049-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Hujuraat Aayah11: وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ بِئْسَ الاِسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الإِيمَانِ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

049-Al-Hujuraat  11

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ ۖ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ ۚ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴿١١﴾

Enyi walioamini! Wanaume wasiwafanyie dhihaka na kudharau wanaume wengineo asaa wakawa bora kuliko wao, wala wanawake kwa wanawake wengineo, asaa wakawa bora kuliko wao. Na wala msifedheheshane kwa kutukanana na wala msiitane majina (mabaya) ya utani. Ubaya ulioje kuita jina la ufasiki baada ya iymaan. Na yeyote asiyetubu, basi hao ndio madhalimu. [Al-Hujuraat: 11]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

حَدَّثَنَا مُوسَى بْنُ إِسْمَاعِيلَ، حَدَّثَنَا وُهَيْبٌ، عَنْ دَاوُدَ، عَنْ عَامِرٍ، قَالَ حَدَّثَنِي أَبُو جُبَيْرَةَ بْنُ الضَّحَّاكِ،  قَالَ فِينَا نَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ فِي بَنِي سَلِمَةَ: ((وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ بِئْسَ الاِسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الإِيمَانِ))قَالَ قَدِمَ عَلَيْنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَلَيْسَ مِنَّا رَجُلٌ إِلاَّ وَلَهُ اسْمَانِ أَوْ ثَلاَثَةٌ فَجَعَلَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ ‏"‏ يَا فُلاَنُ ‏"‏ ‏.‏ فَيَقُولُونَ مَهْ يَا رَسُولَ اللَّهِ إِنَّهُ يَغْضَبُ مِنْ هَذَا الاِسْمِ فَأُنْزِلَتْ هَذِهِ الآيَةُ: ((وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ))

 

Ametuhadithia Muwsaa ibn Ismaa’iyl, ametuhadithia Wuhayb, kutoka kwa Daawuwd, kutoka kwa ‘Aamir amesema: ametuhadithia Jubayrah ibn Adhw-Dhwahaak ambaye amesema:  Aayah hii imeteremshwa kwa ajili yetu Bani Salimah:

 

وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ بِئْسَ الاِسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الإِيمَان

Na wala msiitane majina (mabaya) ya utani. Ubaya ulioje kuita jina la ufasiki baada ya iymaan.

 

Akasema: Pindi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipotufikia, kila mmoja wetu alikuwa ana majina mawili au matatu.  Basi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akawa Anasema:  “Ee fulani!” Lakini wao husema: Ee Rasuli wa Allaah (Usimwite kwa jina hilo), hakika yeye hughadhibika kuitwa kwa jina hilo!  Basi hapo ikateremshwa Aayah hii:

وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ  

Na wala msiitane majina (mabaya) ya utani. 

 

[Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, At-Tirmidhiy, ameisahihisha Al-Albaaniy: Swahiyh Abiy Daawuwd (4962), Swahiyh Ibn Maajah (3030), Swahiyh At-Tirmidhiy (3268),Swahiyh Adab Al-Mufrad (251)]

 

Share