafi'iy katika Al-Ummu (1/231)].
2- Kuzindukana baada ya kupoteza fahamu
Kwani Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) alioga baada ya kupoteza fahamu. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (687) na Muslim (418) katika Hadiyth ndefu iliyopokelewa toka kwa 'Aaishah]. Na hii ilikuwa katika maradhi yake aliyofia.
Na Ijma’a imenukuliwa juu ya kusuniwa hilo, na Maulamaa wanasema kwamba akili kukaa sawa baada ya wendawazimu ni sawa na kupoteza fahamu.
3- Kuhirimia Hijjah na ‘Umrah
Ni kwa Hadiyth ya Zayd bin Thaabit kwamba yeye alimwona Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) amebadili nguo kwa ajili ya kuhirimia na kisha akakoga.[Hadiyth Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy (831). Na tizama Al-Irwaa (149)].
Na mwanamke hata kama atakuwa na hedhi au nifasi ataoga, kwani Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) alimwamrisha Asmaa bint 'Umays akoge wakati alipojifungua katika Hijjah. [Hadiyth Swahiyh: Itakuja katika mlango wa Hijjah]. Haya yataelezwa zaidi katika mlango ha Hijjah.
4- Kuingia Makkah
Ni kwa Hadiyth ya Ibn 'Umar kwamba yeye alikuwa haingii Makkah ila hulala Dhiy Tuwaa mpaka asubuhi, halafu hukoga, kisha huingia Makkah mchana. Inaelezewa kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) alilifanya hilo.[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (1573) na Muslim (1259)].
5- Baada ya kila jimai kama atarudiarudia
Ni kwa Hadiyth ya Abi Raafi'i kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) aliwazungukia wakeze usiku mmoja huku akikoga kwa huyu na kwa yule. Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Kwa nini usikoge mara moja tu"?
Akasema:
((هذا أزكى وأطيب وأطهر ))
((Hili ni utakaso zaidi, jema zaidi na twahara zaidi)). [Hadiyth Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (216) na Ibn Maajah (560)].
6- Baada ya kumwosha maiti (kama Hadiyth ni Swahiyh)
Imepokelewa Hadiyth Marfu’u toka kwa Abu Hurayrah:
(( من غسل ميتا فليغتسل ))
((Mwenye kumwosha maiti, basi akoge)). [Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (3162), At-Tirmidhiy (993) na Ibn Maajah (1461). At-Tirmidhiy, Ibn Hajar na Al-Al Baaniy wamesema ni Hasan. Tizama Al-Irwaa (1/174). Lakini inavyoelekea inahitaji ukaguzi hivi, kwani Hadiyth imekosolewa].
7- Kwa mwenye damu ya istihaadhwah kwa kila Swalaah
Amri ya kukoga kwa mwanamke mwenye damu ya istihaadhwah wakati wa kila Swalaah imekuja katika mjumuiko wa Hadiyth Dhwa’iyf. [Irejee katika Jaami'u Ahkaam An-Nisaa (1/230-237)].
Lakini imethibiti toka kwa Aaishah akisema: “Ummu Habiybah alisumbuliwa na damu ya istihaadhwah kwa muda wa miaka saba. Akaja kumuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu Alayhi wa Aaalihi wa Sallam) kuhusiana na tatizo hilo. Rasuli akamwamuru aoge, na akamwambia kwamba huo ni mshipa. Naye akawa anaoga kwa kila Swalaah.”[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (327) na Muslim (334)].
Ash Shaafi’iy Allaah Amrehemu anasema: “Alilomwamuru Rasuli ni kuoga na kuswali tu, kwani katika maneno yake hakuna amri yoyote ya kuoga kwa kila Swalaah. [Amri hii ya kuoga ni mutwlaq, haionyeshi kukariri. Huenda Ummu Habiybah alifahamu kwamba ametakiwa kufanya hivyo kwa dalili fulani, hivyo akawa anaoga kila anapotaka kuswali. (Fat-h Al-Baary (1/509)].
Na sina shaka yoyote kwamba kuoga kwake kulikuwa ni kwa kupenda kwake mwenyewe kinyume na alivyoamrishwa, na mlango wa hilo uko wazi kwake”. [Sunan Al-Bayhaqy (1/349)].
Ninasema: “Hii ni kauli ya Jamhuri ya Maulamaa toka Salafu na waliokuja baada yao kwamba mwanamke mwenye damu ya istihaadhwah si lazima aoge kila Swalaah”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
051-Niya Ni Sharti Ya Kusihi Kukoga
Alhidaaya.com [3]
Hii ni kwa vile kukoga ni ‘ibaadah isiyojulikana ila kupitia sharia, na kwa ajili hiyo, niya imekuwa ni sharti humo. Niya yenyewe, ni moyo kuazimia tendo la kukoga ikiwa ni kufuata na kuitii Amri ya Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam). Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa) Anasema:
((وما أمروا إلا ليعبدوا الله مخلصين له الدين))
((Na hawakuamrishwa ila kwa ajili ya kumwabudu Allaah wakimtakasia Yeye Dini)). [Al-Bayyinah (98:5)]
Ikhlaasw ni kusudio la kujikurubisha kwa Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa) na kumwelekea Yeye tu katika kutekeleza yale Aliyoyafaradhisha kwa Waja Wake Waumini.
Na Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) anasema:
((إنما الأعمال بالنيات))
((Hakika amali ni kwa niya)).[Hadiyth Swahiyh: Imekwishatajwa].
Na hili la kukoga ni amali. [Angalia Mlango wa ((Niya Ni Sharti Ya Kuswihi Wudhuu uk.40))].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
052-Nguzo Ya Kuoga
Alhidaaya.com [3]
Ni kukieneza kiwiliwili chote kwa maji. Uhalisia hasa wa kuoga ni kububujisha maji kwenye kiwiliwili chote na kufika maji hayo katika kila unywele na ugozi. Na hili limethibiti katika Hadiyth zote zinazoelezea kuhusu picha ya namna alivyokuwa akikoga Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam). (Hadiyth hizi nitazielezea hivi karibuni). Na kati ya Hadiyth hizo ni Hadiyth ya ‘Aaishah (Allaah Amridhie):
((..kisha anamimina maji juu ya kiwiliwili chake chote)). [Hadiyth Swahiyh: Matni na takhriyj yake zitakuja karibu].
Al-Haafidh amesema katika Al-Fat-h (1/361):
“Usisitizo huu (wa kusema “kiwiliwili chake chote”) unaonyesha kwamba yeye alieneza kiwiliwili chake chote kwa josho”.
Na katika Hadiyth ya Jubayr bin Mutw-‘am kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) amesema:
((أما أنا، فآخذ ملء كفي ثلاثا فأصب على رأسي، ثم أفيض بعد ذلك على سائر جسدي))
((Ama mimi, huchukua ujazo wa kiganja changu mara tatu, kisha namimina juu ya kichwa changu, kisha nabubujisha baada ya hapo juu ya kiwiliwili changu chote)). [Hadiyth Swahiyh: Ahmad ameikhariji kwa tamko hili (4/81), na katika Al-Bukhaariy (254) na Muslim (327) kwa ufupisho].
Lingine linaloonyesha kuwa nguzo pekee ya kukoga ni kukieneza kiwiliwili chote kwa maji, ni Hadiyth ya Ummu Salamah aliyesema:
“Nilisema: Ee Rasuli wa Allaah! Mimi ni mwanamke ninayesuka sana nywele, je, nizifumue wakati wa kukoga janaba?” Akasema:
(( لا، إنما يكفيك أن تحثي على رأسك ثلاث حثيات، ثم تفيضين عليك الماء فتطهرين))
(( Hapana, bali yakutosha kumwagia kichwa chako mateko matatu, kisha utajimiminia maji utwaharike)).
Ama kusugua viungo, kusukutua na kupaliza maji wakati wa kukoga, kauli yenye nguvu inasema kuwa hayo yote ni Sunnah kama tutakavyoeleza mbeleni. Na haya ndiyo madhehebu ya Jamhuri.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
053-Yaliyosuniwa Wakati Wa Kukoga (Picha Ya Josho Kamili)
Alhidaaya.com [3]
Mhimili katika mlango huu ni Hadiyth mbili:
1- Hadiyth ya ‘Aaishah (Allaah Amridhie) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) alipokuwa akikoga janaba:
“Alianza, akaiosha mikono yake miwili, kisha akatawadha kama anavyotawadha kwa ajili ya Swalaah, kisha huingiza vidole vyake katika maji, kisha hufikicha kwavyo mizizi ya nywele zake, halafu humimina [Na katika riwaya nyingine: mpaka anapopata uhakika kwamba ameshatotesha ngozi yake, humimina] juu ya kichwa chake mateko matatu kwa mikono yake, kisha humimina maji juu ya ngozi yake yote”. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (330), Abuu Daawuud (251), An-Nasaaiy (1/131), At-Tirmidhiy (105) na Ibn Maajah (603)].
2- Hadiyth ya Maymuuna (Allaah Amridhie). Alisema:
“Nilimtengea Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) maji ya kukoga, akaosha mikono yake mara mbili au tatu, kisha akajimiminia maji kwenye mkono wake wa kushoto kwa kutumia mkono wake wa kulia akaosha utupu wake [Na katika riwaya nyingine: utupu wake pamoja na uchafu ulioipata], kisha alisugua mkono wake kwenye udongo au ukutani [kisha akauosha], kisha alisukutua na kupaliza, akauosha uso wake, mikono yake miwili na kichwa chake, kisha alijimiminia maji juu ya kiwiliwili chake, kisha alisimama kando, akaosha makanyagio yake mawili, nikampa kitambaa, kisha akaambatisha mkono wake hivi na wala hakukitaka”. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (266) na Muslim (317)].
Ninasema:
“Kutokana na Hadiyth hizi mbili na nyinginezo, tunahitimisha tukisema kuwa, linalopendeza ni kuwa kuoga janaba kunatakikana kuwe katika picha ifuatayo:
1- Kuosha mikono miwili mara tatu kabla ya kuiingiza katika chombo au kuanza kukoga kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah:
((Alianza, akaiosha mikono yake miwili….)).
Na katika tamko la Muslim (317) kwa Hadiyth ya Maymuuna:
((Akaosha viganja vyake viwili mara mbili au mara tatu, kisha akaingiza mkono wake katika chombo…)).
Al-Haafidh amesema katika Al-Fat-h (1/429):
“Inawezekana kuwa aliviosha kwa ajili ya kuvisafisha uchafu. Pia yawezekana kuwa huo ni mwosho wa kisharia wakati wa kuamka usingizini”.
2- Kuosha uchafu wa utupu kwa mkono wa kushoto kutokana na maelezo ya Hadiyth ya Maymuunah. Ama kuukamata utupu kwa mkono wa kulia, hilo ni makruhu kutokana na Hadiyth ya Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam):
((إذا بال أحدكم فلا يأخذن ذكره بيمينه، ولا يستنجى بيمينه، ولا يتنفس في الإناء))
((Anapokojoa mmoja wenu, basi asiikamate kabisa dhakari yake kwa mkono wake wa kulia, wala asistanji kwa mkono wake wa kulia, na wala asipumulie ndani ya chombo)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (154) na Muslim (267)].
3- Kuosha mkono (baada ya kuosha utupu) na kuusafisha kwa sabuni au mfano wake kama mchanga. Maymuuna katika Hadiyth yake anasema:
((Kisha akaambatisha mkono wake ardhini akaupangusa kwa udongo, kisha akuosha….)).
Na katika tamko jingine:
((Kisha akapiga ardhi kwa mkono wake wa kushoto, akausugua msuguo wa nguvu)). [Hii ni kauli ya Muslim (317)].
An-Nawawiy katika Sharh Muslim (3/231) anasema:
“Ni kwamba inapendeza kwa anayestanji kwa maji anapomaliza, aoshe mkono wake kwa udongo (mchanga) au “ashnaan” (mada mfano wa sabuni) au ausugulie na mchanga au ukuta ili usafike vizuri kutokana na uchafu”.
4- Kutawadha wudhuu kamili kama anavyotawadha kwa ajili ya Swalaah. Na hili limethibiti katika Hadiyth za ‘Aaishah na Maymuuna.
Al-Haafidh katika Al-Fat-h (1/429) anasema:
“Inawezekana kuwa kuanza kutawadha kabla ya kukoga, ni Sunnah ya kando, kwa kuwa ni lazima kuviosha viungo vya wudhuu pamoja na kiwiliwili chote wakati wa kukoga. Na inawezekana kuwa badala ya kuviosha tena wakati wa kukoga, itatosheleza kuoshwa kwake wakati wa kutawadha. Na yeye ametanguliza kuosha viungo vya wudhuu kwa ajili ya kuvipa hadhi yake, na ili mwenye kukoga apate picha ya twahara zote mbili; kubwa na ndogo”.
Ninasema:
“Kutawadha kabla ya kukoga ni Sunnah kwa Jamhuri ya Maulamaa kinyume na Abuu Thawr, Daawuud na Adh-Dhwaahiriy”. [Fat-h Al-Baariy (1/426), Al-Majmu’u (1/186) na Al-Istidhkaar (3/59)].
Faida Mbili
Faida Ya Kwanza
Hukmu Ya Kusukutua Na Kupaliza Maji Puani Wakati Wa Kukoga
Katika mlango wa wudhuu, tulieleza kwamba Maulamaa wamehitilafiana katika kauli nne kuhusu kusukutua na kupaliza maji puani wakati wa kutawadha. Nasi tulitilia nguvu kwamba ni lazima kusukutua na kupaliza maji puani.
Ama kukoga, Ath-Thawriy, Abuu Haniyfah na wenzake pamoja na Ahmad, Atwaa na Ibn Al-Mubaarak ambao madhehebu yao ni mashuhuri, msimamo wao ni kuwa kusukutua na kupaliza maji puani ni lazima wakati wa kukoga janaba. [Angalia marejeo ya mas-ala katika Nguzo za Wudhuu].
Na kati ya dalili zao ni:
1- Hadiyth iliyopokelewa Marfu’u:
((المضمضة والإستنشاق ثلاثا للجنب فريضة))
((Kusukutua na kupaliza maji puani ni mara tatu, kwa mwenye janaba ni fardhi)). [Hadiyth Mawdhu’u (ya kutungwa): Imefanyiwa "ikhraaj" na Ad-Daara Qutwniy (1/115). Pia imepokelewa Mursal. Tazama kitabu cha Naswb Ar-Raayat (1/87)].
2- Hadiyth iliyopokelewa Marfu’u:
((من ترك موضع شعرة من جسده لم يغسلها فعل به كذا وكذا من النار))
((Mwenye kuacha sehemu ya unywele katika kiwiliwili chake asiuoshe, ataadhibiwa vibaya motoni)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (249), Ibn Maajah (599) na Ahmad (1/94). Angalia Adh Dha’iyfah (930)].
3- Hadiyth iliyopokelewa Marfu’u:
((أداء الأمانة غسل الجنابة، وتحت كل شعرة جنابة))
((Kutekeleza amana ni kukoga janaba, na chini ya kila unywele kuna janaba)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa "ikhraaj" na Ibn Maajah (598) kwa Sanad Dhwa’iyf. Tazama At-Talkhiysw (1/142)].
Hadiyth zote hizi ni Dhwa’iyf na hazifai kutolewa dalili.
4- Ni kitendo chake Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) kilichoelezewa katika Hadiyth ya Maymuuna (kwa kiashirio wazi), na katika Hadiyth ya ‘Aaishah (iliyojumuisha wudhuu), hayo yanabainisha Kauli Yake Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa):
(( وإن كنتم جنبا فاطهروا ))
(( Na mkiwa na janaba, basi jitwaharisheni)). [Al-Maaidah (5:6)].
5- Ni kwamba kuosha kiwiliwili chote ni wajibu, na uso ni sehemu ya kiwiliwili. Na kwa hivyo, imekuwa ni lazima kusukutua na kupaliza maji puani, kwani mawili haya ni sehemu ya uso kama tulivyosema katika mlango wa wudhuu.
Ama waliosema kuwa hilo ni Sunnah, nao ni Maalik, Al-Layth na Al-Awzaa’iy ambao ni Jamhuri, dalili zao ni:
1- Kutawadha wakati wa kukoga si wajibu [kama ilivyotangulia], na kusukutua na kupaliza maji puani ni katika mambo yanayoambatana na wudhuu. Na kama wudhuu haupo, basi yanayoambatana nao pia hupomoka. [Fat-h Al-Baariy (1/443)].
2- Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) kuyafanya mawili hayo, hakuonyeshi kuwa ni wajibu kwa kuwa tu amefanya, bali ni kwa kuonyesha kuwa hayo ni mazuri na yanapendeza kuyafanya. Nayo hayaonyeshi wajibu ila ikiwa ni ubainisho wa mjumuiko uliofungamana na wajibu. Na hapa mambo si hivyo. [Fat-h Al-Baariy (1/432)].
3- Ni kauli ya Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) kwa Abuu Dharri wakati alipomuuliza kuhusu janaba iliyompata akakosa maji:
(( الصعيد الطيب وضوء المسلم، وإن لم يجد الماء عشر حجج، فإذا وجد الماء فليمسه بشرته))
((Mchanga twahara ni kitwaharisho kwa Muislamu hata kama hakupata maji kwa miaka kumi. Na akiyapata maji, basi ayagusishe ngozi yake)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy (124), Abuu Daawuud (233), An-Nasaaiy (1/171) na wengineo kwa njia tofauti. Yenye nguvu zaidi ni ya Abuu Qulaabah toka kwa ‘Amri bin Bijdaan toka kwa Abuu Dharri ikiwa Marfu’u kama ilivyo katika Al-‘Ilal ya Ad Daaraqutwniy (1113), Ibn Abiy Haatim (1/11) na ‘Amri ambaye hajulikani. Hadiyth hii ina ushahidi toka kwa Abuu Hurayrah, na pana mvutano wa yeye kuifanya Hasan. Lakini katika Al-Irwaa, Al-Al Baaniy amesema kuwa ni Swahiyh].
Wamesema: “Al-Basharah” ni ngozi ya nje, na kwa hivyo haihusiani na kusukutua na kupaliza maji.
4- Hadiyth ya Jubayr bin Mutw-am. Amesema: “Tulielezana kuoga janaba mbele ya Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) naye akasema:
(( أما أنا، فآخذ ملء كفي ثلاثا فأصب على رأسي، ثم أفيض بعد ذلك على سائر جسدي))
((Ama mimi, huchukua ujazo wa kiganja changu mara tatu, kisha namimina juu ya kichwa changu, kisha nabubujisha baada ya hapo juu ya kiwiliwili changu chote)). [Hadiyth Swahiyh: Imeelezewa karibuni].
Na katika tamko:
((أما أنا فأحثي على رأسي ثلاث حثيات من ماء فإذا أنا قد طهرت))
((Ama mimi, basi humwagia mateko matatu ya maji juu ya kichwa, na hapo nakuwa nimetwaharika)). [Ash-Shawkaaniy amenukuu toka kwa Al-Haafidh kauli yake: “Neno lake (Basi hapo ninakuwa nishatwaharika), halina asili yoyote sawasawa katika Hadiyth Swahiyh au Hadiyth Dhwa’iyf].
Na tamko hili halifai.
5- Ni neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) kwa Ummu Salamah:
(( إنما يكفيك أن تحثي على رأسك ثلاث حثيات من ماء، ثم تفيضين عليك الماء، فإذا أنت قد طهرت))
(( Hakika yakutosha kumwagia kichwa chako mateko matatu ya maji, kisha utajimiminia maji, na hapo unakuwa umetwaharika)).
Ninasema:
“Lau si Hadiyth ya mwisho ya Ummu Salamah, basi wajibu wa kusukutua na kupaliza maji puani ungelikuwa na sauti ya nguvu. Lakini Hadiyth ya Ummu Salamah, inaonyesha kwa kielelezo cha nguvu kwamba kiasi kitoshelezacho katika kukoga ni kile kilichotajwa, na hakukutajwa humo kusukutua wala kupaliza maji. Na wala haisemwi: “Mawili hayo yanaingia katika neno lake (kisha unajimiminia maji), kwani maana ya kumimina, haiyagusi mawili haya kama inavyoonekana wazi.
Hivyo basi, madhehebu ya Jamhuri inayosema kuwa kusukutua na kupaliza ni jambo mustahabb na wala si wajibu wakati wa kukoga, ndiyo yenye nguvu kwangu. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
Faida Ya Pili
Ni Wakati Gani Miguu Miwili Huoshwa?
Lililo wazi kutokana na Hadiyth ya Maymuuna ni kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) alikawisha kuosha makanyagio yake mawili mpaka pale alipomaliza kukoga.
Al-Bukhaariy katika tamko lake anasema:
“Alipomaliza kukoga, aliosha miguu yake”.
Ama Hadiyth ya ‘Aaishah, hakuna kingine humo zaidi ya kuwa tu Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) alikuwa akitawadha kabla ya kukoga. [Katika riwaya ya Muslim (316) kutoka kwa ‘Aaishah, mwishoni mwa Hadiyth hii anasema: “..kisha akamimina juu ya kiwiliwili chake chote, kisha akaosha miguu yake miwili”. Ni ziada ambayo haikuhifadhiwa. Tizama ‘Ilal Muslim ya Hirawiy (69), Attamhiyd (22/93) na Fat-h Al-Baariy ya Ibn Rajab (1/234)]. Na kwa ajili hiyo, Maulamaa wamekuwa na mielekeo minne kutokana na Hadiyth hizi mbili: [Fat-h Al-Baariy ya Ibn Hajar (1/362), Al-Mughniy (1/288), Sharh Al-‘Umdah (1/371) na Al-Khilaafiyaat cha Al-Bayhaqiy (2/425)].
1- Ni mustahabbu kukawisha kuosha miguu miwili wakati wa kukoga kutokana na Hadiyth ya Maymuuna. Haya ni madhehebu ya Jamhuri.
2- Ni kutawadha wudhuu kamili kabla ya kukoga kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah. Sababu ni kuwa Hadiyth hii inaelezea alivyokuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) akifanya aghalabu kinyume na Hadiyth ya Maymuuna ambaye ameelezea josho moja tu. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy na riwaya ya Maalik na Ahmad.
3- Mtu anakhiyarishwa, ima kuanza kuosha miguu miwili pamoja na wudhuu au kuiosha mwishoni. Hii ni riwaya ya Ahmad.
4- Kama mtu anaoga sehemu isiyo safi, basi ataiosha miguu yake mwishoni. Na kama si hivyo, basi ataiosha mwanzoni wakati akitawadha. Haya ni madhehebu ya Maalik.
Ninasema:
“Mwelekeo huu wa mwisho ndio wenye nguvu zaidi. Lakini pamoja na yote hayo, jambo hili lina wasaa na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi”.
5- Ni kumimina maji juu ya kichwa mara tatu mpaka yafike katika mashina ya nywele.
6- Ni kuanzia upande wa kulia wa kichwa kisha upande wa kushoto.
7- Kufikicha (kusugua) nywele. Hadiyth ya ‘Aaishah inasema:
((Kisha hufikicha nywele zake kwa mkono wake mpaka anapohakikisha kuwa ameilowesha ngozi yake, hapo humiminia juu yake maji mara tatu..)).
Imepokelewa vile vile toka kwa ‘Aaishah akisema:
(( Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) alipokuwa akikoga janaba, hutaka aletewe kitu kama “alhilaab”, huikamata kwa kiganja chake, kisha huanza kwa upande wake wa kulia wa kichwa, kisha upande wake wa kushoto….)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (258) na Muslim (318)].
“Alhilaab” ni chombo kinachojaa mkamuo mmoja wa maziwa ya ngamia (Ma’alim As-Sunan) cha Al-Khattwaabiy (1/69).
Na imepokelewa toka kwa ‘Aaishah vile vile akisema: (( Mmoja wetu alipokuwa akipatwa na janaba, huchukua kwa mkono wake mateko matatu juu ya kichwa chake, kisha huchukua maji kwa mkono wake juu ya upande wake wa kulia na kwa mkono wake mwingine juu ya upande wake wa kushoto. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (277)].
Faida
Je, Ndevu Huasuliwa Wakati Wa Kukoga Janaba?
Jamhuri ya Maulamaa ambao ni Maalik, Abu Haniyfah, Ash-Shaafi’iy na Ibn Hazm wamesema: “Haimlazimu kuziasulia, bali ni jambo mustahabbu”. [Al-Muhalla (2/33), Al-Awsatw (2/127) na At-Tamhiyd (22/95)].
Ninasema:
“Hili mahala pake ni pale yanapokuwa maji yanafika hadi kwenye ngozi, na kama si hivyo, basi ni lazima kuziasulia ili kuyafikisha maji ndani yake. Na la akiba zaidi kwa vyovyote, ni kuziasulia ndevu zake kutokana na ujumuishi wa neno la ‘Aaishah: ((basi huasulia kwayo mashina ya nywele zake”.
8,9- Kumimina na kuyaeneza maji katika kiwiliwili chote kwa kuanzia upande wa kulia kisha wa kushoto.
Kumimina na kueneza maji katika kiwiliwili kizima ni jambo lililothibiti katika Hadiyth zote zinazotoa picha ya josho lake Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam).
Ama kuanzia kulia, ni kwa Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema:
((Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) kulikuwa kunampendeza kuanza kwa kulia akivaa viatu, akitembea, akijitwaharisha na katika mambo yake yote)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (168) na Muslim (268)].
Faida Mbili
Faida Ya Kwanza
Kujimiminia Maji Kiwiliwili Chote Kunakuwa Ni Mara Moja Tu.
Na hili liko wazi katika muktadha wa Hadiyth mbili za ‘Aaishah na Maymuuna. Ndani ya Hadiyth hizi, pametajwa kuoshwa mara tatu mikono miwili na kichwa. Ama kiwiliwili kizima, ‘Aaishah anasema:
((Kisha anamiminia juu ya kiwiliwili chake chote)).
Na Maymuuna anasema:
((Kisha alimiminia juu ya kiwiliwili chake)).
Na Ibn Batwaal amesema: [Fat-h Al-Baariy (1/439)].
“ Na kwa vile suala halikuainishwa kwa idadi, basi lichukuliwe chini ya ilivyotajwa, nayo ni mara moja, kwani asli ni kutozidisha juu yake”.
Ninasema:
“Na hili ni mashuhuri katika madhehebu ya Ahmad na masahibu wa Maalik. Shaykh wa Uislamu amelikhitari hili. Na Jamhuri wamestahabbu kufanya mara tatu”.
Faida Ya Pili
Hukmu Ya Kusugua Viungo Vya Kukoga [Al-Muhalla (2/30), Al-Istidhkaar (3/63), Al-Mughniy (1/290), Bidaayat Al-Mujtahid (1/55) na As-Sayl Al-Jarraar (1/113)]
Maulamaa wamekhitalifiana:
Je, ni sharti kupitisha mkono katika kiwiliwili kizima wakati wa kukoga? Au yatosha kumimina maji tu katika kiwiliwili chote hata kama mtu hakupitisha mkono wake katika kiwiliwili chake?
Au kwa maana nyingine tunasema: Je, kukoga kunatimu kwa kujimiminia maji tu au ni lazima pia kusugua juu ya kitu?
Jamhuri ya Maulamaa (kinyume na Maalik na Al-Mazniy) wanaona kuwa hakuna ulazima kusugua, bali ni mustahabbu. Na lau kama mtu atajimwagia maji mwenyewe katika kiwiliwili chake, basi atakuwa ametekeleza aliyowajibishwa na Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa). Hali kadhalika, akipiga mbizi majini na maji yakaupata mwili wake wote.
Dalili za makundi mawili katika suala hili ni zile zile zilizokwishatangulia kuelezewa katika hukmu ya kusukutua na kupaliza maji puani.
Na lililo wazi ni kuwa kusugua ni jambo mustahabbu na wala si wajibu.
Na Hadiyth ya ‘Imraan ibn Haswiyn – pamoja na Hadiyth ya Ummu Salamah inayatilia nguvu madhehebu haya katika kisa cha “Al-Muzaadatayn”. Humo panaelezwa: ((… na mwisho wa hilo ulikuwa ni kumpa chombo chenye maji yule ambaye imempata janaba, akasema: Nenda, halafu ujimiminie”. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (344)].
Na kwa haya, lau mtu akisimama chini ya bafu la manyunyu (bomba la kuogea), na maji yakafika katika kiwiliwili chake chote, basi kukoga kwake ni sahihi kukiambatana na niya.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
054-Kuoga Mwanamke Janaba
Alhidaaya.com [3]
Anavyooga mwanamke janaba ni sawa na anavyooga mwanamume. Na mwanamke kama amesuka nywele zake, basi haimlazimu kuzifumua bali atalazimika tu kuhakikisha kuwa maji yanafika hadi kwenye mizizi ya nywele. Hii ni kutokana na Hadiyth ya Maymuuna aliyesema:
“Ee Rasuli wa Allaah! Mimi ni mwanamke ninayependa sana kusuka nywele zangu. Je, nizifumue kwa ajili ya kuoga janaba?”
Rasuli akamwambia:
(( Hakika yakutosha kumwagia kichwa chako mateko matatu ya maji, kisha utajimiminia maji, na hapo unakuwa umetwaharika)). [Hadiyth Swahiyh: Imeshatajwa sana nyuma.]
Na imepokelewa na ‘Aaishah aliyesema:
“Tulikuwa tukioga tukiwa na “adh-dhimaad” nailhali tuko na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) sawasawa tukiwa tumehirimia au hatujahirimia”. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (254) na Al-Bayhaqiy (2/182)].
Adh-dhimaad ni dawa ya kupaka kwenye nywele. Inazifanya zishikamane na zinyooke kama zilizonatishwa na gundi na kuwa kama rasta.
Na ‘Aaishah alimshambulia ‘Abdulaah bin ‘Amri kwa kuwaamuru wanawake kufumua nywele zao wakati wa kuoga. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (331), An-Nasaaiy (1/203) na Ibn Maajah (604)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
055-Kuoga Mwanamke Hedhi Na Nifasi
Alhidaaya.com [3]
[Ni kutoka kitabu changu cha Fiqh As-Sunnah Lin An-Nisaai (uk. 49) na Jaami’u Ahkaamin Nisaai cha Shaykh wetu (1/116 na ya baada yake) pamoja na nyongeza kidogo].
Namna ya kuoga hedhi na nifasi ni sawa na kuoga janaba. Lakini pamoja na hivyo, wakati wa kuoga hedhi na nifasi huongezewa yafuatayo:
1- Kutumia sabuni na mfano wake kama mada za kusafishia pamoja na maji.
Hii ni kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah aliyeeleza kwamba Asmaa alimwuuliza Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) kuhusu kuoga hedhi. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) akamwambia:
((Atachukua mmoja wenu maji na mkunazi ajitwaharishe. Ajitwaharishe vizuri, kisha ajimiminie maji kichwani na ajisugue msuguo wa nguvu mpaka maji yafike katika mashina ya kichwa chake. Kisha atajimwagia maji na atachukua kitambaa ajisafishe nacho)).
Asmaa akasema: “Ni vipi atajisafisha nacho”?!
‘Aaishah akasema: “Subhaana Allaah! Unajisafisha nacho hivi”.
‘Aaishah akasema kana kwamba hataki lisikike: “Utafuatisha kwacho athari ya damu)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (314) na Muslim (332) na tamko ni lake].
2- Kufumua nywele ili maji yafike hadi katika mashina ya nywele.
Ni kutokana na neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) katika Hadiyth iliyotangulia:
“Kisha ajimwagie kichwani, na akisugue msuguo wa nguvu mpaka yafike kwenye ngozi ya kichwa”.
Na Hadiyth hii ni dalili ya kuwa haitoshi tu kujimwagia maji kama ilivyo katika josho la janaba, na hasahasa pakizingatiwa kuwa katika Hadiyth hiyo hiyo, bibi huyo alimuuliza kuhusu kuoga janaba naye akasema:
“Kisha ajimwagie kichwani, na akisugue mpaka yafike kwenye ngozi ya kichwa”.
Na hapa Rasuli hakutaja kusugua kwa nguvu ili kutofautisha kati ya josho la janaba na josho la hedhi.
Maulamaa wametofautiana kuhusiana na hukmu ya kufumua nywele wakati wa kuoga hedhi. Ash Shaafi’y, Maalik, na Abuu Haniyfah wanaona kwamba hilo ni jambo mustahabu na wala si lazima. [Al-Mughniy (1/227), Al-Muhallaa (2/38), Nayl Al-Awtwaar (1/311) na Tahdhiyb As-Sunan (1/293) pamoja na Al-‘Awn]. Dalili zao ni:
1- Hadiyth haielezei wazi juu ya ulazima wa kufumua nywele.
2- Hadiyth ya ‘Aaishah aliyoielezea kuhusiana na Hijjah ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) anaposema: “Ikanifikia Siku ya Arafah nami niko hedhini. Nikamlalamikia Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam), naye akaniambia: “Acha ‘Umrah yako, fumua nywele zako na hirimia Hajji..” [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (317) na Muslim (1211)].... ni kuwa, josho hili linahusiana na ihraam, na wala si josho la hedhi. Kwa hivyo, Hadiyth hii haifai kuwa ni dalili.
3- Hadiyth ya ‘Aaishah isemayo kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alimwambia wakati yuko hedhini: “Fumua nywele zako na uoge”.[Isnadi yake ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Maajah (641). Angalia pia Al-Irwaa (1/167).]…ni kuwa jibu la Hadiyth hii ni kama jibu la Hadiyth iliyopita, zote ni Hadiyth moja. Na tamshi la “uoge” wamelichukulia kwa maana ya josho la ihraam.
4- ‘Abdullah bin ‘Amri alipowaamuru wanawake kufumua nywele zao wakati wa kuoga, Bi ‘Aaishah alikipinga kitendo hicho.
Ama Maimamu wanaosema ni wajibu kufumua nywele wakati wa kuoga hedhi, hao ni pamoja na Al Imaam Ahmad, Al Hasan, na Twaawuus. Dalili zao ni Hadiyth hizo hizo zilizopita. Hayo yamehakikiwa na Al-’Allaamah Ibn Al-Qayyim (Rahimahul Laah) [Tahdhiyb As-Sunan (1/293 na kurasa zinazofuatia) pamoja na ‘Awn Al-Ma’abuwd]….. ambaye amezijibu pingamizi za Jamhuri kwa haya yafuatayo:
1- Wanaposema kuhusiana na Hadiyth ya ‘Aaishah wakati akihiji kwamba ilikuwa ni katika ihram, basi ni sahihi. Lakini josho la hedhi ndilo josho lililokaziwa zaidi kuliko majosho mengineyo yote, kwani Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam), ameamuru katika josho hilo mambo ambayo hakuyaamuru katika josho jinginelo kama vile kujitwaharisha kwa ukina na umakinifu zaidi. Na kwa ajili hiyo, alimwamuru azifumue nywele ikiwa ni kumzindusha juu ya ulazima wa kufanya hivyo, kwani kufanya hivyo, kunaondosha hadathi kwa njia fanisi zaidi.
2- Ama Hadiyth yake alipokuwa na hedhi isemayo: “Fumua nywele zako na uoge”… ni kuwa Hadiyth hii kusemwa katika wakati usio wa Hijjah kunawezekana sana na hususan tunapojua kwamba wapokezi wake wa Sanad ni katika waliohifadhi Hadiyth nyingi.
3- Ama ‘Aaishah kukipinga kitendo cha ‘Abdullah bin ‘Amri, bila shaka ilikuwa ni pale bwana huyo alipowaamuru akina mama kufumua nywele zao wakati wa kuoga janaba. Bibi ‘Aaishah alisema: “Anastaajabisha sana Ibn ‘Amri huyu!! Ati anawaamrisha wanawake wafumue nywele zao wakati wa kuoga!! Kwa nini basi asiwaambie wakanyoa nywele zao kabisa!! Mimi nilikuwa naoga pamoja na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) katika chombo kimoja..”[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (331), An Nasaaiy (1/203), na Ibn Maajah (604)].
Bila shaka ni kuwa Bi ‘Aaishah alikuwa akioga pamoja na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) janaba ambapo walikuwa wakiogea chombo kimoja, lakini si katika josho la hedhi!! Na juu ya msingi huu, ni wajibu kwa mwanamke afumue nywele zake hasahasa wakati wa kuoga hedhi na nifasi, na hili ndilo la akiba zaidi. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.
3- Kufuatilisha athari ya damu kwa kitambaa kilichotiwa miski au mafuta uzuri mengine yoyote.
Itakuwa ni vizuri atumie kitambaa au pamba iliyochovewa kidogo miski, kisha aiingize kwenye utupu wake baada ya kuoga. Pia atazisafisha vizuri sehemu zote zilizoingiwa na damu katika mwili wake, na hii yote ni kwa ajili ya kujitakasa na harufu mbaya. Haya yote yamethibiti katika Hadiyth ya ‘Aaishah iliyotangulia.
Mwanamke anaruhusiwa kufanya hivi hata kama yuko katika kipindi cha eda ya kufiwa na mumewe, au mtu wake mwingine kutokana na Hadiyth ya Umuu ‘Atwiyyah inayohusiana na mambo anayokatazwa mwenye eda isemayo: “Wala hatujitii manukato, wala hatuvai nguo za rangi rangi isipokuwa nguo za kawaida zisizovutia. Alitupa ruhusa wakati wa kujitwaharisha pale mmoja wetu anapooga hedhi tujitie kidogo mafuta uzuri”.
Haya yatakuja katika mlango wake katika kitabu hiki InshaAllaah Ta’alaa.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
056-Kukausha Viungo Baada Ya Kuoga
Alhidaaya.com [3]
Katika kuelezea huko nyuma namna Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alivyokuwa akioga, Hadiyth ya Maymuunah inasema: “Nikampa nguo, (na katika riwaya nyingine: taulo), naye hakuichukua huku akiikung’uta mikono yake miwili”. Hadiyth hii imetolewa hoja kwamba ni karaha kujifuta mwili baada ya kuoga. Madai haya hayana mashiko kwa haya yafuatayo:
1-Lililofanyika ni tukio la hali inayoweza kubeba tafsiri tofauti. Inawezekana kuwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) hakuichukua taulo kwa sababu ya jambo jingine lisilohusiana na ukaraha wa kujifuta, bali kwa jambo linalohusiana na taulo yenyewe, au inawezekana alikuwa na haraka na kadhalika.
2-Hadiyth hii ni dalili kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) ilikuwa ni kawaida yake kujifuta. Na kama haikuwa kawaida yake, basi asingeletewa taulo.
3-Kukung’uta maji kwa mkono wake ni dalili kwamba hakuna ukaraha wa kujifuta maji, kwani yote mawili ni tendo la kuondosha maji mwilini.
Kikhulasa tunasema: “Hakuna ubaya kujifuta maji baada ya kuoga. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
057-Masuala Yanayohusiana Na Kuoga
Alhidaaya.com [3]
- Si lazima kutawadha baada ya kuoga
Aliyeoga josho la kisharia na akataka kuswali, basi si lazima atawadhe hata kama alikuwa hajatawadha wakati akioga, kwani twaharisho la janaba linaondosha vile vile twaharisho la hadathi ndogo. Hii ni kwa vile vizuizi vya janaba ni vingi zaidi kuliko vizuizi vya hadathi ndogo. Hivyo basi, kidogo humezwa na kingi.
Imepokelewa na ‘Aaishah akisema: ((Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa hatawadhi baada ya kuoga janaba)). [Hadiyth Swahiyh kwa nyingine: Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhiy (107), An-Nasaaiy (1/137) na Ibn Maajah (579)].
Na katika riwaya nyingine: ((Anaoga na anaswali rakaa mbili, na wala simwoni akifanya wudhuu baada ya kuoga)). [Hadiyth Swahiyh kwa nyingine: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (250) na Ahmad (6/119)].
Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu Anhumaa) amesema: “Kama hukugusa utupu wako baada ya kumaliza kuoga, basi ni wudhuu gani ulio kamili zaidi ya kuoga?” [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na ‘Abdurraaziq katika Al-Muswannaf (1039)].
Ninasema:
“Juu ya haya, panazalikana nukta kwamba si lazima kwa mwenye kuoga janaba kunuwia kuondosha hadathi ndogo. Na haya ndiyo madhehebu ya Jamhuri na Ibn Taymiyah. [Al-Mabsuwtw (1/44), Ash-Sharh As-Swaghiyr (1/65), Al- Ummu (1/36), Majmu’u Al-Fataawaa (21/397) na Al-Muhalla (2/44)].
Ama Mahanbali, wao wanaona kwamba akinuwia twahara mbili, basi zote mbili zitamtosheleza. Lakini akinuwia kuoga janaba tu, basi hana ila hilo alilolinuwia tu. [Al-‘Uddat Sharh Al-‘Umdah (uk.48)].
- Yakikusanyika mawili yenye kuwajibisha kuoga kama hedhi na janaba, au janaba na ijumaa
Hapa josho moja tu litamtosheleza yote mawili kama atayanuwia yote mawili. Hii ni kauli ya Mafuqahaa wengi. [Al-Mughniy (1/292) bali imenukuliwa Ijma’a juu yake katika ((Rahmat Al- Umma Fiy Ikhtilaafi Al-Aimmah)) (uk 51). Na Ijma’a hii imetenguliwa kinyume na Ibn Hazm katika Al-Muhalla (uk.42-47). Mwanachuoni Arifu na Mweledi Al-Albaaniy amekubaliana naye katika Tamaam Al-Minnah (uk 126)].
- Mwanamke akiwa na janaba kisha akaingia hedhini kabla hajaoga
Kauli sahihi zaidi ya Maulamaa ni kuwa haimlazimu kuoga janaba, bali itamlazimu aoge janaba na hedhi kwa pamoja na ayanuwie yote mawili wakati damu ya hedhi inapokatika. Haya ni madhehebu ya Ahmad. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (299) na Muslim (321)].
Maulamaa wengine wanaona kwamba itamlazimu kuoga janaba, kisha hedhi inapokatika, ataoga josho la hedhi. Haya ni madhehebu ya ‘Atwaa, An-Nakh’iy na Al-Hasan.
Nao wengine wamesema kuwa itamlazimu aoshe utupu wake, kisha damu inapokatika aoge.
Kauli zote hizi mbili hazina dalili yoyote, na lililo sahihi na sawa zaidi ni kauli ya kwanza.
Lakini hili halimkatazi kuwa akitaka kuoga janaba au kuuosha utupu wake, kisha aoge damu inapokatika, basi atafanya hivyo na hakuna kosa lolote kwake, lakini si lazima.
- Inajuzu kwa mwanamume kuogea mabaki ya maji ya mkewe
Hili limekwishaelezewa kiuchambuzi katika mlango wa (Hukmu za Maji).
- Inajuzu mume kuoga pamoja na mkewe
Inajuzu wote wawili kuangaliana tupu zao bila ya ukaraha wowote. Imepokelewa na ‘Aaishah akisema:
((Nilikuwa naoga mimi na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) katika chombo kimoja [yeye ananiwahi, nami namwambia: niachie mimi niachie] wote tukiwa na janaba)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (299) na Muslim (321)].
- Haijuzu kuoga uchi hadharani
Kama akijisitiri watu wasimwone, basi hakuna ubaya. Tumekwishaitaja Hadiyth ya Maymuunah akisema: ((Nilimwekea Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) maji ya kuoga [na pazia yake] akaosha mikono yake miwili…..)).
Na imethibiti toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) kwamba Muusa Alayhi Ssalaam alioga uchi, hali kadhalika Ayyuub Alayhi Ssalaam. Lakini hili ni faraghani.
- Anayepatwa na hadathi wakati wa kuoga
Mwenye janaba akipatwa na hadathi kabla ya kumaliza kuoga, basi atakamilisha wala hatoanza upya, kwani hadathi haitengui josho, hivyo basi kuwepo kwake hakuathiri josho, bali ni juu yake kutawadha.
Na hii ni kauli ya Maulamaa wengi akiwemo ‘Atwaa na Ath-Thawry. Ibn Qudaamah na Ibn Al-Mundhir wamelikubali hilo.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
058-Masuala Yanayohusiana Na Mwenye Janaba
Alhidaaya.com [3]
- Inajuzu kwa mwenye janaba kuchelewesha kuoga
Si lazima kuoga mara tu baada ya kupata janaba ingawa kufanya haraka inakuwa ni bora zaidi na utakasifu zaidi.
Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah akisema kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alikutana naye katika njia moja ya Madiynah akiwa na janaba, naye akamhepa asimwone. Kisha alikwenda akaoga. Baadaye alikuja na Rasuli akamwuuliza:
((Ulikuwa wapi ee Abuu Hurayrah?))
Akajibu: “Nilikuwa na janaba, nikaona uzito kukaa nawe nikiwa sina twahara”. Akasema:
((سبحان الله، إن المسلم لا ينجس))
((Subhaana Llaah. Hakika Muislamu hanajsi)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (283) na Muslim (371)].
Na imepokelewa na Anas kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa akiwazungukia wakeze usiku mmoja nailhali wakati huo anao tisa. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (284) na Muslim (309)].
Kisha kuharakisha kuoga janaba, bila shaka kwa ngazi ya kwanza kabisa kunakuwa ni kwa ajili ya Swalaah. Na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa mara nyingine akilala kabla ya kuoga kama tutakavyoona baadaye.
- Inajuzu kwa mwenye janaba kulala kabla ya kuoga, kama atatawadha
Imepokelewa toka kwa ‘Aaishah akisema:
(( Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anapotaka kulala hali ya kuwa ana janaba, huosha utupu wake na hutawadha wudhuu wa Swalaah)).[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (288) na Muslim (305)].
Na ‘Abdullah bin Qays alimwuuliza akimwambia: “Ni vipi alikuwa akifanya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) akiwa na janaba? Je, alikuwa akioga kabla ya kulala, au akilala kabla ya kuoga?” ‘Aaishah akamjibu:
((Yote hayo alikuwa akiyafanya. Huenda akaoga kisha hulala, na wakati mwingine hutawadha kisha hulala)).
Akasema ‘Abdullaah bin Qays: “Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyefanya wasaa katika jambo”.[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (307)].
Na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alimwambia ‘Umar bin Al-Khatwaab alipomuuliza kuhusu janaba inayompata usiku:
((توضأ، واغسل ذكرك، ثم نم))
((Tawadha, osha dhakari yako, kisha lala)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (290) na Muslim (306)].
- Hakuna ubaya kwa mwenye janaba kusoma Qur-aan na kugusa Msahafu
Haya yamekwishaelezewa kwa ufafanuzi katika mlango wa wudhuu. Basi rejea huko.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
059-Je, Inajuzu Kwa Mwenye Hedhi Na Mwenye Janaba Kuingia Msikitini Na Kukaa Humo?
Alhidaaya.com [3]
Jamhuri ya Maulamaa wakiwemo Maimamu wanne na wengineo (kinyume na Adh-Dhwaahiriyyah) wanasema kuwa ni haramu kwa mwenye hedhi, mwenye nifasi na mwenye janaba kukaa Msikitini. Hayo yamepokelewa toka kwa Ibn ‘Abbaas na Ibn Mas-’oud . [Al-Majmu’u (2/184) na baada yake, Al-Mughniy (1/145) na Al-Lubaab Sharh Al-Kitaab (1/43). Ash-Shaafi’iy na Ahmad wamejuzisha kupita Msikitini bila kukaa, na Al-Muhalla (2/184) na baada yake].
Wenye kupinga hili wametoa dalili zifuatazo:
1- Ni Neno Lake Allaah (Subhaanahuu wa Ta’alaa):
((يا أيها الذين آمنوا لا تقربوا الصلاة وأنتم سكارى حتى تعلموا ما تقولون ولا جنبا إلا عابري سبيل حتى تغتسلوا))
((Enyi walioamini! Msikaribie Swalaah hali mmelewa, mpaka myajue mnayoyasema, wala hali mna janaba – isipokuwa mmo safarini – mpaka mkoge)). [An-Nisaai (4:43)]
Wanasema kuwa makusudio ya Swalaah hapa ni sehemu za kuswalia, nazo ni Misikiti. Na katika Aayah, mwenye janaba anazuiliwa kuingia humo isipokuwa tu kama ni msafiri. Kisha wakawaweka mwenye hedhi na mwenye nifasi katika kipimo kimoja na mwenye janaba!!
Wenye kujuzisha hili wamewajibu wakisema:
Hii ni moja kati ya taawili mbili za masalaf katika Aayah hii. Na taawili nyingine ni kuwa makusudio ni Swalaah yenyewe, na si Msikiti. Kwa hivyo basi, maana inakuwa: Na wala msikaribie Swalaah mkiwa na janaba ila baada ya kuoga, isipokuwa kama mko safarini, basi hapo, swalini kwa kutayamamu. Na kwa ajili hiyo, Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa) Anasema baada ya hapo:
((وإن كنتم مرضى أو على سفر....فلم تجدوا ماء فتيمموا))
((Na mkiwa wagonjwa, au mmo safarini………na msipate maji, basi ukusudieni mchanga safi)).
Kisha kuna mlahadha katika kipimo cha mwenye hedhi kwa mwenye janaba, kwani mwenye hedhi ana udhuru na hawezi kuoga kabla ya kutwaharika damu, na wala hawezi kuiondosha hedhi yake kinyume na mwenye janaba ambaye anaweza kuoga.
2- Ni Hadiyth ya Jisrah binti Dujaajah toka kwa ‘Aaishah kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((إنى لا أحل المسجد لحائض ولا جنب))
((Hakika mimi sihalalishi Msikiti kwa mwenye hedhi wala kwa mwenye janaba)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (232), Al-Bayhaqiy (2/442) na Ibn Khuzaymah (2/284). Tazama Al-Irwaa (193)].
Wenye kujuzisha wamejibu wakisema:
Hadiyth hii ni Dhwa’iyf, haifai kutolea hoja, kwani Hadiyth imezungukia kwa Jisrah, naye hawezi kuwa amepokea Hadiyth peke yake.
3- Hadiyth ya Ummu ‘Atwiyya kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) aliamuru kuwatoa vijizee vikongwe, waliotawishwa na wenye hedhi kwenda Swalaah ya ‘Iyd ili washuhudie kheri na du’aa ya Waislamu, na wenye hedhi hukaa kando na sehemu ya kuswalia. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (324) na Muslim (890)].
Wamesema: Na ikiwa hali ni hii kwa upande wa sehemu za kuswalia, basi Misikiti ni awla zaidi kuzuiwa.
Wenye kujuzisha wamejibu wakisema:
Makusudio ya “Al-Muswalla” katika Hadiyth ni Swalaah, kwani Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) na Maswahaba wake walikuwa wakiswali ‘Iyd uwanjani na si Msikitini, na ardhi yote ni twahara, na haijuzu kuzuiliwa huko kuihusu baadhi ya Misikiti tu bila ya mingine. Kisha imepokelewa Hadiyth hiyo hiyo kwa tamko:
((فأما الحيض فيعتزلن الصلاة))
((Ama wenye hedhi, hao hukaa mbali na Swalaah)).
Na Hadiyth hii iko katika Swahiyh Muslim na kwingineko.
4- Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: “Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa akielemeza kichwa chake kwangu nailhali yuko jirani na Msikiti, nami namweka sawa nikiwa hedhini.”
Wamesema: Akajizuilia kumweka sawa Msikitini kwa vile yeye ana hedhi.
Wenye kujuzisha wamejibu wakisema:
Hili walilolitolea dalili haliko wazi. Inawezekana kuwa hakuingia kutokana na sababu nyingine isiyokuwa hedhi kama kuwepo wanaume Msikitini na mfano wa hilo.
Kisha wenye kujuzisha mwenye hedhi na janaba kuingia Msikitini wametoa dalili hizi zifuatazo:
1- Ni utakasifu wa kiasili. Kwa vile hakuna makatazo yoyote sahihi, asili itakuwa ni uhalali. Muislamu ameruhusiwa kuswali mahala popote Swalaah inapomkuta.
2- Imethibiti kwamba washirikina waliingia Msikitini kwa kufungiwa humo na Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam). Na Allaah Amesema:
(( إنما المشركون نجس فلا يقربوا المسجد الحرام بعد عامهم هذا))
((Hakika washirikina ni najsi, basi wasiukaribie Al Masjidul Haraam baada ya mwaka wao huu)).[At-Tawbah (9:28)]
Ama Muislamu, yeye ni twahara kwa hali zote kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam):
((إن المسلم لا ينجس))
((Hakika Muislamu hanajsiki)). [Hadiyth Swahiyh: Imetangulia karibuni].
Hivyo basi, vipi azuiwe Muislamu kuingia, na kafiri aruhusiwe?!
Wenye kupinga wamejibu wakisema:
Sharia imefarakisha kati ya Muislamu na kafiri, na kwa kufarakisha huku, dalili imepatikana juu ya uharamu wa kukaa mwenye janaba na hedhi Msikitini, na imethibiti makafiri kuwekwa mahabusu humo!!. Na sharia inapofarakisha, haijuzu kusawazisha. Na hii ni qiyaas pamoja na matni, nayo imeharibika!!
Ninasema:
“Hii ikiwa imethibiti matni, nalo li wazi!”
3- Hadiyth ya ‘Aaishah isemayo: “Kijakazi mweusi alikuwa katika kitongoji cha Waarabu, wakamwacha huru. Kisha alikwenda kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) akasilimu. Akawa na kijihema ndani ya Msikiti.”[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (439)].
Wamesema: Mwanamke huyu anakaa ndani ya Msikiti wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam), na wanawake kawaida yao ni kupata hedhi, lakini Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) hakumzuia kutokana na hilo, wala hakumwamuru atoke nje ya Msikiti anapopatwa na hedhi.
Wenye kupinga wamejibu wakisema:
Ni dhahiri kwamba mwanamke huyu hakuwa na jamaa zake wala hifadhi isipokuwa Msikiti, akalazimika kuishi humo. Hivyo, hawezi kupimiwa na mwanamke mwingine. Na hili ni tukio la hali maalumu ambalo dalili ya wazi ya kuzuia haipingwi na tukio hili!!
4- Hadiyth ya Abuu Hurayrah kuhusiana na mwanamke aliyekuwa anasafisha Msikiti akafariki, na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) akamuulizia. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (458) na Muslim (956). Kwa wawili hawa kuna shaka kama alikuwa ni mwanamke au mwanamume. Lakini kwa tamko la Hadiyth iliyopo kwa Abuu Khuzaymah na Al-Bayhaqiy (4/48) kwa Sanad Swahiyh, inatilika nguvu kwamba ni mwanamke].
Mwanamke huyu hakulazimika kusafisha Msikiti nyakati zote, na wala Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) hakumkataza akae mbali na Msikiti wakati wa hedhi.
5- Hadiyth ya Abuu Hurayrah kuhusiana na Ahlus Swafah kulala ndani ya Msikiti wakati wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (6452) na At-Tirmidhiy (479).
Wenye kupinga wamejibu wakisema:
Ahlus Swafah hawakuwa na ndugu wala jamaa wala chochote kama inavyoonekana wazi katika matni ya Hadiyth.
6- Imethibiti katika Swahiyh kwamba Ibn ‘Umar alikuwa akilala Msikitini wakati ni kijana kapera. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (3530) na Muslim (2479)].
Na kijana mara nyingi anapolala huota, lakini hakukatazwa kukaa Msikitini wakati anapokuwa na janaba.
Wenye kupinga wamejibu wakisema: Haikuelezwa kwamba Rasuli alilijua hilo akamkubalia!!
Wenye kujuzisha wamejibu wakisema: Lau kama hilo lingefichika kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam), basi kwa Allaah Mtukufu halifichiki, na kwa hivyo, ilitakikana ajulishwe hilo kwa njia ya wahyi ili amkataze.
Imejibiwa: Si lazima wahyi uteremke ili kumjulisha kila kosa linalofanywa na Maswahaba. Ni mara ngapi Maswahaba wamefanya makosa kwa kutojua kwa dalili ya kuuliza kwao maswali wakati wa enzi ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam).
7- ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu Anha) alipopata hedhi wakati wa Hajji, Rasuli alimruhusu kufanya amali zote za Hajji isipokuwa kuzunguka Al-Ka’abah. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (1650). Itakuja kwenye mlango wa Hijjah].
Hii inaonyesha kwamba inajuzu kwake kuingia Msikitini, kwa kuwa mwenye kuhiji lazima aingie humo.
Wenye kupinga wamejibu wakisema:
Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alitaka kumfundisha kwamba inajuzu kwa mwenye hedhi kufanya amali zote za Hijjah isipokuwa twawaaf. Ama hukmu ya kuingia Msikitini, yeye anajua kwamba hilo ni marufuku kwani yeye ndiye msimulizi wa Hadiyth. Kisha Rasuli hakumkataza kuswali akiwa hedhini – na mahujaji wanaswali -. Je, inawezekana tukasema aswali na yeye yuko hedhini?!!
Ninasema: "Jibu hili lina mwelekeo ikiwa patathibiti Hadiyth inayokataza, nayo ni Dhwa’iyf".
8- Hadiyth ya 'Aaishah aliyesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) aliniambia: "Nipe kijijamvi toka Msikitini". Nikamwambia: "Nina hedhi". Akasema: Hedhi yako haiko mkononi mwako". [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (298), Abuu Daawuud (261), At-Tirmidhiy (134) na An-Nasaaiy (1/192)].
Hili linatuhisisha kwamba kijijamvi kilikuweko Msikitini, naye Rasuli akashikilia Bi 'Aaishah aingie Msikitini ili ampatie.
Wenye kupinga wamejibu wakisema:
Hadiyth imekuja kwa tamko jingine lisemalo: " Wakati Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) akiwa Msikitini alisema: ((Ee 'Aaishah! Nipatie nguo)) Akasema: Nina hedhi. Akasema: Hedhi yako haiko mkononi mwako."[Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (299) na An-Nasaaiy (1/192)].
Hadiyth hii iko wazi kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa Msikitini wakati 'Aaishah na kijijamvi alikuwa nje. Akamwamuru aingize mkono wake tu na si mwenyewe.
Ninasema: "Hadiyth hii inabeba hili na lile. Hivyo yatakikana kuipomosha isiwepo kwenye dalili za makundi mawili".
9- Athar ya 'Atwaa bin Yasaar aliyesema: "Niliwaona watu katika Maswahaba wa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) wakikaa Msikitini na wao wana janaba, wanapotawadha wudhuu wa Swalaah."[Isnadi yake ni Hasan: Imefanyiwa ”ikhraaj” na Sa’iyd bin Mansour katika Sunanih (4/1275)].
Ninasema: "Baada ya mapitio haya ya hoja za wenye kupinga na wenye kujuzisha kuhusiana na kukaa Msikitini kwa wenye janaba, hedhi na nifasi, linaloonekana ni kuwa dalili za wapingaji hazipandi kufikia uharamu wa kukata ingawa mimi ninapiga breki katika suala hili. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi".
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
060-Kutayammamu
Alhidaaya.com [3]
(Katika mlango huu, nilifaidika sana kutokana na utafiti uliotayarishwa na kaka yangu Twaariq Saalim (Allaah Amlipe jaza Yake ) kwa ajili ya kujipatia “Master” katika sharia).
Kutayammamu Kilugha Na Kisharia [Al-Majmu’u (2/238), Al-Mughniy (1/148) na Al-Mabsuwtw (1/106)]
Kilugha ni kukusudia. Ikisemwa: ،(تيممت فلانا، يممته، تأممته وأممته)inamaanisha: Nimemkusudia fulani.
Allaah Mtukufu Anasema:
((ولا تيمموا الخبيث منه تنفقون))
((Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya..)). [Al-Baqarah (2:267)].
Ama kisharia, ni kuukusudia mchanga wa juu ya ardhi kwa ajili ya kuhalalika yanayohalalishwa na wudhuu na kuoga.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
061-Usharia Wa Kutayammamu
Alhidaaya.com [3]
Kutayamamu kumethibiti katika Qur-aan, Hadiyth na Ijma’a.
1- Katika Qur-aan, ni Neno Lake Allaah Mtukufu:
((فلم تجدوا ماء فتيمموا صعيدا طيبا))
((na hamkupata maji, basi tayamamuni kwa vumbi lililo safi)). [Al-Maaidah (5:6)]
2- Katika Hadiyth, ni neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam):
((جعلت الأرض كلها لي ولأمتي مسجدا وطهورا، فأينما أدركت رجلا من أمتي الصلاة، فعنده مسجده وعنده طهوره))
(( Ardhi yote imefanywa kwangu na kwa umati wangu kuwa ni sehemu ya kuswalia na kujitwaharishia. Na popote itakapomkuta Swalaah yeyote katika umma wangu, basi hapo ndipo pake pa kuswalia na pake pa kujitwaharisha)). [Hadiyth Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad (2/222) kupitia ‘Amri bin Shu’ayb toka kwa babaye toka kwa babuye].
Na Hadiyth ya ‘Imraan bin Haswiyn, amesema:
“ Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) aliswali, kisha akamwona mtu mmoja kajitenga kando hakuswali na wengine. Akamwambia:
((يا فلان، ما منعك ألا تصلي مع القوم؟))
(( Ee fulani! Una nini usiswali na watu?)) Akajibu: “Ee Rasuli wa Allaah! Nimepata janaba na maji hakuna”. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) akamwambia:
((عليك بالصعيد فإنه يكفيك))
((Tumia vumbi, kwani linakutosheleza)).
Maji yalipopatikana, Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alimpa mtu huyo chombo cha maji akamwambia:
((اغتسل به))
(( Ogea)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (348) na Muslim (1535)].
3- Ama Ijma’a, Ibn Qudaamah katika Al-Mughniy (1/148) amesema:
“Umma wote kwa jumla umejuzisha kutayamamu”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
062-Ni Kipi Kinatosheleza Tayammumi?
Alhidaaya.com [3]
Kutayamamu kunakuwa ni badala ya wudhuu na josho la janaba wakati maji yanapokosekana au kuwa vigumu kuyatumia. An-Nawawiy amesema:
“Haya ndiyo madhehebu yetu. Na hivi ndivyo walivyosema Maulamaa wote katika Maswahaba, Taabi’iyna na waliokuja baada yao isipokuwa ‘Umar bin Al-Khattwaab, ‘Abdullaah bin Mas-’oud na Ibrahiym An-Nakhi’y ambaye ni Taabi’iy. [Imekuja katika Swahiyh Al-Bukhaariy (345) na Muslim (796) kuwa Ibn Mas-’oud amekataza kutayamamu kwa ajili ya janaba na kuwa Abu Muusa alimpinga kwa Aayah.
Ninasema: “Huenda Ibn Mas-’oud kulipinga hilo, kumetolewa juu ya yale yaliyo sahihi kwake toka kwa At-Twabariy (9606) wakati alipolifasiri Neno Lake Allaah Mtukufu: ((أو لامستم النساء)) akisema kuwa الملامسة ni chini ya kujamii].
Hawa wamelizuia, yaani wamezuia kutayamamu kwa ajili ya hadathi kubwa”.
Ibn As-Swibaagh na wengine wamesema kuwa inasemekana kuwa ‘Umar na ‘Abdullaah waliachana na msimamo wao.
Jamaa zetu hawa na Jamhuri wametoa dalili ya Kauli Yake Allaah Mtukufu:
((إذا قمتم إلى الصلاة فاغسلوا وجوهكم))
((Mnaposimama kuswali, basi osheni nyuso zenu)).
Hadi Neno Lake:
((وأن كنتم جنبا فالطهروا))
((Na mkiwa na janaba, basi jitwaharisheni)).
Kisha Allaah Mtukufu Akasema:
((فلم تجدوا ماء فتيمموا))
((na hamkupata maji, basi tayamamuni)).
Na hili linarejea kwa wote wawili; asiye na wudhuu na mwenye janaba. [Al-Majmu’u (2/240)].
Ninasema:
“Kuna dalili nyingine juu ya usharia wa kutayamamu kwa ajili ya hadathi kubwa. Ni Neno Lake Allaah Mtukufu:
((أو جاء أحد منكم من الغائط أو لامستم النساء فلم تجدوا ماء فتيمموا صعيدا طيبا))
((Au mmoja wenu ametoka chooni, au mmewagusa wanawake na msipate maji, basi ukusudieni mchanga safi)). [An-Nisaa (4: 43)].
Makusudio ya kugusana hapa ni tendo la kujamii kwa mujibu wa kauli ya mjumuiko wa Maulamaa akiwemo Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu Anhu). [Tafsiyr At-Twabariy (9583) kwa Sanad Swahiyh kutoka kwake].
Kisha kuna Hadiyth Swahiyh zilizopokelewa toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) zinazofahamisha kuwa kutayamamu hutosheleza janaba. Kati ya Hadiyth hizo ni:
1- Hadiyth tuliokwisha ielezea ya ‘Imraan bin Haswiyn wakati Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alipomwambia mwenye janaba:
((عليك بالصعيد فإنه يكفيك))
((Tumia mchanga, kwani unakutosha)). [Imekubaliwa na Al Bukhaariy na Muslim. Imeelezewa karibuni].
2- Hadiyth ya ‘Ammaar bin Yaasir, amesema: “Nilipata janaba, kisha nilijigaragaza mchangani, nikamjulisha Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) juu ya hilo, akaniambia:
:إنما كان يكفيك هكذا))
((وضرب يديه على الأرض، ومسح وجهه وكفيه
((Hakika ilikuwa inakutosha hivi:
Akapiga mikono yake miwili juu ya ardhi, akaosha uso wake na viganja vyake viwili)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukaariy (338) na Muslim (798)].
Je, Maiti Hutayamamishwa Maji Yakikosekana?
Maiti hutayamamishwa kama aliyehai maji yakikosekana, kwani kuoshwa maiti ni lazima. Tumekwishaeleza nyuma kuwa mchanga hutwaharishiwa maji yakikosekana. [Angalia Al-Muhalla (2/158)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
063-Hali Ambazo Kutayammamu Kunaruhusiwa
Kutayamamu kunaruhusika katika hali mbili:
1- Maji yanapokosekana, ni sawa safarini au mjini.
2- Inapokuwa vigumu kuyatumia. Na hili lina picha mbalimbali zitakazoelezewa baadaye InshaAllaah.
Allaah Mtukufu Anasema:
((وإن كنتم جنبا فالطهروا وإن كنتم مرضى أو على سفر أو جاء أحد منكم من الغائط أو لامستم النساء فلم تجدوا ماء فتيمموا))
((Na mkiwa na janaba, basi jitwaharisheni, na mkiwa wagonjwa au mkiwa safarini, au ametoka mmoja wenu chooni, au mmewagusa wanawake na hamkuyapata maji, basi tayamamuni)). [Al-Maaidah (5:6)].
Si Lazima Safari Iwe Ndefu Ili Msafiri Apate Ruksa Ya Kutayammamu
Endapo maji yatakosekana, itampasa msafiri atayamamu sawasawa ikiwa safari ni ndefu au fupi katika kauli mbili Swahiyh zaidi za Maulamaa, kwa vile safari katika Aayah Tukufu haikuainishwa kama ni fupi au ndefu. [Al-Muhalla (2/116) na Al-Mughniy (1/148)].
Ushahidi wa hilo ni:
1- Hadiyth ya ‘Aaishah (Allaah Amridhie), amesema:
“Tulitoka na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam) katika baadhi ya safari zake. Tulipokuwa Baydaa au Bidhaat Al-Jaysh, kidani changu kilikatika. Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam) alipiga kambi ili kukitafuta, na watu nao wakapiga kambi pamoja naye, hawako sehemu yenye maji na maji hawana. Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam) akalala mpaka akapambaukiwa bila kuwepo maji. Na hapo Allaah Mtukufu Akateremsha Aayah ya kutayamamu:
((فتيمموا صعيدا))
((Basi ukusudieni mchanga)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (334) na Muslim (764)].
2- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Umar kwamba yeye alitokea Al-Juruf na alipofika Al-Mirbad alitayamamu. Alipangusa uso wake na mikono yake miwili na akasali alasiri. Kisha aliingia Madiynah nailhali jua limepanda. Hakurejesha Swalaah. [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Maalik (Twahara uk.73) na Al-Bayhaqiy (1/224)].
Ash-Shaafi’iy amesema: Al-Juruf ni sehemu karibu na Madiynah.
Si Lazima Safari Iwe Halali
Ni sahihi kuwa msafiri hutayamamu katika safari yake (maji yanapokosekana) sawasawa ikiwa alisafiri safari ya halali au safari ya haramu. Kwa kuwa kutayamamu ni faradhi, haijuzu kuacha kinyume na ruksa nyinginezo. Na kwa vile kutayamamu ni hukmu isiyohusiana na safari tu, imeruhusiwa katika safari za haramu kama kupukusa juu ya khufu siku na usiku wake. [Al-Muhalla (2/137), Al-Mughniy (1/150) na Al-Awsatw (2/32)].
Ninasema:
“Na kwa vile faradhi haipomoki kwa msafiri, imekuwa ni lazima kwake afanikishe sharti ya kusihi kutayamamu, lakini madhambi atayapata kutokana na safari yake ya haramu. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
064-Mwenye Maji Kidogo Ambayo Hayatoshi Ila Kwa Baadhi Ya Viungo Vyake
Katika suala hili, Maulamaa wamehitilafiana katika mielekeo miwili:
Wa kwanza:
Ataosha viungo awezavyo kuviosha na vilivyobaki atatayamamu. Haya ni madhehebu ya Ahmad, Ibn Hazm na moja kati ya kauli mbili za Ash-Shaafi’iy. [Al-Muhalla (2/137), Al-Mughniy (1/150) na Al-Awsatw (2/32)].
Hoja yao ni Neno Lake Allaah Mtukufu:
((فاتقوا الله ماستطعتم))
((Mwogopeni Allaah kiasi muwezavyo)). [At-Taghaabun ( 64:16)].
Na kauli yake Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam):
((إذا أمرتكم بأمر فائتوا منه ماستطعتم))
((Nikiwaamuruni jambo, basi lifanyeni kiasi muwezavyo)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (7288) na Muslim (3199)].
Ibn Hazm amesema:
“Na huyu anaweza kuviosha baadhi ya viungo vyake vya wudhuu au kuoga sehemu ya kiwiliwili chake, lakini hawezi sehemu zilizosalia, hapo ikafaradhishwa kwake aoshe kwanza viungo anavyoweza kuviosha katika wudhuu au josho hadi kiungo atakachokifikia, na maji yanapoisha, itamlazimu kutayamamu kwa viungo vilivyosalia kwa kulazimika. Na hilo ni lazima, kwani hana maji mengine ya kujitwaharishia. Basi ni wajibu kwake kufidia kwa mchanga kama Alivyoamuru Allaah Mtukufu”.
Wa pili:
Atatayamamu tu moja kwa moja. Mwelekeo huu ni madhehebu ya Abuu Haniyfah, Maalik na moja ya kauli mbili za Ash Shaafi’iy. Pia mjumuiko wa Masalaf wamesema hili hili. [Al-Majmu’u (2/312) na Majmu’u Al-Fataawaa (21/453)].
Wamesema:
“Haikusanywi pamoja twahara ya maji na twahara ya tayamumi; ni ima hii au ile”.
Ibn Al-Mundhir ametoa dalili kuunga mkono mwelekeo huu akisema: [Al-Awsatw ya Ibn Al-Mundhir (2/34)].
“Allaah Mtukufu Anasema:
((وإن كنتم جنبا فاطهروا))
((Mkiwa na janaba, basi jitwaharisheni))
Amewajibisha kwa mwenye janaba kuoga kwa maji, na kama hakuyapata, basi atayamamu. Na Amewajibisha kwa mwenye kumfanyia mkewe dhwihaar, amwache huru mtumwa, na kama hakumpata, basi afunge miezi miwili. Na alipokuwa mwenye kumiliki sehemu ya mtumwa lakini kiilivyo ni kama hammiliki na Allaah Akamfaradhishia kufunga, basi mwenye maji ya kuoshea baadhi ya viungo vyake tu, amekuwa ni kama asiyenayo Akamfaradhishia kutayamamu. Na jibu kuhusu mwenye kufanya tamattui na ana fedha pungufu za kununulia mnyama wa kuchinja, au aliyevunja kiapo chake na uwezo wake uko chini ya kuwalisha masikini kumi, basi hukmu yao ni kama ya hao tuliowataja.
Ama kufaradhiwa faradhi mbili kwa hao tuliowataja, hilo halijuzu.”
Ninasema:
“Na huenda lililo dhahiri zaidi ni kuwa atatayamamu tu moja kwa moja ili kutokusanya kati ya asili na badali. Pia ni kwa vile, lau kama hana maji ya kutosha kwa viungo vyake vyote vya wudhuu au vya josho na akatumia badali (kutayamamu), basi anakuwa amefanya lile aliloliweza katika Amri ya Allaah na Rasuli Wake pia. Na linalonidhihirikia mimi ni kuwa huyu ambaye anatayamamu baada ya kuosha baadhi ya viungo vyake, bila shaka anakuwa ameipata twahara kwa kutayamamu tu, na wala si kwa kuosha na kutayamamu kwa pamoja, kwani kuosha baadhi ya viungo vyake kunakuwa hakuna maana yoyote baada ya kuwa na uhakika kwamba maji aliyonayo hayamtoshi. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
Mwenye Maji Akihofia Kukabiliwa Na Kiu Yeye Mwenyewe, Au Mwenzake, Au Mnyama Wake Kama Atayatumia
Ibn Al-Mundhir amesema: [Al-Awsatw (2/28)]
“Maulamaa tunaowajua vyema, wote wamekubaliana kuwa msafiri akijihofia nafsi yake kiu naye ana kiasi kidogo tu cha maji ya kujitwaharishia, basi atayabakisha maji yake kwa ajili ya kunywa, na atatayamamu”.
Na Ibn Qudaamah amesema: [Al-Mughniy (1/165). Tazama Al-Majmu’u (2/281)]
“Mwenye kuhofia wanyama wake, huhofia kupotea mali yake. Mfano wake ni kama mtu kuyapata maji, na kati yake na maji hayo kukawa na mwizi anayeweza kupora chochote katika mali yake, au mnyama mkali anayeweza kumdhuru mnyama wake. Na kama akimkuta mwenye kiu anayemhofia kufa, itamlazimu amnyweshe na yeye atatayamamu”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
065-Ikiwa Kuna Maiti, Mwenye Janaba, Mwenye Hedhi na Mwenye Najsi Mwilini, Na Maji Yaliyopo Hayatoshi Ila Kwa Mmoja Wao Tu, Nani Atapewa Kipaumbele?
1- Ikiwa maji ni milki ya mmoja wao, basi atakuwa yeye ndiye mwenye haki nayo zaidi. Hili ndilo lililopitishwa na Jamhuri. [Al-Majmu’u (2/316) na Al-Mughniy (1/170)].
2- Ikiwa hayamilikiwi na yeyote kati yao, basi hukmu ni kama ifuatavyo:
(a) Maiti ana haki zaidi kuliko hao wenye hadathi kama walivyosema Ash-Shaafi’iy na Ahmad. [Al-Majmu’u (2/318) na Al-Mughniy (1/170)].Hii ni kwa sababu mbili:
Sababu ya kwanza ni kuwa huu ndio mwisho wa maiti. Kwa ajili hiyo, amehusishwa na twahara timilifu zaidi kati ya mbili. Walio hai kwa hali yoyote, watayapata maji baadaye.
Sababu ya pili ni kuwa makusudio ya kumwosha maiti ni kumsafisha, na hili haliwezekaniki kwa mchanga, wakati ambapo makusudio ya kujitwaharisha kwa walio hai ni kupata idhini ya kuswali, na hili linapatikana kwa kutayamamu.
(b) Mwenye najsi ndiye mwenye haki zaidi ya maji kuliko wenye hadathi. Wameyasema haya Mashaafi’iy na Mahanbali. [Al-Mughniy (1/171) na Al-Majmu’u (2/319)]
An-Nawawiy amesema: “Kwa sababu hakuna badali ya twahara yake”.
(c) Mwenye hedhi ana haki zaidi kuliko mwenye janaba. Hii ni kutokana na uzito wa hadathi yake, na kwa kuwa yeye anaitekeleza haki ya Allaah Mtukufu na haki ya mumewe ya kuruhusika kumwingilia.
Katika suala hili kuna mvutano. Kwa Mahanbali na Mashaafi’iy kuna njia mbili. Na kwa Mashaafi’iy kuna njia ya tatu, nayo ni kuwa wako sawasawa na watapiga kura. [Al-Mughniy (1/171) na Al-Majmu’u (2/319)]
(d) Akikusanyika mwenye janaba na mwenye hadathi, maji yaliyopo yatatizamwa. Ikiwa yatatosha kuogea janaba, basi mwenye janaba atakuwa na haki zaidi. Na kama hayatoshi, basi mwenye hadathi. [Yaliyotangulia].
(e) Akikusanyika maiti na mwenye najsi mwilini, hapa kuna mvutano. [Al-Mughniy (1/170) na Al-Majmu’u (2/318)]
Atakayekubaliana na sababu tuliyoitaja ya kumtanguliza maiti kabla ya mwenye hadathi, basi maji ni haki ya maiti.
Na atakayekinaika kuwa mwenye najsi mwilini hana badali nyingine ya kutwaharika, basi atakuwa ndiye mwenye haki zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
066-Kutayammamu Mgonjwa Ambaye Anajihofia Madhara Kama Atatumia Maji
Jamhuri ya Maulamaa (Abu Haniyfah, Ash-Shaafi’iy, Ahmad, Ibn Hazm na wengineo), wanaona kuwa ikiwa mgonjwa atajihofia nafsi yake kuhiliki ikiwa atatumia maji, basi inajuzu kwake kutayamamu kwa Neno Lake Allaah Mtukufu:
((وإن كنتم مرضى أو على سفر.....فلم تجدوا ماء فتيمموا))
((Na mkiwa wagonjwa au safarini……na hamkupata maji, basi tayamamuni)). [Al-Maaidah (5:6)].
Amesema Mujaahid: “Hii ni kwa mgonjwa aliyepatwa na janaba. Akijihofia nafsi yake, basi ana ruhusa ya kutayamamu kama msafiri anapokosa maji”. [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na ‘Abdul Raazik kwa Sanad Swahiyh]. Na kwa Neno Lake Allaah Mtukufu:
((ولا تقتلوا أنفسكم))
((Na wala msiziue nafsi zenu)).[An-Nisaai (4:29)].
Hii ni katika wakati ambapo ‘Atwaa na Al-Hasan wamekataza mgonjwa kutayamamu isipokuwa katika hali ya kukosekana maji tu kutokana na Aayah inavyosema. [‘Abdul Raazik amelipokea hili katika Al-Muswannaf (861) kwa Sanad Swahiyh].
Na jibu la hili ni kuwa Aayah ni hoja ya kutupa sisi nguvu, na taqdiyr yake ni:
((Mkiwa wagonjwa; mkashindwa au mkahofia kutumia maji, au mkawa safarini na hamkupata maji, basi tayamamuni)). [Al-Majmu’u (2/330)].
Mgonjwa Akihofia Kuzidi Ugonjwa Wake Au Kukawia Kupona Kwa Kutumia Maji, Je Atatayammamu?
Jamhuri ya Maulamaa (Abu Haniyfah, Maalik, Ash-Shaafi’iy katika moja ya kauli zake mbili na Ibn Hazm), wanaona kwamba si lazima mgonjwa ahofie kuhiliki ndipo atayamamu, bali hata yule ambaye wudhuu unamwongezea ugonjwa au unachelewesha kupona, basi atayamamu kutokana na ujumuishi wa Aayah ya Suwrat Al-Maaidah. [Al-Mabsuwtw (1/121), Al-Majmu’u (2/331), Al-Muhalla (2/116), Al-Awsatw (2/26) na Majmu’u Al-Fataawaa (21/399)].
Na pia kutokana na Kauli Yake Allaah Mtukufu:
((يريد الله بكم اليسر ولا يريد منكم العسر))
((Allaah Anawatakieni wepesi na wala Hawatakieni uzito)). [Al-Baqarah (2:185)]
Ibn Hazm amesema: “Dhiki na uzito vimeondoka (na Sifa zote njema ni za Allaah) sawasawa ikiwa ugonjwa utazidi au haukuzidi. Kadhalika, ikiwa atahofia kuzidi ugonjwa, basi hilo ni uzito na dhiki vilevile”.
Na imepokelewa toka kwa Ahmad na Ash-Shaafiiy katika moja ya kauli zake mbili kwamba ili kuruhusika kutayamamu, ni lazima iwepo hofu ya kudhurika. Na madhehebu ya Jamhuri ndio sahihi zaidi. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
067-Nini Atafanya Mwenye Jeraha?
Alhidaaya.com [3]
Suala hili lina matawi juu ya asli. Ni kuwa, je, inawezekana kukusanya kati ya asili na badali, yaani baina ya wudhuu au ghusli na tayammumi?
Suala hili lishazungumziwa kwa uchambuzi. [Angalia ukurasa wa 192 wa Kitabu hiki].
Waliopinga kukusanya kati ya viwili (asili na badali) kama Abuu Haniyfah na Maalik, nalo ndilo tulilolitilia nguvu katika mlango uliopita, wao wanaangalia kilicho kichache zaidi kwa kilicho kingi zaidi. Ina maana kuwa endapo sehemu kubwa ya mwili ina majeraha, basi mtu atatayamamu bila kuviosha viungo vizima vilivyobakia. Na ikiwa sehemu kubwa ya mwili ni nzima, atauosha mwili na ataacha sehemu yenye majeraha. [Al-Mabsuutw (1/112) na Al-Majmu’u (2/333)].
Ama wale waliojuzisha kukusanya kati ya ghusli na tayammumi, wanasema kuwa ataosha sehemu nzima ya mwili na yenye majeraha ataifanyia tayammumi. Ash-Shaafi’y na Ahmad wamelisema hili, na Shaykh wa Uislamu anaonekana kama amelikhitari. [Al-Mughniy (1/162), Al-Majmu’u (1/162) na Majmu’u Al-Fataawaa (21/466)].
Ninasema: “Inavyoonekana ni kuwa rai ya kwanza ndio sahihi zaidi kama ilivyotangulia, na hakuna katika mlango huu Hadiyth yoyote Swahiyh iliyopokelewa toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam). Lakini pamoja na haya, kuna Hadiyth ya Jaabir iliyopokelewa. Anasema: “Tulitoka kwenda safari. Mtu mmoja kati yetu alijeruhiwa na jiwe kichwani. Alipolala aliota usingizini (akamwaga), na alipoamka aliwauliza wenzake: “Je, mwaweza kunipatia idhni ya kutayamamu? Wakasema: “Hatuwezi kukuruhusu kutayamamu nawe una uwezo wa kuyatumia maji.” Mtu yule alioga akafa. Tulipokuja kwa Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam) alijulishwa hilo naye akasema:
((Wamemwua, Awaue Allaah! Kwa nini wasiulize kama hawajui? Teguzi la asiyejua ni kuuliza. Hakika ilikuwa inamtosheleza tayammumi; akifunge kidonda chake kwa kitambaa, kisha apukuse juu yake, na sehemu iliyobaki ya mwili aioshe)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (336), Ad-Daara Qutwniy (1/190) na Al-Bayhaqiy (1/237). Sanad yake ni Dhwa’iyf. Al-AlBaaniy ameifanya Hadiyth Hasan kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas iliyopo kwa Abuu Daawuud (337) na Ibn Maajah (572). Hadiyth hii ni “Munqatwi-’i” na haifai kutolewa ushahidi].
Hadiyth hii ni Dhwa’iyf. Walioidhoofisha ni Al-Bayhaqiy, Ibn Hazm na wengineo ingawa Al-Albaaniy ameifanya kuwa Hasan.
Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Umar, akisema: “Endapo jeraha halikufungwa, basi ataosha sehemu za pembeni yake tu, na hatoliosha jeraha lenyewe.” [Isnadi yake ni Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bayhaqiy].
Na imepokelewa kwa njia sahihi toka kwa ‘Ubayd bin ‘Umayr kuhusiana na mtu aliyepatwa na janaba akiwa na jeraha. Amesema: “Aoshe sehemu ya pembeni tu, na maji yasikurubie jeraha lake”. [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na ‘Abdul Raaziq (865)].
Na hili liko sanjari na madhehebu ya Abuu Haniyfah na Maalik, nalo ndilo lenye nguvu. Na Allaah Ndiye Mjuzi zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
068-Anayechelea Kudhurika Kwa Maji Baridi, Je Anaweza Kutayammamu Akiwa Na Janaba?
Alhidaaya.com [3]
Anayejihofia kufa kutokana na maji baridi, inajuzu kwake kutayammamu kwa vile anakuwa katika ngazi ya mgonjwa. Huu ni mwelekeo wa Jamhuri ya Maulamaa. [Al-Mabswutw (1/122), Al-Majmu’u (2/330), Al-Istidhkaar (3/173), Al-Mughniy (1/163), Al-Muhalla (2/134) na Majmu’u Al-Fataawaa (21/399)].
Hoja yao katika hili ni:
1- Neno Lake Allaah Mtukufu:
((ولا تقتلوا أنفسكم إن الله كان بكم رحيما))
((Wala msiziue nafsi zenu, hakika Allaah ni Mrehemevu mno kwenu)). [An-Nisaa (4:29)].
2- Ni yaliyopokelewa toka kwa ‘Amri bin Al-‘Aas kwamba wakati alipopelekwa katika vita vya Dhaatu As-Salaasil alisema: “Niliota katika usiku wa baridi kali, nikahofia kufa kama nitaoga. Nikatayammamu, kisha nikaswali na wenzangu Swalaah ya Alfajiri. Tulipowasili kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam), wao walimweleza hilo, akasema:
((Ee ‘Amri! Hivi umeswali na wenzako ukiwa na janaba?))
Nikamwambia: “Nililikumbuka Neno la Allaah Mtukufu:
((ولا تقتلوا أنفسكم إن الله كان بكم رحيما))
nikatayammamu kisha nikaswali. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam) akacheka, na hakusema neno)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (334), Ahmad (3/203), Ad-Daara Qutwniy (1/178), Al-Haakim (1/177) na Al-Bayhaqiy (1/225). Sanad na matni yake zimetiwa doa. Al-Albaaniy katika Al-Irwaa (1/182) amesema ni Swahiyh].
Hadiyth hii ina mvutano, na lenye nguvu ni kuwa ni dhwa’iyf. Lakini pamoja na hivyo, kaida za kisharia zinaitolea ushahidi. Vile vile mwelekeo huu unaungwa mkono na Neno Lake Allaah Mtukufu:
((ما يريد الله ليجعل عليكم من حرج))
((Hataki Allaah kuwafanyieni uzito)). [Al-Maaidah (5:6)].
Na hii ni baada ya kutaja tayammumi. Kana kwamba Ameashiria kuwa tayammumi inaruhusika panapokuwepo uzito wa kutumia maji. Na hakuna shaka kuwa ubaridi mkali wa maji ni katika uzito huo. Lakini inatakikana kutanabahisha kuwa kutayammumi hakuruhusiwi – katika hali hii – ila baada ya kushindwa kupasha maji moto. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
069-Je Anaweza Kutayammamu Mtu Ambaye Wakati Umekuwa Mfinyu Kwake Na Wakati Wa Swalaah Utampita Kama Atatumia Maji?
Alhidaaya.com [3]
Kuna kauli mbili za Maulamaa katika suala hili:
Ya kwanza:
Haijuzu kutayammamu hata kama wakati utampita. Limesemwa hili na Mashaafi’iy, Mahanbali na Abuu Yuusuf. [Al-Mughniy (1/166), Al-Majmu’u (2/280), Al-Istidhkaar (3/171) na Tamaam Al-Minnah (uk.132)]
Dalili zao ni:
1- Neno Lake Allaah Mtukufu:
((إذا قمتم إلى الصلاة فاغسلوا وجوهكم.... فلم تجدوا ماء فتيمموا))
((Mnaposimama kuswali, basi osheni nyuso zenu….na hamkupata maji, basi tayammamuni)). [Al-Maaidah (5:6)].
Wanasema: “Hapa kukosa maji kumefanywa kuwa ni sharti ya kuhalalika kutayammamu”.
2- Hadiyth ya Abuu Hurayrah ikiwa Marfu’u:
((لا يقبل الله صلاة أحدكم إذا أحدث حتى يتوضأ))
((Allaah Hakubali Swalaah ya mmoja wenu anapokuwa na hadathi mpaka atawadhe)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (6954) na Muslim (526)].
3- Hadiyth ya Ibn ‘Umar ikiwa Marfu’u:
((لا تقبل الصلاة بغير طهور ولا صدقة من غلول))
((Swalaah haikubaliwi bila ya wudhuu, wala swadaqah ya mali haramu)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (524), At-Tirmidhiy (1) na Ibn Maajah (272)].
Hapa mtu kaamuriwa kutumia maji. Ikiwa ataiwahi Swalaah, basi vizuri, na kama itampita kwa kuzembea kwake, basi hayo amejitakia mwenyewe.
Ya pili:
Anaweza kutayammamu na kuswali kabla wakati haujampita.
Wamelisema hili Ahlu Rra’ayi (Abuu Haniyfah na wenzake), Al-Awzaa’iy, Maalik, Ibn Hazm. Shaykh wa Uislamu amelikhitari hili. [Al-Mughniy (1/166), Al-Muhalla (2/117), Majmu’u Al-Fataawaa (21/439,456) na Al-Awsatw (2/30)].
Mahanafi wameliwekea hili sharti ya kuwa ni lazima liwe kwa Swalaah ambayo haina badala yake kama Swalaah ya maiti. [Al-Mughniy (1/166), Al-Muhalla (2/117), Majmu’u Al-Fataawaa (21/439,456) na Al-Awsatw (2/30)].
Hoja zao ni:
1- Hadiyth ya Abu Juhaym Al-Answaariy, amesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam) alikuja akitokea upande wa kisima cha Jamal. Mtu mmoja alikutana naye akamsalimia. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam) hakuitikia mpaka alipokwenda ukutani, akapukusa uso na mikono yake. Kisha akamjibu salamu”. [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (337) na Muslim (800)].
Wamesema: “Na hii ni asili katika kujuzu kutayammamu kwa ajili ya kuhofia kupitwa na faradhi”.
2- Ibn ‘Abdul Barri amesema katika Al-Istidhkaar (3/171):
“Kila ambaye hakuyapata maji na akachelea kupitwa na Swalaah, anaweza kutayammamu kama ni mgonjwa au msafiri kwa matni. Na kama ni mkazi na mzima, basi ni kwa maana. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi".
3- Shaykh wa Uislamu amesema:
“Kauli sahihi zaidi ya Maulamaa ni kuwa atatayammamu kwa kila lile analolichelea kupitwa nalo kama Swalaah ya maiti, Swalaah za idi mbili na kadhalika. Swalaah kwa kutayammamu ni bora zaidi kuliko kuiacha ipite..”
Na amesema tena:
“Vile vile, kama hakuweza kuswali Swalaah ya Jamaa ya faradhi ila kwa kutayammamu, basi ataiswali kwa kutayammamu”.
Ninasema:
“Na huenda lililo wazi zaidi ni kuwa mtu atatayammamu ili aiwahi Swalaah, kwani tayammumi imewekwa kwa ajili ya kuuwahi wakati wa Swalaah na kuchelea kupitwa ili kuulinda wakati. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
070-Anayeamka Usingizini Muda Wa Swalaah Ukawa Mfinyu, Je Atayammamu Ili Auwahi Wakati?
Alhidaaya.com [3]
Kuna mielekeo miwili katika suala hili mfano wa ile ya suala lililotangulia: [Al Awsatw (2/30), Al Muhalla (2/117), na Majmuu Al-Fataawaa (22/35-36)]
Wa kwanza:
Atatayammamu na ataswali ndani ya wakati. Hili limesemwa na Maalik, Al-Awzaa’iy, Ath-Thawriy na Ibn Hazm.
Wa pili:
Ataoga na ataswali na hata baada ya kutoka wakati. Huu ni msimamo wa Jamhuri, na Shaykh wa Uislamu ameukhitari.
Msimamo huu ndio wenye nguvu zaidi, kwani wakati kwa mwenye kulala ni pale anapoamka.
Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi wa Aalihii wa Sallam) amesema:
((أما إنه ليس في نوم تفريط، إنما التفريط على من لم يصل الصلاة حتى يجئ وقت الصلاة الأخرى، فمن فعل ذلك فليصلها حين ينتبه بها))
((Ama hakika, hakuna uzembe usingizini, bali uzembe ni kwa yule ambaye hakuswali mpaka ukaingia wakati wa Swalaah nyingine. Mwenye kufanya hivyo, basi aiswali anapoikumbukia)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (1532) na Abuu Daawuud (437).
Na imekuja katika Swahiyh Mbili katika Hadiyth Marfu’u iliyopokelewa na Abuu Hurayrah: “
((من نسي صلاة فليصلها إذا ذكرها لا كفارة لها إلا ذلك))
((Aliyeisahau Swalaah, basi aiswali anapoikumbuka, hakuna kafara yake ila hilo)).
Na katika tamshi la Muslim katika Hadiyth ya Anas:
((من نسي صلاة أو نام عنها فكفارتها أن يصليها إذا ذكرها))
((Aliyeisahau Swalaah, au akalala ikampita, basi kafara yake ni kuiswali anapoikumbuka))].
Ibn Taymiyah amesema (22/35):
“Na kama ni hivyo, kama ataamka kabla ya kuchomoza jua na hakuweza kuoga na kuswali ila baada ya kuchomoza, basi anakuwa ameiswali Swalaah katika wakati wake na wala hazingatiwi kuwa ameipitisha. Ni kinyume na yule aliyeamka mwanzoni mwa wakati. Huyu wakati wake ni kabla ya kuchomoza jua, atahadhari asiuache wakati wa Swalaah ukamtoka".
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
071-Ni Sehemu Ipi Ya Ardhi Inayofaa Kutayamamia?
Alhidaaya.com [3]
Maulamaa wana rai mbili kuhusu mchanga unaofaa kutayamamia:
Rai ya kwanza
Ni uso wowote wa ardhi ikiwa ni changarawe, mlima, mchanga au udongo. Huu ni mwelekeo wa Abuu Haniyfah, Abuu Yuusuf na Maalik. Umekhitariwa na Shaykh wa Uislamu. Pia Ibn Hazm amelikhitari hilo, lakini yeye kashurutisha kuwa endapo kama uso wa ardhi hauna udongo, basi uwe umeshikamana na ardhi. [Al-Istidhkaar (3/157), Al-Mabsuutw (1/108), Majmuu Al-Fataawaa (21/364) na Al-Muhallaa (2/158)].
Kati ya hoja zao ni:
1- Neno Lake Allaah Mtukufu:
((صعيدا زلقا))
((Ardhi tupu)) [Al-Kahf (18:40)]
Na Neno Lake Ta’alaa:
((صعيدا جرزا))
((Ardhi kame)) [Al-Kahf (18:8)]
Amesema katika “Al-Istidhkaar” (3/158): “Al-Juzur” ni ardhi ngumu isiyootesha kitu.
2- Neno lake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((وجعلت لي الأرض مسجدا وطهورا))
((...na ardhi imefanywa kwangu kuwa sehemu ya kuswalia na kitwaharisho)). [Hadiyth Swahiyh: Imetangulia hivi karibuni].
3- Neno lake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((يحشر الناس يوم القيامة على صعيد واحد))
((Watu watafufuliwa siku ya Qiyaamah juu ya ardhi moja)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (4712) na Muslim (472)].
4- Neno lake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((جعلت الأرض كلها لي ولأمتي مسجدا وطهورا، فأينما أدركت رجلا من أمتي الصلاة فعنده مسجده وعنده طهوره))
((Ardhi yote imefanywa kwangu na kwa umati wangu kuwa sehemu ya kuswalia na kitwaharisho, na popote itakapomkuta Swalaah yeyote katika umma wangu, basi hapo ndipo sehemu yake ya kuswalia, na hapo ndipo kitwaharisho chake)). [Hadiyth Hasan: Imetangulia hivi karibuni].
5- Hadiyth ya Abuu Al-Juhaym kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipiga juu ya ukuta kwa mikono yake miwili, akatayamamu, kisha akamjibu mtu maamkizi. [Hadiyth Swahiyh: Imetangulia hivi karibuni].
6- Ni yale yaliyopokelewa toka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba amesema:
“Uso mzuri zaidi wa ardhi ni konde na ardhi ya konde”. [Isnadi yake ni dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Abiy Shaybah (1/161)].
Rai ya pili
Uso wa ardhi ni udongo na kisicho udongo hakifai kutayamamia.
Huu ni mwelekeo wa Ash-Shaafi’iy, Hanbali, Abuu Thawr na Ibn Al-Mundhir. [Al-Mughny (1/155), Al-Majmu’u (2/246), Al-Istidhkaar (3/159) na Al-Awsatw (2/43)].
Kati ya hoja zao ni:
1- Ni ziada iliyokuja katika Hadiyth isemayo:
((وجعلت تربتها لي طهورا))
))na umefanywa udongo wake kwangu ni kitwaharisho)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (522), Ibn Hibaan (1697), Ad-Daara Qutwniy (1/175) na Al-Bayhaqiy (1/213 – 230). Yeye amezungumzia kuhusu ziada, na la sahihi ni kuwa ziada hii ipo].
..katika Hadiyth ya
((جعلت لي الأرض مسجدا))
Wamesema: “Riwaya hii imehusishwa na riwaya isemayo:
((جعلت لي الأرض مسجدا وطهورا))
2- Ni Hadiyth iliyopokelewa toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((أعطيت ما لم يعط أحد من الأنبياء : نصرت بالرعب، وأعطيت مفاتيخ الأرض، وسميت أحمد، وجعل لي التراب طهورا، وجعلت أمتي خير الأمم)).
((Nimepewa mambo ambayo hakupewa Nabii yeyote: Nimenusuriwa kwa kutiwa khofu maadui, nimepewa funguo za ardhi, nimeitwa Ahmad, nimefanyiwa udongo kuwa kitwaharisho, na umma wangu umefanywa umma bora zaidi)). [Hadiyth Munkar: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad (1/98) na Al-Bayhaqiy (1/213)].
Ninasema:
“Yenye nguvu zaidi kwangu ni kauli ya kwanza. Ni kwamba inafaa kutayammamu kwa kila kile kinachoitwa ardhi, au kila kinachobeba chochote cha ardhini kama vumbi na mfano wake. Ama kauli ya pili, hebu tuitazame kwa pande mbili:
Kwanza: Hakuna chochote cha kuthibitisha katika dalili zao kama ulivyoona.
Pili: Wamelichukulia neno “at-turbah” katika Hadiyth kwa maana ya udongo. Na hapa hebu tuangalie. Abuu Hurayrah katika Hadiyth ya Muslim anasema:
“Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alinishika mkono akaniambia:
((خلق الله – عز وجل – التربة يوم السبت، وخلق فيها الجبال يوم الأحد، وخلق الشجر يوم الإثنين ..))
((Allaahu ‘Azza wa Jalla Aliumba udongo (ardhi) siku ya Jumamosi, Akaumba humo milima siku ya Jumapili, na Akaumba miti siku ya Jumatatu…)).
Katika Kamusi ya “Lisaan Al-‘Arab”, mtunzi amesema:
"خلق الله التربة يوم السبت"
“Allaah Ameumba udongo Siku ya Jumamosi”, yaani ardhi.
Ninasema: Na maana hii iko wazi katika Hadiyth, Walillaahi Al-Hamd”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
072-Mwenye Kukosa Vitwaharisho Viwili (Maji Na Mchanga)
Alhidaaya.com [3]
Kauli sahihi zaidi kati ya kauli mbili za Maulamaa kuhusiana na mtu aliyekosa vitwaharisho viwili (maji na mchanga) ni kuwa ataswali katika hali aliyonayo katika wakati wa Swalaah na wala hatoirejesha.
Huu ni mwelekeo wa Ash-Shaafi’iy, Ahmad na Ibn Hazm. Ibn Taymiyyah ameukhitari mwelekeo huu. [Al-Mughniy (1/157), Al-Majmu’u (2/321), Al-Muhallaa (2/138) na Al-Fataawaa (21/467)]
Hoja yao ni Kauli Yake Allaah Mtukufu:
((فاتقوا الله مااستطعتم))
((Basi mcheni Allaah mwezavyo)) [At- Taghaabun ( 64:16]
Na Neno Lake Allaah Mtukufu:
((لا يكلف الله نفسا إلا وسعها))
((Allaah Haikalifishi nafsi yoyote ila kwa uwezo wake)) [Al-Baqarah (2:286)]
Na kauli yake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
((إذا أمرتكم بأمر فائتوا منه مااستطعتم))
((Nikiwaamuruni jambo, basi lifanyeni kwa uwezo wenu)) [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (7288) na Muslim (3199)].
Wamesema: “Huyu amefanya alichoweza katika Swalaah, na jambo la kujitwaharisha ambalo hakuliweza, limemwondokea. Na kwa hilo, anakuwa ametekeleza aliloamuriwa, na mwenye kutekeleza aliloamuriwa, basi hatolipa”.
Ninasema: “Na huenda mwelekeo huu unatiliwa nguvu na Hadiyth ya Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) aliyesema:
“Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimtuma Asyad bin Al-Khudhayr – na hali mimi nasikia – kukitafuta kidani nilichokipoteza. Ukafika wakati wa Swalaah, nao wakaswali bila wudhuu. Kisha wakamjia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakamweleza hilo, na hapo ikateremshwa Aayah ya tayammum”[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (5882) na Muslim (795)].
Na ushahidi hapa ni kuwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwakubalia – wakati walipokosa maji – kuswali bila wudhuu na wala hakuwaamuru kurejesha Swalaah. Na endapo kama watakosa mchanga vile vile, basi hukmu ni hiyo hiyo. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.
Na kwa upande mwengine, Abuu Haniyfah, Asw-haabur Ra-ay (Mahanafi), Maalik na Al-Awzaa’iy, wao wanaona kwamba hatoswali mtu mpaka apate maji ya kutawadhia au mchanga wa kutayamamia, hata kama wakati utatoka. [Al-Awsatw (2/45), Al-Istidhkaar (3/150) na Al-Muhallaa (2/139)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
073-Yanayohusiana Na Niya Ya Kutayammam
Alhidaaya.com [3]
·
Niya ya kuondosha hadathi inatosheleza kuruhusika kuswali
Kauli za Maulamaa zilizo sahihi zaidi zinasema kwamba tayamumi inasimama mahala pa maji moja kwa moja. Yanayoruhusika kwa maji ndiyo yale yale yanayoruhusika kwa tayamumi, na utwahara wake huendelea kama unavyoendelea utwahara wa maji. Akitayamamu kwa ajili ya Swalaah ya Sunnah, anaweza pia kuswalia Swalaah ya faradhi na kinyume chake. Hii ndiyo kauli ya Maulamaa wengi kinyume na Maalik Allaah Amrehemu. [Al-Majmu’u (2/255), Al-Mughniy (1/158), Majmu’u Al-Fataawaa (12/436) na Al-Mabsuutw (1/117)]
Sheikh wa Uislamu anasema: [Majmu’u Al-Fataawaa (21/436)]
“Kauli hii ndio sahihi, na ndiyo iliyoashiriwa na Qur-aan, Sunnah na akili. Tunaona kwamba Allaah Ameifanya tayammum inatwaharisha kama Alivyoyafanya maji Akatuambia:
((فتيمموا صعيدا طيبا فامسحوا بوجوهكم وأيديكم منه ما يريد الله ليجعل عليكم من حرج ولكن يريد ليطهركم))
(( Basi ukusudieni mchanga mzuri, panguseni kwao nyuso zenu na mikono yenu. Allaah Hataki kuwafanyieni uzito lakini Anapenda kukutwaharisheni )). [Al-Maaidah (5:6) ]
Kwa hiyo, mwenye kusema kwamba mchanga hautwaharishi hadathi, basi amekhalifu Qur-aan na Sunnah. Na ikiwa unatwaharisha hadathi, haiwezekani hadathi ikaendelea kuwepo, kwani Allaah Amewatwaharisha Waislamu hadathi kwa tayamumi. Tayamumi inaondosha hadathi na inamtwaharisha mwenye hadathi, lakini uondoshaji huu ni wa muda mpaka pale atakapoweza kuyatumia maji. Tayamumi ni badali ya maji, nayo inabakia ni kitwaharisho madhali maji yamekuwa vigumu kupatikana”.
Ninasema: “Tayamumi imewekwa kisharia kwa ajili ya Swalaah, twawafu, kusoma Qur-aan, kugusa Msahafu na mengineyo yanayoruhusika mtu anapokuwa na wudhuu au baada ya kuoga madhali maji yamekuwa vigumu kupatikana. Mwenye kunuwiya kwa tayamumi yake kuondosha hadathi, ni halali kwake kufanya yale yote anayoruhusika anapokuwa na wudhuu na baada ya kuoga. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
Mwenye Kutayammamu Kwa Niya Ya Kuondosha Janaba, Je Itamtosheleza Na Wudhuu Pia?
Mwenye kutayamumi kwa niya ya kuondosha janaba, niya hiyo itamtosheleza na wudhuu pia kwa mujibu wa kauli sahihi ya Maulamaa kama Abuu Haniyfah na Ash Shaafi’iy. [Al-Mughniy (1/166)]
Na hii ni kwa mambo mawili:
1- Twahara ya viwili hivi ni moja. Inapoondoka moja, humwondosha mwenzake kama mkojo na kinyesi.
2- Tayamumi ni badali ya utumiaji maji, hivyo huchukua hukmu yake. Lenye nguvu zaidi ni kuwa kuoga, hutosheleza na wudhuu pia, na vile vile tayamumi.
Ama mwenye kutayamumi kwa niya ya kuondosha hadathi ndogo, je niya itatosheleza kuondosha janaba pia? Jibu hapa litaangaliwa; mwenye kuliangalia suala mtizamo wa sababu ya kwanza, jibu lake litakuwa ndiyo. Ama mwenye kuliangalia kwa mtizamo wa kuwa tayamumi ni badali ya maji, basi atazuia.
Maalik, Abuu Thawr, Mahanbali na Ibn Hazm, [Al-Mughniy (1/166) na Al-Muhallaa (2/138)]…..wao wanasema kwamba niya ya kimoja, haitoshelezi kingine kutokana na ujumuishi wa kauli ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
(( إنما الأعمال بالنيات، وإنما لكل امرئ ما نوى))
((Hakika matendo ni kwa niya, na kila mtu ni kwa lile alilolinuwiya)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (namba moja)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
074-Namna Sahihi Ya Kutayammamu
Alhidaaya.com [3]
Namna sahihi ya kutayamamu iliyokuja kwa njia sahihi toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni:
Atapiga mtu pigo moja kwenye mchanga kwa mikono miwili, kisha ataipuliza, halafu atajipukusa kwayo uso wake na vitanga vyake viwili.
Haya ni madhehebu ya Mahanbali na Ibn Hazm. Na ndivyo walivyosema baadhi ya Masalafu, na Ibn Taymiyyah amelikhitari. [Al-Mughniy (1/159), Al-Muhallaa (1/146) na Al-Fataawaa (21/422)].
Dalili ya hili ni:
1-Hadiyth iliyoelezewa na ‘Ammaar bin Yaasir akisema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: Ilikuwa inakutosha kufanya hivi”. Na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akapiga ardhi kwa vitanga vyake, akavipuliza, kisha akapukusa kwavyo uso wake na viganja vyake”[Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (338) na Muslim (798).
2-Hadiyth ya Abuu Hurayrah aliposema: “Ilipoteremka Aayah ya tayamumi, sikujua namna ya kutayamamu. Nikamwendea Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) lakini sikumkuta. Nikaondoka kumtafuta nikamwona nikamwelekea. Aliponiona alilijua lililonileta, akaenda haja ndogo, kisha akapiga mikono yake chini, akapukusa kwayo uso wake na viganja vyake”. [Isnadi yake ni laini. Imefanyiwa “ikhraaj” na Ibn Abiy Shaybah (1/159). Hadiyth iliyotangulia inaitilia nguvu].
Na kwa upande mwingine, kundi jingine la Maulamaa linaona kwamba tayamumi ni mapigo mawili: Pigo moja la uso, na pigo jingine la mikono miwili mpaka kwenye viwiko viwili. Haya ni madhehebu ya Hanafiy, Maalik na Ash Shaafi’iy. Ath-Thawriy na Al-Layth wamesema hivi, nalo limepokelewa toka kwa Ibn ‘Umar. Wengine ni Ash-Sha’abiy, Al-Hasan Al-Baswriy na wengineo. [Al-Mabsuwtw (1/106), Al-Istidhkaar (3/162) na Al-Majmu’u (2/242)].
Hoja zao ni:
1- Hadiyth ya Ibn ‘Umar kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema:
((Tayamumi ni mapigo mawili: Pigo la uso, na pigo la mikono miwili hadi kwenye viwiko viwili)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Haakim (1/179) na Al-Bayhaqiy (1/207)].
2- Hadiyth ya Ibn ‘Umar kuhusiana na kisa cha mtu aliyepita kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa ameshughulika, akamsalimia. Ibn ‘Umar anasema: “Alipiga mikono yake miwili ukutani, akapangusa kwayo uso wake, kisha akapiga pigo jingine, akapukusa mikono yake miwili, kisha akaijibu salamu ya mtu yule”.[Hadiyth Dhwa’iyf: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (1/88) na Al-Bayhaqiy (1/207). Imaam Ahmad ameikataa].
3- Yaliyoelezewa na Abuu Juhaym aliposema: “Akasimama mbele ya ukuta, akaukwangua kwa fimbo aliyokuwa nayo, kisha akaweka mikono yake ukutani, halafu akapukusa uso wake na mikono yake, kisha akanijibu salamu”[Hadiyth Munkari: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ash Shaafi’iy katika musnadi yake (130) na Al-Bayhaqiy (1/205). Imekhalifiana na riwaya ya Swahiyh Mbili iliyotangulia].
4-Hadiyth ya ‘Ammaar isemayo kwamba alieleza kuwa walijipangusa kwa mchanga kwa ajili ya kuswali Salatul Fajr wakiwa pamoja na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Wakaupiga mchanga kwa viganja vyao mara nyingine tena, wakajipangusa kwa mikono yao yote hadi kwenye mabega na makwapa kwa matumbo ya viganja vyao. [Hadiyth Mudhtwarib: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (1/84), Ibn Maajah (571), An Nasaaiy (1/168) na Al-Bayhaqiy (1/208)].
Ninasema: “Lenye nguvu ni kuwa tayamumi ni pigo moja tu kwa uso na mikono miwili hadi kwenye viwiko viwili kama tulivyotangulia kusema. Na hii ni kwa mambo mawili:
1-Dalili zote za wenye kukhalifiana na hilo ni dhwa’iyf. Hawana hata Hadiyth moja Marfu’u.
2-Hukmu ya tayamumi inafungamana na mikono miwili basi, dhiraa haiingii. Ni kama kuukata mkono wa mwizi. Hili linaashiriwa na kuhoji Ibn ‘Abbaas kuhusiana na kuainisha sehemu ya kukatwa mkono iliyoelezewa kwenye Aayah kwa mwizi kwa Neno Lake Allaah kuhusiana na tayamumi:
(( فامسحوا بوجوهكم وأيديكم منه))
((Basi pakeni nyuso zenu na mikono yenu kwa mchanga huo)). [Al-Maaidah (5:6)].
Na ukataji kwa mujibu wa Sunnah, ni viganja viwili.
Yanayotengua Tayammumi
Hadathi yoyote inayotengua wudhuu, hutengua tayamumi. Hili halina mvutano wowote kati ya Maulamaa. [Al-Muhallaa cha Ibn Hazm (2/122)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
075-Masuala Mbalimbali Kuhusu Tayammumi
Alhidaaya.com [3]
·
Je, inaswihi kuswali kwa tayamumi endapo maji yatapatikana kabla ya kuanza kuswali?
Ibn ‘Abdul Barri amesema: “Maulamaa wote wanakubaliana kwamba mwenye kutayamamu baada ya kukosa maji, kisha akayapata maji kabla hajaanza kuswali, basi tayamumi yake hubatilika, na hawezi kuswali kwa tayamumi hiyo, bali hurejea katika hali yake ya kabla ya kutayamamu”. [Al-Istidhkaar (3/167)]
·
Mtu ametayamamu akaanza kuswali, kisha maji yakapatikana kabla hajamaliza Swalaah yake, je ataikamilisha Swalaah au ataivunja?
Maulamaa wamehitilafiana katika suala hili kwa kauli mbili:
Ya kwanza: Atalazimika kuivunja Swalaah ili ayatumie maji, kisha aanze tena Swalaah upya.
Haya ni madhehebu ya Abuu Haniyfah na Ahmad. Hivyo hivyo kasema Ath-Thawriy na Ibn Hazm. [Al-Mabsuwtw (1/120), Al-Mughniy (1/167), Al-Istidhkaar (3/170), na Al-Muhallaa (2/126)].
Hoja zao ni:
1- Neno lake Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
(( الصعيد الطيب وضوء المسلم، وإن لم يجد الماء عشر سنين، فإذا وجدت الماء فأمسه جلدك))
((Mchanga safi ni wudhuu kwa Muislamu hata kama hakupata maji miaka kumi. Ukiyapata maji, basi yagusishe ngozi yako)). [Hadiyth Dhwa’iyf: Wamekhitilafiana katika kuifanya Hadiyth Hasan. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhy (124), Abuu Daawuud (329) na An-Nasaaiy (1/171). Tumeitaja katika mlango wa kuoga].
Wamesema: Hii ni kwa mwenye kuyapata maji.
2- Kwa vile ameweza kuyatumia maji, basi tayamumi yake hubatilika na kuwa kana kwamba yuko nje ya Swalaah.
3-Kwa vile tayamumi ni twahara ya dharura, hubatilika kwa kuondoka dharura. Ni kama twahara ya mwanamke mwenye damu ya istihaadhwah inapokatika damu yake.
Ya pili: Ataikamilisha Swalaah yake mpaka mwisho
Haya ni madhehebu ya Maalik na Ash Shaafi’iy, na riwaya ya pili toka kwa Ahmad lakini inasemekana kwamba aliachana nayo. Hivyo hivyo kasema Abuu Thawr, Daawuud na Ibn Al-Mundhir. [Al-Istidhkaar (3/169), Al-Majmu’u (2/357) na Al-Awsatw (2/65)].
Hoja zao ni:
1-Neno Lake Allaah Subhaanahu wa Taalaa:
(( ولا تبطلوا أعمالكم))
((Wala msizibatilishe amali zenu)). [Muhammad (47:33)].
Wanasema: Haijuzu kuivunja Swalaah kwa ajili ya hilo.
2-Twahara ina wakati wake, na Swalaah ina wakati wake. Na mtu baada ya kuingia kwenye Swalaah, anakuwa wakati huo haswali kwa ufaradhi wa twahara. Kwani yeye ametayamamu kama alivyoamrishwa, na kwa kupiga takbiyr, anakuwa ashatoka nje ya wigo wa faradhi ya twahara. Na hapo inakuwa haijuzu tena kuivunja twahara hiyo ambayo muda wake ushapita, au kuvunja rakaa ambazo ameshaziswali kama alivyofaradhishiwa. Na suala hili haliwezi kufanyika ila kwa dalili kutoka kwenye Qur-aan, au Sunnah, au Ijma’a.
Ninasema:
“Ninaloliona lenye nguvu zaidi ni kuwa mtu ataendelea kukamilisha Swalaah yake, kwa vile hakujathibiti lolote lenye kulazimisha kuikata Swalaah baada ya kuianza. Hii ni kama mfano wa mtu anayefunga Swaum ya kafara. Ikiwa ameanza Swaum yake kisha akapata mtumwa wa kumwacha huru, basi hatoivunja Swaum yake. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi."
·
Ikiwa mtu ameswali kwa kutayamamu, kisha maji yakapatikana kabla ya wakati wa Swalaah kumalizika, je ataswali tena?
Huyu hatorejesha tena Swalaah yake kwa mujibu wa kauli mbili sahihi za Maulamaa. Haya ni madhehebu ya Maalik, Ath-Thawriy, Al-Awzaaiy, Al-Mazniy, Atw-Twahaawiy na Ahmad katika moja ya riwaya mbili. Hivi hivi kasema Ibn Hazm. [Angalia Al-Majmu’u (2/353) na Al-Muhallaa (2/139)].
Lakini Abuu Haniyfah na Ash-Shaafi’iy, wao wanasema kwamba ni lazima ailipe upya Swalaah yake wakati anapoyapata maji. [Al-Majmu’u (2/353)].
Ibn Hazm amewajibu akisema: “Ama kauli ya Abuu Haniyfah na Ash-Shaafi’iy, ni wazi kwamba imedoda, kwa kuwa kumwamuru kwao mtu atayamamu na aswali, hakukosekani na; ima wao wamemwamuru kuswali Swalaah ambayo ni faradhi ya Allaah juu yake, au Swalaah ambayo Allaah Hakumfaradhishia, na hakuna la tatu hapo. Na ikiwa mwenye kuwafuata atasema: Wamemwamuru Swalaah ambayo ni faradhi juu yake, tutamwambia: Kwa nini basi aiswali tena baada ya wakati wake ikiwa alitekeleza faradhi yake? Na ikiwa atasema: Bali wamemwamuru Swalaah ambayo si faradhi juu yake, hapo atakuwa amekiri kwamba wao wamemlazimisha jambo lisilo lazima kwake, na hili ni kosa”.
Ninasema:
“Ndio. Si lazima kuswali tena. Lakini ni vizuri kuswali tena madhali muda upo na maji yamepatikana. Na hii ni kwa Hadiyth ya Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy aliyesema:
“Watu wawili walitoka kwenda safari. Ukawakuta wakati wa Swalaah na wao hawana maji. Wakatayamamu kwa mchanga kisha wakaswali. Halafu baadaye walipata maji kabla wakati haujatoka. Mmoja wao akatawadha na kuswali tena, lakini mwingine hakufanya. Halafu walikwenda kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakamweleza walilolifanya. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia yule ambaye hakuswali tena:
(( أصبت السنة وأجزأتك صلاتك))
((Umeipata Sunnah, na Swalaah yako imekutosheleza)).
Kisha akamwambia yule aliyetawadha na kuswali tena:
(( لك الأجر مرتين))
((Una ajri mara mbili)). [Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (334) na An-Nasaaiy (1/213)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
076-Hedhi Na Nifasi
Alhidaaya.com [3]
Damu za kimaumbile zinazomtoka mwanamke zinagawanyika vigawanyo vitatu:
1- Damu ya hedhi
2- Damu ya nifasi
3- Damu ya istihaadhwah
Damu Ya Hedhi
[Majina mengineyo ya hedhi ni: الطمث – العراك – الضحك – الإكثار – الإعصار. (Al-Muhadh-dhab 1/341)]
Ni damu nyeusi, nzito na yenye harufu mbaya. Inamtoka mwanamke toka sehemu maalumu katika nyakati maalumu.
Hedhi ni jambo ambalo Allaah Amewaumbia wanawake wote kama Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alivyomwambia ‘Aaishah kama ilivyo katika Swahiyh Mbili:
(( إن هذا أمر كتبه الله على بنات آدم....))
((Hakika hili ni jambo, Allaah Amelihukumia kwa mabinti wa Aadam)).
Hawwaa (Amani iwe juu yake), yeye ndiye wa mwanzo kuipata. Imepokelewa kwa isnadi Swahiyh kwa Ibn 'Abbaas akisema:
“ Hawwaa alianza kupata damu ye hedhi baada ya kushushwa toka peponi”.
Damu ya hedhi haina mpaka wa uchache wala wingi, bali hilo linategemea maumbile ya mwanamke, kwa vile hakuna dalili yoyote sahihi toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inayobainisha uchache wake au wingi wake.
Shaykh wa Uislamu katika Kitabu cha Al-Fataawa (21/623) anasema:
“Ama wale wanaosema kwamba wingi wa hedhi ni siku kumi na tano na uchache wake ni siku moja kama Ash-Shaafi’iy na Ahmad, au wanaosema kuwa hedhi haina mpaka maalumu kama Maaliki, wao wanasema hayo tu, lakini halijathibiti lolote kuhusiana na hilo toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) au Maswahaba zake. Na marejeo ya yote hayo yanasimamia juu ya maumbile ya mwanamke kama tulivyosema, na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.” [Jaami'u Ahkaamin Nisaa (1/179). Angalia Al-Muhalla (2/191) na Al-Mughniy (1/308)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
077-Kuanza Na Kumalizika Hedhi
Alhidaaya.com [3]
[Jaami'u Ahkaamin Nisaa (1/200) na kurasa zinazofuatia]
1- Kuanza kwa hedhi kunajulikana kwa msukumo wa damu wakati wake, nayo ni damu nyeusi, nzito na yenye harufu mbaya.
2- Kumalizika kwake hujulikana kwa kukatika damu, kuwepo unjano na rangi yenye kumili weusi. Na hili linatokana na mambo mawili:
(a) Ukavu; nako ni kutoka kikiwa kikavu kilichoingizwa katika njia ya uzazi. Yaani ikiwa mwanamke ataingiza kitambaa au pamba katika utupu wake, basi hutoka kikiwa kikavu.
(b) Kuwepo maji meupe yanayotoka katika njia ya uzazi wakati wa kukatika damu ya hedhi.
Imepokelewa na mwachwa huru wa ‘Aaishah akisema:
“Wanawake walikuwa wakimwendea na kitambaa chenye pamba yenye unjano utokanao na damu ya hedhi, kisha wanamuuliza kama wanaweza kuswali, naye huwajibu akisema: “Msifanye haraka mpaka mwone maji meupe”.
Hapa anamaanisha kwamba wametwaharika na hedhi. [Ni Hadiyth Hasan kwa nyingine. Imefanyiwa “ikhraaj” na Maalik (uk 59), Al-Bukhaariy akitoa maelezo (1/420 – Fat-h) na ‘Abdur-Raaziq (1/302) kwa Sanad Dhwa’iyf ingawa ina ushahidi kwa Ad-daaramiy (1/214), na Al-Bayhaqiy (1/337). Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
078-Nini Hukmu Ya Unjano Na Rangi Yenye Kumili Weusi Baada Ya Kutwaharika Na Hedhi?
Alhidaaya.com [3]
Unjano na rangi yenye kumili weusi ni maji anayoyaona mwanamke mithili ya usaha. Maji haya yanakuwa si damu ya hedhi kama yatamtoka mwanamke baada ya kukatika damu au baada ya kukauka. Atazingatiwa yu twahara, ataswali, atafunga na mumewe atamwingilia.
Dalili ya hili ni Hadiyth ya Ummu 'Atwiyyah aliposema:
“Tulikuwa - baada ya kujitwaharisha - hatushughulishwi chochote na rangi yenye kumili weusi au unjano”. [Imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Daawuud (307), An-Nasaaiy (1/186), Ibn Maajah (647) na wengineo. Al-Bukhaariy ameikhariji bila ziada (326)].
Faida
1- Damu inapokatika na mwanamke akawa twahara lakini maji ya kuogea yakakosekana, itambidi atayamamu na mumewe anaruhusika kumwingilia. Hili ndilo tamko la Maulamaa wengi. [Majmu’u Al-Fataawaa (1/625), Al-Muhallaa (2/171), Sharhu Muslim (1/593) na Jaami’u Ahkaamin Nisaa (1/152)]
2- Damu ikiendelea kutoka zaidi ya muda wake wa kawaida, nini atafanya?
Ikiwa kwa mfano damu yake kwa kawaida hutoka kwa muda wa siku sita kila mwezi, kisha ikazidi ikawa siku saba, au nane, au tisa, nini atafanya?
Tunasema: “Hali ya mwanamke huyu haiachani na moja ya mawili:
·
Ima atakuwa anaweza kupambanua na kutofautisha kati ya damu ya hedhi na damu nyingineyo.
Mwanamke huyu ataiangalia damu hii. Ikiwa rangi yake, harufu yake na maumbile yake yako sawa na damu ya hedhi, basi ataendelea kuacha Swalaah, Swaum na kuingiliwa kama alivyokuwa, kwa kuwa hakuna mpaka maalumu wa muda wa kutoka damu hii kama tulivyotangulia kusema. Na kama ataiona inatofautiana na damu ya hedhi, basi ataoga na kuswali.
·
Au atakuwa hawezi kupambanua na kutofautisha kati ya damu ya hedhi na nyingineyo (kuna baadhi ya wanawake wako hivi).
Huyu ataendelea kubakia bila kuswali, wala kufunga, wala kuingiliwa na mumewe mpaka atakapotwaharika, kwa kuwa hakuna mpaka wa upeo wa mwisho wa kutoka damu ya hedhi. [Jaami’u Ahkaamin Nisaa (1/215), na kitabu cha Fataawaal Mar-at cha Ibn ‘Uthaymiyn].
3- Ikiwa damu katika siku zake za mwezi inakuja siku mbili kwa mfano, kisha inakatika siku ya tatu, halafu inarudi tena siku ya nne na kadhalika.
Jibu sahihi la hali hii ni kuwa kukatika damu ndani ya masiku ya hedhi yanayojulikana, hakuzingatiwi bali huhesabiwa ni hedhi. Kinachozingatiwa ni kuonekana alama ya utwahara, nayo ni majimaji meupe ambayo akina mama wanayajua. [Fataawaal Mar-at, Jam’u Muhammad Al-Musnad (uk. 26)].
4- Je, mjamzito hupata hedhi? [Jaami’u Ahkaamin Nisaa (1/208)]
Maulamaa wana mielekeo miwili katika suala hili. Kundi la kwanza ambalo ni la wengi, wanasema kwamba mwanamke mjamzito haingii hedhini. Dalili yao ni Hadiyth ya Abuu Sa’iyd Al Khudriyyi (Radhwiya Allaahu Anhu) isemayo:
(( لا توطأ حامل حتى تضع ولا غير حامل حتى تحيض حيضة ))
((Mjamzito haingiliwi mpaka ajifungue, wala asiye mjamzito mpaka aingie hedhini)). [Hadiyth Hasan Lighayrih. Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (2157), na Ahmad (3/62). Kuna Hadiyth nyingine kama hii kwa Ad Daar Qutwniy (3/257)].
Wanasema:”Linalothibitisha kwamba mwanamke hana kitu katika tumbo lake la uzazi, ni kutokwa na damu ya hedhi, na lau kama mjamzito anapata hedhi, basi hedhi hii haiwezi kuthibitisha kuwa hana kitu tumboni”.
Ama kundi la pili akiwemo Ash Shaafi’iy, wao wanasema kwamba mjamzito hupata damu ya hedhi.
Jibu sahihi kuhusiana na kauli yao hii ni kuwa asili na kaida kuu ya wingi ni kwamba mja mzito hapati hedhi. Lakini inaweza ikamtokezea mwanamke fulani katika hali isiyo ya kawaida akatokwa na damu wakati wa ujauzito. Damu hii itaangaliwa; ikiwa iko sawa na damu ya hedhi kwa rangi, harufu na maumbile, na ikamjia wakati uleule anaopata hedhi, basi itazingatiwa kuwa ni damu ya hedhi. Hapo ataacha Swalaah, Swaum na mumewe hatoruhusiwa kumwingilia. Lakini damu hii haitoingizwa katika hisabu ya eda, kwa kuwa Allaah Anasema:
(( وأولات الأحمال أجلهن أن يضعن حملهن))
(( Wenye mimba muda wao ni kuzaa mimba zao)). [At-Twalaaq (65:4)]
Ama ikiwa damu inayomtoka inatofautiana na sifa za damu ya hedhi na imekuja katika wakati usio wa hedhi, basi si damu ya hedhi na wala haibebi hukmu za hedhi. Itakuwa ni kama damu ya istihaadhwah.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
079-Yaliyoharamishwa Kwa Mwenye Hedhi Na Nifasi
Alhidaaya.com [3]
1- Kuswali
Maulamaa wote wamekubaliana kwamba ni haramu kwa mwenye hedhi au nifasi kuswali, sawasawa ikiwa ni Swalaah ya faradhi au ya Sunnah. Wamekubaliana kwamba ufaradhi wa Swalaah huporomoka, na kuwa hatozilipa atakapotwaharika. [Al-Majmu’u ya An-Nawawiy (2/351) na Al-Muhallaa (2/175) ya Ibn Hazm].
Imepokelewa toka kwa Abu Sa’iyd akisema, Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
(( أليس إذا حاضت لم تصل ولم تصم؟ فذلك نقصان دينها))
((Je, si anapopata hedhi haswali wala hafungi? Basi hilo ni upungufu wa Dini yake)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (1951), Muslim (80) na wengineo].
Na imepokelewa na Mu'aadhah kwamba mwanamke mmoja alimwambia ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha):
"Je, inamtosheleza mmoja wetu Swalaah yake anapotwaharika?" Akamjibu: "Je, wewe ni Mharuriyah? Sisi tulikuwa tukiingia hedhini tukiwa na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na hakuwa akituamrisha, au akasema: Hatuiswali". [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (321) na Muslim (uk. 265)].
“Mharuriyah”, ni sifa ya mwenye kufuata madhehebu ya Khawaariji. Baadhi yao walikuwa wakiwajibisha kulipa Swalaah kwa mwenye hedhi.
Faida
1- Mwanamke akiingia hedhini muda mfupi kabla ya kuingia Swalaah ya alasiri kwa mfano, na hakuwa ameswali adhuhuri, je itamlazimu alipe Swalaah ya adhuhuri baada ya kutwaharika?
Ikiwa kwa mfano itamjia muda mfupi kabla ya alasiri na hakuwa ameswali adhuhuri, basi atailipa Swalaah hiyo ambayo ilimwajibikia kabla ya kupata hedhi wakati anapotwaharika. Hii ndio rai ya Jamhuri ya Maulamaa. Sababu ni kuwa Swalaah ilikuwa imemwajibikia, na ni lazima ailipe madhali wakati wake uliingia hali ya kuwa yuko twahara kwa kiasi cha rakaa.
Hii ni kwa Neno Lake Allaah Mtukufu:
((إنَّ الصَّلاةَ كَانَتْ عَلَى المُؤْمِنِينَ كِتَاباً مَّوْقُوتا))
((Hakika Swalaah ina wakati wake maalumu kwa Waumini)). [An-Nisaa (4:103)]
Kuna kauli nyingineyo isemayo kwamba haimlazimu kuilipa adhuhuri. Wenye kusema hivi wanatoa dalili inayoashiria kuwa wanawake wakati wa enzi ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), walikuwa wakipata hedhi nyakati zote, lakini haikupokelewa kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwamuru mwanamke yeyote kuswali Swalaah iliyompita kabla ya kupata hedhi anapotwaharika.
Shaykh wa Uislamu anasema katika Al-Fataawaa (23/235):
"Dalili yenye nguvu zaidi ni madhehebu ya Abu Haniyfah na Maalik isemayo kuwa halazimiwi na chochote, kwani kulipa kunapasa kwa jambo jipya, na hapa hakuna lolote linalompasa kulipa, mbali na kuwa alichelewesha ucheleweshaji usio wa kuzembea. Ama aliyelala hata kama hakuzembea, basi analolifanya si kulipa, bali huo ni wakati wa Swalaah yake wakati anapoamka na akakumbuka."
2- Anapotwaharika mwenye hedhi muda mfupi kabla ya alasiri kwa mfano, kisha baada ya kuoga wakati wa alasiri ukawa umeshaingia, je, ni lazima aswali adhuhuri?
Anapotwaharika na hedhi na nifasi kabla ya kuingia magharibi, itamlazimu aswali adhuhuri na alasiri za siku hiyo. Vile vile, anapotwaharika kabla ya kuchomoza alfajiri, itamlazimu aswali magharibi na ‘ishaa za usiku huo kwa vile wakati wa Swalaah ya pili ndio wakati wa Swalaah ya kwanza katika hali ya udhuru. Katika Al-Fataawa 2/334, Shaykh wa Uislamu anasema:
"Na kwa haya, ndivyo yalivyo madhehebu ya Jamhuri ya Maulamaa kama Maalik, Ash-Shaafi'iy na Ahmad, na kwamba mwenye hedhi anapotwaharika mwishoni mwa mchana, atazisali adhuhuri na alasiri. Na anapotwaharika mwishoni mwa usiku, ataswali magharibi pamoja na ‘ishaa. Na hivi ndivyo ilivyonukuliwa toka kwa ‘Abdur-Rahmaan bin ‘Awf, Abu Hurayrah na Ibn 'Abbaas, kwa vile wakati ni mmoja kati ya Swalaah mbili katika hali ya udhuru. Hivyo basi, akitwaharika mwishoni mwa mchana, wakati wa adhuhuri hubakia na ataiswali kabla ya alasiri. Na akitwaharika mwishoni mwa usiku, basi wakati wa magharibi hubakia katika hali ya udhuru na ataiswali kabla ya ‘isha. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
2- Kufunga
Imekubalika kwa Ijma’a ya Maulamaa kuwa mwenye hedhi na nifasi hafungi, lakini atazilipa siku za Ramadhwaan. ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) amesema:
"Hilo lilikuwa likitupata (hedhi) na tunaamrishwa kulipa swawm, lakini hatuamrishwi kulipa Swalaah". [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (265) na Abu Daawuud (263)].
Faida
1- Mwenye hedhi akitwaharika kabla ya alfajiri na hakuoga, je, atafunga?
Ikiwa mwenye hedhi atatwaharika kabla ya alfajiri na akanuia kufunga, basi Swawm yake ni sahihi, kwani kusihi kwa swawm yake hakutegemei kuoga, kinyume na Swalaah. Na hii ni kauli ya Jamhuri. [Fat-h Al-Baariy (1/192)]
2- Akitwaharika mwenye hedhi kabla ya kuchwa jua, je, atajizuia kula muda uliobakia?
Si lazima ajizuie kula mchana uliobakia, kwani alikwishafungua tokea mwanzo, lakini siku hiyo atailipa. Imepokelewa toka kwa Ibn Jaryj akisema: "Nilimwambia 'Atwaa: Mwanamke akiingia hedhini, kisha akatwaharika sehemu ya mchana, je atakamilisha? Akasema: Hapana, bali atalipa". [Isnadi yake ni Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na ‘Abdur Raaziq katika Al-Musannaf (1292) kwa Sanad Swahiyh].
3- Kumwingilia (kumjimai)
Maulamaa wote wamekubaliana kwamba haijuzu kumwingilia mwanamke mwenye hedhi katika utupu. [Al-Muhalla (2/162), Majmu’u Al-Fataawaa (21/624) na Tafsiyr At-Twabariy (4/378)]
Allaah Mtukufu Ameliharamisha hilo katika Kauli Yake:
((فَاعْتَزِلُوا النِّسَاءَ فِي المَحِيضِ))
((Basi waepukeni wanawake katika hedhi)). [Al-Baqarah (2:222)]
Na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
(( اصنعوا كل شيئ إلا النكاح))
((Fanyeni kila kitu isipokuwa kujimai)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (203), Abu Daawuud, An-Nasaaiy, At-Tirmidhiy na Ibn Maajah].
Shaykh wa Uislamu katika Al-Fataawaa (21/624) anasema:
"Kumwingilia mwenye nifasi ni kama kumwingilia mwenye hedhi, na hilo ni haramu kwa makubaliano ya Maimam.
Faida
1- Ikiwa Muislamu ataitakidi kuwa ni halali kumwingilia mwanamke mwenye hedhi katika utupu wake, basi atakuwa ni kafiri aliyeritadi. Na lau kama mtu atalifanya hilo bila kuitakidi kuwa ni halali; ima kwa kusahau au kutojua kuwepo hedhi, au hajui kuwa hilo ni haramu, au akalazimishwa, basi hana makosa, na wala hatoi kafara. Na ikiwa atamwingilia kwa kukusudia akijua kwamba mkewe yuko mwezini na kuwa hilo ni haramu na bila kulazimishwa, basi atakuwa ametenda dhambi kubwa, na ni lazima atubie. [An-Nawawiy katika Sharh Muslim (3/204).
Na je, atawajibika kutoa kafara kwa kufanya hivyo?
Jamhuri ya Maulamaa – kinyume na Ahmad – wanasema kuwa hapaswi kutoa kafara.
Ninasema: "Hili ndilo sahihi. Ama Hadiyth ya Ibn 'Abbaas aliyoipokea toka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa anasema kuhusiana na mtu anayemwingilia mkewe akiwa hedhini kwamba ((Anatoa swadaqah dinari moja au nusu dinari)), basi Hadiyth hii ni Dhwa’iyf kwa kauli yenye nguvu, nayo imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Daawuud (264), An Nasaaiy (1/153), na Ibn Maajah (640).. Na kuchukua mali ya Muislamu ni haramu kiasili, na si halali kuitwaa mali hiyo ila kwa matni.
2- Kinachokatazwa kustarehe na mwenye hedhi ni tupu yake basi. Mume anaruhusiwa kumchezea popote atakapo isipokuwa kuingiza dhakari yake katika utupu. [Ni madhehebu ya Ath-Thawriy, Ahmad na Is-haaq. Pia Muhammad bin Al-Hasan na Atw-Twahaawiy katika Mahanafi, na baadhi ya wafuasi wa Maalik. Vile vile ni moja ya kauli mbili za Ash-Shaafi'iy. Aidha, limeungwa mkono na Ibn Al-Mundhir na An-Nawawiy (Fa-th Al-Baariy) (1/404). Ni madhehebu ya Ibn Hazm vile vile].
Na dalili ya hilo ni Hadiyth ya Anas. Anasema kwamba iliposhuka Kauli Yake Allaah Mtukufu:
((فَاعْتَزِلُوا النِّسَاءَ فِي المَحِيضِ))
((Basi waepukeni wanawake katika hedhi)), hapo Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema:
((اصنعوا كل شيئ إلا النكاح))
((Fanyeni kila kitu isipokuwa kujimai)). [Tumeitaja milango iliyopita].
Na imepokelewa toka kwa baadhi ya wakeze Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakisema:
"Alikuwa anapotaka kitu kwa mwenye hedhi, hutupia nguo juu ya utupu wake". [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Abu Daawuud (272) kwa Sanad Swahiyh].
Ninasema: "Lenye kutilia nguvu zaidi kauli hii ni Hadiyth ya Masruuq. Alimwambia Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha): "Ninataka kukuuliza jambo lakini naona hayaa. Akasema: Mimi ni mama yako, na wewe ni mwanangu. Akasema: Ni jambo lipi ambalo mtu anaweza kulifanya kwa mkewe akiwa hedhini? Akasema: Anaweza kufanya mambo yote, isipokuwa utupu wake". [Isnadi yake ni Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Atw-Twabariy katika ((At-Tafsiyr)) (4/378) kwa Sanad Swahiyh, nayo ina njia kadhaa].
Na hakuna shaka kuwa Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) ndio mjuzi zaidi wa hukmu ya suala hili, kwa kuwa yeye ndiye mke wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)”.
Tanbihi
Kauli nyingine ya Maulamaa inasema kuwa linalojuzu kwa mwanamume kustarehe na mkewe wakati wa hedhi ni kila kitu, isipokuwa sehemu iliyopo kati ya kitovu na magoti. Kauli hii ina dalili zake, lakini kauli ya kwanza ndiyo yenye nguvu zaidi. Na Allaah Mtukufu Ndiye Ajuaye Zaidi.m [Haya ni madhehebu ya Maulamaa wengi. Angalia kwenye Jaami’u Ahkaamin Nisaa (1/140) na kurasa zinazofuatia ukipenda].
3- Mwanamke anapotwaharika hedhi, haijuzu kwa mumewe kumwingilia mpaka aoge. Allaah Mtukufu Anasema:
((ولا تَقْرَبُوهُنَّ حَتَّى يَطْهُرْنَ فَإذَا تَطَهَّرْنَ فَأْتُوهُنَّ مِنْ حَيْثُ أَمَرَكُمُ اللَّهُ))
((Wala msiwakurubie mpaka watwaharike, na wanapotwaharika, basi waingilieni pale Alipowaamrisheni Allaah)). [Al-Baqarah (2:222)]
Mujaahid anasema: "Wanawake wana twahara mbili; twahara ya Kauli Yake Allaah Mtukufu:
((حَتَّى يَطْهُرْنَ))
Yaani wanapooga, na hawi halali kwa mumewe mpaka aoge.
Anasema:
((فَأْتُوهُنَّ مِنْ حَيْثُ أَمَرَكُمُ اللَّهُ))
Pale damu inapotoka, na kama hakumwingilia pale Alipoamrisha Allaah, basi si katika wenye kutubia wala wenye kujitwaharisha". [Imefanyiwa “ikhraaj” na ‘Abdur-Raaziq (1272) na Al-Bayhaqiy (1/310) kwa Sanad Swahiyh hadi kwa Mujaahid].
Maulamaa wote wamekubaliana kwamba mwanamke haingiliwi na mumewe – hata kama damu imekatika – mpaka aoge, kinyume na Ibn Hazm.
· Ikiwa mke wa Muislamu ni Ahlul-Kitaab, je atalazimishwa kuoga?
Atalazimishwa kuoga, na mumewe haruhusiwi kumkurubia mpaka baada ya kuoga, kwani Aayah haimbagui mwanamke Muislamu au asiye Muislamu. [Tafsiyr ya Al-Qurtubiy (3/90)].
4- Ni lazima mwanamke mwenye hedhi amgomee mumewe akitaka kumwingilia, lakini kama atazidiwa nguvu, basi habebi jukumu, bali ataomba maghfirah kwa Allaah Mtukufu. [Jaami’u Ahkaamin Nisaa (1/180)]
4- Kutufu
Kwa Ijma’a ya Maulamaa, ni haramu kwa mwenye hedhi kutufu. Na dalili ya hili ni Hadiyth ya Mama wa Waumini 'Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) kwamba alipopata hedhi wakati wa kufanya ‘amali za Hijjah, Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia:
(( إفعلي ما يفعل الحاج غير أن لا تطوفي بالبيت حتى تطهري))
((Fanya ayafanyayo mwenye kuhiji, lakini usitufu Nyumba (Ka'bah) mpaka utwaharike)). [Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (1650)].
Maelezo zaidi yatakuja kuhusiana na hili katika mlango wa Hajji Insha Allaah.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
080-Mambo Yanayoruhusiwa Kwa Mwenye Hedhi
Alhidaaya.com [3]
1- Kusoma nyiradi na Qur-aan
Kama ilivyotangulia nyuma, inajuzu kwa mwenye hedhi au janaba kufanya hivyo kwa kauli yenye nguvu zaidi. Haya ni madhehebu ya Abu Haniyfah, na mashuhuri katika madhehebu ya Ash-Shaaf'iy na Ahmad. [Yamenukuliwa haya na Shaykh wa Uislamu katika Al-Fataawaa (21/459)]
Ibn Hazm katika Al-Muhallaa (1/77, 78) anasema:
"Kusoma Qur-aan, kusujudu kwenye Aayah ya sajdah, kuugusa Msahafu na kufanya nyiradi, hayo ni matendo ya kheri, yaliyosuniwa na yenye thawabu. Basi mwenye kudai kwamba hayo hayafai, basi alete dalili".
2- Kusujudu kama atasikia Aayah ya sajdah
Hakuna ubaya mwanamke mwenye hedhi kusujudu anaposikia Aayah ya sajdah, kwani sajdah si Swalaah, na wala si lazima awe na twahara.
Imethibiti katika Swahiyh Al-Bukhaariy (4862) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisoma Suwrat An-Najm, akasujudu yeye, kisha wakasujudu pamoja naye Waislamu, washirikina, majini na wanaadamu.
Ni mbali kusema kuwa wote walikuwa na wudhuu, kisha sajdah ya kisomo si Swalaah. Az-Zuhriy na Qataadah wamesema hayo hayo kama ilivyo katika Muswannaf wa ‘Abdur-Raaziq. [Jaami’u Ahkaamin Nisaa (1/174) kwa maana yake]
3- Kugusa Msahafu
Hatuijui dalili yoyote ya wazi inayomzuia mwenye hedhi kugusa Msahafu ijapokuwa Maulamaa wengi wanasema kuwa haijuzu kwa mwenye hedhi kugusa Msahafu. Na haya yashaelezewa kwa urefu nyuma.
4- Mume kusoma Qur-aan akiwa kwenye paja la mkewe mwenye hedhi
Ni kwa Hadiyth ya Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) aliyesema:
"Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiisoma Qur-aan na kichwa chake kipo kwenye paja langu nami niko hedhini" [Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (7549) na Muslim (uk. 246) na wengineo].
5- Kuhudhuria Swalaah za ‘Iyd Mbili
Hili halina ubaya, bali ni jambo mustahabu kwa wenye hedhi watoke ili kuhudhuria Swalaah ya ‘Iyd, lakini watakaa kando ya uwanja wa Swalaah.
Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((يخرج العواتق وذوات الخدور والحيض وليشهدن الخير ودعوة المؤمنين، ويعتزل الحيض المصلى))
((Watoke wazee wakongwe, waliotawishwa na wenye hedhi, ili waishuhudie kheri na du’aa za Waumini, lakini wenye hedhi wawe kando ya uwanja wa Swalaah)). [Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy katika sehemu tofauti, kati yake ni nambari (324)].
6- Kuingia Msikitini
Suala hili lina mvutano mkubwa kati ya Maulamaa, nalo limeshachambuliwa hapo kabla. [Ni mwisho wa Mlango wa Kuoga]
Tunachoweza kusema ni kuwa sisi hatujagundua dalili yoyote sahihi na ya wazi inayomzuia mwenye hedhi kuingia Msikitini. Na asili ya jambo lolote ni uhalali mpaka liwepo la kuliharamisha. Lakini pamoja na hayo, kila mmoja aendelee kufanya istikhaarah kwa Allaahu Ta'alaa kuhusu suala hili.
7- Kulishana na kunyweshana na mumewe
Imepokelewa toka kwa Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) akisema:
"Nilikuwa nikinywa huku niko hedhini, kisha nampa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), naye anaweka kinywa chake mahala nilipoweka kinywa changu, kisha anakunywa. Na ninang'ata mnofu wa nyama nikiwa hedhini, kisha ninampa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), naye anaweka kinywa chake mahala pa kinywa changu.” [Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (300), Abuu Daawuud (259), An Nasaaiy (1/59) na Ibn Maajah].
8- Kumtumikia mumewe
Ni kama kumwosha kichwa au kumchana nywele. Imepokelewa na Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anha) akisema:
"Nilikuwa nikimchana Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nywele nami niko hedhini". [Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (295) na Muslim (297)].
9- Kulala na mumewe ndani ya shuka moja
Imepokelewa toka kwa Mama wa Waumini Ummu Salamah (Radhwiya Allaahu ‘anha) akisema:
"Wakati nikiwa na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) tumelala katika shuka, nilipata hedhi, kisha nilijichomoa nikachukua nguo yangu ya hedhi. Akaniuliza: Je, umepata hedhi? Nikamjibu: Ndio, halafu akaniita nikalala naye ndani ya qatifa". [Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (298) na Muslim (296)].
Katika Sharh Muslim (1/954) An-Nawawiy anasema: "Inajuzu kulala na mwenye hedhi katika blanketi moja."
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
081-Damu Ya Nifasi
Alhidaaya.com [3]
Ni damu inayomtoka mwanamke kwa sababu ya kujifungua.
1- Muda wake
Hakuna uchache wa muda wa kutoka kwake. Maulamaa wote wamekubaliana kuwa wakati wowote mwanamke anapoona utwahara – hata kabla ya kumalizika siku arobaini – basi ataoga, ataswali na mumewe anaweza kumwingilia. [Imenukuliwa na At-Tirmidhiy katika As-Sunan (1/429)]
Ama upeo wa juu zaidi wa muda anaosubiri mwanamke endapo damu ya nifasi itaendelea, Jamhuri ya Maulamaa wanaona kuwa ni siku arobaini, kisha ataoga na kuswali. Hili wamelitolea dalili kwa Hadiyth ya Mama wa Waumini Ummu Salamah (Radhwiya Allaahu ‘anha) aliyesema:
"Wakati wa enzi ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihii wa sallam), wanawake wenye nifasi walikuwa wakikaa siku arobaini au masiku arobaini baada ya nifasi". [Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (307), At-Tirmidhiy (139) na Ibn Maajah (648). Wametofautiana katika kuifanya Hadiyth Hasan, lakini kauli yenye nguvu ni kuwa ni Hadiyth Dhwa’iyf. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi. Lakini pamoja na hivyo, inafanyiwa kazi].
2- Maulamaa wote wamekubaliana kuwa nifasi ni kama hedhi katika yote yaliyohalalishwa, yaliyoharamishwa, yaliyo makruhu na yaliyo manduwb. [Nayl Al-Awtwaar ya Ash-Shawkaaniy (1/386)]
3- Nifasi inatofautiana na hedhi kwa kuwa eda haihesabiwi, kwani eda humalizika kwa kujifungua kabla ya kutoka damu ya nifasi. [Al-Mughniy ya Ibn Qudaamah (1/350)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
082-Damu Ya Istihaadhwah
Alhidaaya.com [3]
Ni damu inayomtoka mwanamke katika nyakati zisizo za hedhi au nifasi, na wala haina uhusiano nazo. Ni damu isiyo ya kikawaida au kimaumbile, bali inatokana na mshipa uliokatika wenye kutoa damu nyekundu isiyokatika ila baada ya kupona. [Huitwa kuvuja damu]
Hukmu Yake
Mwanamke anapotokwa na damu hii, anabakia kuwa twahara, na damu haimzuii kuswali au kufunga kwa mujibu wa Ijma’a ya Maulamaa. Ikiwa damu hii itatoka katika wakati usio wa hedhi au nifasi bila kuwa na uhusiano navyo, basi hakuna tatizo.
Ikiwa damu hii haikatiki, nini mwanamke atafanya?
Tunasema:
“Mwanamke huyu haepukani na moja kati ya hali nne:
1- Ima atakuwa anaingia hedhini kawaida na anakijua kipimo cha hedhi yake. Huyu ataangalia kipimo hicho, kisha ataoga na ataswali. Na damu itakayoendelea baada ya hapo, itakuwa ni damu ya istihaadhwah na wala si ya hedhi.
Imepokelewa na Mama wa Waumini 'Aaishah akisema: "Ummu Habiybah alimuuliza Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu damu. Mama wa Waumini 'Aaishah akamwambia: Nimeona beseni lake limejaa damu. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia:
(( امكثي قدر ما كانت تحبسك حيضتك ثم اغتسلي وصلي))
((Kaa kitambo cha hedhi inavyokuzuia, kisha oga na uswali)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (uk. 264), Abuu Daawuud (279), na An-Nasaaiy (1/119)].
2- Ima atakuwa haijui hedhi yake, lakini anaweza kupambanua kati ya damu ya hedhi na damu ya istihaadhwah. Hapo ataisubiri damu yake ya hedhi, ataacha kuswali, kisha ataoga na kuswali baada ya kumalizika hedhi yake.
Imepokelewa na Mama wa Waumini 'Aaishah akisema:
"Alikuja Faatwimah binti Abu Hubaysh kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Mimi ni mwanamke nipataye damu ya istihaadhwah na wala sitwahariki, je, niache kuswali? Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi waalihi wa sallam) akamwambia:
(( لا، إنما ذلك عرق، وليس بحيض، فإذا أقبلت حيضتك فدعي الصلاة، وإذا أدبرت فاغسلي عنك الدم ثم صلي)).
((Hapana, huo ni mshipa, na wala si hedhi, na ikija hedhi yako basi acha Swalaah, na ikimalizika, jitwaharishe kisha swali)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al Bukhaariy (228) Muslim (uk. 262) na wengineo].
3- Ima atakuwa ndio mwanzo wa kupata hedhi na hawezi kupambanua kati ya damu ya hedhi na damu nyingineyo. Huyu ataiangalia hali ya wanawake wengi inavyokuwa. Na kama hali ya wanawake wengi anaoishi nao ni kudumu hedhi yao kwa muda wa siku sita au saba kila mwezi kwa mfano, basi atasubiri pale inapoanza hedhi yake, kisha atahesabu siku sita au saba na kuzifanya ndio siku za hedhi yake, kisha baada ya hapo ataoga. Na damu itakayoendelea baada ya hapo, ataizingatia kuwa ni damu ya istihaadhwah.
Imepokelewa kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Himnah binti Jahsh:
((إنما هذه ركضة من ركضات الشيطان، فتحيضي ستة أو سبعة في علم الله ثم اغتسلي، حتى إذا رأيت أنك قد طهرت واستنقيت فصلي أربعا وعشرين ليلة أو ثلاثا وعشرين وأيامهن، وصومي، فإن ذلك يجزيك، وكذلك فافعلي في كل شهر، كما تحيض النساء وكما يطهرن لميقات حيضهن وطهرن)).
((Hakika hii ni adha katika adha na masumbufu ya shaytwaan. Basi kaa na hedhi yako, siku sita au saba kwa mujibu wa Hukmu ya Allaah, kisha oga. Mpaka utakapoona umetwaharika na umetakasika kabisa, basi swali siku ishirini na tatu au ishirini na nne, na ufunge, hilo litakutosheleza. Fanya hivyo hivyo kila mwezi kama wanavyopata wanawake hedhi na kutwaharika katika nyakati zao)). [Imefanyiwa “ikhraaj” na Abuu Daawuud (287), Ash-Shaafi'iy katika Al-Ummu (1/51), Ibn Maajah (622) na At-Tirmidhiy katika mlango wa 95 wa twahara, na Sanad yake ni Layyin. Katika Al-Irwaa (205), Al-Albaaniy amesema ni Hadiyth Hasan]
4- Ima awe mwanamke amesahau ada yake kwa kiasi chake na wakati wake wa kuja, na hawezi kupambanua kati ya damu ya hedhi na istihaadhwah. [Maulamaa wanamwita mwanamke huyu "mbabaikaji"]
Maulamaa wamezungumza kauli kadhaa kuhusiana na mwanamke huyu. Kauli iliyo dhahiri zaidi ni kuwa mwanamke huyu anakuwa ni kama yule mwanamke anayeanza kupata hedhi ambaye hukmu yake ishaelezwa katika hali ya tatu iliyotangulia. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
083-Hukmu Zinazohusiana Na Mwanamke Mwenye Istihaadhwah
Alhidaaya.com [3]
1- Hukmu yake ni kama mwanamke aliye twahara, hakatazwi lolote katika yale aliyokatazwa mwenye hedhi.
2- Anaruhusiwa kuswali, kufunga, kusoma Qur-aan, kugusa Msahafu, kusujudu sajdah ya kisomo, na sajdah ya kumshukuru Allaah, na mengineyo anayoruhusiwa aliye twahara. Na hii ni kwa Ijma’a’ ya Maulamaa.
3- Halazimiki kutawadha kila Swalaah madhali hakutengukwa na wudhuu, kwani kauli yenye nguvu inaashiria kuwa habari zote zinazogusia hilo ni dhwa’iyf. [Zirejelee katika kitabu cha Jaami’u Ahkaamin Nisaa (1/230) na yanayofuatia]
Lakini lililobora pamoja na hivyo, ni kutawadha au kuoga kwa kila Swalaah kutokana na Hadiyth ya Mama wa Waumini 'Aaishah kwamba Mama wa Waumini Ummu Habiybah alipatwa na damu ya istihaadhwah kwa muda wa miaka saba. Akamuuliza Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu hilo, na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwamrisha akoge akimwambia:
(( هذا عرق))
((Huu ni mshipa)), na akawa anaoga kwa kila Swalaah. [Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (327), Muslim (262) na wengineo].
4-Mumewe anaweza kumwingilia madhali si wakati wa hedhi hata kama damu inamtoka. Hii ndiyo kauli ya Maulamaa wengi. [Al Majmu’u (2/372), na Al-Mughny (1/339)]
5-Inajuzu kukaa ‘itikaaf Msikitini. Imepokelewa na ‘Aaishah akisema:
“Mmoja katika wakeze wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), alikaa naye ‘itikaaf. Alikuwa akitokwa na damu na unjano na beseni liko chini yake huku akiswali”. [Al-Bukhaary]
An-Nawawy katika Sharhu Muslim (1/631) ameinukulu Ijma’a ikisema kwamba mwenye istihaadhwah katika ‘itikaaf, ni kama mwanamke yeyote mwingine mwenye twahara.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/284
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9437&title=01-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D8%B7%D9%91%D9%8E%D9%87%D9%8E%D8%A7%D8%B1%D9%8E%D8%A9%D9%90%20-%20Kitabu%20Cha%20Twahara%20%20%20
[3] http://www.alhidaaya.com/
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9536&title=000-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Utangulizi%20Wa%20Alhidaaya
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9438&title=001-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3ATaarifu%20Ya%20Twahara%20Na%20Umuhimu%20Wake%20%20%20
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9439&title=002-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Aina%20Za%20Twahara
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9440&title=003-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%20Manii%20Ni%20Twahara%20Au%20Najsi%3F
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9441&title=004-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%2C%20Pombe%20Ni%20Najsi%3F
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9442&title=005-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%20Damu%20Ni%20Najsi%3F
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9443&title=006-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%2C%20Matapishi%20Ya%20Mwanadamu%20Ni%20Najsi%3F
[11] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9444&title=007-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Nini%20Hukmu%20Ya%20Majimaji%20Yanayotoka%20Kwenye%20Utupu%20Wa%20Mwanamke%20Au%20Unyevunyevu%20Wa%20Utupu%20Wake%3F
[12] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9534&title=008-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Najsi%20Zinazosamehewa
[13] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9535&title=009-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Namna%20Ya%20Kuzitwaharisha%20Aina%20Za%20Najsi%20Zilizobainishwa%20na%20Hadiyth%20
[14] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9537&title=010-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%2C%20Ni%20Lazima%20%28Kutumia%29%20Maji%20Katika%20Kuondoshea%20Najsi%3F%20Au%20Inajuzu%20Kuondoshea%20Kwa%20Vimiminika%20Vinginevyo%20Au%20Mada%20Nyinginezo%3F%20
[15] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9538&title=011-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kustanji%20%28Kuchamba%29
[16] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9539&title=012-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kitu%20Gani%20Hutumika%20Kustanjia%3F
[17] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9540&title=013-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Baadhi%20Ya%20Adabu%20Za%20Kustanji
[18] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9541&title=014-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Ni%20Vipi%20Mgonjwa%20Wa%20Kichocho%20Au%20Mfano%20Wake%20Anastanji%3F
[19] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9542&title=015-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Adabu%20Za%20Kukidhi%20Haja
[20] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9543&title=016-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%2C%20Inafaa%20Mtu%20Kukojoa%20Kwa%20Kusimama%3F
[21] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9544&title=017-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Sunnah%20Za%20Hulka%20Asilia
[22] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9545&title=018-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kutahiri
[23] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9546&title=019-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kupiga%20Mswaki
[24] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9547&title=020-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%2C%20Kuna%20Wakati%20Maalum%20Wa%20Kukata%20Kucha%2C%20Kukata%20Sharubu%2C%20Kunyofoa%20Nywele%20Za%20Kikwapa%20Na%20Kunyofoa%20Kinena%3F
[25] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9548&title=021-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kufuga%20Ndevu
[26] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9549&title=022-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Twahara%20Za%20Kihukmu
[27] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9550&title=023-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kutawadha%20Kwa%20Maji%20Yanayochuruzika%20Toka%20Viungo%20Vya%20Wudhuu
[28] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9551&title=024-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Inajuzu%20Kwa%20Mwanaume%20Kuogea%20Kwa%20Mabaki%20Ya%20Maji%20%28Aliyojitwaharishia%20Mwanamke%29
[29] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9552&title=025-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Wudhuu%20Taarifu%20Yake%20Na%20Dalili%20Ya%20Usharia%20Wake
[30] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9553&title=026-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Fadhila%20Za%20Wudhuu
[31] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9554&title=027-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Sifa%20Ya%20Wudhuu%20Uliokamilika%20%28Kiujumla%29
[32] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9555&title=028-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Niya%20Ni%20Sharti%20Ya%20Kuswihi%20Wudhuu%20
[33] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9556&title=029-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Nguzo%20Za%20Wudhuu
[34] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9557&title=030-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Sunnah%20Za%20Wudhuu
[35] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9559&title=031-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Yanayotengua%20Wudhuu
[36] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9563&title=032-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Mambo%20Yasiyotengua%20Wudhuu
[37] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9564&title=033-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Wudhuu%20Unapasa%20Kwa%20Ajili%20Ya%20Swalaah%20Tu%20Na%20Si%20Vinginevyo
[38] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9587&title=034-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Mambo%20Ambayo%20Mtu%20Akiyafanya%20Imesuniwa%20Awe%20Na%20Wudhuu
[39] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9599&title=035-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kupaka%20Juu%20Ya%20Vizuizi%20
[40] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9601&title=036-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Hukmu%20Ya%20Kupukusa%20Juu%20Ya%20Khufu%20Mbili
[41] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9600&title=036-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Usharia%20Wa%20Kupaka%20Juu%20Ya%20Khufu%20Mbili
[42] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9602&title=037-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Muda%20Wa%20Kupukusa
[43] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9603&title=038-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Muda%20Wa%20Kupukusa%20Unapoanzia
[44] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9604&title=039-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Mkazi%20Akipukusa%20Kisha%20Akasafiri
[45] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9605&title=040-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Msafiri%20Akipukusa%20Kisha%20Akawasili%20Mjini%20Kwake
[46] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9606&title=041-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Masharti%20Ya%20Kupukusa
[47] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9607&title=042-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%2C%20Khufu%20Iliyotoboka%20Hupukuswa%3F
[48] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9608&title=043-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Mahala%20Pa%20Kupukusa%20Na%20Sifa%20Yake
[49] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9609&title=044-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Yanayotengua%20Kupukusa
[50] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9610&title=045-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Uzindushi%3A%20Kubatilika%20Upukusaji%20Hakumaanishi%20Kutenguka%20Wudhuu
[51] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9611&title=046-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kupaka%20Juu%20Ya%20Soksi%20Na%20Viatu
[52] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9612&title=047-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Tatu%3A%20Kupaka%20Juu%20Ya%20Kinachofunika%20Kichwa
[53] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9613&title=048-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Nne%3A%20Kupaka%20Juu%20Ya%20%E2%80%9CAl%20Jabiyrah%E2%80%9D
[54] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9614&title=049-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kuoga
[55] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9615&title=050-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Majosho%20Yaliyo%20Mustahabbu
[56] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9618&title=051-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Niya%20Ni%20Sharti%20Ya%20Kusihi%20Kukoga
[57] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9619&title=052-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Nguzo%20Ya%20Kuoga
[58] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9620&title=053-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Yaliyosuniwa%20Wakati%20Wa%20Kukoga%20%28Picha%20Ya%20Josho%20Kamili%29
[59] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9627&title=054-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20%20Kuoga%20Mwanamke%20Janaba
[60] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9628&title=055-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kuoga%20Mwanamke%20Hedhi%20Na%20Nifasi%20
[61] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9629&title=056-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kukausha%20Viungo%20Baada%20Ya%20Kuoga
[62] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9631&title=057-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Masuala%20Yanayohusiana%20Na%20Kuoga
[63] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9633&title=058-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Masuala%20Yanayohusiana%20Na%20Mwenye%20Janaba
[64] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9634&title=059-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%2C%20Inajuzu%20Kwa%20Mwenye%20Hedhi%20Na%20Mwenye%20Janaba%20Kuingia%20Msikitini%20Na%20Kukaa%20Humo%3F
[65] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9638&title=060-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kutayammamu%20
[66] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9639&title=061-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Usharia%20Wa%20Kutayammamu
[67] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9640&title=062-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Ni%20Kipi%20Kinatosheleza%20Tayammumi%3F
[68] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9641&title=063-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Hali%20Ambazo%20Kutayammamu%20Kunaruhusiwa
[69] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9642&title=064-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Mwenye%20Maji%20Kidogo%20Ambayo%20Hayatoshi%20Ila%20Kwa%20Baadhi%20Ya%20Viungo%20Vyake
[70] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9643&title=065-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Ikiwa%20Kuna%20Maiti%2C%20Mwenye%20Janaba%2C%20Mwenye%20Hedhi%20na%20Mwenye%20Najsi%20Mwilini%2C%20Na%20Maji%20Yaliyopo%20Hayatoshi%20Ila%20Kwa%20Mmoja%20Wao%20Tu%2C%20Nani%20Atapewa%20Kipaumbele%3F%20
[71] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9644&title=066-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kutayammamu%20Mgonjwa%20Ambaye%20Anajihofia%20Madhara%20Kama%20Atatumia%20Maji
[72] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9645&title=067-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Nini%20Atafanya%20Mwenye%20Jeraha%3F
[73] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9646&title=068-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Anayechelea%20Kudhurika%20Kwa%20Maji%20Baridi%2C%20Je%20Anaweza%20Kutayammamu%20Akiwa%20Na%20Janaba%3F
[74] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9647&title=069-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Je%20Anaweza%20Kutayammamu%20Mtu%20Ambaye%20Wakati%20Umekuwa%20Mfinyu%20Kwake%20Na%20Wakati%20Wa%20Swalaah%20Utampita%20Kama%20Atatumia%20Maji%3F%20
[75] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9648&title=070-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Anayeamka%20Usingizini%20Muda%20Wa%20Swalaah%20Ukawa%20Mfinyu%2C%20Je%20Atayammamu%20Ili%20Auwahi%20Wakati%3F
[76] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9649&title=071-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Ni%20Sehemu%20Ipi%20Ya%20Ardhi%20Inayofaa%20Kutayamamia%3F
[77] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9650&title=072-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Mwenye%20Kukosa%20Vitwaharisho%20Viwili%20%28Maji%20Na%20Mchanga%29
[78] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9651&title=073-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Yanayohusiana%20Na%20Niya%20Ya%20Kutayammam
[79] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9652&title=074-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Namna%20Sahihi%20Ya%20Kutayammamu
[80] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9653&title=075-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Masuala%20Mbalimbali%20Kuhusu%20Tayammumi
[81] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9654&title=076-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Hedhi%20Na%20Nifasi%20%20%20
[82] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9655&title=077-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kuanza%20Na%20Kumalizika%20Hedhi
[83] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9656&title=078-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Nini%20Hukmu%20Ya%20Unjano%20Na%20Rangi%20Yenye%20Kumili%20Weusi%20Baada%20Ya%20Kutwaharika%20Na%20Hedhi%3F
[84] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9657&title=079-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Yaliyoharamishwa%20Kwa%20Mwenye%20Hedhi%20Na%20Nifasi
[85] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9658&title=080-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Mambo%20Yanayoruhusiwa%20Kwa%20Mwenye%20Hedhi
[86] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9659&title=081-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Damu%20Ya%20Nifasi
[87] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9660&title=082-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Damu%20Ya%20Istihaadhwah
[88] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9661&title=083-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Hukmu%20Zinazohusiana%20Na%20Mwanamke%20Mwenye%20Istihaadhwah