Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فَضلِ الذِّكْرِ وَالحَثِّ عليه
01-Mlango Wa Fadhila za Dhikri na Kuhimizwa Juu Yake
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَلَذِكْرُ اللَّـهِ أَكْبَرُ ۗ ﴿٤٥﴾
Na bila shaka kumdhukuru Allaah ndilo kubwa zaidi. [Al-'Ankabuwt: 45]
فَاذْكُرُونِي أَذْكُرْكُمْ ﴿١٥٢﴾
Basi nidhukuruni na Mimi Nitakukumbukeni. [Al-Baqarah: 152]
وَاذْكُر رَّبَّكَ فِي نَفْسِكَ تَضَرُّعًا وَخِيفَةً وَدُونَ الْجَهْرِ مِنَ الْقَوْلِ بِالْغُدُوِّ وَالْآصَالِ وَلَا تَكُن مِّنَ الْغَافِلِينَ ﴿٢٠٥﴾
Na mdhukuru Rabb wako katika nafsi yako kwa unyenyekevu na kwa khofu na kwa ulimi bila sauti kubwa asubuhi na jioni, na wala usiwe miongoni mwa walioghafilika. [Al-A'raaf: 205]
وَاذْكُرُوا اللَّـهَ كَثِيرًا لَّعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴿١٠﴾
Na mdhukuruni Allaah kwa wingi ili mpate kufaulu. [Al-Jumua'ah]
وَالذَّاكِرِينَ اللَّـهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾
Na wanaomdhukuru Allaah kwa wingi wanaume na wanawake, Allaah Amewaandalia Maghfirah na ujira adhimu. [Al-Ahzaab: 35]
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا اللَّـهَ ذِكْرًا كَثِيرًا ﴿٤١﴾
Enyi walioamini! Mdhukuruni Allaah kwa wingi wa kumdhukuru.
وَسَبِّحُوهُ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٤٢﴾
Na Msabbihini asubuhi na jioni. [Al-Ahzaab: 41-42]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( كَلِمَتَانِ خَفِيفَتَانِ عَلَى اللِّسَانِ ، ثَقِيلَتَانِ فِي المِيزَانِ ، حَبِيبَتَانِ إِلَى الرَّحْمانِ : سُبْحَانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ العظيمِ )) . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Maneno mawili ni mepesi ulimini, mazito katika mizani na yanapendwa na Ar-Rahmaan (Mwingi wa Rehma): Subhaana LLaahi wa Bihamdihi Subhaana LLaahil 'Adhiym (Ametakasika Allaah na sifa zote njema anastahiki, Ametakasika Allaah Mtukufu)." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لأَنْ أَقُولَ : سُبْحَانَ اللهِ ؛ وَالحَمْدُ للهِ ؛ وَلاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ ، وَاللهُ أكْبَرُ ، أَحَبُّ إلَيَّ مِمَّا طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kwa mimi kusema: Subhaana Allaah, wal HamduliLLaah, wa Laa Ilaaha Illa Allaah (Ametakasika Allaah, na Sifa zote njema anastahili Allaah na hapana Mola muabudiwa kwa haki ila Allaah na Allaah ni Mkuu) Inanipendeza zaidi kuliko vitu vyote vilivyo chomozewa na jua." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( مَنْ قَالَ لا إلهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَريكَ لَهُ ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ ؛ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ، في يَوْمٍ مِئَةَ مَرَّةٍ كَانَتْ لَهُ عَدْلَ عَشْرِ رِقَابٍ وكُتِبَتْ لَهُ مِئَةُ حَسَنَةٍ ، وَمُحِيَتْ عَنْهُ مِئَةُ سَيِّئَةٍ ، وَكَانَتْ لَهُ حِرْزاً مِنَ الشَّيْطَانِ يَوْمَهُ ذَلِكَ حَتَّى يُمْسِي ، وَلَمْ يَأتِ أَحَدٌ بِأَفْضَلَ مِمَّا جَاءَ بِهِ إِلاَّ رَجُلٌ عَمِلَ أكْثَرَ مِنْهُ )) . وقال : (( مَنْ قَالَ سُبْحَانَ الله وَبِحَمْدِهِ ، في يَوْمٍ مِئَةَ مَرَّةٍ ، حُطَّتْ خَطَايَاهُ ، وَإنْ كَانَتْ مِثْلَ زَبَدِ البَحْرِ )) . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kusema Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa Shariyka lahu, lahul Mulku walahul Hamdu wa Huwa ;alaa kulli shay'in Qadiyr (Hapana Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah, Aliye peke Yake wala hana mshirika, Yeye Ndiye Mwenye Ufalme na sifa zote njema anastahiki Yeye tu Naye ni Muweza wa kufanya kila kitu), kila siku mara mia moja. Zitakuwa kwake sawa na kuacha huru watumwa kumi, na ataandikiwa mema mia moja, na atafutiwa maovu mia moja. Na itakuwa kinga kwake kumkinga na shetani, siku yake hiyo mpaka jioni. Hakuna yeyote atakayelifanya lililo bora zaidi yake, isipokuwa atakayefanya zaidi ya alivyofanya." Na akasema: "Atakayesema: "Subhaana Allaahi wa Bihamdihi (Ametakasika Allaah na sifa zote njema ni Zake), mara mia moja kwa siku, yatafutwa makosa yake, hata kama yalikuwa kama povu la bahari." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 4
وعن أَبي أيوب الأنصاريِّ رضي اللهُ عنه ، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ قَالَ لا إلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ ؛ وَلَهُ الحَمْدُ ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ، عَشْرَ مَرَّاتٍ . كَانَ كَمَنْ أعْتَقَ أرْبَعَةَ أنْفُسٍ منْ وَلَدِ إسْمَاعِيلَ )) . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Ayyuwb Al-Answaariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Atakayesema Laa ilaaha illa LLaahu Wahdahu laa Shariyka lahu, lahul Mulku walahul Hamdu wa Huwa 'alaa kulli shay'in Qadiyr (Hapana Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah, Aliye Peke Yake wala hana mshirika, Yeye Ndiye Mwenye Ufalme na sifa zote njema anastahiki Yeye tu naye ni Muweza wa kufanya kila kitu), mara kumi atakuwa sawa na mwenye kuacha huru nafsi (watumwa) nne katika watoto wa Ismaa'iyl." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أَبي ذَرٍّ رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( ألاَ أُخْبِرُكَ بِأَحَبِّ الكَلاَمِ إِلَى اللهِ ؟ إنَّ أَحَبَّ الكَلاَمِ إِلَى اللهِ : سُبْحَانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ )) . رواه مسلم .
Amesema Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu): Aliniambia mimi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi w sallam): "Je, nikueleze maneno yanayo mpendeza zaidi Allaah? Hakika maneno yanayo mpendeza Allaah ni Subhaana Allaahi wa Bihamdihi." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أَبي مالك الأشعري رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( الطُّهُورُ شَطْرُ الإيمانِ ، وَالحَمْدُ للهِ تَمْلأُ المِيزَانَ ، وَسُبْحَانَ اللهِ وَالحَمْدُ للهِ تَمْلآنِ – أَوْ تَمْلأُ – مَا بَيْنَ السَّمَاوَاتِ وَالأرْضِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Maalik Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kujitwahirisha ni nusu ya Imaan, na AlhamdulliLLaah (Kila sifa njema anastahiki Allaah) linajaza mizani, na Subhaana Allaah (Allaah ameepukana na kila ya upungufu / Ametakasika Allaah) na AlhamdulliLLaah yanajaza baina ya mbingu na ardhi." [Muslim]
Hadiyth – 7
وعن سعد بن أَبي وقاصٍ رضي اللهُ عنه قَالَ: جَاءَ أعْرَابيٌّ إِلَى رَسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : عَلِّمْنِي كَلاَماً أقُولُهُ . قَالَ : (( قُلْ لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَريكَ لَهُ ، اللهُ أكْبَرُ كَبِيراً ، وَالحَمْدُ للهِ كَثيراً ، وَسُبْحَانَ اللهِ رَبِّ العَالِمينَ ، وَلاَ حَولَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِاللهِ العَزِيزِ الحَكِيمِ )) قَالَ : فهؤُلاءِ لِرَبِّي ، فَمَا لِي ؟ قَالَ : (( قُلْ : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي ، وَارْحَمْنِي وَاهْدِنِي ، وَارْزُقْنِي )) . رواه مسلم .
Amesema Sa'ad bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu): Alikuja Bedui kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akaomba: "Nifundishe maneno ambayo nitakuwa nayasema." Akasema: Sema "Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa Sharika lahu, Allaahu Akbar Kabiyra wal Hamdu LiLLaahi Kathiyran wa Subhaana Allaahi Rabbil 'Aalamiyn walaa Hawla walaa Quwwata illa BiLLaahil 'azizil Hakiym" (Hapana Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah, Peke Yake wala hana mshirika. Allaah ni Mkuu sana na Sifa njema zote na nyingi ni Zake na Ametakasika Allaah Rabb wa walimwengu wote. Na hapana hila wala nguvu isipokuwa kuwezeshwa na Allaah, Mwenye Nguvu na Mwenye Hekima)." Akasema: "Haya ni maneno kwa Rabb wangu. Yangu ni yepi?" Akasema: "Sema: Allaahumma Ghfirliy warhamniy wahdiniy warzuqniy (Ee Mola wangu wa haki! Nighufurie (madhambi yangu), na Unirehemu, na Uniongoze na Uniruzuku)." [Muslim]
Hadiyth – 8
وعن ثَوبانَ رضي اللهُ عنه قَالَ : كَانَ رَسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم إِذَا انْصَرَفَ مِنْ صَلاَتِهِ اسْتَغْفَرَ ثَلاثَاً ، وَقَالَ : (( اللَّهُمَّ أنْتَ السَّلاَمُ ، وَمِنْكَ السَّلاَمُ ، تَبَارَكْتَ يَاذَا الجَلاَلِ وَالإكْرَامِ )) قِيلَ لِلأوْزَاعِيِّ - وَهُوَ أحَدُ رواة الحديث - : كَيْفَ الاسْتِغْفَارُ ؟ قَالَ : يقول : أسْتَغْفِرُ الله ، أسْتَغْفِرُ الله . رواه مسلم .
Thawbaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa anapoandoka toka kwenye Swalaah akileta Istighfar (AstaghfiruLLaah - Nisamehe Ee Allaah) mara tatu na baadae akisema: "Allaahumma Antas Salaam wa Minkas Salaam Tabaarakta Yaa Dhal Jalaal wal Ikraam (Ee Mola wangu wa Haki! Wewe Ndiwe Amani na Kwako kunatoka amani, Umetukuka ee Mwenye Enzi na Mwenye Kustahiki Kuheshimika)." Aliulizwa Al-Awzaa'iy, naye ni mmoja wa wapokezi wa Hadiyth: "Hii Istighfar inaletwa vipi?" Akasema: "Sema: AstaghfiruLLaah, AstaghfiruLLaah." [Muslim]
Hadiyth – 9
وعن المغيرة بن شعبة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا فَرَغَ مِنَ الصَّلاَةِ وَسَلَّمَ ، قَالَ : (( لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ، اللَّهُمَّ لاَ مَانِعَ لِمَا أَعْطَيْتَ ، وَلاَ مُعْطِيَ لِمَا مَنَعْتَ ، وَلاَ يَنْفَعُ ذَا الجَدِّ مِنْكَ الجَدُّ )) . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake Mughiyrah bin Shu'bah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa alipomaliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Swalaah yake na kutoa salamu akisema: "Laa ilaaha illaAllaah Wahdahu laa shariyka lahu, lahul Mulku walahul Hamdu wa Huwa 'alaa kuli shay'in Qadiyr. Allaahumma Laa Maani'a limaa A'twayta walaa Mu'twiya limaa Mana'ta walaa yanfa'u dhal jaddi Minkal Jadd (Hapana Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah. Yu Peke Yake wala hana mshirika, Yeye Ndiye Mwenye Ufalme na sifa zote njema anastahiki Yeye tu Naye ni Muweza wa kufanya kila kitu. Ee Rabb wangu! Hapana wa kuzuia Ulichotoa wala hapana wa kutoa Ulichozuia, wala tajiri hautamfaa utajiri wake mbele Yako)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 10
وعن عبدِ الله بن الزُّبَيْرِ رضي الله تَعَالَى عنهما أنَّه كَانَ يَقُولُ دُبُرَ كُلِّ صَلاَةٍ ، حِيْنَ يُسَلِّمُ : (( لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَريكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ . لاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِاللهِ ، لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ ، وَلاَ نَعْبُدُ إِلاَّ إيَّاهُ ، لَهُ النِّعْمَةُ وَلَهُ الفَضْلُ وَلَهُ الثَّنَاءُ الحَسَنُ ، لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ وَلَوْ كَرِهَ الكَافِرُونَ )) قَالَ ابْنُ الزُّبَيْرِ : وَكَانَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم ، يُهَلِّلُ بِهِنَّ دُبُرَ كُلِّ صَلاَةٍ . رواه مسلم .
Alikuwa 'Abdillaah bin Az-Zubayr (Radhwiya Allaahu 'anhu) akisema baada ya kila Swalaah ya faradhi, pindi anapotoa salamu dua ifuatayo: "Laa ilaaha illaAllaahu Wahdahu laa Shariyka lahu, lahul Mulku walahul Hamdu wa Huwa 'alaa kulli shay'in Qadiyr. Laa hawla wala Quwwata illaa BiLLaah laa ilaaha illaAllaahu, walaa na'budu illaa Iyyaahu lahun Ni'matu, walahul Fadhlu, walahuth Thana'ul hasan. Laa ilaaha illaa Allaahu Mukhliswiyna lahud Diyna walaw karihal Kaafiruwn. (Hapana Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah. Yu Peke Yake wala hana mshirika, Yeye Ndiye Mwenye Ufalme na sifa zote njema anastahiki Yeye tu naye ni Muweza wa kufanya kila kitu. Na hapana hila wala nguvu isipokuwa Allaah wala hatumuabudu ila Yeye. Yeye ndiye Mwenye fadhila na Ndiye Mwenye kusifiwa kwema. Hapana Mola wa kuabudiwa isipokuwa Allaah, tunaitakasa Dini Yake japokuwa watachukia makafiri)." Amesema Ibn Az-Zubayr: "Na alikuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akimpwekesha Allaah kwa kuleta (dhikri hii) baada ya kila Swalaah ya faradhi." [Muslim]
Hadiyth – 11
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ فُقَراءَ المُهَاجِرِينَ أَتَوْا رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فقالوا : ذَهَبَ أهْلُ الدُّثورِ بِالدَّرَجَاتِ العُلَى ، وَالنَّعِيمِ المُقِيمِ ، يُصَلُّونَ كَمَا نُصَلِّي ، وَيَصُومُونَ كَمَا نَصُومُ، وَلَهُمْ فَضْلٌ مِنْ أمْوَالٍ ، يَحُجُّونَ ، وَيَعْتَمِرُونَ ، وَيُجَاهِدُونَ ، وَيَتَصَدَّقُونَ . فَقَالَ : (( ألاَ أُعَلِّمُكُمْ شَيْئاً تُدْرِكُونَ بِهِ مَنْ سَبَقَكُمْ ، وَتَسْبَقُونَ بِهِ مَنْ بَعْدَكُمْ ، وَلاَ يَكُون أَحَدٌ أفْضَل مِنْكُمْ إِلاَّ منْ صَنَعَ مِثْلَ مَا صَنَعْتُمْ ؟ )) قالوا : بَلَى يَا رسول الله ، قَالَ : (( تُسَبِّحُونَ ، وَتَحْمَدُونَ ، وَتُكَبِّرُونَ ، خَلْفَ كُلِّ صَلاَةٍ ثَلاثاً وَثَلاثِينَ )) قَالَ أَبُو صالح الراوي عن أَبي هريرة ، لَمَّا سُئِلَ عَنْ كَيْفِيَّةِ ذِكْرِهِنَّ قَالَ : يقول : سُبْحَان اللهِ ، وَالحَمْدُ للهِ واللهُ أكْبَرُ ، حَتَّى يَكُونَ مِنهُنَّ كُلُّهُنَّ ثَلاثاً وَثَلاثِينَ . متفقٌ عَلَيْهِ .
وزاد مسلمٌ في روايته : فَرَجَعَ فُقَراءُ المُهَاجِرينَ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، فقالوا : سَمِعَ إخْوَانُنَا أهْلُ الأمْوَالِ بِمَا فَعَلْنَا فَفَعَلُوا مِثْلَهُ ؟ فَقَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( ذَلِكَ فَضْلُ الله يُؤتِيهِ مَنْ يَشَاءُ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mafukara wa Muhaajiriyn walikuwa kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia: "Wenye mali wameondoka na daraja za juu na neema za daima: Wao wanaswali kama tunavyoswali na wafunga kama tunavyofunga. Na wana fadhila ya mali: Wanakwenda Hijjah, na kutekeleza Umrah, na wanapigana Jihaad na wantoa Swadaqah." Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je, si wafundishi nyinyi kitu ambacho kwayo mutawafikia waliowapiteni na mutashindana na wale watakaokuja baada yenu na hakuna atakaye kuwa bora kuliko nyinyi isipokuwa yule atakayefanya kama munavyofanya?" Wakasema: "Ndio (tuambie) ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Msabihini Allaah(kwa kusema Subhaana Allaah), muhimidini (kwa kusema AlhamduliLLaah) na leteni takbiri baada ya kila Swalaah (ya Faradhi) mara thelethini na tatu (33)." Akasema Abu Swalih mpokezi kutoka kwa Abu Huraiyrah: "Aliulizwa jinsi ya kutekeleza dhikri hii." Akasema: "Wanasema: Subhaana Allaah wal HamduliLLaah wa Allaahu Akbar, mpaka zifike zote hizo mara thelathini na tatu." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na Abu Daawuwd]
Na ameongeza Muslim katika riwaayah yake: "Baada ya muda walirudi tena mafakiri wa Muhaajiriyn kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia: Ndugu zetu wenye mali wamesikia kwa yale tunayofanya na wakawa wanafanya mfano wetu?" Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hiyo ni fadhila kutoka kwa Allaah naye anampatia amtakaye."
Hadiyth – 12
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ سَبَّحَ الله في دُبُرِ كُلِّ صَلاَةٍ ثَلاثاً وَثَلاثِينَ ، وحَمِدَ اللهَ ثَلاثاً وَثَلاَثِينَ ، وَكَبَّرَ الله ثَلاثاً وَثَلاَثِينَ ، وقال تَمَامَ المِئَةِ : لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ وَحدَهُ لا شَريكَ لَهُ ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ، غُفِرَتْ خَطَايَاهُ وَإنْ كَانَتْ مِثْلَ زَبَدِ البَحْرِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote mwenye kumsabih Allaah baada ya kila Swalaah ya faradhi mara thelathini na tatu na akamuhimidi Allaah mara thelathini na tatu na akaleta takbira mara thelathini na tatu na akasema kukamilisha mara mia: Laa ilaaha illaAllaahu Wahdahu laa Shariyka Lahu, Lahul Mulku walahul Hamdu wa Huwa 'alaa kuli shay'in Qadiyr, atasamehewa makosa yake japokuwa yatakuwa kama povu la bahari." [Muslim]
Hadiyth – 13
وعن كعب بن عُجْرَةَ رضي اللهُ عنه ، عن رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مُعَقِّباتٌ لاَ يَخِيبُ قَائِلُهُنَّ – أَوْ فَاعِلُهُنَّ – دُبُرَ كُلِّ صَلاَةٍ مَكْتُوبَةٍ: ثَلاثٌ وَثَلاثونَ تَسْبِيحَةً. وَثَلاثٌ وثَلاَثونَ تَحْمِيدَةً ، وَأرْبَعٌ وَثَلاَثونَ تَكْبِيرَةً )) . رواه مسلم.
Imepokewa kutoka kwake Ka'b bin 'Ujrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Zipo Dhikri baada ya kila Swalaah ya faradhi, mwenye kuzisoma hatavunjika moyo - au mwenye kuzifanya. Hiyo ni kuleta tasbihi mara thelathini na tatu, tahmidi mara thelathini na tatu na takbira mara thelathini na nne." [Muslim]
Hadiyth – 14
وعن سعد بن أَبي وقاص رضي اللهُ عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم كَانَ يَتَعَوَّذُ دُبُرَ الصَّلَواتِ بِهؤُلاءِ الكَلِمَاتِ : (( اللَّهُمَّ إنِّي أَعوذُ بِكَ مِنَ الجُبْنِ وَالبُخْلِ ، وَأعُوذُ بِكَ مِنْ أنْ أُرَدَّ إِلَى أَرْذَلِ العُمُرِ ، وَأعُوذُ بِكَ مِنْ فِتْنَةِ الدُّنْيَا ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ فِتْنَةِ القَبْرِ )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwake Sa'd bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akijikinga baada ya kila Swalaah ya faradhi kwa maneno haya: "Allaahumma inni a'uwdhu bika minal jubni wal bukhli wa a'iuwdhu bika min an uradda ila ardhalil 'umri wa a'uwdhu bika min fitnatid dunyaa wa a'uwdhu bika min fitnatil qabri (Ee Rabb wangu! Hakika mimi najilinda Kwako na uzembe na ubakhili, na najilinda Kwako na kurudishwa kwenye umri wa unyonge kabisa, na najilinda Kwako na fitna ya dunia na najilinda Kwako na fitna ya kaburini)." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 15
وعن معاذ رضي اللهُ عنه : أن رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، أخذ بيده ، وقال : (( يَا مُعَاذُ ، وَاللهِ إنِّي لأُحِبُّكَ )) فَقَالَ : (( أُوصِيكَ يَا مُعَاذُ لاَ تَدَعَنَّ في دُبُرِ كُلِّ صَلاَة تَقُولُ : اللَّهُمَّ أَعِنِّي عَلَى ذِكْرِكَ ، وَشُكْرِكَ، وَحُسْنِ عِبَادَتِكَ )) . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Mu'aadh bin Jabal (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimshika mkono wake na kumwambia: "Ee Mu'aadh! Naapa kwa Allaah kuwa nakupenda." Na akasema: "Nakuusia ee Mu'aadh usiache kusema baada ya kila Swalaah ya faradhi (maneno yafuatayo): "Allaahumma a'iinniy 'alaa Dhikrika wa Shukrika wa Husni 'Ibaadatika (Ee Rabb wangu! Nisaidie juu ya utajo wako na Kushukuriwa Kwako na uzuri wa ibada Yako)." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 16
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا تَشَهَّدَ أَحَدُكُمْ فَلْيَسْتَعِذْ بِاللهِ مِنْ أرْبَعٍ ، يقول : اللَّهُمَّ إنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابِ جَهَنَّمَ ، وَمِنْ عَذَابِ القَبْرِ ، وَمِنْ فِتْنَةِ المَحْيَا وَالْمَمَاتِ ، وَمِنْ شَرِّ فِتْنَةِ المَسِيحِ الدَّجَّالِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapopiga shahada (katika Tahiyyatu) mmoja wenu basi atake ulinzi wa Allaah kwa mambo manne kwa kusema: "Allaahumma Inni A'uwdhu Bika min 'adhaabil qabri wa min fitnatil mahyaa wal mamaat wa min sharri fitnatil Masiyhid Dajjaal (Ee Rabb wangu! Hakika mimi najilinda Kwako na adhabu ya ahanam, na adhabu ya kaburini, na fitna ya uhai na mauti na shari ya fitna ya Masiyhi Dajjaal)." [Muslim]
Hadiyth – 17
وعن عليٍّ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم ، إِذَا قَامَ إِلَى الصَّلاَةِ يَكُونُ مِنْ آخِرِ مَا يَقُولُ بَيْنَ التَّشَهُّدِ وَالتَّسْلِيمِ : (( اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي مَا قَدَّمْتُ وَمَا أخَّرْتُ ، وَمَا أسْرَرْتُ وَمَا أعْلَنْتُ ، وَمَا أسْرَفْتُ ، وَمَا أنْتَ أعْلَمُ بِهِ مِنِّي ، أنْتَ الْمُقَدِّمُ ، وَأنْتَ المُؤَخِّرُ ، لا إلهَ إِلاَّ أنْتَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa anaposimama kwa ajili ya Swalaah maneno ya mwisho anayo yasema baina ya Tashahhud na kutoa salamu ni: "Allaahumma Ghfirli maa qaddamtu wa maa Akhkhartu wa maa asrartu wa maa a'lantu wa maa asraftu wa maa anta a'lamu bihi minniy antal muqaddimu wa antal mu'akhkhiru laa ilaaha illa Anta (Ee Rabb wangu! Nisamehe mimi madhambi niliyotanguliza na yanayokuja, na niliyofanya kwa siri na niliyodhihirisha, niliyoyafanyia isirafu, na yale madhambi, Unayoyajua zaidi kuliko mimi mwenyewe. Wewe Mwenye kutanguliza na Wewe Ndiye Mwenye kuchelewesha. Hapana Mola wa kuabudiwa ila Wewe)." [Muslim]
Hadiyth – 18
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم يُكْثِرُ أنْ يَقُولَ في رُكُوعِهِ وَسُجُودِهِ : (( سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وبِحَمْدِكَ ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي )) متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akikithirisha kusema katika kurukuu na kusujudu: "Subhaanakal Lahumma Rabbaana wa Bihamdika Allahumma Ghfirli (Utakaso ni Wako ee Allaah na sifa zote njema Unastahiki Wewe, ee Rabb Wangu nisamehe)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nisaaiy]
Hadiyth – 19
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ يقولُ في رُكُوعِهِ وَسُجُودِهِ : (( سبُّوحٌ قُدُّوسٌ رَبُّ المَلاَئِكَةِ وَالرُّوحِ )) . رواه مسلم .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa katika Rukuu' na sijdah yake akisema: "Subbuwhun Qudduws Rabbul Malaaikati war Ruuh (Ametakasifu mno Mtukufu mno Rabb wa Malaaikah na roho)." [Muslim]
Hadiyth – 20
وعن ابن عباس رضي الله عنهما : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( فَأمَّا الرُّكُوعُ فَعَظِّمُوا فِيهِ الرَّبَّ عزوجل ، وَأمَّا السُّجُودُ فَاجْتَهِدُوا في الدُّعَاءِ ، فَقَمِنٌ أنْ يُسْتَجَابَ لَكُمْ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ama katika rukuu Mtukuzeni Rabb ndani yake na katika kusujudu fanyeni juhudi katika kuomba duaa. Kwani ni hakika kujibiwa duaa zenu." [Muslim]
Hadiyth – 21
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أقْرَبُ مَا يَكُونُ العَبْدُ مِنْ رَبِّهِ وَهُوَ سَاجِدٌ ، فَأَكْثِرُوا الدُّعَاءَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mja anakuwa karibu na Rabb wake akiwa katika sijdah, hivyo jitahidini na ongezeni duaa (katika hali hiyo ya sijdah)." [Muslim]
Hadiyth – 22
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ يَقُولُ في سجودِهِ : (( اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي ذَنْبِي كُلَّهُ : دِقَّهُ وَجِلَّهُ ، وَأَوَّلَهُ وَآخِرَهُ ، وَعَلاَنِيَتَهُ وَسِرَّهُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisema yafuatayo anaposujudu: "Allaahummaghfirli dhambi kullahu diqqahu wa jillahu, wa awwalahu wa aakhirahu, wa 'alaaniyatahu wa sirrahu (Ee Rabb wangu! Nisamehe dhambi zangu zote, ndogo na kubwa, za mwanzo na za mwisho, na za dhahiri na za siri)." [Muslim]
Hadiyth – 23
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها، قالت : افْتَقَدْتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، ذَاتَ لَيْلَةٍ ، فَتَحَسَّسْتُ ، فإذا هُوَ راكِعٌ – أَوْ سَاجِدٌ – يقولُ : (( سُبْحَانَكَ وَبِحَمْدِكَ ، لاَ إلهَ إِلاَّ أنت )) وفي روايةٍ : فَوَقَعَتْ يَدِي عَلَى بَطْنِ قَدَمَيْهِ ، وَهُوَ في المَسْجِدِ وَهُمَا مَنْصُوبَتَانِ ، وَهُوَ يَقُولُ : (( اللَّهُمَّ إنِّي أَعُوذُ بِرِضَاكَ مِنْ سَخَطِكَ ، وَبِمعَافَاتِكَ مِنْ عُقُوبَتِكَ، وأعُوذُ بِكَ مِنْكَ، لاَ أُحْصِي ثَنَاءً عَلَيْكَ أنْتَ كَمَا أَثْنَيْتَ عَلَى نَفْسِكَ )). رواه مسلم .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nilimkosa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) usiku mmoja, nami nikaanza kumtafuta, nikampata akiwa katika rukuu au sijdah akiomba kwa kusema: "Subhaanaka wa Bihamdika Laa ilaaha illa Anta (Utakaso ni wako na sifa zote njema unastahiki Wewe. Hapana Mola wa kuabudiwa isipokuwa Wewe)."
Na katika riwaayah nyingine: "Mkono wangu ukashika matumbo ya mguu wake yakiwa yamesimamishwa wima akiwa ndani ya Msikiti, naye anasema: "Allaahumma inni a'uwdhu Biridhwaaka min Sakhatwika wa Bimu'aafatika min 'Uquwbatika wa a'uwdhu Bika Minka Laa uhswaa Thanaa'an 'Alayka Anta kamaa Athnayta 'alaa Nafsika (Ee Mola wangu! Mimi ninajilinda kwa radhi Zako dhidi ya ghadhabu Zako, na msamaha Wako dhidi ya adhabu Yako, na ninaomba ulinzi Wako. Mimi sidhibiti kutaja (au kuhesabu) sifa Zako wewe ni kama Ulivyo jisifu Mwenyewe)." [Muslim]
Hadiyth – 24
وعن سعد بن أَبي وقاصٍ رضي الله عنه قَالَ : كنا عِنْدَ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : (( أيعجزُ أحَدُكُمْ أنْ يَكْسِبَ في كلِّ يومٍ ألْفَ حَسَنَةٍ ! )) فَسَأَلَهُ سَائِلٌ مِنْ جُلَسائِهِ : كَيْفَ يَكْسِبُ ألفَ حَسَنَةٍ ؟ قَالَ : (( يُسَبِّحُ مِئَةَ تَسْبِيحَةٍ فَيُكْتَبُ لَهُ ألْفُ حَسَنَةٍ ، أَوْ يُحَطُّ عَنْهُ ألفُ خَطِيئَةٍ )) . رواه مسلم .
Amesema Sa'd bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu): Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), akasema: "Je, anashindwa mmoja wenu kuchuma kila siku hasanah (thawabu) elfu moja?" Akamuuliza muulizaji miongoni mwa waliokuwa katika kikao hicho: "Vipi atachuma mema elfu moja?" Akasema: "Amtakase (Allaah) kwa kuleta Tasbihi mia moja (kwa kusema Subhaana Allaah), hivyo kuandikiwa mema elfu moja au afutiwe madhambi elfu moja." [Muslim]
Hadiyth – 25
وعن أَبي ذر رضي الله عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يُصْبحُ عَلَى كُلِّ سُلاَمَى مِنْ أَحَدِكُمْ صَدَقةٌ : فَكُلُّ تَسْبيحَةٍ صَدَقةٌ ، وَكُلُّ تَحْميدَةٍ صَدَقَةٌ ، وَكُلُّ تَهْلِيلةٍ صَدَقَةٌ ، وَكُلُّ تَكْبيرَةٍ صَدَقَةٌ ، وأمْرٌ بالمَعْرُوفِ صَدَقَةٌ ، وَنَهْيٌ عَنِ المُنْكَرِ صَدَقَةٌ ، وَيجْزئُ مِنْ ذَلِكَ رَكْعَتَانِ يَرْكَعُهُمَا مِنَ الضُّحَى )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Kila kiungo cha mmoja wenu kinapambazukiwa kwa kufanya Swadaqah (jambo jema). Hivyo kila tasbiyh ni swadaqah, na kila tahmiyd ni swadaqah, na kila takbiyra ni swadaqah na kuamrisha mema ni swadaqah na kukataza mabaya ni swadaqah. Na rakaa mbili za Swalaah ya Dhuwhaa unazoswali zatosheleza (kama swadaqah ya yote haya)." [Muslim]
Hadiyth – 26
وعن أم المؤمنين جُويْريَةَ بنت الحارِث رَضِيَ اللهُ عنها: أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم خرجَ مِنْ عِنْدِهَا بُكْرَةً حِيْنَ صَلَّى الصُّبْحَ وَهِيَ في مَسْجِدِها ، ثُمَّ رَجَعَ بَعدَ أنْ أضْحَى وَهِيَ جَالِسَةٌ ، فقالَ : (( مَا زِلْتِ عَلَى الحالِ الَّتي فَارقَتُكِ عَلَيْهَا ؟ )) قالت : نَعَمْ ، فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( لَقَدْ قُلْتُ بَعْدَكِ أرْبَعَ كَلِمَاتٍ ثَلاثَ مَرَّاتٍ ، لَوْ وُزِنَتْ بِمَا قُلْتِ مُنْذُ اليَوْمِ لَوَزَنَتْهُنَّ : سُبْحَانَ الله وَبِحَمْدِهِ عَدَدَ خَلْقِهِ ، وَرِضَا نَفْسِهِ ، وَزِنَةَ عَرْشِهِ ، وَمِدَادَ كَلِمَاتِهِ )) . رواه مسلم .
وفي روايةٍ لَهُ : (( سُبْحانَ الله عَدَدَ خَلْقِهِ ، سُبْحَانَ الله رِضَا نَفْسِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ زِنَةَ عَرْشِهِ ، سُبْحَانَ الله مِدَادَ كَلِمَاتِهِ )) .
وفي رواية الترمذي: (( ألا أُعَلِّمُكِ كَلِمَاتٍ تَقُولِينَهَا؟ سُبحَانَ الله عَدَدَ خَلْقِهِ؛ سُبحَانَ الله عَدَدَ خَلْقِهِ ، سُبحَانَ الله عَدَدَ خَلْقِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ رِضَا نَفْسِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ رِضَا نَفْسِهِ ، سُبْحَانَ الله رِضَا نَفْسِهِ ، سُبْحَانَ الله زِنَةَ عَرْشِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ زِنَةَ عَرشِهِ ، سُبْحَانَ الله زِنَةَ عَرشِهِ ، سُبْحَانَ الله مِدَادَ كَلِمَاتِهِ ، سُبْحَانَ الله مِدَادَ كَلِمَاتِهِ ، سُبْحَانَ الله مِدَادَ كَلِمَاتِهِ )) .
Imepokewa kutoka kwa Mama wa Waumini, Juwayriyah bin Al-Haarith (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitoka chumbani kwake mapema pindi aliposwali Swalaah ya Asubuhi, naye (Juwayriyah) alikuwa akiswali. Baadae alirudi (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) baada ya kuswali Swalaah ya Dhuwhaa, naye (Juwayriyah) alikuwa bado ameketi (katika mswala wake). Akasema: "Bado upo katika hali ile ile niliyokuacha nayo?" Nikasema: "Ndiyo." Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hakika baada ya kuondoka nimesema maneno manne mara tatu, lau zitapimwa na kufananishwa na yale uliyosema asubuhi ya leo basi zitakuwa ni nzito zaidi: Subhaana Allaahi Wa Bihamdihi 'adada Khalqihi wa Ridhwaa' Nafsihi wa zinata 'Arshihi wa midaada Kalimaatih
Namtakasa Allaah (na kila sifa hasi) na namhimidi kwa idadi ya Viumbe Vyake, na kwa idadi ya vilivyoridhiwa na Nafsi Yake, na kwa uzito wa ‘Arshi Yake, na kwa wingi wa wino wa (kuandikia) Maneno Yake. [Muslim]
Na katika riwaayah yake nyengine:
سُبْحانَ الله عَدَدَ خَلْقِهِ ، سُبْحَانَ الله رِضَا نَفْسِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ زِنَةَ عَرْشِهِ ، سُبْحَانَ الله مِدَادَ كَلِمَاتِهِ
"Subhaana Allaahi 'adada Khalqihi, Subhaana Allaahi Ridhwaa' Nafsihi, Subhaana Allaahi zinata 'Arshihi, Subhaana Allaahi midaada Kalimatih
Namtakasa Allaah (na kila sifa hasi) kwa idadi ya Viumbe Vyake, Namtakasa Allaah (na kila sifa hasi) kwa idadi ya vilivyoridhiwa na Nafsi Yake, Namtakasa Allaah (na kila sifa hasi) kwa uzito wa ‘Arshi Yake, Namtakasa Allaah kwa wingi wa wino wa (kuandikia) Maneno Yake.
Na katika riwaayah ya At-Tirmidhiy: "Sikufundishi maneno ambayo utayasema?
سُبحَانَ الله عَدَدَ خَلْقِهِ؛ سُبحَانَ الله عَدَدَ خَلْقِهِ ، سُبحَانَ الله عَدَدَ خَلْقِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ رِضَا نَفْسِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ رِضَا نَفْسِهِ ، سُبْحَانَ الله رِضَا نَفْسِهِ ، سُبْحَانَ الله زِنَةَ عَرْشِهِ ، سُبْحَانَ اللهِ زِنَةَ عَرشِهِ ، سُبْحَانَ الله زِنَةَ عَرشِهِ ، سُبْحَانَ الله مِدَادَ كَلِمَاتِهِ ، سُبْحَانَ الله مِدَادَ كَلِمَاتِهِ ، سُبْحَانَ الله مِدَادَ كَلِمَاتِهِ
"Subhaana Allaahi 'adada Khalqihi, Subhaana Allaahi 'adada Khalqihi, Subhaana Allaahi 'adada Khalqihi, Subhaana Allaahi Ridhwaa' Nafsihi, Subhaana Allaahi Ridhwaa' Nafsihi, Subhaana Allaahi Ridhwaa' Nafsihi, Subhaana Allaahi zinata 'Arshihi, Subhaana Allaahi zinata 'Arshihi, Subhaana Allaahi zinata 'Arshihi, Subhaana Allaahi midaada Kalimatih, Subhaana Allaahi midaada Kalimatih, Subhaana Allaahi midaada Kalimatih.
Namtakasa Allaah (na kila sifa hasi) kwa idadi ya Viumbe Vyake (mara tatu), Namtakasa Allaah (na kila sifa hasi) kwa idadi ya vilivyoridhiwa na Nafsi Yake (mara tatu), Namtakasa Allaah (na kila sifa hasi) kwa uzito wa ‘Arshi Yake (mara tatu), Namtakasa Allaah kwa wingi wa wino wa (kuandikia) Maneno Yake (mara tatu).
Hadiyth – 27
وعن أَبي موسى الأشعري رَضِيَ اللهُ عنه ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَثَلُ الَّذِي يَذْكُرُ رَبَّهُ وَالَّذِي لا يَذْكُرُهُ مَثَلُ الحَيِّ وَالمَيِّتِ )) . رواه البخاري .
ورواه مسلم فَقَالَ : (( مَثَلُ البَيْتِ الَّذِي يُذْكَرُ اللهُ فِيهِ ، وَالبَيْتِ الَّذِي لا يُذْكَرُ اللهُ فِيهِ ، مَثَلُ الحَيِّ والمَيِّتِ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mfano wa yule mwenye kumdhukuru Rabb wake na yule asiye mdhukuru, ni mfano wa aliye hai na maiti." [Al-Bukhaariy]
Na amepokea Muslim kwa kusema: "Mfano wa nyumba ambayo Allaah hutajwa ndani yake na nyumba asiyotajwa Allaah ndani yake, ni mfano wa kilicho hai na maiti."
Hadiyth – 28
وعن أَبي هريرة رَضِيَ اللهُ عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يقول الله تَعَالَى : أنا عِنْدَ ظَنِّ عَبْدِي بِي ، وَأَنَا مَعَهُ إِذَا ذَكَرَنِي ، فإنْ ذَكَرَنِي في نَفْسِهِ ، ذَكَرْتُهُ في نَفْسِي ، وإنْ ذَكَرنِي في ملأٍ ذَكرتُهُ في مَلأٍ خَيْرٍ مِنْهُمْ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Amesema Allaah Ta'aalaa: "Mimi niko katika dhana ya mja Wangu. Nami niko pamoja naye anaponikumbuka; Anaponikumbuka nafsini mwake, Nitamkumbuka Nafsini Mwangu, na anaponikumbuka penye wengi, Nitamkumbuka penye wengi bora zaidi yao." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 29
وعن أَبي هريرة رَضِيَ اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( سَبَقَ المُفَرِّدُونَ )) قالوا : وَمَا المُفَرِّدُونَ ؟ يَا رسولَ الله قَالَ: (( الذَّاكِرُونََ اللهَ كثيراً والذَّاكِرَاتِ )) . رواه مسلم.
وَرُوي : (( المُفَرِّدُونَ )) بتشديد الراءِ وتخفيفها والمشهُورُ الَّذِي قَالَهُ الجمهُورُ : التَّشْديدُ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wameongoza Mufarriduwn." Wakauliza: "Na Mufarriduwn ni kina nani, ee Rasuli wa Allaah?" Akasema: "Wanaume wenye kumdhukuru Allaah kwa wingi na wanawake." [Muslim].
Imepokewa al-Mufarriduwn kwa kuweka shaddah katika herufi "ra" na bila ya shaddah na iliyo mashuhuri ni ile iliyopokewa na Jamhuwr: "Kuweka shaddah."
Hadiyth – 30
وعن جابر رَضِيَ اللهُ عنه قَالَ : سَمِعْتُ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( أفْضَلُ الذِّكْرِ : لا إلهَ إِلاَّ اللهُ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Amesema Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Bora ya dhikri ni kusema Laa ilaaha illaAllaah." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 31
وعن عبد الله بن بسر رَضِيَ اللهُ عنه : أنَّ رجلاً قَالَ : يَا رسولَ الله ، إنَّ شَرَائِعَ الإسْلامِ قَدْ كَثُرَتْ عَليَّ ، فَأَخْبِرْنِي بِشَيءٍ أَتَشَبثُ بِهِ قَالَ : (( لا يَزالُ لِسَانُكَ رَطباً مِنْ ذِكْرِ الله )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Busr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa kuna mtu alisema: "Ee Rasuli wa Allaah! hakika sheria za Kiislamu zimekuwa nyingi juu yangu, nijulishe kitu (chepesi na rahisi) ambacho nitakishika barabara." Akasema: "Uwache ulimi wako uwe majimaji (ujishughulishe sana) katika kumdhukuru Allaah." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 32
وعن جابر رَضِيَ اللهُ عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( من قَالَ : سُبْحان الله وبِحمدِهِ ، غُرِسَتْ لَهُ نَخْلَةٌ في الجَنَّةِ )) . رواه الترمذي، وقال : (( حديث حسن )).
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kusema Subhaana Allaahi wa Bihamdihi, huotesha mtende Peponi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 33
وعن ابن مسعود رَضِيَ اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لَقِيْتُ إبْرَاهِيمَ لَيلَةَ أُسْرِيَ بِي ، فَقَالَ : يَا مُحَمّدُ أقْرِىءْ أُمَّتَكَ مِنِّي السَّلاَمَ ، وَأَخْبِرْهُمْ أنَّ الجَنَّةَ طَيَّبَةُ التُّرْبَةِ ، عَذْبَةُ الماءِ ، وأنَّهَا قِيعَانٌ وأنَّ غِرَاسَهَا : سُبْحَانَ اللهِ ، والحَمْدُ للهِ ، وَلاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ ، واللهُ أكْبَرُ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nilikutana na Ibraahiym ('Alayhis salaam) usiku wa Israa', naye akaniambia: "Ee Muhammad! Watolee salamu Ummah wako kutoka kwangu na uwape habari kuwa Pepo ina mchanga mzuri na maji yake ni matamu na hakika ni pana sana (yenye nafasi muruwa) na kuwa mimea yake ni Subhaana Allaah wal HamduliLLaah wa Laa ilaaha illaaAllaahu wa Allaahu Akabar." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 34
وعن أَبي الدرداءِ رَضِيَ اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( ألا أُنَبِّئُكُمْ بِخَيْرِ أعْمالِكُمْ ، وأزْكَاهَا عِنْدَ مَلِيكِكُمْ ، وأرْفَعِهَا في دَرَجَاتِكُمْ ، وَخَيرٍ لَكُمْ مِنْ إنْفَاقِ الذَّهَبِ والفِضَّةِ ، وَخَيْرٍ لَكُمْ مِنْ أن تَلْقَوا عَدُوَّكُمْ فَتَضْرِبُوا أعْنَاقَهُمْ وَيَضْرِبُوا أعْنَاقَكُمْ ؟ )) قَالَوا : بَلَى ، قَالَ : (( ذِكر الله تَعَالَى )) . رواه الترمذي ، قَالَ الحاكم أَبُو عبد الله : (( إسناده صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Je, siwaambii nyinyi amali bora kwenu, ambayo ni safi kabisa mbele ya mfalme wenu na yenye kunyanyua daraja yenu na ni bora kwenu kuliko kutoa dhahabu na fedha na ni bora kwenu kuliko kukutana na adui zenu na kuwakata shingo zao na wao kukata shingo zenu?" Wakasema: "Ndio." Akasema: "umdhukuru Allaah Ta'aalaa." [At-Tirmidhiy, na akasema Al-Haakim Abu 'Abdillaah kuwa Isnaad yake ni Swahiyh]
Hadiyth – 35
وعن سعد بن أَبي وقاص رَضِيَ اللهُ عنه ، أنَّه دخل مَعَ رسُولِ الله صلى الله عليه وسلم ، عَلَى امْرأةٍ وَبَيْنَ يَدَيْها نَوىً – أَوْ حَصَىً – تُسَبِّحُ بِهِ فَقَالَ : (( أُخْبِرُكِ بما هُوَ أيْسَرُ عَلَيْكِ مِنْ هَذَا - أَوْ أفْضَلُ - )) فَقَالَ : (( سُبْحَانَ الله عَدَدَ مَا خَلَقَ في السَّمَاءِ ، وسُبْحَانَ الله عَدَدَ مَا خَلَقَ في الأرْضِ ، وسُبْحَانَ الله عَدَدَ مَا بَيْنَ ذَلِكَ ، وسُبحَانَ الله عَدَدَ مَا هز خَالِقٌ ، واللهُ أكْبَرُ مِثْلَ ذَلِكَ ، والحَمْدُ للهِ مِثْلَ ذَلِكَ ؛ وَلاَ إلَهَ إِلاَّ اللهُ مِثْلَ ذَلِكَ ، وَلاَ حَولَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِاللهِ مِثْلَ ذَلِكَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Sa'ad bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa walikwenda pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mwanamke ambaye mbele yake kulikuwa na rundo la kokwa za tende au vijiwe, ambazo alikuwa akitumia kusabihi navyo. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Je, nikuambie jambo ambalo ni jepesi kwako kuliko hili au ni bora zaidi?" Akasema: "Subhaana Allaahi kwa idadi ya alivyo viumba katika ardhi na Subhaana Allaahi kwa idadi ya vilivyoko baina yake. Na Subhaana Allaahi kwa idadi ya Alivyoviumba na Atakavyo viumba. Na Allaahu Akbar mfano wa hizo na AlhamduliLLaah mfano wa kama hizo na Laa ilaaha illaAllaahu mfano wa idadi hiyo na Laa Hawla walaa Quwwaata illaa BiLLaahi mfano wa hizo." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 36
وعن أَبي موسى رَضِيَ اللهُ عنه قَالَ : قَالَ لي رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( ألا أدُلُّكَ عَلَى كَنْزٍ مِنْ كُنُوزِ الجَنَّةِ ؟ )) فقلت : بلى يَا رسولَ الله قَالَ : (( لا حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ باللهِ )) متفق عَلَيْهِ .
Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Aliniambia mimi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Sikujulishi wewe hazina miongoni mwa hazina za Peponi?" Nikasema: "Nieleze, ee Rasuli wa Allaah! Akasema: "Laa Hawla walaa Quwwataa illaa BiLLaahi." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawud na At-Tirmidhiy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب ذكر الله تَعَالَى قائماً أَوْ قاعداً ومضطجعاً
ومحدثاً وجنباً وحائضاً إِلاَّ القرآن فَلاَ يحل لجنب وَلاَ حائض
02-Mlango Wa Kumdhukuru Allaah Ta'aalaa kwa Kusimama, Kukaa, Kujilaza na katika Hadathi, Janaba, Hedhi Isipokuwa Kusoma Qur-aan Ambayo Haifai Kusomwa kwa Mwenye Janaba na Hedhi
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿١٩٠﴾
الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ ﴿١٩١﴾
Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na mabadiliko ya mfuatano wa usiku na mchana, bila shaka ni Aayaat (ishara, zingatio) kwa wenye akili. Ambao wanamdhukuru Allaah wakiwa wima, au wamekaa au wamejinyoosha [Aal-'Imraan: 190-191]
Hadiyth – 1
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : كَانَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم يَذْكُرُ اللهَ عَلَى كُلِّ أَحْيَانِهِ . رواهُ مسلم .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akimtaja (akimdhukuru) Allaah Ta'aalaa kila wakati." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عباسٍ رَضِيَ اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَوْ أنَّ أَحَدَكُمْ إِذَا أتَى أهْلَهُ قَالَ : بِسْمِ الله ، اللَّهُمَّ جَنِّبْنَا الشَّيْطَانَ ، وَجَنِّبِ الشَّيْطَانَ مَا رَزَقْتَنَا ، فَقُضِيَ بَيْنَهُمَا وَلَدٌ ، لَمْ يَضُرَّهُ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau mmoja wenu atamwingilia mkewe akasema: "BismiLLaahi Allaahumma Jannibnaa ash-shaytwaana wa Jannibish shaytwaana Maa Razaqtana (Kwa jina la Allaah, ee Rabb wangu! Tuepushe na shetani na umuepushie shetani kile utakacho Turuzuku). Watakapojaaliwa kupata mtoto basi hatadhuriwa (na shetani)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يقوله عِنْدَ نومه واستيقاظه
03-Mlango Wa Anachosema Wakati wa Kulala na Kuamka
Alhidaaya.com [4]
عن حُذَيفَةَ ، وأبي ذرٍ رضي الله عنهما ، قالا : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا أوَى إِلَى فِرَاشِهِ ، قَالَ : (( بِاسْمِكَ اللَّهُمَّ أَحْيَا وَأموتُ )) وَإذَا اسْتَيقَظَ قَالَ : (( الحَمْدُ للهِ الَّذِي أَحْيَانَا بعْدَ مَا أماتَنَا وإِلَيْهِ النُّشُورُ )) . رواه البخاري .
Wamesema Hudhayfah na Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Alikuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anapojilaza kwenye godoro husema: "Bismika Allaahumma amuwtu wa ahyaa (Kwa jina lako, ee Rabb wangu! Ninakufa na kubaki hai)." Na anapoamka husema: "AlhamduliLLaahi ahyaanaa ba'ada maa amaatanaa wa ilayhin Nushuwr (Sifa zote njema anastahiki Allaah ambaye Ametuhuisha baada ya kutufisha na Kwake Tutarudi)." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل حِلَقِ الذكر
والندب إِلَى ملازمتها والنهي عن مفارقتها لغير عذر
04-Mlango Wa Fadhila ya Vikundi vya Dhikri na Kupendeza Kujilazimisha Nayo na Kukatazwa Kujiondosha Bila ya Udhuru
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَاصْبِرْ نَفْسَكَ مَعَ الَّذِينَ يَدْعُونَ رَبَّهُم بِالْغَدَاةِ وَالْعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجْهَهُ ۖ وَلَا تَعْدُ عَيْنَاكَ عَنْهُمْ ﴿٢٨﴾
Na isubirishe nafsi yako pamoja na wale wanaomuomba Rabb wao asubuhi kabla jua kucha na jioni, wanataka Wajihi Wake. Na wala macho yako yasiwavuke [Al-Kahf: 28]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ للهِ تَعَالَى مَلائِكَةً يَطُوفُونَ في الطُّرُقِ يَلْتَمِسُونَ أهْلَ الذِّكْرِ ، فإذا وَجَدُوا قَوْمَاً يَذْكُرُونَ اللهَ عزوجل ، تَنَادَوْا : هَلُمُّوا إِلَى حَاجَتِكُمْ ، فَيَحُفُّونَهُمْ بِأَجْنِحَتِهِم إِلَى السَّمَاءِ الدُّنْيَا ، فَيَسْألُهُمْ رَبُّهُمْ – وَهُوَ أعْلَم - : مَا يقولُ عِبَادي ؟ قَالَ : يقولون : يُسَبِّحُونَكَ ، ويُكبِّرُونَكَ ، وَيَحْمَدُونَكَ ، ويُمَجِّدُونَكَ ، فيقول : هَلْ رَأَوْنِي ؟ فيقولونَ : لا واللهِ مَا رَأَوْكَ . فيقولُ : كَيْفَ لَوْ رَأوْني ؟! قَالَ : يقُولُونَ : لَوْ رَأوْكَ كَانُوا أَشَدَّ لَكَ عِبَادَةً ، وَأَشَدَّ لَكَ تَمْجِيداً ، وأكْثَرَ لَكَ تَسْبِيحاً . فَيقُولُ : فماذا يَسْألونَ ؟ قَالَ : يقُولُونَ : يَسْألُونَكَ الجَنَّةَ . قَالَ : يقولُ : وَهل رَأَوْها ؟ قَالَ : يقولون : لا واللهِ يَا رَبِّ مَا رَأَوْهَا . قَالَ : يقول : فَكيفَ لَوْ رَأوْهَا ؟ قَالَ : يقولون : لَوْ أنَّهُمْ رَأوْهَا كَانُوا أشَدَّ عَلَيْهَا حِرْصاً ، وأشدَّ لَهَا طَلَباً ، وأعْظَمَ فِيهَا رَغْبَةً . قَالَ : فَمِمَّ يَتَعَوَّذُونَ ؟ قَالَ : يقولون : يَتَعَوَّذُونَ مِنَ النَّارِ ؛ قَالَ : فيقولُ : وَهَلْ رَأوْهَا ؟ قَالَ : يقولون : لا واللهِ مَا رَأوْهَا . فيقولُ : كَيْفَ لَوْ رَأوْهَا ؟! قَالَ : يقولون : لَوْ رَأوْهَا كانوا أشَدَّ مِنْهَا فِرَاراً ، وأشَدَّ لَهَا مَخَافَةً . قَالَ : فيقولُ : فَأُشْهِدُكُمْ أنِّي قَدْ غَفَرْتُ لَهُم ، قَالَ : يقولُ مَلَكٌ مِنَ المَلاَئِكَةِ : فِيهم فُلاَنٌ لَيْسَ مِنْهُمْ ، إنَّمَا جَاءَ لِحَاجَةٍ ، قَالَ : هُمُ الجُلَسَاءُ لا يَشْقَى بِهِمْ جَلِيسُهُمْ )) . متفق عَلَيْهِ .وفي رواية لمسلمٍ عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إن للهِ مَلاَئِكَةً سَيَّارَةً فُضُلا يَتَتَبُّعُونَ مَجَالِسَ الذِّكْرِ ، فَإذَا وَجَدُوا مَجْلِساً فِيهِ ذِكْرٌ ، قَعَدُوا مَعَهُمْ ، وَحَفَّ بَعْضُهُمْ بَعْضاً بِأجْنِحَتِهِمْ حَتَّى يَمْلَؤُوا مَا بَيْنَهُمْ وَبَيْنَ السَّماءِ الدُّنْيَا ، فإذَا تَفَرَّقُوا عَرَجُوا وَصَعدُوا إِلَى السَّمَاءِ ، فَيَسْأَلُهُمْ اللهُ عزوجل - وَهُوَ أعْلَمُ - : مِنْ أيْنَ جِئْتُمْ ؟ فَيَقُولُونَ : جِئْنَا مِنْ عِنْدِ عِبادٍ لَكَ في الأرْضِ : يُسَبِّحُونَكَ ، ويُكبِّرُونَكَ ، وَيُهَلِّلُونَكَ ، وَيَحْمَدُونَكَ ، وَيَسْألُونَكَ . قَالَ : وَمَاذا يَسْألُونِي ؟ قالوا : يَسْألُونَكَ جَنَّتَكَ . قَالَ : وَهَلْ رَأَوْا جَنَّتِي ؟ قالوا : لا ، أَيْ رَبِّ . قَالَ : فكيْفَ لَوْ رَأَوْا جَنَّتي ؟! قالوا : ويستجيرونكَ . قَالَ : ومِمَّ يَسْتَجِيرُونِي ؟ قالوا : مِنْ نَارِكَ يَا رَبِّ . قَالَ : وَهَلْ رَأوْا نَاري ؟ قالوا : لا ، قَالَ : فَكَيْفَ لَوْ رَأَوْا نَارِي ؟! قالوا : وَيَسْتَغفِرُونكَ ؟ فيقولُ : قَدْ غَفَرْتُ لَهُمْ ، وَأَعْطَيْتُهُمْ مَا سَألُوا ، وَأجَرْتُهُمْ مِمَّا اسْتَجَارُوا . قَالَ : فيقولون : ربِّ فيهمْ فُلانٌ عَبْدٌ خَطَّاءٌ إنَّمَا مَرَّ ، فَجَلَسَ مَعَهُمْ . فيقُولُ : ولهُ غَفَرْتُ ، هُمُ القَومُ لاَ يَشْقَى بِهِمْ جَلِيسُهُمْ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Anao Malaaikah wanaozunguka majiani, wanawafafuta wanao dhikiri (wanao mtukuza Allaah). Wanapowakuta watu wanamtaja Allaah, wanaita: 'Njooni! Kwenye kile mnachokihitaji.' Watazunguka kwa mbawa zao mpaka kufikia uwingu wa dunia. Rabb wao Atawauliza, hali Anajua zaidi yao: 'Wanasema nini waja Wangu?' Malaaikah watajibu: 'Wanasema: Wanakusabihi na wana kutukuza (kwa kusema Allaahu Akbar) na wanakuhimidi na wanakutukuza.' Kisha Allaah Atawauliza: 'Je, wameniona?' Watajibu: 'Hapana Wa-Allaahi! Hawajakuona.' Atauliza: 'Vipi kama wangeli niona?' Watasema: 'Kama wangeli kuona wangeli kuabudu zaidi, wangeli kutukuza zaidi, na wangeli kutakasa kwa wingi zaidi.' Atauliza: 'Wananimba nini?' Watajibu: 'Wanakuomba Pepo.' Atauliza: 'Je, wameiona?' Watasema: 'Hapana Wa-Allaahi! Ee Rabb hawakuiona.' Atawauliza: 'Vipi kama wangeona?' Watasema: 'Kama wangaliiona wangalikuwa na pupa nayo zaidi, wangeli itaka zaidi, na wangalikuwa na mapenzi nayo makubwa zaidi.' Atauliza: 'Wanajilinda na nini?' Watasema: 'Na moto.' Atauliza: Je, wameuona?' Watajibu: 'Hapana Wa-Allaahi! Hawakuuona.' Atasema: 'Vipi kama wangeuona?' Watasema: 'Kama wangeliuona wangeli kimbia zaidi, na wangeli uogopa zaidi.' Atasema: 'Hapo Allaah atawaambia nini washuhudisha kuwa mimi Nimewasamehe.' Atasema Malaaikah miongoni mwa Malaaikah: 'Kati yao kuna fulani, sio miongoni mwao. Bali alikuja kwa mahitaji (mengine).' Allaah Atasema: 'Hao ndio wenye kikao, na anyekaa nao, kwa ajili yao, hawi na maisha mabaya.' [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah ya Muslim: Kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Anacho kikosi cha Malaaikah wanaotembelea wakitafuta vikao vya dhikri. Wanapopata kikao cha dhikri, wanakaa pamoja nao, na kufunika baadhi yao kwa wengine kwa mbawa zao na baina ya uwingu wa dunia. Pindi wanapoondoka na kuelekea mbinguni. Allaah 'Azza wa Jalla atawauliza japokuwa Anajua zaidi: 'Je, munatoka wapi?' Watajibu: 'Sisi tunatoka kwa waja Wako walio ardhini, na Wanakusabihi, na wanaleta takbiri na tahlili na Wanakuhimidi na Kukuomba.' Atauliza: 'Na Wananiomba nini?' Watajibu: 'Wanakuomba Pepo.' Atauliza: 'Na je, wameiona Pepo Yangu?' Watasema: 'Hapana ee Rabb.' Atauliza: 'Vipi kama wangeliiona Pepo Yangu?' Watasema: 'Na wanataka ulinzi kutoka Kwako.' Atauliza: 'Na wanajilinda na nini?' Watajibu: 'Na Moto Wako, ee Rabb.' Atauliza: 'Na je, wameuona Moto Wangu?' Watajibu: 'Hapana.' Atauliza: 'Vipi kama wangaliuona Moto Wangu?' Watasema: 'Na wanataka msamaha kutoka Kwako.' Atasema: 'Hakika Nimewasamehe na Nimewapatia walichoomba na Nimewalinda kwa walichotaka ulinzi kwacho.' Akasema: Watasema Malaaikah: 'Rabb wetu! Kati yao kuna fulani ambaye ni mja mwenye kufanya madhambi. Hakika yeye alikuwa anapita, akakaa nao.' Atasema: 'Na yeye pia Nimemsamehe. Wao watu ambao hawawi na maisha mabaya."
Hadiyth – 2
وعنه وعن أَبي سعيدٍ رضي الله عنهما ، قالا : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لا يَقْعُدُ قَومٌ يَذكُرُونَ اللهَ عزوجل إِلاَّ حَفَّتْهُمُ المَلائِكَةُ وغَشِيَتْهُمُ الرَّحْمَةُ وَنَزَلَتْ عَلَيْهِمْ السَّكِينَةُ ؛ وَذَكَرَهُمُ اللهُ فِيمَنْ عِنْدَهُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hawakai watu kumdhukuru Allaah isipokuwa huzungukwa na Malaaikah, na hufunikwa na rehma (kutoka kwa Allaah), na huteremkiwa na utulivu na Allaah huwataja kwa walioko Naye." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي واقدٍ الحارث بن عوف رضي الله عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم بَيْنَمَا هُوَ جَالِسٌ في المَسْجِدِ ، والنَّاسُ مَعَهُ ، إذْ أقْبَلَ ثَلاثَةُ نَفَرٍ ، فأقْبَلَ اثْنَانِ إِلَى رسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وَذَهَبَ واحِدٌ ؛ فَوَقَفَا عَلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم . فأمَّا أحَدُهُما فَرَأَى فُرْجةً في الحَلْقَةِ فَجَلَسَ فِيهَا ، وَأمَّا الآخرُ فَجَلَسَ خَلْفَهُمْ ، وأمَّا الثَّالثُ فأدْبَرَ ذاهِباً . فَلَمَّا فَرَغَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( ألاَ أُخْبِرُكُمْ عَنِ النَّفَرِ الثَّلاَثَةِ : أَمَّا أَحَدُهُمْ فَأوَى إِلَى اللهِ فآوَاهُ اللهُ إِلَيْهِ . وَأمَّا الآخَرُ فاسْتَحْيَى فَاسْتَحْيَى اللهُ مِنْهُ ، وأمّا الآخَرُ ، فَأعْرَضَ ، فَأَعْرَضَ اللهُ عَنْهُ )) . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Waaqid Al-Haarith bin 'Awf (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa amekaa Msikitini na watu wakiwa pamoja naye, mara wakaja watu watatu. Wawili (kati ya hao watatu) walikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na watatu wao akaenda zake, wakasimama mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Ama mmoja wao aliona nafasi katika kiako, akaenda akaaa hapo na yule mwingine alikaa nyuma ya kikao hicho. Ama yule watatu aligeuka na kwenda zake. Alipomaliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mazungumzo yake alisema: "Siwajulishi nyinyi kuhusu hawa watu watatu: Ama mmoja wao, alikuja kwa Allaah, Naye Akamjia (kwa kumfunika na kumuweka chini ya ulinzi Wake). Na ama yule wa pili aliona haya na hivyo Allaah kumuonea haya. Na ama yule wa mwisho, aligeuka na kwenda zake, na hivyo Allaah akageuka kutoka Kwake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه قَالَ : خرج معاوية رضي الله عنه عَلَى حَلْقَةٍ في المَسْجِدِ ، فَقَالَ : مَا أجْلَسَكُمْ ؟ قالوا : جَلَسْنَا نَذْكُرُ اللهَ . قَالَ : آللهِ مَا أجْلَسَكُمْ إِلاَّ ذاك ؟ قالوا : مَا أجْلَسَنَا إِلاَّ ذَاكَ ، قَالَ : أما إنِّي لَمْ اسْتَحْلِفْكُمْ تُهْمَةً لَكُمْ ، وَمَا كَانَ أحَدٌ بِمَنْزِلَتِي مِنْ رَسولِ الله صلى الله عليه وسلم أَقَلَّ عَنْهُ حَديثاً مِنِّي : إنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم خَرَجَ عَلَى حَلْقَةٍ مِنْ أصْحَابِهِ فَقَالَ : (( مَا أجْلَسَكُمْ ؟ )) قالوا : جَلَسْنَا نَذْكُرُ الله وَنَحْمَدُهُ عَلَى مَا هَدَانَا للإسْلاَمِ ؛ وَمَنَّ بِهِ عَلَيْنَا . قَالَ : (( آللهِ مَا أجْلَسَكُمْ إِلاَّ ذَاكَ ؟ )) قالوا : واللهِ مَا أجْلَسَنَا إِلاَّ ذَاكَ . قَالَ : (( أمَا إنِّي لَمْ أسْتَحْلِفْكُمْ تُهْمَةً لَكُمْ ، ولكِنَّهُ أتَانِي جِبرِيلُ فَأخْبَرَنِي أنَّ الله يُبَاهِي بِكُمُ المَلاَئِكَةَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy kuwa amesema: Siku moja Mu'aawiyah (Radhwiya Allaahu 'anhu) alizuru Msikiti na kuona Halaqah (duara ya wasomaji). Akauliza: "Ni kipi kilichowafanya nyinyi mkae?" Wakajibu: "Tumekaa ili kumdhukuru Allaah." Akauliza: "Kwa Allaah, hamkukaa ila kwa sababu hiyo." Wakajibu: "Hatukukaa isipokuwa kwa hilo." Akasema: "Ama mimi sikuwaambia muape kwa kuwatuhumu. Na hakuna yeyote katika daraja yangu kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kupokea Hadiyth chache sana kuliko mimi. Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuja katika Halaqah ya Swahaaba zake na kuwauliza: 'Ni kipi kilicho wafanya muwe katika kikao?' Wakajibu: 'Tumekaa ili tumdhukuru Allaah na kumhimidi kwa kutuongoa (kutuingiza) katika Uislamu na kutupatia neema hiyo.' Akauliza: Kwa Allaah, hamkukaa ila kwa sababu hiyo." Wakajibu: "Hatukukaa isipokuwa kwa hilo." Akasema: "Ama kwa hakika! MImi sijawafanya muape kwa kuwatuhumu (au kuwa na shaka) nyinyi, lakini amekuja kwangu Jibriyl na kunipasha habari kuwa Allaah Amefurahi sana na kuwasifu nyinyi mbele ya Malaaikah Zake." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الذكر عِنْدَ الصباح والمساء
05-Mlango Wa Kumtaja Allaah Asubuhi na Jioni
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَاذْكُر رَّبَّكَ فِي نَفْسِكَ تَضَرُّعًا وَخِيفَةً وَدُونَ الْجَهْرِ مِنَ الْقَوْلِ بِالْغُدُوِّ وَالْآصَالِ وَلَا تَكُن مِّنَ الْغَافِلِينَ ﴿٢٠٥﴾
Na mdhukuru Rabb wako katika nafsi yako kwa unyenyekevu na kwa khofu na kwa ulimi bila sauti kubwa asubuhi na jioni, na wala usiwe miongoni mwa walioghafilika. [Al-A'raaf: 205]
وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ غُرُوبِهَا ۖ ﴿١٣٠﴾
Na sabihi ukimhimidi Rabb wako kabla ya kuchomoza jua, na kabla ya kuchwa kwake. [Twaahaa: 130]
وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِبْكَارِ﴿٥٥﴾
Na sabbih na mhimidi Rabb wako jioni na asubuhi. [Gaafir: 55]
فِي بُيُوتٍ أَذِنَ اللَّـهُ أَن تُرْفَعَ وَيُذْكَرَ فِيهَا اسْمُهُ يُسَبِّحُ لَهُ فِيهَا بِالْغُدُوِّ وَالْآصَالِ ﴿٣٦﴾
Katika nyumba ambazo Allaah Ameidhinisha litukuzwe na litajwe humo Jina Lake, wanamsabihi humo asubuhi na jioni.
رِجَالٌ لَّا تُلْهِيهِمْ تِجَارَةٌ وَلَا بَيْعٌ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَإِقَامِ الصَّلَاةِ وَإِيتَاءِ الزَّكَاةِ ۙ يَخَافُونَ يَوْمًا تَتَقَلَّبُ فِيهِ الْقُلُوبُ وَالْأَبْصَارُ ﴿٣٧﴾
Wanaume ambao haiwashughulishi tijara wala uuzaji na kumdhukuru Allaah na kusimamisha Swalaah, na kutoa Zakaah wanakhofu Siku zitakapopinduka humo nyoyo na macho. [An-Nuwr: 36-37]
إِنَّا سَخَّرْنَا الْجِبَالَ مَعَهُ يُسَبِّحْنَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِشْرَاقِ ﴿١٨﴾
Hakika Sisi Tulitiisha milima iwe pamoja naye ikisabbih jioni na baada ya kuchomoza jua. [Swaad: 18]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ قَالَ حِيْنَ يُصْبِحُ وَحينَ يُمْسِي : سُبْحَانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ ، مِئَةَ مَرَّةٍ ، لَمْ يَأتِ أَحَدٌ يَوْمَ القِيَامَةِ بِأفْضَلَ مِمَّا جَاءَ بِهِ ، إِلاَّ أحَدٌ قَالَ مِثْلَ مَا قَالَ أَوْ زَادَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kusema asubuhi na jioni Subhaana Allaahi wa Bihamdihi mara mia moja, hatakuja na jambo (amali) bora yeyote Siku ya Qiyaamah isipokuwa yule aliyesema mfano wake au aliyezidisha." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : جَاءَ رجلٌ إِلَى النبيّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : يَا رسولَ الله مَا لَقِيْتُ مِنْ عَقْرَبٍ لَدَغَتْنِي البَارِحَةَ ! قَالَ : (( أمَا لَوْ قُلْتَ حِيْنَ أمْسَيْتَ : أعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ : لَمْ تَضُرَّك )) . رواه مسلم .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Alikuja mtu kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Niliumwa na nge jana usiku hivyo kupata maumivu makubwa." Akasema: "Ama kama ungelisema pindi kunapoingia usiku A'uwdhu bikalimaati LLaahit Taammaati min sharri maa Khalaq (Ninajilinda kwa maneno timilifu ya Allaah kutokana na shari ya Ulivyo viumba), hivyo nge hangekudhuru." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم ، أنَّه كَانَ يقولُ إِذَا أصْبَحَ : (( اللَّهُمَّ بِكَ أصْبَحْنَا ، وَبِكَ أمْسَيْنَا ، وَبِكَ نَحْيَا ، وَبِكَ نَمُوتُ ، وَإلَيْكَ النُّشُورُ )) . وإذا أمسَى قَالَ : (( اللَّهُمَّ بِكَ أمْسَيْنَا ، وبِكَ نَحْيَا ، وَبِكَ نَمُوتُ . وَإلْيَكَ النُّشُورُ )) . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisema kunapo pambazuka: "Allaahumma bika aswbahna wa bika amsayna wa bika nahyaa wa bika namuwt wa ilaykan nushuwr (Ee Rabb Wangu! Kwa fadhila Zako ndio tunafika asubuhi na Kwako ndio tunafika jioni na kwa neema Yako ndio tunabaki hai na Kwako ndio tunakufa, na Kwako ndio marejeo yetu)." Na anapofikiwa na jioni akisema: "Allaahumma bika amsayna wa bika nahyaa wa bika namuwtu wa ilaykan nushuwr (Ee Rabb Wangu! Kwa fadhila Zako ndio tunafika jioni, na kwa neema Yako ndio tunabaki hai na Kwako ndio tunakufa, na Kwako ndio marejeo yetu)." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ أَبَا بكرٍ الصديق رضي اللهُ عنه قَالَ : يَا رسول الله مُرْني بِكَلِمَاتٍ أقُولُهُنَّ إِذَا أصْبَحْتُ وإذا أمْسَيْتُ ، قَالَ : (( قُلْ : اللَّهُمَّ فَاطِرَ السَّمَاواتِ والأرْضِ عَالِمَ الغَيْبِ والشَّهَادَةِ ؛ رَبَّ كُلِّ شَيْءٍ وَمَلِيكَهُ ، أَشْهَدُ أنْ لا إلَهَ إِلاَّ أنْتَ ، أعُوذُ بِكَ مِنْ شَّرِّ نَفْسِي وَشَرِّ الشَّيْطَانِ وَشِرْكِهِ )) قَالَ : (( قُلْهَا إِذَا أصْبَحْتَ ، وإذَا أمْسَيْتَ ، وإذَا أخَذْتَ مَضْجَعَكَ )) . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Abu Bakr As-Swiddiq (Radhwiya Allaahu 'anhu) aliuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Niamuru mimi kwa maneno (ya duaa) ambayo nitayasoma wakati wa asubuhi na jioni." Akasema: "Sema: Allaahumma Faatwiras Samaawaati wal ardhwi 'Aalimal ghaybi wash-shahaadati Rabba kulli shay'in wa maliykahu Ashhadu an laa illaaha illa Anta A'uwdhu Bika min sharri nafsiy wa sharrish Shaytwaan wa shirkih (Ee Rabb Wangu! Muumbaji wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa yaliyofichikana na yaliyo dhahiri. Rabb na Mwenye kumiliki kila kitu. Nashuhudia ya kwamba hapana muabuduwa wa haki ila Wewe. Ninajilinda Kwako kutokana na shari ya nafsi yangu na shari ya shetani na anavyoitia katika kumshirikisha Allaah)." Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Yaseme hayo asubuhi na jioni na unapokwenda kitandani (kwa ajili ya kulala)." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 5
وعن ابن مسعودٍ رضي اللهُ عنه قَالَ : كَانَ نبيُّ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا أَمْسَى قَالَ : (( أَمْسَيْنَا وأمْسَى المُلْكُ للهِ ، والحَمْدُ للهِ ، لا إلهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَريكَ لَهُ )) قَالَ الراوي : أَرَاهُ قَالَ فِيهِنَّ : (( لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدير ، رَبِّ أسْألُكَ خَيْرَ مَا في هذِهِ اللَّيْلَةِ وَخَيْرَ مَا بَعْدَهَا ، وَأعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا في هذِهِ اللَّيْلَةِ وَشَرِّ مَا بَعْدَهَا ، رَبِّ أعُوذُ بِكَ مِنَ الكَسَلِ ، وَسُوءِ الكِبَرِ ، رَبِّ أعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابٍ في النَّارِ ، وَعَذَابٍ في القَبْرِ )) ، وَإذَا أصْبَحَ قَالَ ذَلِكَ أيضاً (( أصْبَحْنَا وأصْبَحَ المُلْكُ للهِ )) . رواه مسلم .
Amesema Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa inapoingia jioni (usiku) akisema: "Amsaynaa wa amsaal Mulku Lillaahi wal HamduliLLaahi, Laa ilaaha illaAllaahu wahdahu laa Shariyka lahu (Tumeingiliwa na jioni na kuingia usiku katika ufalme wa Allaah na sifa zote njema anastahiki Allaah. Hapana Rabb wa kuabudiwa isipokuwa Allaah Peke Yake hana mshirika kabisa)." Amesema mpokezi: "Naona kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) ndani yake: "Lahul Mulku wa lahul Hamdu wa Huwa 'alaa kulli shay'in Qadiyr. Rabbi As'aluka khayra maa fiy hadhihil laylah wa khayra maa ba'dahaa wa a'uwdhu Bika min sharri maa fiy hadhihil laylah wa sharri maa ba'dahaa, Rabbi a'uwdhu Bika minal kasalwa suuil kibari, Rabbi a'uwdhu Bika min 'adhaabin fii naar wa 'adhaabin fil qabr (Ufalme ni Wake na sifa njema anastahiki Yeye na Yeye tu Ndiye aliye juu ya kila jambo, Mwenye Uwezo mkubwa sana. Rabb wangu nakuomba kheri iliyopo ndani ya usiku huu na kheri ya baada yake. Na ninajilinda Kwako na shari ya yaliyomo ndani ya usiku huu na shari ya baada yake. Rabbi, ninajilinda Kwako na uvivu na ouvu wa uzee, ninajilinda Kwako na adhabu ya Moto na adhabu ya kaburini)." Na kunapo pambazuka akisema hayo pia: "Aswbahnaa wa aswbahal Mulku LiLLaahi (Kupambazuka kwetu na kupambazuka katika ufalme wa Allaah)." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن عبد الله بن خُبَيْب - بضم الخاء المعجمة - رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ لي رَسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( اقْرَأْ : قُلْ هُوَ اللهُ أحَدٌ ، والمُعَوِّذَتَيْنِ حِيْنَ تُمْسِي وَحِينَ تُصْبحُ ، ثَلاثَ مَرَّاتٍ تَكْفيكَ مِنْ كُلِّ شَيْءٍ )) . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Khubayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Soma: Qul Huwa Allaahu Ahad na kinga mbili (Suratul Falaq na Suratun Naas) kunapoingia jioni na kunapo pambazuka mara tatu, zitakutosheleza lwa kila kitu (zitakuwa ni ngao kwako dhidi ya kila kitu kiovu)." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 7
وعن عثمان بن عفان رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَا مِنْ عَبْدٍ يَقُولُ في صَبَاحِ كُلِّ يَوْمٍ وَمَسَاءِ كُلِّ لَيْلَةٍ : بِسْمِ اللهِ الَّذِي لا يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ في الأرْضِ وَلاَ في السَّمَاءِ وَهُوَ السَّمِيعُ العَلِيمُ ، ثَلاثَ مَرَّاتٍ ، إِلاَّ لَمْ يَضُرَّهُ شَيْءٌ )) . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana mja yeyote atakayesema kila siku asubuhi na jioni: BismiLLaahi lladhiy laa yadhuwrru ma'a ismuhu shay'un fil ardhi wa laa fis samaa'i wa Huwas Samiy'ul 'Aliym (Kwa jina la Allaah ambaye kwamba kwa baraka ya Jina Lake, hakitanidhuru kitu chochote ardhini na mbinguni, Naye ni Mwenye husikia Mjuzi) mara tatu ila hatadhurika na chochote." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يقوله عِنْدَ النوم
06-Mlango Wa Anachosema Wakati wa Kulala
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿١٩٠﴾
Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na mabadiliko ya mfuatano wa usiku na mchana, bila shaka ni Aayaat (ishara, zingatio) kwa wenye akili.
الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَـٰذَا بَاطِلًا سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴿١٩١﴾
Ambao wanamdhukuru Allaah wakiwa wima, au wamekaa au wamejinyoosha, na wanatafakari katika kuumbwa mbingu na ardhi (wakisema): Rabb wetu, Hukuumba haya bure, Utakasifu Ni Wako, basi Tukinge na adhabu ya moto. [Aal-'Imraan: 190-191]
Hadiyth – 1
وعن حُذَيْفَةَ ، وأبي ذرٍّ رضي الله عنهما : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا أَوَى إِلَى فِراشِهِ ، قَالَ : (( بِاسْمِكَ اللَّهُمَّ أَحْيَا وأَمُوتُ )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Hudhayfah na Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapojilaza kwenye godoro husema: "Bismika Allaahumma ahyaa wa amuwtu (Kwa Jina Lako, ee Rabb Wangu! Ninabaki hai na kufa)." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن عليٍّ رضي الله عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ لَهُ ولِفَاطِمَةَ رضي الله عنهما : (( إِذَا أَوَيْتُمَا إِلَى فِرَاشِكُمَا – أَوْ إِذَا أَخَذْتُمَا مَضَاجِعَكُمَا – فَكَبِّرا ثَلاَثاً وَثَلاثِينَ ، وَسَبِّحَا ثَلاثاً وَثَلاثِينَ ، واحْمِدا ثَلاثاً وَثَلاثِينَ )) وفي روايةٍ : التَّسْبيحُ أرْبعاً وثلاثينَ ، وفي روايةٍ : التَّكْبِيرُ أرْبعاً وَثَلاَثينَ . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia yeye na Faatwimah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): "Pindi mnapoelekea kwenye kitanda au mnapolala leteni Takbira mara thelathini na tatu, na Tasbihi mara thelathini na tatu na Tahmidi mara thelathini na tatu."
Na katika riwaayah nyingine: "Leteni Tasbihi mara thelathini na nne."
Na katika riwaayah nyingine: "Leteni Takbira mara thelathini na nne." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا أَوَى أَحَدُكُمْ إِلَى فِرَاشِهِ فَليَنْفُضْ فِرَاشَهُ بِدَاخِلَةِ إزَارِهِ فإنَّهُ لا يَدْرِي مَا خَلَفَهُ عَلَيْهِ ، ثُمَّ يَقُولُ : بِاسمِكَ رَبِّي وَضَعْتُ جَنْبي ، وَبِكَ أرْفَعُهُ ، إنْ أَمْسَكْتَ نَفْسِي فَارْحَمْهَا ، وَإنْ أَرْسَلْتَهَا ، فاحْفَظْهَا بِمَا تَحْفَظُ بِهِ عِبَادَكَ الصَّالِحِينَ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapotaka kulala mmoja wenu kwenye godoro lake kwanza akung'ute godoro lake upande wa ndani wa kikoi chake kwa kuwa haelewi alicho kiacha juu yake. Kisha aseme: 'Bismika Rabbiy wadha'tu jambi wabika arfa'uhu in amsakta nafsi farhamhaa wa in arsaltahaa fahfadhhaa bimaa Tahfadhu bihi 'Ibaadikasw Swaalihiyn (Kwa jina Lako, Rabb Wangu! Nimeuweka ubavu wangu, na kwa ajili Yako nina uinua. Kama Utaishika nafsi yangu, basi ihurumie na kama Ukiiachia Ihifadhi kwa kile Unachowahifadhia watu wema)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 4
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، كَانَ إِذَا أخَذَ مَضْجَعَهُ نَفَثَ في يَدَيْهِ ، وَقَرَأَ بالمُعَوِّذَاتِ ، ومَسَحَ بِهِمَا جَسَدَهُ . متفق عَلَيْهِ .
وفي رواية لهما : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إذا أَوَى إِلَى فِرَاشِهِ كُلَّ لَيْلَةٍ جَمَعَ كَفَّيْهِ ، ثُمَّ نَفَثَ فِيهِمَا فَقَرأَ فيهِما : (( قُلْ هُوَ اللهُ أحَدٌ ، وَقَلْ أعُوذُ بِرَبِّ الفَلَقِ ، وَقُلْ أعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ )) ثُمَّ مَسَحَ بِهِما مَا استْطَاعَ مِنْ جَسَدِهِ ، يَبْدَأُ بهما عَلَى رَأسِهِ وَوجْهِهِ ، وَمَا أقْبَلَ مِنْ جَسَدِهِ ، يَفْعَلُ ذَلِكَ ثَلاَثَ مَرَّاتٍ . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapolala hupuliza mikononi mwake Mu'awidhatain na kusoma (Al-Falaq - An- Naas) na kupaka mwili wake kwa hizo." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Na katka riwaayah yao nyingine: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapotaka kulala godoroni kila usiku akivishikanisha vitanga vyake, kisha akipuliza ndani yake na kusoma ( قُلْ هُوَ اللهُ أحَدٌ ، وَقَلْ أعُوذُ بِرَبِّ الفَلَقِ ، وَقُلْ أعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ) na kupaka mwilini mwake kwa sehemu anayoweza akianza kichwani mwake na uso wake na kuendelea kwenye sehemu yake ya mbele. Alikuwa akifanya hivyo mara tatu." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن البراءِ بنِ عازبٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا أَتَيتَ مَضْجعَكَ فَتَوَضَّأْ وَضُوءكَ لِلصَّلاَةِ ، ثُمَّ اضْطَجِعْ عَلَى شِقِّكَ الأيْمَن ، وَقُلْ : اللَّهُمَّ أَسْلَمْتُ نَفْسِي إِلَيْكَ، وَوَجَّهْتُ وَجْهِي إِلَيْكَ، وَفَوضْتُ أَمْرِي إليكَ ، وأَلْجَأتُ ظَهرِي إلَيْكَ ، رَغْبَةً وَرهْبَةً إليكَ ، لا مَلْجَأَ وَلاَ مَنْجَا مِنْكَ إِلاَّ إليكَ ، آمَنْتُ بِكِتابِكَ الَّذِي أنْزَلْتَ، وَبِنَبِيِّكَ الَّذِي أرْسَلْتَ، فإنْ مِتَّ مِتَّ عَلَى الفِطْرَةِ ، وَاجْعَلْهُنَّ آخِرَ مَا تَقُولُ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Al-Baraa' bin 'Azib (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Unapoenda kulala (kwanza) tawadha wudhu wako wa Swalaah, kisha lala kwa ubavu wa kuliyani, kisha sema: Allaahumma inniy aslamtu wajhi Ilayka. Wa Fawwadhtu amriy Ilayka wa alja'tu dhahriy Ilayka raghbatan wa rahbatan Ilayka. Laa maljaa walaa manjaa Minka illaa Ilayka. Aamantu Bikitaabikal ladhiy anzalta wa Binabiyyikal ladhiy arsalta (Ee Rabb Wangu! Hakika nimeukabidhi uso wangu Kwako. Na jambo langu nimeliegemeza Kwako. Na mgongo wangu nimeugeuza Kwako. Hali ya kupenda na kuhofu Kwako. Hakuna pa kukimbilia wala pa kusalimika na Wewe isipokuwa Kwako. Nimekiamini Kitabu Chako ambacho Umekiteremsha, na Nabiy Wako ambaye Umemtuma). Kama utakufa usiku wako huo, basi utakufa katika fitra (Uislamu). Na hayo uyafanye ndiyo mwisho wa maneno yako." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 6
وعن أنس رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا أَوَى إِلَى فِرَاشِهِ قَالَ : (( الحَمْدُ للهِ الَّذِي أَطْعَمَنَا وَسَقَانَا ، وكفَانَا وآوانَا ، فَكَمْ مِمَّنْ لا كَافِيَ لَهُ وَلاَ مُؤْوِيَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapolala godoroni mwake, akisema: "AlhamdulliLLaahi Ladhiy atw'amanaa wa saqaanaa wa kafaanaa wa aaawaanaa fakam mimman laa kaafiya lahu walaa mu'wiya (Sifa zote njema anastahiki Allaah ambaye Ametulisha na Kutunywesha na Kututosheleza na kutupatia hifadhi (makazi), kwani wapo wangapi wasiokuwa na vya kuwatosheleza wala makao)." [Muslim]
Hadiyth – 7
وعن حذيفة رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا أَرَادَ أَنْ يَرْقُدَ ، وَضَعَ يَدَهُ اليُمْنَى تَحْتَ خَدِّهِ، ثُمَّ يَقُولُ : (( اللَّهُمَّ قِني عَذَابَكَ يَوْمَ تَبْعَثُ عِبَادَكَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
ورواه أَبُو داود ؛ من رواية حَفْصَةَ رَضِيَ اللهُ عنها ، وفيهِ أنه كَانَ يقوله ثلاث مراتٍ .
Imepokewa kutoka kwa Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapotaka kulala huweka mkono wake wa kuume chini ya shavu lake, kisha akisema: "Allaahumma Qiniy 'Adhaabaka yawma tab'athu 'Ibaadaka (Ee Rabb Wangu! niepushe na adhabu Yako siku Utakayo wafufua waja Wako)." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Na imepokewa na Abu Daawuwd kutoka kwa Hafswah (Radhwiya Allaahu 'anhaa), amesema: "Alikuwa akirudia mara tatu."
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/280
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10329&title=15-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Kitabu%20Cha%20Adhkaar%20%28Nyiradi%29%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D8%A3%D8%B0%D9%92%D9%83%D8%A7%D8%B1
[4] http://www.alhidaaya.com/
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11245&title=01-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Dhikri%20na%20Kuhimizwa%20Juu%20Yake
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11246&title=02-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kumdhukuru%20Allaah%20Ta%27aalaa%20kwa%20Kusimama%2C%20Kukaa%2C%20Kujilaza%20na%20katika%20Hadathi%2C%20Janaba%2C%20Hedhi%20Isipokuwa%20Kusoma%20Qur-aan%20Ambayo%20Haifai%20Kusomwa%20kwa%20Mwenye%20Janaba%20na%20Hedhi
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11247&title=03-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Anachosema%20Wakati%20wa%20Kulala%20na%20Kuamka
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11248&title=04-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20ya%20Vikundi%20vya%20Dhikri%20na%20Kupendeza%20Kujilazimisha%20Nayo%20na%20Kukatazwa%20Kujiondosha%20Bila%20ya%20Udhuru
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11249&title=05-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kumtaja%20Allaah%20Asubuhi%20na%20Jioni
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11251&title=06-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Anachosema%20Wakati%20wa%20Kulala