1- SWALAH YA ADHUHURI
Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma katika Rakaa mbili za mwanzo Suratul-Faatihah na Surah mbili, hurefusha ya kwanza kuliko ya pili.([1])
Mara nyingine alikuwa akiirefusha urefu ambao ilikuwa inaweza kufika kuqimiwa kwa Swalah ya Adhuhuri, na aliweza mtu kwenda Al-Baqiy' kukidhi haja yake, [kisha aende nyumbani kwake], kutawadha, kisha aje hali ya kuwa Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akiwa bado yuko katika Rakaa ya mwanzo, kwa namna alivyokuwa akiirefusha([2]).
(Pia) walikuwa wakidhania kwamba alikuwa akifanya hivyo ili watu waweze kuidiriki Rakaa ya mwanzo.([3])
Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma katika kila Rakaa ya hizo Rakaa mbili, kadiri ya Aayah thelathini, kiasi cha kusoma As-Sajdah [32-30] na ikiwemo al-Faatihah.([4]) (na kufuatia As-Sajdah [32-30])
Mara nyingine alikuwa akisoma:
((وَالسَّمَاء وَالطَّارِقِ))
((Naapa kwa mbingu na kinachokuja usiku!)) [At-Twaariq: 86-17], na
((وَالسَّمَاء ذَاتِ الْبُرُوجِ))
((Naapa kwa mbingu yenye Buruji!)) [Al-Buruuj: 85-22], na
((وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَى))
((Naapa kwa usiku unapo funika!)) [Al-Layl: 92-21], na mfano wa Surah zilizofanana na hizi.([5])
Na huenda akasoma
((إِذَا السَّمَاء انشَقَّتْ))
((Itapochanika mbingu)) [Al-Inshiqaaq: 84-25], na mfano wake.([6])
Walikuwa wakiweza kuelewa kwamba alikuwa anasoma katika Adhuhuri na Alasiri kutokana na mtikisiko wa ndevu zake.([7])
[1] Al-Bukhaariy na Muslim.
[2] Muslim na Al-Bukhaariy katika Juz-u Al-Qiraat (Makala ya Tilaawah).
[3] Abu Daawuud ikiwa na isnaad Swahiyh na Ibn Khuzaymah (1/165/1).
[4] Ahmad na Muslim.
[5] Abu Daawuud, At-Tirmidhiy na Ibn Khuzaymah (1/67/2). Wawili wa mwisho wamesema kuwa ni Swahiyh.
[6] Ibn Khuzaymah katika Swahiyh yake (1/67/2).
[7] Al-Bukhaariy na Abu Daawuud.
Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F2966&title=023-Sifa%20Ya%20Swalah%20Ya%20Mtume%20%28Swalla%20Allaahu%20%27Alayhi%20Wa%20Aalihi%20Wa%20Sallam%29%3A%20Alivyokuwa%20Akisoma%20%28%D8%B5%D9%84%D9%89%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%20%D8%B9%D9%84%D9%8A%D9%87%20%D9%88%D8%A2%D9%84%D9%87%20%D9%88%D8%B3%D9%84%D9%85%29%20Katika%20Swalah%20Mbalimbali.%201%20-%20Swalah%20Ya%20Adhuhuri