Skip navigation.
Home kabah

Haliym (Bokoboko La Pakistan)

 

VIPIMO:

 

Nyama ya mbuzi au ng’ombe ya mafupa                              2 LB

Mchanganyiko wa dengu                                                        2  Vikombe

(hadesi, mchele, chooko, ngano, dengu n.k

au nunua ya tayari iliyokwishachanganywa)

Kitungu maji (vikate vidogo)                                                  1

Mafuta                                                                                      ¼ Kikombe

Nyana kata ndogo ndogo                                                         1

Thomu na tangawazi iliyosagwa                                              1 Kijiko cha supu

Bizari ya haliym                                                                         2 vijiko vya supu

Nyanya ya kopo                                                                        2  vijiko vya supu

 

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA  

1.Chemsha nyama na chumvi ½ kijiko mpaka iive, toa mafupa.

2. Chemsha mchanganyiko wa dengu mpaka ziive.

3.Katika sufuria weka mafuta, kaanga vitunguu vilainike, tia thomu na tangawizi, bizari ya haliym, nyanya ya kopo. Kaanga mpaka iwive.

4.Tia nyama iliyowiva na supu yake kidogo.

5.Tia mchanganyiko wa dengu tia kwenye mashine ya kusaga (blender), saga na ile supu ya nyama isagike vizuri

6.Mimina kwenye sufuria changanya, tia ndimu kidogo, acha moto mdogo mdogo kwa muda wa dakika 15.

7. Tia katika bakuli, pambia kwa vitunguu vilivyokaangwa vya rangi ya hudhurungi vikavu, pilipili mbichi (ukipenda) na kotmiri, ikiwa kuliwa.