Mke Anayefanya Kazi Anatakiwa Atoe Masurufu Ya Nyumba?
SWALI:
Navyojua mume ni mtu msimamizi wa nyumba kutosheleza nyumba na mahitaji yake kama kodi, chakula na hali kadhalika je ikiwa mke ana kazi yake basi ana lazima ya kutoa nusu kodi na nusu chakula au vitu hivyo ni wajibu wa mume na mke akiwa atatoa basi mapenzi yake?? Maana natatanika
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa ndugu yetu muuliza swali. Bila shaka ni jambo linaloeleweka kuwa mume katika Uislamu anahitajika kumtimizia mkewe mahitaji ya msingi
“Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Allaah baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayoyatoa” (4: 34).
Pia, “Na juu ya baba yake chakula cha kina mama, na nguo zao kwa mujibu wa ada. Wala halazimishwi mtu ila kwa kadiri ya uwezo wake. Mama asitiwe taabuni kwa ajili ya mwanawe, wala baba kwa ajili ya mwanawe” (2: 233).
Mke na mwanamke kwa ujumla katika Uislamu amepatiwa haki ya kuweza kurithi au kuchuma chumo la halali. Kwa
“Wanaume wana sehemu katika wanayoyaacha wazazi na jamaa waliokaribia. Na wanawake wanayo sehemu katika waliyoyaacha wazazi na jamaa walio karibia. Ikiwa kidogo au kingi. Hizi ni sehemu zilizofaridhiwa” (4: 7).
Amesema tena (Subhaanahu wa Ta‘ala): “Wanaume wana fungu katika waliovichuma, na wanawake wana fungu katika waliovichuma. Na muombeni Allaah fadhila Zake. Hakika Allaah ni Mjuzi wa kila kitu” (4: 32).
Baada ya kupatiwa haki mwanamke ya kumiliki
Ikiwa mke anaona mumewe ni dhaifu katika kipato na ni matatizo kutazama nyumba, mke kama huyo anaweza kumsaidia mumewe katika baadhi ya majukumu naye atapata ujira kwa
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha



Assalam Aleikum, nataka
Assalam Aleikum, nataka kuongezea kwa hilo swali; ni usawa kusaidiana kifedha haswa inapokuwa mume hana uwezo wa kuangalia nyumba nzima lakini utatizi unakuja pale inapokuwa mume anakuwa na ushindani yaani wewe unafanya kazi basi lazima utowe nusu nusu ama zaidi, kodi ya nyumba, kisha na chakula juu yake iwe wewe ndiye unayenunua. Je, mke hapa ana haki ya kukataa?