Hukmu Ya Anayeswali Ijumaa Pekee Na Kuacha Swalaah Zilizobaki
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)
SWALI:
Kuna mtu anaswali Ijumaa pekee bila kuswali Fardhi zilizobaki, je, inakubaliwa Swalaah yake?
JIBU:
Haikubaliwi Swalaah yake, kwa hakika amekuwa Kafiri kwa hilo.
Swalaah yake ya Ijumaa, Swawm yake, na matendo yake yote ni batili.
Anasema Aliyetukuka:
"Na kama wangemshirikisha bila shaka yangebatilika yale waliyokuwa wakitenda." [Al-An'aam: 88]
Na Anasema Aliyetakasika:
"Na yeyote atakayekufuru iymaan; basi kwa yakini zimebatilika 'amali zake; naye Aakhirah atakuwa miongoni mwa waliokhasirika." [Al-Maaidah: 5]
Basi yule anayekufuru kufru kubwa au shirki kubwa, huporomoka matendo yake.
Tunamuomba Allaah afya (Atulinde).
Na kuacha Swalaah ni kufru kubwa."
[Nuwr 'Alaa Ad-Darb, 13/339]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/205
[2] http://www.alhidaaya.com/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7279&title=Imaam%20Ibn%20Baaz%3A%20Hukmu%20Ya%20Anayeswali%20Ijumaa%20Pekee%20Na%20Kuacha%20Swalaah%20Zilizobaki