25-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Atakuwa Sayyid (Bwana) Wa Watu Siku Ya Qiyaamah

Fadhila Za  Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

25-Atakuwa Sayyid (Bwana) Wa Watu Siku Ya Qiyaamah

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ، قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ أَنَا سَيِّدُ وَلَدِ آدَمَ وَلاَ فَخْرَ وَأَنَا أَوَّلُ مَنْ تَنْشَقُّ الأَرْضُ عَنْهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلاَ فَخْرَ وَأَنَا أَوَّلُ شَافِعٍ وَأَوَّلُ مُشَفَّعٍ وَلاَ فَخْرَ وَلِوَاءُ الْحَمْدِ بِيَدِي يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلاَ فَخْرَ ‏"‏ ‏.

 

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya-Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mimi Sayyid (Bwana) katika wana wa Aadam Siku ya Qiyaamah wala sijifakharishi kwa kujigamba. Na ni wa kwanza ambaye ardhi itanipasukia Siku ya Qiyaamah wala sijifakharishi kwa kujigamba. Na wa kwanza ambaye nitashufai na wa kwanza ambaye nitakubaliwa shufaa yangu wala sijifakharishi kwa kujigamba, na katika mkono wangu kutakuwepo na bango la sifa, wala sijifakharishi kwa kujigamba)) [Ibn Maajah ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Ibn Maajah (3496), Swahiyh At-Targhiyb (3643)]

 

Share