31-Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: Ipe Mgongo Dunia Allaah Atakupenda

 

Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah:

 

Hadiyth Ya 31

 

ازْهَدْ فِي الدُّنْيَا يُحِبُّكَ اللَّهُ

 

Ipe Mgongo Dunia Allaah Atakupenda

 

Alhidaaya.com

 

 

 Sikiliza Hadiyth:

 

 

عَنْ أَبِي العَبّاسِ سَهلِ بْن سَعْدٍ السّاعِدِيِّ رضي الله عنه  قَالَ : جَاءَ رَجُلُ إِلى النَبِي صلى الله عليه وسلم  فَقَالَ : يَا رَسُولَ اللَّهِ دُلَّنِي عَلَى عَمَلٍ إِذَا عَمِلْتُهُ أَحَبَّنِي اللَّهُ وَأَحَبَّنِي النَّاسُ . فَقَالَ: (( ازْهَدْ فِي الدُّنْيَا يُحِبُّكَ اللَّهُ وَازْهَدْ فِيمَا عِنْدَ النَّاسِ يُحِبُّكَ النّاسُ)) رَوَاهُ ابْنُ مَاجَهْ  وَغَيْرُهُ بِأَسَانِيدَ حَسَنَةٍ. 

 

Imepokelewa kutoka kwa Sahl bin Sa'ad As-Saa’idiyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: “Alikuja mtu kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Nijulishe ‘amali ambayo nikiifanya Allaah Atanipenda na watu pia watanipenda.  Akasema: “Ipe mgongo dunia Allaah Atakupenda, na vipe mgongo vilivyomo kwa watu, watu watakupenda.” [Ibn Maajah na wengineo kwa mtiririko mzuri wa isnaad]*

 

*Hata hivyo Wanavyuoni wa Hadiyth wameeleza kuwa Hadiyth hii ni dhaifu kutokana na udhaifu wa sanad yake japo An-Nawawiy kaitumia na kasema ina sanad nzuri.

 

 

 

 

Share