Supu Ya Adesi Na Brokoli

Supu Ya Adesi Na Brokoli

Vipimo

Adesi - 1 Kikombe cha chai

Brokoli - 1 Msongo

Viazi - 2

Kitunguu - 1 Kikubwa

Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa - 1 Kijiko cha chai

Karoti - 2

Nyanya - 1

Parsley - ¼ Kikombe

Pilipili manga - 1 Kijiko cha chai

Chumvi - Kiasi

Kidonge cha supu - 1

Ndimu - 1 Kijiko cha supu

Mafuta ya zaytuni - Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Osha adesi na chemsha hadi iive.
  2. Katakata karoti, viazi, brokoli, nyanya na vitunguu.
  3. Kisha chemsha pamoja karoti, brokoli na viazi hadi ziwive.
  4. Tia mafuta katika sufuria na ukaange vitunguu mpaka vilainike, tia thomu, kisha nyanya na endelea kukaanga.
  5. Halafu tia pilipili manga, kidonge cha supu na chumvi.
  6. Kisha mimina vile vitu ulivyochemsha pamoja na supu yake katika mkaango.
  7. Tia vitu vyote katika mashine ya kusagia.
  8. Tia parsley na usage kidogo tu.
  9. Kisha rudisha katika sufuria kwenye moto, tia ndimu na ipike kidogo kwa muda wa dakika moja tu na itakuwa tayari kwa kuliwa.
Share