Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب الخروج يوم الخميس ، واستحبابه أول النهار
01-Mlango Wa Kupendeza Kusafiri Siku ya Alkhaamis na Kupendeza Kuondoka Mwanzo wa Mchana
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن كعب بن مالك رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم خَرَجَ في غَزْوَةِ تَبُوكَ يَوْمَ الخَمِيس ، وَكَانَ يُحِبُّ أنْ يَخْرُجَ يَوْمَ الْخَميسِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
وفي رواية في الصحيحين: لقَلَّمَا كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَخْرُجُ إِلاَّ في يَوْمِ الخَمِيسِ.
Imepokewa kutoka kwa Ka'ab bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitoka kwa ajili ya Vita vya Taabuk siku ya Alkhamisi. Na alikuwa akipenda kutoka siku ya Alkhamis." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Katika riwaayah iliyopo katika Swahiyh mbili: Ni mara chache sana Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akitoka isipokuwa siku ya Alkhamisi.
Hadiyth – 2
وعن صخر بن وَداعَةَ الغامِدِيِّ الصحابيِّ رضي الله عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( اللَّهُمَّ بَارِكْ لأُمَّتِي في بُكُورِهَا )) وَكَانَ إِذَا بَعَثَ سَرِيَّةً أَوْ جَيْشَاً بَعَثَهُمْ مِنْ أوَّلِ النَّهَارِ . وَكَانَ صَخْرٌ تَاجِراً ، وَكَانَ يَبْعَثُ تِجَارَتَهُ أوَّلَ النَّهَار ، فَأَثْرَى وَكَثُرَ مَالُهُ . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Swahaba, Swakhr bin Wadaa'ah Al-Ghaamidy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ee Mola! Ubariki Ummah wangu katika kuwahi kwao." Na alikuwa anapotuma mwanzo wa mchana. Na Swakhr alikuwa ni mfanya biashara, naye alikuwa daima akituma biashara zake mwanzo wa mchana, hivyo biashara yake ikashamiri na mali yake kuongezeka." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب طلب الرفقة وتأميرهم عَلَى أنفسهم واحداً يطيعونه
02-Mlango Wa Kupendeza Kusafiri kwa Kikundi Chini ya Kiongozi na Kumtii
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمرَ رضي اللهُ عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لَوْ أنَّ النَّاسَ يَعْلَمُونَ مِنَ الوحدَةِ مَا أعْلَمُ، مَا سَارَ رَاكبٌ بِلَيْلٍ وَحْدَهُ ! )) رواه البخاري.
Imepokewa Kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau kwamba watu wangejua katika upweke ninayoyajua, basi msafiri asingekwenda usiku hali ya kuwa peke yake." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن عمرِو بن شُعَيْبٍ، عن أبيه، عن جَدهِ رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( الرَّاكِبُ شَيْطَانٌ ، وَالرَّاكِبَانِ شَيْطَانَانِ ، وَالثَّلاَثَةُ رَكْبٌ )) رواه أَبُو داود والترمذي والنسائي بأسانيد صحيحةٍ ، وقال الترمذي : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Amru bin Shu'ayb kutoka kwa babake kutoka kwa babu yake (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msafiri mmoja ni shetani, na wasafiri wawili ni mashetani wawili na wasafiri watatu ni msafara." [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai kwa Isnaad Swahiyh na akasema At-Tirmidhiy ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 3
وعن أَبي سعيد وأبي هُريرة رضي اللهُ تَعَالَى عنهما، قالا : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا خَرَجَ ثَلاَثَةٌ في سَفَرٍ فَليُؤَمِّرُوا أحَدَهُمْ )) حديث حسن ، رواه أَبُو داود بإسنادٍ حسن .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy na Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wakitoka watu watatu katika safari wamfanye mmoja wao kiongozi." [Hadiyth Hasan, Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Hasan]
Hadiyth – 4
وعن ابن عبّاسٍ رضي الله عنهما ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( خَيْرُ الصَّحَابَةِ أرْبَعَةٌ ، وَخَيْرُ السَّرَايَا أرْبَعُمِئَةٍ ، وَخَيْرُ الجُيُوشِ أرْبَعَةُ آلاَفٍ ، وَلَنْ يُغْلَبَ اثْنَا عَشَرَ ألْفاً مِنْ قِلةٍ )) رواه أَبُو داود والترمذي، وقال : (( حديث حسن )).
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Bora wa masahibu katika kikundi ni wanne, na bora wa kipote kidogo cha jeshi ni watu mia nne na bora wa jeshi ni elfu nne na jeshi la watu elfu kumi na mbili haliwezi kushindwa kwa sababu ya uchache." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب آداب السير والنـزول والمبيت
والنوم في السفر واستحباب السُّرَى والرفق بالدواب
ومراعاة مصلحتها وأمر من قصّر في حقها بالقيام بحقها
وجواز الإرداف عَلَى الدابة إِذَا كانت تطيق ذلك
03-Mlango Wa Adabu za Safari na Kuteremka na Kupumzika Usiku Kuwahurumia Wanyama na Kuchunga Maslahi Yao na Haki Zao na Kufaa Kulala Juu ya Mnyama Ikiwa Anaweza Jambo Hilo
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هُريرةَ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا سَافَرْتُمْ فِي الخِصْبِ ، فَأعْطُوا الإبلَ حَظَّهَا مِنَ الأَرْضِ ، وَإِذَا سَافَرْتُمْ في الجدْبِ ، فَأسْرِعُوا عَلَيْهَا السَّيْرَ ، وَبَادِرُوا بِهَا نِقْيَهَا ، وَإِذَا عَرَّسْتُمْ ، فَاجْتَنِبُوا الطَّرِيقَ ؛ فَإنَّهَا طُرُقُ الدَّوَابِّ ، وَمَأوَى الهَوَامِّ بِاللَّيْلِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mnapo safiri katika ardhi yenye rutuba wapatieni ngamia wenu haki yao kutoka katika ardhi na mnapo safiri kwenye jangwa nendeni nao haraka sana harakisheni kuhifadhi nguvu zao. Na mnapo simama usiku kwa ajili ya kupumzika, jiepusheni na barabara kwani hiyo ni njia ya wanyama na mapumziko ya wadudu wengine usiku." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي قتادة رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا كَانَ فِي سَفَرٍ ، فَعَرَّسَ بِلَيْلٍ اضْطَجَعَ عَلَى يَمِينهِ ، وَإِذَا عَرَّسَ قُبَيلَ الصُّبْحِ نَصَبَ ذِرَاعَهُ ، وَوَضَعَ رَأسَهُ عَلَى كَفِّهِ . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa safarini, akalala usiku hulalia ubavu wake wa kulia. Na akilala karibu na asubuhi, anasimamisha dhiraa yake, na anaweka kichwa chake katika kiganja chake. [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( عَلَيْكُمْ بِالدُّلْجَةِ ، فَإنَّ الأرْضَ تُطْوَى بِاللَّيْلِ )) رواه أَبُو داود بإسناد حسن .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Safirini usiku kwani ardhi (masafa) hufupishwa usiku." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Hasan]
Hadiyth – 4
وعن أَبي ثَعْلَبَةَ الخُشَنِيِّ رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ النَّاسُ إِذَا نَزَلُوا مَنْزِلاً تَفَرَّقُوا في الشِّعَابِ وَالأوْدِيَةِ . فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ تَفَرُّقكُمْ فِي هذِهِ الشِّعَابِ وَالأوْدِيَةِ إنَّمَا ذلِكُمْ مِنَ الشَّيْطَانِ ! )) فَلَمْ يَنْزِلُوا بَعْدَ ذَلِكَ مَنْزِلاً إِلاَّ انْضَمَّ بَعْضُهُمْ إِلَى بَعْضٍ . رواه أَبُو داود بإسناد حسن .
Imepokewa kwake Abu Tha'labah Al-Khushaniy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Watu walikuwa wanaposhuka mahali (sehemu) wanatawanyika, katika vichaka na mabonde. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Hakika kutawanyika kwenu kwenye vichaka na mabonde ni jambo kutoka kwa shetani." Kwa hiyo hakushuka mahali baada ya hapo, isipokuwa watapoungana baadhi yao na wengine. [Abu Daawuwd kwa Isnaad Hasan]
Hadiyth – 5
وعن سهل بن عمرو – وقيل : سهل بن الربيع بن عمرو الأنصاري المعروف بابن الحنظلِيَّة ، وَهُوَ من أهل بيعة الرِّضْوَانِ رضي الله عنه ، قَالَ : مَرَّ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم بِبَعِيرٍ قَدْ لَحِقَ ظَهْرُهُ بِبَطْنِهِ ، فَقَالَ : (( اتَّقُوا الله في هذِهِ البَهَائِمِ المُعجَمَةِ ، فَارْكَبُوهَا صَالِحَةً ، وَكُلُوهَا صَالِحَةً )) رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwake Sahl bin 'Amruw - na inasemwa Sahl bin A-Rabii' bin 'Amruw Al-Answaariy maarufu Ibnil Handhaliyyah (Radhwiya Allaahu 'anhu) naye ni katika watu wa ba'iah Ridhwaan (kabla ya Hudaybiyah) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita kwenye ngamia ambaye tumbo lake limeshikana na mgongo wake (amekondeana). Akasema: "Mcheni Allaah katika hawa wanyama wasiozungumza. Wapandeni wakiwa wazima, na kuleni nyama zake wakiwa wazima." [Abuu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Hadiyth – 6
وعن أَبي جعفر عبد الله بن جعفر رضي الله عنهما ، قَالَ : أردفني رسولُ الله صلى الله عليه وسلم ذَاتَ يَوْمٍ خَلْفَهُ ، وَأسَرَّ إليَّ حَدِيثاً لا أُحَدِّثُ بِهِ أحَداً مِنَ النَّاسِ ، وَكَانَ أحَبَّ مَا اسْتَتَرَ بِهِ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم لِحاجَتِهِ هَدَفٌ أَوْ حَائِشُ نَخْلٍ . يَعنِي : حَائِطَ نَخْلٍ . رواه مسلم هكَذَا مُختصراً .
وزادَ فِيهِ البَرْقاني بإسناد مسلم - بعد قَوْله : حَائِشُ نَخْلٍ - فَدَخَلَ حَائِطاً لِرَجُلٍ مِنَ الأنْصَارِ ، فَإذا فِيهِ جَمَلٌ ، فَلَمَّا رَأى رَسولَ الله صلى الله عليه وسلم جَرْجَرَ وذَرَفَتْ عَيْنَاهُ ، فَأتَاهُ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم فَمَسَحَ سَرَاتَهُ - أيْ : سِنَامَهُ - وَذِفْرَاهُ فَسَكَنَ ، فَقَالَ : (( مَنْ رَبُّ هَذَا الجَمَلِ ؟ لِمَنْ هَذَا الجَمَلُ ؟ )) فَجَاءَ فَتَىً مِنَ الأنْصَارِ ، فَقَالَ : هَذَا لِي يَا رسولَ الله . قَالَ : (( أفَلاَ تَتَّقِي اللهَ في هذِهِ البَهِيمَةِ الَّتي مَلَّكَكَ اللهُ إيَّاهَا ؟ فَإنَّهُ يَشْكُو إلَيَّ أنَّكَ تُجِيعُهُ وتُدْئِبُهُ )) رواه أَبُو داود كرواية البرقاني .
Abu Ja'far 'Abdillaah bin Ja'far (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alinikalisha siku moja nyuma yake akaninog'oneza maneno sitamueleza yoyote katika watu. Na alichopenda zaidi kujisitiri nacho Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa haja zake ilikuwa ni nyuma ya ukuta au ukuta wa mtende. [Muslim]
Na ameongeza Al-Barqaaniy ameongeza katika Isnaad ya Muslim baada ya kauli yake: Ukuta wa mtende, akaingia katika bustani la mtu miongoni mwa Answari kupitia katika ukuta wake, hapo akakuta ngamia. Ngamia huyo alipomuona Rasuli wa Allaah (Swalla allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akagumia na kububujikwa machozi. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuendea akampapasa nundu yake, Ngamia akatulia. akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ni nani bwana wa ngamia huyu?, Ngamia huyu ni wa nani?" Akaja kijana wa Ki-Answaar akasema: "Ni wangu, ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Humuogopi Allaah katika hawa wanyama ambao Allaah amekumilikisha? Kwani yeye amenishtakia kuwa wewe unakalisha njaa na unamtabisha." [Abu Daawuwd ameipokea kama riwaayah ya Al-Barqaaniy]
Hadiyth – 7
وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : كُنَّا إِذَا نَزَلْنَا مَنْزِلاً ، لاَ نُسَبِّحُ حَتَّى نَحُلَّ الرِّحَال . رواه أَبُو داود بإسناد عَلَى شرط مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema kuwa tulikuwa tunashuka mahali hatuswali hadi kwanza tufungue vipando." [Abu Daawuwd kwa Isnaad kwa sharti ya Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب إعانة الرفيق
04-Mlango Wa Kumsaidia Rafiki
Alhidaaya.com [4]
Katika Safari Zipo Hadiyth nyingi katika mlango huu ambazo tumetangulia kuzitaja, kama: "Na Allaah anamsaidia mja maadamu mja yu katika kumsaidia nduguye." Na Hadiyth: "Kila jema ni swadaqa", na mfano wake.
Hadiyth – 1
وعن أَبي سعيد الخدري رضي اللهُ عنه ، قَالَ : بَيْنَمَا نَحْنُ في سَفَرٍ إذْ جَاءَ رَجُلٌ عَلَى رَاحِلَةٍ لَهُ ، فَجَعَلَ يَصْرِفُ بَصَرَهُ يَمِيناً وَشِمَالاً ، فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ كَانَ مَعَهُ فَضْلُ ظَهْرٍ فَلْيَعُدْ بِهِ عَلَى مَنْ لاَ ظَهْرَ لَهُ ، وَمَنْ كَانَ لَهُ فَضْلُ زَادٍ فَلْيَعُدْ بِهِ عَلَى مَنْ لاَ زَادَ لَهُ )) ، فَذَكَرَ مِنْ أصْنَافِ المَالِ مَا ذَكَرَهُ ، حَتَّى رَأيْنَا ، أنَّهُ لاَ حَقَّ لأَحَدٍ مِنَّا فِي فَضْلٍ . رواه مسلم .
Imepokewa kwa Abu Sa'iid Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Tulikuwa safarini pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaja mtu juu ya kipando chake, akawa anageuza jicho lake kulia na kushoto. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Mwenye kipando cha zaidi ampe asiyekuwa nacho." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akataja aina za mali mpaka tukadhani kuwa hakuna haki kwa mmoja wetu kuwa na ziada katika chochote." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن جابر رضي اللهُ عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم : أنَّهُ أرَادَ أنْ يَغْزُوَ ، فَقَالَ : (( يَا مَعْشَرَ المُهَاجِرِينَ وَالأَنْصَارِ ، إن مِنْ إخْوَانِكُمْ قَوْماً لَيْسَ لَهُمْ مَالٌ ، وَلاَ عَشِيرةٌ ، فَلْيَضُمَّ أحَدكُمْ إِلَيْهِ الرَّجُلَيْنِ أَو الثَّلاَثَةَ ، فَمَا لأَحَدِنَا مِنْ ظَهْرٍ يَحْمِلُهُ إِلاَّ عُقْبةٌ كَعُقْبَةٍ )) يَعْني أحَدهِمْ ، قَالَ : فَضَمَمْتُ إلَيَّ اثْنَيْنِ أَوْ ثَلاَثَةً مَا لِي إِلاَّ عُقْبَةٌ كَعقبة أحَدِهِمْ مِنْ جَمَلِي . رواه أَبُو داود .
Imepokewa kutoka kwake Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipotaka kwenda katika vita alikuwa anatuambia: "Enyi kongamano la Muhajirina na Answaar! Hakika wapo miongoni mwenu ndugu zenu kaumu ambao hawana mali wala familia, hivyo kila mmoja wenu achukue watu wawili au watatu kwa sababu ya upungufu wa vipandio (wanyama wa kupanda), na kila mmoja apande kwa zamu. Nami niliunganisha watu wawili au watatu miongoni mwao na kushirikiana kwa zamu sawasawa katika kumpanda ngamia wangu." [Abu Daawuwd]
Hadiyth – 3
وعن جابر رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يَتَخَلَّفُ في المَسير ، فَيُزْجِي الضَّعِيف ، وَيُرْدِفُ وَيَدْعُو لَهُ . رواه أَبُو داود بإسناد حسن .
Kutoka kwake Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikaa nyuma ya msafara, akisaidia wanyonge, na kubeba wanaotembea kwa miguu, na kuwaombea. [Abu Daawuwd kwa Isnaad Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يقول إذا ركب دَابَّة للسفر
05-Mlango Wa Unachosema Unapopanda Mnyama kwa Ajili ya Safari
Alhidaaya.com [4]
قَالَ الله تَعَالَى :
وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ الْفُلْكِ وَالْأَنْعَامِ مَا تَرْكَبُونَ﴿١٢﴾
Na Akakufanyieni katika merikebu na wanyama mnaowapanda.
لِتَسْتَوُوا عَلَىٰ ظُهُورِهِ ثُمَّ تَذْكُرُوا نِعْمَةَ رَبِّكُمْ إِذَا اسْتَوَيْتُمْ عَلَيْهِ وَتَقُولُوا سُبْحَانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَـٰذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنِينَ﴿١٣﴾
Ili mlingamane sawasawa juu ya mgongo wake, kisha mkumbuke neema ya Rabb wenu mtakapolingamana sawasawa juu yao, na mseme: Utakasifu ni wa (Allaah) Ambaye Ametutiishia haya, na tusingeliweza wenyewe kumdhibiti.
وَإِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا لَمُنقَلِبُونَ﴿١٤﴾
Na hakika kwa Rabb wetu, bila shaka tutarejea. [Az-Zukhruf: 12-14]
Hadiyth – 1
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا اسْتَوَى عَلَى بَعِيرِهِ خَارِجاً إِلَى سَفَرٍ ، كَبَّرَ ثَلاثاً ، ثُمَّ قَالَ : (( سُبْحَانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنِينَ ، وَإنَّا إِلَى رَبِّنَا لَمُنْقَلبُونَ . اللّهُمَّ إنا نسألكَ في سفرنا هذا البرّ والتَّقوى ، ومنَ العملِ ما ترضى ، اللَّهُمَّ هَوِّن عَلَيْنَا سَفَرَنَا هَذَا ، وَاطْوِ عَنَّا بُعْدَهُ . اللَّهُمَّ أنْتَ الصَّاحِبُ في السَّفَرِ ، والخَلِيفَةُ في الأهْلِ . اللَّهُمَّ إنِّي أعُوذُ بِكَ مِنْ وَعْثَاءِ السَّفَرِ ، وَكَآبَةِ المَنْظَرِ ، وَسُوءِ المُنْقَلَبِ في المالِ وَالأَهْلِ وَالوَلَدِ )) وَإِذَا رَجَعَ قَالَهُنَّ وَزَادَ فِيهِنَّ : (( آيِبُونَ ، تَائِبُونَ ، عَابِدُونَ ، لِرَبِّنَا حَامِدُونَ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapokaa sawa juu ya ngamia wake akiwa anaenda safari hupiga Takbira mara tatu, kisha anasema Utukufu ni wa ambaye ametudhalilishia hiki na hatukuwa wenye kukipanda, na hakika sisi kwa Rabb wetu ni wenye kurudi. Ee Rabb wetu hakika sisi tunakuomba katika safari yetu hii wema na ucha-Mungu, na katika matendo unayoyaridhia, Ee Rabb turahisishie safari yetu hii, na tukunjie umbali wake. Ee Rabb Wewe ni rafiki safarini, na Mwangalizi katika familia, Ee Rabb mimi nataka hifadhi Kwako ya mashaka ya safari, na mandhari yenye huzuni, na ubaya wa kurejea katika mali na mke na watoto." Alipokuwa anarudi safarini aliyasema na kuongeza ndani yake: "Aayibuuna Taa'ibuna 'Aabiduuna LiRabbina Haamiduuna - Sisi ni wenye kurejea kwenye kutubia wenye kumuabudu Rabb wenye kumsifu." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن عبد الله بن سَرجِسَ رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا سَافَرَ يَتَعَوَّذُ مِنْ وَعْثَاءِ السَّفَرِ ، وَكَآبَةِ المُنْقَلَبِ ، وَالْحَوْرِ بَعْدَ الكَوْنِ ، وَدَعْوَةِ المَظْلُومِ ، وَسُوءِ المَنْظَرِ في الأَهْلِ وَالمَالِ . رواه مسلم .
'Abdillaah bin Sarjis (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisafiri huomba hifadhi kutokana na mashaka ya safari, huzuni ya kurejea, na hasara baada ya faida, na maombi ya mwenye kudhulumiwa, na ubaya wa mandhari katika mke na mali. [Muslim]
Hadiyth – 3
عن عَلِي بن ربيعة ، قَالَ : شهدت عليَّ بن أَبي طالب رضي الله عنه ، أُتِيَ بِدَابَّةٍ لِيَرْكَبَهَا ، فَلَمَّا وَضَعَ رِجْلَهُ في الرِّكَابِ ، قَالَ : بِسْمِ اللهِ ، فَلَمَّا اسْتَوَى عَلَى ظَهْرِهَا ، قَالَ : الحَمْدُ للهِ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنينَ ، وَإنَّا إِلَى رَبِّنَا لَمُنْقَلِبُونَ ، ثُمَّ قَالَ : الحمْدُ للهِ ، ثَلاثَ مَرَّاتٍ ، ثُمَّ قَالَ : اللهُ أكْبَرُ ، ثَلاثَ مَرَّاتٍ ، ثُمَّ قَالَ : سُبْحَانَكَ إنّي ظَلَمْتُ نَفْسِي فَاغْفِرْ لِي إنَّهُ لاَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلاَّ أنْتَ ، ثُمَّ ضَحِكَ ، فَقيلَ : يَا أمِيرَ المُؤمِنِينَ ، مِنْ أيِّ شَيْءٍ ضَحِكْتَ ؟ قَالَ : رَأيتُ النبيَّ صلى الله عليه وسلم فَعَلَ كَمَا فَعَلْتُ ثُمَّ ضَحِكَ ، فقُلْتُ : يَا رسول اللهِ ، مِنْ أيِّ شَيْءٍ ضَحِكْتَ ؟ قَالَ : (( إنَّ رَبَّكَ تَعَالَى يَعْجَبُ مِنْ عَبدِهِ إِذَا قَالَ : اغْفِرْ لِي ذُنُوبِي ، يَعْلَمُ أنَّهُ لاَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ غَيْرِي )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن ))، وفي بعض النسخ: (( حسن صحيح )) . وهذا لفظ أَبي داود .
'Aliy bin Rabiy’ah (رضي الله عنه) amesema: Nimemshuhudia 'Aliy bin Abiy Twaalib (رضي الله عنه) akiletewa mnyama ampande. Alipoweka mguu wake kwenye kipando alisema:
بِسْمِ اللهِ
Alipolingana juu ya mgongo wake alisema:
الحَمْدُ للهِ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنينَ ، وَإنَّا إِلَى رَبِّنَا لَمُنْقَلِبُونَ
Kisha akasema:
الحمْدُ للهِ
AlhamduliLlaah (Himdi Anastahiki Allaah) mara tatu.
Kisha akasema:
اللهُ أكْبَرُ
Allaahu Akbar (Allaah Ni Mkubwa) mara tatu.
Kisha akasema:
سُبْحَانَكَ إنّي ظَلَمْتُ نَفْسِي فَاغْفِرْ لِي إنَّهُ لاَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلاَّ أنْتَ
Subhaanak inniy dhwalamtu nafsiy Faghfirliy, innahu laa yaghfirudh-dhunuwba illa Anta.
Kutakasika ni Kwako, hakika mimi nimedhulumu nafsi yangu, basi Nighufurie, kwani hakuna mwenye kughufuria dhambi ila Wewe.
Kisha akacheka. Akaulizwa: Ee Amiri wa Waumini! Unacheka nini?
Akasema: Nilimuona Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akifanya kama nilivyofanya, kisha akacheka. Nikamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Unacheka nini? Akasema: “Hakika Rabb wako Anamridhia mja Wake anaposema: Nighufurie dhambi zangu, anajua kuwa hakuna anayeghufuria dhambi isipokuwa Yeye (Allaah).”
[Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy, amesema ni Hadiyth Hasan. Na katika baadhi ya mapokezi ni Hadiyth Hasan Swahiyh, na hii ni lafdhi ya Abuu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تكبير المسافر إِذَا صعد الثنايا وشبهها وتسبيحه إِذَا هبط الأودية ونحوها
والنهي عن المبالغة برفع الصوتِ بالتكبير ونحوه
06-Mlango Wa Msafiri Anatakiwa Kutoa Takbira Anapopanda na Kutoa Tasbihi Anaposhuka na Kubwa na Mfano Wake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن جابر رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كُنَّا إِذَا صَعِدْنَا كَبَّرْنَا ، وَإِذَا نَزَلْنَا سَبَّحْنَا . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) Amesema: Tulipokuwa tunapanda tulikuwa tunapiga Takbira na tunaposhuka tunatoa Tasbihi (Subhana Allaah). [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمرَ رضي اللهُ عنهما ، قَالَ : كَانَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم وجيُوشُهُ إِذَا عَلَوا الثَّنَايَا كَبَّرُوا ، وَإِذَا هَبَطُوا سَبَّحُوا . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na jeshi lake walikuwa wakipanda kilima wanaleta Takbira na waliposhuka wakitoa Tasbihi. [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 3
وعن ابن عمرَ رضي اللهُ عنهما ، قَالَ : كَانَ النَّبي صلى الله عليه وسلم إِذَا قَفَلَ مِنَ الحَجِّ أَوْ العُمْرَةِ ، كُلَّمَا أوْفَى عَلَى ثَنِيَّةٍ أَوْ فَدْفَدٍ كَبَّرَ ثَلاثَاً ، ثُمَّ قَالَ : (( لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ . آيِبُونَ ، تَائِبُونَ ، عَابِدُونَ ، سَاجِدُونَ ، لِرَبِّنَا حَامِدُونَ ، صَدَقَ اللهُ وَعْدَهُ ، وَنَصَرَ عَبْدَهُ ، وَهَزَمَ الأحْزَابَ وَحْدَهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
وفي رواية لمسلم : إِذَا قَفَلَ مِنَ الجيُوشِ أَو السَّرَايَا أَو الحَجِّ أَو العُمْرَةِ .
Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anaporudi Hijjah au 'Umrah alikuwa kila anapopanda kilima au mwinuko anapiga Takbira mara tatu, kisha anasema: "Hapana Mola ila Allaah tu hana mshirika. sisi ni wenye kurejea wenye kutubia wenye kumwabudu wenye kumsujudia Rabb wetu wenye kumsifu. Allaah ametimiza Ahadi Yake na kumsaidia mja Wake na akayashinda majeshi ya adui peke Yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah ya Muslim: Alipokuwa anarudi kutoka katika vita au kikosi kidogo au Hijjah au 'Umrah.
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رجلاً قَالَ : يَا رسول الله ، إنّي أُريدُ أنْ أُسَافِرَ فَأوْصِني ، قَالَ : (( عَلَيْكَ بِتَقْوَى اللهِ ، وَالتَّكْبِيرِ عَلَى كلِّ شَرَفٍ )) فَلَمَّا وَلَّى الرَّجُلُ ، قَالَ : (( اللَّهُمَّ اطْوِ لَهُ البُعْدَ ، وَهَوِّنْ عَلَيْهِ السَّفَرَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mtu mmoja alisema: 'Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi ninataka kusafiri, nakuomba uniusiye." Akasema: "Jilazimishe kumcha Allaah na kutoa Takbira juu ya kila mahali penye mwinuko." Yule mtu alipoanza safari, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimuombea: "Ee Rabb! Mfupishie umbali (wa safari yake) na mfanyie sahali safari yake." [At-Tirmidhiy, na akasrema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 5
وعن أَبي موسى الأشعريِّ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كنّا مَعَ النبيِّ صلى الله عليه وسلم في سَفَرٍ ، فَكُنَّا إِذَا أشْرَفْنَا عَلَى وَادٍ هَلَّلْنَا وَكَبَّرْنَا وَارتَفَعَتْ أصْوَاتُنَا ، فَقَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( يَا أيُّهَا النَّاسُ ، ارْبَعُوا عَلَى أنْفُسِكُمْ ، فَإنَّكُمْ لاَ تَدْعُونَ أصَمَّ وَلاَ غَائِباً ، إنَّهُ مَعَكُمْ ، إنَّهُ سَمِيعٌ قَرِيبٌ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Abu Muwsaa Al-Ash'ariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Tulikuwa pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika safari, tukawa kila tunapopanda mlima tukitoa Tahlil (Laa ILLaaha Illa Allaah) na Takbir kwa sauti kubwa. Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Enyi watu! Musizikalifishe nafsi zenu kwani nyinyi hamumuombi aliye kiziwi wala asiyekuwepo. Hakika Yeye yu pamoja nanyi, hakika Yeye Anasikia na yu karibu." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب الدعاء في السفر
07-Mlango Wa Kusuniwa Duaa Katika Safari
Alhidaaya.com [4]
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( ثلاثُ دَعَوَاتٍ مُسْتَجَابَات لاَ شَكَّ فِيهِنَّ : دَعْوَةُ المَظْلُومِ ، وَدَعْوَةُ المُسَافِرِ ، وَدَعْوَةُ الوَالِدِ عَلَى وَلَدِهِ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) . وليس في رواية أَبي داود : (( عَلَى وَلَدِهِ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Maombi matatu ni yenye kujibiwa hapana shaka yoyote. Maombi ya mwenye kudhulimiwa na maombi ya msafiri na maombi ya mzazi juu ya mtoto wake." [Abu Daawuw na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan na hakina katika riwaayah ya Abuu Daawuwd: "Juu ya mtoto wake."]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يدعو بِهِ إِذَا خاف ناساً أَوْ غيرهم
08-Mlango Wa Duaa Atakayoomba Mtu Pindi Akiwaogopa Watu au Wengineo
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي موسى الأشعريِّ رضي اللهُ عنه: أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا خَافَ قَوْماً، قَالَ : (( اللَّهُمَّ إنَّا نَجْعَلُكَ في نُحُورِهِمْ ، وَنَعُوذُ بِكَ مِنْ شُرُورِهِمْ )) رواه أَبُو داود والنسائي بإسنادٍ صحيحٍ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwaogopa watu anasema: "Ee Rabb wangu wa haki hakika sisi tunakuweka shingoni mwao na tunataka hifadhi Kwako na shari zao." [Abu Daawuwd na An-Nasaaiy kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يقول إِذَا نزل منْزلاً
09-Mlango Wa Anachosema Anayeshukia Mahali
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن خولة بنتِ حَكِيمٍ رضي الله عنها، قالت: سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يَقُولُ : (( مَنْ نَزَلَ مَنْزِلاً ثُمَّ قَالَ : أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ ، لَمْ يَضُرَّهُ شَيْءٌ حَتَّى يَرْتَحِلَ مِنْ مَنْزِلِهِ ذَلِكَ )) رواه مسلم .
Amesema Khawlah bint Haakim (Radhwiya Allaahu 'anha) kuwa: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Yeyote anayeshuka mashukio yoyote kisha akasema: 'A'udhu Bikalimati Llaahit Taammaati min sharri maa Khalaq - Ninajikinga kwa maneno ya Allaah yaliyokamilika kutokana na shari ya kila alichokiumba', hatodhuriwa na kitu chochote mpaka aondoke sehemu hiyo." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا سَافَرَ فَأقْبَلَ اللَّيْلُ، قَالَ: (( يَا أرْضُ، رَبِّي وَرَبُّكِ اللهُ ، أعُوذُ بِاللهِ مِنْ شَرِّكِ وَشَرِّ مَا فِيكِ ، وَشَرِّ مَا خُلِقَ فِيكِ ، وَشَرِّ مَا يَدِبُّ عَلَيْكِ ، وَأعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ أسَدٍ وَأسْوَدٍ ، وَمِنَ الحَيَّةِ وَالعَقْرَبِ ، وَمِنْ سَاكِنِ البَلَدِ ، وَمِنْ وَالِدٍ وَمَا وَلَدَ )) رواه أَبُو داود .
Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anaposafiri utakapoingia usiku anasema: "Ee ardhi, Rabb wangu na Rabb wako ni Allaah najilinda kwa Allaah dhidi ya shari yako, na shari iliyo ndani yako, na shari ya vilivyoumbwa ndani yako, na dhidi ya shari vinavyotambaa juu yako, na ninajilinda kwa Allaah dhidi ya shari ya simba, na weusi, (Al Aswad), na dhidi ya nyoka na nge, na dhidi ya wakazi wa mji, na dhidi ya mzazi na alichokizaa." [Abu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب تعجيل المسافرالرجوع إِلَى أهله إِذَا قضى حاجته
10-Mlango Wa Kupendekezwa Kurudi Haraka Msafiri kwa Familia Yake Anapomaliza Haja Yake
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( السَّفَرُ قِطْعَةٌ مِنَ العَذَابِ، يَمْنَعُ أحَدَكُمْ طَعَامَهُ وَشَرابَهُ وَنَوْمَهُ، فَإذَا قَضَى أحَدُكُمْ نَهْمَتَهُ مِنْ سَفَرِهِ ، فَلْيُعَجِّلْ إِلَى أهْلِهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Safari ni kipande cha adhabu, inamzuia mmoja wenu chakula chake, kinywaji chake na usingizi wake. Hivyo, mmoja wenu atakapomaliza haja yake katika safari yake, na arudi haraka kwa watu wake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب القدوم عَلَى أهله نهاراً وكراهته في الليل لغير حاجة
11-Mlango Wa Kupendekezwa Kurudi kwa Familia Yake Mchana na Karaha Kurudi Usiku Bila ya Haja Yoyote
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن جابر رضي اللهُ عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا أطال أحَدُكُمُ الغَيْبَةَ فَلاَ يَطْرُقَنَّ أهْلَهُ لَيْلاً )) .
وفي روايةٍ : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم نَهَى أنْ يَطْرُقَ الرَّجُلُ أهْلَهُ لَيْلاً . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mmoja wenu anaporefusha kupotea kwake (safarini) Asigongee familia yake usiku."
Na katika riwaayah nyingine ni kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza mtu kurudi katika familia yake usiku." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن أنسٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم لا يَطْرُقُ أهْلَهُ لَيْلاً ، وَكَانَ يَأتِيهمْ غُدْوَةً أَوْ عَشِيَّةً . متفقٌ عَلَيْهِ .
Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa hagongei familia yake usiku, alikuwa anawajia asubuhi au jioni (mwisho wa mchana)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يقول إِذَا رجع وإذا رأى بلدته
12-Mlango Wa Anachosema Anaporudi Kutoka Safari na Kuona Mji Wake
Alhidaaya.com [4]
وعن أنس رضي اللهُ عنه ، قَالَ : أقْبَلْنَا مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم حَتَّى إِذَا كُنَّا بِظَهْرِ الْمَدِينَةِ ، قَالَ : (( آيِبُونَ ، تَائِبُونَ ، عَابِدُونَ ، لِرَبِّنَا حَامِدُونَ )) فَلَمْ يَزَلْ يَقُولُ ذَلِكَ حَتَّى قَدِمْنَا المَدِينَةَ . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa: Tulikuwa tunarudi pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mpaka tukafika mahali ambapo Madiynah ilikuwa inaonekana, hapo alisema: "Sisi ni wenye kurejea wenye kutubia wenye kumwabudu Rabb wetu wenye kumsifu." Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliendelea kukariri hayo mpaka tukawasili Madiynah. [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب ابتداء القادم بالمسجد الذي في جواره وصلاته فيه ركعتين
13-Mlango Wa Sunnah ya Mwenye Kurejea Kutoka Safari Kuanzia Msikiti Ulio Karibu Yake na Kuswali Rakaa Mbili Ndani Yake
Alhidaaya.com [4]
عن كعب بن مالِك رضي اللهُ عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا قَدِمَ مِنْ سَفَرٍ ، بَدَأ بِالْمَسْجِدِ فَرَكَعَ فِيهِ رَكْعَتَيْنِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ka'b bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akianza Msikitini anaporudi kutoka safari na kuswali rakaa mbili ndani yake. [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم سفر المرأة وحدها
14-Mlango Wa Kuharamishwa Mwanamke Kusafiri Peke Yake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه، قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: (( لاَ يَحِلُّ لامْرَأَةٍ تُؤْمِنُ بِاللهِ وَالْيَومِ الآخِرِ تُسَافِرُ مَسِيرَةَ يَوْمٍ وَلَيْلَةٍ إِلاَّ مَعَ ذِي مَحْرَمٍ عَلَيْهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Si halali kwa mwanamke anayemuamini Allaah na Siku ya Mwisho kusafiri mwendo wa mchana kutwa na usiku kucha ila awe pamoja na mahramu yake." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن ابن عباس رضي الله عنهما : أنَّهُ سَمِعَ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( لاَ يَخْلُوَنَّ رَجُلٌ بِامْرَأَةٍ إِلاَّ وَمَعَهَا ذُو مَحْرَمٍ ، وَلاَ تُسَافِرُ المَرْأةُ إِلاَّ مَعَ ذِي مَحْرَمٍ )) فَقَالَ لَهُ رَجُلٌ : يَا رسولَ الله ، إنَّ امْرَأتِي خَرَجَتْ حَاجَّةً ، وَإنِّي اكْتُتِبْتُ في غَزْوَةِ كَذَا وَكَذَا ؟ قَالَ : (( انْطَلِقْ فَحُجَّ مَعَ امْرَأَتِكَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba amemsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwanamme asikae faragha na mwanamke peke yao isipokuwa kuwe pamoja naye maharimu wake wala asisafiri mwanamke ila pamoja na maharimu wake. Yule mtu akamwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mke wangu ameazimia kuhiji nami nimejiandikisha kushiriki katika vita kadhaa na kadhaa?" Akasema: "Nenda kahiji na mkeo." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/280
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10321&title=07-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Kitabu%20Cha%20Nidhamu%20Za%20Safari%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A2%D8%AF%D8%A7%D8%A8%20%D8%A7%D9%84%D8%B3%D9%91%D9%8E%D9%81%D8%B1
[4] http://www.alhidaaya.com/
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11073&title=01-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kusafiri%20Siku%20ya%20Alkhaamis%20na%20Kupendeza%20Kuondoka%20Mwanzo%20wa%20Mchana
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11074&title=02-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kusafiri%20kwa%20Kikundi%20Chini%20ya%20Kiongozi%20na%20Kumtii
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11075&title=03-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Adabu%20za%20Safari%20na%20Kuteremka%20na%20Kupumzika%20Usiku%20Kuwahurumia%20Wanyama%20na%20Kuchunga%20Maslahi%20Yao%20na%20Haki%20Zao%20na%20Kufaa%20Kulala%20Juu%20ya%20Mnyama%20Ikiwa%20Anaweza%20Jambo%20Hilo
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11078&title=04-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kumsaidia%20Rafiki
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11079&title=05-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Unachosema%20Unapopanda%20Mnyama%20kwa%20Ajili%20ya%20Safari
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11080&title=06-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Msafiri%20Anatakiwa%20Kutoa%20Takbira%20Anapopanda%20na%20Kutoa%20Tasbihi%20Anaposhuka%20na%20Kubwa%20na%20Mfano%20Wake
[11] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11081&title=07-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kusuniwa%20Duaa%20Katika%20Safari
[12] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11082&title=08-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Duaa%20Atakayoomba%20Mtu%20Pindi%20Akiwaogopa%20Watu%20au%20Wengineo
[13] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11083&title=09-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Anachosema%20Anayeshukia%20Mahali
[14] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11084&title=10-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendekezwa%20Kurudi%20Haraka%20Msafiri%20kwa%20Familia%20Yake%20Anapomaliza%20Haja%20Yake
[15] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11085&title=11-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendekezwa%20Kurudi%20kwa%20Familia%20Yake%20Mchana%20na%20Karaha%20Kurudi%20Usiku%20Bila%20ya%20Haja%20Yoyote
[16] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11086&title=12-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Anachosema%20Anaporudi%20Kutoka%20Safari%20na%20Kuona%20Mji%20Wake
[17] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11087&title=13-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Sunnah%20ya%20Mwenye%20Kurejea%20Kutoka%20Safari%20Kuanzia%20Msikiti%20Ulio%20Karibu%20Yake%20na%20Kuswali%20Rakaa%20Mbili%20Ndani%20Yake
[18] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11088&title=14-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuharamishwa%20Mwanamke%20Kusafiri%20Peke%20Yake