Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة قول الإنسان : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي إنْ شِئْتَ
بل يجزم بالطلب
079-Mlango Wa Ukaraha wa Mtu Kusema: Ee Mola Wangu Nisamehe Ukipenda Bali Aazimie katika Maombi
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
وعن أبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قال : (( لاَ يَقُولَنَّ أَحَدُكُمْ : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي إنْ شِئْتَ : اللَّهُمَّ ارْحَمْنِي إنْ شِئْتَ ، لِيَعْزِم المَسْأَلَةَ ، فَإنَّهُ لاَ مُكْرِهَ لَهُ )) . متفق عليه .
وفي رواية لمسلم : (( وَلكِنْ لِيَعْزِمْ وَلْيُعَظمِ الرَّغْبَةَ فَإنَّ اللهَ تَعَالَى لاَ يَتَعَاظَمُهُ شَيْءٌ أَعْطَاهُ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asiseme mmoja wenu: 'Ee Mola wangu nisamehe ukitaka. Ee Mola wangu nirehemu Ukitaka.' Bali aazimie katika kumuomba Allaah kwa sababu hakuna wa kumlazimisha Yeye (Allaah)." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Na riwaayah ya Muslim: "Lakini aazimie na awe na matumaini makubwa, kwani hakuna kitu chochote ambacho ni kikubwa kwa Allaah Ta'aalaa kutoa."
Hadiyth – 2
وعن أنس رضي الله عنه قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إذا دَعَا أحَدُكُمْ فَلْيَعْزِم المَسْأَلَةَ ، وَلاَ يَقُولَنَّ : اللَّهُمَّ إنْ شِئْتَ ، فَأَعْطِنِي ، فَإنَّهُ لاَ مُسْتَكْرِهَ لَهُ )) . متفق عليه .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapoomba mmoja wenu aazimie kwa dhati na asiseme: 'Ee Mola wangu! Ukitaka nipe'. Kwa sababu hakuna wa Kumkalifisha kitu dhidi ya Utashi Wake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11399&title=079-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Mtu%20Kusema%3A%20Ee%20Mola%20Wangu%20Nisamehe%20Ukipenda%20Bali%20Aazimie%20katika%20Maombi