Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Twahara
060-Kutayammamu
Alhidaaya.com [1]
(Katika mlango huu, nilifaidika sana kutokana na utafiti uliotayarishwa na kaka yangu Twaariq Saalim (Allaah Amlipe jaza Yake ) kwa ajili ya kujipatia “Master” katika sharia).
Kutayammamu Kilugha Na Kisharia [Al-Majmu’u (2/238), Al-Mughniy (1/148) na Al-Mabsuwtw (1/106)]
Kilugha ni kukusudia. Ikisemwa: ،(تيممت فلانا، يممته، تأممته وأممته)inamaanisha: Nimemkusudia fulani.
Allaah Mtukufu Anasema:
((ولا تيمموا الخبيث منه تنفقون))
((Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya..)). [Al-Baqarah (2:267)].
Ama kisharia, ni kuukusudia mchanga wa juu ya ardhi kwa ajili ya kuhalalika yanayohalalishwa na wudhuu na kuoga.
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9638&title=060-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Twahara%3A%20Kutayammamu%20