30-Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: Allaah Amefaridhisha Mambo Ya Kuwajibika Basi Msiyapoteze

 

Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah:

 

Hadiyth Ya 30

 

إنّ اللهَ تَعَالى فَرَضَ فَرَائِضَ فَلاَ تُضَيّعوها

 

Hakika Allaah Amefaridhisha Faraaidhw

 

(Mambo Ya Kuwajibika Katika Dini) Basi Msiyapoteze

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Sikiliza Hadiyth:

 

 

عَنْ أَبيِ ثَعْلَبَةَ الخُشَنِيِّ جُرْثُومِ بْن نَاشرٍ رضي الله عنه عَنْ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنّ اللهَ تَعَالى فَرَضَ فَرَائِضَ فَلاَ تُضَيّعوهاَ وَحَدَّ حُدُودَاً فَلاتَعْتَدُوهَا وَحَرّمَ أَشْياءَ فَلاَتَنْتَهِكُوهَا وَسَكَتَ عَنْ أَشْيَاءَ رَحْمَةً لَكُمْ غَيْرَ نِسْيانٍ فَلا تَبْحَثُوا عَنْهَا)) حَدِيثٌ حَسَنٌ، رَوَاهُ الدَّارَقُطْنِيّ وَغَيْرُهُ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Tha'alabah Al-Khushaniyy Jurthuwm bin Naashir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ”Hakika Allaah Amefaridhisha faraaidhw (Mambo ya kuwajibika katika Dini) hivyo msiyapoteze. Na Akaweka mipaka basi msiivuke. Na Ameharamisha mambo kwa hivyo msiyahalifu. Na Amenyamazia mambo kutokana na rahmah (Yake) kwenu wala hakusahau kwa hivyo msiyadadisi.”  [Hadiyth Hasan Ad-Daaraqutwniy na wengineo]

 

 

 

Share