(Mabustani Ya Swalihina)
كِتابُ الأُمور الْمُنْهى عَنْها
17-Kitabu Cha Mambo Yaliyokatazwa
Alhidaaya.com [2]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الغيبة والأمر بحفظ اللسان
001-Mlango Wa Kuharamishwa Kusengenya na Amri ya Kuhifadhi Ulimi
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا ۚ أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ﴿١٢﴾
Na wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi. Je, anapenda mmoja wenu kwamba ale nyama ya nduguye aliyekufa? Basi mmelichukia hilo! Na mcheni Allaah! Hakika Allaah Ni Mwingi wa Kupokea Tawbah, Mwenye Kurehemu. [Al-Hujuraat: 12]
وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولَـٰئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْئُولًا ﴿٣٦﴾
Na wala usifuate usiyo na elimu nayo. Hakika masikio na macho na moyo; vyote hivyo vitaulizwa. [Al-Israa: 36]
مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾
Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf: 18]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاللهِ وَاليَوْمِ الآخِرِ فَلْيَقُلْ خَيْراً أَوْ لِيَصْمُتْ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho na aseme jambo zuri au anyamaze." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي موسى رضي اللهُ عنه قَالَ : قُلْتُ : يَا رسولَ اللهِ أَيُّ المُسْلمِينَ أفْضَلُ ؟ قَالَ : (( مَنْ سَلِمَ المُسْلِمُونَ مِنْ لِسَانِهِ وَيَدِهِ )) متفق عَلَيْهِ .
Amesema Abu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilisema: "Ee Rasuli wa Allaah! ni Waislamu gani walio bora?" Akasema: "Muislamu ni yule ambaye Waislamu wenzake wamesalimika kutokana na shari za ulimi na mikono yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن سهل بن سعد رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ يَضْمَنْ لِي مَا بَيْنَ لَحْيَيْهِ وَمَا بَيْنَ رِجْلَيْهِ أَضْمَنْ لَهُ الجَنَّةَ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake Sahl bin Sa'ad (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kunidhaminia (kulinda) kilichoko baina ya taya zake (yaani ulimi) na kile kilicho baina ya miguu yake (utupu wake), basi nitamdhaminia Peponi." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّه سمع النبيَّ صلى الله عليه وسلم يقول : (( إنَّ العَبْدَ لَيَتَكَلَّمُ بالكَلِمَةِ مَا يَتَبَيَّنُ فِيهَا يَزِلُّ بِهَا إِلَى النَّارِ أبْعَدَ مِمَّا بَيْنَ المَشْرِقِ والمَغْرِبِ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika mja huendelea kuzungumza maneno ambayo ni ya kutaka kheri na kuyatafakari, basi anaepushwa na Moto kwa umbali ulio baina ya mashariki na magharibi." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 5
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إنَّ العَبْدَ لَيَتَكَلَّمُ بِالكَلِمَةِ مِنْ رِضْوَانِ الله تَعَالَى مَا يُلْقِي لَهَا بَالاً يَرْفَعُهُ اللهُ بِهَا دَرَجاتٍ ، وإنَّ العَبْدَ لَيَتَكَلَّمُ بِالكَلَمَةِ مِنْ سَخَطِ اللهِ تَعَالَى لا يُلْقِي لَهَا بَالاً يَهْوِي بِهَا في جَهَنَّمَ )) . رواه البخاري .
Amesimulia Abuu Hurayrah (رضي الله عنه): Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: "Hakika mja huzungumza maneno yenye kumridhisha Allaah (سبحانه وتعالى) bila kuyapa umuhimu wowote, na Allaah Akamnyanyulia kwayo daraja nyingi Na hakika mja huzungumza maneno yenye kumkasirisha Allaah (سبحانه وتعالى) bila kuyapa umuhimu wowote, yakaja kumporomosha ndani ya Jahannam.” [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 6
وعن أَبي عبد الرحمن بِلالِ بن الحارِثِ المُزَنِيِّ رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : ((إنَّ الرَّجُلَ لَيَتَكَلَّمُ بِالكَلِمَةِ مِنْ رِضْوَانِ اللهِ تَعَالَى مَا كَانَ يَظُنُّ أنْ تَبْلُغَ مَا بَلَغَتْ يَكْتُبُ اللهُ لَهُ بِهَا رِضْوَانَهُ إِلَى يَومِ يَلْقَاهُ ، وإنَّ الرَّجُلَ لَيَتَكَلَّمُ بِالكَلِمَةِ مِنْ سَخَطِ اللهِ مَا كَانَ يَظُنُّ أنْ تَبْلُغَ مَا بَلَغَتْ يَكْتُبُ الله لَهُ بِهَا سَخَطَهُ إِلَى يَوْمِ يَلْقَاهُ )). رواه مالك في المُوَطَّأ ، والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Abuu 'Abdir-Rahmaan Bilaal bin Al-Haarith Al-Muzniy (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Kwa hakika mja atazungumza neno linalomridhisha Allaah, wala asidhani kuwa litafikia lilipofikia, Allaah Amuandikie kwa neno hilo Radhi Zake hadi Siku ya Qiyaamah. Na Kwa hakika mja atazungumza neno linalomkasirisha Allaah, wala asidhani kuwa litafikia lilipofikia, Allaah Amuandikie kwa neno hilo hasira Zake hadi Siku ya Qiyaamah)) [Maalik katika Muwattwa na At-Tirmidhiy ambaye amesema Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 7
وعن سفيان بن عبد الله رضي اللهُ عنه قَالَ : قُلْتُ : يَا رسولَ الله حدِّثني بأَمْرٍ أَعْتَصِمُ بِهِ قَالَ : (( قلْ : رَبِّيَ اللهُ ثُمَّ اسْتَقِمْ )) قُلْتُ : يَا رسولَ اللهِ ، مَا أخْوَفُ مَا تَخَافُ عَلَيَّ ؟ فَأَخَذَ بِلِسانِ نَفْسِهِ ، ثُمَّ قَالَ : (( هَذَا )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Amesema Sufyaan bin 'Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Niambie mimi jambo ambalo nitashikana nalo imara." Akasema: "Sema: Rabb Wangu ni Allaah, kisha kuwa na msimamo." Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Ni kitu gani ambacho unanihofia sana?" Akashika ulimi wake, kisha akasema: "Huu." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 8
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لا تُكْثِرُوا الكَلاَمَ بِغَيْرِ ذِكْرِ اللهِ؛ فَإنَّ كَثْرَةَ الكَلاَمِ بِغَيْرِ ذِكْرِ اللهِ تَعَالَى قَسْوَةٌ لِلقَلْبِ ! وإنَّ أبْعَدَ النَّاسِ مِنَ اللهِ القَلْبُ القَاسِي )) . رواه الترمذي .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usizungumze sana bila kumdhukuru Allaah, kwani maneno mengi bila ya kumtaja Allaah Ta'aalaa yanaufanya moyo uwe mgumu. Na hakika mtu aliye mbali zaidi na Allaah ni yule mwenye moyo ngumu." [At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 9
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ وَقَاهُ اللهُ شَرَّ مَا بَيْنَ لَحْيَيْهِ ، وَشَرَّ مَا بَيْنَ رِجْلَيْهِ دَخَلَ الجَنَّةَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuokolewa na Allaah na ouvu wa kilicho baina ya taya zake mbili (ulimi) na ubaya wa kilichoko baina ya miguu yake (utupu), ataingia Peponi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 10
وعن عقبة بن عامرٍ رضي اللهُ عنه قَالَ : قُلْتُ : يَا رسولَ اللهِ مَا النَّجَاةُ ؟ قَالَ : (( أَمْسِكْ عَلَيْكَ لِسَانَكَ ، وَلْيَسَعْكَ بَيْتُكَ ، وابْكِ عَلَى خَطِيئَتِكَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Amesema 'Uqbah bin 'Aamir (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Ni nini kuokoka (kufuzu)?" Akasema: "Uzuilie ulimi wako, na kaa ndani ya nyumba yako na ulie kwa madhambi yako uliyo yafanya." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 11
وعن أَبي سعيد الخدري رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إِذَا أصْبَحَ ابْنُ آدَمَ ، فَإنَّ الأعْضَاءَ كُلَّهَا تَكْفُرُ اللِّسانَ ، تَقُولُ : اتَّقِ اللهَ فِينَا ، فَإنَّما نَحنُ بِكَ ؛ فَإنِ اسْتَقَمْتَ اسْتَقَمْنَا ، وإنِ اعْوَجَجْتَ اعْوَجَجْنَا )) . رواه الترمذي .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapoamka mwanadamu asubuhi viungo vyake vyote vinauomba ulimi vikisema: 'Mche Allaah kwa ajili yetu, kwani sisi tunakufuata wewe, ukinyooka na kusimama wima nasi pia tutasimama wima na ukienda kombo, nasi pia tutakwenda kombo." [At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 12
وعن مُعَاذٍ رضي اللهُ عنه قَالَ : قُلْتُ : يَا رَسُولَ اللهِ ، أَخْبِرْني بِعَمَلٍ يُدْخِلُني الجَنَّةَ وَيُبَاعِدُني مِنَ النَّارِ ؟ قَالَ : (( لَقَدْ سَألتَ عَنْ عَظيمٍ ، وإنَّهُ لَيَسيرٌ عَلَى مَنْ يَسَّرَهُ اللهُ تَعَالَى عَلَيْهِ: تَعْبُدُ الله لا تُشْرِكُ بِهِ شَيْئاً ، وَتُقِيمُ الصَّلاَةَ ، وتُؤتِي الزَّكَاةَ ، وتَصُومُ رَمَضَانَ ، وتَحُجُّ البَيْتَ )) ثُمَّ قَالَ : (( ألاَ أدُلُّكَ عَلَى أبْوابِ الخَيْرِ ؟ الصَّوْمُ جُنَّةٌ ، وَالصَّدَقَةُ تُطْفِئُ الخَطِيئَةَ كَما يُطْفِئُ المَاءُ النَّارَ ، وَصَلاَةُ الرَّجُلِ مِنْ جَوْفِ اللَّيْلِ )) ثُمَّ تَلا : [ تَتَجَافَى جُنُوبُهُمْ عَنِ المَضَاجِعِ ] حَتَّى بَلَغَ [ يَعْمَلُونَ ] ثُمَّ قَالَ : (( ألا أُخْبِرُكَ بِرَأسِ الأَمْرِ ، وَعَمُودِهِ ، وَذِرْوَةِ سِنَامِهِ )) قُلْتُ : بَلَى يَا رسولَ اللهِ ، قَالَ : (( رَأسُ الأمْر الإسْلامُ ، وَعَمُودُهُ الصَّلاَةُ ، وَذِرْوَةِ سِنَامِهِ الجِهادُ )) ثُمَّ قَالَ : (( ألاَ أُخْبِرُكَ بِمِلاكِ ذَلِكَ كُلِّهِ ! )) قُلْتُ : بلَى يَا رَسولَ اللهِ ، فَأخَذَ بِلِسانِهِ وقال : (( كُفَّ عَلَيْكَ هَذَا )) قُلْتُ : يَا رسولَ الله وإنَّا لَمُؤاخَذُونَ بما نَتَكَلَّمُ بِهِ ؟ فقالَ : (( ثَكِلَتْكَ أُمُّكَ ! وَهَلْ يَكُبُّ الناسَ فِي النَّارِ عَلَى وُجُوهِهِمْ إِلاَّ حَصَائِدُ أَلْسِنَتِهِمْ ؟ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح ))
Imepokewa kutoka kwake Mu'aadh bin Jabal (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Nilisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Nipe habari ya amali itakayonitia mimi Peponi, na kuniepusha na moto." Akasema: "Umeuliza jambo kubwa, nalo ni sahali kwa aliyemsahilishia Allaah Ta'aalaa: Ni kumuabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, na kusimamisha Swalaah, na kutoa Zakaah, na kufunga Ramadhwaan, na kwenda kuhiji katika nyumba (yaani Ak-Ka'abah)." Kisha akasema: "Nikujulishe wewe milango ya kheri? Saumu ni kinga, na swadaqah hufuta madhambi kama maji yanavyozima moto; pia Swalaah ya mtu katikati ya usiku." Kisha akasoma: "Mbavu zao zinatengana na vitanda"...Hadi akafikia: "Wakiyatenda" [As-Sajdah: 16-17]. Kisha akasema: "Je, nikujulishe kichwa cha jambo, na nguzo zake na kilele chake?" Nikamwambia: "Kwa nini ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Kichwa cha jambo hili ni Uislamu, na nguzo yake ni Swalaah, na kilele cha juu kabisa ni Jihadi." Kisha akasema: "Nikupe habari ya kutamalaki yote hayo?" Nikamwambia: "Kwa nini ee Rasuli wa Allaah, kwani sisi tutapatilizwa kwa tuyasemayo?" Akasema: "Uwe ni mwenye kukoswa na mamako ee Mu'aadh! Jua, kuwa watu watatoswa motoni kwa nyuso zao isipokuwa ni kwa mavuno ya ndimi zao!" [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 13
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أَتَدْرُونَ مَا الْغِيبَةُ ؟ )) قالوا : اللهُ وَرَسُولُهُ أعْلَمُ ، قَالَ : (( ذِكْرُكَ أخَاكَ بِما يَكْرَهُ )) قِيلَ : أفَرَأيْتَ إنْ كَانَ في أخِي مَا أقُولُ ؟ قَالَ : (( إنْ كَانَ فِيهِ مَا تَقُولُ ، فقد اغْتَبْتَهُ ، وإنْ لَمْ يَكُنْ فِيهِ مَا تَقُولُ فَقَدْ بَهَتَّهُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliuliza: "Je, munajua maana ya Ghiybah (useng'enyaji)?" Wakasema: "Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi." Akasema: "Ni kumtaja (kuzungumza) ndugu yako kwa anayo chukia." Pakasemwa: "Unaonaje ikiwa ndugu yangu anayo ninayosema?" Akasema: "Ikiwa analo unalosema, basi hakika umemseng'enya na ikiwa hana unalosema itakuwa umemkashifu." [Muslim]
Hadiyth – 14
وعن أَبي بَكْرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ في خُطْبَتِهِ يَوْمَ النَّحْرِ بِمِنًى في حَجَّةِ الوَدَاعِ : (( إنَّ دِماءكُمْ ، وَأمْوَالَكُمْ ، وأعْرَاضَكُمْ ، حَرَامٌ عَلَيْكُمْ كَحُرْمَةِ يَوْمِكُمْ هَذَا، في شَهْرِكُمْ هَذَا، في بَلَدِكُمْ هَذَا، ألا هَلْ بَلَّغْتُ )) متفق عَلَيْهِ.
Imepokewa kutoka kwake Abu Bakrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema katika Khutbah yake siku ya kuchinja hapo Minaa katika Hijjah ya Kuaga: "Hakika damu zenu, mali zenu na heshima zenu ni tukufu (hivyo ni haramu juu yenu) kama utukufu wa siku yenu ya leo, katika mwezi wenu huu, katika mji wenu huu Ehee je sikufikisha." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 15
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : قُلْتُ للنبيّ صلى الله عليه وسلم : حَسْبُكَ مِنْ صَفِيَّةَ كذَا وكَذَا . قَالَ بعضُ الرواةِ : تَعْنِي قَصيرَةً ، فقالَ : (( لَقَدْ قُلْتِ كَلِمَةً لَوْ مُزِجَتْ بِمَاءِ البَحْرِ لَمَزَجَتْهُ ! )) قالت : وَحَكَيْتُ لَهُ إنْسَاناً فَقَالَ : (( مَا أُحِبُّ أنِّي حَكَيْتُ إنْساناً وإنَّ لِي كَذَا وَكَذَا )) . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nilimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Inatosha kwako kujua ya kwamba Swafiyyah ni kadha na kadha." Wamesema baadhi ya wapokezi: "Akimaanisha kuwa ni mfupi." Akasema: "Hakika umesema neno lau lingetiwa katika bahari, lingebadilisha tamu au harufu ya maji hayo." Akasema (Radhwiya Allaahu 'anhaa): "Nilimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakati mmoja mambo yasiyo mazuri kuhusu mtu." Akasema: "Sipendi kabisa kusikia jambo lolote lisilokuwa zuri kuhusu mtu yoyote, hata kama nitapatiwa kitu kadha na kadha." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 16
وعن أنسٍ رَضِيَ اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لَمَّا عُرِجَ بي مَرَرْتُ بِقَومٍ لَهُمْ أظْفَارٌ مِنْ نُحَاسٍ يَخْمِشُونَ وُجُوهَهُمْ وَصُدُورَهُمْ فَقُلْتُ : مَنْ هؤُلاءِ يَا جِبرِيلُ ؟ قَالَ : هؤُلاءِ الَّذِينَ يَأكُلُونَ لُحُومَ النَّاسِ ، وَيَقَعُونَ في أعْرَاضِهِمْ ! )) . رواه أَبُو داود .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nilipopandishwa mbinguni (katika usiku wa Miraji) nilipita kwa kaumu waliokuwa na makucha ya shaba waliyokuwa wakikwaruza nyuso zao na vifua vyao." Nikauliza: "Hawa ni kina nani, ee Jibriyl?" Akasema: "Hawa ni wale ambao kwamba walikuwa wakila nyama za watu na kuwatweza (kuwataharisha)." [Abuu Daawuwd]
Hadiyth – 17
وعن أَبي هريرة رَضِيَ اللهُ عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( كُلُّ المُسْلِمِ عَلَى المُسْلِمِ حَرَامٌ : دَمُهُ وَعِرْضُهُ وَمَالُهُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kila Muislamu ni haramu kwa Muislamu mwenzake: Damu yake, cheo chake, na mali yake." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم سماع الغيبة
وأمر من سمع غيبةً مُحرَّمةً بِرَدِّها والإنكارِ عَلَى قائلها
فإنْ عجز أَوْ لَمْ يقبل منه فارق ذلك المجلس إن أمكنه
002-Mlango Wa Uharamu wa Kusikiliza Kusengenya na Amri kwa Mwenye Kusikia Kumkataza Msemaji na Akishindwa au Asipokubali Kutoka Kwake Basi Aondoke Kwenye kikao
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَإِذَا سَمِعُوا اللَّغْوَ أَعْرَضُوا عَنْهُ ﴿٥٥﴾
Na wanaposikia maneno ya upuuzi hujitenga nayo [Al-Qaswasw: 55]
وَالَّذِينَ هُمْ عَنِ اللَّغْوِ مُعْرِضُونَ ﴿٣﴾
Na ambao wanajiepusha na mambo ya upuuzi. [Al-Muuminuwn: 3]
وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولَـٰئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْئُولًا ﴿٣٦﴾
Na wala usifuate usiyo na elimu nayo. Hakika masikio na macho na moyo; vyote hivyo vitaulizwa. [Al-Israa: 36]
وَإِذَا رَأَيْتَ الَّذِينَ يَخُوضُونَ فِي آيَاتِنَا فَأَعْرِضْ عَنْهُمْ حَتَّىٰ يَخُوضُوا فِي حَدِيثٍ غَيْرِهِ ۚ وَإِمَّا يُنسِيَنَّكَ الشَّيْطَانُ فَلَا تَقْعُدْ بَعْدَ الذِّكْرَىٰ مَعَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿٦٨﴾
Na unapowaona wale wanaoshughulika kuzisakama Aayaat Zetu, jitenge nao mpaka watumbukie kwenye mazungumzo mengineyo. Na kama shaytwaan akikusahaulisha, basi baada ya kukumbuka, usikae pamoja na watu madhalimu. [Al-An'aam: 68]
Hadiyth – 1
وعن أَبي الدرداء رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( مَنْ رَدَّ عَنْ عِرْضِ أخيهِ ، رَدَّ اللهُ عَنْ وَجْهِهِ النَّارَ يَومَ القيَامَةِ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwake Abu Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kurudisha cheo na heshima ya nduguye, Allaah Atauepusha uso wake na moto Siku ya Qiyaamah." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 2
وعن عِتبَانَ بنِ مَالكٍ رضي اللهُ عنه ، في حديثه الطويل المشهور الَّذِي تقدَّمَ في بابِ الرَّجاء قَالَ : قام النبيّ صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي فَقَالَ : (( أيْنَ مالِكُ بنُ الدُّخْشُمِ ؟ )) فَقَالَ رَجُلٌ : ذَلِكَ مُنَافِقٌ لا يُحِبُّ اللهَ ولا رَسُولهُ ، فَقَالَ النبيّ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَقُلْ ذَلِكَ ألاَ تَراهُ قَدْ قَالَ : لا إلهَ إِلاَّ اللهُ يُريدُ بِذَلكَ وَجْهَ اللهِ ! وإنَّ الله قَدْ حَرَّمَ عَلَى النَّارِ مَنْ قَالَ : لا إلهَ إِلاَّ اللهُ يَبْتَغي بِذَلِكَ وَجْهَ اللهِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Amesema 'Itbaan bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) katika Hadiyth ndefu mashuhuri ambayo imetangulia kutajwa katika mlango "Kuwa na Matumaini" kwamba: "Alisimama Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuswali akasema: "Yu wapi Maalik bin Ad-Dukhshum?" Akasema mtu mmoja: "Yule ni mnafiki ambaye hampendi Allaah wala Rasuli Wake." Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Usiseme hivyo, je huoni kuwa amesema Laa ilaaha Illa Allaah akitaka ridhaa za Allaah. Hakika Allaah amemharamishia moto yeyote anayesema Laa ilaaha Illa Allaah akitafuta ridhaa ya Allaah kwa hilo." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن كعب بن مالك رضي اللهُ عنه في حديثه الطويل في قصةِ تَوْبَتِهِ وَقَدْ سبق في باب التَّوبةِ. قَالَ : قَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم وَهُوَ جالِسٌ في القَومِ بِتَبُوكَ : (( مَا فَعَلَ كَعبُ بن مالكٍ ؟ )) فَقَالَ رَجلٌ مِنْ بَنِي سَلمَةَ: يَا رسولَ الله ، حَبَسَهُ بُرْدَاهُ والنَّظَرُ في عِطْفَيْهِ . فَقَالَ لَهُ مُعاذُ بنُ جبلٍ رضي اللهُ عنه : بِئْسَ مَا قُلْتَ ، والله يَا رسولَ الله مَا علمنا عَلَيْهِ إِلاَّ خَيْراً ، فَسَكَتَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم . متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema Ka'ab bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) katika Hadiyth ndefu kuhusu kusamehewa kwake na tayari Hadiyth hii imetangulia kuelezwa katika mlango wa "Tawbah": Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliuliza alipokuwa amekaa na kaumu huko Tabuwk: "Ka'ab amefanya nini?" Akasema mtu mmoja kutoka kwa Bani Salamah: "Ee Rasuli wa Allaah! Amezuiliwa na burga zake kwa mbili (nguo) na kuangalia mabega yake kwa kibri." Mu'aadh bin Jabal (Radhwiya Allaahu 'anhu) akamwambia: "Ni jambo baya ulilosema! Naapa kwa Allaah, ee Rasuli wa Allaah! Hatujui chochote kwake isipokuwa kheri." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alinyamaza." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يباح من الغيبة
003-Mlango Wa Yanayoruhusiwa katika Kusengenya
Alhidaaya.com [4]
Jua ya kwamba kuseng'enya kunakubalika kwa lengo sahihi linalo kubaliwa na sheria ambalo haliwezi kufikiwa ila kwa kufanya hivyo. Nazo ni sababu Sita:
1) Kudhulumiwa: Inafaa kwa aliyedhulumiwa kupeleka mashtaka yake kwa Sultani, Kadhi na watu wengineo wenye mamlaka au uwezo wa kumrudishia haki yake kutoka kwa dhalimu kwa kusema: "Fulani amenidhulumu kwa kitu kadha."
2) Kutaka usaidizi katika kubadilisha Munkar na kumrudisha aliye asi katika njia ya sawa, kwa kusema: "Na aseme kumwambia yule ambae anatarajiwa uwezo wake katika kuondoa Munkar fulani anafanya kadha, hivyo mzuilie na mfano wake huo." Na makusudio yake yanakuwa ni kufikia katika kuondosha Munkar, na ikiwa hatakuwa na lengo hilo basi itakuwa ni haramu.
3) Kutaka Fatwa: Hivyo kumwambia mufti: "Babangu au ndugu yangu au mume wangu au fulani amenidhulumu kwa kitu kadha. Je, ana haki nacho hicho? Na njia gani nitatumia kumalizana naye na kupata haki yangu na kuondosha dhulma? Na mfano wa hayo. Jambo hili linakubaliwa kwa haja. Lakini iliyo bora zaidi ni kusema: "Unasemaje kuhusu mtu, ambaye ana jambo fulani? Katika kufanya hivyo atapata lengo lake bila ya kumtaja yule mtu mwenyewe. Pamoja na hivyo, kutaja jina la mtu inakubaliwa kama tutakavyo taja mfano wa Hind in shaa Allaah Ta'aalaa.
4) Kuwatahadharisha Waislamu na shari na kuwanasihi, na hilo ni kwa njia zifuatazo:
i) Miongoni mwayo ni kuwakosoa wapokezi na mashahidi (wa Hadiyth za Nabiy Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na hilo ni jaizi kwa kukubaliwa na waaislamu wote. Bali jambo hilo ni wajibu kwa haja.
ii) Kutaka ushauri katika kutaka mahusiano ya kindoa na mwanadamu au kushirikiana naye au kuweka amana kwake au kuamiliana naye au mengineyo mbali na hayo au kutaka kuwa jirani yake. Na inapasa kwa mwenye kutoa ushauri asifiche hali yake bali ataje ubaya wake ikiwa upo ambao anao kwa njia ya nasiha.
iii) Anapomuona Fakihi anaingia katika Bid'ah (uzushi) au fasili ambaye anafundisha elimu na akahofu huenda akadhurika yule Fakihi kwa kufanya hivyo. Inatakiwa apatiwe nasaha ya kubainisha hali yake kwa sharti awe na nia nzuri. Na hili ni jambo ambalo hukosewa. Na hakika huenda mzungumzaji akabeba katika hilo chuki na hivyo shetani humvalisha yeye hilo. Na kumpatia yeye matumaini kuwa amemnasihi, hivyo kupata ufahamu juu ya jambo hilo.
iv) Kuwa na mlezi ambaye hatekelezi wajibu wake inavyotakiwa: Hii ni kutokana kuwa si mtu mwema kwake na ima ni fasiki au ameghafilika na wajibu wake na mfano wa hayo. Ni wajibu kukumbushwa hilo kwa yule mwenye jukumu la ulezi kwa ujumla kujivua na kazi hiyo na kumpatia mtu mwengine ambaye anafaa au kuambiwa aamiliane naye kwa ile hali aliyo nayo wala asimpoteze. Na afanye juhudi katika kumuhimiza juu ya kusimama imara (Istiqaamah) au kumbadilisha.
5) Kufanya ufasiki na ufisadi kwa dhahiri au kuzua kama mfano wa anaye kunywa pombe wazi wazi na kuwaonea watu na kuchukua ushuru na mkusanyaji wa mali kwa dhulma na kutawala katika mambo kwa batili. Hivyo, inafaa kumtaja kwa anayo yadhihirisha na ni haramu kumtaja kwa aibu asiyokuwa nayo isipokuwa kufaa kwake kuwe ni kwa sababu nyengine katika yale tuliyoyataja.
6) Kumtambua na kumtambulisha: Ikiwa mtu tayari anajulikana kwa lakabu kama ya kilema, au kiziwi, au kipofu, au kengeza na mengineyo. Kwa hayo inajuzu, lakini haifai (na ni haramu) kutumia jina hilo kumtweza na kumdhalilisha. Na lau inawezekana kumtambulisha kwa yasiyokuwa hayo basi itakuwa bora zaidi.
Hizi sababu sita, wamezitaja wanazuoni na nyingi kati ya hizo wamekubaliyana kwazo. Na dalili ya nukta hizi ni Hadiyth nyingi Swahiyh na mashuhuri. Na miongoni mwazo ni:
Hadiyth – 1
عن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ رجلاً اسْتَأذَنَ عَلَى النبيّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : (( ائْذَنُوا لَهُ ، بِئسَ أخُو العَشِيرَةِ ؟ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba mtu mmoja alitaka idhini kumuona Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naye alisema: "Mpatieni idhini aingie; ni mtu mbaya katika kabila lake." [Al-Bukhaariy na Muslim] Al-Bukhaariy ameitolea hoja katika kuruhusu kuwasengenya mafisadi na waenezaji fitina.
Hadiyth – 2
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَا أظُنُّ فُلاناً وفُلاناً يَعْرِفانِ مِنْ دِينِنَا شَيْئاً )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Sidhanii kuwa fulani na fulani wanajua chochote katika Dini yetu." [Al-Bukhaariy]. Amesema Al-Layth bin Sa'ad, mmoja wa wapokezi wa Hadiyth hii: "Watu hawa wawili walikuwa ni wanafiki."
Hadiyth – 3
وعن فاطمة بنتِ قيسٍ رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : أتيت النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، فقلتُ : إنَّ أَبَا الجَهْم وَمُعَاوِيَةَ خَطَبَانِي ؟ فَقَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( أمَّا مُعَاوِيَةُ ، فَصُعْلُوكٌ لاَ مَالَ لَهُ ، وأمَّا أَبُو الجَهْمِ ، فَلاَ يَضَعُ العَصَا عَنْ عَاتِقِهِ )) متفق عَلَيْهِ .
وفي رواية لمسلم : (( وَأمَّا أَبُو الجَهْمِ فَضَرَّابٌ لِلنِّساءِ )) وَهُوَ تفسير لرواية : (( لا يَضَعُ العَصَا عَنْ عَاتِقِهِ )) وقيل : معناه : كثيرُ الأسفارِ .
Amesema Faatwimah bint Qays (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nilikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) nikamwambia: "Hakika Abul Jahm na Mu'awiyah wameniposa?" Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ama Mu'awiyah ni masikini na hana mali yoyote na ama Abul Jahm fimbo yake haitoki kwenye mabega yake." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Na katika riwaayah ya Muslim: "Na ama Abul Jahm ni mtu anaye piga wanawake sana." Na hii ni tafsiri ya riwaayah yenyewe: "Haachi fimbo begani mwake." Na inasemekana: "Maana yake ni anasafiri sana."
Hadiyth – 4
وعن زيد بن أرقم رَضِيَ اللهُ عنه قَالَ : خرجنا مَعَ رسُولِ الله صلى الله عليه وسلم في سَفَرٍ أصَابَ النَّاسَ فِيهِ شِدَّةٌ ، فَقَالَ عبدُ اللهِ بن أُبَيّ : لاَ تُنْفِقُوا عَلَى مَنْ عِندَ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم حَتَّى يَنْفَضُّوا ، وقال : لَئِنْ رَجَعْنَا إِلَى المَدِينَةِ لَيُخْرِجَنَّ الأَعَزُّ مِنْهَا الأَذَلَّ ، فَأَتَيْتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فَأخْبَرْتُهُ بذلِكَ ، فَأرْسَلَ إِلَى عبدِ الله بن أُبَيِّ ، فَاجْتَهَدَ يَمِينَهُ : مَا فَعلَ ، فقالوا : كَذَبَ زيدٌ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، فَوَقَعَ في نَفْسِي مِمَّا قَالُوهُ شِدَّةٌ حَتَّى أنْزلَ اللهُ تَعَالَى تَصْدِيقِي : [ إِذَا جَاءكَ المُنَافِقُونَ ] ثُمَّ دعاهُمُ النبيّ صلى الله عليه وسلم لِيَسْتَغْفِرَ لَهُمْ فَلَوَّوْا رُؤُوسَهُمْ . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Zayd bin Arqam (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Tulitoka pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika safari ambayo watu katika safari hiyo walipatwa na matatizo. 'Abdullaah bin Ubayy aliwaambia watu wake, walio kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) msiwape kitu mpaka wamuache. Na akasema: 'Kama tutarudi Madiynah, wenye nguvu watawatoa wanyonge humo'. Nikamwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza kuhusu suala hilo naye akaapa kuwa hakusema hayo. Wakasema: 'Zayd amemuogopea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)'. Walichokisema kikanipa matatizo nafsini mwangu mpaka Allaah Aliposhusha thibitisho la ukweli wangu katika, "Wanapokujia (ee Muhammad صلى الله عليه وسلم ) wanafiki." [Al-Munaafiquwn: 1]. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akawaita ili awaombee maghfira wakageuza vichwa vyao wakakataa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : قالت هِنْدُ امْرَأةُ أَبي سفْيَانَ للنَّبيِّ صلى الله عليه وسلم : إنَّ أَبَا سُفْيَانَ رَجُلٌ شَحِيحٌ وَلَيْسَ يُعْطِينِي مَا يَكْفيني وولَدِي إِلاَّ مَا أَخَذْتُ مِنْهُ، وَهُوَ لا يَعْلَمُ ؟ قَالَ : (( خُذِي مَا يَكْفِيكِ وَوَلدَكِ بِالمَعْرُوفِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Hind, mke wa Abu Sufyaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) alimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hakika Abu Sufyaan ni bakhili sana, hivyo hanipi hela zinazo nitosha mimi pamoja na mtoto wangu isipokuwa ninazochukua kwake bila ya yeye kujua?" Akasema: "Chukua hela zinazo kutosha wee na mtoto wako kwa wema." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم النميمة
وهي نقل الكلام بَيْنَ الناس عَلَى جهة الإفساد
004-Mlango Wa Kuharamishwa Umbeya, Nako ni Kueneza Maneno Baina ya Watu kwa Njia ya Kuleta Ufisadi
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ﴿١١﴾
Mwingi wa kukashifu, mpitaji huku na kule kwa kufitinisha. [Al-Qalam: 11]
مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾
Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf: 18]
Hadiyth – 1
وعن حُذَيْفَةَ رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لا يَدْخُلُ الجَنَّةَ نَمَّامٌ )).متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hataingia Peponi mmbeya (mwenezaji uvumi / msingiziaji) [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن ابن عباسٍ رضي الله عنهما : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم مرَّ بِقَبْرَيْنِ فَقَالَ : (( إنَّهُمَا يُعَذَّبَانِ ، وَمَا يُعَذَّبَانِ في كَبيرٍ ! بَلَى إنَّهُ كَبِيرٌ : أمَّا أَحَدُهُمَا ، فَكَانَ يَمْشِي بِالنَّمِيمَةِ ، وأمَّا الآخَرُ فَكَانَ لاَ يَسْتَتِرُ مِنْ بَوْلِهِ )) . متفق عَلَيْهِ . وهذا لفظ إحدى روايات البخاري .
Amesimulia Ibn 'Abbaas (رضي الله عنهما): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliyapitia makaburi mawili na akasema: “Hakika hawa wawili wanaadhibiwa, na wala hawaadhibiwi kwa sababu ya jambo kubwa (la kuwashinda kulitekeleza au kujiepusha nalo).” Kisha hapo hapo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ”Hapana! Bali ni kubwa (dhambi kubwa na adhabu zake)! Ama mmoja wao, huyu alikuwa akipita kufitinisha watu, na ama mwingine, huyu alikuwa hajikingi na mkojo wake [anapokojoa].” [Al-Bukhaariy na Muslim]" [Al-Bukhaariy na Muslim, na hili tamshi ni moja ya riwaayah za Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 3
وعن ابن مسعود رضي الله عنه : أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( أَلاَ أُنَبِّئُكُمْ مَا العَضْهُ ؟ هي النَّمَيمَةُ ؛ القَالَةُ بَيْنَ النَّاسِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Je, niwajulishe nyinyi 'Adhhu ni nini? Huo ni uongo na kuzungusha maneno baina ya watu." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن نقل الحديث وكلام الناس
إِلَى ولاة الأمور إِذَا لَمْ تَدْعُ إِلَيْهِ حاجة كخوف مفسدة ونحوه
005-Mlango Wa Kukatazwa Kuchukua Hadiyth, Maneno ya Watu na Kuyapeleka kwa Viongozi Ikiwa Hapana Haja Yoyote Kama Hofu ya Ufisadi na Mfano Wake
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ ۚ ﴿٢﴾
Na shirikianeni katika wema na taqwa, na wala msishirikiane katika dhambi na uadui. [Al-Maaidah: 2]
وعن ابن مسعودٍ رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لا يُبَلِّغُنِي أَحَدٌ مِنْ أصْحَابِي عَنْ أَحَدٍ شَيْئاً ، فإنِّي أُحِبُّ أنْ أخْرُجَ إِلَيْكُمْ وأنَا سَليمُ الصَّدْرِ )) . رواه أَبُو داود والترمذي .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: " Asinifikishie Swahaaba wangu yeyote jambo baya lolote kuhusu mtu mwengine, kwani mimi napenda kukutana nanyi kifua changu kikiwa safi kabisa (bila ya kuwa na kinyongo na yeyote)." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب ذمِّ ذِي الوَجْهَيْن
006-Mlango Wa Shutuma kwa Mwenye Nyuso Mbili
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
يَسْتَخْفُونَ مِنَ النَّاسِ وَلَا يَسْتَخْفُونَ مِنَ اللَّـهِ وَهُوَ مَعَهُمْ إِذْ يُبَيِّتُونَ مَا لَا يَرْضَىٰ مِنَ الْقَوْلِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ بِمَا يَعْمَلُونَ مُحِيطًا ﴿١٠٨﴾
Wanajificha watu wasiwaone (wakitenda machafu) na wala hawajifichi kwa Allaah (wakamwonea haya), Naye Yu pamoja nao (kwa Ujuzi Wake) pale wanapokesha kupanga makri kwa maneno Asiyoyaridhia. Na Allaah daima kwa yale wayatendayo, Ni Mwenye Kuyazunguka (kwa Ujuzi Wake). [An-Nisaa: 108]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( تَجِدُونَ النَّاسَ مَعادِنَ : خِيَارُهُم في الجَاهِلِيَّةِ خِيَارُهُمْ في الإسْلاَمِ إِذَا فَقُهُوا ، وتَجِدُونَ خِيَارَ النَّاسِ في هَذَا الشَّأنِ أَشَدَّهُمْ كَرَاهِيَةً لَهُ ، وَتَجِدُونَ شَرَّ النَّاسِ ذَا الوَجْهَينِ ، الَّذِي يَأتِي هؤُلاءِ بِوَجْهٍ ، وَهَؤُلاءِ بِوَجْهٍ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Utawapata watu wenye nasaba nzuri wakijifakhiri kwayo: Walio bora katika ujahiliyah (zama za ujinga), ndio wanakuwa bora katika Uislamu wanapo fahamu (na kujua hukumu za kisheria). Na utawakuta walio bora katika jambo hili (la idara na uongozi) ni wenye kulichukia mno. Na utawapata wabaya zaidi miongoni mwa watu ni wale wenye nyuso mbili (wanafiki), ambao wanakuja kwa hawa kwa uso mmoja na kwa hawa kwa uso mwengine." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن محمد بن زيدٍ : أنَّ ناساً قالوا لِجَدِّهِ عبدِ اللهِ بن عمر رضي الله عنهما : إنَّا نَدْخُلُ عَلَى سَلاَطِيننَا فَنَقُولُ لَهُمْ بِخِلاَفِ مَا نَتَكَلَّمُ إِذَا خَرَجْنَا مِنْ عِنْدِهِمْ . قَالَ : كُنَّا نَعُدُّ هَذَا نِفَاقاً عَلَى عَهْدِ رسُولِ الله صلى الله عليه وسلم . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Muhammad bin Zayd kuwa watu walikuja wakamwambia babu yake, 'Abdillaah bin 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): "Hakika sisi tunaingia kwa masultani wetu na kuwaambia wao kinyume na yale tunayozungumza tunapotoka kwao." Akasema: "Hakika sisi tulikuwa tukiona jambo hilo kuwa ni unafiki katika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الكذب
007-Mlango Wa Kuharamishwa Uongo
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ ﴿٣٦﴾
Na wala usifuate usiyo na elimu nayo. [Al-Israa: 36]
مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾
Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf: 18]
Hadiyth – 1
وعن ابن مسعود رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ الصِّدْقَ يَهْدِي إِلَى البِرِّ ، وإنَّ البِرَّ يَهْدِي إِلَى الجَنَّةِ ، وإنَّ الرَّجُلَ لَيَصْدُقُ حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اللهِ صِدِّيقاً . وإنَّ الكَذِبَ يَهْدِي إِلَى الفُجُورِ ، وإنَّ الفُجُورَ يَهْدِي إِلَى النَّارِ ، وإنَّ الرَّجُلَ لَيَكْذِبُ حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اللهِ كَذَّاباً )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika ukweli unamuongoza mtu katika wema na wema unampeleka mtu Peponi. Na hakika mtu huendelea kusema ukweli mpaka akaitwa mkweli mbele ya Allaah. Na hakika uwongo unampeleka mtu katika uchafu na uchafu unampeleka mtu Motoni. Na mtu huendelea kusema uwongo mpaka akaandikwa kuwa ni muongo mbele ya Allaah." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( أرْبَعٌ مَنْ كُنَّ فِيهِ ، كَانَ مُنَافِقاً خَالِصاً ، وَمَنْ كَانَتْ فِيهِ خَصْلَةٌ مِنْهُنَّ ، كَانَتْ فِيهِ خَصْلَةٌ مِنْ نِفاقٍ حَتَّى يَدَعَهَا : إِذَا أؤْتُمِنَ خانَ ، وَإِذَا حَدَّثَ كَذَبَ ، وَإِذَا عَاهَدَ غَدَرَ ، وَإِذَا خَاصَمَ فَجَرَ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu yeyote akiwa na mambo manne atakuwa mnafiki hasa, na ataekuwa na moja katika hayo manne atakuwa na sifa moja ya unafiki mpaka aliache: Kama akiaminiwa anaondoa uaminifu; na akizungumza anaongopa; na anapotoa ahadi hivunja; na anapogombana anaiacha haki na kuwa jeuri." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( مَنْ تَحَلَّمَ بِحُلْمٍ لَمْ يَرَهُ ، كُلِّفَ أنْ يَعْقِدَ بَيْنَ شَعِيرَتَيْن وَلَنْ يَفْعَلَ ، وَمَنِ اسْتَمَعَ إِلَى حَديثِ قَوْمٍ وَهُمْ لَهُ كَارِهُونَ ، صُبَّ في أُذُنَيْهِ الآنُكُ يَوْمَ القِيَامَةِ ، وَمَنْ صَوَّرَ صُورَةً عُذِّبَ وَكُلِّفَ أنْ يَنْفُخَ فِيهَا الرُّوحَ وَلَيْسَ بنافِخٍ )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kubuni ndoto mbaya ambayo hakuona, atalazimishwa Siku ya Qiyaamah kufunga fundo baina ya mbegu za shayiri na hataweza. Na mwenye kusikiliza mazungumzo ya watu na wao wanachukia hilo, atamiminiwa risasi iliyo yeyushwa masikioni mwake Siku ya Qiyaamah. Na mwenye kuchora picha ataadhibiwa na kukalifishwa kupuliza ndani yake uhai na hataweza kufanya hivyo." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 4
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( أَفْرَى الفِرَى أنْ يُرِيَ الرَّجُلُ عَيْنَيْهِ مَا لَمْ تَرَيَا )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwake Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Uongo ulio mkubwa zaidi ni kwa mtu kudai kuwa ameona kitu kwa macho yake ambacho hakukiona." [Al-Bukhaariy]. Na maana yake ni kusema: "Kuona kitu ambacho hukuona."
Hadiyth – 5
وعن سَمُرَةَ بنِ جُنْدُبٍ رضي الله عنه قَالَ : كَانَ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم مِمَّا يُكْثِرُ أنْ يَقُولَ لأَصْحَابِهِ : (( هَلْ رَأَى أَحَدٌ مِنْكُمْ مِنْ رُؤْيَا ؟ )) فَيَقُصُّ عَلَيْهِ مَنْ شَاءَ اللهُ أنْ يَقُصَّ، وإنَّهُ قَالَ لنا ذَات غَدَاةٍ : (( إنَّهُ أَتَانِيَ اللَّيْلَةَ آتِيَانِ ، وإنَّهُمَا قَالا لِي : انْطَلِقْ ، وإنِّي انْطَلَقتُ مَعَهُمَا ، وإنَّا أَتَيْنَا عَلَى رَجُلٍ مُضْطَجِعٍ ، وَإِذَا آخَرُ قائِمٌ عَلَيْهِ بِصَخْرَةٍ ، وَإِذَا هُوَ يَهْوِي بِالصَّخْرَةِ لِرَأْسِهِ ، فَيَثْلَغُ رَأسَهُ ، فَيَتَدَهْدَهُ الحَجَرُ هَا هُنَا ، فَيَتْبَعُ الحَجَرَ فَيَأخُذُهُ فَلاَ يَرْجِعُ إِلَيْهِ حَتَّى يَصِحَّ رَأسُهُ كَما كَانَ ، ثُمَّ يَعُودُ عَلَيْهِ ، فَيَفْعَلُ بِهِ مِثْلَ مَا فَعَلَ المَرَّةَ الأوْلَى ! )) قَالَ: (( قُلْتُ لهما : سُبْحانَ اللهِ ! مَا هَذَان ؟ قَالا لي : انْطَلِقِ انْطَلِقْ ، فَانْطَلَقْنَا ، فَأَتَيْنَا عَلَى رَجُلٍ مُسْتَلْقٍ لِقَفَاهُ ، وَإِذَا آخَرُ قَائِمٌ عَلَيْهِ بِكَلُّوبٍ مِنْ حَديدٍ ، وَإِذَا هُوَ يَأتِي أحَدَ شِقَّيْ وَجْهِهِ فَيُشَرْشِرُ شِدْقَهُ إِلَى قَفَاهُ ، ومِنْخَرَهُ إِلَى قَفَاهُ ، وعَيْنَهُ إِلَى قَفَاهُ ، ثُمَّ يَتَحَوَّلُ إِلَى الجانبِ الآخَرِ ، فَيَفْعَلُ بِهِ مِثْلَ مَا فَعَلَ بالجَانِبِ الأوَّلِ ، فَمَا يَفْرَغُ مِنْ ذَلِكَ الجانبِ حَتَّى يَصِحَّ ذَلِكَ الجانبُ كما كَانَ ، ثُمَّ يَعُودُ عَلَيْهِ فَيَفْعَلُ مِثْلَ مَا فَعَلَ فِي المرَّةِ الأُوْلَى )) قَالَ : (( قُلْتُ : سُبْحَانَ اللهِ ! مَا هذانِ ؟ قالا لي : انْطَلِقِ انْطَلِقْ ، فَانْطَلَقْنَا ، فَأَتَيْنَا عَلَى مِثْلِ التَّنُّورِ )) فَأَحْسِبُ أنَّهُ قَالَ : (( فإذا فِيهِ لَغَطٌ ، وأصْواتٌ ، فَاطَّلَعْنَا فِيهِ فإذا فِيهِ رِجَالٌ وَنِساءٌ عُرَاةٌ ، وَإِذَا هُمْ يَأتِيِهمْ لَهَبٌ مِنْ أسْفَلَ مِنْهُمْ ، فإذا أتاهُمْ ذَلِكَ اللَّهَبُ ضَوْضَوْا . قُلْتُ : مَا هَؤلاءِ ؟ قَالا لِي : انْطَلِقِ انْطَلِقْ ، فَانْطَلَقْنَا ، فَأَتَيْنَا عَلَى نَهْرٍ )) حَسِبْتُ أنَّهُ كَانَ يَقُولُ : (( أَحْمَرُ مِثْلُ الدَّمِ ، وَإِذَا في النَّهْرِ رَجُلٌ سابحٌ يَسْبَحُ ، وَإِذَا عَلَى شَطِّ النَّهْرِ رَجُلٌ قَدْ جَمَعَ عِنْدَهُ حِجَارَةً كثيرةً ، وَإِذَا ذَلِكَ السَّابحُ يَسْبَحُ ، مَا يَسْبَحُ ، ثُمَّ يَأتِي ذَلِكَ الَّذِي قَدْ جَمَعَ عِنْدَهُ الحِجَارَةَ ، فَيَفْغَرُ لَهُ فاهُ، فَيُلْقِمُهُ حَجَراً، فَينْطَلِقُ فَيَسْبَحُ ، ثُمَّ يَرْجِعُ إِلَيْهِ، كُلَّمَا رَجَعَ إِلَيْهِ ، فَغَرَ لَهُ فَاهُ ، فَألْقَمَهُ حَجَراً ، قُلْتُ لهُما : مَا هذانِ ؟ قالاَ لِي : انْطَلِقِ انْطَلِقْ ، فَانْطَلَقْنَا ، فَأَتَيْنَا عَلَى رَجُلٍ كَريهِ المرْآةِ ، أَوْ كَأكْرَهِ مَا أنتَ رَاءٍ رجُلاً مَرْأىً ، فإذا هُوَ عِنْدَهُ نَارٌ يَحُشُّهَا وَيَسْعَى حَوْلَهَا . قُلْتُ لَهُمَا : مَا هَذَا ؟ قالاَ لي : انْطَلِقِ انْطَلِقْ ، فَانْطَلَقْنَا ، فَأتَيْنَا عَلَى رَوْضَةٍ مُعْتَمَّةٍ فِيهَا مِنْ كُلِّ نَوْرِ الرَّبيعِ ، وَإِذَا بَيْنَ ظَهْرَي الرَّوْضَةِ رَجُلٌ طَويلٌ لا أَكادُ أَرَى رَأسَهُ طُولاً في السَّماءِ ، وَإِذَا حَوْلَ الرَّجُلِ مِنْ أَكْثَرِ وِلدانٍ رَأيْتُهُمْ قَطُّ ، قُلْتُ : مَا هَذَا ؟ وَمَا هؤلاءِ ؟ قالا لي : انْطَلقِ انْطَلقْ ، فَانْطَلَقْنَا ، فَأَتَيْنَا إِلَى دَوْحَةٍ عَظيمةٍ لَمْ أَرَ دَوْحَةً قَطُّ أعْظمَ مِنْهَا ، وَلاَ أحْسَنَ ! قالا لي : ارْقَ فِيهَا ، فارْتَقَيْنَا فِيهَا إِلَى مَدينَةٍ مَبْنِيَّةٍ بِلَبنٍ ذَهَبٍ وَلَبنٍ فِضَّةٍ ، فَأَتَيْنَا بَابَ المَدِينَةِ فَاسْتَفْتَحْنَا ، فَفُتِحَ لَنَا فَدَخَلْنَاها ، فَتَلَقَّانَا رِجالٌ شَطْرٌ مِنْ خَلْقِهِمْ كأَحْسَنِ مَا أنت راءٍ ! وَشَطْرٌ مِنْهُمْ كأقْبَحِ مَا أنتَ راءٍ ! قالا لَهُمْ : اذْهَبُوا فَقَعُوا في ذَلِكَ النَّهْرِ ، وَإِذَا هُوَ نَهْرٌ مُعْتَرِضٌ يَجْرِي كأنَّ ماءهُ المَحْضُ في البَيَاضِ ، فَذَهَبُوا فَوَقَعُوا فِيهِ . ثُمَّ رَجَعُوا إلَيْنَا قَدْ ذَهَبَ ذَلِكَ السُّوءُ عَنْهُمْ ، فَصَارُوا في أحْسَنِ صُورَةٍ )) قَالَ : (( قالا لِي : هذِهِ جَنَّةُ عَدْنٍ ، وهذاك مَنْزِلُكَ ، فسَمَا بَصَري صُعُداً ، فإذا قَصْرٌ مِثْلُ الرَّبَابَةِ البَيضاءِ ، قالا لي : هذاكَ مَنْزلكَ ؟ قلتُ لهما : باركَ اللهُ فيكُما ، فذَراني فأدخُلَه . قالا لي : أمَّا الآنَ فَلاَ ، وأنتَ دَاخِلُهُ ، قُلْتُ لَهُمَا : فَإنِّي رَأيتُ مُنْذُ اللَّيْلَة عَجَباً ؟ فما هَذَا الَّذِي رأيتُ ؟ قالا لي : أمَا إنَّا سَنُخْبِرُكَ : أَمَّا الرَّجُلُ الأوَّلُ الَّذِي أَتَيْتَ عَلَيْهِ يُثْلَغُ رَأسُهُ بالحَجَرِ ، فإنَّهُ الرَّجُلُ يَأخُذُ القُرآنَ فَيَرفُضُهُ ، ويَنَامُ عَنِ الصَّلاةِ المَكتُوبَةِ . وأمَّا الرَّجُلُ الَّذِي أتَيْتَ عَلَيْهِ يُشَرْشَرُ شِدْقُهُ إِلَى قَفَاهُ ، ومِنْخَرُهُ إِلَى قَفَاهُ ، وَعَيْنُهُ إِلَى قَفَاهُ ، فإنَّهُ الرَّجُلُ يَغْدُو مِنْ بَيْتِهِ فَيَكْذِبُ الكِذْبَةَ تَبْلُغُ الآفاقَ . وأمَّا الرِّجَالُ والنِّسَاءُ العُراةُ الَّذِينَ هُمْ في مثْلِ بناءِ التَّنُّورِ ، فَإنَّهُمُ الزُّنَاةُ والزَّواني ، وأما الرجلُ الذي أتيتَ عَليهِ يَسْبَحُ في النهرِ ، ويلقم الحجارةَ ، فإنَّهُ آكلُ الربا ، وأمَّا الرَّجُلُ الكَريهُ المرآةِ الَّذِي عِنْدَ النَّارِ يَحُشُّهَا وَيَسْعَى حَوْلَهَا ، فإنَّهُ مالكٌ خازِنُ جَهَنَّمَ ، وأمَّا الرَّجُلُ الطَّويلُ الَّذِي في الرَّوْضَةِ ، فإنَّهُ إبراهيم صلى الله عليه وسلم ، وأمَّا الولدان الَّذِينَ حَوْلَهُ ، فكلُّ مَوْلُودٍ ماتَ عَلَى الفِطْرَةِ )) وفي رواية البَرْقانِيِّ : (( وُلِدَ عَلَى الفِطْرَةِ )) فَقَالَ بعض المُسلمينَ : يَا رسولَ الله ، وأولادُ المُشركينَ فقالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( وأولادُ المشركينَ ، وأما القومُ الذينَ كانُوا شَطْرٌ مِنْهُمْ حَسَنٌ ، وشَطْرٌ مِنْهُمْ قَبيحٌ ، فإنَّهُمْ قَومٌ خَلَطُوا عَمَلاً صَالِحاً وآخَرَ سَيِّئاً ، تَجاوَزَ الله عنهم )) . رواه البخاري .
وفي روايةٍ لَهُ : (( رَأيْتُ اللَّيْلَةَ رَجُلَيْنِ أتيَانِي فأخْرَجَانِي إِلَى أرْضٍ مُقَدَّسَةٍ )) ثُمَّ ذَكَرَهُ وقال : (( فَانْطَلَقْنَا إِلَى نَقْبٍ مثلِ التَّنُّورِ ، أعْلاهُ ضَيِّقٌ وَأسْفَلُهُ واسِعٌ ؛ يَتَوَقَّدُ تَحْتَهُ ناراً ، فإذا ارْتَفَعَتِ ارْتَفَعُوا حَتَّى كَادُوا أنْ يَخْرُجُوا ، وَإِذَا خَمَدَتْ ! رَجَعُوا فِيهَا ، وفيها رِجالٌ ونِساءٌ عراةٌ )) . وفيها : (( حَتَّى أتَيْنَا عَلَى نَهْرٍ مِنْ دَمٍ )) ولم يشكَّ (( فِيهِ رَجُلٌ قائِمٌ عَلَى وَسَطِ النَّهْرِ وعلى شطِّ النَّهرِ رجلٌ ، وبينَ يديهِ حِجارةٌ ، فأقبلَ الرجلُ الذي في النَّهرِ ، فَإذَا أرَادَ أَنْ يَخْرُجَ رَمَى الرَّجُلُ بِحَجَرٍ في فِيهِ ، فَرَدَّهُ حَيثُ كَانَ ، فَجَعَلَ كُلَّمَا جَاءَ لِيَخْرُجَ جَعَلَ يَرْمِي في فِيهِ بِحَجَرٍ ، فَيْرَجِعْ كما كَانَ )) . وفيها : (( فَصَعِدَا بي الشَّجَرَةَ ، فَأدْخَلاَنِي دَاراً لَمْ أرَ قَطُّ أحْسَنَ مِنْهَا ، فيهَا رِجَالٌ شُيُوخٌ وَشَبَابٌ )) . وفيها : (( الَّذِي رَأيْتَهُ يُشَقُّ شِدْقُهُ فَكَذَّابٌ ، يُحَدِّثُ بِالكِذْبَةِ فَتُحْمَلُ عَنْهُ حَتَّى تَبْلُغَ الآفَاقَ ، فَيُصْنَعُ بِهِ مَا رَأَيْتَ إِلَى يَومِ القِيَامَةِ )) ، وَفِيهَا : (( الَّذِي رَأيْتَهُ يُشْدَخُ رَأسُهُ فَرَجُلٌ عَلَّمَهُ اللهُ القُرْآنَ ، فَنَامَ عَنْهُ بِاللَّيْلِ ، وَلَمْ يَعْمَلْ فِيهِ بالنَّهارِ ، فَيُفْعَلُ بِهِ إِلَى يَوْمِ القِيَامَةِ ، والدَّارُ الأولَى الَّتي دَخَلْتَ دَارُ عَامَّةِ المُؤمِنِينَ ، وأمَّا هذِهِ الدَّارُ فَدَارُ الشُّهَداءِ ، وأنا جِبْرِيلُ ، وهذا مِيكائيلُ ، فَارْفَعْ رَأْسَكَ ، فَرَفَعْتُ رَأسِي ، فإذَا فَوْقِي مِثْلُ السَّحابِ ، قالا : ذاكَ مَنْزِلُكَ ، قُلْتُ : دَعَانِي أدْخُلُ مَنْزِلي ، قالا : إنَّهُ بَقِيَ لَكَ عُمُرٌ لَمْ تَسْتَكْمِلْهُ ، فَلَوِ اسْتَكْمَلْتَهُ أتَيْتَ مَنْزِلَكَ )) . رواه البخاري .
Amesema Samurah bin Jundub (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwauliza sana Swahaaba zake: "Yupo yeyote miongoni mwenu aliyeona ndoto?" Yule ambaye aliona ndoto alikuwa anahadithia yale ambayo Allaah amemtaka ahadithie. Na hakika alituambia mchana mmoja: "Hakika walikuja kwangu watu wawili jana usiku na wakaniambia: 'Twende pamoja.' Nami nikaenda pamoja nao mpaka tukafika kwa mtu aliyekuwa amelala chini, na mwengine amesimama juu yake akiwa na jiwe kubwa mkononi mwake. Alikuwa akimpiga kichwani mwake nalo, hivyo kukanyaga kichwa chake. Baada ya jiwe kubwa kumponda linabingirika masafa kidogo kutoka kwake. Yule mpondaji akalifuata na kulichukua na akarudi ile hali yake ya awali (kama kilivyo kuwa mwanzo). kisha anarudia kumponda na anamfanya kama alivyo mfanya mara ya kwanza." Akasema: "Nikawauliza: Ametakasika Allaah! Hawa ni kina nani?" Wakaniambia: "Twende, twende." Tukaondoka na kufika kwa mtu aliyekuwa amelala chini, na mwengine amesimama juu yake akiwa na kulabu ya chuma (ncha yake ikiwa imechongoka na ina makali) mkononi mwake. Naye alikuwa akija upande wake mmoja na kuukata mdomo wake mpaka shingoni mwake, na kisha kurarua pua yake mpaka shingoni mwake na kulifumua jicho lake mpaka shingoni mwake. Kisha anageuza upande wake mwengine na kufanya kama alivyofanya upande ule wa awali. Hamalizi upande huu wa pili mpaka ule upande wa kwanza urudi kama ulivyokuwa, kisha anarudia tena na kufanya kama alivyofanya awali. Akasema: "Nikasema: Ametakasika Allaah! Hawa ni kina nani?": Wakaniambia: "Twende zetu, twende zetu." Nasi tukaondoka mpaka tukakifikia kitu kilicho fanana na tanuri, nami nikadhania kuwa alisema: "Humo ndani ghafla tukasikia yakitoka makelele na sauti." Nasi tukaangalia tukawaona wanaume na wanawake waliokuwa uchi na mwako wa moto ulikuwa ukiwajilia kutoka chini. Na unapowafikia huo mwako basi walikuwa wanalia. Nikawauliza: "Hawa ni kina nani?" Wakaniambia: "Twende twende." Nasi tuliondoka mpaka tukafika mtoni. Nilidhania kuwa alikuwa amesema kitu: "Maji ya mto huo yalikuwa mekundu mfano wa damu na humo ndani kulikuwa na mwongeleaji. Ukingoni mwa mto huo alisimama mtu na mlima wa mawe. Mwongeleaji alipokuwa anakuja upande wake alikuwa anampiga na jiwe, hivyo kuukanyaga uso wake, na kunfanya kurudi. Anaaza kuongelea tena, na anapo karibia ukingo wa mto mara nyengine tena, yule mtu aliyesimama ukingoni anampiga tena na jiwe ambalo linauponda uso wake." Niliwauliza: "Hawa ni kina nani?" Wakasema: "Twende, twende." Tukaondoka mpaka tukafika kwa mtu mwenye sura mbaya kabisa, ambaye kwa sura hizo alikuwa haangaliki akiwa karibu na moto mkali, naye alikuwa anauzunguka. Nikauliza: "Huyu ni nani?" Wakaniambia: "Twende, twende." Tuliondoka na kufiki katika bustani ambalo lilikuwa na maua aina yote ya majira ya kuchipua. Katikati ya bustani hilo kulikuwa na mtu aliyekuwa mrefu sana mpaka sikuweza kuona kichwa chake ambacho kilikuwa ni kama kinagusa mbingu, na huku amezungukwa na watoto wengi sana amabo sikuona mfano wake kabla ya hapo. Nikawauliza: "Huyu ni mtu gani? Na hawa watoto ni kina nani?" Wakaniambia: "Twende, twende." Tukaondoka mpaka tukafika katika mti mkubwa wala sijaona mti aina yake kwa ukubwa na uzuri. wakaniambia : "Panda juu." Tulipanda mpaka tukafika katika mji uliojengwa na matofali ya dhahabu na fedha yaliyo pangwa moja baada ya jengine. Tulifika katika mlango wa mji, tukafunguliwa, nasi tukaingia na kuwaona watu nusu ya miili yao ikiwa mizuri sana sijawahi kuona uzuri kama huo na nusu ya pili mbaya sana na wala sijaona ubaya wa mtu kama huo. Wakaniambia: "Nendeni mukaingie katika mto ule." Mto wenyewe ulikuwa ukipita katikati ya mji na maji yake yalikuwa safi na meupe. Waliingia ndani ya mto huo na walipotoka ile sehemu yote ya mwili iliyokuwa mbaya ilitoweka na wakawa wazuri kabisa. Akasema: "Wakaniambia: Hii ndio Pepo ya Edeni na ile ndiyo nyumba yako." Nilinyanyua macho yangu juu na kuona kasri nyeupe kama kipande cha kiwingu. Wakaniambia: "Hii ndiyo sehemu yako." Niliwaambia: "Allaah Awabariki nyote wawili! Niacheni niingie." Wakasema: "Sio sasa, lakini utaingia bila shaka yoyote siku moja." Nikawaambia: "Hakika nimeona maajabu mengi usiku wa leo. Haya niliyoyaona ni mambo gani?" Wakaniambia: "Ama sasa tutakueleza yote yaliyopita: "Ama yule mtu wa kwanza ambaye alikuwa akipondwa kichwa chake na jiwe kubwa, hakika ni mtu aliyehifadhi Qur-aan na kisha kuisahau na kuipuuza na alikuwa hatekelezi Swalaah za Faradhi. Na ama yule mtu aliyekuwa na kulabu ya chuma mkononi mwake, naye alikuwa akiukata mdomo wake mpaka shingoni mwake, na kisha kurarua pua yake mpaka shingoni mwake na kulifumua jicho lake mpaka shingoni mwake, hakika yeye ni mtu aliyekuwa akitoka asubuhi mapema na kueneza uongo ambao unaenea ulimwengu mzima. Na ama wale wanaume au wanawake. Na ama yule tuliyempata akiogelea na akirushiwa mawe, ni mlaji wa riba. Na ama kwa yule mtu mwenye sura mbaya, ambaye alikuwa haangaliki na aliyekuwa akiuzunguka moto ni Maalik, mlindaji wa Moto. Na ama yule mtu mrefu sana katika bustani ni Ibraahiym ('Alayhis salaam) na wale watoto waliomzunguka ni wale watoto walioaga dunia katika Fitrah (maumbile na Uislamu)."
Na katika riwaayah ya Al-Barqaaniy: "Waliozaliwa katika Fitrah." Wakasema baadhi ya Waislamu: "Ee Rasuli wa Allaah! na watoto wa wazazi mushirikina (watakuaje)?" Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Na hata watoto wa mushrikina. Na ama wale watu ambao upande mmoja ulikuwa mzuri na mwengine mbaya, ni wale watu waliofanya amali njema na mbaya, ambao wamesamehewa na allaah." [Al-Bukhaariy]
Na katika riwaayah yake nyengine: "Niliwaona usiku watu wawili ambao walikuja kwangu na kunipeleka katika ardhi tukufu." Na akataja kama ilivyo hapo juu. Na akasema: "Tukafika katika shimo liliokuwa katika ardhi kama tanuri, juu (mdomoni mwake) lilikuwa jembamba na chini pana. Ndani yake kulikuwa na moto, mwako wa moto unapopanda juu walikuwa wakinyanyuliwa mpaka karibu kutupwa nje ya hilo tanuri na mwako unapofifia basi hurudishwa chini ya tanuri. Na ndani yake kulikuwa na wanaume na wanawake waliokuwa uchi." Kisha tukaja mpaka katika mto wa damu na hapana shaka katika hili. Ndani ya mto huo kulikuwa na mtu amesimama katikati yake na mwengine alikuwa amesimama ukingoni mwake akiwa na mlima wa mawe mbele yake. Yule aliyekuwa katikati alikuwa anataka kutoka nje ya mto, na yule aliyekuwa ukingoni alikuwa akimrushia mawe, hivyo kumfanya arudi alikotoka. Jambo hili lilikuwa likifanyika kila wakati yule mtu alipotaka kutoka nje ya mto. Kisha wakapanda nami mti na kuniingiza katika nyumba ambayo sijawahi kuiona mfano wake kwa uzuri. Ndani ya nyumba hiyo kulikuwa na wazee na vijana. Riwaayah inaendelea: Nikaambiwa: Akikatwa mashavu yake ni mtu ambaye anaeneza uongo ambao unasambaa ulimwengu mzima, naye ataadhibiwa hivyo mpaka siku ya Qiyaamah." Na ndani yake: "Na yule uliyomuona akivyogwa na jabali kwenye kichwa ni mtu aliyefundishwa na Allaah Qur-aan, lakini akawa analala usiku, kuisahau na hakuifanyia kazi mchana. Atafanywa hivyo mpaka Siku ya Qiyaamah. Na ile nyumba ya mwanzo uliyoingia ni nyumba ya Waumini wa kawaida na ama nyumba hii ni ya mashahidi. Na mimi ni Jibriyl na huyu ni Mikail. Tafadhali nyanyua macho yako sasa, nami nikainua macho yangu juu, nikaona kitu mfano wa mawingu. Wakaniambia: "Hii ndiyo nyumba yako." Nikasema: "Niacheni niingie nyumba yangu." Wakasema: "Hakika bado una miaka ambayo hujakamilisha, na pindi utakapokamilisha miaka hiyo iliyobaki utaingia katika nyumba yako." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب بيان مَا يجوز من الكذب
008-Mlango Wa Kubainisha Ruhusa ya Kusema Uongo
Alhidaaya.com [4]
اعلَمْ أنَّ الكَذِبَ ، وإنْ كَانَ أصْلُهُ مُحَرَّماً ، فَيَجُوزُ في بَعْضِ الأحْوَالِ بِشُروطٍ قَدْ أوْضَحْتُهَا في كتاب : " الأَذْكَارِ " ، ومُخْتَصَرُ ذَلِكَ : أنَّ الكلامَ وَسيلَةٌ إِلَى المَقَاصِدِ ، فَكُلُّ مَقْصُودٍ مَحْمُودٍ يُمْكِنُ تَحْصِيلُهُ بِغَيْرِ الكَذِبِ يَحْرُمُ الكَذِبُ فِيهِ ، وإنْ لَمْ يُمْكِنْ تَحْصِيلُهُ إِلاَّ بالكَذِبِ ، جازَ الكَذِبُ . ثُمَّ إنْ كَانَ تَحْصِيلُ ذَلِكَ المَقْصُودِ مُبَاحاً كَانَ الكَذِبُ مُبَاحاً ، وإنْ كَانَ وَاجِباً ، كَانَ الكَذِبُ وَاجِباً . فإذا اخْتَفَى مُسْلِمٌ مِنْ ظَالِمٍ يُريدُ قَتْلَهُ ، أَوْ أَخذَ مَالِهِ وأخفى مالَه وَسُئِلَ إنْسَانٌ عَنْهُ ، وَجَبَ الكَذِبُ بإخْفَائِه . وكذا لو كانَ عِندَهُ وديعَةٌ ، وأراد ظالمٌ أخذها ، وجبَ الكذبُ بإخفائها . وَالأحْوَطُ في هَذَا كُلِّهِ أن يُوَرِّيَ . ومعْنَى التَّوْرِيَةِ : أنْ يَقْصِدَ بِعِبَارَتِهِ مَقْصُوداً صَحيحاً لَيْسَ هُوَ كَاذِباً بالنِّسْبَةِ إِلَيْهِ ، وإنْ كَانَ كَاذِباً في ظَاهِرِ اللَّفْظِ ، وبالنِّسْبَةِ إِلَى مَا يَفْهَمُهُ المُخَاطَبُ ، وَلَوْ تَرَكَ التَّوْرِيَةَ وَأطْلَقَ عِبَارَةَ الكَذِبِ ، فَلَيْسَ بِحَرَامٍ في هَذَا الحَالِ .
وَاسْتَدَل العُلَمَاءُ بِجَوازِ الكَذِبِ في هَذَا الحَالِ بِحَديثِ أُمِّ كُلْثُومٍ رَضِيَ اللهُ عنها، أنها سمعتْ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( لَيْسَ الكَذَّابُ الَّذِي يُصْلِحُ بَيْنَ النَّاسِ ، فَيَنْمِي خَيْراً أَوْ يَقُولُ خَيْراً )) . متفق عَلَيْهِ .
زاد مسلم في رواية : قالت أُمُّ كُلْثُومٍ : وَلَمْ أسْمَعْهُ يُرَخِّصُ في شَيْءٍ مِمَّا يَقُولُ النَّاسُ إِلاَّ في ثَلاَثٍ، تَعْنِي : الحَرْبَ ، والإصْلاَحَ بَيْنَ النَّاسِ ، وَحَديثَ الرَّجُلِ امْرَأَتَهُ ، وَحديثَ المَرْأَةِ زَوْجَهَا .
Jueni ya kwamba japokuwa uongo asili yake ni haramu, lakini inaruhusiwa katika baadhi ya hali kwa masharti ambayo nimeyaweka wazi katika kitabu changu cha Al-Adhkaar. Na muhtasari wa hayo ni: Hakika mazungumzo ni njia ya kufikia lengo la halali, hivyo kila lengo zuri ambalo linaweza kufikiwa kwa ukweli inakuwa ni haramu kusema uongo. Na ikiwa haliwezi kufikiwa isipokuwa kwa kusema uongo, hapo uongo unajuzu kuutumia. Kisha ikiwa kufikia lengo hilo ni mubaha, hivyo kusema uongo pia utakuwa ni mubaha na ikiwa ni wajibu, hivyo uongo itakuwa ni wajibu. Kwa mfano, ikiwa Muislamu amejificha kutokana na dhalimu ambaye anataka kumuua au kuchukua mali yake na akaficha mali yake na akaulizwa mtu kuhusu yeye, katika hilo ni wajibu kusema uongo. Na hivyo hivyo kama mtu atakuwa ameweka amana ya mtu mwengine, na dhalimu akawa anataka kuichukua hiyo amana ya mtu ni wajibu kuificha hiyo amana ya watu. Na lililo bora katika jambo hili ni kutumia Tawriyah. Na maana ya Tawriyah ni kukusudia kwa kutumia ibara ambayo lengo lake ni sahihi kwake yeye lenye maana kadha ambayo itamfanya msikilizaji kuelewa vingine na japokuwa dhahiri yake ni uongo. Na lau pia ataacha Tawriyah na kutumia ibara ya uongo moja kwa moja haitakuwa haramu katika hali hii.
Na wanazuoni wametoa dalili katika kujuzisha uongo katika hali hii kwa ile Hadiyth ya Umm Kulthuwm bint 'Uqbah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) ya kwamba amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Si muongo yule mwenye kusuluhisha baina ya watu, hivyo kuifikia kheri au kusema maneno mazuri." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy].
Ameongeza Muslim katika riwaayah yake: "Amesema Umm Kulthuwm (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Na sijawahi kumsikia kuruhusu uongo katika mambo wanayozungumza watu ila katika hali tatu: yaani katika wakati wa vita, na kusuluhisha baina ya watu na mazungumzo ya mume kwa mkewe na mke kwa mumewe."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الحثّ عَلَى التثبت فيما يقوله ويحكيه
009-Mlango Wa Kuhimiza Kuthibitisha kwa Anayosema
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ ﴿٣٦﴾
Na wala usifuate usiyo na elimu nayo. [Al-Israa: 36]
مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾
Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf: 18]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( كَفَى بالمَرْءِ كَذِباً أنْ يُحَدِّثَ بِكُلِّ مَا سَمِعَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Inatosha kwa mtu kuwa muongo kwa kuhadithia (bila kuchunguza) kila analolisikia." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن سَمُرَةَ رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ حَدَّثَ عَنِّي بِحَديثٍ يَرَى أَنَّهُ كَذِبٌ فَهُوَ أَحَدُ الكَاذِبينَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kunizuilia mimi Hadiyth ambayo anajua wazi kuwa ni uongo, basi yeye ni miongoni mwa waongo." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أسماء رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ امْرأةً قالت : يَا رسولَ الله ، إنَّ لِي ضَرَّةً فهل عَلَيَّ جُنَاحٌ إنْ تَشَبَّعْتُ مِنْ زَوْجِي غَيْرَ الَّذِي يُعْطِيني ؟ فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( المُتَشَبِّعُ بِما لَمْ يُعْطَ كَلاَبِسِ ثَوْبَيْ زُورٍ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake Asmaa (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba wakati mmoja alikuja mwanamke na kuuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi nina mke mwenza. Je, ninaruhusiwa kumwambia mke mwenza kuwa mume wangu amenipatia kitu ambacho hakunipatia?" Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Mwenye kudai kuwa amepatiwa kitu na kumbe hajapatiwa ni kama anayevaa mavazi mawili ya uongo." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب بيان غلظ تحريم شهادة الزُّور
010-Mlango Wa Kuharamishwa Ushuhuda wa Uwongo
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَاجْتَنِبُوا قَوْلَ الزُّورِ ﴿٣٠﴾
Na jiepusheni na kauli za uongo. [Al-Hajj: 30]
وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ ﴿٣٦﴾
Na wala usifuate usiyo na elimu nayo. [Al-Israa: 36]
مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾
Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf: 18]
إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤﴾
Hakika Rabb wako bila shaka Yu tayari Anaziona nyenendo zao zote. [Al-Fajr: 14]
وَالَّذِينَ لَا يَشْهَدُونَ الزُّورَ ﴿٧٢﴾
Na wale ambao hawashuhudii uongo. [Al-Furqaan: 72]
وعن أَبي بَكْرَةَ رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( ألاَ أُنَبِّئُكُمْ بِأكْبَرِ الكَبَائِرِ ؟ )) قُلْنَا : بَلَى يَا رسولَ اللهِ . قَالَ : (( الإشْراكُ باللهِ ، وعُقُوقُ الوَالِدَيْنِ )) وكَانَ مُتَّكِئاً فَجَلَسَ ، فَقَالَ : (( ألا وَقولُ الزُّورِ )) فما زال يُكَرِّرُهَا حَتَّى قلنا : لَيْتَهُ سَكَتَ . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Bakrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Je, niwajulishe nyinyi madhambi makubwa kuliko yote?" Tukasema: "Kwa nini tusitake, ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Kumshirikisha Allaah na kuwaasi wazazi wawili." Akakaa sawa baada ya kuwa ameegemea mto, akasema: "Jiepusheni na kauli ya urongo." Na kutoa ushahidi wa uongo aliendelea kuirudia kauli hiyo mpaka tukasema afadhali angelinyamaza." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم لعن إنسان بعينه أَوْ دابة
011-Mlango Wa Kukatazwa Kumlaani Mtu au Mnyama
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي زيدٍ ثابت بن الضَّحَّاك الأنصاريِّ رضي اللهُ عنه ، وَهُوَ من أهلِ بَيْعَةِ الرِّضْوَانِ ، قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ حَلَفَ عَلَى يَمِينٍ بِمِلَّةٍ غَيْرِ الإسْلاَمِ كاذِباً مُتَعَمِّداً ، فَهُوَ كَما قَالَ ، وَمَنْ قَتَلَ نَفْسَهُ بِشَيءٍ ، عُذِّبَ بِهِ يَومَ القِيَامَةِ ، وَلَيْسَ عَلَى رَجُلٍ نَذْرٌ فيما لا يَمْلِكُهُ ، وَلَعْنُ المُؤْمِنِ كَقَتْلِهِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Zayd Thaabit bin Adh-Dhahaak Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu), naye ni miongoni mwa watu walioshuhudia Bay'ah ya Rhidhwaan ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuapa kwa makusudi yamini ya uwongo kwa dini isiyokuwa ya Uislamu, huwa ni kama alivyosema. Na mwenye kujiua kwa kitu chochote, ataadhibiwa nacho Siku ya Qiyaamah. Na hapana nadhiri kwa mtu kutoa kitu asicho miliki na kumlaani Muisalmu ni sawa na kumuua." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( لاَ يَنْبَغِي لِصِدِّيقٍ أنْ يَكُونَ لَعَّاناً )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haifai (haitakiwi) kwa mtu ambaye ni mkweli kuwa na sifa ya kulaani." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي الدرداءِ رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ يَكُونُ اللَّعَانُونَ شُفَعَاءَ ، وَلاَ شُهَدَاءَ يَوْمَ القِيَامَة )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wala wenye kulaani sana hawawezi kuwa ni mwenye kuwaombea wenziwao wala kuwa mashahidi Siku ya Qiyaamah." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن سَمُرَةَ بْنِ جُنْدُبٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَلاَعَنُوا بِلَعْنَةِ اللهِ ، وَلاَ بِغَضَبِهِ ، وَلاَ بِالنَّارِ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Samurah bin Jundub (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usimlaani yeyote kati yenu kwa laana ya Allaah wala kwa Ghadhabu Zake wala pia kwa moto." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 5
وعن ابن مسعود رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لَيْسَ المُؤْمِنُ بالطَّعَّانِ ، وَلاَ اللَّعَّانِ ، وَلاَ الفَاحِشِ ، وَلاَ البَذِيِّ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hawi kabisa Muumini na sifa ya kusuta, wala kulaani, wala kutusi wala kutumia lugha chafu." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth hasan]
Hadiyth – 6
وعن أَبي الدرداء رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ العَبْدَ إِذَا لَعَنَ شَيْئاً ، صَعدَتِ اللَّعْنَةُ إِلَى السَّماءِ ، فَتُغْلَقُ أبْوابُ السَّماءِ دُونَهَا ، ثُمَّ تَهْبِطُ إِلَى الأرْضِ ، فَتُغْلَقُ أبْوابُهَا دُونَها ، ثُمَّ تَأخُذُ يَميناً وَشِمالاً ، فَإذا لَمْ تَجِدْ مَسَاغاً رَجَعَتْ إِلَى الَّذِي لُعِنَ ، فإنْ كَانَ أهْلاً لِذلِكَ ، وإلاَّ رَجَعَتْ إِلَى قَائِلِهَا )) . رواه أَبُو داود .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika mja anapokilaani kitu chochote, laana hiyo hupanda mpaka mbinguni, na hapo milango yote ya mbinguni hufungwa mbele yake. Kwa ajili hiyo hushuka tena ardhini, na pia hufungwa milango mbele (dhidi) yake. Kisha hugeuka upande wa kuume na kushotoni na ikiwa haitapata nafasi ya kuingilia, itarudi kwa yule aliye laaniwa ikiwa atafaa kupata laana hiyo. Na ikiwa ni kinyume na hivyo basi itarudi kwa yule aliye laani." [Abu Daawuwd]
Hadiyth – 7
وعن عمران بن الحُصَيْنِ رضي الله عنهما ، قَالَ : بَيْنَمَا رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم في بَعْضِ أسْفَارِهِ ، وَامْرأةٌ مِنَ الأنْصَارِ عَلَى نَاقَةٍ ، فَضَجِرَتْ فَلَعَنَتْهَا ، فَسَمِعَ ذَلِكَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم فقالَ : (( خُذُوا مَا عَلَيْهَا وَدَعُوهَا ؛ فَإنَّهَا مَلْعُونَةٌ )) قَالَ عمْرانُ : فَكَأنِّي أَرَاهَا الآنَ تَمْشِي في النَّاسِ مَا يَعْرِضُ لَهَا أحَدٌ . رواه مسلم .
Amesema 'Imraan bin Al-Huswayn (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Tulipokuwa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika baadhi ya safari zake na wakati mmoja mwanamke mmoja wa Ki-Answaar alikuwa pamoja nasi. Alikuwa amempanda ngamia wa kike, na kwa ile shida na matatizo yaliyo kuwepo alimlaani. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimsikia, akasema: "Chukua vitu vilivyo juu yake na umwache kwani amelaaniwa." Akasema 'Imraan: "Hakika ni kama kwamba namwangalia ngamia huyo akipita miongoni mwa watu na hakuna anayeshughulika naye kabisa." [Muslim]
Hadiyth – 8
وعن أَبي بَرْزَةَ نَضْلَةَ بْنِ عُبَيْدٍ الأَسْلَمِيِّ رضي اللهُ عنه قَالَ : بَيْنَمَا جَارِيَةٌ عَلَى نَاقَةٍ عَلَيْهَا بَعْضُ مَتَاعِ القَوْمِ . إِذْ بَصُرَتْ بِالنَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، وَتَضَايَقَ بِهِمُ الجَبَلُ فَقَالَتْ : حَلْ ، اللَّهُمَّ الْعَنْهَا. فَقَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تُصَاحِبْنَا نَاقَةٌ عَلَيْهَا لَعْنَةٌ )) . رواه مسلم .
Amesema Abu Barzah Nadhlah bin 'Ubayd Al-Aslamiyy (Radhwiya Allaahu 'anhu): Kijakazi mmoja alikuwa amempanda ngamia aliyekuwa amebeba samani za watu wake (kabila lake). Mara kwa ghafla akamuona Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na zile njia za majabalini zilikuwa ndogo sana, hivyo kumfanya aseme kwa hasira: "Ee Allaah! Mlaani (huyu ngamia)." Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Asifuatane nasi ngamia ambaye ana laana juu yake." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب جواز لعن أصحاب المعاصي غير المعينين
012-Mlango Wa Ruhusa Kuwalaani Watu wa Maasi Bila Kuwataja Majina
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
أَلَا لَعْنَةُ اللَّـهِ عَلَى الظَّالِمِينَ﴿١٨﴾
Tanabahi! Laana ya Allaah iko juu ya waliodhulumu. [Huwd: 18]
فَأَذَّنَ مُؤَذِّنٌ بَيْنَهُمْ أَن لَّعْنَةُ اللَّـهِ عَلَى الظَّالِمِينَ ﴿٤٤﴾
Basi mtangazaji atatangaza baina yao kwamba: Laana ya Allaah iwe juu ya madhalimu! [Al-A'raaf: 44]
وَثَبَتَ فِي الصَّحِيحِ أَنَّ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( لَعنَ اللهُ الوَاصِلَةَ وَالمُسْتَوْصِلَةَ )) وَأنَّهُ قَالَ : (( لَعَنَ اللهُ آكِلَ الرِّبَا )) وأنَّهُ لَعَنَ المُصَوِّرِينَ ، وأنَّهُ قَالَ : (( لَعَنَ اللهُ مَنْ غيَّرَ مَنَارَ الأَرْضِ )) أيْ حُدُودَهَا ، وأنَّهُ قَالَ : (( لَعَنَ اللهُ السَّارِقَ يَسْرِقُ البَيْضَةَ )) ، وأنَّهُ قَالَ : (( لَعَنَ اللهُ مَنْ لَعَنَ وَالِدَيهِ )) وَ(( لَعَنَ اللهُ من ذَبَحَ لِغَيْرِ اللهِ )) ، وَأنَّه قَالَ : (( مَنْ أَحْدَثَ فِيهَا حَدَثاً أَوْ آوَى مُحْدِثاً فَعَلَيْهِ لَعْنَةُ اللهِ وَالمَلاَئِكَة والنَّاسِ أجْمَعينَ )) ، وأنَّه قَالَ : (( اللَّهُمَّ الْعَنْ رِعْلاً ، وَذَكْوَانَ، وعُصَيَّةَ : عَصَوُا اللهَ وَرَسُولَهُ )) وهذِهِ ثَلاَثُ قَبَائِلَ مِنَ العَرَبِ . وأنَّه قَالَ : (( لَعَنَ اللهُ اليَهُودَ اتَّخَذُوا قُبُورَ أنْبِيَائِهِمْ مَسَاجِدَ )) وأنهُ (( لَعَنَ المُتَشَبِّهِينَ مِنَ الرِّجَالِ بالنِّساءِ والمُتَشَبِّهاتِ مِنَ النِّسَاءِ بالرِّجالِ )) .
وَجَميعُ هذِهِ الألفاظِ في الصحيح ؛ بعضُها في صَحيحَيّ البُخاري ومسلمٍ ، وبعضها في أحَدِهِمَا ، وإنما قصدت الاختِصَارَ بالإشارةِ إِلَيهمَا ، وسأذكر معظمها في أبوابها من هَذَا الكتاب ، إن شاء الله تَعَالَى .
Imethubutu katika Hadiyth Swahiyh kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: " Allaah Amemlaani mwenye kuunganisha nywele zake kwa nywele nyengine na mwenye kutaka kufanywa hivyo." [Al-Bukhaariy na Muslim]. Na kuwa pia amesema: "Allaah Amemlaani mwenye kula riba." [Al-Bukhaariy na Muslim]. Na kuwa yeye (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amemlaani anayechora picha." [Al-Bukhaariy].
Na kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah Amemlaani mwenye kubadilisha au kufuta mipaka ya ardhi." [Muslim]. Na kuwa amesema: "Allaah Amemlaani mwizi mwenye kuiba hata yai." [Al-Bukhaary na Muslim]. Na kuwa amesema: "Allaah Anamlaani mwenye kuwalaani wazazi wake." [Muslim]. Na pia: "Allaah Amemlaani mwenye kuchinja kwa asiyekuwa Allaah." [Muslim]. Na kuwa amesema: "Mwenye kuzua jambo baya ndani yake (Katika mji wa Madiynah) uzushi au kuanzisha jambo (Linalokwenda kinyume na sheria), juu yake iwe laana ya Allaah, Malaaikah Zake na watu wote kwa jumla." [Al-Bukhaariy na Muslim]. Na pia amesema: "Ee Allaah! Walaani Ri'lan, na Dhakwaan, na 'Uswayyah, kwani wamemuasi Allaah na Rasuli Wake." [Muslim]. Na haya ni makabila matatu ya Kiarabu. Na pia amesema: "Allaah Awalaani Mayahudi, kwani wamefanya makaburi ya Manabiy wao kuwa ni Msikiti." [Al-Bukhaariy na Muslim]. Na amesema: "Wamelaaniwa wanaume wenye kujifananisha na wanawake, na wanawake wenye kujifananisha na wanaume." [Al-Bukhaary].
Na lafdhi zote zipo katika Swahiyh, baadhi yake zipo katika Swahiyh ya Al-Bukhaary na Muslim, na baadhi yake katika moja wapo ya Swahiyh hizo mbili. Na hakika nilikusudia kuzileta kwa muhtasari kwa kuziashiria. Na nitazitaja nyingi miongoni mwazo katika milango mingine ya kitabu hichi, Anapo penda Allaah Ta'aalaa.
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم سب المسلم بغير حق
013-Mlango Wa Kukatazwa Kumtusi Muislamu Bila ya Haki
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾
Na wale wanaowaudhi Waumini wa kiume na Waumini wa kike bila ya kuwa wamechuma kosa, basi kwa yakini wamejibebea usingiziaji mkuu wa dhulma na dhambi bayana. [Al-Ahzaab: 58]
Hadiyth – 1
وعن ابن مسعود رضي اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( سِبَابُ المُسْلِمِ فُسُوقٌ ، وَقِتالُهُ كُفْرٌ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kumtukana Muislamu ni ufasiki na kumwua ni ukafiri." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي ذرٍ رضي اللهُ عنه : أنهُ سَمِعَ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقول : (( لاَ يَرْمِي رَجُلٌ رَجُلاً بِالفِسْقِ أَوِ الكُفْرِ ، إِلاَّ ارْتَدَّتْ عَلَيْهِ ، إنْ لَمْ يَكُنْ صَاحِبُهُ كذَلِكَ )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mtu hamwiti mtu mwengine kuwa ni fasiki au kafiri isipokuwa hurudi kwake sifa hiyo ikiwa mwenye kuitwa hana jambo hilo." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( المُتَسَابَّانِ مَا قَالاَ فَعَلَى البَادِي منهُما حَتَّى يَعْتَدِي المَظْلُومُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wanapo tukanana watu wawili, yule aliyeanza ndiye mwenye kulaumiwa mpaka atakapovuka mipaka aliye dhulumiwa." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه، قَالَ : أُتِيَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم ، بِرَجُلٍ قَدْ شرِبَ قَالَ : (( اضربوهُ )) قَالَ أَبُو هريرةَ : فَمِنَّا الضارِبُ بيَدِهِ ، والضَّارِبُ بِنَعْلِهِ ، والضَّارِبُ بِثَوْبِهِ . فَلَمَّا انْصَرَفَ ، قَالَ بَعْضُ القَوْمِ : أخْزَاكَ اللهُ ! قَالَ : (( لا تَقُولُوا هَذَا ، لا تُعِينُوا عَلَيْهِ الشَّيْطَان )) . رواه البخاري .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Aliletwa mtu kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa amekunywa pombe, akasema: "Mpigeni." Akasema Abu Huraiyrah: "Kuna miongoni mwetu waliompiga kwa mikono, na wengine kwa viatu na wengine kwa nguo zao." Alipoondoka yule mtu, baadhi ya watu walianza kusema: "Allaah akupe hizaya." Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Musiseme hivyo, musimsaidie shetani juu yake." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 5
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقول : (( مَنْ قَذَفَ مَمْلُوكَهُ بِالزِّنَى يُقَامُ عَلَيْهِ الحَدُّ يَومَ القِيَامَةِ ، إِلاَّ أَنْ يَكُونَ كما قَالَ )) . متفق عَلَيْهِ .
Amsema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kumtuhumu mtumwa wake kuwa amezini atasimamishwa adhabu Siku ya Qiyaamah isipokuwa iwe ni kama alivyosema (iwe ni kweli)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم سب الأموات بغير حق ومصلحةٍ شرعية
014-Mlango Wa Kukatazwa Kutukana Walio Kufa Bila ya Haki na Maslahi ya Kisheria
Alhidaaya.com [4]
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لا تَسُبُّوا الأَمْوَاتَ ، فَإنَّهُمْ قَدْ أفْضَوْا إِلَى مَا قَدَّمُوا )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwake 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba RAsuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Musiwatukane waliofariki kwani wao tayari wanakumbana na yale waliyoyakadimisha." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الإيذاء
015-Mlango Wa Kukatazwa Kuudhi
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾
Na wale wanaowaudhi Waumini wa kiume na Waumini wa kike bila ya kuwa wamechuma kosa, basi kwa yakini wamejibebea usingiziaji mkuu wa dhulma na dhambi bayana. [Al-Ahzaab: 58]
Hadiyth – 1
وعن عبدِ الله بن عمرو بن العاصِ رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( المُسْلِمُ مَنْ سَلِمَ المُسْلِمُونَ مِنْ لِسَانِهِ وَيَدِهِ ، والمُهَاجِرُ مَنْ هَجَرَ مَا نَهَى اللهُ عَنْهُ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Asa (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muislamu mzuri (na wa sawa) ni yule ambaye Waislamu wengine wanasalimika na shari za ulimi wake na mkono wake na Muhaajir ni yule anayeyahama yale aliyomkataza Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن عبدِ الله بن عمرو بن العاصِ رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ أحَبَّ أنْ يُزَحْزَحَ عَنِ النَّارِ ، ويُدْخَلَ الجَنَّةَ ، فَلْتَأْتِهِ مَنِيَّتُهُ وَهُوَ يُؤْمِنُ بِاللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، وَلْيَأْتِ إِلَى النَّاسِ الَّذِي يُحِبُّ أنْ يُؤْتَى إِلَيْهِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayependwa kulindwa na kuepushwa na Moto na kuingizwa Peponi, anatakiwa akutane na kifo akiwa anamuamini Allaah na Siku ya Mwisho, na aamiliane na watu kwa njia ambayo yeye anapenda watu waamiliane naye." [Muslim]. Hii ni sehemu ya Hadiyth ndefu ambayo tumetangulia kuitaja katika mlango "Wajibu wa Kuwatii Viongozi."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن التباغض والتقاطع والتدابر
016-Mlango Wa Kukatazwa Kubughudhiana na Kukatana na Kupeana Nyongo
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ ﴿١٠﴾
Hakika Waumini ni ndugu [Al-Hujuraat: 10]
أَذِلَّةٍ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ أَعِزَّةٍ عَلَى الْكَافِرِينَ ﴿٥٤﴾
Wanyenyekevu kwa Waumini, washupavu juu ya makafiri [Al-Maaidah: 45]
مُّحَمَّدٌ رَّسُولُ اللَّـهِ ۚ وَالَّذِينَ مَعَهُ أَشِدَّاءُ عَلَى الْكُفَّارِ رُحَمَاءُ بَيْنَهُمْ ۖ ﴿٢٩﴾
Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ni Rasuli wa Allaah. Na wale walio pamoja naye ni wakali zaidi dhidi ya makafiri wanahurumiana baina yao. [Al-Fat-h: 29]
Hadiyth – 1
وعن أنس رضي اللهُ عنه : أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( لاَ تَبَاغَضُوا ، وَلاَ تَحَاسَدُوا ، وَلاَ تَدَابَرُوا ، وَلاَ تَقَاطَعُوا ، وَكُونُوا عِبَادَ اللهِ إخْوَاناً ، وَلاَ يَحِلُّ لِمُسْلِمٍ أنْ يَهْجُرَ أخَاهُ فَوْقَ ثَلاَثٍ )). متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msichukiane wala msihusudiane, wala msipeane nyongo, wala msikate uhusiano, lakini kuweni enyi waja wa Allaah ndugu. Na haifai kwa Muislamu kuhama nduguye zaidi ya siku tatu." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( تُفْتَحُ أبْوابُ الجَنَّةِ يَوْمَ الإثْنَيْنِ ويَوْمَ الخَمْيِسِ ، فَيُغْفَرُ لِكُلِّ عَبْدٍ لا يُشْرِكُ بِاللهِ شَيْئاً ، إِلاَّ رَجُلاً كَانَتْ بينهُ وَبَيْنَ أخِيهِ شَحْناءُ فَيُقَالُ : أنْظِرُوا هَذَيْنِ حَتَّى يَصْطَلِحَا ! أَنْظِرُوا هَذَينِ حَتَّى يَصْطَلِحَا ! )) . رواه مسلم .
وفي روايةٍ لَهُ : (( تُعْرَضُ الأعْمالُ في كُلِّ يَوْمِ خَمِيسٍ وإثْنَيْن )) وذَكَرَ نَحْوَهُ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Milango ya Pepo hufunguliwa siku ya Jumatatu na Alkhamisi, hivyo kusamehewa kila mja asiyemshirikisha Allaah na kitu chochote isipokuwa mtu ambaye ana uadui (utesi) baina yake na nduguye. Atasema: 'Waacheni hawa wawili mpaka wafanye mapatano baina yao!' [Muslim].
Na katika riwaayah yake nyengine: "Huonyeshwa amali kila siku ya Jumatatu na Alkhamisi", na akataja mfano wa hiyo riwaayah ya mwanzo.
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الحسد
017-Mlango Wa Kukatazwa Hasadi
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
أَمْ يَحْسُدُونَ النَّاسَ عَلَىٰ مَا آتَاهُمُ اللَّـهُ مِن فَضْلِهِ ۖ ﴿٥٤﴾
Au wanawahusudu watu (Nabiy Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم na Waumini) kwa yale Aliyowapa Allaah katika Fadhila Zake? [An-Nisaa: 54]
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه: أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إيَّاكُمْ وَالحَسَدَ ؛ فَإنَّ الحَسَدَ يَأكُلُ الحَسَنَاتِ كَمَا تَأكُلُ النَّارُ الحَطَبَ )) أَوْ قَالَ : (( العُشْبَ )) . رواه أَبُو داود .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Tahadharini hasadi, kwani hasadi hula hasanati (amali njema) kama moto unavyokula kuni." au alisema: "Majani/malisho." [Abuu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النَّهي عن التجسُّس
والتَّسَمُّع لكلام من يكره استماعه
018-Mlango Wa Kupeleleza na Kusikiliza Mazungumzo kwa Wasiotaka Usikiliza
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَلَا تَجَسَّسُوا ﴿١٢﴾
Na wala msichunguzane [Al-Hujuraat: 12]
وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾
Na wale wanaowaudhi Waumini wa kiume na Waumini wa kike bila ya kuwa wamechuma kosa, basi kwa yakini wamejibebea usingiziaji mkuu wa dhulma na dhambi bayana. [Al-Ahzaab: 58]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إيَّاكُمْ وَالظَّنَّ ، فَإنَّ الظَّنَّ أَكْذَبُ الحَدِيثِ ، ولا تحسَّسوا وَلاَ تَجَسَّسُوا وَلاَ تَنَافَسُوا ، وَلاَ تَحَاسَدُوا ، وَلاَ تَبَاغَضُوا ، وَلاَ تَدَابَرُوا ، وَكُونُوا عِبَادَ اللهِ إخْوَاناً كَمَا أَمَرَكُمْ .المُسْلِمُ أَخُو المُسْلِمِ ، لاَ يَظْلِمُهُ ، وَلاَ يَخْذُلُهُ وَلاَ يَحْقِرُهُ ، التَّقْوَى هاهُنَا التَّقْوَى هاهُنَا )) وَيُشِيرُ إِلَى صَدْرِهِ (( بِحَسْبِ امْرِىءٍ مِنَ الشَّرِّ أنْ يَحْقِرَ أخَاهُ المُسْلِمَ ، كُلُّ المُسْلِمِ عَلَى المُسْلِمِ حَرَامٌ : دَمُهُ ، وَعِرْضُهُ ، وَمَالُهُ . إنَّ اللهَ لاَ يَنْظُرُ إِلَى أجْسَادِكُمْ ، وَلاَ إِلَى صُوَرِكُمْ ، وَلكِنْ يَنْظُرُ إِلَى قُلُوبِكُمْ وأعْمَالِكُمْ )) .
وَفِي رواية : (( لاَ تَحَاسَدُوا، وَلاَ تَبَاغَضُوا ، وَلاَ تَجَسَّسُوا ، وَلاَ تَحَسَّسُوا ، وَلاَ تَنَاجَشُوا وَكُونُوا عِبَادَ اللهِ إخْواناً )) .
وفي رواية : (( لاَ تَقَاطَعُوا ، وَلاَ تَدَابَرُوا ، وَلاَ تَبَاغَضُوا ، وَلاَ تَحَاسَدُوا ، وَكُونُوا عِبَادَ اللهِ إخْواناً )) وَفِي رِواية : (( وَلاَ تَهَاجَرُوا وَلاَ يَبِعْ بَعْضُكُمْ عَلَى بَيْعِ بَعْضٍ )) . رواه مسلم بكلّ هذِهِ الروايات ، وروى البخاريُّ أكْثَرَهَا .
Imepokewa kutoka kwake Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Tahadharini na dhana, kwani dhana ni uwongo mkubwa katika mazungumzo. Wala msiulizie ulizie kuhusu makosa ya watu wala msipeleleze wala msishindane katika kupata kitu cha mtu mwengine wala msihusudiane wala msichukiane wala msiwakane nyongo, lakini kuweni enyi waja wa Allaah ndugu kama Alivyo waamuru. Muislamu ni ndugu wa Muislamu: hamdhulumu, wala haachi kumsaidia, wala hamdhuru. Uchamungu uko hapa - akaashiria kwenye kifua chake. Yamtosha mtu kuwa ni miongoni mwa shari kumdharau ndugu yake Muislamu. Kila Muislamu ni haramu kwa Muislamu mwenzake: damu yake, cheo chake na mali yake. Hakika Allaah Hatizami miili yenu wala sura zenu, lakini Anaangalia mioyo yenu na amali zenu."
Na katika riwaayah nyengine: "Msihusudiane, wala msichukiane, wala msipelelezane, wala msiulizie ulizie kuhusu makosa ya watu wengine, wala msiongezeane bei (pasina kuwa na haja ya kununua), lakini kuweni enyi waja wa Allaah ndugu."
Na katika riwaayah nyengine: "Wala msisusiane, wala msipeane nyongo, wala msichukiane, wala msihusudiane, lakini kuweni ndugu enyi waja wa Allaah."
Na katika riwaayah nyengine: "Wala msitengane, wala wasinunue baadhi yenu kilichokwisha kuuziwa wenzenu." [Muslim kwa riwaayah zote hizo, na Al-Bukhaariy amepokea nyingi miongoni mwa hizo riwaayah]
Hadiyth – 2
وعن معاوية رضي الله عنه قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقول : (( إنَّكَ إنِ اتَّبَعْتَ عَوْرَاتِ المُسْلِمينَ أفْسَدْتَهُمْ ، أَوْ كِدْتَ أنْ تُفْسِدَهُمْ )) . حديث صحيح ، رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Amesema Mu'awiyah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika ukifuata katika kuangazia makosa ya Waislamu utawafisidi (utawaharibu) au utaelekea katika kuwafisidi." [Hadiyth Swahiyh, Abuu Daawud kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 3
وعن ابن مسعود رضي الله عنه : أنَّهُ أُتِيَ بِرَجُلٍ فَقِيلَ لَهُ : هَذَا فُلاَنٌ تَقْطُرُ لِحْيَتُهُ خَمْراً ، فَقَالَ : إنَّا قَدْ نُهِيْنَا عَنِ التَّجَسُّسِ، ولكِنْ إنْ يَظْهَرْ لَنَا شَيْءٌ، نَأخُذ بِهِ . حديث حسن صحيح ، رواه أَبُو داود بإسنادٍ عَلَى شَرْطِ البخاري ومسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba aliletwa mtu kwake na kuambiwa: "Huyu ni fulani, ambaye ndevu zake zinanuka pombe." Akasema: "Hakika tumekatazwa jambo tunalichukua kama lilivyo." [Hadiyth Hasan Swahiyh, Abu Daawuwd kwa Isnaad nzuri kulingana na sharti zilizowekwa na Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن سوء الظنّ بالمسلمين من غير ضرورة
019-Mlango Wa Kukatazwa Kuwa na Dhana Mbaya kwa Waislamu Bila ya Dharura
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ ۖ ﴿١٢﴾
Enyi walioamini! Jiepusheni sana na dhana, kwani hakika baadhi ya dhana ni dhambi. [Al-Hujuraat: 12]
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إيَّاكُمْ والظَّنَّ ، فإنَّ الظَّنَّ أكْذَبُ الحَدِيثِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Tahadharini na dhana, kwani dhana ni uwongo mkubwa katika mazungumzo." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم احتقار المسلمين
020-Mlango Wa Kukatazwa Kuwadharau Waislamu
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ ۖ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ ۚ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴿١١﴾
Enyi walioamini! Wanaume wasiwafanyie dhihaka na kuwadharau wanaume wengineo asaa wakawa bora kuliko wao, wala wanawake kwa wanawake wengineo, asaa wakawa bora kuliko wao. Na wala msifedheheshane kwa kutukanana, na wala msiitane majina (mabaya) ya utani. Ubaya ulioje kuita jina la ufasiki baada ya Iymaan! Na yeyote asiyetubu, basi hao ndio madhalimu. [Al-Hujuraat: 11]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( بِحَسْبِ امْرِئٍ مِنَ الشَّرِّ أنْ يَحْقِرَ أَخَاهُ المُسْلِمَ )) . رواه مسلم ، وَقَدْ سبق قريباً بطوله .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Inatosha kwa mtu kuwa ni miongoni mwa watu wanaofanya shari kwa kumdharau ndugu yake Muislamu." [Muslim], na imetajwa karibuni kwa urefu.
Hadiyth – 2
وعن ابن مسعودٍ رضي الله عنه ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لا يَدْخُلُ الجَنَّةَ مَنْ كَانَ فِي قَلْبِهِ مِثْقَالُ ذَرَّةٍ مِنْ كِبْرٍ ! )) فَقَالَ رَجُلٌ : إنَّ الرَّجُلَ يُحِبُّ أَنْ يَكُونَ ثَوْبُهُ حَسَناً ، وَنَعْلُهُ حَسَنةً ، فَقَالَ : (( إنَّ اللهَ جَمِيلٌ يُحِبُّ الجَمَالَ ، الكِبْرُ : بَطَرُ الحَقِّ ، وَغَمْطُ النَّاسِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaah bin Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hataingia Peponi yeyote mwenye katika moyo wake chembe ya kiburi." Akasema mtu mmoja: "Hakika mtu anapenda kuwa na nguo nzuri na viatu vizuri?" Akasema: "Hakika Allaah ni Mzuri na anapenda vizuri. Kiburi ni kukataa haki na kudharau watu." [Muslim].
Hadiyth – 3
وعن جُندب بن عبدِ الله رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( قَالَ رَجُلٌ : وَاللهِ لا يَغْفِرُ اللهُ لِفُلانٍ ، فَقَالَ اللهُ عزوجل : مَنْ ذا الَّذِي يَتَأَلَّى عَلَيَّ أنْ لا أغْفِرَ لِفُلانٍ ! فَإنِّي قَدْ غَفَرْتُ لَهُ ، وَاحْبَطْتُ عَمَلَكَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake Jundub bin 'Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu mmoja alisema: Wa-Allaahi (Naapa kwa Allaah)! Allaah Hatamsamehe fulani." Allaah 'Azza wa Jalla akasema: "Ni mtu gani huyu anayeapa kwa jina Langu kuwa sitamsamehe fulani. Hakika Mimi nimemsamehe na Nimebatilisha amali yako." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن إظهار الشماتة بِالمُسْلِم
021-Mlango Wa Kukatazwa kufurahi kwa Baya Linalomkumba Muislamu
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ ﴿١٠﴾
Hakika Waumini ni ndugu [Al-Hujuraat: 10]
إِنَّ الَّذِينَ يُحِبُّونَ أَن تَشِيعَ الْفَاحِشَةُ فِي الَّذِينَ آمَنُوا لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ ﴿١٩﴾
Hakika wale wanaopenda uenee uchafu wa kashfa kwa wale walioamini, watapata adhabu iumizayo duniani na Aakhirah. [An-Nuwr: 19]
وعَن وَائِلَةَ بن الأسقع رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لا تُظْهِرِ الشَّمَاتَةَ لأَخِيكَ فَيَرْحَمَهُ اللهُ وَيَبْتَلِيكَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Waathilah bin Al-Asqa' (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usifurahi kwa msiba alioupata nduguyo hivyo Allaah Akamrehemu na akakutia wewe katika mtihani." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الطعن في الأنساب الثابتة في ظاهر الشرع
022-Mlango Wa Kukatazwa Kukashifu (Kutusi) Nasaba
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾
Na wale wanaowaudhi Waumini wa kiume na Waumini wa kike bila ya kuwa wamechuma kosa, basi kwa yakini wamejibebea usingiziaji mkuu wa dhulma na dhambi bayana. [Al-Ahzaab: 58]
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( اثْنَتَان في النَّاسِ هُمَا بهم كُفْرٌ : الطَّعْنُ فِي النَّسَبِ ، وَالنِّيَاحَةُ عَلَى المَيِّتِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mambo mawili wanayoyafanya watu ni katika matendo ya ukafiri: Kukashifu na kutusi ukoo wa mtu na kuomboleza maiti." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الغش والخداع
023-Mlango Wa Kukatazwa Kughushi na Kuhadaa
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾
Na wale wanaowaudhi Waumini wa kiume na Waumini wa kike bila ya kuwa wamechuma kosa, basi kwa yakini wamejibebea usingiziaji mkuu wa dhulma na dhambi bayana. [Al-Ahzaab: 58]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( مَنْ حَمَلَ عَلَيْنَا السِّلاَحَ فَلَيْسَ مِنَّا ، وَمَنْ غَشَّنَا فَلَيْسَ مِنَّا )) . رواه مسلم .
وفي رواية لَهُ : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، مَرَّ عَلَى صُبْرَةِ طَعَامٍ فَأدْخَلَ يَدَهُ فِيهَا فَنَالَتْ أصابِعُهُ بَلَلاً ، فَقَالَ : (( مَا هذَا يَا صَاحِبَ الطَّعَامِ ؟ )) قَالَ : أصَابَتهُ السَّمَاءُ يَا رسول الله . قَالَ : (( أفَلاَ جَعَلْتَهُ فَوقَ الطَّعَامِ حَتَّى يرَاهُ النَّاسُ ! مَنْ غشَّنَا فَلَيْسَ مِنَّا )) .
Imepokewa kutoka kwake Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kubeba silaha kupigana dhidi yetu, si katika sisi. Na mwenye kutughushi, si katika sisi." [Muslim]
Na katika riwaayah yake nyengine, kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita mbele ya chakula kilichokuwa kimewekwa, akaingiza mkono wake, hivyo vidole vyake kupata umande. Akasema: "Hii ni nini, ee mwenye chakula hiki?" Akajibu: "Kimenyeshwa na mvua, ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Kwa nini hukukiweka juu ya chakula ili kipate kuonekana na watu? Mwenye kutughushi, si katika sisi." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( لاَ تَنَاجَشُوا )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wala msiongezeane bei (pasina kuwa na haja ya kununua)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 3
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، نَهى عن النَّجْشِ . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikataza kuongezeana bei." [Al-Bukhaariy, Muslim, An-Nasaaiy na Ibn Maajah]
Hadiyth – 4
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : ذَكَرَ رَجُلٌ لِرَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم : أنَّهُ يُخْدَعُ في البُيُوعِ ؟ فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ بَايَعْتَ ، فَقُلْ : لاَ خِلاَبَةَ )) . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Alielezwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ya kuwa kuna mtu mmoja ambaye anadanganywa sana katika biashara. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Unapoingia katika biashara (kununua) na mtu yeyote mwambie, 'Hakuna udanganyifu'." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik, Abu Daawuwd na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 5
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ خَبَّبَ زَوْجَةَ امْرِئٍ ، أَوْ مَمْلُوكَهُ ، فَلَيْسَ مِنَّا )) . رواهُ أَبُو داود .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumharibu na kumhadaa mke wa mtu au kijakazi, basi si miongoni mwetu." [Abuu Daawuwd].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الغدر
024-Mlango Wa Kukatazwa Kuvunja Ahadi
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَوْفُوا بِالْعُقُودِ ۚ ﴿١﴾
Enyi walioamini! Timizeni mikataba. [Al-Maaidah: 1]
وَأَوْفُوا بِالْعَهْدِ ۖ إِنَّ الْعَهْدَ كَانَ مَسْئُولًا ﴿٣٤﴾
Na timizeni ahadi, hakika ahadi itakuwa ni ya kuulizwa. [Al-Israa: 34]
Hadiyth – 1
وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أرْبَعٌ مَنْ كُنَّ فِيهِ كَانَ مُنافِقاً خَالِصاً ، وَمَنْ كَانَتْ فِيهِ خَصْلَةٌ مِنْهُنَّ كَانَ فِيهِ خَصْلَةٌ مِنَ النِّفَاقِ حَتَّى يَدَعَها : إِذَا اؤْتُمِنَ خَانَ ، وَإِذَا حَدَّثَ كَذَبَ ، وَإِذَا عَاهَدَ غَدَرَ ، وَإِذَا خَاصَمَ فَجَرَ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu yeyote akiwa na mambo manne atakuwa mnafiki hasa, na kama atakuwa na moja katika hayo manne atakuwa na sifa moja ya unafiki mpaka aliache; kama akiaminiwa anaongopa; na anapotoa ahadi huvunja na anapogombana anaicha haki na kuwa jeuri." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن مسعودٍ ، وابن عمر ، وأنس رضي الله عنهم قالوا : قَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم : (( لِكُلِّ غادِرٍ لِواءٌ يَوْمَ القِيَامَةِ ، يُقَالُ : هذِهِ غَدْرَةُ فلانٍ )) . متفق عَلَيْهِ .
Wamesema Ibn Mas'uwd, na Ibn 'Umar na Anas (Radhwiya Allaahu 'anhum) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kwa kila mwenye kuvunja ahadi atakuwa na bendera (kama ishara na alama) Siku ya Qiyaamah na patatangazwa: 'Huyu ni yule aliyevunja ahadi na fulani." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي سعيدٍ الخدريّ رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لِكُلِّ غَادِرٍ لِوَاءٌ عِنْدَ اسْتِهِ يومَ القِيَامَةِ يُرْفَعُ لَهُ بِقَدَرِ غَدْرِهِ ، ألاَ وَلاَ غَادِرَ أعْظَمُ غَدْراً مِنْ أمِيرِ عَامَّةٍ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kwa kila mwenye kuvunja ahadi atakuwa na bendera watu wengine wakiwa nyuma yake Siku ya Qiyaamah ambayo atanyanyuliwa kiasi cha uvunjaji wake na ahadi. Sikilizeni na tanabahini! Hapana mvunjaji mkubwa wa ahadi kama amiri (kiongozi mabaye si mkweli kwa watu wake)." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( قَالَ الله تَعَالَى : ثَلاَثَةٌ أنا خَصْمُهُمْ يَوْمَ القِيَامَةِ : رَجُلٌ أعْطَى بي ثُمَّ غَدَرَ ، وَرَجُلٌ بَاعَ حُرَّاً فَأَكَلَ ثَمَنَهُ ، وَرَجُلٌ اسْتَأجَرَ أجيراً ، فَاسْتَوْفَى مِنْهُ ، وَلَمْ يُعْطِهِ أجْرَهُ )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah Ta'aalaa Amesema: 'Watu aina tatu Nitapigana nao Siku ya Qiyaamah; mtu anayeweka miadi kwa kuapa kwa jina Langu kisha akavunja ahadi hiyo; na mtu aliyemuuza mtu aliye huru kisha akala thamani yake; na mtu aliyemwajiri mtu mwengine ambaye alifanya kazi kamili lakini akakosa kumlipa ujira wake." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن المنِّ بالعطية ونحوها
025-Mlango Wa Kukatazwa Kumsimanga Mtu kwa Ulichompa na Mfano Wake
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُبْطِلُوا صَدَقَاتِكُم بِالْمَنِّ وَالْأَذَىٰ ﴿٢٦٤﴾
Enyi walioamini! Msibatilishe swadaqah zenu kwa masimbulizi na udhia [Al-Baqarah: 264]
الَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمْوَالَهُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ثُمَّ لَا يُتْبِعُونَ مَا أَنفَقُوا مَنًّا وَلَا أَذًى ۙ ﴿٢٦٢﴾
Wale wanaotoa mali zao katika Njia ya Allaah kisha hawafuatishii kwa waliyoyatoa masimbulizi wala udhia [Al-Baqarah: 262]
وعن أَبي ذَر رضي الله عنه ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( ثَلاَثَةٌ لاَ يُكَلِّمُهُمُ اللهُ يَوْمَ القِيَامَةِ ، وَلاَ يَنْظُرُ إلَيْهِمْ ، وَلاَ يُزَكِّيِهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَليمٌ )) قَالَ : فَقَرَأَهَا رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ثلاثَ مِرارٍ : قَالَ أَبُو ذرٍ : خَابُوا وخَسِرُوا مَنْ هُمْ يَا رسول الله ؟ قَالَ : (( المُسْبِلُ ، والمَنَّانُ ، وَالمُنْفِقُ سِلْعَتَهُ بالحَلِفِ الكَاذِبِ )) . رواه مسلم .
وفي روايةٍ لَهُ : (( المُسْبِلُ إزَارَهُ )) يَعْنِي : المُسْبِلَ إزَارَهُ وَثَوْبَهُ أسْفَلَ مِنَ الكَعْبَيْنِ لِلخُيَلاَءِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah Hatazungumza na watu aina tatu Siku ya Qiyaamah wala Hatawaangalia na wala Hatawatakasa na watakuwa na adhabu iumizayo." Akasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliikariri kauli hii mara tatu." Akasema Abu Dharr: "Watu hao wamehasirika, ni kina nani ee Rasuli wa Allaah?" Akasema: "Mwenye kuburuza nguo kwa kiburi; na mwenye kujionyesha kwa fadhila aliyomfanyia mtu mwengine; na mwenye kuuza mali duni kwa kiapo cha uongo." [Muslim]
Na katika riwaayah yake nyengine: "Mwenye kuburuza kikoi chake." Yaani: "Mwenye kuburuza kikoi chake na nguo yake chini ya kongo mbili kwa kiburi."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الافتخار والبغي
026-Mlango Wa Kukatazwa Kujifakhiri na Ujeuri
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
فَلَا تُزَكُّوا أَنفُسَكُمْ ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ اتَّقَىٰ ﴿٣٢﴾
Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa. [An-Najm: 32]
إِنَّمَا السَّبِيلُ عَلَى الَّذِينَ يَظْلِمُونَ النَّاسَ وَيَبْغُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ ۚ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ﴿٤٢﴾
Hakika sababu (ya kulaumiwa) ni juu ya wale wanaodhulumu watu na wanakandamiza katika ardhi bila ya haki. Hao watapata adhabu iumizayo. [Ash-Shuwraa: 42]
Hadiyth – 1
وعن عياضِ بن حمارٍ رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ اللهَ تَعَالَى أوْحَى إلَيَّ أنْ تَوَاضَعُوا حَتَّى لا يَبْغِيَ أَحَدٌ عَلَى أحَدٍ ، وَلاَ يَفْخَرَ أَحَدٌ عَلَى أحَدٍ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake 'Iyaadh bin Himaar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ta'aalaa Amenifunulia mimi kuwa niwe mnyenyekevu mpaka mtu mmoja asiwe mjeuri kwa mwengine wala asijifakhiri mtujuu ya mtu mwengine." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا قَالَ الرجُلُ : هَلَكَ النَّاسُ ، فَهُوَ أهْلَكُهُمْ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pindi anaposema mtu: Watu wameangamia (wamekufa), basi ni yeye ndiye aliyeangamia." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الهجران بين المسلمين فوق ثلاثة أيام
إِلاَّ لبدعة في المهجور ، أَوْ تظاهرٍ بفسقٍ أَوْ نحو ذَلِكَ
027-Mlango Wa Kukatazwa Kuhamana Baina ya Waislamu Wawili Zaidi ya Siku Tatu ila Ikiwa ni Mtu wa Bid'ah au Ufasiki na Mfano Wake
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ ﴿١٠﴾
Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu. [Al-Hujuraat: 10]
وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ ۚ ﴿٢﴾
Na wala msishirikiane katika dhambi na uadui. [Al-Maaidah: 2]
Hadiyth – 1
وعن أنس رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لا تَقَاطَعُوا ، وَلاَ تَدَابَرُوا ، وَلاَ تَبَاغَضُوا ، وَلاَ تَحَاسَدُوا ، وَكُونُوا عِبَادَ اللهِ إخْوَاناً ، وَلاَ يَحِلُّ لِمُسْلِمٍ أَنْ يَهْجُرَ أَخَاهُ فَوْقَ ثَلاَث )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wala msisusiane, wala msipeane nyongo, wala msichukiane, wala msihusudiane, lakini kuweni ndugu enyi waja wa Allaah. Na haifai kwa Muislamu kumhama nduguye zaidi ya siku tatu." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Hadiyth – 2
وعن أَبي أيوبَ رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( لا يَحِلُّ لِمُسْلِمٍ أنْ يَهْجُرَ أَخَاهُ فَوْقَ ثَلاَثِ لَيَالٍ : يَلْتَقِيَانِ ، فَيُعْرِضُ هَذَا ، وَيُعْرِضُ هَذَا ، وخَيْرُهُما الَّذِي يَبْدَأُ بِالسَّلاَمِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Ayyuwb (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Si halali kwa Muislamu kumhama nduguye kwa zaidi ya siku tatu kwa jinsi ya kwamba wanakutana huku kila mmoja akimpa nyongo mwenzake. Na mbora kati yao ni yule anayeanza kutoa salamu (kumsalimia mwenziwe)." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( تُعْرَضُ الأَعْمَالُ في كلِّ اثْنَيْنِ وَخَمْيسٍ ، فَيَغْفِرُ اللهُ لِكُلِّ امْرِئٍ لا يُشْرِكُ باللهِ شَيْئاً ، إِلاَّ امْرَءاً كَانَتْ بَيْنَهُ وَبَيْنَ أخِيهِ شَحْنَاءُ ، فَيقُولُ : اتْرُكُوا هذَيْنِ حَتَّى يَصْطَلِحَا )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Milango ya Pepo hufunguliwa siku ya Jumatatu na Alkhamis, hivyo kusamehewa kila mja asiyemshirikisha Allaah kwa kitu chochote isipokuwa mtu ambaye ana uadui (utesi) baina yake na nduguye. Atasema: 'Waacheni hawa wawili mpaka wafanye mapatano baina yao! Waacheni hawa wawili mpaka wafanye mapatano baina yao!." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن جابر رضي الله عنه قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( إنَّ الشَّيْطَانَ قَدْ يَئِسَ أنْ يَعْبُدَهُ المُصَلُّونَ فِي جَزِيرَةِ العَرَبِ ، وَلَكِنْ في التَّحْرِيشِ بَيْنَهُمْ )) . رواه مسلم .
Amesema Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika shetani amevunjika moyo kabisa kuwa hataabudiwa na Waislamu (wenye kuswali) katika Bara Arabu, hivyo anajaribu kuleta utesi na kuleta ufisadi baina yao na kubadilisha mioyo yao." [Muslim].
Hadiyth – 5
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ يَحِلُّ لِمُسْلِمٍ أنْ يَهْجُرَ أخَاهُ فَوْقَ ثَلاَثٍ ، فَمَنْ هَجَرَ فَوْقَ ثَلاَثٍ فَمَاتَ ، دَخَلَ النَّارَ )) . رواه أَبُو داود بإسناد عَلَى شرط البخاري ومسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haifai kwa Muislamu kumhama nduguye zaidi ya siku tatu. Na yeyote atakaye mhama mwenziwe zaidi ya siku tatu akafa (katika hali hiyo) ataingia motoni." [Abu Daawuwd kwa Isnaad zinazo afikiana na masharti ya Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أَبي خِراشٍ حَدْرَدِ بنِ أَبي حَدْرَدٍ الأسلميِّ . ويقالُ : السُّلمِيّ الصحابي رضي الله عنه : أنَّه سمع النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( مَنْ هَجَرَ أخَاهُ سَنَةً فَهُوَ كَسَفْكِ دَمِهِ )) . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Abu Khiraash Hadrad bin Abu Hadrad Al-Aslamiyy na pia anajulikana kama As-Sulamiyy As-Swahabiy (ambaye ni Swahaaba) (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa alimsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Yeyote anayemhama nduguye mwaka mzima ni kama amemwaga damu yake (yaani amemuua). [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh].
Hadiyth – 7
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنًّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَحِلُّ لِمُؤْمِنٍ أنْ يَهْجُرَ مُؤْمِناً فَوقَ ثَلاَثٍ ، فإنْ مَرَّتْ بِهِ ثَلاَثٌ ، فَلْيَلْقَهُ فَلْيُسَلِّمْ عَلَيْهِ ، فَإنْ رَدَّ عَلَيْهِ السَّلامَ فَقَدِ اشْتَرَكَا في الأجْرِ ، وَإنْ لَمْ يَرُدَّ عَلَيْهِ فَقَدْ بَاءَ بِالإثْمِ ، وَخَرَجَ المُسَلِّمُ مِنَ الهِجْرَةِ )) . رواه أَبُو داود بإسناد حسن . قَالَ أَبُو داود : (( إِذَا كَانَتْ الهِجْرَةُ للهِ تَعَالَى فَليسَ مِنْ هَذَا في شَيْءٍ ))
Imepokewa kutoka kwake Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haifai kwa Muumini kumhama nduguye Muumini kwa zaidi ya siku tatu. Baada ya siku tatu, inafaa aende kukutana naye na kumsalimia. Ikiwa atajibu hiyo salamu basi wote wawili wameshirikiana katika thawabu. Na ikiwa hatajibu hiyo salamu basi atakuwa na dhambi, na yule wa kwanza (aliyetoa salamu) atajivua na jukumu la kuhamana (na kukata urafiki)." [Abu Daawuwd, kwa Isnaad iliyo Swahiyh]. Amesema Abu Daawuwd: "Ikiwa kutozungumza ni kwa ajili ya Allaah Ta'aalaa, hatakuwa na dhambi yoyote."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن تناجي اثنين دون الثالث بغير إذنه
إِلاَّ لحاجةٍ وَهُوَ أن يتحدثا سراً بحيث لا يسمعهما وفي معناه مَا إِذَا تحدثا
بلسان لا يفهمه
028-Mlango Wa Kukatazwa Kunong'onezana Wawili Pasina wa Tatu Bila Idhini yake Isipokuwa kwa Haja (Dharura)
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّمَا النَّجْوَىٰ مِنَ الشَّيْطَانِ ﴿١٠﴾
Hakika mnong’ono unatokana na shaytwaan [Al-Mujaadalah: 10]
Hadiyth – 1
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إِذَا كانُوا ثَلاثَةً ، فَلاَ يَتَنَاجَى اثْنَانِ دُونَ الثَّالِثِ )) . متفق عَلَيْهِ .
ورواه أَبُو داود وزاد : قَالَ أَبُو صالح : قُلْتُ لابنِ عُمرَ : فَأرْبَعَةً ؟ قَالَ : لا يَضُرُّكَ .
ورواه مالك في "الموطأ" : عن عبد الله بن دينارٍ ، قَالَ : كُنْتُ أنَا وابْنُ عُمَرَ عِنْدَ دَارِ خَالِدِ بنُ عُقْبَةَ الَّتي في السُّوقِ ، فَجَاءَ رَجُلٌ يُريدُ أنْ يُنَاجِيَهُ ، وَلَيْسَ مَعَ ابْنِ عُمَرَ أَحَدٌ غَيْرِي ، فَدَعَا ابْنُ عُمَرَ رَجُلاً آخَرَ حَتَّى كُنَّا أَرْبَعَةً ، فَقَالَ لِي وَللرَّجُلِ الثَّالِثِ الَّذِي دَعَا : اسْتَأْخِرَا شَيْئاً ، فَإنِّي سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يقُولُ : (( لا يَتَنَاجَى اثْنَانِ دُونَ وَاحِدٍ )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mkiwa watu wa tatu (katika kikao), wawili kati yao wasinong'onezane bila ya yule wa tatu." [Al-Bukhaary, Muslim, Abu Daawuwd na Maalik].
Na amepokea Abu Daawuwd na akaongeza: Amesema Abu Swaalih: "Nilimuuliza Ibn 'Umar: Je wakiwa watu wane?" Akasema: "Katika hali hiyo hatakuwa na madhara yoyote (hapa tatizo)."
Na amepokea Maalik katika Al-Muwatwa kwamba 'Abdillaah bin Dinaar amesema: "Nilikuwa pamoja na Ibn 'Umar ndani ya nyumba ya Khaalid bin 'Uqbah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye alikuwa sokoni. Alikuja mtu ambaye alitaka kumnong'oneza na hakukuwa na mtu mwengine isipokuwa mimi. Ibn 'Umar alimuita mtu mwengine na hivyo tukawa watu wane. Hapo akaniambia mimi na yule mtu wa tatu aliyemuita, jiongeeni kidogo kwani nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: 'Hawanong'onezani watu wawili na kumuacha mmoja kando."
Hadiyth – 2
وعن ابن مسعود رضي الله عنه : أنَّ رسول اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إِذَا كُنْتُمْ ثَلاَثَةً ، فَلاَ يَتَنَاجَى اثْنَانِ دُونَ الآخَرِ حَتَّى تَخْتَلِطُوا بِالنَّاسِ ، مِنْ أجْلِ أنَّ ذَلِكَ يُحْزِنُهُ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Munapokuwa watu watatu, wasinong'onezane watu wawili pasina yule watatu mapak mchanganyikane na watu wengine, kwani jambo hilo litamhuzunisha sana." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن تعذيب العبد والدابة
والمرأة والولد بغير سبب شرعي أَوْ زائد عَلَى قدر الأدب
029-Mlango Wa Kukatazwa Kumuadhibu Mtumwa na Mnyama na Mwanamke na Mtoto Bila ya Sababu ya Kisheria au Zaidi ya Kile Kiwango cha Kutia Adabu
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَبِذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ وَالْجَارِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَالْجَارِ الْجُنُبِ وَالصَّاحِبِ بِالْجَنبِ وَابْنِ السَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ مُخْتَالًا فَخُورًا ﴿٣٦﴾
Na wafanyieni ihsaan wazazi wawili na jamaa wa karibu, na mayatima, na masikini na jirani mwenye ujamaa na jirani asiye na ujamaa na rafiki wa karibu, na msafiri aliyeishiwa masurufu, na wale iliyowamiliki mikono yenu ya kulia. Hakika Allaah Hapendi mwenye majivuno mwenye kujifakharisha. [An-Nisaa: 36]
Hadiyth – 1
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( عُذِّبَتِ امْرَأَةٌ في هِرَّةٍ سَجَنَتْها حَتَّى مَاتَتْ ، فَدَخَلَتْ فِيهَا النَّارَ ، لاَ هِيَ أَطْعَمَتْهَا وَسَقَتْهَا ، إذْ حَبَسَتْهَا ، وَلاَ هِيَ تَرَكَتْهَا تَأكُلُ مِنْ خَشَاشِ الأَرْضِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ameadhibiwa mwanamke kwa sababu ya paka aliyemfunga mpaka akafa, akaingizwa motoni kwa ajili ya jambo hilo, kwani alipomfunga hakumpa chakula wala hakumpa maji, na wala hakumwacha ale vijidudu vya ardhi." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وَعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّهُ مَرَّ بِفِتْيَانٍ مِنْ قُرَيْشٍ قَدْ نَصَبُوا طَيراً وَهُمْ يَرْمُونَهُ ، وَقَدْ جَعَلُوا لِصَاحِبِ الطَّيْرِ كُلَّ خَاطِئَةٍ مِنْ نَبْلِهمْ ، فَلَمَّا رَأَوْا ابْنَ عُمَرَ تَفَرَّقُوا ، فَقَالَ ابْنُ عُمَرَ : مَنْ فَعَلَ هَذَا ؟ لَعَنَ اللهُ مَنْ فَعَلَ هَذَا ، إنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم لَعَنَ مَنِ اتَّخَذَ شَيْئاً فِيهِ الرُّوحُ غَرَضاً . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa walipita vijana wa Ki-Quraysh, wakiwa wamemshika ndege na wanamlenga shabaha. Hakika ni kuwa walikuwa wamepanga na mwenye ndege kuwa mishale yote itakayokosa shabaha itakuwa yake. Walipomuona Ibn 'Umar walikimbia. Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) akauliza: "Nani alifanya hivi?" Allaah Amlaani aliyefanya jambo hili. Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amemlaani yeyote anayelenga shabaha kitu chenye roho." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أنس رضي الله عنه قَالَ : نهى رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم أن تُصْبَرَ البَهَائِمُ . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Amekataza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwanyima wanyama chakula mpaka wafe." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي عليٍّ سويدِ بن مُقَرِّنٍ رضي الله عنه قَالَ : لَقَدْ رَأَيْتُنِي سَابِعَ سَبْعَةٍ مِنْ بَنِي مُقَرِّنٍ مَا لَنَا خَادِمٌ إِلاَّ وَاحِدَةٌ لَطَمَهَا أصْغَرُنَا فَأَمَرَنَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم أنْ نُعْتِقَهَا . رواه مسلم .
وفي روايةٍ : (( سَابعَ إخْوَةٍ لِي )) .
Amesema Abu 'Aliy Suwayd bin Muqarrin (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilikuwa mimi mmoja katika watu saba wa ukoo wa Bani Muqarrin na hatukuwa na mtumwa ila mmoja tu. Mdogo wetu kabisa alimpiga kofi, kwa ajili hiyo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alituamuru tumuache huru. [Muslim].
Na katika riwaayah nyengine: "Nilikuwa na ndugu saba."
Hadiyth – 5
وعن أَبي مسعودٍ البدْرِيِّ رضي الله عنه قَالَ: كُنْتُ أضْرِبُ غُلامَاً لِي بالسَّوْطِ، فَسَمِعْتُ صَوْتاً مِنْ خَلْفِي : (( اعْلَمْ أَبَا مَسْعُودٍ )) فَلَمْ أفْهَمِ الصَّوْتِ مِنَ الغَضَبِ ، فَلَمَّا دَنَا مِنِّي إِذَا هُوَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم ، فإذا هُوَ يَقُولُ : (( اعْلَمْ أَبَا مَسْعُودٍ أنَّ اللهَ أقْدَرُ عَلَيْكَ مِنْكَ عَلَى هَذَا الغُلامِ )) . فَقُلتُ : لا أضْرِبُ مَمْلُوكاً بَعْدَهُ أَبَداً .
وَفِي روايةٍ : فَسَقَطَ السَّوْطُ مِنْ يَدِي مِنْ هَيْبَتِهِ .
وفي روايةٍ : فَقُلتُ : يَا رسولَ الله ، هُوَ حُرٌّ لِوَجْهِ اللهِ تَعَالَى ، فَقَالَ : (( أمَا لَوْ لَمْ تَفْعَلْ ، لَلَفَحَتْكَ النَّارُ ، أَوْ لَمَسَّتْكَ النَّارُ )) . رواه مسلم بهذه الروايات .
Amesema Abu Mas'uwd Al-Badriy (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilikuwa mara moja nikimpiga mtumwa wangu na koboko, nikasikia sauti nyuma yangu: "Tanabahi na ujue, ee Abu Mas'uwd." Sikufahamu sauti hiyo kwa ghadhabu nilizokuwa nazo. Alipofika karibu nami, ndipo nilipojua kuwa ni Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naye alikuwa anasema: "Tanabahi na ujue, ee Abu Mas'uwd! Hakika Allaah ana uwezo na nguvu zaidi kuliko ulio nao juu ya mtumwa huyu." Nikamwambia: "Sitampiga mtumwa baada ya leo milele."
Na katika riwaayah nyengine: "Kiboko kikaanguka kutoka katika mkono wangu kwa haiba yake."
Na katika riwaayah nyengine: Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Huyu mtumwa wangu yupo huru kwa ajili ya kutaka radhi za Allaah Ta'aalaa." Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Lau hukufanya hivyo, ungechomwa katika moto au moto ungekugusa." [Muslim kwa riwaayah zote hizi].
Hadiyth – 6
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ ضَرَبَ غُلاَمَاً لَهُ حَدّاً لَمْ يَأتِهِ ، أَوْ لَطَمَهُ ، فإنَّ كَفَارَتَهُ أنْ يُعْتِقَهُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumuadhibu mtumwa wake kwa kumpiga au kumchapa kofi la uso bila ya makosa yoyote, kafara yake itakuwa ni kumuacha huru (mtumwa huyo)." [Muslim]
Hadiyth – 7
وعن هِشام بن حكيمِ بن حِزَامٍ رضي الله عنهما : أنَّه مَرَّ بالشَّامِ عَلَى أُنَاسٍ مِنَ الأَنْبَاطِ ، وَقَدْ أُقيِمُوا في الشَّمْسِ ، وَصُبَّ عَلَى رُؤُوسِهِمُ الزَّيْتُ ! فَقَالَ : مَا هَذَا ؟ قيل : يُعَذَّبُونَ في الخَرَاجِ - وفي رواية : حُبِسُوا في الجِزْيَةِ - فَقَالَ هِشَامٌ : أشهدُ لَسَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( إنَّ اللهَ يُعَذِّبُ الَّذِينَ يُعَذِّبُونَ النَّاس في الدُّنْيَا )) . فَدَخَلَ عَلَى الأمِيرِ ، فَحَدَّثَهُ ، فَأَمَرَ بِهِمْ فَخُلُّوا . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake Hishaam bin Hakiym bin Hizaam (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa alipita Shaam (Syria) na akawaona watu wa Anbaat (masikini wakulima wasiokuwa Waislamu wala Waarau) waliokuwa wamesimamishwa kwenye jua na wakamiminiwa mafuta vichwani. Akasema (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Hii ni nini?" Akaambiwa: "Wanaadhibiwa ili waweze kutoa ushuru." Na katika riwaayah nyengine: "Wamefungwa kwa ajili ya kupata jizya kutoka kwao." Hishaam alisema: "Nashuhudia ya kwamba nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: 'Hakika Allaah Atawaadhibu wale ambao kwamba wanawaadhibu watu hapa duniani." Baada ya hapo alikwenda kwa Amiri na kumwelezea kuhusu Hadiyth hii. Amiri aliamuru watu hao waachiliwe (wasiwe ni wenye kuadhibiwa)." [Muslim]
Hadiyth – 8
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : رأى رسولُ الله صلى الله عليه وسلم حِمَاراً مَوْسُومَ الوَجْهِ ، فَأَنْكَرَ ذَلِكَ ؟ فَقَالَ : (( واللهِ لا أسِمُهُ إِلاَّ أقْصَى شَيْءٍ مِنَ الوَجْهِ )) وأمَرَ بِحِمَارِهِ فَكُوِيَ في جَاعِرَتَيْهِ ، فَهُوَ أوَّلُ مَنْ كَوَى الجَاعِرَتَيْنِ . رواه مسلم .
Amesema Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimuona punda aliyekuwa ametiwa alama kwenye uso wake, alikataza jambo hilo na kuchukizwa sana. Akasema Ibn 'Abbaas: "Wa-Allaahi! Sitamtia alama punda wangu isipokuwa sehemu iliyo mbali sana na uso wake." Aliamuru punda wake aletwe na atiwe alama kwenye mapaja yake, hivyo akawa wa kwanza katika kutia alama punda kwenye mapaja. [Muslim]
Hadiyth – 9
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم مَرَّ عَلَيْهِ حِمَارٌ قَدْ وُسِمَ في وَجْهِهِ ، فَقَالَ : (( لَعَنَ اللهُ الَّذِي وَسَمَهُ )) . رواه مسلم .
وفي رواية لمسلم أَيضاً: نهى رسول الله صلى الله عليه وسلم عَنِ الضَّرْبِ في الوَجْهِ ، وَعَنِ الوَسْمِ في الوَجْهِ
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa mara moja punda alipita mbele ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa ametiwa alama kwenye uso wake. Akasema: "Allaah Amlaani yule aliyemtia alama usoni mwake." [Muslim].
Na katika riwaayah ya Muslim: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kupigwa mnyama kwenye uso na kutiwa alama sehemu hiyo."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم التعذيب بالنار
في كل حيوان حَتَّى النملة ونحوها
030-Mlango Wa Kuharamishwa Kuadhibu Mnyama Yoyote Hata Chungu na Mfano Wake Kutumia Moto
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ : بعثنا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم في بَعْثٍ، فَقَالَ : (( إنْ وَجَدْتُمْ فُلاَناً وَفُلاناً )) لِرَجُلَيْنِ مِنْ قُرَيْشٍ سَمَّاهُمَا (( فَأَحْرِقُوهُمَا بالنَّارِ )) ثُمَّ قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم حِيْنَ أرَدْنَا الخرُوجَ: (( إنِّي كُنْتُ أَمَرْتُكُمْ أنْ تُحْرِقُوا فُلاناً وفُلاناً ، وإنَّ النَّارَ لا يُعَذِّبُ بِهَا إِلاَّ الله ، فإنْ وَجَدْتُمُوهُما فاقْتُلُوهُما )) . رواه البخاري.
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alituma kikosi kwa ajili ya Jihadi, na akawaambia: "Mukimpata fulani na fulani (akawataja watu wawili wa Ki-Quraysha) wachomeni kwa moto." Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akatuambia tulipokuwa tayari kuondoka: "Hakika nilikuwa nimewaamuru muwachome fulani na fulani, lakini ni Allaah tu Anayeadhibu kwa moto. Hivyo mukiwapata wauweni." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن ابن مسعودٍ رضي الله عنه قَالَ : كنَّا مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم في سَفَرٍ ، فانْطَلَقَ لحَاجَتِهِ ، فَرَأيْنَا حُمَّرَةً مَعَهَا فَرْخَانِ ، فَأَخَذْنَا فَرْخَيْهَا ، فَجَاءتِ الحُمَّرَةُ فَجَعَلَتْ تَعْرِشُ فَجَاءَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ : (( مَنْ فَجَعَ هذِهِ بِوَلَدِهَا ؟ ، رُدُّوا وَلَدَهَا إِلَيْها )) . ورأَى قَرْيَةَ نَمْلٍ قَدْ حَرَّقْنَاهَا ، فَقَالَ : (( مَنْ حَرَّقَ هذِهِ ؟ )) قُلْنَا : نَحْنُ قَالَ : (( إنَّهُ لا يَنْبَغِي أنْ يُعَذِّبَ بالنَّارِ إِلاَّ رَبُّ النَّارِ )) . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح
Amesema Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu): Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika safari na tuliposimama sehemu kwa mapumziko, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliondoka kwenda kutekeleza haja yake. Tulimuona ndege mwekundu pamoja na watoto wake wawili. Tulivichukua vitoto vyake, yule mama alifadhaika sana kuona hayo na akaanza kupiga ardhi kwa mbawa zake. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alirudi na kuuliza: "Ni nani aliyemtatiza ndege huyu kwa kuchukua watoto wake? Warudisheni vitoto vyake." Na baada ya hapo akaona kichuguu (kijiji cha chungu) kimechomwa, akasema: "Kwa hakika haifai yeyote kuadhibu kwa moto isipokuwa Rabb wa moto." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم مطل الغني بحقٍّ طلبه صاحبه
031-Mlango Wa Kuharamishwa kwa Mtu Mwenye Uwezo Kukataa Kulipa Deni
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا ﴿٥٨﴾
Hakika Allaah Anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe. [An-Nisaa: 58]
فَإِنْ أَمِنَ بَعْضُكُم بَعْضًا فَلْيُؤَدِّ الَّذِي اؤْتُمِنَ أَمَانَتَهُ ﴿٢٨٣﴾
Na ikiwa mmoja wenu amewekewa amana na mwengine, basi airudishe yule ambaye ameaminiwa amana ya mwenzake [Al-Baqarah: 283]
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَطْلُ الغَنِيِّ ظُلْمٌ، وَإِذَا أُتْبعَ أَحَدُكُمْ عَلَى مَلِيءٍ فَلْيَتْبَع )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haifai kwa tajiri kukwepa kulipa deni, ni dhulma. Na mmoja wenu atakaposhawishiwa kwa mwenye uwezo, basi na akubali." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة عود الإنسان في هبة لَمْ يُسلِّمها
إِلَى الموهوب لَهُ وفي هبة وهبها لولده وسلمها أَوْ لَمْ يسلمها
وكراهة شرائه شَيْئاً تصدّق بِهِ من الَّذِي تصدق عَلَيْهِ
أَوْ أخرجه عن زكاة أَوْ كفارة ونحوها
وَلاَ بأس بشرائه من شخص آخر قَدْ انتقل إِلَيْهِ
032-Mlango Wa Karaha ya Kurudisha Hiba (Zawadi) Ambayo Bado Hajaikabidhi kwa Mwenye Kupewa, na Hiba Aliyompa Mtoto Wake na Akaipokea au Hata Kama Hakuipokea, Karaha ya Kununua Kitu Alichokitoa Swadaqah kutoka kwa Aliyempa Swadaqah au Zakaa au Kafara na Mfano Wake, Wala Hakuna Ubaya Kuinunua Kutoka kwa Mtu Mwingine Ambae Imehamia Kwake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن ابن عباس رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( الَّذِي يَعُودُ في هِبَتِهِ كَالكَلْبِ يَرْجِعُ في قَيْئِهِ )) . متفق عَلَيْهِ .
وفي رواية : (( مَثَلُ الَّذِي يَرْجِعُ في صَدَقَتِهِ ، كَمَثَلِ الكَلْبِ يَقِيءُ ، ثُمَّ يَعُودُ في قَيْئِهِ فَيَأكُلُهُ )) .
وفي روايةٍ : (( العائِدُ في هِبَتِهِ كالعائِدِ في قَيْئِهِ )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuirudia zawadi yake ni kama mbwa aliyekula matapishi yake." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Na katika riwaayah nyengine: "Mfano wa mwenye kurudia swadaqah yake ni kama mfano wa mbwa anaye tapika, kisha akayarudia matapishi yake na kuyala."
Na katika riwaayah: "Mwenye kuirudia zawadi ni kama mwenye kuyarudia matapishi yake."
Hadiyth – 2
وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه قَالَ : حَمَلْتُ عَلَى فَرَسٍ في سَبيلِ اللهِ فَأَضَاعَهُ الَّذِي كَانَ عِندَهُ ، فَأَرَدْتُ أن أشْتَرِيَهُ ، وَظَنَنْتُ أنَّهُ يَبِيعُهُ بِرُخْصٍ ، فَسَأَلْتُ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : (( لاَ تَشْتَرِهِ وَلاَ تَعُدْ فِي صَدَقَتِكَ وإنْ أعْطَاكَهُ بِدِرْهَمٍ ؛ فَإنَّ العَائِدَ في صَدَقَتِهِ كَالعَائِدِ في قَيْئِهِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Amesema 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilimtoa farasi wangu swadaqah kwa ajili ya Jihadi katika njia ya Allaah, lakini yule niliyempatia alikuwa hamtizami vyema, hivyo nikafikiria kumnunua kutoka kwake na nikadhania kuwa angemuuza kwa bei nafuu. Nikamuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu jambo hilo, naye akaniambia: "Usimnunue na wala usiirudie swadaqah yako hata kama atakupa kwa dirhamu moja, kwani bila shaka anyeirudia swadaqah yake ni sawa na aliyeyarudia matapishi yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تأكيد تحريم مال اليتيم
033-Mlango Wa Uharamu wa Kula Mali ya Yatima
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَىٰ ظُلْمًا إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا ۖ وَسَيَصْلَوْنَ سَعِيرًا ﴿١٠﴾
Hakika wale wanaokula mali ya mayatima kwa dhulma hapana shaka kwamba wanakula katika matumbo yao moto, na watauingia moto uliowashwa vikali mno. [An-Nisaa: 10]
وَلَا تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلَّا بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ ﴿١٥٢﴾
Na wala msiikaribie mali ya yatima isipokuwa kwa njia njema ya manufaa [Al-An'aam: 152]
وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْيَتَامَىٰ ۖ قُلْ إِصْلَاحٌ لَّهُمْ خَيْرٌ ۖ وَإِن تُخَالِطُوهُمْ فَإِخْوَانُكُمْ ۚ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ الْمُفْسِدَ مِنَ الْمُصْلِحِ ۚ ﴿٢٢٠﴾
Na wanakuuliza kuhusu mayatima. Sema: Kuwatengenezea (ya kuwafaa) ni kheri zaidi. Na mkichanganya mambo yenu na yao basi hao ni ndugu zenu. Na Allaah Anamjua fisadi na mtengenezaji. [Al-Baqarah: 220]
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( اجْتَنِبُوا السَّبْعَ المُوبِقَاتِ ! )) قالُوا : يَا رَسُولَ اللهِ ، وَمَا هُنَّ ؟ قَالَ : (( الشِّرْكُ باللهِ ، والسِّحْرُ ، وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتي حَرَّمَ اللهُ إِلاَّ بالحَقِّ ، وأكلُ الرِّبَا ، وأكْلُ مَالِ اليَتِيمِ ، والتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ ، وقَذْفُ المُحْصَنَاتِ المُؤْمِنَاتِ الغَافِلاَتِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Jiepusheni na madhambi saba yanayoangamiza." Watu wakauliza: "Ee Rasuli wa Allaah ni yepi hayo?" Akasema: "Kumshirikisha Allaah, na uchawi, na kuua nafsi ambayo Allaah Ameiharamisha isipokuwa kwa haki, na kula riba, kula mali ya yatima, kukimbia siku ya vita na kuwatuhumu kwa zinaa wanawake waliohifadhiwa na Allaah, Waumini wasiyo na habari ya zinaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تغليظ تحريم الربا
034-Mlango Wa Ukubwa wa uharamu wa Riba
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
الَّذِينَ يَأْكُلُونَ الرِّبَا لَا يَقُومُونَ إِلَّا كَمَا يَقُومُ الَّذِي يَتَخَبَّطُهُ الشَّيْطَانُ مِنَ الْمَسِّ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ قَالُوا إِنَّمَا الْبَيْعُ مِثْلُ الرِّبَا ۗ وَأَحَلَّ اللَّـهُ الْبَيْعَ وَحَرَّمَ الرِّبَا ۚ فَمَن جَاءَهُ مَوْعِظَةٌ مِّن رَّبِّهِ فَانتَهَىٰ فَلَهُ مَا سَلَفَ وَأَمْرُهُ إِلَى اللَّـهِ ۖ وَمَنْ عَادَ فَأُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ ۖ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿٢٧٥﴾
Wale wanaokula riba hawatosimama (Siku ya Qiyaamah) ila kama anavyosimama yule aliyezugwa na shaytwaan kwa kuguswa na kupatwa. Hivyo kwa sababu wao wamesema: Hakika biashara ni kama riba. Na Allaah Amehalalisha biashara na Ameharamisha riba. Na atakayefikiwa na mawaidha kutoka kwa Rabb wake akakoma, basi ni yake yale yaliyopita, na hukumu yake iko kwa Allaah. Na atakayerudia basi hao ni watu wa motoni, wao humo ni wenye kudumu.
يَمْحَقُ اللَّـهُ الرِّبَا وَيُرْبِي الصَّدَقَاتِ ۗ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ كَفَّارٍ أَثِيمٍ ﴿٢٧٦﴾
Allaah Huifuta baraka (mali ya) riba na Huzibariki swadaqah. Na Allaah Hampendi kila aliye mwingi wa kukufuru apapiae madhambi.
إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَآتَوُا الزَّكَاةَ لَهُمْ أَجْرُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ وَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ﴿٢٧٧﴾
Hakika wale walioamini na wakatenda mema na wakasimamisha Swalaah na wakatoa Zakaah, (hao) watapata ujira wao kutoka kwa Rabb wao, na wala hakuna khofu juu yao na wala wao hawatohuzunika.
Enyi walioamini! Mcheni Allaah na acheni yaliyobakia katika riba ikiwa nyinyi ni Waumini. [Al-Baqarah: 275-278]
وعن ابن مسعود رضي الله عنه قَالَ: لَعَنَ رسول الله صلى الله عليه وسلم آكِلَ الرِّبَا وَمُوكِلَهُ . رواهُ مسلم ، زاد الترمذي وغيره : وَشَاهِدَيْهِ وَكَاتِبَهُ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Amemlani mwenye kula riba na mwenye kumuwakilisha. [Muslim]. Na akaongeza At-Tirmidhiy na wengineo na mashahidi wake na muadhishi wake.
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الرياء
035-Mlango Wa Uharamu wa Riya
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ ﴿٥﴾
Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah hali ya kuwa ni wenye kumtakasia Dini, wenye kujiengua na upotofu kuelemea Dini ya haki [Al-Bayyinah: 5]
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُبْطِلُوا صَدَقَاتِكُم بِالْمَنِّ وَالْأَذَىٰ كَالَّذِي يُنفِقُ مَالَهُ رِئَاءَ النَّاسِ ﴿٢٦٤﴾
Enyi walioamini! Msibatilishe swadaqah zenu kwa masimbulizi na udhia kama yule ambaye anatoa mali yake kwa kujionyesha kwa watu [Al-Baqarah: 264]
يُرَاءُونَ النَّاسَ وَلَا يَذْكُرُونَ اللَّـهَ إِلَّا قَلِيلًا ﴿١٤٢﴾
Wakijionyesha kwa watu na wala hawamdhukuru Allaah isipokuwa kidogo tu. [An-Nisaa: 142]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( قَالَ الله تَعَالَى : أنَا أغْنَى الشُّرَكَاءِ عَنِ الشِّرْكِ ، مَنْ عَمِلَ عَمَلاً أشْرَكَ فِيهِ مَعِي غَيْرِي تَرَكْتُهُ وَشِرْكَهُ )) . رواه مسلم .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Amesema Allaah Ta'aalaa: Mimi ni mkwasi kwa wenye kunishirikisha kutokana na shirki hiyo. Mwenye kufanya amali ambayo kwayo Amenishirikisha Mimi na mwengine, Nitamuacha yeye na shirki yake." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول : (( إنَّ أَولَ النَّاسِ يُقْضَى يَومَ القِيَامَةِ عَلَيْهِ رَجُلٌ اسْتُشْهِدَ ، فَأُتِيَ بِهِ ، فَعَرَّفَهُ نِعْمَتَهُ ، فَعَرَفَهَا ، قَالَ : فَمَا عَمِلْتَ فِيهَا ؟ قَالَ : قَاتَلْتُ فِيكَ حَتَّى اسْتُشْهِدْتُ . قَالَ : كَذَبْتَ ، وَلَكِنَّكَ قَاتَلْتَ لأَنْ يُقَالَ : جَرِيءٌ ! فَقَدْ قِيلَ ، ثُمَّ أُمِرَ بِهِ فَسُحِبَ عَلَى وَجْهِهِ حَتَّى أُلْقِيَ في النَّارِ. وَرَجُلٌ تَعَلَّمَ العِلْمَ وَعَلَّمَهُ ، وَقَرَأَ القُرآنَ ، فَأُتِيَ بِهِ فَعَرَّفَهُ نِعَمَهُ فَعَرَفَهَا . قَالَ: فَمَا عَمِلْتَ فِيهَا ؟ قَالَ : تَعَلَّمْتُ العِلْمَ وَعَلَّمْتُهُ ، وَقَرَأتُ فِيكَ القُرآنَ ، قَالَ : كَذَبْتَ ، وَلكِنَّكَ تَعَلَّمْتَ لِيُقَالَ : عَالِمٌ ! وَقَرَأتَ القُرْآنَ لِيُقَالَ : هُوَ قَارِئٌ ؛ فَقَدْ قِيلَ ، ثُمَّ أُمِرَ بِهِ فَسُحِبَ عَلَى وَجْهِهِ حَتَّى أُلْقِيَ في النَّارِ . وَرَجُلٌ وَسَّعَ اللهُ عَلَيْهِ ، وَأعْطاهُ مِنْ أصْنَافِ المَالِ ، فَأُتِيَ بِهِ فَعَرَّفَهُ نِعَمَهُ ، فَعَرَفَهَا . قَالَ : فَمَا عَمِلْتَ فِيهَا ؟ قَالَ: مَا تَرَكْتُ مِنْ سَبيلٍ تُحِبُّ أنْ يُنْفَقَ فِيهَا إِلاَّ أنْفَقْتُ فِيهَا لَكَ. قَالَ : كَذَبْتَ ، ولكِنَّكَ فَعَلْتَ لِيُقَالَ : جَوَادٌ ! فَقَدْ قِيلَ ، ثُمَّ أُمِرَ بِهِ فَسُحِبَ عَلَى وَجْهِهِ حَتَّى أُلْقِيَ في النَّارِ )) . رواه مسلم .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: Hakika mtu wa kwanza atakaye hukumiwa Siku ya Qiyaamah ni mtu aliyekufa shahidi (vitani). Ataletwa na kuonyeshwa neema zote alizopatiwa, naye atakubali. Ataulizwa: "Ulizitumia vipi neema hizo?" Atajibu: "Nilipigana kwa ajili yako mpaka nikafa." Ataambiwa: "Umesema uwongo, hakika wewe ulipigana ili uitwe: Shujaa! Kwa hakika uliitwa hivyo." Kisha Ataamrisha ashikwe kwenye paji lake la uso, akokotwe mpaka motoni. Mtu mwengine ni yule aliyejifunza elimu na akaifundisha na akaisoma Qur-aan Ataletwa na kuonyeshwa neema zote alizopatiwa, naye atakubali. Ataulizwa na kusoma Qur-aan kwa ajili yako." Ataambiwa: "Umesema uwongo, hakika wewe ulijifunza ili uitwe: Mwanachuoni! Na ulisoma Qur-aan ili uitwe Qaari (msomaji mzuri wa Qur-aan). Kwa hakika uliitwa hivyo." Kisha Ataamrisha ashikwe mpaka atiwe motoni. Na mtu mwengine ni yule aliyepanuliwa na Allaah, na akapatiwa aina zote za mali. Ataletwa na kuonyeshwa neema zote alizopatiwa, naye atakubali. Ataulizwa: "Ulizitumia vipi neema hizo?" Atajibu: "Hakuna njia yoyote ambayo Unapenda itolewe mali kwayo isipokuwa nilitoa kwa ajili yako." Ataambiwa: "Umesema uwongo, lakini wewe ulifanya hivyo ili uitwe: Mtoaji sana! Kwa hakika uliitwa hivyo." Kisha ataamrisha ashikwe mpaka motoni." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أن نَاساً قَالُوا لَهُ : إنَّا نَدْخُلُ عَلَى سَلاَطِيننَا فَنَقُولُ لَهُمْ بِخِلاَفِ مَا نَتَكَلَّمُ إِذَا خَرَجْنَا مِنْ عِندِْهِمْ ؟ قَالَ ابنُ عُمَرَ رضي الله عنهما : كُنَّا نَعُدُّ هَذَا نِفاقاً عَلَى عَهْدِ رسول الله صلى الله عليه وسلم . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba kulikuja watu waliomuuliza: "Hakika sisi tunaingia kwa sultani wetu na kumwambia yeye kinyume na yale tunayozungumza tunapotoka kwake." Akasema: "Hakika sisi tulikuwa tukiona jambo hilo kuwa ni nifaki (unafiki) katika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 4
وعن جُندب بن عبد اللهِ بن سفيان رضي الله عنه قَالَ : قَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ سَمَّعَ سَمَّعَ الله بِهِ ، وَمَنْ يُرائِي يُرائِي اللهُ بِهِ )) . متفق عَلَيْهِ .
ورواه مسلم أَيضاً من رواية ابن عباس رضي الله عنهما .
Imepokewa kutoka kwake Jundub bin 'Abdillaah bin Sufyaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kutaka asikike (kwa lile alilofanya ili watu wamsifu) Allaah Atamfanya asikike kwa hilo (kwa kuonyesha niya yake ya hakika Siku ya Qiyaamah), na yule mwenye kujonyesha, Allaah Atamuonyesha kwa hicho (kuionyesha nia yake halisi, kwa kumdhalilisha)." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Na Muslim ameipokea Hadiyth hii kutokana na riwaayah ya Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa).
Hadiyth – 5
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ تَعَلَّمَ عِلْماً مِمَّا يُبْتَغَى بِهِ وَجْهُ اللهِ عزوجل لاَ يَتَعَلَّمُهُ إِلاَّ لِيُصِيبَ بِهِ عَرَضاً مِنَ الدُّنْيَا ، لَمْ يَجِدْ عَرْفَ الجَنَّةِ يَوْمَ القِيَامَةِ )) . رواه أَبُو داود بإسنادٍ صحيحٍ
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kujifunza elimu, ambayo huwa ni kwa ajili ya kupata radhi za Allaah Ta'aalaa, kisha mtu akajifunza si kwa lengo hilo isipokuwa apate mapato ya kidunia hatapata harufu ya Pepo Siku ya Qiyaamah." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يتوهم أنَّه رياء وليس هُوَ رياء
036-Mlango Wa Mambo Yanayodhaniwa ni Riya Lakini si Riya
Alhidaaya.com [4]
وعن أَبي ذرٍ رضي الله عنه قَالَ : قِيلَ لِرسولِ الله صلى الله عليه وسلم : أرَأيْتَ الرَّجُلَ الَّذِي يَعْمَلُ العَمَلَ مِنَ الخَيْرِ ، وَيَحْمَدُهُ النَّاسُ عَلَيْهِ ؟ قَالَ : (( تِلْكَ عَاجِلُ بُشْرَى المُؤْمِنِ )) . رواه مسلم .
Amesema Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu): Aliulizwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Unaonaje kwa mtu ambaye anafanya amali za kheri na watu wakawa wanamsifu kwa hayo?" Akasema: "Hii bishara ya haraka kwa Muumini." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم النظر إِلَى المرأة الأجنبية والأمرد الحسن
لغير حاجة شرعية
037-Mlango Wa Uharamu wa Kumwangalia Mwanamke wa Kando na Mvulana Mzuri Bila Haja ya Kisheria
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
قُل لِّلْمُؤْمِنِينَ يَغُضُّوا مِنْ أَبْصَارِهِمْ ﴿٣٠﴾
Waambie Waumini wanaume wainamishe macho yao [An-Nuwr: 30]
إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولَـٰئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْئُولًا ﴿٣٦﴾
Hakika masikio na macho na moyo; vyote hivyo vitaulizwa. [Al-Israa: 36]
يَعْلَمُ خَائِنَةَ الْأَعْيُنِ وَمَا تُخْفِي الصُّدُورُ﴿١٩﴾
(Allaah) Anajua khiyana za macho na yale yanayoficha vifua. [Ghaafir: 19]
إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤﴾
Hakika Rabb wako bila shaka Yu tayari Anaziona nyenendo zao zote. [Al-Fajr: 14]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( كُتِبَ عَلَى ابْن آدَمَ نَصِيبُهُ مِنَ الزِّنَا مُدْرِكُ ذَلِكَ لا مَحَالَةَ : العَيْنَانِ زِنَاهُمَا النَّظَرُ ، وَالأُذُنَانِ زِنَاهُمَا الاسْتِمَاعُ ، وَاللِّسَانُ زِناهُ الكَلاَمُ ، وَاليَدُ زِنَاهَا البَطْشُ ، وَالرِّجْلُ زِنَاهَا الخُطَا ، والقَلْبُ يَهْوَى وَيَتَمَنَّى ، وَيُصَدِّقُ ذَلِكَ الفَرْجُ أَوْ يُكَذِّبُهُ )) . متفق عَلَيْهِ . هَذَا لفظ مسلمٍ ، ورواية البخاري مختصرَةٌ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema kwamba: "Binaadamu huandikiwa sehemu yake ya zinaa, hilo humpata bila ya matatizo: Macho mawili zinaa yao ni kuangalia; na masikio mawili zinaa yao ni kusikia; na ulimi zinaa yake ni mazungumzo; na mkono zinaa yake ni kushika (yaliyo haramu); na mguu zinaa yake ni kutembea (kuyaendelea yaliyo haramu); na moyo nao hutamani, na husadikisha hayo utupu wake au hukataa (kuyaendea)." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni tamishi la Muslim. Na Al-Bukhaariy ameipokea kwa muhtasari].
Hadiyth – 2
وعن أَبي سعيد الخُدريِّ رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إيّاكُمْ والجُلُوس فِي الطُّرُقَاتِ ! )) قالوا : يَا رسولَ الله ، مَا لَنَا مِنْ مَجَالِسِنَا بُدٌّ ، نَتَحَدَّثُ فِيهَا . فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( فَإذَا أبَيْتُمْ إِلاَّ المَجْلِسَ ، فَأَعْطُوا الطَّرِيقَ حَقَّهُ )) قَالُوا : وَمَا حَقُّ الطَّريقِ يَا رسولَ اللهِ ؟ قَالَ : (( غَضُّ البَصَرِ ، وَكَفُّ الأَذَى ، وَرَدُّ السَّلاَمِ ، والأمرُ بالمَعْرُوفِ ، والنَّهيُ عنِ المُنْكَرِ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nawatahadharisha nyinyi katika kukaa kwenu njiani." Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, ikiwa hapana budi kukaa (katika sehemu hizo) kwani tunazungumza na kujadiliana ndani yake." Wakauliza: Rasuli wa Allaah: " Ikiwa ni hivyo basi ipatieni njia yake." Akawaambia: "Na haki za njia ni zipi ee Rasuli wa Allaah?" Akasema: "Kuinamisha macho chini, na kuondoa uchafu (pingamizi), na kurudisha salamu, na kuamrisha mema na kukataza maovu." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي طلحة زيد بن سهل رضي الله عنه قَالَ : كُنَّا قُعُوداً بالأفْنِيَةِ نَتَحَدَّثُ فِيهَا فَجَاءَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم فَقَامَ عَلَيْنَا ، فَقَالَ : (( مَا لَكُمْ وَلِمَجَالسِ الصُّعُدَاتِ ؟ اجْتَنِبُوا مَجَالِسَ الصُّعُدَاتِ )) فقُلْنَا : إنَّمَا قَعَدْنَا لِغَيْرِ مَا بَأسٍ ، قَعَدْنَا نَتَذَاكَرُ ، وَنَتَحَدَّثُ . قَالَ : (( إمَّا لاَ فَأَدُّوا حَقَّهَا : غَضُّ البَصَرِ ، وَرَدُّ السَّلاَمِ ، وَحُسْنُ الكَلاَمِ )) . رواه مسلم .
Kutoka kwa Abu Twalha Zayd bin Sahl (Radhwiya Allaahu 'anhu): Tulikuwa tumekaa na huku tunazungumza kwenye baraza mara Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaja na kusimama mbele yetu. Akauliza: "MUna nini nyinyi mbona munakaa kwenye njia? Jiepusheni na vikao vya barabarani." Tukasema: "Hakika sisi tumekaa kwa mambo yasiyo na matatizo na kwa nia nzuri. Tumekaa tunakumbuka na kuzungumza." Akasema: "Ikiwa hamuna budi mpaka mukae katika sehemu hizo basi ipatieni barabara haki yake: Kuinamisha macho chini, na kurudisha salamu, na kuzungumza maneno mazuri." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن جرير رضي الله عنه قَالَ : سألت رسول الله صلى الله عليه وسلم عن نَظَرِ الفَجْأَةِ فَقَالَ : (( اصْرِفْ بَصَرَكَ )) . رواه مسلم .
Amesema Jariyr (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu kumtizama mwanamke kwa bahati mbaya (bila ya kukusudia)? Akasema: "Geuza macho yako (upande mwingine)." [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أُم سَلَمَة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : كنتُ عِنْدَ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، وعندهُ مَيْمُونَة ، فَأقْبَلَ ابنُ أُمِّ مَكْتُومٍ ، وَذَلِكَ بَعْدَ أنْ أُمِرْنَا بِالحِجَابِ فَقَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( احْتَجِبَا مِنْهُ )) فَقُلْنَا : يَا رسولَ اللهِ ، ألَيْسَ هُوَ أعْمَى ! لاَ يُبْصِرُنَا ، وَلاَ يَعْرِفُنَا ؟ فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( أفَعَمْيَاوَانِ أنتُما أَلَسْتُمَا تُبْصِرَانِهِ !؟ )) . رواه أَبُو داود والترمذي، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Amesema Ummu Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nilikuwa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pamoja na Maymunah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) na mara akaingia Ibn Maktuwm. Tukio hili lilitokea baada ya kuwa tumeamriwa kuvaa hijabu. Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Jifinikeni kutokana naye." Tukasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, yeye si ni kipofu, hatuoni sisi wala hatujui?" Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Nanyi pia ni vipofu. Je, nyinyi hamumuoni?" [Abu Daawuwd an At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 6
وعن أَبي سعيد رَضِيَ اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَنْظُرُ الرَّجُلُ إِلَى عَوْرَةِ الرَّجُلِ ، وَلاَ المَرْأَةُ إِلَى عَوْرَةِ المَرْأَةِ ، وَلاَ يُفْضِي الرَّجُلُ إِلَى الرَّجُلِ في ثَوْبٍ وَاحِدٍ ، وَلاَ تُفْضي المَرْأةُ إِلَى المَرْأَةِ في الثَّوْبِ الواحِدِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asiangalie mwanaume utupu wa mwanaume mwenziwe, wala mwanamke utupu wa mwanamke mwenziwe. Asijifunike mwanaume katika shuka moja na mwanaume mwenziwe wala mwanamke asijifunike na mwanamke mwenziwe ndani ya shuka moja." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الخلوة بالأجنبية
038-Mlango Wa Kukaa Faragha na Mwanamke wa Kando
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاءِ حِجَابٍ ۚ ﴿٥٣﴾
Na mnapowauliza wake zake haja, waulizeni nyuma ya pazia. [Al-Ahzaab: 53]
Hadiyth – 1
وعن عقبة بن عامر رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إيَّاكُمْ وَالدُّخُولَ عَلَى النِّسَاءِ ! )) فَقَالَ رَجُلٌ مِنَ الأنْصَارِ : أفَرَأيْتَ الحَمْوَ ؟ قَالَ : (( الحَمْوُ المَوْتُ ! )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Uqbah bin 'Aamir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Jiepushenina kuwazuru wanawake (wasio maharimu zenu)." Akauliza mtu miongoni mwa Answaar: "Unaonaje kuhusu Hamwa?" (Ni jamaa wa karibu wa mume kama ndugu, na mtoto wa ndugu yake na mtoto wa ami yake, na kadhalika). Akasema: "Huyu Hamwa ni mauti (ni hatari zaidi)." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن ابن عباس رضي الله عنهما : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( لاَ يَخْلُونَّ أَحَدكُمْ بامْرَأَةٍ إِلاَّ مَعَ ذِي مَحْرَمٍ )) . متفق عَليْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asikae faragha mmoja wenu na mwanamke isipokuwa awe pamoja na maharimu yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن بُريدَةَ رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( حُرْمَةُ نِسَاءِ المُجَاهِدِينَ عَلَى القَاعِدِينَ كَحُرْمَةِ أُمَّهَاتِهِمْ ، مَا مِنْ رَجُلٍ مِنَ القَاعِدِيْنَ يَخْلُفُ رَجُلاً مِنَ المُجَاهِدِينَ في أهْلِهِ ، فَيَخُونُهُ فِيهِمْ إِلاَّ وَقَفَ لَهُ يَوْمَ القِيَامَةِ ، فَيَأْخُذُ مِنْ حَسَنَاتِهِ مَا شَاءَ حَتَّى يَرْضى )) ثُمَّ التَفَتَ إلَيْنَا رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: (( مَا ظَنُّكُمْ ؟ )). رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Uharamu wa wanawake wa Mujahidina kwa wenye kubakia nyuma ni kama uharamu wa mama zao. Hapana mtu miongoni mwa walio baki nyuma atakaye kuwa mwangalizi wa familia ya mtu miongoni mwa Mujahidina, kisha akamhini isipokuwa atamsimamia Siku ya Qiyaamah na kuchukua thawabu zake anazotaka mpaka aridhike." Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitugeukia sisi na kusema: "Je, munadhania nini?" [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم تشبه الرجال بالنساء
وتشبه النساء بالرجال في لباس وحركة وغير ذَلِكَ
039-Mlango Wa Uharamu wa Wanaume Kushabihiana na Wanawake na Kinyume Chake Katika Mavazi, Mwendo na Mengineo
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : لَعَنَ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم المُخَنَّثِينَ مِنَ الرِّجَالِ ، وَالمُتَرَجِّلاَتِ مِنَ النِّسَاءِ .
وفي رواية : لَعَنَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم المُتَشَبِّهِينَ مِنَ الرِّجَالِ بالنِّسَاءِ ، والمُتَشَبِّهَاتِ مِنَ النِّسَاءِ بالرِّجَالِ . رواه البخاري .
Amesema Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amewalaani wanaume wenye kuwaiga wanawake na wanawake wenye kuwaiga wanaume.
Na katika riwaayah nyengine: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amewalaani wanaume wenye kujishabahisha na wanawake, na wanawake wenye kujifananisha na wanaume." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ : لَعَنَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم الرَّجُلَ يَلْبَسُ لِبْسَةَ المَرْأَةِ ، والمَرْأَةَ تَلْبِسُ لِبْسَةَ الرَّجُلِ . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amemlaani mwanaume mwenye kuvaa vazi la mwanamke na mwanake anayevaa vazi la mwanaume." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( صِنْفَانِ مِنْ أهْلِ النَّارِ لَمْ أَرَهُمَا : قَومٌ مَعَهُمْ سِيَاطٌ كَأذْنَابِ البَقَرِ يَضْرِبُونَ بِهَا النَّاسَ ، وَنِسَاءٌ كَاسِيَاتٌ عَارِيَاتٌ مُمِيلاَتٌ مَائِلاَتٌ ، رُؤُوسُهُنَّ كَأَسْنِمَةِ البُخْتِ المائِلَةِ لاَ يَدْخُلْنَ الجَنَّةَ ، وَلاَ يَجِدْنَ رِيحَهَا ، وإنَّ رِيحَهَا لَيُوجَدُ مِنْ مَسِيرَةِ كَذَا وَكذَا )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuili wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Aina mbili ya watu ni watu wa motoni, bado sijawaona: Watu wenye mijeledi sawa na mikia ya ng'ombe wanayoitumia kupiga watu. Na pia wanawake waliovaa nguo (Kaasiyaat) lakini wapo uchi ('Aariyaat) ambao hugeuza mabega yao kwa maringo na kutembea mwendo wa kimalaya. Vichwa vyao vitakuwa kama nundu ya ngamia (yaani wanazifanya vikubwa kwa kujifunga kilemba au kitambara kichwani au mfano wake). Hawataingia Peponi wala hata kuisikia harufu yake, japokuwa harufu yake itasikika masafa kadhaa na kadhaa." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن التشبه بالشيطان والكفار
040-Mlango Wa Kukatazwa Kujifananisha na Shetani na Makafiri
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن جابر رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَأكُلُوا بِالشِّمَالِ ، فَإنَّ الشَّيْطَانَ يَأكُلُ ويَشربُ بِالشِّمَالِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usile kwa mkono wa kushoto, kwani shetani anakula na kunywa kwa mkono wa kushoto." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَأكُلَنَّ أَحَدُكُمْ بِشِمَالِهِ ، وَلاَ يَشْرَبَنَّ بِهَا ، فَإنَّ الشَّيْطَانَ يَأْكُلُ بِشِمَالِهِ وَيَشْرَبُ بِهَا )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asile mmoja wenu kwa mkono wa kushoto wala ainywe nao, kwani shetani anakula kwa mkono wa kushoto na kunywa nao." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ اليَهُودَ وَالنَّصَارى لاَ يَصْبغُونَ ، فَخَالِفُوهُمْ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Mayahudi na Manaswara (wakiristo) hawatii rangi nywele zao, hivyo fanyeni kinyume na wao." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب نهي الرجل والمرأة عن خضاب شعرهما بسواد
041-Mlango Wa Kukatazwa Mwanaume na Mwanamke Kutia Rangi Nyeusi katika Nywele zao
Alhidaaya.com [4]
عن جابر رضي الله عنه قَالَ : أُتِيَ بِأَبِي قُحَافَةَ والِدِ أَبي بَكْرٍ الصِّدِّيقِ رضي الله عنهما ، يَومَ فَتْحِ مَكَّةَ وَرَأسُهُ وَلِحْيَتُهُ كَالثَّغَامَةِ بَيَاضاً . فَقَالَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( غَيِّرُوا هَذَا وَاجْتَنِبُوا السَّوَادَ )) . رواه مسلم .
Amesema Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu): Aliletwa Abu Quhaafah, babake Abu Bakar As-Swiddiyq (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) siku iliyofunguliwa Makkah na ilhali kichwa chake na ndevu zake zilikuwa nyeupe pepepe mfano wa Thaghaamah (ni mti unaotoa maua na matunda meupe). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Mbadilisheni hii (rangi yake ya nywele) na jiepusheni na rangi nyeusi." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن القَزَع وَهُوَ حلق بعض الرأس
دون بعض ، وإباحة حَلْقِهِ كُلّهِ للرجل دون المرأة
042-Mlango Wa Kukatazwa Kunyoa na Kubakishia Vijisehemu Visivyo Nyolewa (Denge) na Kukubaliwa Kunyoa Zote kwa Wanaume na Wala si kwa Wanawake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : نهَى رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم عن القَزَعِ . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kunyoa na kubakisha vijisehemu bila ya kuvinyoa. [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : رأَى رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم صَبِيّاً قَدْ حُلِقَ بَعْضُ شَعْرِ رَأسِهِ وَتُرِكَ بَعْضُهُ ، فَنَهَاهُمْ عَنْ ذَلِكَ ، وقال : (( احْلِقُوهُ كُلَّهُ ، أَوِ اتْرُكُوهُ كُلَّهُ )) . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح عَلَى شرط البخاري ومسلم .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimuona mtoto ambaye amekatwa nywele sehemu moja ya kichwa chake na kuachwa sehemu nyengine, akawakataza jambo hilo. Na akasema: "Mnyoweni zote (nywele) au mwacheni zote." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh kulingana na sharti ya Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عبد الله بن جعفر رضي الله عنهما : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، أمْهَلَ آلَ جَعْفَر ثَلاَثاً ثُمَّ أتَاهُمْ فَقَالَ : (( لاَ تَبْكُوا عَلَى أخِي بَعْدَ اليَوْمِ )) ثُمَّ قَالَ : (( ادْعُوا لِي بَنِي أَخِي )) فَجِيءَ بِنَا كَأنَّنَا أفْرُخٌ فَقَالَ : (( ادْعُوا لِي الحَلاَّقَ )) فَأمرَهُ ، فَحَلَقَ رُؤُوسَنَا . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح عَلَى شرط البخاري ومسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Ja'far (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaruhusu watoto wa Ja'far kuwa na huzuni kwa ajili yake kwa muda wa siku tatu. Kisha akaja kwao na kuwaambia: "Musilie kwa ajili ya ndugu yangu baada ya leo." Kisha akasema: "Niitieni watoto wa ndugu yangu." Kwa ajili ya huzuni tuliyokuwa nayo hali yetu ilikuwa kama vifaranga. Akasema: "Niitieni kinyozi." (Alipofika) alimuamuru atunyoe, naye (kinyozi) akafanya hivyo." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh kulingana na sharti ya Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 4
وعن عليٍّ رضي الله عنه قَالَ : نَهَى رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم أنْ تَحْلِقَ المَرْأةُ رَأسَهَا . رواه النسائي .
Amesema 'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amewakataza wanawake kunyoa nywele za vichwa vyao. [An-Nasaaiy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم وصل الشعر والوشم
والوشر وهو تحديد الأسنان
043-Mlango Wa Uharamu wa Kuunganisha Nywele, Kuchanjwa na Kujaliza Meno
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِن يَدْعُونَ مِن دُونِهِ إِلَّا إِنَاثًا وَإِن يَدْعُونَ إِلَّا شَيْطَانًا مَّرِيدًا ﴿١١٧﴾
Hawaombi badala Yake isipokuwa miungu ya kike na hawaombi isipokuwa shaytwaan muasi.
لَّعَنَهُ اللَّـهُ ۘ وَقَالَ لَأَتَّخِذَنَّ مِنْ عِبَادِكَ نَصِيبًا مَّفْرُوضًا ﴿١١٨﴾
Allaah Amemlaani. Na (shaytwaan) akasema: Kwa hakika nitashika katika waja Wako sehemu maalumu.
وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا ﴿١١٩﴾
Na hakika nitawapoteza, na nitawashawishi matamanio ya kulaghai, na nitawaamrisha. Basi watakata masikio ya wanyama (wawatukuze), na nitawaamrisha watabadili Uumbaji wa Allaah. Na atakayemfanya shaytwaan kuwa rafiki mwandani badala ya Allaah basi kwa yakini amekhasirika khasara bayana. [An-Nisaa: 117-119]
Hadiyth – 1
وعن أسماءَ رضي الله عنها : أنَّ امْرَأَةً سَأَلَتِ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَتْ : يا رسولَ اللهِ إنَّ ابْنَتِي أصَابَتْهَا الحَصْبَةُ ، فَتَمَرَّقَ شَعْرُهَا ، وإنّي زَوَّجْتُهَا ، أفَأَصِلُ فِيهِ ؟ فقالَ : (( لَعَنَ اللهُ الوَاصِلَةَ وَالمَوْصُولَةَ )) . متفق عليه .
وفي روايةٍ : (( الوَاصِلَةَ ، والمُسْتوْصِلَةَ )) .
Imepokewa kutoka kwa Asmaa (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba mwanamke fulani alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ee Rasuli wa Allaah! Binti yangu amepatwa na surua zikapuputika nywele zake, nami nimemuozesha; Je, niziunganishe?" Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamjibu: "Allaah Amemlaani mwenye kuunganisha nywele zake (au nywele za mwengine kwa nywele nyengine) na mwenye kuungwa (au kuvaa nywele hizo)." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaaiy]
Na katika riwaayah nyengine: "Mwenye kuunganisha nywele na mwenye kumtaka mwengine amfanyie kazi hiyo (mwenye kutamani kuzivaa nywele hizo za bandia)."
Hadiyth – 2
وعن حُميدِ بنِ عبد الرحْمانِ : أنَّهُ سَمِعَ مُعَاوِيَةَ رضي الله عنه ، عامَ حَجَّ على المِنْبَرِ وَتَنَاوَلَ قُصَّةً مِنْ شَعْرٍ كَانَتْ في يَدِ حَرَسِيٍّ فَقَالَ : يَا أهْلَ المَدِينَةِ أيْنَ عُلَمَاؤُكُمْ ؟! سَمِعتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، يَنْهَى عَنْ مِثْلِ هذِهِ ، ويقُولُ : (( إنَّمَا هَلَكَتْ بَنُوإسْرَائِيلَ حينَ اتَّخَذَهَا نِسَاؤُهُمْ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Humayd bin 'Abdur-Rahmaan kuwa alimsikia Mu'awiyah (Radhwiya Allaahu 'anhu), mwaka wa Hijjah, akiwa juu ya mimbari, akiwa ameshika nywele zilizokatwa katika mikono ya Harasiy (mtoto wa Amiri), akasema: "Enyi watu wa Madiynah! Wako wapi wanazuoni wenu? Nimemsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akikataza tabia hii (nywele za bandia) na alikuwa akisema: 'Hakika walihiliki Bani Israiyl pale wake zao walipo ichukua tabia hii (ya kuunganisha nywele).' [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 3
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم لَعَنَ الوَاصِلَةَ والمُسْتَوْصِلَةَ ، والوَاشِمَةَ والمُسْتَوشِمَةَ . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amemlaani mwenye kuunganisha nywele zake na mwenye kutaka mwengine amuunganishe nywele hizo na mchanjaji kwenye mwili na mwenye kuchanjwa. [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy].
Hadiyth – 4
وعن ابن مسعود رضي الله عنه قال : لَعَنَ اللهُ الوَاشِمَاتِ والمُسْتَوشِمَاتِ وَالمُتَنَمِّصَاتِ ، والمُتَفَلِّجَاتِ لِلْحُسْنِ ، المُغَيِّرَاتِ خَلْقَ الله ، فَقَالَتْ لَهُ امْرَأَةٌ في ذَلِكَ فَقَالَ : وَمَا لِي لاَ ألْعَنُ مَنْ لَعَنَهُ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وَهُوَ فِي كِتَابِ اللهِ ؟ قالَ اللهُ تعالى : [ وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانْتَهُوا ] [ سورة الحشر : 7 ] . متفق عليه .
Amesema Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu): Allaah Amewalaani wenye kuchanja, na wenye kuchanjwa, na wenye kunyoa nyusi, na wenye kuchonga meno kwa urembo, na wenye kubadilisha umbile la Allaah. Akamuuliza yeye mwanamke kuhusu jambo hilo. Akamjibu kwa kusema: "Kwa nini nisimlaani yule aliyelaaniwa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na aliyelaaniwa katika Kitabu cha Allaah. Amesema Allaah Ta'aalaa: 'Na lolote analokupeni Rasuli basi lichukueni, na analokukatazeni, basi jiepusheni' [Al-Hashr: 7]." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nisaaiy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن نتف الشيب من اللحية
والرأس وغيرهما ، وعن نتف الأمرد شعر لحيته عند أول طلوعه
044-Mlango Wa Kukatazwa Kung'oa Mvi Kwenye Ndevu, Kichwa na Sehemu Nyengineyo na Kunyoa Ndevu kwa Kijana
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عمرو بن شعيب ، عن أبيهِ ، عن جَدِّهِ رضي الله عنه ، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَ تَنْتِفُوا الشَّيْبَ ؛ فَإنَّهُ نُورُ المُسْلِمِ يَوْمَ القِيَامَةِ )) حديث حسن ، رواه أبو داود، والترمذي، والنسائي بأسانيد حسنة ، قال الترمذي : (( هو حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Amruw bin Shu'ayb kutoka kwa babake kutoka kwa babu yake (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Musing'oe mvi kwani hizo ni nuru ya Musliamu Siku ya Qiyaamah." [Hadiyth Hasan iliyopokewa na Abu Daawuwd, na At-Tirmidhiy, na An-Nasaaiy kwa Isnaad zilizo Hasan (nzuri). Na amesema At-Tirmidhiy kuwa hii ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 2
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ عَمِلَ عَمَلاً لَيْسَ علَيْهِ أمْرُنَا فَهُوَ رَدٌّ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kufanya amali isiyokuwa na hukumu yetu, itakataliwa." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الاستنجاء باليمين
ومس الفرج باليمين من غير عذر
045-Mlango Wa Karaha ya Kustanji kwa Mkono wa Kulia na Kuishika Dhakari Yake kwa Mkono wa Kulia Bila Udhuru
Alhidaaya.com [4]
وعن أبي قتادة رضي الله عنه ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( إذا بَالَ أَحَدُكُمْ ، فَلاَ يَأخُذَنَّ ذَكَرَهُ بِيَمِينِهِ ، وَلاَ يَسْتَنْجِ بِيَمِينِهِ ، وَلاَ يَتَنَفَّسْ فِي الإنَاءِ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapokojoa mmoja wenu asiishike dhakari yake kwa mkono wake wa kuume na asistanji kwa mkono wake wa kuume wala asipumue katika chombo (anapokunywa kinywaji)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة المشي في نعل واحدة أو خف واحد
لغير عذر وكراهة لبس النعل والخف قائماً لغير عذر
046-Mlango Wa Karaha ya Kutembea na Kiatu Kimoja au Soksi Moja Bila Udhuru Wowote na Karaha ya Kuvaa Viatu au Soksi kwa Kusimama Bila Udhuru
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَيَمشِ أحَدُكُمْ فِي نَعْلٍ وَاحِدَةٍ ، لِيَنْعَلْهُمَا جَمِيعاً ، أو لِيَخْلَعْهُمَا جَمِيعاً )) .
وفي رواية : (( أو لِيُحْفِهِمَا جَمِيعاً )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asitembee mmoja wenu na kiatu kimoja, na avae vyote au avue vyote."
Na katika riwaayah nyengine: "Au aiache miguu yote mitupu (atembee bila viatu)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أبي هريرة رضي الله عنه ، قال : سمعت رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إذا انْقَطَعَ شِسْعُ نَعْلِ أَحَدِكمْ ، فَلاَ يَمْشِ في الأُخْرَى حَتَّى يُصْلِحَهَا )) . رواهُ مسلم .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Unapokatika ukanda mmoja wa kiatu cha mmoja wenu, asitembee na kile kiatu chengine mpaka akitengeneze (akirekebihse)." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن جابر رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم نَهَى أنْ يَنْتَعِلَ الرَّجُلُ قَائِماً . رواه أبو داود بإسناد حسن .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amemkataza mtu kuvaa viatu akiwa amesimama." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن ترك النار في البيت عند النوم
ونحوه سواء كانت في سراج أو غيره
047-Mlango Wa Kukatazwa Kuacha Moto katika Nyumba Wakati wa Kulala na Mfano Wake Kama Taa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَ تَتْرُكُوا النَّارَ فِي بُيُوتِكُمْ حِينَ تَنَامُونَ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Musiache moto katika nyumba zenu wakati munapolala." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه ، قال : احْتَرَقَ بَيْتٌ بالمَدِينَةِ عَلَى أهْلِهِ مِنَ اللَّيْلِ ، فَلَمَّا حُدِّثَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم بِشَأنِهِم ، قالَ : (( إنَّ هذِهِ النَّارَ عَدُوٌّ لَكُمْ ، فَإذا نِمْتُمْ ، فَأطْفِئُوهَا )) متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: "IIiungua nyumba moja Madiynah juu ya wenyewe usiku mmoja. Alipoelezewa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu jambo hilo alisema: 'Hakika huu m oto ni adui kwenu, hivyo mukienda kulala uzimeni'." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن جابر رضي الله عنه ، عن رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( غَطُّوا الإنَاءَ ، وَأَوْكِئُوا السِّقَاءَ ، وَأَغْلِقُوا الأَبْوَابَ . وَأطْفِئُوا السِّرَاجَ ، فإنَّ الشَّيْطَانَ لاَ يَحُلُّ سِقَاءً ، وَلاَ يَفْتَحُ بَاباً ، وَلاَ يَكْشِفُ إنَاءً . فإنْ لَمْ يَجِدْ أَحَدُكُمْ إلاَّ أنْ يَعْرُضَ عَلَى إنَائِهِ عُوداً ، وَيَذْكُرَ اسْمَ اللهِ ، فَلْيَفْعَل ، فإنَّ الفُوَيْسِقَةَ تُضْرِمُ عَلَى أهْلِ البَيْتِ بَيْتَهُمْ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Finikeni vyombo vyenu, na fungeni viriba vya kuekea maji, na fungeni milango, na zimeni taa kwa sababu shetani hafunui viriba vilivyo fungwa wala hafungui milango wala hafungui vyombo vilivyo finikwa. Ikiwa mmoja wenu hatapata cha kufinikia vyombo isipokuwa kuweka kijiti juu ya chombo au kutaja jina la Allaah, afanye hivyo. Huenda wakati mwengine panya akaangusha kandili (taa au koroboi) na hivyo kuchoma nyumba watu wake wakiwa ndani." [Muslim].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن التكلف
وهو فعل وقول ما لا مصلحة فيه بمشقة
048-Mlango Wa Kukatazwa Takilifu, Nayo ni Kufanya Kitendo na Kusema Maneno Ambayo Hayana Maslahi na Ndani yake Yapo Mashaka
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
قُلْ مَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُتَكَلِّفِينَ ﴿٨٦﴾
Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Sikuombeni ujira wowote juu ya hili, na wala mimi si miongoni mwa wenye kujidai kuzusha chochote kisichohusu. [Swaad: 86]
Hadiyth – 1
وعن عمر رضي الله عنه قال : نُهِينَا عَنِ التَّكَلُّفِ . رواه البخاري .
Amesema 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu): Tumekatazwa kupindukia (kuzidisha katika mambo). [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن مسروقٍ ، قال : دَخَلْنَا على عبدِ اللهِ بْنِ مَسعُودٍ رضي الله عنه فقال : يا أَيُّهَا النَّاسُ ، مَنْ عَلِمَ شَيْئاً فَلْيَقُلْ بِهِ ، وَمَنْ لَمْ يَعْلَمْ ، فَلْيَقُلْ : اللهُ أعْلَمُ ، فَإنَّ مِنَ العِلْمِ أَنْ يَقُولَ لِمَا لاَ يَعْلَمُ : اللهُ أعْلَمُ . قالَ اللهُ تَعَالَى لِنَبِيِّهِ صلى الله عليه وسلم : [ قُلْ مَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُتَكَلِّفِينَ ] . رواه البخاري .
Amesema Masruwq: Tulimzuru 'Abdillaah bin Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) siku moja, naye akatuambia: "Enyi watu! Mwenye kujua kitu chochote, anaweza kuzungumza kukihusu hicho. Na asiyehua, basi aseme: Allaah Anajua, kwani ni katika ujuzi wa elimu kusema kwa asiyejua: Allaah Anajua zaidi. Hakika Allaah Ta'aalaa Alimwambia Nabiy Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Sikuombeni ujira wowote juu ya hili, na wala mimi si miongoni mwa wenye kujidai kuzusha chochote kisichohusu. [Swaad: 86]." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم النياحة على الميت ولطم الخد وشق الجيب
ونتف الشعر وحلقه والدعاء بالويل والثبور
049-Mlango Wa Uharamu Kuomboleza Maiti kwa Kujipiga Mashavu, Kuchana Nguo, Kung'oa Nywele, Kunyoa na Kujiombea Maangamivu
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عمر بن الخطاب رضي الله عنه قال : قال النَّبِيّ صلى الله عليه وسلم : (( المَيِّتُ يُعَذَّبُ فِي قَبْرِهِ بِمَا نِيحَ عَلَيْهِ )) .
وَفِي روايةٍ : (( مَا نِيحَ عَلَيْهِ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Khattwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Maiti anaadhibiwa kaburini mwake kwa kuliliwa."
Na katika riwaayah nyengine: "Kwa kuliliwa." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن ابن مسعود رضي الله عنه قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لَيْسَ مِنَّا مَنْ ضَرَبَ الخُدُودَ ، وَشَقَّ الجُيُوبَ ، وَدَعَا بِدَعْوَى الجَاهِلِيَّةِ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Si miongoni mwetu mwenye kujipiga uso, na kuchana nguo zake na kuomba kwa duaa za kijahiliya anapopatikana na msiba." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 3
وَعَنْ أبي بُرْدَةَ ، قال : وَجعَ أبو مُوسَى ، فَغُشِيَ عَلَيْهِ ، وَرَأسُهُ فِي حِجْرِ امْرَأَةٍ مِنْ أهْلِهِ ، فَأَقْبَلَتْ تَصِيحُ بِرَنَّةٍ فَلَمْ يَسْتَطِعْ أنْ يَرُدَّ عَلَيْهَا شَيْئاً ، فَلَمَّا أفَاقَ قَالَ : أنَا بَرِيءٌ مِمَّنْ بَرِىءَ مِنْهُ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم إنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم بَرِيءٌ مِنَ الصَّالِقَةِ ، والحَالِقَةِ ، والشَّاقَّةِ . متفق عليه .
Amesema Abu Burdah: Abu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) aliumwa sana na akazimia hali kichwa chake kiko pajani kwa mke wake. Kuona hali yake hiyo mkewe alianza kulia kwa sauti kubwa, naye Abu Muwsaa hakuweza kumzuilia wala kumwambia chochote kwa sababu ya udhaifu wake. Alipozinduka akasema: "Mimi siko pamoja na yule aliyemkataa mwanamke anayelia kwa mayowe; na anye nyoa nywele zake (kwa msiba) na anayechana nguo)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 4
وعن المغيرة بن شعبة رضي الله عنه قال : سمعتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( مَنْ نِيحَ عَلَيْهِ ، فَإنَّهُ يُعَذَّبُ بِمَا نِيحَ عَلَيهِ يَومَ القِيَامَةِ )) . متفق عليه .
Amesema Al-Mughiyrah bin Shu'bah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kuliliwa, hakika yeye ataadhibiwa kwa alicholiliwa Siku ya Qiyaamah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أُمِّ عَطِيَّةَ نُسَيْبَةَ – بِضَمِّ النون وفتحها – رضي الله عنها ، قالت : أخَذَ عَلَيْنَا رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم عِندَ البَيْعَةِ أنْ لاَ نَنُوحَ . متفق عليه .
Amesema Umm 'Atwiyyah Nusaybah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amechukua kwetu hatutalia kwa mayowe (wakati wa msiba)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 6
وعن النعمان بن بشير رضي الله عنهما ، قال : أُغْمِيَ عَلَى عَبدِ اللهِ بْنِ رَوَاحَةَ رضي الله عنه ، فَجَعَلَتْ أُخْتُهُ تَبْكِي، وَتَقُولُ : وَاجَبَلاهُ ، وَاكَذَا ، وَاكَذَا : تُعَدِّدُ عَلَيْهِ . فقالَ حِينَ أفَاقَ : مَا قُلْتِ شَيْئاً إلاَّ قِيلَ لِي أنْتَ كَذَلِكَ ؟! . رواه البخاري .
Amesema Nu'maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Alipozirai 'Abdillaah bin Rawaahah (Radhwiya Allaahu 'anhu), dadake alianza kumlilia kwa sauti huku anasema: "Ee jabali langu (mwenye haiba ya hali ya juu miongoni mwa watu) na kadha na kadha, akihesabu sifa zake nzuri." Alipopata fahamu alisema: "Hukusema lolote katika hayo isipokuwa niliulizwa: Je, wewe uko hivo?" [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 7
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قال : اشْتَكَى سَعْدُ بنُ عُبَادَةَ رضي الله عنه شَكْوَى ، فَأتاهُ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم ، يَعُودُهُ مَعَ عَبدِ الرَّحمانِ بْنِ عَوفٍ ، وَسَعْدِ بن أبي وقَّاصٍ ، وعبدِ اللهِ بن مسعودٍ رضي الله عنهم . فَلَمَّا دَخَلَ عَلَيْهِ ، وَجَدَهُ في غَشْيَةٍ فَقالَ : (( أقَضَى ؟ )) قالوا : لا يا رسول اللهِ ، فَبكَى رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فَلَمَّا رَأى القَوْمُ بُكَاءَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم بَكَوْا ، قال : (( ألاَ تَسْمَعُونَ ؟ إنَّ اللهَ لاَ يُعَذِّبُ بِدَمْعِ العَيْنِ ، وَلاَ بِحُزْنِ القَلْبِ، وَلكِنْ يُعَذِّبُ بِهذَا )) - وَأشَارَ إلَى لِسَانِهِ - أو يَرْحَمُ )) . متفق عليه.
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Sa'ad bin 'Ubadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) alikuwa anaumwa sana, hivyo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimtembelea akiwa pamoja na 'Abdur-Rahmaan bin 'Awf na Sa'as bin Abi Waqqaas na 'Abdillaah bin Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alilia kuiona hali yake na watu walipomuona Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akilia nao pia wakalia. Akasema: "Sikilizeni! Hakika Allaah hamuadhibu kwa kutokwa na machozi wala kwa huzuni ya moyo, anaadhibu kwa hili." Na hapo akaashiria mdomo wake, kisha akasema: "Au anawahurumia." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 8
وعن أبي مالك الأشعري رضي الله عنه قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( النَّائِحَةُ إذا لَمْ تَتُبْ قَبلَ مَوْتِهَا تُقَامُ يَومَ القِيَامَةِ وَعَلَيْهَا سِربَالٌ مِنْ قَطِرَانٍ ، وَدِرْعٌ مِنْ جَرَبٍ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Maalik Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwanamke mwenye kulia kwa mayowe ikiwa hatatubu kabla ya kufa kwake, atafufuliwa Siku ya Qiyaamah akiwa amevaa koto la lami na deraya iliyoshika kutu." [Muslim]
Hadiyth – 9
وعن أَسِيد بن أبي أَسِيدٍ التابِعِيِّ ، عن امْرَأةٍ مِنَ المُبَايِعاتِ ، قالت : كان فِيما أخَذَ عَلَيْنَا رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فِي المَعْرُوفِ الَّذِي أخَذَ عَلَيْنَا أنْ لاَ نَعْصِيَهُ فِيهِ : أنْ لا نَخْمِشَ وَجْهَاً ، وَلاَ نَدْعُوَ وَيْلاً ، وَلاَ نَشُقَّ جَيْباً ، وأنْ لاَ نَنْشُرَ شَعْراً . رواه أبو داود بإسناد حسن .
Imepokewa kutoka kwa Usayd bin Abi Usayd, Tadi'iy kutoka kwa mwanamke aliyechukua bay'ah kwamba: "Katika mambo ambayo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alichukua ahadi kutoka kwetu, ni kufanya mabo mema na kuwa hatutamuasi kabisa, nayo ni: Hatutakwaruza nyuso zetu, wala kuomba maangamivu wala kuchana nguo na kuwa pia hatutafumua nywele zetu (kwa sababu ya msiba)." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Hasan].
Hadiyth – 10
وعن أبي موسى رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قال : (( مَا مِنْ مَيِّتٍ يَمُوتُ فَيَقُومُ بَاكِيهِمْ فَيَقُولُ : وَاجَبَلاَهُ ، واسَيِّدَاهُ ، أو نَحْوَ ذلِكَ إلاَّ وُكِّلَ بِهِ مَلَكَانِ يَلْهَزَانِهِ : أهكَذَا كُنْتَ ؟ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapofariki mtu akasimama wenye kumlilia kwa kusema: "Ee mlima miongoni mwetu, ee mtemi na bwana wetu', au mfano wake isipokuwa huwakilishwa Malaaikah wawili wanaompiga ngumi kwenye kifua chake na kumuuliza: 'Je, ulikuwa hivo'?" [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan].
Hadiyth – 11
وعن أبي هريرة رضي الله عنه ، قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( اثْنَتَانِ فِي النَّاسِ هُمَا بِهِمْ كُفْرٌ : الطَّعْنُ فِي النَّسَبِ ، وَالنِّيَاحَةُ عَلَى المَيِّتِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Watu aina mbili miongoni mwa watu wana ukafiri: Kusuta nasaba na kuomboleza juu ya maiti." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النَّهي عن إتيان الكُهّان والمنجِّمين
والعُرَّاف وأصحاب الرمل والطوارق بالحصى وبالشعير ونحو ذلك
050-Mlango Wa Kukatazwa Kuwaendea Makuhani na Wapiga Bao na Ramli
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عائشة رضي الله عنها ، قالت : سأل رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم أنَاسٌ عَنِ الكُهَّانِ، فَقَالَ : (( لَيْسُوا بِشَيءٍ )) فَقَالُوا : يا رَسُولَ اللهِ إنَّهُمْ يُحَدِّثُونَا أحْيَاناً بِشَيءٍ، فَيَكُونُ حَقّاً ؟ فقالَ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( تِلْكَ الكَلِمَةُ مِنَ الحَقِّ يَخْطَفُهَا الجِنِّيُّ فَيَقُرُّهَا فِي أُذُنِ وَلِيِّهِ ، فَيَخْلِطُونَ مَعَهَا مئَةَ كَذْبَةٍ )) . متفق عليه .
وفي رواية للبخاري عن عائشة رضي الله عنها : أنَّها سمعتْ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( إنَّ المَلائِكَةَ تَنْزِلُ فِي العَنَانِ - وَهُوَ السَّحَابُ - فَتَذْكُرُ الأَمْرَ قُضِيَ فِي السَّماءِ ، فَيَسْتَرِقُ الشَّيْطَانُ السَّمْع ، فَيَسْمَعُهُ ، فَيُوحِيَهُ إلَى الكُهَّانِ ، فَيَكْذِبُونَ مَعَهَا مِئَةَ كَذْبَةٍ مِنْ عِنْدِ أَنْفُسِهِمْ )) .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Aliulizwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na watu kuhusu makuhani, akasema: "Wao si chochote na hawana kitu." Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika wao wakati mwengine huzungumzia kitu na kikawa kweli." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hiyo ni kalima ya kweli ambayo shetani huipata kwa bahati na hivyo kuifikisha kwa rafiki yake. Ukweli huu wanachanganya na uwongo mia moja." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika Malaaikah hushuka kwenye kiwingu na hutaja mambo ambayo yamepitishwa mbinguni. Shetani husikia hayo kibahati na baadaye kuyafikisha kwa makuhani, hivyo kuongeza pamoja nayo uwongo mia moja kutoka katika nafsi ao wenyewe."
Hadiyth – 2
وعن صَفِيَّةَ بِنتِ أبي عُبيدٍ ، عن بعض أزواجِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، ورَضِيَ اللهُ عنها ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( مَنْ أَتَى عَرَّافاً فَسَأَلَهُ عنْ شَيْءٍ فَصَدَّقَهُ ، لَمْ تُقْبَلْ لَهُ صَلاَةٌ أرْبَعِينَ يَوماً )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa kwa Swafiyyah bint Abu 'Ubayd (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kutoka kwa baadhi ya wakeze Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)alisema: "Mwenye kwenda kwa mtu anayedai kuwa anajua kitu chake kilichopotea, akamuuliza kuhusu kitu chochote na akamsadiki haitokubaliwa Swalaah yake kwa siku arobaini." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعَنْ قَبِيصَةَ بنِ المُخَارِقِ رضي الله عنه قال : سمعتُ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( العِيَافَةُ ، وَالطِّيَرَةُ ، والطَّرْقُ ، مِنَ الجِبْتِ )) . رواه أبو داود بإسناد حسن .
Amesema Qabiyswah bin Al-Mukhaariq (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Kuangalilia (kupigana bao), na mkosi, na kuruka kwa ndege ni katika Jibt." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Hasan]
Hadiyth – 4
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قال : قال رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنِ اقْتَبَسَ عِلْماً مِنَ النُّجُوم ، اقْتَبَسَ شُعْبَةً مِنَ السِّحْرِ زَادَ ما زَادَ )) . رواه أبو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kujifunza sehemu ya elimu kuhusu nyota ni kama amejifunza sehemu ya sihiri (uchawi). Na kila anapozidi kuendelea kusoma ndio anazidi kuingia katika sihiri." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 5
وعن مُعاوِيَةَ بنِ الحَكَمِ رضي الله عنه قال : قلتُ : يا رسُولَ اللهِ إنِّي حديثُ عَهْدٍ بالجاهِليَّةِ ، وَقَدْ جَاءَ اللهُ تَعَالَى بالإسْلاَمِ ، وإنَّ مِنَّا رِجَالاً يَأتُونَ الكُهَّانَ ؟ قال : (( فَلاَ تأتِهِمْ )) قُلْتُ : وَمِنَّا رِجَالٌ يَتَطَيَّرُونَ ؟ قَالَ : (( ذَلِكَ شَيْءٌ يَجِدُونَهُ فِي صُدُورِهِمْ ، فَلاَ يَصُدُّهُمْ )) قُلْتُ : وَمِنَّا رِجَالٌ يَخُطُّونَ ؟ قَالَ : (( كَانَ نَبِيٌّ مِنَ الأنْبِيَاءِ يَخُطُّ ، فَمَنْ وَافَقَ خَطَّهُ ، فَذَاكَ )) . رواه مسلم .
Amesema Mu'awiyah bin Al-Hakam (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilimuuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi nimetoka hivi karibuni katika Ujahiliyah na hakika Allaah Ta'aalaa na Uislamu. Na wapo miongoni mwetu ambao bado wanawaendea makuhani." Akasema: "Musiende kwao." Nikasema: "Miongoni mwetu wako wanao ongozwa na bahati." Alisema: "Hilo ni jambo wanaolipata katika vifua vyao (na akili zao). Wasiwakataze hilo ule muono wao kwani jambo hilo halileti manufaa wala madhara." Nikasema na miongoni mwetu kuna watu wanachora? Akasema: Kulikuwa Nabiy miongoni mwa Manabiy anachora anae afikiana na mchoro wake itakuwa kama hivyo. [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أَبي مَسعودٍ البدريِّ رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم نَهَى عَنْ ثَمَنِ الكَلْبِ ، وَمَهْرِ البَغِيِّ ، وَحُلْوَانِ الكاهِنِ . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikataza kutumia thamani ya mbwa (baada ya kuuzwa) na pato la malaya na ada anayopatiwa kuhani. [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن التَّطَيُّرِ
051-Mlango Wa Kukatazwa Kuamini Fali (Mkosi)
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أنس رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ عَدْوَى وَلاَ طِيَرَةَ ، وَيُعْجِبُني الفَألُ )) قالُوا : وَمَا الفَألُ ؟ قَالَ : (( كَلِمَةٌ طَيِّبَةٌ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoa kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana magonjwa ya kuambikizwa wala kisirani lakini ninapenda Al-Fa'lu." Akaulizwa: "Al-Fa'lu ni nini?" Akasema: "Neno zuri." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawud na At-Tirmidhiy].
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لا عَدْوَى وَلاَ طِيَرَةَ . وإنْ كَانَ الشُّؤمُ في شَيْءٍ فَفِي الدَّارِ ، وَالمَرْأَةِ ، والفَرَسِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana magonjwa ya kuambukizwa wala kisirani. Ikiwa kungekuwa na mkasi basi ingekuwa katika nyumba, mwanamke na farasi." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik, Abu Daawud na At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 3
وعن بُريْدَةَ رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ لا يَتَطَيَّرُ . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa haamini kabisa mambo ya fali na kisirani." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 4
وعن عُروة بن عامر رضي الله عنه قال : ذُكِرَتِ الطِّيَرَةُ عِنْدَ رَسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فقالَ : (( أحْسَنُهَا الفَألُ . وَلاَ تَرُدُّ مُسْلِماً فإذا رَأى أحَدُكُمْ ما يَكْرَهُ ، فَليْقلْ : اللَّهُمَّ لاَ يَأتِي بِالحَسَناتِ إلاَّ أنْتَ ، وَلاَ يَدْفَعُ السَّيِّئَاتِ إلاَّ أنْتَ ، وَلاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إلاَّ بِكَ )) حديث صحيح رواه أبو داود بإسناد صحيح .
Amesema 'Urwah bin 'Aamir (Radhwiya Allaahu 'anhu): Ilitajwa mikosi mbele ya Rasuli wa Alaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), akasema: "Iliyo bora zaidi ni Al-fa'ul, na fali haimrudishi nyuma Muislamu, hivyo akiona mmoja wenu linalomchukiza na aseme: 'Allaahumma laa yaatiy bil hasanaati illaa Anta walaa yadfa'u as-sayyi'ati ilaa Anta walaa Hawla walaa Quwwata illa Bika (Ee Rabb Wangu! Jambo zuri haliji ila kutoka Kwako wala hapana wa kuondosha jambo ovu isipokuwa Wewe wala hapana hila wala nguvu isipokuwa kuwezeshwa na wewe'." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم تصوير الحيوان في بساط
أو حجر أو ثوب أو درهم أو مخدة أو دينار أو وسادة وغير ذلك
وتحريم اتخاذ الصور في حائط وسقف وستر وعمامة وثوب ونحوها
والأمر بإتلاف الصورة
052-Mlango Wa Uharamu wa Kuchora Wanyama katika Busati au Mawe, Nguo, Dirhamu, Dinari (Hela), Mto na Kadhalika na Uharamu wa Kuwa na Picha katika Ukuta, Pazia, Kilemba, Nguo na Mfano wake na Amri ya Kufuta Picha
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قال : (( إنَّ الَّذينَ يَصْنَعُونَ هذِهِ الصُّوَرَ يُعَذَّبُونَ يَوْمَ القِيامَةِ ، يُقَالُ لَهُمْ : أحْيُوا مَا خَلَقْتُمْ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema: "Hakika wanaotengeneza hizi picha wataadhibiwa Siku ya Qiyaamah, wataambiwa vipeni uhai mlivyo viumba." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قَدِمَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم مِنْ سَفَرٍ ، وَقَدْ سَتَرْتُ سَهْوَةً لِي بِقِرامٍ فِيهِ تَمَاثيلُ ، فَلَمَّا رَآهُ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم تَلَوَّنَ وَجْهُهُ، وقالَ: (( يَا عائِشَةُ ، أشَدُّ النَّاسِ عَذَاباً عِندَ اللهِ يَوْمَ القِيَامَةِ الَّذينَ يُضَاهُونَ بِخَلْقِ اللهِ ! )) قَالَتْ : فَقَطَعْنَاهُ فَجَعَلْنَا مِنهُ وِسَادَةً أوْ وِسَادَتَيْنِ . متفق عليه .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alifika, kutoka safarini, akanikuta nimeweka pazia yangu yenye mapicha. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipoiona uso wake ulibadilika rangi na kusoma: "Ee 'Aaishah! Walio na adhabu kali kuliko watu wote Siku ya Qiyaamah ni wale wanaoiga umbile aliloliumba Allaah." 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) akasema: "Tukaikata, na tukafanya kutokana nayo mto, mmoja au miwili." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na An-Nisaaiy]
Hadiyth – 3
وعن ابن عباس رضي اللهُ عنهما ، قال : سمعتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( كُلُّ مُصَوِّرٍ في النَّارِ يُجْعَلُ لَهُ بِكُلِّ صُورَةٍ صَوَّرَهَا نَفْسٌ فَيُعَذِّبُهُ في جَهَنَّمَ )) . قال ابن عباس : فإنْ كُنْتَ لاَ بُدَّ فَاعِلاً ، فَاصْنعِ الشَّجَرَ وَمَا لاَ رُوحَ فِيهِ. متفق عليه.
Amesema Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Kila mwenye kutengeneza picha ataingizwa motoni, atajaaliwa kwa kila picha aliyochora nafsi itakayomuadhibu ndani ya Jahanamu." Akasema Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): "Na ikiwa huna budi ufanye (shughuli hiyo ya kuchora) basi tengeneza (picha ya) miti na vitu visivyokuwa na roho." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن ابن عباس رضي اللهُ عنهما ، قال : سمعتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( مَنْ صَوَّرَ صُورَةً فِي الدُّنْيَا ، كُلِّفَ أَنْ يَنْفُخَ فِيهَا الرُّوحَ يَومَ القِيَامَةِ وَلَيْسَ بِنَافِخٍ )) . متفق عليه .
Amesema Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kuchora picha ataadhibiwa na kukalifishwa kupuliza ndani yake uhai na hataweza kufanya hivyo." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 5
وعن ابن مسعودٍ رضي اللهُ عنه قال : سمعتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( إنَّ أشَدَّ النَّاسِ عَذَاباً يَومَ القِيَامَةِ المُصَوِّرُونَ )) . متفق عليه .
Amesema Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika aliye na adhabu kali zaidi ya wote Siku ya Qiyaamah ni watengeneza picha." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nisaaiy]
Hadiyth – 6
وعن أبي هريرة رضي اللهُ عنه قال : سمعتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( قال اللهُ تَعَالَى : وَمَنْ أظْلَمُ مِمَّنْ ذَهَبَ يَخْلُقُ كَخَلْقِي ؟ فَلْيَخْلُقُوا ذَرَّةً أوْ لِيَخْلُقُوا حَبَّةً ، أوْ لِيَخْلُقُوا شَعِيرَةً )) . متفق عليه .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Amesema Allaah Ta'aalaa: Hakuna aliye dhulumu zaidi ya yule anaye jaribu kuumba kama Nilivyoumba, basi ajaribu kuumba atomu (ni kitu kidogo sana ambacho hakiwezi kuonekana ila kwa ala ya kukuza kitu) au aiumbe chembe moja ya nafaka au aiumbe shayri." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 7
وعن أبي طلحة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَ تَدْخُلُ المَلاَئِكَةُ بَيْتاً فيهِ كَلْبٌ وَلاَ صُورَةٌ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Twalhah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Malaaikah hawaingii nyumba iliyo na mbwa ndani yake wala iliyo na picha au masanamu." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawud, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na Ibn Maajah].
Hadiyth – 8
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قال : وَعَدَ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم جِبْرِيلُ أنْ يَأتِيَهُ ، فَرَاثَ عَلَيْهِ حَتَّى اشْتَدَّ عَلَى رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فَخَرَجَ فَلَقِيَهُ جِبريلُ فَشَكَا إلَيهِ ، فَقَالَ : إنَّا لاَ نَدْخُلُ بَيْتاً فِيهِ كَلْبٌ وَلاَ صُورَةٌ . رواهُ البُخاري .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Mara moja Jibriyl aliahidi kumzuru Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) lakini alichukua muda mrefu mpaka likamkera Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) jambo hilo. Alipotoka nyumbani kwake alikutana na Jibriyl na kumlalamikia kuhusu hilo. Akasema Jibriyl: "Hakika sisi hatuingii nyumba iliyo na mbwa ndani yake wala iliyo na picha au masanamu." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 8
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : واعدَ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، جبريلُ عليهِ السَّلامُ ، في سَاعَةٍ أنْ يَأتِيَهُ ، فَجَاءتْ تِلْكَ السَّاعَةُ وَلَمْ يَأتِهِ ! قَالَتْ : وَكَانَ بِيَدِهِ عَصاً، فَطَرَحَهَا مِنْ يَدِهِ وَهُوَ يَقُولُ : (( ما يُخْلِفُ اللهُ وَعْدَهُ وَلاَ رُسُلُهُ )) ثُمَّ التَفَتَ ، فإذَا جَرْوُ كَلْبٍ تَحْتَ سَرِيرِهِ . فقالَ : (( مَتَى دَخَلَ هَذَا الكَلْبُ ؟ )) فَقُلْتُ : واللهِ مَا دَرَيْتُ بِهِ ، فَأمَرَ بِهِ فَأُخْرِجَ ، فَجَاءهُ جِبْرِيلُ (عَلَيْهِ السَّلام) ، فقال رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( وَعَدْتَنِي، فَجَلَسْتُ لَكَ وَلَمْ تَأتِني )) فقالَ : مَنَعَنِي الكَلْبُ الَّذِي كانَ في بَيْتِكَ ، إنَّا لاَ نَدْخُلُ بَيْتاً فِيهِ كَلْبٌ وَلاَ صُورَةٌ . رواه مسلم .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Mara moja Jibriyl alimuahidi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa atamtembelea baada ya muda (usiku). Jibriyl hakufika wakati huo wa miadi. Akasema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa na fimbo mkononi mwake ambayo aliitupa, huku anasema: 'Allaah Hakhalifu ahadi Yake wala wajumbe Wake'." Kisha akatizama na kumuona mbwa chini ya kitanda chake cha mbao, na hapo akauliza: "Mbwa huyu ameingia lini?" Nikasema: "Wa-Allaahi! Sikumuona kabisa akiingia." Akaamuru atolewe, naye akatolewa. Jibriyl alikuja wakati huo, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: 'Uliniahidi kuwa utanizuru, nami nimekataa kukungojea lakini hukufika." Akasema: "Amenizuia mimi yule mbwa aliyekuwa ndani ya nyumba yako. Hakika sisi hatuingii nyumba iliyo na mbwa ndani yake wala iliyo na picha au masanamu." [Muslim]
Hadiyth – 9
وعن أبي الهَيَّاجِ حَيَّانَ بِن حُصَيْنٍ ، قال : قال لي عَليُّ بن أبي طالب رضي اللهُ عنه : ألاَ أبْعَثُكَ عَلَى مَا بَعَثَنِي عَلَيْهِ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ؟ أن لاَ تَدَعَ صُورَةً إلاَّ طَمَسْتَهَا ، وَلاَ قَبْراً مُشْرفاً إلاَّ سَوَّيْتَهُ . رواه مسلم .
Amesema Abil Hayyaaj Hayyan bin Huswayn: Aliniambia mimi 'Ali bin Abi Twaalib (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Je, sikutumi kwa alilonituma kwayo Rasuli wa Allaah? Usiache picha yoyote isipokuwa umeifutilia mbali (au sanamu isipokuwa umelivunja) wala kaburi lolote ambalo limenyanyuliwa isipokuwa umelisawazisha." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم اتخاذ الكلب إلا لصيد أو ماشية أو زرع
053-Mlango Wa Uharamu wa Kufuga Mbwa Ila kwa Kuwinda au kwa Kulinda Wanyama au Mazao
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما، قال : سمعتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( مَنِ اقْتَنَى كَلْباً إلاَّ كَلْبَ صَيْدٍ أوْ مَاشِيَةٍ فَإنَّهُ يَنْقُصُ مِنْ أجْرِهِ كُلَّ يَومٍ قِيرَاطَانِ )) . متفق عليه .
وفي رواية : (( قِيرَاطٌ )) .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kuweka mbwa asiekuwa wa kuwinda au wa kulinda mali na mifugo (kama ngamia, kondoo na mbuzi), hakika thawabu zake kila siku Qiyraat mbili." [Al-Bikhaariy na Muslim].
Na katika riwaayah nyengine: "Qiyraat moja."
Hadiyth – 2
وعن أبي هريرة رضي الله عنه قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ أمْسَكَ كَلْباً، فَإنَّهُ ينْقُصُ مِنْ عَمَلِهِ كُلَّ يَومٍ قِيرَاطٌ إلاَّ كَلْبَ حَرْثٍ أوْ مَاشِيَةٍ )) . متفق عليه .
وفي رواية لمسلم : (( مَنْ اقْتَنَى كَلْباً لَيْسَ بِكَلْبِ صَيْدٍ، وَلاَ مَاشِيَةٍ وَلاَ أرْضٍ، فَإنَّهُ يَنْقُصُ مِنْ أجْرِهِ قِيرَاطَانِ كُلَّ يَوْمٍ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Atakaye kuwa na mbwa, hakika yeye anapungukiwa kila siku na Qiyraat moja ya amali zake isipokuwa mbwa wa kulinda mazao au wanyama." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah ya Muslim: "Mwenye kumueka mbwa ambaye si wa kuwinda wala wa kulinda ardhi, hakika atapungukiwa katika ajri yake Qiyraat mbili kila siku."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهية تعليق الجرس في البعير وغيره من الدواب
وكراهية استصحاب الكلب والجرس في السفر
054-Mlango Wa Ukaraha wa Kuwafunga Kengele Ngamia na Wanyama Wengine na Ukaraha wa Kumchukua Mbwa na Kengele katika Safari
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرة رضي الله عنه قال : قالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَصْحَبُ المَلاَئِكَةُ رُفْقَةً فِيهَا كَلْبٌ أوْ جَرَسٌ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Malaaikah wa rehma hawafuati msafara ulio na mbwa au kengele." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أبي هريرة رضي الله عنه قال : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( الجَرَسُ مَزَامِيرُ الشَّيْطَانِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kengele ni katika zumari za shetani." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة ركوب الجَلاَّلة
وهي البعير أو الناقة التي تأكل العَذِرَة
فإنْ أكلت علفاً طاهراً فطاب لَحمُهَا ، زالت الكراهة
055-Mlango Wa Ukaraha wa Kumpanda Jalaalah, Naye ni Ngamia Anayekula Kinyaa Lakini Anapokula Malisho Yaliyo Tohara Husafishika Nyama Yake na Kuondoka Ukaraha Huo
Alhidaaya.com [4]
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قال : نهَى رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم عَنِ الجَلاَّلَةِ في الإبِلِ أنْ يُرْكَبَ عَلَيْهَا . رواه أبو داود بإسناد صحيح .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Amekataza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kupandwa jalala wa ngamia. [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن البصاق في المسجد
والأمر بإزالته منه إذا وجد فيه
والأمر بتنـزيه المسجد عن الأقذار
056-Mlango Wa Kukatazwa Kutema Mate Msikitini, Amri ya Kuyaondoa Yanapopatikana na Amri ya Kusafisha Msikiti
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أنس رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قال : (( البُصاقُ في المَسْجِدِ خَطِيئَةٌ ، وَكَفَّارَتُهَا دَفْنُهَا )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kutema mate Msikitini ni kosa na kafara lake ni kuyafukia." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم رَأَى في جِدَارِ القِبْلَةِ مُخَاطاً ، أَوْ بُزَاقاً ، أَوْ نُخَامَةً ، فَحَكَّهُ . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliona katika ukuta wa Qiblah kamasi, au mate, au kohozi, akalikwangua." [Al-Bukhaariy, Muslim na Maalik]
Hadiyth – 3
وعن أنس رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ هذِهِ المَسَاجِدَ لاَ تَصْلُحُ لِشَيءٍ مِنْ هَذَا البَوْلِ وَلاَ القَذَرِ ، إنَّمَا هي لِذِكْرِ اللهِ تَعَالَى ، وَقِراءةِ القُرْآنِ )) أَوْ كَمَا قَالَ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika haifai kuitumia Misikiti kwa ajili ya kukojoa ndani yake wala kuichafua (kwa kuitia najisi). Hakika hiyo Misikiti ni kwa ajili ya kumdhukuru Allaah Ta'aalaa na kusoma au kama alivyosema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الخصومة في المسجد ورفع الصوت فِيهِ
ونشد الضالة والبيع والشراء والإجارة ونحوها من المعاملات
057-Mlango Wa Ukaraha wa Kugombana Msikitini, Kunyanyua Sauti Ndani Yake, Kusaka Kitu Kilichopotea, Kuuza, Kununua na Kuajiri na Mfano Wake katika Muamala
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّه سمعَ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( مَنْ سَمِعَ رَجُلاً يَنْشُدُ ضَالَّةً في المَسْجِدِ فَلْيَقُلْ : لاَ رَدَّها اللهُ عَلَيْكَ ، فإنَّ المَسَاجِدَ لَمْ تُبْنَ لِهذَا )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kumsikia mtu yeyote akitafuta kitu kilichopotea Msikitini, amwambie: 'Allaah asikurudishie kitu chako', kwani Misikiti haikujengwa kwa sababu ya hilo." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا رَأيْتُمْ مَنْ يَبِيعُ أَوْ يَبْتَاعُ في المَسْجِدِ ، فَقُولُوا : لا أرْبَحَ اللهُ تِجَارَتَكَ ، وَإِذَا رَأَيْتُمْ مَنْ يَنْشُدُ ضَالَّةً فَقُولُوا : لا رَدَّهَا الله عَلَيْكَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Unapomuona mtu anafanya biashara ya kuuza au kununua Msikitini, mwambie: 'Allaah asikupatie faida katika biashara yako.' Na unapomuona mtu anasaka kitu kilichompotea, basi mwambie: 'Allaah asikurudishie kitu chako'." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 3
وعن بُريَدَةَ رضي الله عنه : أنَّ رَجُلاً نَشَدَ في المَسْجِدِ فَقَالَ : مَنْ دَعَا إِلَى الجَمَلِ الأَحْمَرِ ؟ فَقَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لا وَجَدْتَ ؛ إنَّمَا بُنِيَتِ المََسَاجِدُ لِمَا بُنِيَتْ لَهُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa kulikuwa na mtu mmoja aliyekuwa akitangaza ndani ya Msikiti kwa kusema: "Ni nani aliyemuita ngamia mwekundu?" Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Heri usimpate, hakika Msikiti imejengwa kwa lengo iliyo jengewa." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن عمرو بن شعيب ، عن أبيه ، عن جدِّهِ رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم نَهَى عَن الشِّراءِ والبَيْعِ في المَسْجِدِ ، وَأنْ تُنْشَدَ فِيهِ ضَالَّةٌ ؛ أَوْ يُنْشَدَ فِيهِ شِعْرٌ . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Amruw bin Shu'ayb kutoka kwa babake, kutoka kwa babu yake (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kununua na kuuza Msikitini na kusaka ndani yake kitu kilichopotea au kuimbwa ndani yake mashairi. [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 5
وعن السائبِ بن يزيد الصحابي رضي الله عنه قَالَ : كُنْتُ في المَسْجِدِ فَحَصَبَنِي رَجُلٌ ، فَنَظَرْتُ فَإذَا عُمَرُ بْنُ الخَطَّابِ رضي الله عنه فَقَالَ : اذْهَبْ فَأتِنِي بِهذَينِ ، فَجِئْتُهُ بِهِمَا ، فَقَالَ : مِنْ أيْنَ أَنْتُمَا ؟ فَقَالاَ : مِنْ أهْلِ الطَّائِفِ ، فَقَالَ : لَوْ كُنْتُمَا مِنْ أهْلِ البَلَدِ ، لأَوْجَعْتُكُمَا ، تَرْفَعَانِ أصْوَاتَكُمَا في مَسْجِدِ رَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم ! رواه البخاري .
Amesema Saaib bin Yaziyd, ambaye ni Swahaaba (Radhiwya Allaahu 'anhu): Nilikuwa Msikitini, mara mtu mmoja akanipiga mimi kwa kijiwe. Nikamuangalia na kumuona kuwa ni 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu), naye akaniambia: "Nenda ukaniletee wale watu wawili." Nikaja nao kwake, naye akawauliza: "Nyinyi munatoka wapi?" Wakasema: "Sisi ni watu wa Twaaif." Akawambia: "Lau mungekuwa ni watu wa mji huu (yaani Madiynah) ningewaadhibu, kwani nyinyi munanyanyua sauti zenu katika Msikiti wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." [Al-Bukhaariy].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب نهي من أكل ثوماً أَوْ بصلاً
أَوْ كراثاً أَوْ غيره مِمَّا لَهُ رائحة كريهة عن
دخول المسجد قبل زوال رائحته إِلاَّ لضرورة
058-Mlango Wa Kukatazwa Kuingia Msikitini Baada ya Kula Kitunguu Thaumu au Maji au Karoti au Vitu Vyengine Vyovyote Vyenye Harufu Mbaya Kabla ya Kuondoka Harufu hiyo Isipokuwa kwa Dharura
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ أكَلَ مِنْ هذِهِ الشَّجَرَةِ - يعني : الثُّومَ - فَلاَ يَقْرَبَنَّ مَسْجِدَنَا )) . متفق عَلَيْهِ .
وفي روايةٍ لمسلم : (( مساجدنا )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kula mti huu - yaani thaumu (kitunguu saumu) - asiusongelee Msikiti wetu." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd].
Na katika riwaayah ya Muslim: "Misikiti yetu."
Hadiyth – 2
وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ أَكَلَ مِنْ هذِهِ الشَّجَرَةِ فَلاَ يَقْرَبَنَّا ، وَلاَ يُصَلِّيَنَّ مَعَنَا )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kula mti huu asitusongelee wala asiswali na sisi." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن جابر رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ أكَلَ ثُوماً أَوْ بَصَلاً فَلْيَعْتَزلنا ، أو فَلْيَعْتَزِلْ مَسْجِدَنَا )) . متفق عَلَيْهِ .
وفي روايةٍ لمسلم : (( مَنْ أكَلَ البَصَلَ ، والثُّومَ ، والكُرَّاثَ ، فَلاَ يَقْرَبَنَّ مَسْجِدَنَا ، فَإنَّ المَلاَئِكَةَ تَتَأَذَّى مِمَّا يَتَأَذَّى مِنْهُ بَنُو آدَمَ )) .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kula thaumu au kitunguu maji ajitenge asiwe na sisi au auache Msikiti wetu." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy].
Na katika riwaayah ya Muslim: "Mwenye kula kitunguu maji na thaumu na karoti asiusogelee Msikiti wetu kwani Malaaikah wanaudhika kwa yanayo waudhi binadamu."
Hadiyth – 4
وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه : أنَّه خَطَبَ يومَ الجمْعَةِ فَقَالَ في خطبته : ثُمَّ إنَّكُمْ أيُّهَا النَّاسُ تَأكُلُونَ شَجَرتَيْنِ مَا أرَاهُمَا إِلاَّ خَبِيثَتَيْن : البَصَلَ ، وَالثُّومَ . لَقَدْ رَأَيْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، إِذَا وَجدَ ريحَهُمَا مِنَ الرَّجُلِ في المَسْجِدِ أَمَرَ بِهِ ، فَأُخْرِجَ إِلَى البَقِيعِ ، فَمَنْ أكَلَهُمَا ، فَلْيُمِتْهُمَا طَبْخاً . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa alihutubu Siku ya Ijumaa akasema katika hotuba yake: "Kisha, hakika enyi watu! Nyinyi mnakula miti miwili ambayo siioni isipokuwa ni mibaya: Kitunguu maji na thaumu. Hakika nimemuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pindi anaposikia harufu ya hivyo vitu viwili kutoka kwa mtu yeyote Msikitini, akiamuru atolewe apelekwe mpaka al-Baqi' (sehemu ya mbali). Hivyo, yeyote anayetaka kula vitu hivyo mwanzo azipike (ili aiondoe harufu yake)." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الاحتباء يوم الجمعة والإمام يخطب
لأنَّه يجلب النوم فيفوت استماع الخطبة ويخاف انتقاض الوضوء
059-Mlango Wa Ukaraha wa Ihtibaa Siku ya Ijumaa Imamu Akiwa Ahutubu Kwani Linamletea Mtu Usingizi Hivyo Kukosa Kusikia Hotuba na Kuwa na Hofu ya Kutokwa na wudhuu
Alhidaaya.com [4]
عن مُعاذِ بن أنس الجُهَنِيِّ رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم نَهَى عَنِ الحِبْوَةِ يَومَ الجُمعَةِ وَالإمَامُ يَخْطُبُ . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقالا : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Mu'aadh bin Anas Al-Juhaniy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikataza Hibwah (ni mtu kukunja miguu yake na kuyaleta kwenye tumbo lake na kuyafunga na kitambara pamoja na mgongo wake na kukikaza) Siku ya Ijumaa Imamu anapohutubu." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب نهي من دخل عَلَيْهِ عشر ذي الحجة
وأراد أنْ يضحي عن أخذ شيء من شعره أَوْ أظفاره حَتَّى يضحّي
060-Mlango Wa Kukatazwa kwa Anayetaka Kuchinja Kukata Nywele au Kucha Zake Mpaka Achinje Pindi Linapoingia Kumi la Kwanza la Dhul Hijjah
Alhidaaya.com [4]
عن أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ كَانَ لَهُ ذِبْحٌ يَذْبَحُهُ ، فَإذَا أَهَلَّ هِلاَلُ ذِي الحِجَّةِ ، فَلاَ يَأخُذَنَّ من شَعْرِهِ وَلاَ مِنْ أظْفَارِهِ شَيْئاً حَتَّى يُضَحِّيَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Umm Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuwa na mnyama anayetaka kumchinja (siku ya Iydul Adhha), basi ajizuwie kukata nywele na kucha zake pindi unapoandama mwezi wa Dhul Hijjah mpaka achinje." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الحلف بمخلوق
كالنبي والكعبة والملائكة والسماء والآباء والحياة والروح
والرأس وحياة السلطان ونعمة السلطان وتربة فلان والأمانة ، وهي
من أشدها نهياً
061-Mlango Wa Kukatazwa Kuapa kwa Viumbe Kama Nabiy, Ka'abah, Malaaikah, Mbingu, Baba, Uhai, Roho, Kichwa, Neema ya Sultani, Mchanga wa Fuani (Kaburi) na Amana, Nayo Imekatazwa kwa Ukali Zaidi
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ الله تَعَالَى يَنْهَاكُمْ أنْ تَحْلِفُوا بِآبائِكُمْ ، فَمَنْ كَانَ حَالِفاً ، فَلْيَحْلِفْ بِاللهِ ، أَوْ لِيَصْمُتْ )) . متفق عَلَيْهِ .
وفي رواية في الصحيح : (( فَمَنْ كَانَ حَالِفاً فَلاَ يَحْلِفْ إِلاَّ بِاللهِ ، أَوْ لِيَسْكُتْ )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Anawakatazeni kuapia kwa baba zenu, mwenye kuapa basi amuapie Allaah au anyamaze." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن عبد الرحمان بن سَمُرَةَ رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَحْلِفُوا بِالطَّوَاغِي ، وَلاَ بِآبَائِكُمْ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abdir-Rahmaan bin Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usiape kwa Twawaaghiy wala kwa baba zenu." [Muslim]. Twawaaghiyt ni wingi wa Twaaghiyah nayo ina maana ya masanamu. Na miongoni mwayo ni Hadiyth: "Hili ni Twaaghiyah la Daws", yaani ni sanamu lao wanalo liabudu. Na imepokewa katika riwaayah isipokuwa ya Muslim: "Bit Twawaaghiyt", nayo ni mwingi wa Twaaghuwt yenye maana ya shetani na sanamu.
Hadiyth – 3
وعن بُريدَةَ رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ حَلَفَ بِالأمَانَةِ فَلَيْسَ مِنَّا )) حديث صحيح ، رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuapa kama amana si katika sisi." [Hadiyth Swahiyh iliyopokewa na Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Hadiyth – 4
وعن بُريدَةَ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ حَلَفَ فَقَالَ : إنِّي بَرِيءٌ مِنَ الإسْلاَمِ ، فَإنْ كَانَ كَاذِباً ، فَهُوَ كمَا قَالَ ، وإنْ كَانَ صَادِقاً ، فَلَنْ يَرْجِعَ إِلَى الإسْلاَمِ سَالِماً )) . رواه أَبُو داود .
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuapa, akasema: 'Mimi niko mbali na Uislamu, ikiwa ni muongo, basi atakuwa kama alivyosema na akiwa ni mkweli hatarudi katika Uislamu akiwa salama." [Abu Daawuwd]
Hadiyth – 5
وعن ابن عمر رضي الله عنهما: أنَّهُ سَمِعَ رَجُلاً يقُولُ: لاَ وَالكَعْبَةِ، فَقَالَ ابنُ عُمَرَ : لاَ تَحْلِفْ بَغَيْرِ اللهِ ، فَإنِّي سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( مَنْ حَلَفَ بِغَيرِ اللهِ ، فقد كَفَرَ أَوْ أشْرَكَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa alisikia mtu akisema: "Naapa kwa Ka'abah." Ibn 'Umar akamwambia: "Usiape kwa asiyekuwa Allaah, kwani nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: 'Mwenye kuapa kwa asiyekuwa Allaah, hakika amekufuru au amefanya shirki'." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تغليظ اليمين الكاذبة عمداً
062-Mlango Wa Uzito wa Kula Yamini Ya Uongo Kwa Makusudi
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن مسعودٍ رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ حَلَفَ عَلَى مَالِ امْرِئٍ مُسْلِمٍ بِغَيرِ حَقِّهِ ، لَقِيَ اللهَ وَهُوَ عَلَيْهِ غَضْبَانُ )) قَالَ : ثُمَّ قَرَأَ عَلَيْنَا رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، مِصْدَاقَهُ مِنْ كِتَابِ الله عزوجل : [ إنَّ الَّذِينَ يَشْتَرُونَ بِعَهْدِ اللهِ وَأَيْمَانِهِمْ ثَمَناً قَلِيلاً أُولَـٰئِكَ لَا خَلَاقَ لَهُمْ فِي الْآخِرَةِ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ اللَّـهُ وَلَا يَنظُرُ إِلَيْهِمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٧٧﴾] [ آل عمران : 77] . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuapa kiapo cha uwongo ili apate kuchukua mali ya mtu Muislamu pasi na haki, atakutana na Allaah akiwa Ameghadhibika naye." Akasema (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Kisha, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akatusomea aya katika Kitabu cha Allaah Ta'aalaa kuunga mkono kauli hiyo: '
إنَّ الَّذِينَ يَشْتَرُونَ بِعَهْدِ اللهِ وَأَيْمَانِهِمْ ثَمَناً قَلِيلاً أُولَـٰئِكَ لَا خَلَاقَ لَهُمْ فِي الْآخِرَةِ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ اللَّـهُ وَلَا يَنظُرُ إِلَيْهِمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٧٧﴾
Hakika wale wanaobadilisha Ahadi ya Allaah na viapo vyao kwa thamani ndogo, hao hawana sehemu yoyote katika Aakhirah na wala Allaah Hatowasemesha na wala Hatowatazama Siku Ya Qiyaamah na wala Hatowatakasa na watapata adhabu iumizayo'. [Aal-'Imraan: 77]. [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy].
Hadiyth – 2
وعن أَبي أُمَامَة إياس بن ثعلبة الحارثي رضي الله عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنِ اقْتَطَعَ حَقَّ امْرِىءٍ مُسْلِمٍ بِيَمِينِهِ ، فَقَدْ أَوْجَبَ اللهُ لَهُ النَّارَ . وَحَرَّمَ عَلَيْهِ الجَنَّةَ )) فَقَالَ لَهُ رَجُلٌ : وَإنْ كَانَ شَيْئاً يَسِيراً يَا رسولَ اللهِ ؟ قَالَ : (( وإنْ كَانَ قَضِيباً مِنْ أرَاكٍ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Umamah Iyaas bin Tha'labah Al-Haarithiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumnyang'anya mtu Muislamu haki yake kwa yamini la uwongo, imekuwa ni wajibu kwa Allaah kumuingiza motoni na kumharamishia Jannah." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عبد اللهِ بن عمرو بن العاصِ رضي الله عنهما، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( الكَبَائِرُ : الإشْرَاكُ بِاللهِ ، وَعُقُوقُ الوَالِدَيْنِ ، وَقَتْلُ النَّفْسِ ، واليَمِينُ الغَمُوسُ )) . رواه البخاري .
وفي روايةٍ لَهُ : أنَّ أعْرابِياً جَاءَ إِلَى النبيّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : يا رسولَ اللهِ مَا الكَبَائِرُ ؟ قَالَ : (( الإشْرَاكُ بِاللهِ )) قَالَ : ثُمَّ مَاذا ؟ قَالَ : (( اليَمِينُ الغَمُوسُ )) قلتُ : وَمَا اليَمِينُ الغَمُوسُ ؟ قَالَ : (( الَّذِي يَقْتَطِعُ مَالَ امْرِئٍ مُسْلِمٍ ! )) يعني بِيَمِينٍ هُوَ فِيهَا كَاذِبٌ .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Madhambi makubwa ni: Kumshirikisha Allaah, na kuwaasi wazazi wawili, na kuua nafsi na kula yamini la uwongo."[Al-Bukhaariy].
Na katika riwaayah yake nyengine: "Alikuja Mbedui kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), akauliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Madhambi makubwa ni yepi?" Akasema: "Kumshirikisha Allaah." Akauliza tena: "Kisha ni gani?" Akasema: "Yamini la uwongo." Akasema: "Yamini la uwongo ni nini?" Akasema: "Ni ile ambayo kwayo hunyang'anywa Muislamu mali yake", yaani kwa yamini ambalo ndani yake yuwasema uwongo.
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب ندب من حلف عَلَى يَمينٍ فرأى غيرها خيراً مِنْهَا
أنْ يفعل ذَلِكَ المحلوف عَلَيْهِ ثُمَّ يُكَفِّر عن يمينه
063-Mlango Wa Sunnah kwa Mwenye Kula Yamini Akaona Kufanya Kinyume na Yamini Hiyo Ndiyo Bora, Hivyo Alifanye Hilo Kisha Afanye Kafara la Kufanya Kinyume na Yamini Lake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عبد الرحمان بن سَمُرَةَ رضي الله عنه قَالَ : قَالَ لي رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( وَإِذَا حَلَفْتَ عَلَى يَمِينٍ ، فَرَأيْتَ غَيْرَهَا خَيْراً مِنْهَا ، فَأتِ الَّذِي هُوَ خَيرٌ وَكَفِّرْ عَنْ يَمِينِكَ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abdir-Rahmaan bin Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Na kama utakula yamini na akaona kisicho kuwa yamini yako ndicho bora basi fanya ambacho ni bora na itolee kafara yamini yako." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawud, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ حَلَفَ عَلَى يَمينٍ ، فَرَأى غَيْرَهَا خَيْراً مِنْهَا ، فَلْيُكَفِّرْ عَنْ يَمِينِهِ ، وَلْيَفْعَلِ الَّذِي هُوَ خَيْرٌ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Mwenye kula yamini na akaona kisicho kuwa yamini yako ndicho bora, aitolee kafara yamini na afanye ambacho ni bora." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي موسى رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إنِّي واللهِ إنْ شاءَ اللهُ لا أحْلِفُ عَلَى يَمِينٍ ، ثُمَّ أَرَى خَيراً مِنْهَا إِلاَّ كَفَّرْتُ عَنْ يَمِينِي ، وَأَتَيْتُ الَّذِي هُوَ خَيْرٌ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Na mimi Wa-Allaahi! Allaah akitaka, sitakula yamini, halafu nikaona kinyume chake ni bora kuliko yamini hiyo isipokuwa nitaitolea kafara yamini yangu na nitakifanya ambacho ni bora zaidi." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لأَنْ يَلَجَّ أَحَدُكُمْ في يَمِينِهِ في أهْلِهِ آثَمُ لَهُ عِنْدَ اللهِ تَعَالَى مِنْ أنْ يُعْطِي كَفَّارَتَهُ الَّتي فَرَضَ اللهُ عَلَيْهِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kuendelea mmoja wenu na yamini yake kwa jambo linalohusu familia yake, dhambi yake ni kubwa zaidi mbele ya Allaah kuliko kutoa kafara ambayo Allaah Ameiwajibisha juu yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب العفو عن لغو اليمين
وأنَّه لا كفارة فِيهِ ، وَهُوَ مَا يجري عَلَى اللسان بغير
قصد اليمين كقوله عَلَى العادة : لا والله ، وبلى والله ، ونحو ذَلِكَ
064-Mlango Wa Kusamehewa kwa Kutotekeleza Yamini ya Upuuzi Kuwa Halina Kafara, Nayo ni Kusema kwa Ulimi Bila ya Kukusudia Yamini Kama Kauli Yake ya Ada: Sivyo Wa-Allaahi na Ndio Wa-Allaahi na Mfano wake
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ ﴿٨٩﴾
Allaah Hatokuchukulieni kwa viapo vyenu vya upuuzi, lakini Atakuchukulieni kwa (kuvunja) viapo mlivyoapa kwa niyyah mlioifunga thabiti. Basi kafara yake ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu, au kuwavisha nguo, au kuacha huru mtumwa. Lakini asiyeweza kupata (katika hayo), basi afunge Swiyaam siku tatu. Hiyo ndio kafara ya viapo vyenu mnapoapa. Na hifadhini yamini zenu. [Al-Maaidah: 89]
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : أُنْزِلَتْ هذِهِ الآية : [ لاَ يُؤاخِذُكُمُ اللهُ بِاللَّغْوِ في أَيْمَانِكُمْ ] في قَوْلِ الرَّجُلِ : لا واللهِ ، وَبَلَى واللهِ . رواه البخاري .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Ayah hii iliteremshwa: 'Allaah Hatokuchukulieni kwa viapo vyenu vya upuuzi' (Aal-'Imraan: 89), kwa mtu anaye kuwa na mazoea ya kusema: 'Sivyo hivyo Wa-Allaahi na ndio Wa-Allaahi'." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الحلف في البيع وإنْ كان صادقاً
065-Mlango Wa Ukaraha wa Kula Yamini katika Biashara Hata Akiwa Mkweli
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرةَ رضي الله عنه قال : سَمِعتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( الحَلِفُ مَنْفَقَةٌ لِلسِّلْعَةِ ، مَمْحَقَةٌ لِلْكَسْبِ )) . متفق عليه .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Kuapa sana katika biashara huenda kukaongeza mauzo lakini inafuta faida yote uliyopata." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 2
وعن أبي قتادة رضي الله عنه : أنَّه سمعَ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( إيَّاكُمْ وَكَثْرَةَ الحَلِفِ فِي البَيْعِ ، فَإنَّهُ يُنَفِّقُ ثُمَّ يَمْحَقُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Jiepusheni na kuapa yamini sana katika kuuza (bidhaa zenu), kwani hilo mwanzo huboresha biashara na kisha huleta hasara." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة أنْ يسأل الإنسان بوجه الله عزوجل
غير الجنة ، وكراهة منع من سأل بالله تعالى وتشفع به
066-Mlango Wa Ukaraha wa Mtu Kuomba kwa Jina la Allaah Mbali na Jannah na Ukaraha wa Kumkataza Mwenye Kuomba kwa Allaah Ta'aalaa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن جابر رضي الله عنه قالَ : قالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ يُسْأَلُ بِوَجْهِ اللهِ الا الجَنَّةُ )) . رواه أبو داود .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakiombwi kwa jina la Allaah ila Jannah." [Abu Daawuwd]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قال : قال رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنِ اسْتَعَاذَ بِاللهِ ، فَأعِيذُوهُ ، وَمَنْ سَأَلَ بِاللهِ ، فأَعْطُوهُ ، وَمَنْ دَعَاكُمْ ، فَأَجِيبُوهُ ، وَمَنْ صَنَعَ إلَيْكُمْ مَعْرُوفاً فَكَافِئُوهُ ، فَإنْ لَمْ تَجِدُوا ما تُكَافِئُونَهُ بِهِ فَادْعُوا لَهُ حَتَّى تَرَوْا أَنَّكُمْ قَد كَافَأْتُمُوهُ )) . حديث صحيح رواه أبو داود والنسائي بأسانيد الصحيحين .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kutaka ulinzi kwa Allaah atapatiwa, na mwenye kutaka kitu kwa Allaah, pia atamtekelezea. Na mwenye kukualika itikia mwaliko wake, na mwenye kuwafanyia wema, na mlipeni na mkikosa cha kumlipa basi muombeeni dua mpaka mkinai kuwa mmemlipa kwa wema aliowafanyia." [Hadiyth Swahiyh iliyonukuliwa na Abu Daawuwd na An-Nasaaiy kwa Isnaad zilizo Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم قوله : شاهنشاه للسلطان وغيره
لأن معناه ملك الملوك ، ولا يوصف بذلك غير الله سبحانه وتعالى
067-Mlango Wa Uharamu wa Kujiita Shaahinshah kwa Sultani na Wengineo Kwani Maana yake ni Mfalme wa Wafalme na kwa Hilo Hasifiwi Nalo ila Allaah Ta'aalaa
Alhidaaya.com [4]
وعن أبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم قال : (( إنَّ أَخْنَعَ اسْمٍ عِنْدَ اللهِ عزوجل رَجُلٌ تَسَمَّى مَلِكَ الأَمْلاَكِ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika majina yaliyo dhalili mno na mabaya mbele ya Allaah Ta'aalaa ni mtu kujiita Malikal Amlaak (Mfalme wa Wafalme)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daaawud na At-Tirmidhiy].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن مخاطبة الفاسق والمبتدع ونحوهما بِسَيِّد ونحوه
068-Mlango Wa Kukatazwa Kumuita Fasiki na Mzushi na Mfano Wao kwa Jina la Bwana na Mfano wake
Alhidaaya.com [4]
عن بُريَدَةَ رضي الله عنه قالَ : قالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَقُولُوا لِلْمُنَافِقِ سَيِّدٌ، فَإنَّهُ إنْ يَكُ سَيِّداً فَقَدْ أسْخَطْتُمْ رَبَّكُمْ عزوجل )) . رواه أبو داود بإسنادٍ صحيح.
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usimuite mnafiki Bwana, kwani akiwa yeye atakuwa ni bwana, hakika mtakuwa mmemkasirisha Rabb wenu 'Azza wa Jalla." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة سب الحمّى
069-Mlango Wa Ukaraha wa Kuitukana Homa
Alhidaaya.com [4]
عن جابر رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم دخلَ على أُمِّ السَّائِبِ ، أو أُمِّ المُسَيّبِ فَقَالَ : (( مَا لَكِ يَا أُمَّ السَّائِبِ – أو يَا أُمَّ المُسَيَّبِ – تُزَفْزِفِينَ ؟ )) قَالَتْ : الحُمَّى لاَ بَارَكَ اللهُ فِيهَا ! فَقَالَ : (( لاَ تَسُبِّي الحُمَّى فَإنَّهَا تُذْهِبُ خَطَايَا بَنِي آدَمَ كَمَا يُذْهِبُ الكِيْرُ خَبَثَ الحَدِيدِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimzuru Ummus Saaib au Ummul Musayyab (Radhwiya Allaahu 'anhu), akamuuliza: "Una nini, ee Ummus Saaib au ee Ummus Musayyab? kwa nini unatetemeka?" Akasema: "Ni homa, Allaah Asiibariki." Akasema (Swalla Allaahu 'alyhi wa aalihi wa sallam): "Usiitukane homa, kawani inaondosha makosa ya mwanadamu kama vile tanuri (ya moto inayotumiwa na mfuaji vyuma) inavyosafisha uchafu wa chuma." [Muslim].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن سب الريح ، وبيان ما يقال عند هبوبها
070-Mlango Wa Kukatazwa Kutukana Upepo na Kubainisha Kinacho Semwa Wakati wa Kuvuma Kwake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي المنذِرِ أُبي بن كعب رضي الله عنه قال : قالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَسُبُّوا الرِّيحَ ، فَإِذَا رَأَيْتُمْ مَا تَكْرَهُونَ ، فَقُولُوا : اللَّهُمَّ إنَّا نَسْأَلُكَ مِنْ خَيْرِ هذِهِ الرِّيحِ وَخَيْرِ مَا فِيهَا وخَيْرِ مَا أُمِرَتْ بِهِ . وَنَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ هذِهِ الرِّيحِ وَشَرِّ مَا فِيهَا وَشَرِّ مَا أُمِرَتْ بِهِ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Mundhir Ubayy bin Ka'ab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usiutukane upepo, mukiona munayo yachukia, semeni: 'Allaahumma inniy nasaluka min khayri haadhihir riyh wa khayri maa fiyhaa wa khayri maa umirat bihi wa na'uwdhu bika min sharri haadhihir riyh wa sharri maa umirat bihi (Ee Rabb wangu! Hakika sisi tunakuomba kheri ya upepo huu na kheri iliyo ndani yake na kheri kilicho amrishwa kwayo. Na tunajilinda Kwako na shari ya upepo huu na shari iliyoko ndani yake na shari kilicho amrishwa kwayo)." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh].
Hadiyth – 2
وعن أبي هريرة رضي الله عنه قال : سمعتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( الرِّيحُ مِنْ رَوحِ اللهِ ، تَأتِي بِالرَّحْمَةِ ، وَتَأتِي بِالعَذَابِ ، فَإذَا رَأَيْتُمُوهَا فَلاَ تَسُبُّوهَا ، وَسَلُوا اللهَ خَيْرَهَا ، وَاسْتَعِيذُوا باللهِ مِنْ شَرِّهَا )) . رواه أبو داود بإسناد حسن .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Upepo ni baraka kutoka kwa Allaah, unakuja pamoja na rehema na adhabu. Hivyo, mnapouona musiutukane na mtakeni Allaah Awapatieni kheri kutoka kwa huo upepo na takeni ulinzi kwa Allaah kutokana na shari yake (huo upepo)." [Abu aawuwd kwa Isnaad iliyo Hasan]
Hadiyth – 3
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كان النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم إذا عَصَفَتِ الرِّيحُ قال : (( اللَّهُمَّ إنِّي أسْألُكَ خَيْرَهَا وَخَيْرَ مَا فِيهَا وَخَيْرَ مَا أُرْسِلَتْ بِهِ ، وأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّهَا وَشَرِّ مَا فِيهَا وَشَرِّ مَا أُرْسِلَتْ بِهِ )) . رواه مسلم .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Alikuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) unapovuma upepo wa nguvu akiomba: "Allaahumma inniy asaluka khayrahaa wa khayra maa fiyhaa wa khayra maa ursilat bihi wa a'uwdhu bika min sharrihaa wa sharri maa fiyhaa wa sharri maa ursilat bihi (Ee Rabb wangu! Hakika mimi ninakuomba kheri yake na kheri iliyo ndani yake na kheri kilicho amrishwa kwayo. Na ninajilinda Kwako na shari ya upepo huu na shari iliyoko ndani yake na shari kilicho amrishwa kwayo)." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة سب الديك
071-Mlango Wa Ukaraha wa Kumtukana Jogoo
Alhidaaya.com [4]
عن زيد بن خالد الجُهَنِيِّ رضي الله عنه قال : قال رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَسُبُّوا الدِّيكَ فَإنَّهُ يُوِقِظُ لِلصَّلاَةِ )) . رواه أبو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Zayd bin Khaalid Al-Juhaniy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Musimtukane jogoo, kwani yeye anawaamsha kwa ajili ya Swalaah." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن قول الإنسان : مُطِرنا بنَوء كذا
072-Mlango Wa Kukatazwa kwa Mtu Kusema: Tumepata Mvua Kutokana na Nyota Kadha
Alhidaaya.com [4]
عن زيد بن خالد رضي الله عنه قال : صلَّى بنا رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم صَلاَةَ الصُّبْحِ بِالحُدَيْبِيَّةِ في إثْرِ سَمَاءٍ كَانَتْ مِنَ اللَّيْلِ ، فَلَمَّا انْصَرَفَ أقْبَلَ عَلَى النَّاسِ ، فقالَ : (( هَلْ تَدْرُونَ مَاذَا قالَ رَبُّكُمْ ؟ )) قالُوا : اللهُ وَرَسُولُهُ أعْلَمُ . قال : (( قالَ : أصْبَحَ مِنْ عِبَادِي مُؤْمِنٌ بِي ، وَكَافِرٌ ، فَأَمَّا مَنْ قَالَ : مُطِرْنَا بِفَضْلِ اللهِ وَرَحْمَتِهِ ، فَذلِكَ مُؤْمِنٌ بِي كَافِرٌ بِالكَوْكَبِ ، وأَما مَنْ قَالَ مُطِرْنَا بِنَوءِ كَذَا وَكَذَا ، فَذلكَ كَافِرٌ بِي مُؤْمِنٌ بِالكَوْكَبِ )) . متفق عليه .
Amesema Zayd bin Khaalid (Radhwiya Allaahu 'anhu): Alituswalisha sisi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Swalaah ya Asubuhi katika Hudaybiyah baada ya mvuaa zilizonyesha usiku uliopita. Alipomaliza akawaelekea watu na kuwauliza: "Je, mnaelewa Alichosema Rabb wenu?" Wakajibu: "Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi." Akasema: "Baadhi ya waja wangu wamepambazukiwa na asubuhi wakiwa Wananiamini na baadhi Wamenikufuru; ama aliyesema tumepata mvua kwa fadhila ya Allaah na Rehema Zake, basi huyo ni mwenye kuniamini na mwenye kukufuru nyota; ama mwenye kusema tumepata mvua kutokana na nyota kadha wa kadha huyo Amenikufuru na ni mwenye kuamini nyota." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم قوله لمسلم : يا كافر
073-Mlango Wa Uharamu wa Kumwambia Muislamu: Ee Kafiri
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما ، قال : قالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إذَا قَالَ الرَّجُلُ لأَخِيهِ : يَا كَافِرُ ، فَقَدْ بَاءَ بِهَا أَحَدُهُمَا ، فَإنْ كانَ كَمَا قَالَ وَإلاَّ رَجَعَتْ عَلَيْهِ )) متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapomwambia mtu ndugu yake, ee kafiri! Basi hakika (ukafiri huo utakuwa) umethibiti kati ya mmoja wao. Ikiwa ni kama alivyosema (aliyeitwa hivyo atakuwa kama alivyoambiwa kafiri) na ikiwa ni kinyume na hivyo ukafiri utarudi kwake (yaani msemaji)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أبي ذرٍّ رضي الله عنه : أنَّه سَمِعَ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( مَنْ دَعَا رَجُلاً بالكُفْرِ ، أو قالَ : عَدُوَّ اللهِ ، وَلَيْسَ كَذلكَ إلاَّ حَارَ عَلَيْهِ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kumuita mtu mwengine kafiri au akasema: adui wa Allaah na si kama alivyosema isipokuwa sifa hiyo hurudi kwake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الفحش وبذاء اللسان
074-Mlango Wa Kukatazwa Kutoa Maneno Machafu na ya Kishenzi
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن مسعودٍ رضي الله عنه ، قال : قالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لَيْسَ المُؤْمِنُ بالطَّعَّانِ ، وَلاَ اللَّعَّانِ ، وَلاَ الفَاحِشِ ، وَلاَ البَذِيِّ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini hawi ni mwenye kusuta wala kulaani kutupa maneno machafu wala kutusi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 2
وعن أنسٍ رضي الله عنه قال : قالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَا كَانَ الفُحْشُ فِي شَيْءٍ إلاَّ شَانَهُ ، وَمَا كَانَ الحَيَاءُ فِي شَيْءٍ إلاَّ زَانَهُ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Utumiaji wa maneno machafu hauchang'anyiki na kitu chochote isipokuwa hukichafua. Na haya haiwi pamoja na kitu chochote isipokuwa hukirembehsa." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة التقعير في الكلام
والتشدُّق فيه وتكلف الفصاحة واستعمال وحشي اللُّغة
ودقائق الإعراب في مخاطبة العوام ونحوهم
075-Mlango Wa Ukaraha wa Mazungumzo ya Kukera na kuvupa Mipaka Ndani Yake na Kujikalifisha katika Ufasaha na Kutumia Lugha Mbaya
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن مسعود رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( هَلَكَ المُتَنَطِّعُونَ )) قَالَهَا ثَلاَثاً . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wameangamia wenye kushadidisha mambo." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قال : (( إنَّ اللهَ يُبْغِضُ البَلِيغَ مِنَ الرِّجَالِ الَّذي يَتَخَلَّلُ بِلِسَانِهِ كَمَا تَتَخَلَّلُ البَقَرَةُ )) . رواه أبو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Anamchukia mwenye kugeuza ulimi wake kwa ufasaha wa mazungumzo miongoni mwa wanaume sawa na vile anavyofanya ng'ome anapokuwa kala malisho yake." [Abu Daawud na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 3
وعن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قال : (( إنَّ مِنْ أحَبِّكُمْ إِلَيَّ ، وأقْرَبِكُمْ مِنِّي مَجْلِساً يَومَ القِيَامَةِ ، أحَاسِنكُمْ أَخْلاَقَاً ، وإنَّ أَبْغَضَكُمْ إلَيَّ ، وأبْعَدَكُمْ مِنِّي يَومَ القِيَامَةِ ، الثَّرْثَارُونَ وَالمُتَشَدِّقُونَ وَالمُتَفَيْهِقُونَ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) . وقد سبق شرحه في بَابِ حُسْنِ الخُلُقِ .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir bin 'Abdillaah (radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika watakaopendwa zaidi na watakao kuwa karibu nami Siku ya Qiyaamah ni wale wenye tabia nzuri. Na hakika nitakaowachukia na watakao kuwa mbali nami Siku ya Qiyaamah ni wale ma-tharthar (wale wenye kuzungumza sana kwa kujikalifisha) na mutashaddiquwn (wanaorefusha mazungumzo yao kwa watu na waazungumza kwa kujaza midomo yaokwa majisifu) na mutafayhiquwn (Wenye kiburi)." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة قوله : خَبُثَتْ نَفْسي
076-Mlango Wa Ukaraha wa Mtu Kusema Nafsi Yangu Imekuwa Mbaya
Alhidaaya.com [4]
عن عائشة رضي الله عنها ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَ يَقُولَنَّ أَحَدُكُمْ : خَبُثَتْ نَفْسي ، وَلكِنْ لِيَقُلْ : لَقِسَتْ نَفْسي )) متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asiseme mmoja wenu, 'Khabuthat nafsiy (kichefuchefu kimenizidi kwa ajili ya kuvimbiwa)'." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة تسمية العنب كرماً
077-Mlango Wa Ukaraha wa Kuziita Zabibu kwa Jina Karm
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرة رضي الله عنه ، قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تُسَمُّوا العِنَبَ الكَرْمَ ، فَإنَّ الكَرْمَ المُسْلِمُ )) متفق عليه ، وهذا لفظ مسلم .
وفي رواية : (( فَإنَّمَا الكَرْمُ قَلْبُ المُؤمِنِ )) . وفي رواية للبخاري ومسلم :
(( يَقُولُونَ الكَرْمُ ، إنَّمَا الكَرْمُ قَلْبُ المُؤْمِنِ )) .
Imepoewa kutoka kwake Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msiite zabibu Karm, hakika Al-Karm ni Muislamu." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Muslim].
Na katika riwaayah nyengine: "Kwa hakika si kitu kingine bali Al-Karm ni moyo wa Muumini."
Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy na Muslim: "Watu husema: 'Al-Karm (ukarimu).' Hakika si kitu kingine bali Al-Karm ni moyo wa Muumini."
Hadiyth – 2
وعن وائلِ بنِ حُجرٍ رضي الله عنه ، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَ تَقُولُوا : الكَرْمُ ، وَلكِنْ قُولُوا : العِنَبُ ، والحَبَلَةُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Waail bin Hujr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Musiseme: 'Al-Karam', lakini semeni: 'Al-'inab (zabibu) na Al-Habalah (zabibu)'." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن وصف محاسن المرأة لرجل
إلاَّ أن يحتاج إلى ذلك لغرض شرعي كنكاحها ونحوه
078-Mlango Wa Kukatazwa Kuusifu Uzuri wa Mwanamke Mbele ya Mwanaume ila Anapohitajia Hilo kwa Haja Inayokubaliwa na Sheria Kama Kumuoa na Mfano Wake
Alhidaaya.com [4]
عن ابن مسعودٍ رضي الله عنه ، قال : قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تُبَاشِرِ المَرْأَةُ المَرْأَةَ ، فَتَصِفَهَا لِزَوْجِهَا كَأَنَّهُ يَنْظُرُ إلَيْهَا )) . متفق عليه .
imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwanamke asimguse mwanamke mwenziwe sehemu zake za siri kisha amsifie mumewe uzuri wake wa kimaumbile kama kwamba anamuona." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة قول الإنسان : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي إنْ شِئْتَ
بل يجزم بالطلب
079-Mlango Wa Ukaraha wa Mtu Kusema: Ee Mola Wangu Nisamehe Ukipenda Bali Aazimie katika Maombi
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَ يَقُولَنَّ أَحَدُكُمْ : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي إنْ شِئْتَ : اللَّهُمَّ ارْحَمْنِي إنْ شِئْتَ ، لِيَعْزِم المَسْأَلَةَ ، فَإنَّهُ لاَ مُكْرِهَ لَهُ )) . متفق عليه .
وفي رواية لمسلم : (( وَلكِنْ لِيَعْزِمْ وَلْيُعَظمِ الرَّغْبَةَ فَإنَّ اللهَ تَعَالَى لاَ يَتَعَاظَمُهُ شَيْءٌ أَعْطَاهُ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asiseme mmoja wenu: 'Ee Mola wangu nisamehe ukitaka. Ee Mola wangu nirehemu Ukitaka.' Bali aazimie katika kumuomba Allaah kwa sababu hakuna wa kumlazimisha Yeye (Allaah)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Na riwaayah ya Muslim: "Lakini aazimie na awe na matumaini makubwa, kwani hakuna kitu chochote ambacho ni kikubwa kwa Allaah Ta'aalaa kutoa."
Hadiyth – 2
وعن أنس رضي الله عنه قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إذا دَعَا أحَدُكُمْ فَلْيَعْزِم المَسْأَلَةَ ، وَلاَ يَقُولَنَّ : اللَّهُمَّ إنْ شِئْتَ ، فَأَعْطِنِي ، فَإنَّهُ لاَ مُسْتَكْرِهَ لَهُ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapoomba mmoja wenu aazimie kwa dhati na asiseme: 'Ee Mola wangu! Ukitaka nipe'. Kwa sababu hakuna wa Kumkalifisha kitu dhidi ya Utashi Wake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة قول : ما شاء اللهُ وشاء فلان
080-Mlango Wa Ukaraha wa Kusema: Akipenda Allaah na Akapenda Fulani
Alhidaaya.com [4]
عن حُذَيْفَةَ بنِ اليمانِ رضي الله عنه ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَ تَقُولُوا : مَا شَاءَ اللهُ وَشَاءَ فُلاَنٌ ؛ وَلكِنْ قُولُوا : مَا شَاءَ اللهُ ، ثُمَّ شَاءَ فُلاَنٌ )) . رواه أبو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwake Hudhayfah bin Al-Yamaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Usiseme: 'Akitaka Allaah na kutaka fulani', lakini sema: 'Akipenda Allaah, kishaa akapenda fulani'." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الحديث بعد العشاء الآخرة
081-Mlango Wa Ukaraha wa Mazungumzo Baada ya Ishaa ya Mwisho
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي بَرْزَةَ رضي الله عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم كان يكرهُ النَّومَ قَبْلَ العِشَاءِ والحَديثَ بَعْدَهَا . متفقٌ عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Barzah (Radhwiya Allaah 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akichukia kulala kabla ya Ishaa na mazungumzo baada yake. [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
عن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم صَلَّى العِشَاء في آخِرِ حَيَاتِهِ ، فَلَمَّا سَلَّمَ قال : (( أرأيْتَكُمْ لَيْلَتَكُمْ هذِه ؟ فَإنَّ عَلَى رَأسِ مِئَةِ سَنَةٍ لاَ يَبْقَى مِمَّنْ هُوَ علَى ظَهْرِ الأرْضِ اليَومَ أحَدٌ )) . متفق عليه .
Imepokewa kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliswalisha Ishaa katika mwisho wa maisha yake, pindi alipomaliza alisema: "Munajua kitu kuhusu usiku wenu huu? Hakika mwisho wa miaka mia kutoka sasa, hakuna mtu yeyote ambaye yuko katika ardhi atabaki hai wakati huo." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أنس رضي الله عنه : أنَّهم انتظروا النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم ، فَجَاءهُمْ قَريباً مِنْ شَطْرِ اللَّيْلِ فَصَلَّى بِهِمْ - يَعْنِي : العِشَاءَ - ثمَّ خَطَبنا فقالَ : (( ألاَ إنَّ النَّاسَ قَدْ صَلُّوا ، ثُمَّ رَقَدُوا ، وَإنَّكُمْ لَنْ تَزَالُوا فِي صَلاَةٍ مَا انْتَظَرْتُمُ الصَّلاَةَ )) . رواه البخاري .
Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) anasimulia kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliakhirisha usiku mmoja Swalaah ya Ishaa mpaka nusu ya usiku. Baada ya Swalaah alitukabili na kusema: "Baadhi ya watu waliswali na kwenda kulala lakini waliosuburi (ili kuwahi Swalaah ya jamaa) walikuwa katika Swalaah kuanzia walipoanza kuingojea." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم امتناع المرأة من فراش زوجها
إِذَا دعاها ولم يكن لَهَا عذر شرعي
082-Mlango Wa Uharamu wa Mke Kukataa Mwito wa Mumewe Anapomuita Kitandani na Hana Udhuru Wowote wa Kisheria
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا دَعَا الرَّجُلُ امْرَأتَهُ إِلَى فِرَاشِهِ فَأبَتْ ، فَبَاتَ غَضْبَانَ عَلَيْهَا ، لَعَنَتْهَا المَلاَئِكَةُ حَتَّى تُصْبحَ )) متفق عَلَيْهِ .
وفي رواية : (( حَتَّى تَرْجعَ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapomuita mume, mkewe kwenye firasha (kwa jimai) na asije, hivyo mume kulala akiwa na hasira, mke analaaniwa na Malaaikah mpaka kunapopambazuka." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah nyengine: "Mpaka atakaporudi (na kumtekelezea mumewe mahitaji yake)."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم صوم المرأة تطوعاً وزوجها حاضر إِلاَّ بإذنه
083-Mlango Wa Uharamu wa Mwanamke Kufunga na Mumewe Yupo Nyumbani (Au Mjini) Bila ya Idhini Yake
Alhidaaya.com [4]
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَحِلُّ لِلْمَرْأَةِ أَنْ تَصُومَ وَزَوْجُهَا شَاهِدٌ إِلاَّ بِإذْنِهِ ، وَلاَ تَأذَنَ فِي بَيْتِهِ إِلاَّ بِإذْنِهِ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Si halali kwa mwanamke kufunga sawm na mumewe yupo (mjini) isipokuwa kwa idhini yake. Na pia haifai kwake kumkubalia mtu kuingia nyumbani kwake isipokuwa kwa idhini ya mumewe." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم رفع المأموم رأسه من الركوع
أَو السجود قبل الإمام
084-Mlango Wa Uharamu wa Kunyanyua Maamuma Kichwa chake Kutoka katika Rukuu au Sijda Kabla ya Imam
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أمَا يَخْشَى أحَدُكُمْ إِذَا رَفَعَ رَأسَهُ قَبْلَ الإمَامِ أنْ يَجْعَلَ اللهُ رَأسَهُ رَأسَ حِمَارٍ ! أَوْ يَجْعَلَ اللهُ صُورَتَهُ صُورَةَ حِمَارٍ )) متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kea Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hivi kwa nini haogopi mmoja wenu anapoinua kichwa chake kabla ya Imam, Allaah Akakibadilisha kuwa kichwa cha punda au Allaah Kuifanya sura yake kuwa ya punda." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة وضع اليد عَلَى الخاصرة في الصلاة
085-Mlango Wa Ukaraha wa Kuweka Mkono Kiunoni katika Swalaah
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم نَهَى عن الخَصْرِ في الصَّلاَةِ . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kuweka mkono kiunoni katika Swalaah." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الصلاة بحضرة الطعام ونفسه تتوق إِلَيْهِ
أَوْ مَعَ مدافعة الأخبثين : وهما البول والغائط
086-Mlango Wa Ukaraha wa Kuswali Pindi Chakula Kinapokuwa Tayari na Nafsi yake Imevutiwa Kwayo au Kushikwa na Haja Mbili: Nazo ni Ndogo na Kubwa
Alhidaaya.com [4]
عن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( لا صَلاَةَ بِحَضْرَةِ طَعَامٍ ، وَلاَ وَهُوَ يُدَافِعُهُ الأَخْبَثَانِ )) . رواه مسلم .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hapana Swalaah pindi chakula kinapokuwa tayari wala anapotingwa na uchafu wa aina mbili (yaani haja ndogo na kubwa)." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن رفع البصر إِلَى السماء في الصلاة
087-Mlango Wa Kukatazwa Kunyanyua Macho Juu Mbinguni katika Swalaah
Alhidaaya.com [4]
عن أنس بن مالك رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَا بَالُ أقْوامٍ يَرْفَعُونَ أبْصَارَهُمْ إِلَى السَّمَاءِ في صَلاَتِهِمْ ! )) فَاشْتَدَّ قَولُهُ في ذَلِكَ حَتَّى قَالَ :(( لَيَنْتَهُنَّ عَنْ ذَلِكَ ، أَوْ لَتُخطفَنَّ أَبْصَارُهُمْ ! )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wana nini watu wanaonyanyua macho yao juu mbinguni wakiwa katika Swalaah zao." Akawa mkali na kuwaonya wasifanye hivyo mpaka akasema: "Wakome kufanya hivyo au watapofolewa macho yao." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الالتفات في الصلاة لغير عذر
088-Mlango Wa Ukaraha wa Kugeuka Geuka katika Swalaah Bila Udhuru Wowote
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : سألت رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم عَنِ الالتفَاتِ في الصَّلاَةِ ، فَقَالَ : (( هُوَ اخْتِلاَسٌ يَخْتَلِسُهُ الشَّيْطَانُ مِنْ صَلاَةِ العَبْدِ )) . رواه البخاري .
Amasema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu kugeuka (upande wa kulia na kushoto) katika Swalaah, akasema: "Kufanya hivyo ni udokozi anaodokoa shetani katika Swalaah ya mja." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن أنس رَضِيَ اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إيَّاكَ والالتِفَاتَ فِي الصَّلاَةِ ، فَإنَّ الالتفَاتَ في الصَّلاَةِ هَلَكَةٌ ، فَإنْ كَانَ لاَ بُدَّ ، فَفِي التَّطَوُّعِ لاَ في الفَريضَةِ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Jiepushe na kugeuka geuka katika Swalaah, kwani kugeuka katika Swalaah ni maangamivu. Ikiwa hapana budi mpaka ugeuke basi iwe sio katika Swalaah ya faradhi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الصلاة إِلَى القبور
089-Mlango Wa Kukatazwa Kuswali Makaburini
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي مَرْثَدٍ كَنَّازِ بْنِ الحُصَيْنِ رضي الله عنه قَالَ : سَمِعْتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( لا تُصَلُّوا إِلَى القُبُورِ ، وَلاَ تَجْلِسُوا عَلَيْهَا )) . رواه مسلم .
Amesema Abu Marthad Kannaaz bin Al-Huswayn (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Msiswali kwa kuelekea makaburi wala musikae juu yake." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم المرور بَيْنَ يدي المصلِّي
090-Mlango Wa Uharamu wa Kupita Mbele ya Wenye Kuswali
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي الجُهَيْمِ عبد اللهِ بن الحارِثِ بن الصِّمَّةِ الأنْصَارِيِّ رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لَوْ يَعْلَمُ المَارُّ بَيْنَ يَدَيِ المُصَلِّي مَاذَا عَلَيْهِ لَكَانَ أنْ يَقِفَ أرْبَعِينَ خَيْراً لَهُ مِنْ أنْ يَمُرَّ بَيْنَ يَدَيْهِ )) قَالَ الراوي : لا أدْرِي قَالَ : أرْبَعينَ يَوماً ، أَوْ أرْبَعِينَ شَهْراً ، أَوْ أرْبَعِينَ سَنَةً .متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abil Juhaym 'Abdillaah bin Al-Haarith bin Asw-Swimmah Al-Answariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)amesema: "Lau ungejua madhambi anayopata mwenye kupita mbele ya mtu anayeswali basi ingekuwa ni bora kwake kusimama arobaini kuliko kupita mbele yake." Amesema mpokezi wa Hadiyth hii: "Sina hakika alisema siku arobaini au miezi arobaini au miaka arobaini." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة شروع المأموم في نافلة
بعد شروع المؤذن في إقامة الصلاة
سواء كَانَتْ النافلة سنة تلك الصلاة أَوْ غيرها
091-Mlango Wa Ukaraha wa Kuanza Maamuma Swalaah ya Sunnah Baada ya Muadhini Kukimu Swalaah
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( إِذَا أُقِيمَتِ الصَّلاَةُ فَلاَ صَلاَةَ إِلاَّ المَكْتُوبَةَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kunapo kimiwa Swalaah, hapana Swalaah inayo ruhusiwa isipokuwa ile ya faradhi." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة تخصيص يوم الجمعة بصيام أَوْ ليلته بصلاة من بين الليالي
092-Mlango Wa Ukaraha wa Kuihusisha Siku ya Ijumaa kwa Funga au Usiku wake kwa Swalaah Miongoni mwa Masiku Mengine
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لا تَخُصُّوا لَيْلَةَ الجُمُعَةِ بِقِيَامٍ مِنْ بَيْنِ اللَّيَالِي ، وَلاَ تَخُصُّوا يَومَ الجُمُعَةِ بِصِيَامٍ مِنْ بَيْنِ الأَيَّامِ ، إِلاَّ أَنْ يَكُونَ فِي صَومٍ يَصُومُهُ أحَدُكُمْ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msikhusishe usiku wa Ijumaa kwa ajili ya kuswali Swalaah za Sunnah baina ya masiku mengine wala msikhusishe siku ya Ijumaa kwa ajili ya funga baina ya siku nyengine isipokuwa iwe ni funga ambayo hufunga mmoja wenu." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( لاَ يَصُومَنَّ أحَدُكُمْ يَوْمَ الجُمُعَةِ إِلاَّ يَوماً قَبْلَهُ أَوْ بَعْدَهُ )) . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Asifunge mmoja wenu siku ya Ijumaa isipokuwa siku kabla yake au baada yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن محمد بن عَبَّادٍ ، قَالَ : سَأَلْتُ جَابِراً رضي الله عنه : أنَهَى النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم عَنْ صَومِ الجُمُعَةِ ؟ قَالَ : نَعَمْ . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Muhammad bin 'Abbaad: Nilimuuliza Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Hivi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kufunga siku ya Ijumaa?" Akamjibu: "Ndiyo." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أُمِّ المُؤمِنِينَ جويرية بنت الحارث رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم دَخَلَ عَلَيْهَا يَوْمَ الجُمُعَةِ وهِيَ صَائِمَةٌ ، فَقَالَ : (( أصُمْتِ أمْسِ ؟ )) قالت : لا ، قَال: (( تُرِيدِينَ أنْ تَصُومِي غَداً ؟ )) قالتْ : لاَ . قَالَ : (( فَأَفْطِرِي )) . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Mama wa Waumini, Juwayriyah bint Al-Haarith (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimtembelea siku ya Ijumaa akiwa amefunga, akamuuliza: "Je, ulifunga jana?" Akasema: "Hapana." Akauliza tena: "Je, una niya ya kufunga kesho?" Akasema: "Hapana." Akamwambia: "Fungua (yaani usiendelee kufunga siku ya leo)." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الوصال في الصوم
وَهُوَ أنْ يصوم يَومَينِ أَوْ أكثر وَلاَ يأكل وَلاَ يشرب بينهما
093-Mlango Wa Uharamu wa Al-Wiswaal katika Funga, Nayo ni kwa Mtu Kufunga Siku Mbili au Zaidi Wala Hali Chakula wala Hanywi Chochote Baina Yake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة وعائشة رضي الله عنهما : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم نهى عن الوِصَالِ .متفق عَلَيْهِ.
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah na 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikataza funga ya Al-Aiswaal (kuunganisha). [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : نَهَى رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم عَنِ الوِصَالِ . قالوا : إنَّكَ تُواصِلُ ؟ قَالَ : (( إنِّي لَسْتُ مِثْلَكُمْ ، إنِّي أُطْعَمُ وَأُسْقَى )) . متفق عَلَيْهِ . وهذا لفظ البخاري .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikataza Al-Wiswaal Akaulizwa: "Mbona wewe unaunganisha?" Akajibu: "Hakika mimi si kama nyinyi, ninalishwa na kunyweshwa (yaani na Allaah)." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الجلوس عَلَى قبر
094-Mlango Wa Uharamu wa Kukaa Juu ya Kaburi
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لأنْ يَجْلِسَ أحَدُكُمْ عَلَى جَمْرَةٍ ، فَتُحْرِقَ ثِيَابَهُ فَتَخْلُصَ إِلَى جِلْدِهِ خَيْرٌ لَهُ مِنْ أنْ يَجْلِسَ عَلَى قَبْرٍ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Laiti mmoja wenu angalikalia kaa la moto ikaunguza nguo zake na ukapenya hadi kwenye ngozi yake ni bora zaidi kuliko kukaa juu ya kaburi." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن تجصيص القبر والبناء عليه
095-Mlango Wa Kukatazwa Kulipiga Plasta Kaburi na Kulijengea
Alhidaaya.com [4]
عن جابر رضي الله عنه قَالَ : نَهَى رسولُ الله صلى الله عليه وسلم أن يُجَصَّصَ القَبْرُ ، وأنْ يُقْعَدَ عَلَيْهِ ، وَأنْ يُبْنَى عَلَيْهِ . رواه مسلم .
Amesema Jaabir: Amekataza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kulipiga plasta, na kukaliwa juu yake na kulijengea. [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تغليظ تحريم إباق العبد من سيده
096-Mlango Wa Uzito wa Uharamu wa Mtumwa Kutoroka Kutoka kwa Bwana Wake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن جرير رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( أَيُّمَا عَبْدٍ أَبَقَ ، فَقَدْ بَرِئَتْ مِنْهُ الذِّمَّةُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jariyr bin 'Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtumwa yeyote anayekimbia (kutoka kwa bwana wake), hakika anakosa (na kuwa mbali) ulinzi wa Uislamu aliopatiwa." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن جرير رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا أَبَقَ العَبْدُ ، لَمْ تُقْبَلْ لَهُ صَلاَةٌ )) . رواه مسلم .
وفي روايةٍ : (( فَقَدْ كَفَرَ )) .
Imepokewa kutoka kwa Jariyr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pindi anapotoroka mtumwa (kutoka kwa bwana wake), Swalaah yake haitakubaliwa." [Muslim]
Na katika riwaayah nyengine: "Hakika amekufuru."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم الشفاعة في الحدود
097-Mlango Wa Uharamu wa Kumuombea Mtu katika Adhabu (Hadd)
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
الزَّانِيَةُ وَالزَّانِي فَاجْلِدُوا كُلَّ وَاحِدٍ مِّنْهُمَا مِائَةَ جَلْدَةٍ ۖ وَلَا تَأْخُذْكُم بِهِمَا رَأْفَةٌ فِي دِينِ اللَّـهِ إِن كُنتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۖ ﴿٢﴾
Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanamme mpigeni kila mmoja katika wawili hao mijeledi mia. Na wala isiwashikeni huruma kwa ajili yao katika Hukmu ya Allaah mkiwa nyinyi mnamwamini Allaah na Siku ya Mwisho. [An-Nuwr: 2]
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ قُرَيْشاً أهَمَّهُمْ شَأْنُ المَرْأَةِ المَخْزُومِيَّةِ الَّتي سَرَقَتْ ، فقَالُوا : مَنْ يُكَلِّمُ فِيهَا رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ؟ فقالوا : وَمَنْ يَجْتَرِئُ عَلَيْهِ إِلاَّ أُسَامَةُ بْنُ زَيْدٍ ، حِبُّ رَسُولِ اللهِِ صلى الله عليه وسلم . فَكَلَّمَهُ أُسَامَةُ ، فَقَالَ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( أتَشْفَعُ في حَدٍّ مِنْ حُدُودِ اللهِ تَعَالَى ؟! )) ثُمَّ قَامَ فاخْتَطَبَ ، ثُمَّ قَالَ : (( إنَّمَا أهْلَكَ الَّذِينَ قَبْلَكُمْ أنَّهُمْ كَانُوا إِذَا سَرَقَ فِيِهمُ الشَّرِيفُ تَرَكُوهُ ، وَإِذَا سَرَقَ فِيهِمُ الضَّعِيفُ ، أَقَامُوا عَلَيْهِ الحَدَّ ، وَايْمُ اللهِ لَوْ أنَّ فَاطِمَةَ بِنْتَ مُحَمَّدٍ سَرَقَتْ لَقَطَعْتُ يَدَهَا )) . متفق عَلَيْهِ .
وفي روايةٍ : فَتَلوَّنَ وَجْهُ رَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : (( أتَشْفَعُ في حَدٍّ مِنْ حُدُودِ اللهِ !؟ )) فَقَالَ أُسَامَةُ : اسْتَغْفِرْ لِي يَا رَسُولَ اللهِ . قَالَ : ثُمَّ أَمَرَ بِتِلْكَ المَرْأَةِ فَقُطِعَتْ يَدُهَا .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Maquraysh walikuwa na hamu sana kwa kesi ya mwanamke kutoka katika Makhzuum ambaye kwamba aliiba, wakasema: "Nani atazungumza na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya jambo hilo?" Wakasema: "Nani anaweza kuzungumza naye ila Usamah bin Zayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye ni kipenzi cha Rasuli wa Allaah?" Usamah alikwenda na kuzungumzu naye, hapo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Unamuombea msamaha kwa Hadd (adhabu) miongoni mwa adhabu alizotoa Allaah Ta'aalaa?" Kisha alisimama na kuhutubia watu kwa kusema: "Hakika waliangamia waliokuwa kabla yenu kwa sababu alipoiba mtukufu miongoni mwao alikuwa akiachiliwa na anapoiba dhaifu miongoni mwao basi walikuwa wakimuadhibu. Naapa kwa Allaah! Lau Faatimah bint Muhammad angeiba basi ningemkata mkono wake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah nyengine: "Uso wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ulibadilika rangi (kwa ghadhabu)." Akasema: "Unamuombea msamaha kwa Hadd miongoni mwa adhabu alizotoa Allaah?" Akasema Usamah (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Ee Rasuli wa Allaah! Niombee msamaha." Akasema: "Kisha akaletwa yule mwanamke, hivyo kukatwa mkono wake."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن التغوط في طريق الناس
وظلِّهم وموارد الماء ونحوها
098-Mlango Wa Kukatazwa Kwenda Haja Njiani, Mapito ya Watu, Sehemu ya Vivuli, katika Maji na Mfano wake
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾
Na wale wanaowaudhi Waumini wa kiume na Waumini wa kike bila ya kuwa wamechuma kosa, basi kwa yakini wamejibebea usingiziaji mkuu wa dhulma na dhambi bayana. [Al-Ahzaab: 58]
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( اتَّقُوا اللاَّعِنَيْنِ )) قالوا : وَمَا اللاَّعِنَانِ ؟ قَالَ : (( الَّذِي يَتَخَلَّى في طَرِيقِ النَّاسِ أَوْ في ظِلِّهِمْ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ogopeni laana mbili." Akaulizwa: "Na ni zipi hizo laana mbili?" Akasema: "Ni yule ambaye anakidhi haja yake katika ya njia inayotumiwa na watu au katika kivuli chao (sehemu ambayo watu hupumzika)." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن البول ونحوه في الماء الراكد
099-Mlango Wa Kukatazwa Kukojoa na Mfano Wake Katika Maji Yaliyotua
Alhidaaya.com [4]
عن جابر رضي الله عنه : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم نَهَى أنْ يُبَالَ في المَاءِ الرَّاكِدِ . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza (mtu yeyote) kukidhi haja yake ndani ya maji yaliyotuama. [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة تفضيل الوالد بعض أولاده
على بعض في الهبة
100-Mlango Wa Ukaraha wa Mzazi Kuwapendelea Baadhi ya Watoto Wake Juu ya Wengine Katika Hiba
Alhidaaya.com [4]
عن النعمان بن بشير رضي الله عنهما : أنَّ أباه أتَى بِهِ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم فقال : إنِّي نَحَلْتُ ابْنِي هَذَا غُلاماً كَانَ لِي ، فقال رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( أكُلَّ وَلَدِكَ نَحَلْتَهُ مِثْلَ هَذَا ؟ )) فقال : لا ، فقالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( فَأرْجِعهُ )) .
وفي روايةٍ: فقال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( أَفَعَلْتَ هذَا بِوَلَدِكَ كُلِّهِمْ ؟ )) قال : لا ، قال : (( اتَّقُوا الله واعْدِلُوا فِي أوْلادِكُمْ )) فَرَجَعَ أبي ، فَرَدَّ تِلْكَ الصَّدَقَةَ .
وفي روايةٍ : فقال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( يَا بَشيرُ ألَكَ وَلَدٌ سِوَى هَذَا ؟ )) فقالَ : نَعَمْ ، قال : (( أكُلَّهُمْ وَهَبْتَ لَهُ مِثْلَ هذَا ؟ )) قال : لا ، قال : (( فَلاَ تُشْهِدْنِي إذاً فَإنِّي لاَ أشْهَدُ عَلَى جَوْرٍ )) .
وفي روايةٍ : (( لاَ تُشْهِدْنِي عَلَى جَوْرٍ )) .
وفي رواية : (( أشْهِدْ عَلَى هذَا غَيْرِي ! )) ثُمَّ قال : (( أيَسُرُّكَ أنْ يَكُونُوا إلَيْكَ في البِرِّ سَواءً ؟ )) قال : بَلَى ، قال : (( فَلا إذاً )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa An-Nu'maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa, baba yake alimpeleka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Hakika nimempa mtumwa mwanangu huyu." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza: "Watoto wako wote umewapa kama hivyo?" Akajibu: "Hapana." Akamwambia: "Basi mrudishe."
Na katika riwaayah nyengine: Akasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Umefanya hivyo kwa watoto wako wote?" Akajibu: "Hapana." Akasema: "Mcheni Allaah na mfanye uadilifu kati ya watoto wenu." Alirudi babangu na kurejesha zawadi hiyo.
Na katika riwaayah nyengine: Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ee Bashiyr! Je, una watoto wengine mbali na huyu?" Akajibu: "Ndio." Akasema: "Je, umewapatia wote mfano wa huyu?" Akajibu: "Hapana." Akasema: "Hivyo, usinifanye mimi kuwa shahidi kwani mimi siwi shahidi wa udhalimu."
Na katika riwaayah nyengine: "Usinifanye shahidi kwa udhalimu."
Na katika riwaayah nyengine: "Mfanye asiyekuwa mimi kuwa shahidi." Kisha akasema: "Je, unapenda watoto wako wakutendee wema sawasawa." Akajibu: "Ndio." Akasema: "Hivyo, usifanye udhalimu sasa." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم إحداد المرأة على ميت فوق ثلاثة أيام
إلا على زوجها أربعة أشهر وعشرة أيام
101-Mlango Wa Uharamu wa Mwanamke Kukaa na Msiba wa Maiti Zaidi ya Siku Tatu Isipokuwa kwa Mumewe Ambao ni Miezi Minne na Siku Kumi
Alhidaaya.com [4]
عن زينب بنتِ أبي سلمة رضي الله عنهما ، قالت : دَخَلْتُ عَلَى أُمِّ حَبِيبَةَ رضيَ اللهُ عنها ، زَوجِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم ، حِينَ تُوُفِّيَ أبُوهَا أبُو سُفْيَانَ بن حرب رضي الله عنه ، فَدَعَتْ بِطِيبٍ فِيهِ صُفْرَةُ خَلُوقٍ أوْ غَيرِهِ ، فَدَهَنَتْ مِنهُ جَارِيَةً ، ثُمَّ مَسَّتْ بِعَارِضَيْهَا ، ثُمَّ قَالَتْ : واللهِ مَا لِي بِالطِّيبِ مِنْ حَاجَةٍ ، غَيْرَ أنِّي سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقُولُ عَلَى المِنْبَرِ : (( لا يَحِلُّ لامْرَأَةٍ تُؤْمِنُ بِاللهِ وَاليَوْمِ الآخِرِ أنْ تُحِدَّ على مَيِّتٍ فَوقَ ثَلاَثِ لَيَالٍ ، إلاَّ علَى زَوْجٍ أرْبَعَةَ أشْهُرٍ وَعَشْراً )) .
قالَتْ زَيْنَبُ : ثُمَّ دَخَلْتُ عَلَى زَيْنَبَ بنْتِ جَحْشٍ رضي اللهُ عنها حينَ تُوُفِّيَ أَخُوهَا ، فَدَعَتْ بِطِيبٍ فَمَسَّتْ مِنْهُ ثُمَّ قَالَتْ : أمَا وَاللهِ مَا لِي بِالطِّيبِ مِنْ حَاجَةٍ ، غَيرَ أنِّي سَمِعْتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقُولُ عَلَى المِنْبَرِ : (( لا يَحِلُّ لامْرَأَةٍ تُؤْمِنُ بِاللهِ وَاليَوْمِ الآخِرِ أنْ تُحِدَّ على مَيِّتٍ فَوقَ ثَلاَثٍ، إلاَّ علَى زَوْجٍ أرْبَعَةَ أشْهُرٍ وَعَشْراً )). متفق عليه .
Amesema Zaynab Bint Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Niliingia kwa Umm Habibah (Radhwiya Allaahu 'anhaa), mke wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipofariki baba yake Abu Sufyaan bin Harb (Radhwiya Allaahu 'anhu), akataka (yaani Umm Habibah) aletewe manukato ndani yake mna sufrah, Khaluq au mwengine akampaka baadhi yake kijakazi, kisha akapaka mashavuni mwake, kisha akasema: "Wa-Allaahi, sina haja ya manukato isipokuwa mimi nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya minbar akisema: 'Haifai kwa mwanamke anayemuamini Allaah na Siku ya Mwisho kukaa msiba kwa sababu ya maiti zaidi ya siku tatu isipokuwa kwa mume wake kwa muda wa miezi minne na siku kumi'." Akasema Zaynab: Kisha nikaingia kwa Zaynab bint Jahsh (Radhwiya Allaahu 'anhaa) alipofariki kaka yake, akataka aletewe manukato, akapata kidogo, kisha akasema: "Ama Wa-Allaahi, sina haja ya manukato isipokuwa mimi nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya mimbar akisema: 'Haifai kwa mwanamke anayemuamini Allaah na Siku ya Mwisho kukaa msiba kwa sababu ya maiti zaidi ya siku tatu isipokuwa kwa mume wake kwa muda wa miezi minne na siku kumi'." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم بيع الحاضر للبادي وتلقي الركبان
والبيع على بيع أخيه والخِطبة على خطبته إلا أنْ يأذن أو يردّ
102-Mlango Wa Uharamu kwa Mtu wa Mjini Kununua kwa Mtu wa Kijijini na Kupokea Njiani Msafara wa Wafanya Biashara, na Kuuza katika Mauzo ya Nduguye, na Posa Juu ya Posa yake Isipokuwa Akitoa Ruhusa au Akikataliwa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أنس رضي الله عنه ، قالَ : نهَى رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم أنْ يَبيعَ حَاضِرٌ لِبَادٍ وإنْ كانَ أخَاهُ لأَبِيهِ وَأُمِّهِ . متفق عليه .
Amesema Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu): Amekataza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) watu wa mjini kuuza bidhaa za aliyetoka mshambani hata akiwa za kaka yake, baba na mama yake. [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قال : قالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَتَلَقَّوُا السِّلَعَ حَتَّى يُهْبَطَ بِهَا إلَى الأَسْوَاقِ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msipokee wafanaya biashara kwa kununua bidhaa kutoka kwao kwa kukutana nao njiani kabla haujafika sokoni." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قال : قالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَتَلَقَّوُا الرُّكْبَانَ ، وَلاَ يَبِعْ حَاضِرٌ لِبَادٍ )) فقالَ لَهُ طَاووسٌ : مَا : لاَ يَبيعُ حَاضِرٌ لِبَادٍ ؟ قال : لاَ يَكُونُ لَهُ سِمْسَاراً . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msiende kuupokea njiani msafara wa wafanya biashara na wala mtu wa mjini (kwa kujifanya dalali) asiuze bidhaa ya aliyetoka shamba." Akamuuliza yeye Twaa'uws: "Nini maana ya wa mjini asiuze mali ya mtu wa kijijini (shamba)?" Akamjibu: "Asiwe dalali." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أبي هريرة رضي الله عنه قال : نَهَى رسولُ الله صلى الله عليه وسلم أنْ يَبِيعَ حَاضِرٌ لِبَادٍ ، وَلاَ تَنَاجَشُوا وَلاَ يَبِيع الرَّجُلُ عَلَى بَيْعِ أخْيِهِ ، وَلاَ يَخْطُبُ عَلَى خِطْبَةِ أخِيهِ ، وَلاَ تَسْأَلُ المَرْأَةُ طَلاَقَ أُخْتِهَا لِتَكْفَأَ مَا فِي إنائِهَا .
وفي رواية قال : نَهَى رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم عَنِ التَّلَقِّي، وَأَنْ يَبْتَاعَ المُهَاجِرُ لِلأعْرَابِيِّ ، وَأَنْ تَشْتَرِطَ المَرْأةُ طَلاَقَ أُخْتِهَا ، وأنْ يَسْتَامَ الرَّجُلُ على سَوْمِ أخِيهِ ، وَنَهَى عَنِ النَّجْشِ والتَّصْرِيَةِ . متفق عليه .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Amekataza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mtu wa mjini kuuza bidhaa za mtu aliyetoka kijijini wala msihadaiane wala mtu asiuze katikamauzo ya nduguye wala asipose mmoja wenu juu ya posa ya nduguye, wala mwanamke asitake dada yake aachwe ili aolewe yeye na achukue sehemu yake.
Na katika riwaayah nyengine: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kupokea bidhaa njiani, na amekataza mtu mjini kuuza bidhaa za mtu wa shamba, na mwanamke kuolewa kwa sharti la kuachwa mwenzake. Na mtu kununua au kutaka maafikiani ya kibiashara ya ndugu yake na amekataza ulaghai wa ndani na kuacha kumkama mnyama ili kumhadaa mnunuzi." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم قال : (( لاَ يَبِعْ بَعْضُكُمْ عَلَى بَيْعِ بَعْضٍ ، وَلاَ يَخْطُبْ عَلَى خِطْبَةِ أخِيهِ إلاَّ أنْ يَأذَنَ لَهُ )) . متفق عليه ، وهذا لفظ مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ibnm 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wala baadhi yenu wasiuze katika mauzo ya baadhi ya wengine wala asipose mmoja wenu juu ya posa ya nduguye isipokuwa anapompatia idhini." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hili ni tamshi la Muslim]
Hadiyth – 6
وعن عقبة بن عامر رضي الله عنه : أنَّ رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم قال : (( المُؤْمِنُ أَخُو المُؤْمِنِ ، فَلاَ يَحِلُّ لِمُؤْمِنٍ أنْ يَبْتَاعَ عَلَى بَيْعِ أخِيهِ وَلاَ يَخْطُبَ عَلَى خِطْبَةِ أخِيهِ حَتَّى يذَرَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa "Uqbah bin 'Aamir kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini ni ndugu yake Muumini mwengine, hivyo si halali kwa Muumini kuuza katika mauzo ya nduguye wala asipose juu ya posa ya nduguye mpaka ajitoe (kwa kutotaka kumuoa huyo mwanamke)." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن إضاعة المال في غير وجوهه
التي أذن الشرع فيها
103-Mlango Wa Kukatazwa Kufuja Mali kwa Njia Ambayo Haikuidhinishwa na Sheria
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرة رضي الله عنه قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ اللهَ تعالى يَرْضَى لَكُمْ ثَلاَثاً ، ويَكْرَهُ لَكُمْ ثَلاَثاً : فَيَرْضَى لَكُمْ أنْ تَعْبُدُوهُ ، وَلاَ تُشْرِكُوا بِهِ شَيئاً ، وَأَنْ تَعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللهِ جَمِيعاً وَلاَ تَفَرَّقُوا ، وَيَكْرَهُ لَكُمْ : قِيلَ وَقَالَ ، وَكَثْرَةَ السُّؤَالِ ، وإضَاعَةَ المَالِ )) . رواه مسلم
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ta'aalaa Anawaridhia mambo matatu na Anachukia mambo matatu kwenu: Anawaridhia muwe ni wenye kumuabudu Yeye wala usimshirikishe na chochote, na mushikamane na kamba ya Allaah wala musifarikiane. Na Anachukia kwenu nyinyi: Uvumi (na kuzungumza sana mazungumzo yasiyo na faida), na kuuliza maswali mengi na kufuja mali." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ورَّادٍ كاتب المغيرة، قال : أَمْلَى عَلَيَّ المُغِيرَةُ بْنُ شُعْبَةَ في كِتابٍ إلَى مُعَاوِيَةَ رضي الله عنه : أنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يَقُولُ فِي دُبُرِ كُلِّ صَلاَةٍ مَكْتُوبَةٍ : (( لاَ إلهَ إلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لهُ ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ، اللَّهُمَّ لاَ مَانِعَ لِمَا أَعْطَيْتَ ، وَلاَ مُعْطِيَ لِمَا مَنَعْتَ ، وَلاَ يَنْفَعُ ذَا الجَدِّ مِنْكَ الجَدُّ )) وَكَتَبَ إلَيْهِ أَنَّهُ كَانَ يَنْهَى عَنْ قِيلَ وَقَالَ ، وَإضَاعَةِ المَالِ ، وَكَثْرَةِ السُّؤَالِ ، وَكَانَ يَنْهَى عَنْ عُقُوقِ الأُمَّهَاتِ ، وَوَأْدِ البَنَاتِ ، وَمَنْعٍ وَهَاتِ . متفق عليه
Amesema Warraad, mwandishi wa Mughiyrah bin Shu'bah (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Mughiyrah bin Shu'bah (Radhwiya Allaahu 'anhu) alinifanya imla ya baruwa kwenda kwa Mu'awiyah, kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anasema baada ya kila Swalaah ya faradhi: "Laa ilaaha illa Allaah wahdahu laa shariyka lahu, lahul Mulku wa lahul Hamdu wa Huwa 'alaa kuli shayyin Qadiyr, Allaahumma laa maani'a lima a'twayta wa laa Mu'twiya lima mana'ta wa laa yanfa'u dhal jaddi minkal jadd (Hakuna mola anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Allaah Peke Yake Hana mshirika, mwenye Ufalme na Mwenye kila Sifa Nzuri, Naye ni Muweza wa kila kitu. Ee Rabb Wangu! Hakuna wa kuzuia Ulichokitoa; na wala hakuna anayekitoa Unachokizuia; na wala hautamfaa Kwako mwenye utajiri wake)." Na pia akamwandikia kwamba: "Alikuwa (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anakataza maneno ya kipuuzi, na kufuja mali na kuuliza maswali mengi. Na pia (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) alikataza kuwaasi akina mama, na kuwazika wasichana wakiwa hai na kumpokonya (kumchukulia) mtu haki yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الإشارة إلى مسلم بسلاح ونحوه
سواء كان جاداً أو مازحاً ، والنهي عن تعاطي السيف مسلولاً
104-Mlango Wa Kukatazwa Kumuashiria muislamu kwa Silaha na Mfano wake Sawa ni kwa Kweli au Mzaha na Katazo la Kuwa na Upanga Nje ya Ala yake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرة رضي الله عنه ، عن رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم قال : (( لاَ يُشِرْ أحَدُكُمْ إلَى أخِيهِ بِالسِّلاحِ ، فَإنَّهُ لاَ يَدْرِي لَعَلَّ الشَّيْطَانَ يَنْزعُ فِي يَدِهِ ، فَيَقَع فِي حُفْرَةٍ مِنَ النَّارِ )) . متفق عليه .
وفي رواية لمسلم قال : قال أبو القاسم صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ أشَارَ إلَى أخِيهِ بِحَدِيدَةٍ ، فَإنَّ المَلاَئِكَةَ تَلْعَنُهُ حَتَّى يَنْزعَ ، وَإنْ كَانَ أخَاهُ لأَبِيهِ وَأُمِّهِ ))
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asimuashirie mmoja wenu nduguye kwa silaha, kwani yeye hajui huenda shetani akaitowa mkononi mwake (akaleta maafa, kujeruhi, au kifo), hivyo kumfanya aingie katika shimo la moto." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na Musli katika riwaayah yake amesema: Amesema Abul Qaasim: "Mwenye kumuashiria chuma nduguye, hakika Malaaikah anamlaani mpaka akiondoshe, japokuwa atakuwa ni ndugu yake halisa (kwa baba na mama)."
Hadiyth – 2
وعن جابر رضي الله عنه قال : نهى رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم أنْ يُتَعَاطَى السَّيْفُ مَسْلُولاً . رواه أبو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Amesema Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu): Amekataza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mtu kumpatia upanga usiokuwa katika ala yake mwenziwe. [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الخروج من المسجد بعد الأذان
إلا لعذر حتى يصلي المكتوبة
105-Mlango Wa Ukaraha wa kutoka Msikitini Baada ya Adhana Isipokuwa kwa Udhuru Mpaka Aswali Swalaah ya Faradhi
Alhidaaya.com [4]
عن أبي الشَّعْثَاءِ ، قالَ : كُنَّا قُعُوداً مَع أبي هريرة رضي الله عنه في المَسْجِدِ ، فَأَذَّن المُؤَذِّنُ ، فَقَامَ رَجُلٌ مِنَ المَسْجِدِ يَمْشِي ، فَأَتْبَعَهُ أبُو هُريرَةَ بَصَرَهُ حَتَّى خَرَجَ مِنَ المَسْجِدِ ، فقال أبو هريرة : أمَّا هذَا فَقَدْ عَصَى أبا القَاسِمِ صلى الله عليه وسلم . رواه مسلم .
Amesema Abu Ash-Sha'athaa: Tulikuwa tumekaa pamoja na Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Msikitini, mara muadhini akaadhini. Hapo akasimama mtu mmoja akawa anatembea (kutaka kutoka nje ya Msikiti). Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) akamfuata kwa kumwangalia mpaka akatoka Msikitini. Hapo, Abu Huraiyrah akasema: "Ama mtu huyu hakika amemuasi Abul Qaasim (yaani Muhammad Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة رد الريحان لغير عذر
106-Mlango Wa Ukaraha wa Kurudisha Zawadi ya Manukato Bila Udhuru
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرة رضي الله عنه قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ عُرِضَ عَلَيْهِ رَيْحَانٌ ، فَلاَ يَرُدَّهُ ، فَإنَّهُ خَفيفُ المَحْمِلِ ، طَيِّبُ الرِّيحِ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kupatiwa zawadi ya manukato asirudishe, kwani ni nyepesi kubebwa na yenye harufu nzuri." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أنس بن مالكٍ رضي الله عنه : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ لاَ يَرُدُّ الطِّيبَ . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuwa ni mwenye kurudisha zawadi ya manukato. [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة المدح في الوجه لمن خيف عليه مفسدة
من إعجاب ونحوه ، وجوازه لمن أمِنَ ذلك في حقه
107-Mlango Wa Ukaraha wa Kumsifu Mtu Mbele Yake kwa Anayehofiwa Ufisadi Kama Vile Kiburi na Mfano Wake na Kufaa kwa Yule Anayeaminiwa katika Haki Yake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه قال : سَمِعَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم رَجُلاً يُثْنِي عَلَى رَجُلٍ وَيُطْرِيهِ في المِدْحَة ، فقالَ : (( أهْلَكْتُمْ – أوْ قَطَعْتُمْ – ظَهْرَ الرَّجُلِ )) . متفق عليه .
Amesema Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimsikia mtu mmoja akimsifu mwenziwe na kutupa mipaka katika kumsifu, akasema: "Amemuangamiza (amemuua) au ameuvunja mgongo wa huyo mtu." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]
Hadiyth – 2
وعن أبي بكرة رضي الله عنه : أنَّ رجلاً ذُكِرَ عند النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَأَثْنَى عَلَيْهِ رَجُلٌ خَيْراً ، فقال النبيّ صلى الله عليه وسلم : (( وَيْحَكَ ! قَطَعْتَ عُنُقَ صَاحِبِكَ )) يَقُولُهُ مِرَاراً : (( إنْ كَانَ أحَدُكُمْ مَادِحاً لاَ مَحَالَةَ فَلْيَقُلْ : أحْسِبُ كَذَا وَكَذَا إنْ كَانَ يَرَى أنَّهُ كَذَلِكَ وَحَسِيبُهُ اللهُ ، وَلاَ يُزَكّى عَلَى اللهِ أحَدٌ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Bakrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mara moja mtu mmoja alitajwa mbele ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na mtu mwengine akamsifu kwa kheri. Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ole wako! Umekata shingo ya sahibu yako." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikariri jambo hilo: "Ikiwa mtu hana budi mpaka amsifu (mtu yeyote), aseme: 'Ninamuhesabu (ninamchukulia) yeye ni kadha na kadha, ikiwa kweli anaona kuwa yeye yuko hivyo na Allaah Atamhesabu kwa hilo, wala hakuna anayeweza kujisifu kwa usafi mbele ya Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن همام بن الحارث ، عن المِقْدَادِ رضي الله عنه : أنَّ رَجُلاً جَعَلَ يَمْدَحُ عُثْمانَ رضي الله عنه ، فَعَمِدَ المِقْدَادُ ، فَجَثَا عَلَى رُكْبَتَيْهِ ، فَجَعَلَ يَحثو في وَجْهِهِ الحَصْبَاءَ . فقالَ لَهُ عُثْمَانُ : مَا شَأنُكَ ؟ فقال : إنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قال : (( إذَا رَأَيْتُمُ المَدَّاحِينَ ، فَاحْثُوا فِي وُجُوهِهِمُ التُّرَابَ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoks kwa Hammaam bin Al-Haarith kutoka kwa Al-Miqdaad (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mtu mmoja alikuwa akimsifu 'Uthmaan (Radhwiya Allaahu 'anhu). Miqdaad alipiga magoti na kuanza kumrushia changarawe mdomoni mwa mzungumzaji. Akamwambia yeye 'Uthmaan (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Una nini wewe (mbona unafanya hivyo)?" Akasema (Miqdaad): "Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: 'Mukimuona mtu anamsifu mwenziwe mbele yake, basi mtieni usoni mwake mchanga'." [Muslim]
فهذهِ الأحاديث في النَهي ، وجاء في الإباحة أحاديث كثيرة صحيحة .
قال العلماءُ : وطريق الجَمْعِ بين الأحاديث أنْ يُقَالَ : إنْ كان المَمْدُوحُ عِنْدَهُ كَمَالُ إيمانٍ وَيَقينٍ ، وَرِيَاضَةُ نَفْسٍ ، وَمَعْرِفَةٌ تَامَّةٌ بِحَيْثُ لاَ يَفْتَتِنُ ، وَلاَ يَغْتَرُّ بِذَلِكَ ، وَلاَ تَلْعَبُ بِهِ نَفْسُهُ ، فَليْسَ بِحَرَامٍ وَلاَ مَكْرُوهٍ ، وإنْ خِيفَ عَلَيْهِ شَيءٌ مِنْ هذِهِ الأمورِ ، كُرِهَ مَدْحُهُ في وَجْهِهِ كَرَاهَةً شَديدَةً ، وَعَلَى هَذا التَفصِيلِ تُنَزَّلُ الأحاديثُ المُخْتَلِفَةُ فِي ذَلكَ .
وَمِمَّا جَاءَ فِي الإبَاحَةِ قَولُهُ صلى الله عليه وسلم لأبي بكْرٍ رضي الله عنه : (( أرْجُو أنْ تَكُونَ مِنْهُمْ )) أيْ مِنَ الَّذِينَ يُدْعَونَ مِنْ جَمِيعِ أبْوابِ الجَنَّةِ لِدُخُولِهَا . متفق عليه .
وَفِي الحَدِيثِ الآخر : (( لَسْتَ مِنْهُمْ )) : أيْ لَسْتَ مِنَ الَّذِينَ يُسْبِلُونَ أُزُرَهُمْ خُيَلاَءَ . رواه البخاري .
وَقالَ صلى الله عليه وسلم لعُمَرَ رضي الله عنه : (( مَا رَآكَ الشَّيْطَانُ سَالِكاً فَجّاً إلاَّ سَلَكَ فَجّاً غَيْرَ فَجِّكَ )) . متفق عليه .
والأحاديثُ في الإباحة كثيرةٌ ، وقد ذكرتُ جملةً مِنْ أطْرَافِهَا في كتاب " الأذكار"
Wamesema wanazuoni: Na njia ya kuoanisha baina ya Hadiyth ni kauli: Ikiwa kusifiwa mbele yake yule mwenye ukamilifu wa Imani na yakini na mtu anaye inyima nafasi yake na mwenye maarifa barabara ya maadili ya Dini, hivyo kutofitinika wala kuhadaika wala nafsi yake haitamchezea kwa hilo. Katika mas-ala haya ya kusifiwa hakutakuwa haramu wala makruhu. Na ikiwa anahofiwa kwa mambo haya yaliotajwa, inakuwa ni makruhu kumsifu mbele yake, na ukaraha ni mkali na mzito zaidi. Na kwa mujibu wa tafsili hizi tunapata Hadiyth tofauti katika hilo. Na katika Hadiyth zinazoelezea kuruhusiwa kumsifu mtu mbele yake ni:
Kauli ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa Abu Bakar (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Ninatarajia kuwa utakuwa miongoni mwao." [Al-Bukhaariy na Muslim], yaani miongoni mwa wale watakaoitwa kuingia Peponi kwa kupitia milango yote.
Na Hadiyth nyengine: "Wewe si miongoni mwao." [Al-Bukhaariy], yaani wewe ni katika wale wanaoburuza vikoi vyao kwa kiburi.
Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Shetani hakuoni ukitembea njiani isipokuwa huacha njia hiyo na kuchukua nyengine." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na Hadiyth katika mlango huu ambazo zinaruhusu kumsifu mtu mbele yake ni nyingi, baadhi yake nimezitaja katika kitabu changu cha al-Adhkaar.
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الخروج من بلد وقع فيها الوباء
فراراً منه وكراهة القدوم عليه
108-Mlango Wa Ukaraha wa Kutoka katika Mji Ambao Umekumbwa na Ugonjwa wa Kuambukiza na Kuingia Ndani yake (Haifai Kuingia Wala Kutoka katika Mji Huo)
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
أَيْنَمَا تَكُونُوا يُدْرِككُّمُ الْمَوْتُ وَلَوْ كُنتُمْ فِي بُرُوجٍ مُّشَيَّدَةٍ ۗ ﴿٧٨﴾
Popote mtakapokuwa yatakufikieni mauti, japo mkiwa katika minara (au ngome) imara na madhubuti. [An-Nisaa: 78]
وَلَا تُلْقُوا بِأَيْدِيكُمْ إِلَى التَّهْلُكَةِ ۛ ﴿١٩٥﴾
Wala msijitupe katika maangamizi [Al-Baqarah: 195]
Hadiyth – 1
وعن ابن عباس رضي الله عنهما : أنَّ عمرَ بن الخطاب رضي الله عنه خرج إلى الشَّامِ حَتَّى إذا كَانَ بسَرْغَ لَقِيَهُ أُمَرَاءُ الأَجْنَادِ - أَبُو عُبَيْدَةَ بنُ الجَرَّاحِ وأصْحَابُهُ - فَأخْبَرُوهُ أنَّ الوَبَاءَ قَدْ وَقَعَ بِالشَّامِ . قَال ابن عباس : فقال لي عمر : ادْعُ لِي المُهَاجِرِينَ الأَوَّلِينَ ، فَدَعَوْتُهُمْ فَاسْتَشَارَهُمْ وَأخْبَرَهُمْ أنَّ الوَبَاءَ قَدْ وَقَعَ بالشَّامِ ، فَاخْتَلَفُوا ، فَقَالَ بَعْضُهُمْ : خَرَجْتَ لأَمْرٍ ، وَلاَ نَرَى أنْ تَرْجِعَ عَنْهُ . وَقَالَ بَعضهم : مَعَكَ بَقِيَّةُ النَّاسِ وأصْحَابُ رسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وَلاَ نَرَى أنْ تُقْدِمَهُمْ عَلَى هَذَا الوَبَاء . فقال : ارْتَفِعُوا عَنِّي . ثُمَّ قَالَ : ادْعُ لِي الأَنْصَارَ ، فَدَعَوْتُهُمْ ، فَاسْتَشَارَهُمْ ، فَسَلَكُوا سَبيلَ المُهَاجِرينَ ، وَاخْتَلَفُوا كاخْتِلاَفِهِمْ ، فقال : ارْتَفِعُوا عَنِّي . ثُمَّ قَالَ : ادْعُ لِي مَنْ كَانَ هاهُنَا مِنْ مَشْيَخَةِ قُريشٍ مِنْ مُهَاجِرَةِ الفَتْحِ ، فَدَعَوْتُهُمْ ، فَلَمْ يَخْتَلِفْ عَلَيْهِ مِنْهُمْ رَجُلاَنِ ، فَقَالُوا : نَرَى أنْ تَرْجِعَ بِالنَّاسِ ، وَلاَ تُقْدِمَهُمْ عَلَى هَذَا الوَبَاءِ ، فَنَادَى عُمَرُ رضي الله عنه في النَّاسِ : إنِّي مُصَبحٌ عَلَى ظَهْرٍ ، فَأَصْبِحُوا عليْهِ ، فقال أبو عبيدة بن الجراح رضي الله عنه : أفِراراً مِنْ قَدَرِ الله ؟ فقالَ عُمرُ رضي الله عنه : لو غَيْرُكَ قَالَهَا يا أبا عبيدَةَ ! – وَكَانَ عُمَرُ يَكْرَهُ خِلاَفَهُ – نَعَمْ ، نَفِرُّ مِنْ قَدَرِ اللهِ إلى قَدَرِ اللهِ ، أرَأيْتَ لَو كَانَ لَكَ إبِلٌ ، فَهَبَطَتْ وَادِياً لَهُ عُدْوَتَانِ ، إحْدَاهُمَا خَصْبَةٌ ، وَالأُخْرَى جَدْبَةٌ ، أَلَيسَ إنْ رَعَيْتَ الخصْبَةَ رَعَيْتَهَا بِقَدَرِ اللهِ ، وَإنْ رَعَيْتَ الجَدْبَةَ رَعَيْتَهَا بِقَدَرِ اللهِ ؟ قَالَ : فَجَاءَ عَبدُ الرَّحمانِ بنُ عَوفٍ رضي الله عنه ، وَكَانَ مُتَغَيِّباً في بَعْضِ حاجَتِهِ ، فقالَ : إنَّ عِنْدِي من هَذَا علماً ، سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( إِذَا سَمِعْتُمْ بِهِ بأرْضٍ فَلاَ تَقْدِمُوا عَلَيْهِ ، وَإِذَا وَقَعَ بِأرْضٍ وَأنْتُمْ بِهَا فَلاَ تَخْرُجُوا فِراراً مِنْهُ )) فحمِدَ اللهَ تَعَالَى عمرُ رضي الله عنه وانصَرَفَ . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu), alitoka kwenda Shaam, alipofika Sargha, 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) alikutana na Kamanda wa Jeshi la Kiislamu - Abu 'Ubayda 'Aamir bin Al-Jarrah akiwa na wenzake, nao wakamueleza kuwa tauni iko katika ardhi ya Shaam. Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: 'Umar akasema: "Niitie Muhaajirun wa mwanzo." Nikawaita na akawataka ushauri na akawaeleza kuwa tauni iko Shaam, wakatofautiana katika rai zao. Baadhi yao wakasema: "Tumetoka kwa jambo ili tulifanikishe, hatuoni sababu kwa nini tuache kulifanikisha", na baadhi yao wakasema: "Unao watu pamoja nawe na wengine ni Swahaaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hatuoni sababu ya wewe kuwapeleka katika tauni hii." 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) akasema: "Sasa hivi niacheni na nendeni mukaniitie Answaar." Nikaenda kuwaita, akawataka ushauri, na wakaipita njia ya Muhaajirun, na wakakhitilafiana kama walivyo khitilafiana wao (Muhaajirun). 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) akasema: "Nendeni ." Kisha akasema: "Niitie wazee wa Kiquraysh wa hapa katika waliohama mwaka wa kufunguliwa Makkah." Nikawaita, nao hawakukhitilafiana, walisema: "Tunaona urudi na hao watu na usiwapeleke kwenye tauni." "Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) akatoa wito (tangazo) kwa watu huku akisema: "Mimi asubuhi nitaamka safari (ya kurudi) kwa hiyo nanyi fanyeni safari." Abu 'Ubaydah bin Al-Jarraah (Radhwiya Allaahu 'anhu) akasema: "Unaukimbia Uwezo (Qadar) wa Allaah?" 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) akasema: "Hayo angali yasema mwengine (lakini si wewe) Abu 'Ubaydah! Kisha 'Umar akajibu: "Ndiyo, tunakimbia Qadar ya Allaah kwa kukimbilia kwenye Qadar ya Allaah, uanonaje kama ungalikuwa na ngamia wakawa katika jangwa lina pande mbili, moja ina rutubu na nyengine kama hivi, je, huoni kuwa utawalisha katika sehemu ya rutuba, utakuwa umewalisha kwa Uwezo (Qadar) wa Allaah na kama ungewalisha kwa Qadar ya Allaah?" Akasema: Muda huo huo akawa ametokea 'Abdur-Rahmaan bin 'Awf (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye hakuwepo kwenda alikwenda kutafuta baadhi ya mahitaji yake akasema: "Katika hili mimi nina ujuzi. Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: 'Kama mtasikia (hiyo tauni) iko kwenye ardhi fulani msiende huko, na kama itakuwa katika ardhi, nanyi mko hapo msitoke kuikimbia." Baada ya maneno hayo 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) akamshukuru Allaah, kisha akaondoka (kurudi Madiynah). [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أسامة بن زيد رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا سَمِعْتُمُ الطَّاعُونَ بِأَرْضٍ ، فَلاَ تَدْخُلُوهَا ، وَإِذَا وَقَعَ بِأرْضٍ ، وأنْتُمْ فِيهَا ، فَلاَ تَخْرُجُوا مِنْهَا )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Usamah bin Zayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mnaposikia kuwa tauni iko kwenye ardhi fulani msiingie humo, na kama itakuwa katika ardhi, nanyi mko hapo msitoke kuikimbia." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب التغليظ في تحريم السحر
109-Mlango Wa Uzito wa Uharamu wa Uchawi
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَمَا كَفَرَ سُلَيْمَانُ وَلَـٰكِنَّ الشَّيَاطِينَ كَفَرُوا يُعَلِّمُونَ النَّاسَ السِّحْرَ ﴿١٠٢﴾
Na Sulaymaan hakukufuru lakini mashaytwaan ndio waliokufuru, wanafundisha watu sihiri [Al-Baqarah: 102]
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( اجْتَنِبُوا السَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ )) . قالوا : يَا رسولَ اللهِ ، وَمَا هُنَّ ؟ قَالَ : (( الشِّرْكُ باللهِ ، وَالسِّحْرُ ، وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتي حَرَّمَ اللهُ إِلاَّ بِالحَقِّ ، وأكْلُ الرِّبَا ، وأكْلُ مَالِ اليَتِيمِ ، وَالتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ ؛ وَقَذْفُ المُحْصَنَاتِ المُؤْمِنَاتِ الغَافِلاَتِ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Jiepusheni na madhambi saba yanayoangamiza." Watu wakauliza: "Ee Rasuli wa Allaah ni yapo hayo?" Akasema: "Kumshirikisha Allaah, na uchawi, na kuua nafsi ambayo Allaah Ameiharamisha isipokuwa kwa haki, na kula riba, kula mali ya yatima, kukimbia siku ya vita na kuwatuhumu kwa zinaa wanawake waliohifadhiwa na Allaah, Waumini wasiyo na habari ya zinaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن المسافرة بالمصحف إِلَى بلاد الكفار
إِذَا خيف وقوعه بأيدي العدوّ
110-Mlango Wa Kukatazwa Kusafiri na Msahafu katika Nchi ya Makafiri Ikihofiwa Kuingia Mkononi Mwa Adui
Alhidaaya.com [4]
عن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : نَهَى رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم أنْ يُسَافَرَ بالقُرْآنِ إِلَى أرْضِ العَدُوِّ . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Amekataza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mtu kusafiri na Qur-aan katika ardhi ya maadui. [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم استعمال إناء الذهب وإناء الفضة
في الأكل والشرب والطهارة وسائر وجوه الاستعمال
111-Mlango Wa Uharamu wa Kutumia Vyombo vya Dhahabu, Fedha katika Kula, Kunywa, Tohara na Njia Zote za Matumizi yake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أُمِّ سلمة رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( الَّذِي يَشْرَبُ في آنِيَةِ الفِضَّةِ ، إنَّمَا يُجَرْجِرُ في بَطْنِهِ نَارَ جَهَنَّمَ )) متفق عَلَيْهِ .
وفي رواية لمسلم : (( إنَّ الَّذِي يَأكُلُ أَوْ يَشْرَبُ في آنِيَةِ الفِضَّةِ والذَّهَبِ )) .
Imepokewa kutoka kwa Ummu Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayekunywa katika chombo cha fedha anaangushia moto tumboni mwake." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]
Na katika riwaayah ya Muslim: "Hakika anayekula au kunywa katika chombo cha fedha na dhahabu."
Hadiyth – 2
وعن حُذَيفَةَ رَضِيَ اللهُ عنه ، قَالَ : إنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم نهانا عنِ الحَريِرِ ، وَالدِّيبَاجِ ، وَالشُّرْبِ في آنِيَةِ الذَّهَبِ وَالفِضَّةِ ، وقالَ : (( هُنَّ لَهُمْ في الدُّنْيَا ، وَهِيَ لَكُمْ فِي الآخِرَةِ )) . متفق عَلَيْهِ .
وفي رواية في الصحيحين عن حُذيْفَةَ رَضِيَ اللهُ عنه : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( لاَ تَلْبسُوا الحَرِيرَ وَلاَ الدِّيبَاجَ ، وَلاَ تَشْرَبُوا فِي آنِيَةِ الذَّهَبِ وَالفِضَّةِ وَلاَ تَأكُلُوا في صِحَافِهَا )) .
Amesema Hudhayfah (Radhyewiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametukataza kuvaa hariri na dibaji na kunywa katika vyombo vya dhahabu na fedha na akasema: "Vitu hivyo ni vyao hapa duniani na ni vyenu Aakherah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah nyengine katika Swahiyh mbili kutoka kwa Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Musivae nguo za hariri wala dibaji wala musinywe katika vyombo vya dhahabu na fedha wala musile katika sinia zake."
Hadiyth – 3
وعن أنس بن سِيِرين ، قَالَ : كنتُ مَعَ أنس بن مالك رَضِيَ اللهُ عنه ، عِنْدَ نَفَرٍ مِنَ المَجُوسِ ؛ فَجِيءَ بفَالُوذَجٍ عَلَى إنَاءٍ مِنْ فِضَّةٍ ، فَلَمْ يَأَكُلْهُ ، فَقِيلَ لَهُ : حَوِّلْهُ ، فَحَوَّلَهُ عَلَى إناءٍ مِنْ خَلَنْجٍ وَجِيءَ بِهِ فَأَكَلَهُ . رواه البيهقي بإسناد حسن .
Amesema Anas bin Siyriyn: Nilikuwa na Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) pamoja na baadhi ya Majusai. Mara ikaletwa tamutamu katika chombo cha fedha, naye (Radhwiya Allaahu 'anhu) akakataa kula ndani yake. Yule aliyeleta aliambiwa abadilishe chombo hicho, naye akafanya hivyo na kuleta (tamutamu hiyo) katika chombo cha Khalanj (ni mti ulio na rangi baina ya majano na nyekundu ambao mbao zake hutumiwa kutengeneza vyombo) na Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) akala. [Al-Bayhaqiy kwa Isnaad iliyo Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم لبس الرجل ثوباً مزعفراً
112-Mlango Wa Uharamu wa Mwanamume Kuvaa Nguo ya Zafarani
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أنس رضي الله عنه قَالَ : نَهَى النبيُّ صلى الله عليه وسلم أنْ يَتَزَعْفَرَ الرجُل . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza mwanamume kutumia zafarani. [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Hadiyth – 2
وعن عبد اللهِ بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : رأى النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم عَلَيَّ ثَوْبَيْنِ مُعَصْفَرَيْنِ ، فَقَالَ : (( أُمُّكَ أمَرَتْكَ بِهَذا ؟ )) قلتُ: أَغْسِلُهُمَا ؟ قَالَ: (( بَلْ أَحْرِقْهُمَا )) .
وفي رواية ، فَقَالَ : (( إنَّ هَذَا مِنْ ثِيَابِ الكُفَّارِ فَلاَ تَلْبَسْهَا )) . رواه مسلم .
Amesema 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniona nikiwa nimevaa vipande viwili vya nguo ya zafarani (rangi ya manjano). Akaniuliza: "Je, mamako ndiye aliyekuamuru kuvaa hizi?" Nikasema: "Je, nizifue?" Akasema: "Zichome."
Na katika riwaayah nyengine, alisema: "Hakika hizi ni katika nguo za makafiri, hivyo usuzivae." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن صمت يوم إلَى الليل
113-Mlango Wa Kukatazwa Kukaa Kimya Kuanzia Asubuhi Mpaka Usiku
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عليٍّ رضي الله عنه قَالَ : حَفِظْتُ عَنْ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ يُتْمَ بَعْدَ احْتِلاَمٍ ، وَلاَ صُمَاتَ يَومٍ إِلَى اللَّيْلِ )) . رواه أَبُو داود بإسناد حسن .
Kutoka kwa 'Ali (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimehifadhi kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hakuna anayebaki kuwa yatima baada kubaleghe wala hakuna maana kunyamaza (kuwa kimya bila kuzungumza) kuanzia asubuhi mpaka usiku." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Hasan]. Amesema Al-Khattwaabiy katika kuitafsiri hii Hadiyth: "Ilikuwa miongoni mwa sifa za Kijahiliya kunyamaza, Uislamu ukakataza jambo hilo na kuwaamuru watu wawe ni wenye kumdhukuru Allaah na kuzungumza mazungumzo ya kheri."
Hadiyth – 2
وعن قيس بن أَبي حازم ، قَالَ : دَخَلَ أَبُو بكر الصِّدِّيق رضي الله عنه عَلَى امْرأَةٍ مِنْ أحْمَسَ يُقَالُ لَهَا : زَيْنَبُ ، فَرَآهَا لاَ تَتَكَلَّمُ . فَقَالَ : مَا لَهَا لا تتكلمُ ؟ فقالوا : حَجَّتْ مصمِتةً ، فقالَ لها : تَكَلَّمِي ، فَإنَّ هَذَا لاَ يَحِلُّ ، هَذَا مِنْ عَمَلِ الجَاهِليَّةِ ، فَتَكَلَّمَتْ . رواه البخاري .
Amesema Qays bin Abu Haazim: Aliingia Abu Bakar Asw-Swiddiq (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mwanamke mmoja wa kabila la Ahmas aliyekuwa akiitwa Zaynab na kumuona hazungumzi. Akauliza: "Ana nini mbona hazungumzi?" Wakamjibu: "Ameapa kukaa kimya." Akamwambia: "Zungumza kwani jambo hilo si halali na ni amali za siku za Ujahiliya." Hapo akaanza kuzungumza. [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم انتساب الإنسان
إِلَى غير أَبيه وَتَولِّيه إِلَى غير مَواليه
114-Mlango Wa Uharamu wa Mtu Kujinasibisha kwa Asiyekuwa Baba Yake na Mtumwa Anayemkimbia Bwana Wake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن سعد بن أَبي وقاص رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنِ ادَّعَى إِلَى غَيْرِ أبِيهِ وَهُوَ يَعْلَمُ أنَّهُ غَيْرُ أبِيهِ ، فالجَنَّةُ عَلَيْهِ حَرَامٌ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Sa'ad bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kujinasibisha kwa asiyekuwa babake hali anaelewa kuwa hivyo si babake, basi itaharamishwa kwake Jannah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ تَرْغَبُوا عَنْ آبَائِكُمْ ، فَمَنْ رَغِبَ عَنْ أبِيهِ ، فَهُوَ كُفْرٌ )) . متفق عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msiwakatae baba zenu, atakayemkataa babake atakuwa amefanya tendo la ukafiri." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن يزيد بن شريكِ بن طارِقٍ ، قَالَ : رَأيتُ عَلِيّاً رضي الله عنه عَلَى المِنْبَرِ يَخْطُبُ ، فَسَمِعْتُهُ يقُولُ : لاَ واللهِ مَا عِنْدَنَا مِنْ كِتَابٍ نَقْرؤُهُ إِلاَّ كِتَابَ اللهِ ، وَمَا في هذِهِ الصَّحِيفَةِ ، فَنَشَرَهَا فَإذَا فِيهَا أَسْنَانُ الإبِلِ ، وَأشْيَاءُ مِنَ الجَرَاحَاتِ ، وَفِيهَا : قَالَ رسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( المَدينَةُ حَرَمٌ مَا بَيْنَ عَيْرٍ إِلَى ثَوْرٍ ، فَمَنْ أحْدَثَ فِيهَا حَدَثاً ، أَوْ آوَى مُحْدِثاً ، فَعَلَيْهِ لَعْنَةُ اللهِ وَالمَلاَئِكَةِ وَالنَّاسِ أجْمَعِينَ ، لاَ يَقْبَلُ اللهُ مِنْهُ يَومَ القِيَامَةِ صَرْفاً وَلاَ عَدْلاً . ذِمَّةُ المُسْلِمينَ وَاحِدَةٌ ، يَسْعَى بِهَا أَدْنَاهُمْ ، فَمَنْ أَخْفَرَ مُسْلِماً ، فَعَلَيْهِ لَعْنَةُ اللهِ وَالمَلائِكَةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ ، لاَ يَقْبَلُ اللهُ مِنْهُ يَومَ القِيَامَةِ صَرْفاً وَلاَ عَدْلاً . وَمَن ادَّعَى إِلَى غَيرِ أَبيهِ ، أَوْ انْتَمَى إِلَى غَيرِ مَوَاليهِ ، فَعَلَيْهِ لَعْنَةُ اللهِ وَالمَلاَئِكَةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعينَ ؛ لاَ يَقْبَلُ اللهُ مِنْهُ يَومَ القِيَامَةِ صَرْفاً وَلاَ عَدْلاً )) . متفق عَلَيْهِ .
Amesema Yaziyd bin Shariyk bin Twaariq: Nilimuona 'Ali (Radhwiya Allaahu 'anhu) juu ya minbar akihutubu, nikamsikia akisema: "Naapa kwa Allaah! Hatuna kitabu chengine tunacho kisoma isipokuwa Kitabu cha Allaah (Qur-aan) na zilizomo ndani ya sahifa. Tunapofungua Kitabu hichi tunapata maelezo ya miaka ya ngamia (viwango vya zakah) na mambo yanayohusu fidia ya jeraha (damu iliyo mwagwa). Na pia kinataja kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: 'Madiynah ni mji mtukufu baina ya majabali mawili ya 'Ayr na Thawr. Mwenye kuzua ndani yake au akampatia makao (himaya) mzushi, atakuwa na laana ya Allaah na Malaaikah na watu wote. Allaah Hatakubali kutoka kwake Siku ya Qiyaamah toba yake wala fidia. Dhamana ya Waislamu wote ni moja (kwani hadhi na majukumu yao yako sawa) wala chini kabisa miongoni mwao anaweza kutoa himaya. Yeyote mwenye kuvunja himaya aliyopewa na kumtweza Muislamu, juu yake laana ya Allaah, na Malaaikah na watu wote. Allaah Hatakubali kutoka kwake Siku ya Qiyaamah toba yake wala fidia. Na mwenye kujinasibisha kwa asiyekuwa baba yake au mtumwa anayekimbia na kwenda kwa bwana mwengine, ni juu yake laana ya Allaah, na Malaaikah na wtau wote. Allaah Hatakubali kutoka kwake Siku ya Qiyaamah toba yake wala fidia." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي ذَرٍّ رضي الله عنه : أنَّه سَمِعَ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( لَيْسَ مِنْ رَجُلٍ ادَّعَى لِغَيرِ أَبِيهِ وَهُوَ يَعْلَمُهُ إِلاَّ كَفَرَ ، وَمَنِ ادَّعَى مَا لَيْسَ لَهُ ، فَلَيْسَ مِنَّا ، وَلَيَتَبَوَّأْ مَقْعَدَهُ مِنَ النَّارِ ، وَمَنْ دَعَا رَجُلاً بالكُفْرِ ، أَوْ قَالَ : عَدُو اللهِ ، وَلَيْسَ كَذَلِكَ إِلاَّ حَارَ عَلَيْهِ )) . متفق عَلَيْهِ ، وهذا لفظ رواية مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Haitokei kwa mtu kujinasibisha na asiyekuwa baba yake hali anamuelewa isipokuwa amekufuru. Na mwenye kujinasibisha kwa kitu kisichokuwa chake, si katika sisi, basi ajiandalie makazi yake motoni. Na menye kumnasibisha mtu na ukafiri au akamwambia: 'Adui wa Allaah', naye si hivyo isipokuwa ukafiri hurudi kwake." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hili ni tamshi la Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب التحذير من ارتكاب
ما نهى الله عزوجل أَو رسوله صلى الله عليه وسلم عنه
116-Mlango Wa Kuonywa katika Kufanya Aliyo Kataza Allaah 'Azza wa Jalla au Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
فَلْيَحْذَرِ الَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنْ أَمْرِهِ أَن تُصِيبَهُمْ فِتْنَةٌ أَوْ يُصِيبَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٦٣﴾
Basi watahadhari wale wanaokhalifu amri yake, isije kuwasibu fitnah au ikawasibu adhabu iumizayo. [An-Nuwr: 63]
وَيُحَذِّرُكُمُ اللَّـهُ نَفْسَهُ ۗ ﴿٣٠﴾
Na Allaah Anakutahadharisheni na Nafsi Yake [Aal-'Imraan: 30]
إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ ﴿١٢﴾
Hakika mkamato wa kuadhibu wa Rabb wako bila shaka ni mkali. [Al-Buruwj: 12]
وَكَذَٰلِكَ أَخْذُ رَبِّكَ إِذَا أَخَذَ الْقُرَىٰ وَهِيَ ظَالِمَةٌ ۚ إِنَّ أَخْذَهُ أَلِيمٌ شَدِيدٌ﴿١٠٢﴾
Na hivyo ndivyo Mkamato wa Rabb wako unavyokuwa Anapokamata miji na huku ikifanya dhulma. Hakika Mkamato Wake unaumiza vikali. [Huwd: 102]
وعن أبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم قالَ : (( إنَّ اللهَ تَعَالَى يَغَارُ ، وَغَيْرَة اللهِ ، أنْ يَأْتِيَ المَرْءُ مَا حَرَّمَ اللهُ عَلَيْهِ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Hakika Allaah Ta'aalaa, Hukasirika, na Hasira Zake zinachocheka (zinazidi kuwa kubwa) wakati mtu anapotenda yale yaliyokatazwa (yaliyoharamishwa) na Yeye Allaah." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب ما يقوله ويفعله من ارتكب منهياً عنه
117-Mlango Wa Anachosema wa Anachofanya Mwenye Kufanya Alichokatazwa
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَإِمَّا يَنزَغَنَّكَ مِنَ الشَّيْطَانِ نَزْغٌ فَاسْتَعِذْ بِاللَّـهِ ۖ ﴿٣٦﴾
Na utakapokuchochea uchochezi kutoka kwa shaytwaan, basi omba kinga kwa Allaah. [Fusw-swilat: 41]
إِنَّ الَّذِينَ اتَّقَوْا إِذَا مَسَّهُمْ طَائِفٌ مِّنَ الشَّيْطَانِ تَذَكَّرُوا فَإِذَا هُم مُّبْصِرُونَ ﴿٢٠١﴾
Hakika wale wenye taqwa zinapowagusa pepesi za shaytwaan hukumbuka, basi mara wao huwa wenye kuona kwa utambuzi. [Al-A'raaf: 201]
وَالَّذِينَ إِذَا فَعَلُوا فَاحِشَةً أَوْ ظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ ذَكَرُوا اللَّـهَ فَاسْتَغْفَرُوا لِذُنُوبِهِمْ وَمَن يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلَّا اللَّـهُ وَلَمْ يُصِرُّوا عَلَىٰ مَا فَعَلُوا وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴿١٣٥﴾
Na ambao wanapofanya machafu au wakajidhulumu nafsi zao (kwa maasi), humdhukuru Allaah wakaomba Maghfirah kwa madhambi yao. Na nani anayeghufuria madhambi isipokuwa Allaah. Na hawaendelei katika waliyoyafanya na hali wanajua.
أُولَـٰئِكَ جَزَاؤُهُم مَّغْفِرَةٌ مِّن رَّبِّهِمْ وَجَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ وَنِعْمَ أَجْرُ الْعَامِلِينَ ﴿١٣٦﴾
Hao jazaa yao ni Maghfirah kutoka kwa Rabb wao na Jannaat zipitazo chini yake mito, wadumu humo. Ni uzuri ulioje ujira wa watendaji (wema). [Aal-'Imraan: 135-136]
وَتُوبُوا إِلَى اللَّـهِ جَمِيعًا أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٣١﴾
Na tubuni kwa Allaah nyote, enyi Waumini mpate kufaulu. [An-Nuwr: 31]
وعن أبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم قال: (( مَنْ حَلَفَ فَقَالَ في حَلفِهِ : بِاللاَّتِ وَالعُزَّى ، فَلْيَقُلْ : لاَ إلَهَ إلاَّ اللهُ ، وَمَنْ قَالَ لِصَاحِبهِ : تَعَالَ أُقَامِركَ فَلْيَتَصَدَّقْ )) .متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Aliyekula kiapo na akasema katika kiapo chake kwa kutekeleza: 'Naapa kwa laata na 'uzzaa (hawa wawili walikuwa ni masanamu waliokuwa wakiabudiwa na Maquraysh wa Makkah kabla ya wao Kusilimu), basi aseme: 'Laa ilaaha illa Allaah (Hapana Mola Muabudiwa isipokuwa Allaah)'. Na mwenye kumwambia mwenzake, 'Njoo nicheze nawe kamari', basi atowe Swadaqah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/280
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10331&title=17-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Kitabu%20Cha%20Mambo%20Yaliyokatazwa%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D8%A3%D9%85%D9%88%D8%B1%20%D8%A7%D9%84%D9%92%D9%85%D9%8F%D9%86%D9%87%D9%89%20%D8%B9%D9%8E%D9%86%D9%92%D9%87%D8%A7
[4] http://www.alhidaaya.com/
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11292&title=001-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuharamishwa%20Kusengenya%20na%20Amri%20ya%20Kuhifadhi%20Ulimi
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11293&title=002-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kusikiliza%20Kusengenya%20na%20Amri%20kwa%20Mwenye%20Kusikia%20Kumkataza%20Msemaji%20na%20Akishindwa%20au%20Asipokubali%20Kutoka%20Kwake%20Basi%20Aondoke%20Kwenye%20kikao
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11294&title=003-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Yanayoruhusiwa%20katika%20Kusengenya
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11295&title=004-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuharamishwa%20Umbeya%2C%20Nako%20ni%20Kueneza%20Maneno%20Baina%20ya%20Watu%20kwa%20Njia%20ya%20Kuleta%20Ufisadi
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11296&title=005-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuchukua%20Hadiyth%2C%20Maneno%20ya%20Watu%20na%20Kuyapeleka%20kwa%20Viongozi%20Ikiwa%20Hapana%20Haja%20Yoyote%20Kama%20Hofu%20ya%20Ufisadi%20na%20Mfano%20Wake
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11297&title=006-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Shutuma%20kwa%20Mwenye%20Nyuso%20Mbili
[11] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11298&title=007-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuharamishwa%20Uongo
[12] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11299&title=008-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kubainisha%20Ruhusa%20ya%20Kusema%20Uongo
[13] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11300&title=009-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuhimiza%20Kuthibitisha%20kwa%20Anayosema
[14] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11301&title=010-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuharamishwa%20Ushuhuda%20wa%20Uwongo
[15] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11302&title=011-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kumlaani%20Mtu%20au%20Mnyama
[16] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11303&title=012-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ruhusa%20Kuwalaani%20Watu%20wa%20Maasi%20Bila%20Kuwataja%20Majina
[17] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11304&title=013-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kumtusi%20Muislamu%20Bila%20ya%20Haki
[18] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11305&title=014-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kutukana%20Walio%20Kufa%20Bila%20ya%20Haki%20na%20Maslahi%20ya%20Kisheria
[19] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11306&title=015-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuudhi
[20] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11307&title=016-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kubughudhiana%20na%20Kukatana%20na%20Kupeana%20Nyongo
[21] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11308&title=017-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Hasadi
[22] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11309&title=018-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupeleleza%20na%20Kusikiliza%20Mazungumzo%20kwa%20Wasiotaka%20Usikiliza
[23] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11310&title=019-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuwa%20na%20Dhana%20Mbaya%20kwa%20Waislamu%20Bila%20ya%20Dharura
[24] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11311&title=020-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuwadharau%20Waislamu
[25] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11312&title=021-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20kufurahi%20kwa%20Baya%20Linalomkumba%20Muislamu
[26] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11313&title=022-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kukashifu%20%28Kutusi%29%20Nasaba%20%20
[27] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11314&title=023-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kughushi%20na%20Kuhadaa
[28] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11315&title=024-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuvunja%20Ahadi
[29] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11316&title=025-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kumsimanga%20Mtu%20kwa%20Ulichompa%20na%20Mfano%20Wake
[30] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11317&title=026-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kujifakhiri%20na%20Ujeuri
[31] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11318&title=027-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuhamana%20Baina%20ya%20Waislamu%20Wawili%20Zaidi%20ya%20Siku%20Tatu%20ila%20Ikiwa%20ni%20Mtu%20wa%20Bid%27ah%20au%20Ufasiki%20na%20Mfano%20Wake
[32] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11319&title=028-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kunong%27onezana%20Wawili%20Pasina%20wa%20Tatu%20Bila%20Idhini%20yake%20Isipokuwa%20kwa%20Haja%20%28Dharura%29
[33] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11320&title=029-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kumuadhibu%20Mtumwa%20na%20Mnyama%20na%20Mwanamke%20na%20Mtoto%20Bila%20ya%20Sababu%20ya%20Kisheria%20au%20Zaidi%20ya%20Kile%20Kiwango%20cha%20Kutia%20Adabu
[34] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11321&title=030-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuharamishwa%20Kuadhibu%20Mnyama%20Yoyote%20Hata%20Chungu%20na%20Mfano%20Wake%20Kutumia%20Moto
[35] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11322&title=031-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuharamishwa%20kwa%20Mtu%20Mwenye%20Uwezo%20Kukataa%20Kulipa%20Deni
[36] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11323&title=032-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Karaha%20ya%20Kurudisha%20Hiba%20%28Zawadi%29%20Ambayo%20Bado%20Hajaikabidhi%20kwa%20Mwenye%20Kupewa%2C%20na%20Hiba%20Aliyompa%20Mtoto%20Wake%20na%20Akaipokea%20au%20Hata%20Kama%20Hakuipokea%2C%20Karaha%20ya%20Kununua%20Kitu%20Alichokitoa%20Swadaqah%20kutoka%20kwa%20Aliyempa%20Swadaqah
[37] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11324&title=033-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kula%20Mali%20ya%20Yatima
[38] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11325&title=034-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukubwa%20wa%20uharamu%20wa%20Riba
[39] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11326&title=035-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Riya
[40] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11327&title=036-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Mambo%20Yanayodhaniwa%20ni%20Riya%20Lakini%20si%20Riya
[41] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11328&title=037-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kumwangalia%20Mwanamke%20wa%20Kando%20na%20Mvulana%20Mzuri%20Bila%20Haja%20ya%20Kisheria
[42] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11357&title=038-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukaa%20Faragha%20na%20Mwanamke%20wa%20Kando
[43] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11358&title=039-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Wanaume%20Kushabihiana%20na%20Wanawake%20na%20Kinyume%20Chake%20Katika%20Mavazi%2C%20Mwendo%20na%20Mengineo
[44] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11359&title=040-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kujifananisha%20na%20Shetani%20na%20Makafiri
[45] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11360&title=041-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Mwanaume%20na%20Mwanamke%20Kutia%20Rangi%20Nyeusi%20katika%20Nywele%20zao
[46] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11361&title=042-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kunyoa%20na%20Kubakishia%20Vijisehemu%20Visivyo%20Nyolewa%20%28Denge%29%20na%20Kukubaliwa%20Kunyoa%20Zote%20kwa%20Wanaume%20na%20Wala%20si%20kwa%20Wanawake
[47] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11362&title=043-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kuunganisha%20Nywele%2C%20Kuchanjwa%20na%20Kujaliza%20Meno
[48] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11363&title=044-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kung%27oa%20Mvi%20Kwenye%20Ndevu%2C%20Kichwa%20na%20Sehemu%20Nyengineyo%20na%20Kunyoa%20Ndevu%20kwa%20Kijana
[49] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11364&title=045-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Karaha%20ya%20Kustanji%20kwa%20Mkono%20wa%20Kulia%20na%20Kuishika%20Dhakari%20Yake%20kwa%20Mkono%20wa%20Kulia%20Bila%20Udhuru
[50] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11365&title=046-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Karaha%20ya%20Kutembea%20na%20Kiatu%20Kimoja%20au%20Soksi%20Moja%20Bila%20Udhuru%20Wowote%20na%20Karaha%20ya%20Kuvaa%20Viatu%20au%20Soksi%20kwa%20Kusimama%20Bila%20Udhuru
[51] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11366&title=047-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuacha%20Moto%20katika%20Nyumba%20Wakati%20wa%20Kulala%20na%20Mfano%20Wake%20Kama%20Taa
[52] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11367&title=048-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Takilifu%2C%20Nayo%20ni%20Kufanya%20Kitendo%20na%20Kusema%20Maneno%20Ambayo%20Hayana%20Maslahi%20na%20Ndani%20yake%20Yapo%20Mashaka
[53] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11368&title=049-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20Kuomboleza%20Maiti%20kwa%20Kujipiga%20Mashavu%2C%20Kuchana%20Nguo%2C%20Kung%27oa%20Nywele%2C%20Kunyoa%20na%20Kujiombea%20Maangamivu
[54] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11369&title=050-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuwaendea%20Makuhani%20na%20Wapiga%20Bao%20na%20Ramli
[55] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11370&title=051-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuamini%20Fali%20%28Mkosi%29
[56] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11371&title=052-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kuchora%20Wanyama%20katika%20Busati%20au%20Mawe%2C%20Nguo%2C%20Dirhamu%2C%20Dinari%20%28Hela%29%2C%20Mto%20na%20Kadhalika%20na%20Uharamu%20wa%20Kuwa%20na%20Picha%20katika%20Ukuta%2C%20Pazia%2C%20Kilemba%2C%20Nguo%20na%20Mfano%20wake%20na%20Amri%20ya%20Kufuta%20Picha
[57] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11372&title=053-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kufuga%20Mbwa%20Ila%20kwa%20Kuwinda%20au%20kwa%20Kulinda%20Wanyama%20au%20Mazao
[58] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11373&title=054-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kuwafunga%20Kengele%20Ngamia%20na%20Wanyama%20Wengine%20na%20Ukaraha%20wa%20Kumchukua%20Mbwa%20na%20Kengele%20katika%20Safari
[59] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11374&title=055-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kumpanda%20Jalaalah%2C%20Naye%20ni%20Ngamia%20Anayekula%20Kinyaa%20Lakini%20Anapokula%20Malisho%20Yaliyo%20Tohara%20Husafishika%20Nyama%20Yake%20na%20Kuondoka%20Ukaraha%20Huo
[60] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11375&title=056-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kutema%20Mate%20Msikitini%2C%20Amri%20ya%20Kuyaondoa%20Yanapopatikana%20na%20Amri%20ya%20Kusafisha%20Msikiti
[61] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11376&title=057-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kugombana%20Msikitini%2C%20Kunyanyua%20Sauti%20Ndani%20Yake%2C%20Kusaka%20Kitu%20Kilichopotea%2C%20Kuuza%2C%20Kununua%20na%20Kuajiri%20na%20Mfano%20Wake%20katika%20Muamala
[62] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11378&title=058-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuingia%20Msikitini%20Baada%20ya%20Kula%20Kitunguu%20Thaumu%20au%20Maji%20au%20Karoti%20au%20Vitu%20Vyengine%20Vyovyote%20Vyenye%20Harufu%20Mbaya%20Kabla%20ya%20Kuondoka%20Harufu%20hiyo%20Isipokuwa%20kwa%20Dharura
[63] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11379&title=059-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Ihtibaa%20Siku%20ya%20Ijumaa%20Imamu%20Akiwa%20Ahutubu%20Kwani%20Linamletea%20Mtu%20Usingizi%20Hivyo%20Kukosa%20Kusikia%20Hotuba%20na%20Kuwa%20na%20Hofu%20ya%20Kutokwa%20na%20wudhuu
[64] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11380&title=060-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20kwa%20Anayetaka%20Kuchinja%20Kukata%20Nywele%20au%20Kucha%20Zake%20Mpaka%20Achinje%20Pindi%20Linapoingia%20Kumi%20la%20Kwanza%20la%20Dhul%20Hijjah
[65] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11381&title=061-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuapa%20kwa%20Viumbe%20Kama%20Nabiy%2C%20Ka%27abah%2C%20Malaaikah%2C%20Mbingu%2C%20Baba%2C%20Uhai%2C%20Roho%2C%20Kichwa%2C%20Neema%20ya%20Sultani%2C%20Mchanga%20wa%20Fuani%20%28Kaburi%29%20na%20Amana%2C%20Nayo%20Imekatazwa%20kwa%20Ukali%20Zaidi
[66] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11382&title=062-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uzito%20wa%20Kula%20Yamini%20Ya%20Uongo%20Kwa%20Makusudi
[67] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11383&title=063-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Sunnah%20kwa%20Mwenye%20Kula%20Yamini%20Akaona%20Kufanya%20Kinyume%20na%20Yamini%20Hiyo%20Ndiyo%20Bora%2C%20Hivyo%20Alifanye%20Hilo%20Kisha%20Afanye%20Kafara%20la%20Kufanya%20Kinyume%20na%20Yamini%20Lake
[68] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11384&title=064-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kusamehewa%20kwa%20Kutotekeleza%20Yamini%20ya%20Upuuzi%20Kuwa%20Halina%20Kafara%2C%20Nayo%20ni%20Kusema%20kwa%20Ulimi%20Bila%20ya%20Kukusudia%20Yamini%20Kama%20Kauli%20Yake%20ya%20Ada%3A%20Sivyo%20Wa-Allaahi%20na%20Ndio%20Wa-Allaahi%20na%20Mfano%20wake
[69] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11385&title=065-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kula%20Yamini%20katika%20Biashara%20Hata%20Akiwa%20Mkweli
[70] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11386&title=066-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Mtu%20Kuomba%20kwa%20Jina%20la%20Allaah%20Mbali%20na%20Jannah%20na%20Ukaraha%20wa%20Kumkataza%20Mwenye%20Kuomba%20kwa%20Allaah%20Ta%27aalaa
[71] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11387&title=067-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kujiita%20Shaahinshah%20kwa%20Sultani%20na%20Wengineo%20Kwani%20Maana%20yake%20ni%20Mfalme%20wa%20Wafalme%20na%20kwa%20Hilo%20Hasifiwi%20Nalo%20ila%20Allaah%20Ta%27aalaa
[72] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11388&title=068-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kumuita%20Fasiki%20na%20Mzushi%20na%20Mfano%20Wao%20kwa%20Jina%20la%20Bwana%20na%20Mfano%20wake
[73] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11389&title=069-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kuitukana%20Homa
[74] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11390&title=070-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kutukana%20Upepo%20na%20Kubainisha%20Kinacho%20Semwa%20Wakati%20wa%20Kuvuma%20Kwake
[75] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11391&title=071-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kumtukana%20Jogoo
[76] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11392&title=072-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20kwa%20Mtu%20Kusema%3A%20Tumepata%20Mvua%20Kutokana%20na%20Nyota%20Kadha
[77] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11393&title=073-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kumwambia%20Muislamu%3A%20Ee%20Kafiri
[78] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11394&title=074-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kutoa%20Maneno%20Machafu%20na%20ya%20Kishenzi
[79] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11395&title=075-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Mazungumzo%20ya%20Kukera%20na%20kuvupa%20Mipaka%20Ndani%20Yake%20na%20Kujikalifisha%20katika%20Ufasaha%20na%20Kutumia%20Lugha%20Mbaya
[80] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11396&title=076-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Mtu%20Kusema%20Nafsi%20Yangu%20Imekuwa%20Mbaya
[81] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11397&title=077-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kuziita%20Zabibu%20kwa%20Jina%20Karm
[82] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11398&title=078-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuusifu%20Uzuri%20wa%20Mwanamke%20Mbele%20ya%20Mwanaume%20ila%20Anapohitajia%20Hilo%20kwa%20Haja%20Inayokubaliwa%20na%20Sheria%20Kama%20Kumuoa%20na%20Mfano%20Wake
[83] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11399&title=079-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Mtu%20Kusema%3A%20Ee%20Mola%20Wangu%20Nisamehe%20Ukipenda%20Bali%20Aazimie%20katika%20Maombi
[84] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11400&title=080-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kusema%3A%20Akipenda%20Allaah%20na%20Akapenda%20Fulani
[85] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11401&title=081-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Mazungumzo%20Baada%20ya%20Ishaa%20ya%20Mwisho
[86] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11402&title=082-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Mke%20Kukataa%20Mwito%20wa%20Mumewe%20Anapomuita%20Kitandani%20na%20Hana%20Udhuru%20Wowote%20wa%20Kisheria
[87] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11403&title=083-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Mwanamke%20Kufunga%20na%20Mumewe%20Yupo%20Nyumbani%20%28Au%20Mjini%29%20Bila%20ya%20Idhini%20Yake
[88] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11404&title=084-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kunyanyua%20Maamuma%20Kichwa%20chake%20Kutoka%20katika%20Rukuu%20au%20Sijda%20Kabla%20ya%20Imam
[89] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11405&title=085-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kuweka%20Mkono%20Kiunoni%20katika%20Swalaah
[90] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11406&title=086-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kuswali%20Pindi%20Chakula%20Kinapokuwa%20Tayari%20na%20Nafsi%20yake%20Imevutiwa%20Kwayo%20au%20Kushikwa%20na%20Haja%20Mbili%3A%20Nazo%20ni%20Ndogo%20na%20Kubwa
[91] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11407&title=087-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kunyanyua%20Macho%20Juu%20Mbinguni%20katika%20Swalaah
[92] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11408&title=088-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kugeuka%20Geuka%20katika%20Swalaah%20Bila%20Udhuru%20Wowote
[93] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11409&title=089-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kuswali%20Makaburini
[94] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11410&title=090-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kupita%20Mbele%20ya%20Wenye%20Kuswali
[95] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11411&title=091-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kuanza%20Maamuma%20Swalaah%20ya%20Sunnah%20Baada%20ya%20Muadhini%20Kukimu%20Swalaah
[96] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11412&title=092-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kuihusisha%20Siku%20ya%20Ijumaa%20kwa%20Funga%20au%20Usiku%20wake%20kwa%20Swalaah%20Miongoni%20mwa%20Masiku%20Mengine
[97] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11413&title=093-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Al-Wiswaal%20katika%20Funga%2C%20Nayo%20ni%20kwa%20Mtu%20Kufunga%20Siku%20Mbili%20au%20Zaidi%20Wala%20Hali%20Chakula%20wala%20Hanywi%20Chochote%20Baina%20Yake
[98] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11414&title=094-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kukaa%20Juu%20ya%20Kaburi
[99] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11415&title=095-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kulipiga%20Plasta%20Kaburi%20na%20Kulijengea
[100] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11416&title=096-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uzito%20wa%20Uharamu%20wa%20Mtumwa%20Kutoroka%20Kutoka%20kwa%20Bwana%20Wake
[101] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11417&title=097-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kumuombea%20Mtu%20katika%20Adhabu%20%28Hadd%29
[102] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11418&title=098-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kwenda%20Haja%20Njiani%2C%20Mapito%20ya%20Watu%2C%20Sehemu%20ya%20Vivuli%2C%20katika%20Maji%20na%20Mfano%20wake
[103] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11419&title=099-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kukojoa%20na%20Mfano%20Wake%20Katika%20Maji%20Yaliyotua
[104] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11420&title=100-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Mzazi%20Kuwapendelea%20Baadhi%20ya%20Watoto%20Wake%20Juu%20ya%20Wengine%20Katika%20Hiba
[105] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11421&title=101-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Mwanamke%20Kukaa%20na%20Msiba%20wa%20Maiti%20Zaidi%20ya%20Siku%20Tatu%20Isipokuwa%20kwa%20Mumewe%20Ambao%20ni%20Miezi%20Minne%20na%20Siku%20Kumi
[106] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11422&title=102-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20kwa%20Mtu%20wa%20Mjini%20Kununua%20kwa%20Mtu%20wa%20Kijijini%20na%20Kupokea%20Njiani%20Msafara%20wa%20Wafanya%20Biashara%2C%20na%20Kuuza%20katika%20Mauzo%20ya%20Nduguye%2C%20na%20Posa%20Juu%20ya%20Posa%20yake%20Isipokuwa%20Akitoa%20Ruhusa%20au%20Akikataliwa
[107] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11424&title=103-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kufuja%20Mali%20kwa%20Njia%20Ambayo%20Haikuidhinishwa%20na%20Sheria
[108] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11425&title=104-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kumuashiria%20muislamu%20kwa%20Silaha%20na%20Mfano%20wake%20Sawa%20ni%20kwa%20Kweli%20au%20Mzaha%20na%20Katazo%20la%20Kuwa%20na%20Upanga%20Nje%20ya%20Ala%20yake
[109] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11426&title=105-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20kutoka%20Msikitini%20Baada%20ya%20Adhana%20Isipokuwa%20kwa%20Udhuru%20Mpaka%20Aswali%20Swalaah%20ya%20Faradhi
[110] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11427&title=106-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kurudisha%20Zawadi%20ya%20Manukato%20Bila%20Udhuru
[111] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11428&title=107-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kumsifu%20Mtu%20Mbele%20Yake%20kwa%20Anayehofiwa%20Ufisadi%20Kama%20Vile%20Kiburi%20na%20Mfano%20Wake%20na%20Kufaa%20kwa%20Yule%20Anayeaminiwa%20katika%20Haki%20Yake
[112] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11429&title=108-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kutoka%20katika%20Mji%20Ambao%20Umekumbwa%20na%20Ugonjwa%20wa%20Kuambukiza%20na%20Kuingia%20Ndani%20yake%20%28Haifai%20Kuingia%20Wala%20Kutoka%20katika%20Mji%20Huo%29
[113] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11430&title=109-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uzito%20wa%20Uharamu%20wa%20Uchawi
[114] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11431&title=110-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kusafiri%20na%20Msahafu%20katika%20Nchi%20ya%20Makafiri%20Ikihofiwa%20Kuingia%20Mkononi%20Mwa%20Adui
[115] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11432&title=111-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kutumia%20Vyombo%20vya%20Dhahabu%2C%20Fedha%20katika%20Kula%2C%20Kunywa%2C%20Tohara%20na%20Njia%20Zote%20za%20Matumizi%20yake
[116] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11433&title=112-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Mwanamume%20Kuvaa%20Nguo%20ya%20Zafarani
[117] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11434&title=113-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kukaa%20Kimya%20Kuanzia%20Asubuhi%20Mpaka%20Usiku
[118] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11435&title=114-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Mtu%20Kujinasibisha%20kwa%20Asiyekuwa%20Baba%20Yake%20na%20Mtumwa%20Anayemkimbia%20Bwana%20Wake
[119] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11436&title=116-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuonywa%20katika%20Kufanya%20Aliyo%20Kataza%20Allaah%20%27Azza%20wa%20Jalla%20au%20Rasuli%20Wake%20%28Swalla%20Allaahu%20%27alayhi%20wa%20aalihi%20wa%20sallam%29%20
[120] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11437&title=117-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Anachosema%20wa%20Anachofanya%20Mwenye%20Kufanya%20Alichokatazwa