Mchuzi Wa Kamba (Prawns) Kwa Sosi Ya Nyanya Na Kotmiri

Mchuzi Wa Kamba (Prawns) Kwa Sosi Ya Nyanya Na Kotimiri
 

 

Vipimo 

 

Kamba -  1 Lb                

Vitunguu -   3 katakata

Nyanya -  4 zisage

Pilipili za kijani - kiasi 3

Kitunguu saumu (thomu/garlic) - 1 kijiko cha chai

Tangawizi - 1 kijiko cha chai

Uzile (bizari ya pilau ya unga-Jiyra) - ½ kijiko cha chai

Bizari ya mchuzi - 1 kijiko cha chai

Pilipili ya unga -  ½ kijiko cha chai

Nyanya ya kopo -  2 vijiko vya supu

Chumvi -  kiasi

Ndimu  - nusu kamua

Kotimiri - kiasi katakata

Mafuta - 1/4 kikombe

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Changanya kamba na  thomu, tangawizi, pilipili manga, pilipili ya unga, jira,  na chumvi.
  2. Katakata vitunguu weka pembeni.
  3. Katakata pilipili sehemu mbili kwa urefu.
  4. Saga nyanya au katakata weka pembeni.
  5. Weka mafuta katika kikaangio au sufuria.
  6. Kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi ya ligh brown.
  7. Tia nyanya na tia nyanya kopo kaanga kidogo
  8. Tia bizari ya mchuzi
  9. Tia maji kidogo upate sosi.
  10. Tia kamba uache katika moto, koroga uache kamba wapikike (kama ni wa freezer hawachukui muda kuiva).
  11. Tia ndimu kidogo
  12. Mwagia kotimiri ulokatakata, ikiwa tayari kuliwa

 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kuburudika)

 

 

 

Share