14-Hadiyth: Fadhila Za 'Ilmu Na 'Ulamaa: Anayejifunza Au Kufundisha ‘Ilmu Msikitini Yuko Katika Daraja La Mujaahid Fiy SabiliLLaah

Hadiyth: Fadhila Za ‘Ilmu Na ‘Ulamaa

 

Hadiyth Ya 14

Anayejifunza Au Kufundisha ‘Ilmu Msikitini

Yuko Katika Daraja La Mujaahid Fiy SabiliLLaah

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ : سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ : (مَنْ جَاءَ مَسْجِدِي هَذَا لَمْ يَأْتِهِ إِلَّا لِخَيْرٍ يَتَعَلَّمُهُ أَوْ يُعَلِّمُهُ فَهُوَ بِمَنْزِلَةِ الْمُجَاهِدِ فِي سَبِيلِ اللَّهِ ، وَمَنْ جَاءَ لِغَيْرِ ذَلِكَ فَهُوَ بِمَنْزِلَةِ الرَّجُلِ يَنْظُرُ إِلَى مَتَاعِ غَيْرِهِ)   

 

Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema:  Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: "Yeyote anayekuja kwenye Msikiti wangu huu, na anakuja tu kwa kusudio zuri, kama vile kujifunza au kufundisha, daraja lake ni kama ya yule Mujaahid fiy SabiliLLaah. Yeyote anayekuja kwa sababu nyingine yoyote, daraja lake ni ya mtu ambaye analinda mali ya watu wengine.” [Ahmad  (14/257), Ibn Maajah (223), ameisahihisha Al-Albaaniy: Swahiyh Ibn Maajah (187)]

 

 

 

Share