Anaomba Toba Kisha Anarudia Tena Kufanya Kosa Kila Mara. Vipi Aweze Kuimarika Bila Kurudi Makosani?

 

SWALI:

 

assalaam  alykum  swala  ni  mambo  gani  ambayo  natakiwa  kufanya  ila nisirudie  kosa  baada  ya  kutubu, kwani  huwa  najitahidi  kutubu huwenda  isipite  hata  miezi  mitatu  hurirejea  kosa lile  lile nililotubu   najitahidi  kujizuia  kwa  kubadilsha  mazingara  lakini  bado shetani  hunizidi nguvu  naomba  msaada  kuhusiana  na  hili

 


 

 

 

JIBU

 

 

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho

.

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kurudia katika kosa baada ya kutubia.

 

Yapo mambo mengi ambayo unaweza kufanya ili kujitenga na maasiya na makosa hayo ambayo unayarudia.

 

Hakika ni maumbile ya mwanaadamu kurudia kosa baada ya muda. Hata hivyo, inatakiwa ufanye juhudi nyingi za kuweza kutorudia lakini ukikosa inabidi urudi utake msamaha kwake. Ikiwa utaweza kutimiza yale masharti ya kusamehewa basi InshaAllaah Allaah Aliyetukuka Atakusamehe. Jaribu sana utimize masharti yafuatayo:

 

  1. Kuacha maasiya.
  2. Kujuta katika kufanya hayo maasiya.
  3. Kuazimia kutorudia makosa hayo.
  4. Ukiwa umemkosea mwanaadamu mwenzako basi uombe msamaha kutoka kwake.

 

Baada ya kurudia kosa basi utarudia mfumo huo ulio juu katika kuomba msamaha. Ama mambo ambayo yanaweza kukusaidia ili kukupatia kinga ili usirudie makosa hayo kwa kiasi ulicho nacho sasa ni kama yafuatayo:

 

  1. Kuifanya Qur-aan kuwa rafiki yako wa karibu sana. Na haitakiwi kuisoma peke yake bali unatakiwa uisome pamoja na kufahamu na kujua maana yake. Na baada ya kujua maana yake kufanya juhudi kutekeleza yaliyo ndani kwa kiasi kikubwa sana.
  2. Kuifahamu Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na kujaribu sana kufuata yale tuliyofundishwa ndani yake.
  3. Kuyafahamu majina ya Allaah Aliyetukuka na kujua maana ya kila jina pamoja na sifa Zake.
  4. Kuleta adhkaar za asubuhi na jioni pamoja na adhkaar nyingine ambazo zinapatikana katika viungo vifuatavyo:

 

Hiswnul-Muslim: Du’aa Na Adhkaar Kusoma Na Kwa Kusikiliza (Toleo Lilohaririwa)

 

027-Hiswnul-Muslim: Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni

 

 

 

  1. Kufanya urafiki na watu walio Waumini ili kuweza kusaidiana katika kufanya mema na kuacha mabaya.

 

Kufanya hayo kutatusaidia sana katika kujiepusha na makosa ambayo unayarudia rudia kila wakati.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share