Hilaal: Waislamu Wote Duniani Wafuate Mwandamo Mmoja Wafunge Na Kula ‘Iyd Siku Moja ?

 

Hilaal: Waislamu Wote Duniani Wafuate Mwandamo Mmoja

Wafunge (Swiyaam) Na Kula ‘Iyd Siku Moja ?

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

SWALI:

 

nilimskia sheikh mmoja katika kipindi cha televisheni anasema kwamba haiwezekani watu wote duniani kupata sikukuu siku moja kwa sababu kuna nchi zimepishana kwa takribani masaa 24,na kutoa mfano kwamba, Honolulu Marekani jumamosi saa 3 asubuhi, New Zealand ni saa 2 asubuhi Ijumaa. je hii ni kweli na kweli inawezekana ikawa ni sababu ya kutowezekana kufunga na kufungua siku moja dunia nzima??

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Ni kweli kuwa zipo sehemu ambazo zimetofautiana kwa masaa takriban 23 kama ulivyosikia  lakini huyo shekhe kachanganya baina ya sehemu. Jua linachomoza Wellington, New Zealand mwanzo kabla ya Hawaii – Honolulu, USA, yaani ikiwa New Zealand ni saa mbili siku ya Ijumaa, Honolulu itakuwa Alkhamisi saa tatu asubuhi. Hata hivyo tofauti hiyo si sababu kabisa kwa Waislamu duniani kutofunga na kutofungua pamoja.

 

Ni hakika isiyopingika kabisa kuwa kuanzia wakati ambao mawasiliano yamekuwa ni sahali kupatikana kote duniani mwezi umekuwa ukionekana Mashariki ya kati. Na kwa sasa kama katika nchi ya Tanzania na Kenya baada ya Waislamu kuchukua umuhimu mkubwa wa kuangalia mwezi ukawa mwandamo wa sehemu hii unakwenda sambamba na ule wa Mashariki ya Kati.

 

Tufahamu kuwa tofauti baina ya sehemu hiyo na sehemu za Mashariki na magharibi ya ulimwengu haizidi masaa 12. Hakika mazungumzo hayo ni watu tu kutafuta vizisababu visivyokuwa na msingi wowote wa kidini.

 

Ni ajabu kuwa mashekhe hao wamejikita kuzungumza kulalamika kuhusu mwezi wa kimataifa pekee wala huwasikii kuzungumza matatizo ya rai kama:

 

1.      Kuzingatia mipaka ya kila nchi.

2.      Kuzingatia umbali wa farsakh 24.

3.      Kuzingatia masafa ya qasri.

4.      Kuzingatia tofauti za matlai.

5.      Kuzingatia usawa wa bahari (sea level).

6.      Kuzingatia maeneo ya mashariki na magharibi.

7.      Kuzingatia kusadifu.

 

Hata hivyo, kuna baadhi ya Wanachuoni wanaoonelea kila mtu afunge na mwezi wa nchi yake au utakaotangazwa na Kiongozi wa Kiislamu wa nchi yake.

 

Kifupi, haya mas-alah yana ikhtilaaf na haipaswi upande mmoja kuwalaumu wengine au kuwabeza.

 

Tafadhali bonyeza viungo vifuatavyo upate manufaa zaidi:

 

Kuandama Mwezi – Afuate Nchi Anayoishi Au Unapoandama Nchi Yoyote?

 

Kuonekana Kwa Mwezi Mwandamo Sehemu Tofauti Na Kuanza Funga

 

Kufuata Mwezi Wa Kitaifa Au Wa Kimataifa; Kupishana Masaa; Wazee Zamani Walikuwa Wanapataje Habari Kuhusu Mwezi Wa Kimataifa

 

Utata wa Kufunga Swawm na Kufungua Kutokana Na Kutofautiana Kuhusu Mwandamo Wa Mwezi

 

Ni Sawa Kumfuata Mume Kwa Msimamo Wa Mwezi Wa Kitaifa Japokuwa Alikuwa Akifuata Unapoonekana Popote Duniani?

 

Nilifunga Na Waliochelewa Kufunga Nikasafiri Kwa Wale Waliwahi Kufunga Nao Kwao Ni Siku Ya ‘Iyd, Je, Niendelee Kufunga?

 

Tunaambiwa Wanaofuata Mwezi Wa Kimataifa Wamekosea Na Walipe Swawm Je, Ni Sawa?Mwandamo Wa Mwezi, Kila Mji Ufuate Mwezi Unapoonekena Kwao Au Mwandamo Wa Kimataifa?

 

Mwezi Ulionekana Siku Moja Nchi Nyingine Mapema Zaidi Yetu Je, Tulipe Siku Hiyo?

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share