Mitai
VIPIMO
Unga wa ngano 1 1/2 Kikombe
Baking powder 1 Kijiko cha chai
Baking soda ¼ Kijiko cha chai
Kungumanga(nutmeg) 3/4-1 kijiko cha chai
Chumvi ½ kijiko cha chai
Sukari 1 kijiko cha supu
Hamira 1/2 Kijiko cha supu
Yai 1
Maziwa ½ Kikombe
Mafuta ya kukaangia
SHIRA
Sukari 1 Kikombe
Maji ½ Kikombe
Iliki au Mdalasini ¼ kijiko cha chai (ya unga)
NAMNA YA KUTAYARISHA
1. Kwenye bakuli, changanya pamoja unga, baking powder, baking soda, chumvi, sukari, kungumanga na hamira.
2. Katika kibakuli, piga mayai na maziwa pamoja.
3. Changanya mchanganyiko wa mayai na wa unga ; na ukande
4. Ikisha fura, sukuma unga
5. Pasha moto mafuta na uchome hadi iwe rangi ya dhahabu, upande zote mbili.
6. Ipikie shira lakini isiwe nzito .
7. Tia mitai na upepete hadi sukari ienee kote na zitakuwa tayari kuliwa.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


